Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 04

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 03

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 04
    Hadithi

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 04

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaAugust 28, 2025Updated:August 28, 20254 Comments10 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02

    “Kumwambia Ukweli Zahoro kua Adui Kimya ni wewe, kilicho mbele ni kumpata  Binti yetu Moana Kisha kutafuta njia ya kuelekea Duniani. Baada ya Kisasi  sitawalazimiaha Zahoro na Moana kuishi Kuzimu. Watachagua wapi wanataka  kuishi” Alisema Anna, Alice alifuta chozi lake Kisha akamwambia Anna 

    “Kama ni hivyo basi tunaweza kua kitu kimoja lakini sitakusaidia kuelekea  Duniani ikiwa Kuna njia, Mimi nitaitawala Patiosa Milele kuenzi Wazazi wetu.  Kwasasa nitaungana nawe kurejea Patiosa kwa ajili ya kumpata Mtoto na  kupambana Mfalme Selasi. Wote wakatabasamu.

    SEHEMU YA NNE

    Dunia Halisi. 

    Miaka Mingi ilikua imepita, yalifanyika majaribio mengi ya kukitafuta Kijiji Cha  Nzena bila mafanikio. Wanasayansi wakubwa walishindwa kutatua Fumbo Hilo,  isipokua Mwanasayansi Mmoja aliyejizolea umaarufu Kila kona ya Dunia. 

    Alikua na ushawishi Mkubwa sana, alikua tajiri na mwenye nguvu. Aliweza  kufanya tafsiri zilizoonekana kua ngumu, yeye aliweza kupata majibu ndani ya  muda mfupi sana. Alipoulizwa kuhusu Nzena alionesha Kigugumizi, hakua na jibu  lolote lile.

    Eneo ambalo Kijiji kilipotelea palijengwa Makumbusho ya Nchi ya Ganza.  Makumbusho ambayo yalikua maarufu sana Kila kona ya Dunia, historia ya  kilichotokea Nzena kilitokea Miaka Mingi iliyopita huko Mashariki ya mbali, zaidi  ya Miaka Miatatu.  

    Siku Moja, taarifa mbaya zilianza kusambaa zikimhusu Mwanasayansi Steve  Mbasa, Mwanasayansi anayetumainiwa. Taarifa zilisambaa kwa Kasi sana kwenye  Mitandao mbali mbali ya Kijamii kua umashuhuri wote alionao Steve Mbasa  hautokani na Sayansi ya kawaida isipokua Pete ya kifalme kutoka Mji wa Patiosa. 

    Taarifa ilieleza kua, hata Umri wa Steve Mbasa unasogea taratibu sana  ukilinganisha na Watu aliozaliwa nao Mwaka mmoja, taarifa iliendelea mbali zaidi  na kusema kua Steve Mbasa ana Miaka 93 lakini anaonekana kama mwenye Miaka  50 kutokana na Pete hiyo ya Miujiza. 

    Taarifa hii ilimfikia Steve Mbasa mwenyewe akiwa kwenye Moja ya nyumba zake  za kifahari, kilicho mchukiza zaidi ni Mtu aliyeibua taarifa hizo alikua ni rafiki  yake wa karibu aliyeitwa GGB. Hawa wote ni Wanasayansi Mashuhuri sana  Duniani, lakini GGB aliibua skendo hiyo kwa nia Fulani. 

    Taarifa hii ilizua taharuki kote Duniani, ilimchafua sana Steve Mbasa, akatupa  glasi yenye waini ndani yake Kisha akampigia simu GGB. Lakini simu ya GGB  haikupatikana, taarifa ziliendelea kutoka, pamoja na Vipande vya video  vilivyomwonesha GGB mwenye Miaka 93 akieleza Siri ya Sayansi ya Steve  Mbasa. 

    GGB aliwaeleza Watu kua yeye na Steve Mbasa walifanikiwa kufika Kuzimu  kupitia Pango Moja la Siri sana ambalo kwasasa limejifunga. Akasema walipitia  kwenye Pango Moja wakajikuta wapo Kuzimu kwenye Mji mmoja uitwao Patiosa.  Mji uliokua ukiongozwa na Mfalme mmoja aitwaye Munis. 

    GGB na Steve Mbasa walifanikiwa kumfikia Mfalme na kumwahidi kua  wangemwonesha lango la kuelekea Duniani, akasema Mfalme aliwapenda sana  GGB na mwenzake Steve Mbasa. Walijitambulisha wao ni Wanasayansi Wanaokua  kwa Kasi sana. 

