Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 07
    Hadithi

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 07

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 2, 2025Updated:September 2, 202524 Comments11 Mins Read868 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 06Β 

    Walipofika shangwe liliibuka kwa Wananchi waliamini kua kumwaga DamuΒ  kutawasaidia Mji wao kuendelea kua na nguvu zaidi. Miongoni mwa WalioletwaΒ 

    mbele ya Mfalme alikuwepo Mtoto Moana. Chozi lilimtoka Anna alipomwonaΒ  Moana akiwa amefungwa minyororo.Β 

    β€œMoana” aliita Anna kwa sauti ya Juu, Moana alimtazama Mama yake KishaΒ  alimpa tabasamu la matumaini.Β 

    Mfalme akawaambia walinzi kua Watu watatu watakua wa mwisho kuuawaΒ  Asubuhi hiyo, Watu hao ni Moana, Anna na Zahoro. Walitengwa hukuΒ  wakishuhudia namna Watu wengine wakiuawa kwa kuchinjwa kama Kuku KishaΒ  Damu kutiwa kwenye chombo maalumu kwa ajili ya sadaka.Β  Endelea

    SEHEMU YA SABA

    Walikua wanauawa kikatili sana Kisha miili Yao kutupwa kwenye tanuli la moto,Β  ilikua ni kama Ibada kwao wakiaminishwa na Mganga Segebuka kua Damu hizoΒ  zitafanya Mji wao kua na nguvu zaidi.Β 

    Mfalme alikuwa ameketi akivalia mavazi yenye kung’aa, mkononi alikuaΒ  ameshikilia kitu Fulani. Mtoto Moana alikua akilia Kila alivyoona Mtu akiuawaΒ  mbele yake, ilikua kadhia kwake ila kwa Mfalme Selasi ilikua ni furaha kuonaΒ  anatowesha maono ya Segebuka kua atakuja Mtu kutoka kwenye Damu ya MfalmeΒ  wa zamani kuchukua Ufalme.Β 

    Walipomaliza kuwaua wale wengine ilikua ni zamu ya akina Zahoro. WalisogezwaΒ  wote watatu kwa pamoja, kabla zoezi halijaanza Mfalme akalisimamisha KishaΒ  akasemaΒ 

    β€œNitaondoa Maisha Yao kwa Mikono yangu” Kisha akageuka kumtazamaΒ  Segebuka, ni kama walikua wamepanga jambo Fulani kwa pamoja. Shangwe naΒ  vifijo viliendelea, wakifurahia kumwaga Damu walizoamini zimebeba Matumaini.Β 

    Mfalme Selasi akaagiza akina Zahoro wafungwe kwanza vitambaa vyeusi usoni iliΒ  hukumu Yao ipite gizani mbele Yao. Mara Moja walifungwa vitambaa usoni iliΒ  kuzuia macho Yao yasione chochote, katikati ya hofu na Mashaka ukimyaΒ  ulitawala kwa kiasi kikubwa, Kila mmoja alishangaa.Β 

    Mfalme Selasi alipanga Kuwauwa kwa kutumia Bastola lakini ilianza kusikikaΒ  sauti ya Kutisha iliyosambaa Kila kona, sauti hiyo ilikua ikisemaΒ 

    β€œMwisho Umefika, mwisho Umefika, mwisho Umefika” Kila mmoja alijitahidiΒ  kutafuta kwa macho ilipotokea sauti hiyo, lakini ilikua Kila Sehemu ya Mji waΒ  Patiosa

    Sauti hiyo ilisambaza woga, baadhi ya Watu walianza kukimbia kurejea Makwao,Β  Mfalme Selasi akachomoa Bastola na kumweka usoni SegebukaΒ 

    β€œNi sauti ya nini?” aliuliza Mfalme. Japo alikua anafanya yote lakini aliaminiΒ  anaweza kubadilisha hatima iliyosemwa na Mganga wake Segebuka. JashoΒ  likimbubujika, Segebuka akamwambia Mfalme SelasiΒ 

