Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 06Β
Walipofika shangwe liliibuka kwa Wananchi waliamini kua kumwaga DamuΒ kutawasaidia Mji wao kuendelea kua na nguvu zaidi. Miongoni mwa WalioletwaΒ
mbele ya Mfalme alikuwepo Mtoto Moana. Chozi lilimtoka Anna alipomwonaΒ Moana akiwa amefungwa minyororo.Β
βMoanaβ aliita Anna kwa sauti ya Juu, Moana alimtazama Mama yake KishaΒ alimpa tabasamu la matumaini.Β
Mfalme akawaambia walinzi kua Watu watatu watakua wa mwisho kuuawaΒ Asubuhi hiyo, Watu hao ni Moana, Anna na Zahoro. Walitengwa hukuΒ wakishuhudia namna Watu wengine wakiuawa kwa kuchinjwa kama Kuku KishaΒ Damu kutiwa kwenye chombo maalumu kwa ajili ya sadaka.Β Endelea
SEHEMU YA SABA
Walikua wanauawa kikatili sana Kisha miili Yao kutupwa kwenye tanuli la moto,Β ilikua ni kama Ibada kwao wakiaminishwa na Mganga Segebuka kua Damu hizoΒ zitafanya Mji wao kua na nguvu zaidi.Β
Mfalme alikuwa ameketi akivalia mavazi yenye kungβaa, mkononi alikuaΒ ameshikilia kitu Fulani. Mtoto Moana alikua akilia Kila alivyoona Mtu akiuawaΒ mbele yake, ilikua kadhia kwake ila kwa Mfalme Selasi ilikua ni furaha kuonaΒ anatowesha maono ya Segebuka kua atakuja Mtu kutoka kwenye Damu ya MfalmeΒ wa zamani kuchukua Ufalme.Β
Walipomaliza kuwaua wale wengine ilikua ni zamu ya akina Zahoro. WalisogezwaΒ wote watatu kwa pamoja, kabla zoezi halijaanza Mfalme akalisimamisha KishaΒ akasemaΒ
βNitaondoa Maisha Yao kwa Mikono yanguβ Kisha akageuka kumtazamaΒ Segebuka, ni kama walikua wamepanga jambo Fulani kwa pamoja. Shangwe naΒ vifijo viliendelea, wakifurahia kumwaga Damu walizoamini zimebeba Matumaini.Β
Mfalme Selasi akaagiza akina Zahoro wafungwe kwanza vitambaa vyeusi usoni iliΒ hukumu Yao ipite gizani mbele Yao. Mara Moja walifungwa vitambaa usoni iliΒ kuzuia macho Yao yasione chochote, katikati ya hofu na Mashaka ukimyaΒ ulitawala kwa kiasi kikubwa, Kila mmoja alishangaa.Β
Mfalme Selasi alipanga Kuwauwa kwa kutumia Bastola lakini ilianza kusikikaΒ sauti ya Kutisha iliyosambaa Kila kona, sauti hiyo ilikua ikisemaΒ
βMwisho Umefika, mwisho Umefika, mwisho Umefikaβ Kila mmoja alijitahidiΒ kutafuta kwa macho ilipotokea sauti hiyo, lakini ilikua Kila Sehemu ya Mji waΒ Patiosa
Sauti hiyo ilisambaza woga, baadhi ya Watu walianza kukimbia kurejea Makwao,Β Mfalme Selasi akachomoa Bastola na kumweka usoni SegebukaΒ
βNi sauti ya nini?β aliuliza Mfalme. Japo alikua anafanya yote lakini aliaminiΒ anaweza kubadilisha hatima iliyosemwa na Mganga wake Segebuka. JashoΒ likimbubujika, Segebuka akamwambia Mfalme SelasiΒ
βKama unaweza kunimaliza itakua vyema Mfalme kuliko kushuhudia Mapinduzi,Β hatma haiko tena Upande wako. Unaangushwaβ alisema Segebuka akiwaΒ anaonekana kukata tamaa na kua tayari kwa lolote lile litakalo tokea,Β hakukwepesha macho yake Bali alikua akimtazama Mfalme tofauti na siku zoteΒ alivyokua akimpa heshima ya Juu sana Mfalme kwa kutomtazama usoni.Β Β
βUlisena tunaweza kubadilisha hatima, imekuaje?β Aliuliza Mfalme, sura yakeΒ ilionesha ni namna gani alivyokua amechanganikiwa. Aliamini ana nguvu zaΒ kupambana na yeyote atakayejitokeza mbele yake lakini Mtu pekee aliyempaΒ tumaini aliimaliza tumaini hiyo, mkono alioshikilia Bastola ulikua unatetemekaΒ sana.Β