    Mfalme Munis akawaeleza kua angewapa nguvu za Miujiza kidogo kutoka kwenye  Pete yake ili wawe Wanasayansi hatari zaidi lakini kwa sharti la kumwonesha 

    Lango la Kuelekea Duniani. Mfalme Munis alikua na kiu kubwa ya kwenda  Duniani, lakini GGB anasema. Siku Moja Steve Mbasa alimwambia Mfalme kua  wafanye safari ya Siri kuelekea Langoni kwani wao wanategemea kurudi Duniani. 

    Walimwambia kua safari hiyo isihusishe mlinzi yeyote wa Mji wa Patiosa. Wala  familia ya Mfalme Munis, lakini Mfalme akafikiria kidogo Kisha akawaambia kua  ili aweze kutoa nguvu kutoka kwenye Pete ni lazima Mke wake awepo pamoja na  Watoto wao wawili Mapacha ambao ni Anna na Alice. 

    GGB anasema alishangaa sana kuona Steve akisema mambo ambayo  hawakukubaliana, Kisha akamwita Steve chemba na kumuuliza ni kwanini  alimwambia hivyo Mfalme Munis. Steve akamwambia GGB kua anaitaka Pete ya  Mfalme Munis kwani ni ya Miujiza mikubwa sana, GGB anasema wakaingia  kwenye mzozano baina Yao lakini Steve Mbasa akamwambia GGB kua  wangeitumia pamoja Pete hiyo kua matajiri, Wanasayansi Mashuhuri zaidi  Duniani. 

    GGB anasema alikubali kwa shingo upande huku akijua fika kua wanafanya Kosa  kubwa kwa kupanga njama za kuiba Pete hiyo kutoka kwa Mfalme. Basi,  walikubaliana na Mashariti ya Mfalme Munis. 

    Usiku wa siku hiyo, Mfalme aliondoka jumba la Kifalme na familia yake kwa Siri  sana, waliongozana na GGB na Steve Mbasa Hadi nje kabisa ya Mji wa Patiosa.  Walipofika huko walimwambia Mfalme aiache familia yake kwanza ili akalione  lango peke yake Kisha warudi ili wakabidhiane nguvu.  

    Walianza safari nyingine ndefu kwa kutumia farasi huku Mfalme Munis akiwauliza  ni kwanini wameiacha familia yake mbali kiasi kile. Baadaye Mfalme  alisimamisha Farasi na kudai kua hawezi kwenda mbali kiasi hicho na kuiacha  Familia yake eneo la Msitu lenye Wanyama wakali. 

    GGB anasema alishangaa uamuzi wa ghafla na wa tamaa wa Steve Mbasa wa  kuuchomoa Upanga wa Mfalme Kisha kumlazimisha ashuke kwenye farasi. Kisha  haraka Steve Mbasa alimuuwa Mfalme kwa kumkata na Upanga shingoni,  akaichukua Pete wakaondoka hapo kwa Mguu na kurejea pangoni Kisha kurudi  Duniani.

    GGB anasema walipofika nyumbani, Steve Mbasa alimwambia GGB waiamuru  hiyo Pete kama ambavyo Mfalme alikua alifanya Kisha Miujiza hutokea. Kitu Cha  Kwanza waliamuru kiasi kikubwa Cha pesa kitokee, wote walistaajabu kilitokea  kiasi kikubwa Cha pesa, Kila walichosema kilifanyika haraka sana. 

    Wakakubaliana kua Pete hiyo itakua Yao wote lakini baadaye Steve alimgeuka  GGB na kuamua kujimilikisha nguvu zote peke yake. Kwa hasira GGB alifunga  safari ya Siri kurudi Kuzimu kupitia pangoni ili akawaambie familia ya Mfalme  kua aliyemuuwa Mfalme ni Steve Mbasa, awaambie ndiye anayeimiliki Pete lakini  alipofika pangoni hakukuta njia ya Kuzimu isipokua Pango lisilo na chochote. 

    GGB alilia sana baada ya kutambua kua asingeweza kurudi Kuzimu kwani lango  lilikua limejifunga. Aliishi na Siri hiyo kwa Miaka Mingi tokea wakiwa vijana,  alizitumia pesa zake alizozipata kwa kufanya tafiti mbalimbali kama  Mwanasayansi. 

    Taarifa ya GGB ilimgadhibisha sana Steve Mbasa. Simu za Waandishi wa Habari  na viongozi mbalimbali zilizidi kumtia hasira Steve Mbasa, Kila Mtu alimwona  GGB kama Mtu aliyekosa hoja za Msingi za Kisayansi, hakuna Mwanasayansi  aliyeamini alichokua anakizungumza lakini alifanikiwa kumchafua Steve Mbasa  kwa baadhi ya Watu ambao waliamini hakua Mwanasayansi wa kawaida. 

    Kuzimu. 

