Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 07

    Vilabu Vyamwaga Mabilioni Dirisha La Usajili EPL Likivunja Rekodi

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 06

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 07
    Hadithi

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 07

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 2, 2025Updated:September 2, 20253 Comments11 Mins Read861 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 06 

    Walipofika shangwe liliibuka kwa Wananchi waliamini kua kumwaga Damu  kutawasaidia Mji wao kuendelea kua na nguvu zaidi. Miongoni mwa Walioletwa 

    mbele ya Mfalme alikuwepo Mtoto Moana. Chozi lilimtoka Anna alipomwona  Moana akiwa amefungwa minyororo. 

    “Moana” aliita Anna kwa sauti ya Juu, Moana alimtazama Mama yake Kisha  alimpa tabasamu la matumaini. 

    Mfalme akawaambia walinzi kua Watu watatu watakua wa mwisho kuuawa  Asubuhi hiyo, Watu hao ni Moana, Anna na Zahoro. Walitengwa huku  wakishuhudia namna Watu wengine wakiuawa kwa kuchinjwa kama Kuku Kisha  Damu kutiwa kwenye chombo maalumu kwa ajili ya sadaka.  Endelea

    SEHEMU YA SABA

    Walikua wanauawa kikatili sana Kisha miili Yao kutupwa kwenye tanuli la moto,  ilikua ni kama Ibada kwao wakiaminishwa na Mganga Segebuka kua Damu hizo  zitafanya Mji wao kua na nguvu zaidi. 

    Mfalme alikuwa ameketi akivalia mavazi yenye kung’aa, mkononi alikua  ameshikilia kitu Fulani. Mtoto Moana alikua akilia Kila alivyoona Mtu akiuawa  mbele yake, ilikua kadhia kwake ila kwa Mfalme Selasi ilikua ni furaha kuona  anatowesha maono ya Segebuka kua atakuja Mtu kutoka kwenye Damu ya Mfalme  wa zamani kuchukua Ufalme. 

    Walipomaliza kuwaua wale wengine ilikua ni zamu ya akina Zahoro. Walisogezwa  wote watatu kwa pamoja, kabla zoezi halijaanza Mfalme akalisimamisha Kisha  akasema 

    “Nitaondoa Maisha Yao kwa Mikono yangu” Kisha akageuka kumtazama  Segebuka, ni kama walikua wamepanga jambo Fulani kwa pamoja. Shangwe na  vifijo viliendelea, wakifurahia kumwaga Damu walizoamini zimebeba Matumaini. 

    Mfalme Selasi akaagiza akina Zahoro wafungwe kwanza vitambaa vyeusi usoni ili  hukumu Yao ipite gizani mbele Yao. Mara Moja walifungwa vitambaa usoni ili  kuzuia macho Yao yasione chochote, katikati ya hofu na Mashaka ukimya  ulitawala kwa kiasi kikubwa, Kila mmoja alishangaa. 

    Mfalme Selasi alipanga Kuwauwa kwa kutumia Bastola lakini ilianza kusikika  sauti ya Kutisha iliyosambaa Kila kona, sauti hiyo ilikua ikisema 

    “Mwisho Umefika, mwisho Umefika, mwisho Umefika” Kila mmoja alijitahidi  kutafuta kwa macho ilipotokea sauti hiyo, lakini ilikua Kila Sehemu ya Mji wa  Patiosa

    Sauti hiyo ilisambaza woga, baadhi ya Watu walianza kukimbia kurejea Makwao,  Mfalme Selasi akachomoa Bastola na kumweka usoni Segebuka 

    “Ni sauti ya nini?” aliuliza Mfalme. Japo alikua anafanya yote lakini aliamini  anaweza kubadilisha hatima iliyosemwa na Mganga wake Segebuka. Jasho  likimbubujika, Segebuka akamwambia Mfalme Selasi 

    “Kama unaweza kunimaliza itakua vyema Mfalme kuliko kushuhudia Mapinduzi,  hatma haiko tena Upande wako. Unaangushwa” alisema Segebuka akiwa  anaonekana kukata tamaa na kua tayari kwa lolote lile litakalo tokea,  hakukwepesha macho yake Bali alikua akimtazama Mfalme tofauti na siku zote  alivyokua akimpa heshima ya Juu sana Mfalme kwa kutomtazama usoni.  

