Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi) KOTI JEUSI – 10
    Hadithi

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi) KOTI JEUSI – 10

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 7, 2024Updated:May 7, 202461 Comments6 Mins Read8K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia ” Dakika saba pekee zilitosha kwa Marcus kupata mahali pa kuanza Uchunguzi wake, walitolewa vijana hao wakiwa wamevimba sehemu mbalimbali za Miili yao.”

    Tuendelee Sasa 

    SEHEMU YA KUMI 


    Wiki mbili baada kifo cha Mzee Yusuf.

    Adela alikua ameketi chumbani kwake huku mkononi akiwa ameshikilia kadi moja, aliikumbuka kadi hiyo alipewa na Babu Yake Marehemu Bilionea Yusuf. Kadi ilikua na Namba na Jina lililoandikwa Susan Mbeno.

    Aliitafakari kadi hiyo, Mungu aliweka akili ya kiutu uzima kwa Binti huyu wa Kitajiri. Kipawa cha kufikiri kilikua juu sana tofauti na umri wake, aliitazama kwa zaidi ya dakika sita huku akitafakari ni kwanini Babu yake alimpatia kadi hiyo, moyo ulimdunda.

    Akaielekea simu ya Mezani na kuipiga namba hiyo akiamini Babu yake alihitaji yeye azungumze na huyo Susan Mbeno, akiwa anasubiria simu ipokelewe alikua akitetemeka huku akijawa na woga wa ajabu sana, kabla hata haijapokelewa aliikata.

     Akaketi kitandani akiwa analia huku akisema

    “Sitaki, sitaki, staki” sauti hii ilipenya kwenye masikio ya Bi Choro aliyekua akipiga deki sakafu kando ya chumba cha Adela, ikampeleka hadi chumbani humo na kumkuta akiwa analia. 

    “Adela unalia nini?” alihoji Bi Choro kwa upole sana

    “Bibi sitaki kusema, sitaki Mimi” alisema Adela akimkumbatia Bi Choro

    “Hutaki kusema nini?”

    “Bibi sitaki Mimi” alisema akiwa analia, Bi Choro alijitahidi sana kumhoji Adela lakini hakusema kingine zaidi ya kudondosha chozi.

    “Basi pumzika Adela, usiwe na hofu, usiogope. Mlinzi yupo, Mimi nipo hakuna mwingine 

    atakayekuja, upo salama sawa?” alisema Bi Choro, aliamini kifo cha Mzee Yusuf ndiyo sababu ya Binti huyo kulia kwani kipindi hicho alikua akisakamwa sana na wapelelezi.

     

     Baadaye Adela akapitiwa na Usingizi, Bi Choro akamlaza vizuri kisha akatoka.

    ***

    “Mapigo yake ya moyo yanazidi kushuka, jitihada zifanyike haraka” ilikua ni sauti ya Dokta 

    akiwaelekeza Madaktari na Manesi ambao walikua ndani ya chumba kimoja alicholazwa Adela, 

    mitambo ilionesha kushuka sana kwa mapigo yake hali iliyoonesha wazi kuwa angefariki muda 

    mchache Ujao. Alikua akishindwa kuhema, macho yalimtoka pima. 

    “Mwanangu Mimi, Adelaaaa” Sofia alikua akimlilia Binti yake, walikesha hapo kwa usiku mzima na nusu ya siku mpya, Hamza hakumwacha Dada yake.

     Akamweleza kua Madaktari wanafanya jitihada ili kuokoa Maisha ya Binti huyo lakini hiyo haikutosha kumtuliza, alilia mfululizo.

    Jioni saa 10:12 Daktari aliandika muda ambao Mtoto Adela alifariki Dunia, taarifa iliyomfanya Sofia apoteze fahamu zaidi ya mara tano. Kifo cha Binti huyo kiliandikwa na Daktari aliyekua akimtibia kua alifariki kwa mshituko wa moyo uliotokana na njozi aliyokua ameiyota Binti huyo, sisi tunaifahamu ndoto ya Binti huyo lakini taarifa ya kifo hicho kiliwashangaza walio wengi.

    Maneno ya chini chini yakawa mengi, familia hiyo ikatajwa na walioifahamu kuwa inaandamwa na mzimu wa kifo, wengine wakihusisha vifo hivyo na imani za Freemason lakini kwa mpelelezi Daudi Mbaga aliyeko Kigoma aliuona urejeo wa Muuwaji ndani ya familia hiyo, saa 12:00 kengele ya Kanisa la Roma ilipokua ikigonga, Daudi Mbaga alimpigia tena simu Jasusi Marcus aliyekua kituo cha Polisi walipohifadhiwa wale Wanachuo.

