Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    In the name of LOVE – 08

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » In the name of LOVE – 10
    Hadithi

    In the name of LOVE – 10

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoSeptember 28, 2025Updated:September 28, 20253 Comments10 Mins Read755 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia sehemu ya tisa ya In the name of LOVE

    “Kumbe haikua inshu kubwa sana Mpenzi, Presha ilipanda kidogo. Ah!  Mama yangu naye akalikuza sana” alisema huku naye akichukua kipande  Cha tunda kwa kutumia mkono wake Kisha akaliweka Mdomoni. 

    “Na vipi kuhusu hiyo simu, una furaha sana”  

    “Eeh! Mama alikua akinipa mrejesho kuhusu Hali Baba” alisema Zaylisa.  Niliguna tu Kisha niliendelea kula matunda. 

    Siku iliyofuata asubuhi mapema, Zaylisa aliniaga kua anaenda kumjulia  Hali Baba yake, tukakumbushana kua ilikua ni siku ya Clara kurudi kutoka  Arusha. Endelea

    SEHEMU YA KUMI

    Zaylisa alipoondoka, niliitafuta tena lile Bahasha yenye jina langu,  haikuwepo popote pale, niliitafuta sana lakini halikuwepo, jasho lilikua  linanitoka. Nilipoona kua siwezi kuipata nilielekea bafuni kwa ajili ya  kuoga, nilipomaliza kuoga Maji ya baridi nilirudi chumbani na kuanza  kujifuta Maji, mara nilisikia ‘alam’  

    “Mh! Itakua Clara huyo” nilijisemea tu, nilimalizia kujifuta Maji. Kisha  nilitoka chumbani taratibu nikaelekea sebleni, nilimkuta Matilda  akiendelea na usafi, aliponiona alinisalimia 

    Baada ya salamu Niliketi kochini nikisubiria kuambiwa kua Clara alikua  amerudi, kwakua tulikwaruzana alipoondoka sikutaka kuonesha Wazi kua  nilikua najali kuhusu yeye maana niliamini hakupenda niendelee kuishi  kwake, nilijishughulisha na kuangalia Televisheni. 

    Matilda aliendelea na kazi zake bila kusema chochote kile, nilizuga kwa  muda kidogo. Nilipoona kua Matilda hawezi kusema chochote  nilijikoholesha Kisha nikamuuliza 

    “Dada Yako hajarudi?” niliuliza kwa sauti iliyoonesha kutojali. Matilda  alinitazama Kisha akanijibu kwa sauti ya utaratibu 

    “Ndiyo” nilimtazama 

    “Hajarudi? Wakati nimesikia Mtu akibisha hodi?”  

    “Walikosea nyumba, ni mafundi wa Umeme” alisema.

    “Aah! Unafikiri najali sana? Hapana wala sijali” nilisema ili kumwonesha  Matilda kua nilikua sijali kuhusu Clara lakini ukweli ni kwamba licha ya  yote ila yeye alisaidia Maisha yangu. 

    “Haujali kuhusu nini?” aliniuliza kwa sauti ya utaratibu iliyojaa heshima. 

    “Ah! Nazungumza mwenyewe” nilizuga Kisha niliondoka pale sebleni  nikarudi chumbani. Nilihisi kutamani sana kumwona Clara japo nilikua na  hasira naye, sikujua Hali ile ilitokana na Nini.  

    “Kwanza sijali kuhusu wewe, urudi au usirudi wala hainihusu Mimi”  nilijisemea kwa sauti ya kunung’unika. Nilihisi Kuna Upendo Fulani ndani  yangu juu ya Clara lakini sikujua ulikua Upendo wa aina gani.  

    Mara sauti ya Alam ya Getini ililia tena, Ilinishtua. Nikafungua mlango  haraka ili nikaangalie ni Nani aliyekua getini, nilipofika sebleni nilimwona  Matilda akielekea getini, nilizuga naelekea lilipo friji ili kupata Maji ya  kunywa ya Baridi. Sikutaka Matilda agundue kua nilikua na kiu ya kutaka  kumwona Clara. 