Ile sauti ya ajabu ilizidi kusogea, haikua sauti ngeni kwa Zahoro na Anna, ilikua niΒ sauti ya Alice pacha wa Anna. Alikua na nguvu ya kuitumia sauti yake kuangamizaΒ maadui zake. Kwa namna sauti ilivyokua inazidi kusogea karibu zaidi ilioneshaΒ Alice alikua ameshafika ndani ya Mji wa PatiosaΒ Β
Mfalme alishusha Bastola yake, Zahoro na Anna walitazamana Kisha Zahoro alikubali kumpokea Alice kwa mara ya kwanza licha ya kua aliuwa Watu wengiΒ sana. Chozi lilimbubujika Zahoro, Mtoto wao alikua amefungwa na mnyororo,Β hakuna aliyeweza kumsaidia mwenzake isipokua kutazama mambo yalivyokuaΒ yakiendelea.Β
Mfalme Selasi baada ya kuona mambo sio mazuri, akakimbilia ndani ili kuangaliaΒ afanye nini. Upepo ulianza kuvuma kuashiria Alice alikua amefika, katikati yaΒ Upepo mkali akatokea Alice.Β
Askari wa Mfalme Selasi wakajaribu kupambana na Alice lakini ilikua niΒ mpambano wa kujidanganya, Alice alikua na nguvu za ajabu, aliweza kuamrishaΒ jambo likatokea papo hapo. Kila askari aliyekutana na macho ya Alice aliugeuzaΒ Upanga na kujimaliza.
Watu waliobakia walianza kukimbia, Segebuka alisimama akimtazama Alice.Β Kisha alipiga goti na kusemaΒ
βSijawahi kupata kushuhudia Binadamu mwenye nguvu kama wewe.βΒ Akainamisha kichwa chake kumpa heshima, Alice hakuona kama ilikua ni sawaΒ kummaliza Segebuka, alimtazama tu Kisha aliikata minyororo iliyowashikiliaΒ Anna, Zahoro na Moana Kisha akawaambiaΒ
βTazameni nyuma yenuβ walimwona Mfalme Selasi akiondoka kwa farasi kishaΒ lango la kuingilia Mji wa Patiosa lilifungwa.Β
βTokeni hapa, Mimi nitapambana na hila zote za Mji huu, hakikisheni mnampataΒ Mfalmeβ alipomaliza kuongea walisikia sauti za Askari wakija Upande wao,Β halikua kundi dogo Bali ni Maelfu ya Askari wa Mji wa Patiosa wakiwa naΒ Mapanga na Mikuki.Β
Anna na Zahoro kitu Cha kwanza kilikua kuhakiki kuhusu Hali ya Moana,Β walimkumbatia kwa furaha sana Kisha Zahoro akasemaΒ
βInabidi tulipate jicho la Mfalme Selasi, jicho pekee Ndilo ufunguo wa Lango laΒ Kuzimuβ kwakua alikua na ramani ya Ufalme wote kutokana na maono ya ndotoΒ alizoota, alijua ni wapi kilipo chumba kilichohifadhi jicho Hilo la ajabu.Β
Zahoro alielekea ndani ya Jumba la Kifalme, alikutana na walinzi kadhaa lakiniΒ alikua na mazoezi ya kupambana nao bila kupepesa macho, alikua fundi waΒ kutumia Upanga. Alipopata nafasi ya kushikilia Upanga alihakikisha anamwagaΒ Damu Hadi kukifikia chumba Cha Mfalme Selasi. Alipofika hapo, aligunduaΒ sanduku lilikua tupuΒ
βMfalme amechukua jicho, anaelekea kulifungua lango Kisha aondokeβ alisemaΒ Zahoro kwa sauti ya chini Kisha haraka alirudi alipomwacha Anna na MtotoΒ Moana, wakati huo Alice alikua ameshikilia Upanga akipambana na Maelfu yaΒ Askari wa Patiosa.Β
βInabidi tumfuate Mfalmeβ alisema Zahoro Kisha haraka walianza kukimbiaΒ kuelekea eneo ambalo Farasi walikua wamefungiwa Kisha walichukua farasiΒ wawili, Anna na Mtoto walikwea farasi mmoja, Zahoro naye alikua juu ya FarasiΒ mwingine.Β