    “Ulisena tunaweza kubadilisha hatima, imekuaje?” Aliuliza Mfalme, sura yake  ilionesha ni namna gani alivyokua amechanganikiwa. Aliamini ana nguvu za  kupambana na yeyote atakayejitokeza mbele yake lakini Mtu pekee aliyempa  tumaini aliimaliza tumaini hiyo, mkono alioshikilia Bastola ulikua unatetemeka  sana. 

    Ile sauti ya ajabu ilizidi kusogea, haikua sauti ngeni kwa Zahoro na Anna, ilikua ni  sauti ya Alice pacha wa Anna. Alikua na nguvu ya kuitumia sauti yake kuangamiza  maadui zake. Kwa namna sauti ilivyokua inazidi kusogea karibu zaidi ilionesha  Alice alikua ameshafika ndani ya Mji wa Patiosa  

    Mfalme alishusha Bastola yake, Zahoro na Anna walitazamana Kisha Zahoro alikubali kumpokea Alice kwa mara ya kwanza licha ya kua aliuwa Watu wengi  sana. Chozi lilimbubujika Zahoro, Mtoto wao alikua amefungwa na mnyororo,  hakuna aliyeweza kumsaidia mwenzake isipokua kutazama mambo yalivyokua  yakiendelea. 

    Mfalme Selasi baada ya kuona mambo sio mazuri, akakimbilia ndani ili kuangalia  afanye nini. Upepo ulianza kuvuma kuashiria Alice alikua amefika, katikati ya  Upepo mkali akatokea Alice. 

    Askari wa Mfalme Selasi wakajaribu kupambana na Alice lakini ilikua ni  mpambano wa kujidanganya, Alice alikua na nguvu za ajabu, aliweza kuamrisha  jambo likatokea papo hapo. Kila askari aliyekutana na macho ya Alice aliugeuza  Upanga na kujimaliza.

    Watu waliobakia walianza kukimbia, Segebuka alisimama akimtazama Alice.  Kisha alipiga goti na kusema 

    “Sijawahi kupata kushuhudia Binadamu mwenye nguvu kama wewe.”  Akainamisha kichwa chake kumpa heshima, Alice hakuona kama ilikua ni sawa  kummaliza Segebuka, alimtazama tu Kisha aliikata minyororo iliyowashikilia  Anna, Zahoro na Moana Kisha akawaambia 

    “Tazameni nyuma yenu” walimwona Mfalme Selasi akiondoka kwa farasi kisha  lango la kuingilia Mji wa Patiosa lilifungwa. 

    “Tokeni hapa, Mimi nitapambana na hila zote za Mji huu, hakikisheni mnampata  Mfalme” alipomaliza kuongea walisikia sauti za Askari wakija Upande wao,  halikua kundi dogo Bali ni Maelfu ya Askari wa Mji wa Patiosa wakiwa na  Mapanga na Mikuki. 

    Anna na Zahoro kitu Cha kwanza kilikua kuhakiki kuhusu Hali ya Moana,  walimkumbatia kwa furaha sana Kisha Zahoro akasema 

    “Inabidi tulipate jicho la Mfalme Selasi, jicho pekee Ndilo ufunguo wa Lango la  Kuzimu” kwakua alikua na ramani ya Ufalme wote kutokana na maono ya ndoto  alizoota, alijua ni wapi kilipo chumba kilichohifadhi jicho Hilo la ajabu. 

    Zahoro alielekea ndani ya Jumba la Kifalme, alikutana na walinzi kadhaa lakini  alikua na mazoezi ya kupambana nao bila kupepesa macho, alikua fundi wa  kutumia Upanga. Alipopata nafasi ya kushikilia Upanga alihakikisha anamwaga  Damu Hadi kukifikia chumba Cha Mfalme Selasi. Alipofika hapo, aligundua  sanduku lilikua tupu 

    “Mfalme amechukua jicho, anaelekea kulifungua lango Kisha aondoke” alisema  Zahoro kwa sauti ya chini Kisha haraka alirudi alipomwacha Anna na Mtoto  Moana, wakati huo Alice alikua ameshikilia Upanga akipambana na Maelfu ya  Askari wa Patiosa. 