    Baada ya dakika mbili alirudi ndani, alinikuta nikiwa nimeketi kitini, mbele  yangu kukiwa na meza ndogo niliyoweka glasi. Nilizisikia hatua zake lakini  ghafla zilipotea, nilikua nimempa mgongo hivyo ilinibidi nigeuka niangalie  kama Kuna Ugeni wowote au yeye alipotelea wapi 

    Nilipogeuka nilikutana naye macho kwa macho, ilikua kama nimemshtua  hivi maana alikua amesimama akiniangalia. Alijishtukia Kisha alizuga kua  alikua bize na Mambo yake, sikutaka kumuuliza chochote kile nilikaza sura  yangu. Nilielewa kua hapakua na ujio wa Mtu yeyote yule pale ndani 

    Sikuacha kujiuliza kua Clara atarudi saa ngapi, kingine nilijiuliza hisia ile ya  kutaka kumwona Clara ilitokana na Nini, masaa yalienda. 

    Hapakua na Clara wala hapakua na ujio wa yeyote yule, hata simu ya  Zaylisa ilikua haipatikani. Ilinifanya nijiulize maswali mengi ambayo  hayakua na Majibu. Nilikua Mtu wa kuingia na kutoka chumbani, mara  nikae sebleni, mara niende kukaa eneo la Bustani ilimradi tu nisikie geti  likigongwa 

    Hadi Giza linaingia palikua kimya sana, Giza lilinikuta nikiwa nimeketi  kwenye Bembea ndani ya Bustani nzuri ya mauwa. Taratibu niliondoka  nikarudi ndani, nilimkuta Matilda akiwa ameshikilia kisikilizio Cha simu ya  Mezani, aliponiona wala hakushtuka 

    Nilimwona ni Mtu mnyonge aliyejawa na huzuni, Ilinishtua kidogo.  Nikataka kufahamu sababu ya mabadiliko yake, nilisogea taratibu Hadi 

    alipokua amesimama, alikua akiniangalia Hadi namfikia, macho yake  yalipoteza uchangamfu kabisa 

    “Wewe” nilimwita, namna alivyokua akinitazama ni kama Mtu aliyezama  sana mawazoni, jicho lake kwangu halikubanduka. Aliweka kisikilizio  Sehemu yake Kisha akanitazama kwa jicho lile lile la huzuni 

    “Si naongea na wewe, mbona umekua mnyonge hivyo?” nilimuuliza wakati  huo tayari na Mimi nilikua nimeingiwa na wasiwasi japo kidogo. 

    “Dada hapatikani kwenye simu yake, mara ya mwisho niliongea naye  Mchana kua anaondoka na ndege ya Mchana kutoka Arusha, angefika huku  mapema sana” alisema, kidogo nilisisimka. Nikameza funda zito la mate  huku nikitafakari, nikamuuliza 

    “Hakukwambia kua atapitia popote?” nilimuuliza kwa sauti ya utaratibu  iliyojaa umakini sana huku macho yangu yakishindwa kuvumilia wasiwasi  nilionao 

    Matilda akanitazama kwa sura ile ile ya huzuni Kisha chozi kidogo  lilimtoka, halikua chozi la kawaida, lilikua chozi la Upendo na kujali.  Akajifuta kwa kutumia mkono wake wa kulia Kisha nikaisikia sauti yake ya  kuvuta hewa  

    “Hapana, alisema anakuja Moja kwa moja lakini pia alisema akifika  ataongea na wewe kuhusu jambo muhimu” alisema Matilda, alizidi  kunifanya nisisimke kwa wasiwasi  

    “Mimi?” nilihoji huku kidole kikiwa kinaonesha kifua changu, nilitaka  uhakika wa alichokisema Matilda. 