    β€œKama unaweza kunimaliza itakua vyema Mfalme kuliko kushuhudia Mapinduzi,Β  hatma haiko tena Upande wako. Unaangushwa” alisema Segebuka akiwaΒ  anaonekana kukata tamaa na kua tayari kwa lolote lile litakalo tokea,Β  hakukwepesha macho yake Bali alikua akimtazama Mfalme tofauti na siku zoteΒ  alivyokua akimpa heshima ya Juu sana Mfalme kwa kutomtazama usoni.Β Β 

    β€œUlisena tunaweza kubadilisha hatima, imekuaje?” Aliuliza Mfalme, sura yakeΒ  ilionesha ni namna gani alivyokua amechanganikiwa. Aliamini ana nguvu zaΒ  kupambana na yeyote atakayejitokeza mbele yake lakini Mtu pekee aliyempaΒ  tumaini aliimaliza tumaini hiyo, mkono alioshikilia Bastola ulikua unatetemekaΒ  sana.Β 

    Ile sauti ya ajabu ilizidi kusogea, haikua sauti ngeni kwa Zahoro na Anna, ilikua niΒ  sauti ya Alice pacha wa Anna. Alikua na nguvu ya kuitumia sauti yake kuangamizaΒ  maadui zake. Kwa namna sauti ilivyokua inazidi kusogea karibu zaidi ilioneshaΒ  Alice alikua ameshafika ndani ya Mji wa PatiosaΒ Β 

    Mfalme alishusha Bastola yake, Zahoro na Anna walitazamana Kisha Zahoro alikubali kumpokea Alice kwa mara ya kwanza licha ya kua aliuwa Watu wengiΒ  sana. Chozi lilimbubujika Zahoro, Mtoto wao alikua amefungwa na mnyororo,Β  hakuna aliyeweza kumsaidia mwenzake isipokua kutazama mambo yalivyokuaΒ  yakiendelea.Β 

    Mfalme Selasi baada ya kuona mambo sio mazuri, akakimbilia ndani ili kuangaliaΒ  afanye nini. Upepo ulianza kuvuma kuashiria Alice alikua amefika, katikati yaΒ  Upepo mkali akatokea Alice.Β 

    Askari wa Mfalme Selasi wakajaribu kupambana na Alice lakini ilikua niΒ  mpambano wa kujidanganya, Alice alikua na nguvu za ajabu, aliweza kuamrishaΒ  jambo likatokea papo hapo. Kila askari aliyekutana na macho ya Alice aliugeuzaΒ  Upanga na kujimaliza.

    Watu waliobakia walianza kukimbia, Segebuka alisimama akimtazama Alice.Β  Kisha alipiga goti na kusemaΒ 

    β€œSijawahi kupata kushuhudia Binadamu mwenye nguvu kama wewe.”  Akainamisha kichwa chake kumpa heshima, Alice hakuona kama ilikua ni sawaΒ  kummaliza Segebuka, alimtazama tu Kisha aliikata minyororo iliyowashikiliaΒ  Anna, Zahoro na Moana Kisha akawaambiaΒ 

    β€œTazameni nyuma yenu” walimwona Mfalme Selasi akiondoka kwa farasi kishaΒ  lango la kuingilia Mji wa Patiosa lilifungwa.Β 

    β€œTokeni hapa, Mimi nitapambana na hila zote za Mji huu, hakikisheni mnampataΒ  Mfalme” alipomaliza kuongea walisikia sauti za Askari wakija Upande wao,Β  halikua kundi dogo Bali ni Maelfu ya Askari wa Mji wa Patiosa wakiwa naΒ  Mapanga na Mikuki.Β 

    Anna na Zahoro kitu Cha kwanza kilikua kuhakiki kuhusu Hali ya Moana,Β  walimkumbatia kwa furaha sana Kisha Zahoro akasemaΒ 

    β€œInabidi tulipate jicho la Mfalme Selasi, jicho pekee Ndilo ufunguo wa Lango laΒ  Kuzimu” kwakua alikua na ramani ya Ufalme wote kutokana na maono ya ndotoΒ  alizoota, alijua ni wapi kilipo chumba kilichohifadhi jicho Hilo la ajabu.Β 

    Zahoro alielekea ndani ya Jumba la Kifalme, alikutana na walinzi kadhaa lakiniΒ  alikua na mazoezi ya kupambana nao bila kupepesa macho, alikua fundi waΒ  kutumia Upanga. Alipopata nafasi ya kushikilia Upanga alihakikisha anamwagaΒ  Damu Hadi kukifikia chumba Cha Mfalme Selasi. Alipofika hapo, aligunduaΒ  sanduku lilikua tupuΒ 