    “Inabidi tumfuate Mfalme” alisema Zahoro Kisha haraka walianza kukimbia  kuelekea eneo ambalo Farasi walikua wamefungiwa Kisha walichukua farasi  wawili, Anna na Mtoto walikwea farasi mmoja, Zahoro naye alikua juu ya Farasi  mwingine. 

    Waliondoka kulielekea lango ambalo lilikua na askari wa kutosha kwa ajili ya  kuwazuia.  

    Zahoro alining’inia kwenye farasi mithiri ya digidigi mwenye hasira Kisha alianza  kukata shingo za Askari kama feni, alipoinuka Upanga wake ulikua unamwagika  Damu. Moana alitabasamu akimwona Baba yake akipambana kwenye Uwanja wa  vita.  

    Kisha akiteremeka kwa Kasi na kumwachia farasi, alianza mapigano ya Upanga  kwa Kasi sana alihakikisha anaharakisha mpambano ili wamwahi Mfalme Selasi  aliyekua akikimbia. 

    Ndani ya dakika tatu zilitosha kwa Zahoro kumaliza kazi Kisha alilifungua lango  Kisha alimkwea farasi, wakaongoza njia pekee iliyokua ikitoka ndani ya Mji huo,  upande mwingine yalijaa Maji hivyo walikua na uhakika kua Mfalme aliitumia njia  hiyo kutokomea. 

    Aliongoza safari kwa kumliza farasi atembee kwa Kasi sana, nyuma yake Anna  pamoja na Moana walikua wakifuatia, Upanga uliendelea kusikika ndani ya Mji  wa Patiosa, Alice alikua akipambana na Maelfu ya Askari wa Mji huo. 

    Askari walikua wengi sana kiasi kwamba Alice alianza kuzidiwa, lakini Kila  alipokumbuka kuhusu kifo Cha Baba Yao na Mama yao ilimlazimu kuendelea  kupiga Upanga.  

    Upande wa pili, Zahoro alikua akikimbia na farasi kwa Kasi ya ajabu sana. Alijua  kama watamkosa Mfalme Selasi basi njia ya kuelekea Duniani isingelikuwepo tena  na pengine wangelisubiria kwa Miaka Mingi. 

    Farasi aliendelea kupiga kelele huku akikita kwato zake ardhini kwa kishindo  kizito sana, Kila hatua ilimfanya Zahoro avute Upepo mkali uliombatana na baridi  Kali la Msituni, Giza lilikua limetanda lakini macho makali ya Farasi yalikua  yakimulika mbele. 

    Baada ya kitambo kirefu, Farasi wa Zahoro aligoma kusonga mbele. Alikita miguu  yake na kufunga breki katikati ya Msitu ulio Kimya sana huku sauti pekee  iliyosikika baada ya Farasi kutulia ilikua ni sauti ya kusukumwa kwa majani  makavu. 

    Palikua kimya huku pakiwa na ishara ya jambo lisilo la kawaida, kusimama kwa  farasi kuliashiria jambo Fulani, Zahoro akashuka kutoka juu ya Farasi. Kisha  Upanga ukawa mkononi ili kujikinga na Adui atakaye jitokeza mbele yake. 

    Aliyalazimisha macho yake kutazama katikati ya Giza nene, hisia isiyo ya kawaida  ilimwambia asogee mbele zaidi kwa hatua takribani tano. 

    Aliposogea kidogo mbele akamwona Farasi akiwa amesimama kando ya njia.  Akajua sasa kua Mfalme Selasi hakua mbali na eneo Hilo, akatazama kulia Kisha  kushoto asijuwe Mfalme atakuwa ameelekea wapi. 

    Akajiuliza “Atakua upande upi?” akatikisa kope za macho yake kama aliyeingiwa  na mdudu hivi Kisha akaamua kuelekea Upande wa kulia ambako yule Farasi  alikuwepo, alizama Msituni huku akipapasia. Palikua Giza sana, alisonga mbele  huku akiamini kua Mfalme Selasi asingeliweza kujificha Bali aliingia Msituni  hapo kwa ajili ya jambo Fulani la Siri. 