    Zahoro alifanikiwa kufika pangoni akiwa na maumivu makali sana ya Mguu.  Aliugulia maumivu huku akiwaza ni wapi alipo Anna, alijiegemza kwenye jiwe  kubwa akiendelea na tafakari. 

    Mara alisikia kishindo, Kisha alimwona Anna akiingia Pangoni.  

    “Anna” aliita Zahoro akiwa ameushikilia Mguu wake unaovuja Damu. Taratibu  Anna alisogea karibu na Zahoro Kisha alimwambia 

    “Pole kwa maumivu Zahoro, nilifanya Kila jitihada kuhakikisha unajua salama”  alisema Anna huku akihangaika kuwasha moto ili amtibie Zahoro kwa dawa za  Mitishamba. Alice alisimama lango la Pango kwa Siri sana akimtazama Zahoro Kisha aliondoka zake.

    Basi, Anna aliitumia Mitishamba aliyoifahamu kumtibia Zahoro. Kisha baada ya  Dakika kadhaa za kumaliza kumtibia waliketi wakizungumza mawili matatu, Razaro alimuuliza Anna ni wapi wangempata Moana. 

    Anna alikua akiijua Kuzimu vizuri sana sababu alizaliwa na kukulia Kuzimu,  aliujua Mji wa kutisha wa Patiosa unaoongozwa na Mfalme Selasi. Alikaa kimya  kidogo, hakutaka kumweleza Zahoro juu ya Siri ya Adui Kimya. 

    “Wanaweza kua Upande wa pili wa Mto, pengine tunaweza kumpata huko.  Unapaswa kupona haraka Zahoro.” 

    “Ni sawa, siwezi kuruhusu Moana apotee mbele ya Macho yangu.” Alisema  Zahoro.  

    Aliendelea na matibabu ya Mitishamba na mazoezi ya Hapa na pale, Anna alikua  akitoka kwenda kuchukua chakula nje, huko alikua akikutana na Pacha wake Alice,  walipanga mipango Mingi ya Siri ya Namna ya kuingia Patiosa. Lakini Anna  alimweleza Alice kua, Zahoro ni Mwanaume wa maono. Siku Moja kupitia ndoto  zake atagundua Siri ya kutoka Kuzimu na kuelekea Duniani. 

    Maisha yaliendelea, siku zilizogea kwa Kasi huku Zahoro akiendelea kupona  majeraha ya Mguu wake. Mara nyingi Zahoro alipokua amelala, Anna alikaa  macho ili kumtazama Zahoro kama alikua akiota ndoto ya matumaini. 

    Usiku mmoja, wakiwa wamelala. Zahoro alianza kutaja jina la Selasi, Mfalme  katili wa Mji wa Patiosa, wakati anaiota ndoto hiyo alikua akitokwa na jasho Kali  sana. Anna hakujua ni kwanini Zahoro Zahorita Mfalme huyo asiyemjua wala hata  kusikia kuhusu habari zake. 

    Zahoro aliendelea kumtaja Selasi pamoja na Mji wa Patiosa. Kisha alizinduka  kutoka Usingizini, akikutana na macho makavu ya Anna.  

    Alikua mchovu na mwenye wasiwasi sana, aligundua Anna alikua akimfuatilia.  Alimtazama Kisha alimwambia 

    “Nimeuona Mji uitwao Patiosa ukiongozwa na Mfalme mwenye jicho Moja  aitwaye Selasi.” Alisema, Anna alistaajabu kwa namna ambavyo Zahoro aliyapatia  maelezo hayo kuhusu Mfalme na huo Mji.

    “Huo Mji upo hapa Kuzimu, ndiko aliko Moana.” Alisema Zahoro Kisha aliketi  sawa sawa halafu akaendelea 

    “Huko Kuna Siri ya njia ya kuelekea Duniani.” Anna alishtuka, akamuuliza “Siri ipi hiyo” Zahoro alimtazama Anna Kisha akamjibu kwa utaratibu “Jicho la Mfalme Selasi Ndiyo Njia ya kurejea Duniani.” 

    “Jicho?” 

    “Ndiyo, hilo ni funguo ya kufungua lango. Jicho lake Hilo amelihifadhi kwa Siri  kwenye Gaston maalum. Ni jicho lenye maana Ndiyo maana alilitoa na kulificha,  Ndiyo Siri ya yeye kua na jicho Moja” Anna alipoyasikia maelezo haya hakujua  afurahi au alie maana yalikua ni maelezo yaliyoshiba haswa. 

    “Zahoro, natamani wewe na Moana muende Duniani. Munastahili kuishi Sehemu  nzuri na salama kuliko hapa” alisema Anna Kisha taratibu alijiegemza kwenye  bega la Zahoro.  

