Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Inonga Amejiuza AFCON Sitashangaa Akiondoka Simba
    Africa | CAF

    Inonga Amejiuza AFCON Sitashangaa Akiondoka Simba

    MhaririBy MhaririFebruary 1, 20242 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Inonga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Akiwa katika hatua ya robo fainali ya michuano ya mataifa barani Afrika na timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DR Congo) mlinzi wa kati wa klabu ya Simba Henock Inonga Baka ni wazi sasa uongozi wa klabu ya Simba unakuna vichwa kuona watafanya mbinu gani kumshawishi kubaki katika mitaa ya Msimbazi.

    Tumeitazama michuano hii kuanzia hatua ya awali yaani ya makundi mpaka hatua hii ya robo fainali inayotarajiwa kuanza siku chache zijazo na hakuna atakayepinga kuwa Inonga amekua na kiwango bora sana ambacho mpaka kupata nafasi ya kuanza katika kikosi chao inaonesha si lelemama kwani DR Congo imejaa wachezaji wengi kutoka ligi kubwa barani Ulaya.

    Kuna taarifa zimekua zinazagaa mitandaoni kwamba beki huyu kisiki amemalizana na klabu ya FAR Rabat kutoka nchini Morocco kwa mkataba wa awali ili akimaliza mkataba wake katika klabu ya Simba basi wamchukue na mara nyingi watu husema tetesi muda mwingine huwa ni kweli na ikumbukwe kuwa kikosi cha FAR kinaongozwa na kocha wa zamani wa klabu ya Yanga Nasreddine Nabi.

    Ukiachana na kocha Nabi lakini pia inadaiwa Al Ahly ya Misri nao wameonyesha nia  kumtaka beki huyo mwenye thamani ya Dola laki tano ambayo sawa na shilingi bilioni 1.2 ambaye amebakisha mkataba wa mwaka mmoja ndani ya timu hiyo.

    Hivi karibuni uongozi wa klabu ya Simba ambao ndio wamiliki halali wa mchezaji huyo umeweka wazi kuwa endapo itakuja ofa kubwa ya mabilioni ya fedha watatengeza msimamo na kuzungumza na klabu ambayo inahitaji huduma ya beki wao wa kimataifa, Enock Inonga Baka.

    Kwa haya yote yanayotokea nadhani pia ni funzo kwa wachezaji wetu wa Tanzania kuamini na kuonesha kuwa wanatakiwa kupambana ili kuhakikisha kuwa wanapata mafanikio makubwa na kutumikia vyema vilabu vyao.

    SOMA ZAIDI:Walioleta VAR AFCON Wana Nafasi Yao Moyoni Mwangu

    AFCON 2023 inonga

    2 Comments

    1. Pingback: Chama Amedhihirisha Kuwa Viongozi Simba Ni Wababaifu - Kijiweni

    2. Pingback: Safari Ya Afcon Na Heshima Kubwa Kwa Ligi Za Afrika - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.