Waliondoka kulielekea lango ambalo lilikua na askari wa kutosha kwa ajili yaΒ kuwazuia.Β Β
Zahoro aliningβinia kwenye farasi mithiri ya digidigi mwenye hasira Kisha alianzaΒ kukata shingo za Askari kama feni, alipoinuka Upanga wake ulikua unamwagikaΒ Damu. Moana alitabasamu akimwona Baba yake akipambana kwenye Uwanja waΒ vita.Β Β
Kisha akiteremeka kwa Kasi na kumwachia farasi, alianza mapigano ya UpangaΒ kwa Kasi sana alihakikisha anaharakisha mpambano ili wamwahi Mfalme SelasiΒ aliyekua akikimbia.Β
Ndani ya dakika tatu zilitosha kwa Zahoro kumaliza kazi Kisha alilifungua langoΒ Kisha alimkwea farasi, wakaongoza njia pekee iliyokua ikitoka ndani ya Mji huo,Β upande mwingine yalijaa Maji hivyo walikua na uhakika kua Mfalme aliitumia njiaΒ hiyo kutokomea.Β
Aliongoza safari kwa kumliza farasi atembee kwa Kasi sana, nyuma yake AnnaΒ pamoja na Moana walikua wakifuatia, Upanga uliendelea kusikika ndani ya MjiΒ wa Patiosa, Alice alikua akipambana na Maelfu ya Askari wa Mji huo.Β
Askari walikua wengi sana kiasi kwamba Alice alianza kuzidiwa, lakini KilaΒ alipokumbuka kuhusu kifo Cha Baba Yao na Mama yao ilimlazimu kuendeleaΒ kupiga Upanga.Β Β
Upande wa pili, Zahoro alikua akikimbia na farasi kwa Kasi ya ajabu sana. AlijuaΒ kama watamkosa Mfalme Selasi basi njia ya kuelekea Duniani isingelikuwepo tenaΒ na pengine wangelisubiria kwa Miaka Mingi.Β
Farasi aliendelea kupiga kelele huku akikita kwato zake ardhini kwa kishindoΒ kizito sana, Kila hatua ilimfanya Zahoro avute Upepo mkali uliombatana na baridiΒ Kali la Msituni, Giza lilikua limetanda lakini macho makali ya Farasi yalikuaΒ yakimulika mbele.Β
Baada ya kitambo kirefu, Farasi wa Zahoro aligoma kusonga mbele. Alikita miguuΒ yake na kufunga breki katikati ya Msitu ulio Kimya sana huku sauti pekeeΒ iliyosikika baada ya Farasi kutulia ilikua ni sauti ya kusukumwa kwa majaniΒ makavu.Β
Palikua kimya huku pakiwa na ishara ya jambo lisilo la kawaida, kusimama kwaΒ farasi kuliashiria jambo Fulani, Zahoro akashuka kutoka juu ya Farasi. KishaΒ Upanga ukawa mkononi ili kujikinga na Adui atakaye jitokeza mbele yake.Β
Aliyalazimisha macho yake kutazama katikati ya Giza nene, hisia isiyo ya kawaidaΒ ilimwambia asogee mbele zaidi kwa hatua takribani tano.Β
Aliposogea kidogo mbele akamwona Farasi akiwa amesimama kando ya njia.Β Akajua sasa kua Mfalme Selasi hakua mbali na eneo Hilo, akatazama kulia KishaΒ kushoto asijuwe Mfalme atakuwa ameelekea wapi.Β
Akajiuliza βAtakua upande upi?β akatikisa kope za macho yake kama aliyeingiwaΒ na mdudu hivi Kisha akaamua kuelekea Upande wa kulia ambako yule FarasiΒ alikuwepo, alizama Msituni huku akipapasia. Palikua Giza sana, alisonga mbeleΒ huku akiamini kua Mfalme Selasi asingeliweza kujificha Bali aliingia MsituniΒ hapo kwa ajili ya jambo Fulani la Siri.Β
Taratibu alianza kuhisi Nuru machoni pake, alianza kuona mwangaza mkali sana.Β Aliamua kuufuata mwanga ulio mbele yake, sasa alikua akiona Kila kitu hivyoΒ hata mwendo wake haukua mdogo. Alijua mwanga huo ulikua na uhusiano waΒ moja kwa Moja na Mfalme Selasi.Β