    *** 

    Asubuhi ya Siku iliyofuata, Anna alijikuta akiamka peke yake. Alipoangaza  hakumwona Zahoro, alijiweka sawa kiakili kabla ya kutoka ndani ya Pango na  kuelekea juu ya Mlima. Alimwona Zahoro akifanya mazoezi ya Upanga, aliachia  tabasamu sababu alijua tayari Zahoro alikua ameshapona kwa ajili ya safari ya  kuelekea upande wa pili wa Mto. 

    Pamoja na yote, Bado Anna aliamini siyo muda muafaka wa kumweleza ukweli  Zahoro. Japo nafsi yake ilikua ikimsuta lakini aliamini wakati ukifika atamweleza  ukweli Zahoro, aliamini kua kwa kuujua ukweli kutabadilisha Imani ya Zahoro juu  yake. 

    Baada ya mazoezi Zahoro alirejea pangoni akiwa imara kuliko wakati wowote  huku moyo wake ukimsukuma kuelekea Upande wa pili wa Mto kwa ajili ya  kumtafuta Moana. Anna aliendelea kuitafakari ndoto ya Zahoro, aliijua njia mpya  ya kupata lango la kuelekea Duniani, ni kwa kuiba jicho la Mfalme Selasi wa  Patiosa. 

    Alishusha pumzi zake Kisha alimuuliza Zahoro.

    “Unajisikia kua imara sasa?” Zahoro alimtazama Anna Kisha akamwambia 

    “Kuliko wakati wowote ule katika Maisha yangu. Nahitaji kufika Patiosa sasa”  alisema kwa Ujasiri na kujiamini sana. 

    “Unapajua?”  

    “Nina hakika na nilichokiota wakati huu, tuuvuke Mto kwanza kwa mara ya  Kwanza” alisema Zahoro, Anna alishusha pumzi zake. Alijua asingeliweza kuizima  ndoto ya Zahoro. Akamsogelea Kisha akamwambia 

    “Kwa ajili ya Moana, nipo tayari kwa lolote. Lakini tunapaswa kua makini sana,  pengine si Mji wa kawaida kama unavyoweza kufikiria” alisema Anna, ilibidi  watoke waelekee juu ya Mlima. Huko walipata nafasi nzuri ya kuzungumza na  kupanga mipango Yao. 

    Mchana wa siku hiyo walianza safari ya kuelekea Mji wa Patiosa. Anna alikua  akiufahamu vyema Mji huo lakini hakutaka kumwambia Zahoro, alijua ni hatari  kiasi gani walikua wakiifuata. 

    Basi, ili asionekane anajua chochote aliigiza kua mwoga kwa Kila hatua huku  wakiwa kimya. Walitembea taratibu Hadi walipofika kwenye Kingo ya Mto,  mahali ambapo walitengana na Mtoto wao Moana. Walisimama kwa majonzi  Kisha Zahoro aliongea kwa sauti ya chini akamwambia Anna 

    “Nina amini, Mji wa Patiosa una majibu ya maswali mengi. Siri nyingi  zitafunguka” alisema akimtazama Anna ambaye alianza kuonesha Mashaka huku  akijiuliza kama Zahoro aliota jambo lingine aliloamua kulifanya Siri. Wakati  wakiwa hapo wanazungumza, Alice alikua amesimama kwa mbali akiwatazama. 

    “Kuna jambo lingine uliliota?” akauliza Anna. Zahoro akamjibu 

    “Hakuna zaidi ya nilicho kusimulia. Lakini Nina uhakika na Mji wa Patiosa,  utaenda kutegua kitendawili” Alisema Zahoro Kisha alimshika mkono Anna  wakashuka taratibu Hadi chini, Zahoro alionekana kua makini sana, aliangaza  huku na kule kabla ya kuanza kutafuta Mtumbwi. 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx 

    riwaya riwaya mpya riwaya za bure riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua soma riwaya bure

    4 Comments

    1. Danny McLaughlin on August 28, 2025 6:38 pm

      I loved as much as youll receive carried out right here The sketch is attractive your authored material stylish nonetheless you command get bought an nervousness over that you wish be delivering the following unwell unquestionably come more formerly again as exactly the same nearly a lot often inside case you shield this hike

      Reply
    2. Deirdre4923 on August 28, 2025 8:41 pm

      https://shorturl.fm/jXcQc

      Reply
    3. Gidioni on August 28, 2025 10:52 pm

      Adimin unachelewa sana adi tunasahau

      Reply
    4. Oscar Lockman on August 29, 2025 12:20 am

      Thanks I have recently been looking for info about this subject for a while and yours is the greatest I have discovered so far However what in regards to the bottom line Are you certain in regards to the supply

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi August 28, 2025

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 04

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02 “Kumwambia Ukweli Zahoro kua Adui Kimya ni wewe, kilicho…

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 03

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.