    β€œMfalme amechukua jicho, anaelekea kulifungua lango Kisha aondoke” alisemaΒ  Zahoro kwa sauti ya chini Kisha haraka alirudi alipomwacha Anna na MtotoΒ  Moana, wakati huo Alice alikua ameshikilia Upanga akipambana na Maelfu yaΒ  Askari wa Patiosa.Β 

    β€œInabidi tumfuate Mfalme” alisema Zahoro Kisha haraka walianza kukimbiaΒ  kuelekea eneo ambalo Farasi walikua wamefungiwa Kisha walichukua farasiΒ  wawili, Anna na Mtoto walikwea farasi mmoja, Zahoro naye alikua juu ya FarasiΒ  mwingine.Β 

    Waliondoka kulielekea lango ambalo lilikua na askari wa kutosha kwa ajili yaΒ  kuwazuia.Β Β 

    Zahoro alining’inia kwenye farasi mithiri ya digidigi mwenye hasira Kisha alianzaΒ  kukata shingo za Askari kama feni, alipoinuka Upanga wake ulikua unamwagikaΒ  Damu. Moana alitabasamu akimwona Baba yake akipambana kwenye Uwanja waΒ  vita.Β Β 

    Kisha akiteremeka kwa Kasi na kumwachia farasi, alianza mapigano ya UpangaΒ  kwa Kasi sana alihakikisha anaharakisha mpambano ili wamwahi Mfalme SelasiΒ  aliyekua akikimbia.Β 

    Ndani ya dakika tatu zilitosha kwa Zahoro kumaliza kazi Kisha alilifungua langoΒ  Kisha alimkwea farasi, wakaongoza njia pekee iliyokua ikitoka ndani ya Mji huo,Β  upande mwingine yalijaa Maji hivyo walikua na uhakika kua Mfalme aliitumia njiaΒ  hiyo kutokomea.Β 

    Aliongoza safari kwa kumliza farasi atembee kwa Kasi sana, nyuma yake AnnaΒ  pamoja na Moana walikua wakifuatia, Upanga uliendelea kusikika ndani ya MjiΒ  wa Patiosa, Alice alikua akipambana na Maelfu ya Askari wa Mji huo.Β 

    Askari walikua wengi sana kiasi kwamba Alice alianza kuzidiwa, lakini KilaΒ  alipokumbuka kuhusu kifo Cha Baba Yao na Mama yao ilimlazimu kuendeleaΒ  kupiga Upanga.Β Β 

    Upande wa pili, Zahoro alikua akikimbia na farasi kwa Kasi ya ajabu sana. AlijuaΒ  kama watamkosa Mfalme Selasi basi njia ya kuelekea Duniani isingelikuwepo tenaΒ  na pengine wangelisubiria kwa Miaka Mingi.Β 

    Farasi aliendelea kupiga kelele huku akikita kwato zake ardhini kwa kishindoΒ  kizito sana, Kila hatua ilimfanya Zahoro avute Upepo mkali uliombatana na baridiΒ  Kali la Msituni, Giza lilikua limetanda lakini macho makali ya Farasi yalikuaΒ  yakimulika mbele.Β 

    Baada ya kitambo kirefu, Farasi wa Zahoro aligoma kusonga mbele. Alikita miguuΒ  yake na kufunga breki katikati ya Msitu ulio Kimya sana huku sauti pekeeΒ  iliyosikika baada ya Farasi kutulia ilikua ni sauti ya kusukumwa kwa majaniΒ  makavu.Β 

    Palikua kimya huku pakiwa na ishara ya jambo lisilo la kawaida, kusimama kwaΒ  farasi kuliashiria jambo Fulani, Zahoro akashuka kutoka juu ya Farasi. KishaΒ  Upanga ukawa mkononi ili kujikinga na Adui atakaye jitokeza mbele yake.Β 

    Aliyalazimisha macho yake kutazama katikati ya Giza nene, hisia isiyo ya kawaidaΒ  ilimwambia asogee mbele zaidi kwa hatua takribani tano.Β 