    “Nitazungumza nao baadae, warudishe Mahabusu” aliagiza Marcus huku simu ya Daudi Mbaga 

    ikiwa hewani, akakimbilia nje sehemu ambayo aliamini ni salama zaidi kuipokea

    “Nasikiliza” alisema Marcus

    “Binti Adela amefariki, mwili upo St. Augustino Hospital Kinondoni, wahi ukauchunguze Marcus” 

    Ilikua ni taarifa iliyomshtua Marcus, Adela alikua ni miongoni mwa Watu walio katika listi yake ya upelelezi ikiaminika kuwa ndiye aliyemuona Muuwaji kwa mujibu wa ripoti ya Daudi Mbaga.

    “Yule Binti amefariki?”

    “Ndiyo, nasikia kifo chake kimetokana na ndoto aliyoiota, hii haiwezekani Marcus, lipo jambo nyuma yake” 

    “Sawa, natoka hewani” alisema Marcus kisha alikata simu. Alichezesha kope za macho yake huku akiwa amejawa na Mshangao, watasemaje amefariki kutokana na ndoto tu? Hata yeye akatia walakini kua Muuwaji amerudi tena, hii ikaongeza joto zaidi la kuamini Sakina hakua Muuwaji halisi.

    Saa moja mbele, Marcus anafika Hospitali Kinondoni alipoelekezwa na Daudi Mbaga. Hakuwapigia simu wafiwa, alifika na kuuliza Mapokezi, kwanza alijitambulisha kua ni Askari polisi kisha alisema

    “Nimekuja kumtazama Mgonjwa anaitwa Adela kutoka katika familia ya Bilionea Yusuf” alisema, kwa heshima ya kazi yake, Binti aliye mapokezi akachota taarifa haraka kwenye kompyuta ili kujua kama walikua na Mgonjwa anayeitwa Adela kutokea kwenye familia ya kitajiri. 

    “Samahani, ameshafariki”

    “Mwili wake uko wapi?”

    “Mochwari daraja la kwanza”

    “Ahsante” akasema Jasusi Marcus, Yule Mdada akamuelekeza mahali ilipo Mochwari daraja la 

    kwanza ambalo Miili ya watu matajiri iliwekwa huko tena ilikua michache mno. Akaishika korido aliyoelekezwa, akiwa amebakisha hatua kadhaa kufika alipishana na Daktari Mmoja, akamsimamisha.

    Lengo la Marcus lilikua ni kumsalimia kisha amuulize kama Mochwari kuna waangalizi wa maiti, Daktari huyo alionekana kuwa mwenye hofu sana, mkononi alikua na Bahasha ya kaki iliyotuna.

    “Samahani, Naitwa Marcus ni afisa wa polisi. Nauliza kama muda huu kuna waangalizi wa maiti” alisema Marcus, yule Daktari wa kiume akawa anababaika kumjibu Marcus akionekana kujawa na woga fulani ndani yake hadi Marcus alishangaa, mara ile bahasha ilianguka na bunda moja la pesa likatoka, haraka yule Daktari akaliokota na kulirudisha kwenye Bahasha akioneka kuwa na hofu sana kisha akaondoka bila kumpa jibu la Uhakika.

    “Daktari anapata wapi bunda la pesa tena akiwa sehemu ya kazi?” alijiuliza Marcus kabla ya 

    kupuuzia, mawazo na akili yake yakawa kuelekea Mochwari. 

    Akafika mbele ya Mlango wa Mochwari, aliona mlango ulikua na upenyo fulani wa wazi ambao 

    ulionesha ndani, ilionekana aliyeingia au kutoka aliacha Mlango wazi, wakati analitafakari hilo 

    alimwona Mtu aliyefunika sura kwa kutumia kofia ya koti jeusi akiwa ana randa randa Mochwari 

    tena hakuonekana kabisa kuwa Daktari. 

    Mavazi pekee yalimfanya Marcus achomoe Bastola yake kisha taratibu akaufungua mlango huo 

    ambao ulionekana kumpa taarifa Mtu aliye ndani ya chumba hicho, naye akaganda huku akiwa 

    ameshikilia jokofu moja la kuhifadhia Maiti. 

    “Wewe ni Nani?” aliuliza Marcus, lakini Mtu huyo alionesha wazi kua ni Mwoga. Alikua akitetemeka, alikua amempa mgongo Marcus aliye mita kadhaa.

