Kote duniani biashara ya mpira ndivyo ilivyo mchezaji ni kama mfanya biashara tu siku bidhaa yake ikiwa poa ndio nyakati ambayo hua anatafuta mteja ambaye ataifikia gharama ya bei yake.
Kinachoendelea hivi sasa kwa mchezaji Stephanie Aziz Ki ni yeye kutoongeza mkataba MPYA ndani ya Yanga SC, siyo habari nzuri sana kuzisikia kutoka klabuni hapo na mchezaji wao. Aziz ni moyo wa timu kwasasa hilo halina ubishi, mabao yake mengi yaliifanya Yanga kufikia baadhi ya malengo ya Klabu.
Boss anakuna kichwa kuhusu wino mpya wa mfanyakazi wake, ni wakati mgumu kwake kwani anafahamu namna alivyowahi kuinasa saini hiyo hakuwa kazi rahisi kuipata vita ilikuwa tena dhidi ya Mtani wao Simba SC. Leo linapokuja jambo kama hili mchezaji anapata kigugumuzi cha kuongeza mkataba wala hatupaswi kuanza kumshangaa mchezaji, tumuelewe kuwa hii ndio kazi yake, hayo ni maisha yake kaja Tanzania kutengeza kipato.
Inaarifiwa kuwa STEPHEN AZIZ KI ana ofa mbili kutoka Al Ahly na Orlando Pirates, amewapa Yanga unafuu wa offer ili aweze kusaini kwao na mahitaji yake kutoka kwa vyanzo vyangu anahitaji kiasi cha dola 500,000 ili aweze kusaini ikiwa ni sawa na BILLION 1.2 za Kitanzania.
Mpaka hivi sasa Wananchi hawana kiasi hicho na klabu kwa mujibu wa vyanzo imejipiga mpaka Dola 350,000 za Kimarekani wapo tayari kumpa ila Aziz ameshikilia zifike 500,000 ili asaini, jitihada zinaendelea ila kinachohitajika ni huo mzigo.
Mpaka hivi sasa Aziz hajasaini KARATASI yoyote ndani ya Jangwani.
Kinachobaki kwenye timu na klabuni milele ni Mwanachama na Shabiki pekee yao, wachezaji, benchi la ufundi pamoja na Viongozi wa timu hua siyo watu wa kudumu kwaiyo tukiyajua hayo wala hatuingii kwenye kumshangaa mchezaji. Ikitokea wameelewana katika ya boss na mchezaji ili aendelee kusalia, basi itakuwa poa sana na kama ikitokea imeshindikana ni kumtakia kheri mchezaji popote aendako.
Maoni Yako Ni Yapi? Tuambie Kwenye Comments
Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.
Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii [email protected]