    Aliposogea kidogo mbele akamwona Farasi akiwa amesimama kando ya njia.Β  Akajua sasa kua Mfalme Selasi hakua mbali na eneo Hilo, akatazama kulia KishaΒ  kushoto asijuwe Mfalme atakuwa ameelekea wapi.Β 

    Akajiuliza β€œAtakua upande upi?” akatikisa kope za macho yake kama aliyeingiwaΒ  na mdudu hivi Kisha akaamua kuelekea Upande wa kulia ambako yule FarasiΒ  alikuwepo, alizama Msituni huku akipapasia. Palikua Giza sana, alisonga mbeleΒ  huku akiamini kua Mfalme Selasi asingeliweza kujificha Bali aliingia MsituniΒ  hapo kwa ajili ya jambo Fulani la Siri.Β 

    Taratibu alianza kuhisi Nuru machoni pake, alianza kuona mwangaza mkali sana.Β  Aliamua kuufuata mwanga ulio mbele yake, sasa alikua akiona Kila kitu hivyoΒ  hata mwendo wake haukua mdogo. Alijua mwanga huo ulikua na uhusiano waΒ  moja kwa Moja na Mfalme Selasi.Β 

    Alikatiza Msitu, aliyapita Majani na nyasi kuufuata ule Mwanga. Hatimaye alifikaΒ  mahali ambapo palikua Ndiyo chanzo Cha huo mwanga, alimwona Mfalme SelasiΒ  kwa mbali aliwa amesimama kando ya Mwanga kwenye Mti mkubwa wenyeΒ  Pango, Naam! Hapa ndipo ilipo njia ya kuelekea Duniani.Β 

    Mfalme Selasi alikuwa mwingi wa kuangalia huku na kule akionekana kusubiriaΒ  jambo Fulani hapo, Kisha Zahoro akakatiza bwawa dogo kwa haraka na kutokeaΒ  upande wa pili, akabakiza hatua chache kufika alipo Mfalme.Β 

    Aliushuhudia Upepo mkali sana ukitoka kwenye lile Pango, kiasi kwamba hataΒ  kofia ya Kifalme ilimtoka Mfalme Selasi.Β Β 

    Zahoro akatambua sasa huwenda hiyo njia ilikua ikifunguka, lengo la MfalmeΒ  lilikua ni Kukimbia kuelekea Duniani.Β 

    Haraka Zahoro akaanza kukimbia kwa Kasi kumfuata Mfalme ambaye alikuaΒ  akipiga hatua kuzama ndani ya Pango Hilo, kitendo bila kukawia haraka Zahoro akamfikia Mfalme na kumvuta Mkono, akamtoa ndani ya Pango

    Mkononi Mfalme Selasi alikua ameshikilia Bastola, akaielekeza kwa ZahoroΒ Β 

    β€œUsijaribu kunizuia Kijana, nitakuuwa hapa na maiti Yako haitapatikana” alisemaΒ  Mfalme, akionekana kuvizia taratibu kwa jicho lake la kushoto akiangalia njia.Β  Zahoro akatazama namna Mlango ulivyokua ukifungukaΒ 

    Wakati ambapo Kuzimu ilikua Usiku, upande wa Duniani ilikua ni Mchana. AlionaΒ  Mabdhari ya kupendeza sana, lakini kizuizi kilikua ni Mfalme Selasi aliyeshikiliaΒ  Bastola.Β 

    Mfalme Selasi akaanza kurudi nyuma nyuma ili kuingia pangoni, Zahoro akapigaΒ  mahesabu afanye nini ili amzuie Mfalme asiingia humo maana alijua fika kuaΒ  kama Mfalme ataingia na mlango utajifunga.Β 

    Licha ya kushikilia Bastola, mkono mwingine aliishikilia mfuko Fulani mweusi,Β  humo ndimo lilimo jicho la Mfalme lenye ufunguo wa kufunga na kufungua NjiaΒ  ya kuelekea Duniani, kutokana na papara na wasiwasi akajikuta akidondoshaΒ  mfuko huoΒ 

    Akakaza Bastola kuelekea kwa Zahoro huku akipiga hesabu ya namna ganiΒ  ataokota Mfuko Kila hatua aliyoipiga, taratibu Zahoro naye alisogea.Β 