    “Nakuuliza tena, wewe ni Nani?” akahoji Marcus huku akiwa amenyoosha vizuri Bastola yake, kama alivyoambiwa na Daudi Mbaga naye hisia zake akazihamishia hivyo hivyo kua kifo cha Mtoto Adela si kifo cha Mshituko kama ambavyo ripoti ya Daktari ilisema, alihisi uwepo wa mambo yasiyo ya kawaida.

    “Geuka taratibu mikono ikiwa juu” akapaza sauti Marcus huku akiamini moja kwa moja kua huyo Mtu si Mzuri ndiyo maana alikua akipekua kwenye Majokofu hayo. Mtu huyo akageuka huku kichwa akiwa amekiinamishia chini, Marcus akamtaka ainue kichwa chake.

    Taratibu akainua kichwa akiwa anatetemeka, Marcus hakuyaamini macho yake. Mtu huyo alikua nani? ZIKIFIKA COMMENTS 100 naahia sehemu ya 11

     

    Jiunge WhatsApp Channel Ya KIJIWENI Ili Kuwa Wa Kwanza Kupata Updates Za RIWAYA Hii Kwa Kubonyeza Hapa 

    SOMA Uchambuzi Na Makala Mbalimbali Kwa Kubonyeza Hapa

     



     

    KOTI JEUSI Koti Jeusi Kijiweni riwaya ya koti jeusi

    61 Comments

    1. Ediger on May 7, 2024 10:23 am

      Hivi hizi story nzuri hivi mnazitoaga wapi

      Reply
      • Swamadu on May 7, 2024 10:38 am

        Ya leo imekuwa fupi sana kaka

        Reply
        • Ms chunnie on May 7, 2024 11:31 am

          Au alikua hamza jaman nna was was😅💔

          Reply
          • Ummy Mohammed on May 7, 2024 11:50 am

            Mhh atakua nani au mzee mwenyeweo

            Reply
      • Joseph on May 7, 2024 11:06 am

        Kila sku inazid kunoga

        Reply
      • Joseph Jackson on May 7, 2024 11:12 am

        Achia bhana admin
        Achia mzigo huo

        Reply
      • Rajity on May 7, 2024 4:26 pm

        Ya leo fupi sana km

        Reply
    2. Sencha bacsem on May 7, 2024 10:32 am

      Apo tunasema utamu unakata ebu malizieni hiyo ya 11 Tena ingewezekana mungetoa yote tu duh big up sana

      Reply
    3. 🌟 boe on May 7, 2024 10:34 am

      Doooh story Kali sana

      Reply
    4. Veronica kitundu on May 7, 2024 10:34 am

      Daah atakuwa ninani uyo

      Reply
    5. Mr dream on May 7, 2024 10:35 am

      Tamu

      Reply
    6. Becka on May 7, 2024 10:36 am

      Kaka upewe maua yako

      Reply
    7. Urban on May 7, 2024 10:50 am

      Leta mwendelezo

      Reply
      • Bastora mg ✍️ on May 8, 2024 1:45 pm

        🔥🔥🔥

        Reply
    8. Yg on May 7, 2024 10:50 am

      Daaah

      Reply
    9. Upcoming Billionaire on May 7, 2024 10:51 am

      Afu simulizi fupi hazileti ladha kabisa an story ndio inaanza kunoga kueleweka akn ndio ishafika mwisho

      Reply
    10. Christina on May 7, 2024 10:59 am

      Pokea mauwa yako ndugu duuuuh

      Reply
    11. Lizzy on May 7, 2024 11:02 am

      Noma sana 🙌🥰

      Reply
    12. Mugabo on May 7, 2024 11:06 am

      Daaah sana

      Reply
    13. richard on May 7, 2024 11:13 am

      Mbona fupi fupi tena

      Reply
    14. Ally Mnandowa on May 7, 2024 11:13 am

      Hauna bayaa

      Reply
    15. Asha on May 7, 2024 11:21 am

      Yaleo fupi mno😹😹😹anyway muuaji hopefully atapatkana sehem ya 11 tumechoka kuhisi

      Reply
    16. Mhe.Laizer on May 7, 2024 11:25 am

      Amazing novel

      Reply
    17. Mhe.Laizer on May 7, 2024 11:26 am

      Achilia tu bhnaaa

      Reply
    18. Husler on May 7, 2024 11:26 am

      Chap shekh tunasubiri

      Reply
    19. Ammar Hassanain on May 7, 2024 11:26 am

      Hatari faya, km nacheki movie aised

      Reply
    20. The chiza on May 7, 2024 11:27 am

      Nimeacha kuisoma maana sehm ya 9 haijatoka

      Reply
      • Mhariri on May 7, 2024 12:53 pm

        Habari Mdau Wa Kijiweni , Sehemu Ya 09 Imetoka Jana Saa 3 Usiku Unaweza Kuisoma Hapa KOTI JEUSI (Sehemu Ya Tisa) KOTI JEUSI – 09 ISOME HAPA ➡️➡️ https://www.kijiweni.co.tz/koti-jeusi-sehemu-ya-tisa-koti-jeusi-09/