    Taratibu alianza kuhisi Nuru machoni pake, alianza kuona mwangaza mkali sana.  Aliamua kuufuata mwanga ulio mbele yake, sasa alikua akiona Kila kitu hivyo  hata mwendo wake haukua mdogo. Alijua mwanga huo ulikua na uhusiano wa  moja kwa Moja na Mfalme Selasi. 

    Alikatiza Msitu, aliyapita Majani na nyasi kuufuata ule Mwanga. Hatimaye alifika  mahali ambapo palikua Ndiyo chanzo Cha huo mwanga, alimwona Mfalme Selasi  kwa mbali aliwa amesimama kando ya Mwanga kwenye Mti mkubwa wenye  Pango, Naam! Hapa ndipo ilipo njia ya kuelekea Duniani. 

    Mfalme Selasi alikuwa mwingi wa kuangalia huku na kule akionekana kusubiria  jambo Fulani hapo, Kisha Zahoro akakatiza bwawa dogo kwa haraka na kutokea  upande wa pili, akabakiza hatua chache kufika alipo Mfalme. 

    Aliushuhudia Upepo mkali sana ukitoka kwenye lile Pango, kiasi kwamba hata  kofia ya Kifalme ilimtoka Mfalme Selasi.  

    Zahoro akatambua sasa huwenda hiyo njia ilikua ikifunguka, lengo la Mfalme  lilikua ni Kukimbia kuelekea Duniani. 

    Haraka Zahoro akaanza kukimbia kwa Kasi kumfuata Mfalme ambaye alikua  akipiga hatua kuzama ndani ya Pango Hilo, kitendo bila kukawia haraka Zahoro akamfikia Mfalme na kumvuta Mkono, akamtoa ndani ya Pango

    Mkononi Mfalme Selasi alikua ameshikilia Bastola, akaielekeza kwa Zahoro  

    “Usijaribu kunizuia Kijana, nitakuuwa hapa na maiti Yako haitapatikana” alisema  Mfalme, akionekana kuvizia taratibu kwa jicho lake la kushoto akiangalia njia.  Zahoro akatazama namna Mlango ulivyokua ukifunguka 

    Wakati ambapo Kuzimu ilikua Usiku, upande wa Duniani ilikua ni Mchana. Aliona  Mabdhari ya kupendeza sana, lakini kizuizi kilikua ni Mfalme Selasi aliyeshikilia  Bastola. 

    Mfalme Selasi akaanza kurudi nyuma nyuma ili kuingia pangoni, Zahoro akapiga  mahesabu afanye nini ili amzuie Mfalme asiingia humo maana alijua fika kua  kama Mfalme ataingia na mlango utajifunga. 

    Licha ya kushikilia Bastola, mkono mwingine aliishikilia mfuko Fulani mweusi,  humo ndimo lilimo jicho la Mfalme lenye ufunguo wa kufunga na kufungua Njia  ya kuelekea Duniani, kutokana na papara na wasiwasi akajikuta akidondosha  mfuko huo 

    Akakaza Bastola kuelekea kwa Zahoro huku akipiga hesabu ya namna gani  ataokota Mfuko Kila hatua aliyoipiga, taratibu Zahoro naye alisogea. 

    “Usisogee Kijana nitakuuwa” akasema Mfalme Selasi, lakini Zahoro hakuacha  kupiga hatua za mgando. Kitendo Cha Mfalme Selasi kuinama aokote mfuko  akampa mwanya Zahoro kumfikia, papo hapo kabla hata Zahoro hajamgusa  Mfalme, akapigwa Risasi ya Bega. Kisha Mfalme akafyatua nyingine lakini bahati  mbaya kwake risasi zilikua zimeisha. 

    Zahoro alipoligundua Hilo akamvaa Mfalme na kuanza kumshushia kipigo kizito,  Kisha akauokota ule mfuko. Pale pale taratibu Lango la Kuzimu likaanza kujifunga  kwasababu hapakua na Mtu anayeingia humo. 