    β€œUsisogee Kijana nitakuuwa” akasema Mfalme Selasi, lakini Zahoro hakuachaΒ  kupiga hatua za mgando. Kitendo Cha Mfalme Selasi kuinama aokote mfukoΒ  akampa mwanya Zahoro kumfikia, papo hapo kabla hata Zahoro hajamgusaΒ  Mfalme, akapigwa Risasi ya Bega. Kisha Mfalme akafyatua nyingine lakini bahatiΒ  mbaya kwake risasi zilikua zimeisha.Β 

    Zahoro alipoligundua Hilo akamvaa Mfalme na kuanza kumshushia kipigo kizito,Β  Kisha akauokota ule mfuko. Pale pale taratibu Lango la Kuzimu likaanza kujifungaΒ  kwasababu hapakua na Mtu anayeingia humo.Β 

    Mfalme Selasi akiwa chini, Zahoro akiwa juu yake. Taratibu mkono wa MfalmeΒ  Selasi ukapapasa pembeni na kuokota jiwe, Kisha akalipeleka usoni kwa Zahoro kwa nguvu. Akafanikiwa kumsukumiza Zahoro pembeni, Giza likaanza kuingiaΒ  hapo sababu mlango wa kutoka kuzimu ulishaanza kujifungaΒ 

    Haraka Mfalme Selasi akiwa na wenge akaanza kutafuta ule mfuko wenye jichoΒ  lake lenye Miujiza. Bahati nzuri kwake akafanikiwa kuupata, wakati huo Zahoro akiwa chini akigaa gaa kwa maumivu makali ya kupigwa na jiwe

    β€œAaggghh‼” Mfalme Selasi akagugumia kidogo, akasogea kwenye mlango waΒ  kutokea Kuzimu Kisha akalitoa lile jicho kwenye mfuko, akalionyeshea kwenyeΒ  mlangoΒ 

    Lile jicho likawaka mwanga mwekundu, Kisha pole pole mlango wa KuzimuΒ  ukaanza kufunguka upya. Mfalme Selasi akaanza kufurahi, wakati huo mwangaΒ  ulikua ukianza kutawala eneo lote kwasababu Mlango ulikua unafunguka.Β 

    Zahoro Kila alivyojaribu kunyanyuka alihisi kizungu-zungu, maumivu ya kichwa.Β  Ulikua ni wakati wa Mfalme Selasi kuondoka. Akageuka kumtazama Zahoro KishaΒ  akamwambiaΒ 

    β€œUtaishi Kuzimu Milele” akamalizia kwa Kicheko kikubwa, Ghafla Mfalme SelasiΒ  akapigwa Mshale Mgongoni, akapigwa na Mshale mwingine bega la kulia naΒ  mwingine bega la Kushoto.Β 

    Zahoro alipoangalia ni Nani aliyemshambulia alimwona Anna akiwa ameshikiliaΒ  Mshale, kando yake yupo Moana. Alijikuta akiachia tabasamu la furaha naΒ  maumivuΒ 

    Mfalme Selasi licha ya kupigwa Mshale na kuanguka chini, Bado alianzaΒ  kujiburuza ili atoke Kuzimu, lakini Zahoro alimzuia kwa kumvuta nyuma KishaΒ  akamwambiaΒ 

    β€œWewe ndiye utakayeishi Kuzimu Milele” mara Anna na Moana walifika naΒ  kulichukua jicho kutoka kwa Mfalme Selasi.Β Β 

    β€œUtalipa kwa kifo Cha Wazazi Wangu, kama ulivyofanya kwetu ndivyoΒ  tutakavyofanya kwako pia.” Alisema Anna, Mfalme Selasi akamwambia AnnaΒ 

    β€œNajua unachokitafuta ni Nini Ndiyo maana unataka kwenda Duniani, lakini weweΒ  si wa huko. Wewe ni Mali ya Kuzimu” Anna alikunja uso wake Kisha akamuulizaΒ 

    β€œUnajua nini wewe?” Wakati huo Damu nyingi zilikua zikimtoka Mfalme Selasi,Β  akamwambia AnnaΒ 