Alikatiza Msitu, aliyapita Majani na nyasi kuufuata ule Mwanga. Hatimaye alifikaΒ mahali ambapo palikua Ndiyo chanzo Cha huo mwanga, alimwona Mfalme SelasiΒ kwa mbali aliwa amesimama kando ya Mwanga kwenye Mti mkubwa wenyeΒ Pango, Naam! Hapa ndipo ilipo njia ya kuelekea Duniani.Β
Mfalme Selasi alikuwa mwingi wa kuangalia huku na kule akionekana kusubiriaΒ jambo Fulani hapo, Kisha Zahoro akakatiza bwawa dogo kwa haraka na kutokeaΒ upande wa pili, akabakiza hatua chache kufika alipo Mfalme.Β
Aliushuhudia Upepo mkali sana ukitoka kwenye lile Pango, kiasi kwamba hataΒ kofia ya Kifalme ilimtoka Mfalme Selasi.Β Β
Zahoro akatambua sasa huwenda hiyo njia ilikua ikifunguka, lengo la MfalmeΒ lilikua ni Kukimbia kuelekea Duniani.Β
Haraka Zahoro akaanza kukimbia kwa Kasi kumfuata Mfalme ambaye alikuaΒ akipiga hatua kuzama ndani ya Pango Hilo, kitendo bila kukawia haraka Zahoro akamfikia Mfalme na kumvuta Mkono, akamtoa ndani ya Pango
Mkononi Mfalme Selasi alikua ameshikilia Bastola, akaielekeza kwa ZahoroΒ Β
βUsijaribu kunizuia Kijana, nitakuuwa hapa na maiti Yako haitapatikanaβ alisemaΒ Mfalme, akionekana kuvizia taratibu kwa jicho lake la kushoto akiangalia njia.Β Zahoro akatazama namna Mlango ulivyokua ukifungukaΒ
Wakati ambapo Kuzimu ilikua Usiku, upande wa Duniani ilikua ni Mchana. AlionaΒ Mabdhari ya kupendeza sana, lakini kizuizi kilikua ni Mfalme Selasi aliyeshikiliaΒ Bastola.Β
Mfalme Selasi akaanza kurudi nyuma nyuma ili kuingia pangoni, Zahoro akapigaΒ mahesabu afanye nini ili amzuie Mfalme asiingia humo maana alijua fika kuaΒ kama Mfalme ataingia na mlango utajifunga.Β
Licha ya kushikilia Bastola, mkono mwingine aliishikilia mfuko Fulani mweusi,Β humo ndimo lilimo jicho la Mfalme lenye ufunguo wa kufunga na kufungua NjiaΒ ya kuelekea Duniani, kutokana na papara na wasiwasi akajikuta akidondoshaΒ mfuko huoΒ
Akakaza Bastola kuelekea kwa Zahoro huku akipiga hesabu ya namna ganiΒ ataokota Mfuko Kila hatua aliyoipiga, taratibu Zahoro naye alisogea.Β
βUsisogee Kijana nitakuuwaβ akasema Mfalme Selasi, lakini Zahoro hakuachaΒ kupiga hatua za mgando. Kitendo Cha Mfalme Selasi kuinama aokote mfukoΒ akampa mwanya Zahoro kumfikia, papo hapo kabla hata Zahoro hajamgusaΒ Mfalme, akapigwa Risasi ya Bega. Kisha Mfalme akafyatua nyingine lakini bahatiΒ mbaya kwake risasi zilikua zimeisha.Β
Zahoro alipoligundua Hilo akamvaa Mfalme na kuanza kumshushia kipigo kizito,Β Kisha akauokota ule mfuko. Pale pale taratibu Lango la Kuzimu likaanza kujifungaΒ kwasababu hapakua na Mtu anayeingia humo.Β
Mfalme Selasi akiwa chini, Zahoro akiwa juu yake. Taratibu mkono wa MfalmeΒ Selasi ukapapasa pembeni na kuokota jiwe, Kisha akalipeleka usoni kwa Zahoro kwa nguvu. Akafanikiwa kumsukumiza Zahoro pembeni, Giza likaanza kuingiaΒ hapo sababu mlango wa kutoka kuzimu ulishaanza kujifungaΒ
Haraka Mfalme Selasi akiwa na wenge akaanza kutafuta ule mfuko wenye jichoΒ lake lenye Miujiza. Bahati nzuri kwake akafanikiwa kuupata, wakati huo Zahoro akiwa chini akigaa gaa kwa maumivu makali ya kupigwa na jiwe