    Mfalme Selasi akiwa chini, Zahoro akiwa juu yake. Taratibu mkono wa Mfalme  Selasi ukapapasa pembeni na kuokota jiwe, Kisha akalipeleka usoni kwa Zahoro kwa nguvu. Akafanikiwa kumsukumiza Zahoro pembeni, Giza likaanza kuingia  hapo sababu mlango wa kutoka kuzimu ulishaanza kujifunga 

    Haraka Mfalme Selasi akiwa na wenge akaanza kutafuta ule mfuko wenye jicho  lake lenye Miujiza. Bahati nzuri kwake akafanikiwa kuupata, wakati huo Zahoro akiwa chini akigaa gaa kwa maumivu makali ya kupigwa na jiwe

    “Aaggghh‼” Mfalme Selasi akagugumia kidogo, akasogea kwenye mlango wa  kutokea Kuzimu Kisha akalitoa lile jicho kwenye mfuko, akalionyeshea kwenye  mlango 

    Lile jicho likawaka mwanga mwekundu, Kisha pole pole mlango wa Kuzimu  ukaanza kufunguka upya. Mfalme Selasi akaanza kufurahi, wakati huo mwanga  ulikua ukianza kutawala eneo lote kwasababu Mlango ulikua unafunguka. 

    Zahoro Kila alivyojaribu kunyanyuka alihisi kizungu-zungu, maumivu ya kichwa.  Ulikua ni wakati wa Mfalme Selasi kuondoka. Akageuka kumtazama Zahoro Kisha  akamwambia 

    “Utaishi Kuzimu Milele” akamalizia kwa Kicheko kikubwa, Ghafla Mfalme Selasi  akapigwa Mshale Mgongoni, akapigwa na Mshale mwingine bega la kulia na  mwingine bega la Kushoto. 

    Zahoro alipoangalia ni Nani aliyemshambulia alimwona Anna akiwa ameshikilia  Mshale, kando yake yupo Moana. Alijikuta akiachia tabasamu la furaha na  maumivu 

    Mfalme Selasi licha ya kupigwa Mshale na kuanguka chini, Bado alianza  kujiburuza ili atoke Kuzimu, lakini Zahoro alimzuia kwa kumvuta nyuma Kisha  akamwambia 

    “Wewe ndiye utakayeishi Kuzimu Milele” mara Anna na Moana walifika na  kulichukua jicho kutoka kwa Mfalme Selasi.  

    “Utalipa kwa kifo Cha Wazazi Wangu, kama ulivyofanya kwetu ndivyo  tutakavyofanya kwako pia.” Alisema Anna, Mfalme Selasi akamwambia Anna 

    “Najua unachokitafuta ni Nini Ndiyo maana unataka kwenda Duniani, lakini wewe  si wa huko. Wewe ni Mali ya Kuzimu” Anna alikunja uso wake Kisha akamuuliza 

    “Unajua nini wewe?” Wakati huo Damu nyingi zilikua zikimtoka Mfalme Selasi,  akamwambia Anna 

    “Unaenda kutafuta Pete ya Baba Yako, Mimi naijua ilipo. Namjua anayeitumia  huko Duniani, bila Mimi kamwe hutoipata” Anna aligeuka akamtazama Zahoro Kisha Zahoro akamuuliza Mfalme Selasi

    “Kama utasema ilipo basi nitakupatia jicho lako. Utajitibia na kupona, ipo kwa  Nani?” Mfalme Selasi akaachia Kicheko Cha maumivu huku Damu ikimtoka  Mdomoni. 

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya NANE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx 

     

    riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua soma riwaya bure

    3 Comments

    1. Marcel3316 on September 2, 2025 4:53 pm

      https://shorturl.fm/ptAnw

      Reply
    2. Reginald McGlynn on September 2, 2025 7:36 pm

      Your blog is a beacon of light in the often murky waters of online content. Your thoughtful analysis and insightful commentary never fail to leave a lasting impression. Keep up the amazing work!

      Reply
    3. Columbus Little on September 3, 2025 3:40 am

      Wonderful web site Lots of useful info here Im sending it to a few friends ans additionally sharing in delicious And obviously thanks to your effort

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 2, 2025

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 07

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 06  Walipofika shangwe liliibuka kwa Wananchi waliamini kua kumwaga Damu …

    Vilabu Vyamwaga Mabilioni Dirisha La Usajili EPL Likivunja Rekodi

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 06

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 05

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.