        Reply
    21. Alli on May 7, 2024 11:43 am

      Mambo ni 🔥

      Reply
    22. Martin on May 7, 2024 11:49 am

      Story fupi ya leo

      Reply
    23. Contawa on May 7, 2024 11:49 am

      Big up

      Reply
    24. Rehema on May 7, 2024 11:50 am

      Fupi

      Reply
    25. matokeo tiganyilana David on May 7, 2024 11:51 am

      Daaah! kiongozi kazi ni nzuri sana

      Reply
    26. Liah on May 7, 2024 12:02 pm

      Upewe maua yako bt ziwe ndefu kidogo ya leo fup

      Reply
      • Muddy AS on May 7, 2024 1:13 pm

        Sophia anaonekana kuujua mchezo. Kama sio muuaji basi anamjua muuaji

        Reply
    27. Gabriel Marwa on May 7, 2024 12:10 pm

      🔥🔥🔥

      Reply
    28. Yusra cute on May 7, 2024 12:13 pm

      Umetubania

      Reply
    29. wittie on May 7, 2024 12:15 pm

      Nzuri sana

      Reply
    30. Lady G on May 7, 2024 12:21 pm

      Ya leo fupi sana jamaniii

      Reply
    31. Grey on May 7, 2024 12:27 pm

      Tisha asee achia

      Reply
    32. Joram on May 7, 2024 12:27 pm

      Dah hii story inasisismua balaaa

      Reply
    33. Valence on May 7, 2024 12:29 pm

      Aiseee chaaaap

      Reply
    34. Seb Jr. on May 7, 2024 12:29 pm

      Admin umepiga hasa. Maua kwako 💐💐

      Reply
    35. Mzopola Tobias on May 7, 2024 12:34 pm

      Moyo unatamani kusema ni Sofia ila ngoja nisubiri nione..

      Reply
    36. Rumbyambya Jr on May 7, 2024 12:38 pm

      Mbona kama ni Martha😂, honestly nahisi muuwaji ni Martha sema sehemu ya 11 muhimu Asmini bhn weee

      Reply
    37. Kibasa on May 7, 2024 1:03 pm

      Kwani haturuhusiwi kupata nyongeza ya siku🤗🤗🤗

      Reply
    38. Lamar on May 7, 2024 1:08 pm

      Mtunzi apewe maua yakee

      Reply
    39. Alhajmwema on May 7, 2024 3:18 pm

      🤝🏿

      Reply
    40. Patrick on May 7, 2024 3:27 pm

      Mh!

      Reply
    41. Fatuma Ngabo on May 7, 2024 3:45 pm

      Weka inayofuata please

      Reply
    42. Happie on May 7, 2024 3:48 pm

      Muuaji nahic ni martha🤔

      Reply
    43. PRINCE KEJALA on May 7, 2024 3:53 pm

      Jaman binti adela kwanin Mapema hv

      Reply
    44. Kuchii on May 7, 2024 4:12 pm

      Daaaaaaah aseeeee

      Reply
    45. Kenzoh on May 7, 2024 4:47 pm

      Ni fire

      Reply
    46. Hyerad on May 7, 2024 5:18 pm

      Shughuli imeshika moto

      Reply
    47. Sharyoon on May 7, 2024 5:36 pm

      Jamani mimi sehemu ya 8 na 9 sijazisomaaa

      Reply
    48. Enock S on May 7, 2024 7:30 pm

      Dondosha inayofuata

      Reply
    49. Stuart on May 7, 2024 7:53 pm

      Tupe 11

      Reply
    50. Idrissu on May 7, 2024 8:20 pm

      Duuuh 🔥🔥. Ila nmehuzunka sana kifo cha Adela 🤢

      Reply
    51. Msuya on May 7, 2024 8:44 pm

      Very dramatical and sensesional story!!!

      Reply
    52. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tatu) KOTI JEUSI – 14 - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.