βAaggghhβΌβ Mfalme Selasi akagugumia kidogo, akasogea kwenye mlango waΒ kutokea Kuzimu Kisha akalitoa lile jicho kwenye mfuko, akalionyeshea kwenyeΒ mlangoΒ
Lile jicho likawaka mwanga mwekundu, Kisha pole pole mlango wa KuzimuΒ ukaanza kufunguka upya. Mfalme Selasi akaanza kufurahi, wakati huo mwangaΒ ulikua ukianza kutawala eneo lote kwasababu Mlango ulikua unafunguka.Β
Zahoro Kila alivyojaribu kunyanyuka alihisi kizungu-zungu, maumivu ya kichwa.Β Ulikua ni wakati wa Mfalme Selasi kuondoka. Akageuka kumtazama Zahoro KishaΒ akamwambiaΒ
βUtaishi Kuzimu Mileleβ akamalizia kwa Kicheko kikubwa, Ghafla Mfalme SelasiΒ akapigwa Mshale Mgongoni, akapigwa na Mshale mwingine bega la kulia naΒ mwingine bega la Kushoto.Β
Zahoro alipoangalia ni Nani aliyemshambulia alimwona Anna akiwa ameshikiliaΒ Mshale, kando yake yupo Moana. Alijikuta akiachia tabasamu la furaha naΒ maumivuΒ
Mfalme Selasi licha ya kupigwa Mshale na kuanguka chini, Bado alianzaΒ kujiburuza ili atoke Kuzimu, lakini Zahoro alimzuia kwa kumvuta nyuma KishaΒ akamwambiaΒ
βWewe ndiye utakayeishi Kuzimu Mileleβ mara Anna na Moana walifika naΒ kulichukua jicho kutoka kwa Mfalme Selasi.Β Β
βUtalipa kwa kifo Cha Wazazi Wangu, kama ulivyofanya kwetu ndivyoΒ tutakavyofanya kwako pia.β Alisema Anna, Mfalme Selasi akamwambia AnnaΒ
βNajua unachokitafuta ni Nini Ndiyo maana unataka kwenda Duniani, lakini weweΒ si wa huko. Wewe ni Mali ya Kuzimuβ Anna alikunja uso wake Kisha akamuulizaΒ
βUnajua nini wewe?β Wakati huo Damu nyingi zilikua zikimtoka Mfalme Selasi,Β akamwambia AnnaΒ
βUnaenda kutafuta Pete ya Baba Yako, Mimi naijua ilipo. Namjua anayeitumiaΒ huko Duniani, bila Mimi kamwe hutoipataβ Anna aligeuka akamtazama Zahoro Kisha Zahoro akamuuliza Mfalme Selasi
βKama utasema ilipo basi nitakupatia jicho lako. Utajitibia na kupona, ipo kwaΒ Nani?β Mfalme Selasi akaachia Kicheko Cha maumivu huku Damu ikimtokaΒ Mdomoni.Β
Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya NANE
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β
Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xxΒ
24 Comments
https://shorturl.fm/ptAnw
Your blog is a beacon of light in the often murky waters of online content. Your thoughtful analysis and insightful commentary never fail to leave a lasting impression. Keep up the amazing work!
Wonderful web site Lots of useful info here Im sending it to a few friends ans additionally sharing in delicious And obviously thanks to your effort
https://shorturl.fm/PabqU
https://shorturl.fm/PabqU
https://shorturl.fm/zbbOE
https://shorturl.fm/87tZT
https://shorturl.fm/aFvIH
ek4nwk
https://shorturl.fm/IFCJA
sihv1d
https://shorturl.fm/LB0YC
https://shorturl.fm/nNcA0
https://shorturl.fm/vWXDi
https://shorturl.fm/B4693
https://shorturl.fm/FXH4A
https://shorturl.fm/tL4gk
https://shorturl.fm/V8XXo
https://shorturl.fm/yJ1gB
https://shorturl.fm/AIA9W
u6jlti
https://shorturl.fm/LWoaD
https://shorturl.fm/0933z
**mind vault**
mind vault is a premium cognitive support formula created for adults 45+. Itβs thoughtfully designed to help maintain clear thinking