    β€œUnaenda kutafuta Pete ya Baba Yako, Mimi naijua ilipo. Namjua anayeitumiaΒ  huko Duniani, bila Mimi kamwe hutoipata” Anna aligeuka akamtazama Zahoro Kisha Zahoro akamuuliza Mfalme Selasi

    β€œKama utasema ilipo basi nitakupatia jicho lako. Utajitibia na kupona, ipo kwaΒ  Nani?” Mfalme Selasi akaachia Kicheko Cha maumivu huku Damu ikimtokaΒ  Mdomoni.Β 

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya NANE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xxΒ 

     

    riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua soma riwaya bure

    24 Comments

    1. Marcel3316 on September 2, 2025 4:53 pm

      https://shorturl.fm/ptAnw

      Reply
    2. Reginald McGlynn on September 2, 2025 7:36 pm

      Your blog is a beacon of light in the often murky waters of online content. Your thoughtful analysis and insightful commentary never fail to leave a lasting impression. Keep up the amazing work!

      Reply
    3. Columbus Little on September 3, 2025 3:40 am

      Wonderful web site Lots of useful info here Im sending it to a few friends ans additionally sharing in delicious And obviously thanks to your effort

      Reply
    4. Jayden3045 on September 3, 2025 12:06 pm

      https://shorturl.fm/PabqU

      Reply
    5. Israel1675 on September 3, 2025 12:57 pm

      https://shorturl.fm/PabqU

      Reply
    6. April2935 on September 3, 2025 5:28 pm

      https://shorturl.fm/zbbOE

      Reply
    7. Coraline2188 on September 3, 2025 8:20 pm

      https://shorturl.fm/87tZT

      Reply
    8. Christina3243 on September 4, 2025 1:34 am

      https://shorturl.fm/aFvIH

      Reply
    9. πŸ–± πŸ”΅ New Notification: 1.95 Bitcoin from partner. Review transfer >> https://graph.org/ACTIVATE-BTC-TRANSFER-07-23?hs=be441b2e1d42ef6822280d15ec9ad240& πŸ–± on September 4, 2025 10:59 pm

      ek4nwk

      Reply
    10. Kristen2150 on September 5, 2025 2:30 am

      https://shorturl.fm/IFCJA

      Reply
    11. πŸ“† πŸŽ‰ Exclusive Deal: 0.75 BTC reward waiting. Claim today β†’ https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=be441b2e1d42ef6822280d15ec9ad240& πŸ“† on September 6, 2025 4:59 am

      sihv1d

      Reply
    12. Beatrice1815 on September 6, 2025 11:17 am

      https://shorturl.fm/LB0YC

      Reply
    13. Darren2153 on September 13, 2025 9:16 am

      https://shorturl.fm/nNcA0

      Reply
    14. Alina172 on September 17, 2025 9:37 am

      https://shorturl.fm/vWXDi

      Reply
    15. Francesco4354 on September 18, 2025 8:05 am

      https://shorturl.fm/B4693

      Reply
    16. Darby1804 on September 18, 2025 8:00 pm

      https://shorturl.fm/FXH4A

      Reply
    17. Andre2401 on September 19, 2025 5:59 am

      https://shorturl.fm/tL4gk

      Reply
    18. Neal4409 on September 19, 2025 6:08 am

      https://shorturl.fm/V8XXo

      Reply
    19. Kaden4494 on September 20, 2025 3:05 am

      https://shorturl.fm/yJ1gB

      Reply
    20. Stanley3427 on September 20, 2025 12:25 pm

      https://shorturl.fm/AIA9W

      Reply
    21. πŸ“‰ πŸ’Έ BTC Deposit - 2.4 BTC waiting. Tap to claim => https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=be441b2e1d42ef6822280d15ec9ad240& πŸ“‰ on September 21, 2025 3:06 am

      u6jlti

      Reply
    22. Lachlan212 on September 22, 2025 9:12 am

      https://shorturl.fm/LWoaD

      Reply
    23. Chloe2118 on September 25, 2025 2:21 am

      https://shorturl.fm/0933z

      Reply
    24. mind vault on October 15, 2025 2:20 pm

      **mind vault**

      mind vault is a premium cognitive support formula created for adults 45+. It’s thoughtfully designed to help maintain clear thinking

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.