    “Ndiyo” alisema Matilda akiwa anamaliza kufuta chozi, alinitazama kwa  jicho lililojaa Siri fulani nisiyoifahamu. Nilimeza funda zito la mate 

    “Alisema ni jambo gani Hilo?” niliuliza huku nikisikia mapigo ya Moyo  Wangu yakienda mbio, nilipepesa macho yangu haraka haraka. Kichwani  nilikua na jambo Moja ambalo niliamini lilikua muhimu nalo ni kufukuzwa  nyumbani kwa Clara kutokana na kilichotokea kati ya Zaylisa na Clara. 

    Nilikuna nywele zangu katika Hali ya kuchanganyikiwa huku nikisubiria  jibu la Matilda 

    “Hakuniambia, lakini…..” nilikua makini, Matilda alitaka kusema jambo  Fulani ambalo nilihisi lilikua likimfanya anitazame kwa jicho kavu 

    Moyo Wangu ulikua ukijisemea na kuhimiza kua Matilda aseme haraka ili  nijuwe kama alitaka kunifukuza au laa. Alipoanza kunyanyua midomo yake 

    mara Mlango uligongwa, haukuwa mlango wa geti Bali ulikua ni mlango wa  kuingilia sebleni, nilimtazama Matilda 

    Hisia zangu ziliniambia alikua Clara au Zaylisa, nilitegemea ujio wao. Mtu  asiyeifahamu nyumba asingeliweza kuingia getini Kisha kuja kugonga  mlango wa kuingilia Sebleni.  

    Sote tulijawa na kiu ya kutaka kujua alikua ni Nani, mlango uliendelea  kugongwa ndipo nilipoanza kuhisi pengine alikua Mtu mgeni,  isingeliwezekana kwa Zaylisa au Clara kugonga mlango muda wote huo  maana ilikua inaelekea dakika Moja. 

    Matilda alielekea mlangoni huku nikimsindikiza kwa macho ya utayari wa  kumwona mgongaji, pumzi zangu zilikua kama za kuhesabu huku nikiweka  umakini zaidi mlangoni, sikuruhusu jicho langu hata Moja kufumba 

    Matilda alipotekenya kitasa niliyasikia mapigo ya Moyo Wangu  yakiongezeka, mara nilipatwa na Hali ya Ubaridi sana niliposikia sauti ya  Mwanaume akiuliza. 

    “Hapa ni nyumbani kwa Clara?” Matilda aligeuka kunitazama Mimi, Kila  mmoja alikua na wasiwasi maana kutopatikana kwa Clara Kisha ujio wa  Mwanaume tusiyemfahamu kulifanya wasiwasi uongezeke. Nilitembea  taratibu Hadi mlangoni, nikamwona Mwanaume mmoja mwenye ndevu  nyingi nyeusi, mnene kidogo, mfupi kiasi na mwenye macho yaliyoingia  ndani, alikua amevalia tisheti nyeusi na Suruali ya kaki. 

    Nilimtazama juu Hadi chini, alikua mgeni machoni pangu hata machoni pa  Matilda maana hata sura ya Matilda ilionesha Wazi kua alikua akimwona  kwa mara ya kwanza. 

    Alikua na sauti nzito ya Kiume. 

    “Ndiyo” niliitikia kwa sauti ya taratibu iliyojaa wasiwasi na kiu ya kutaka  kujua ni kwanini alikua akiulizia. 

    Alinitazama kwa sekunde kadhaa, ghafla tulisikia geti likifunguliwa ilibidi  sote tuangalie getini, aliingia Zaylisa akiwa anayumba kama Mtu aliyelewa,  sote tulihamisha umakini kutoka kwa yule Mwanaume kuelekea kwa  Zaylisa. 

    Nilikua wa kwanza kumkimbilia na kumdaka asianguke, huku kichwa  changu kikizunguka maswali mengi sana yasiyo na Majibu. Niligeuka  kumtazama Matilda aliyekua tayari ameshafika tuliposimama, naye  alinitazama kwa jicho lenye maswali mengi sana

    Kisha sote kwa pamoja Mimi na Matilda tuligeuka kumtazama yule  Mwanaume pale tulipomwacha, tulishangaa hakuwepo, Zaylisa alikua  amezima mikononi mwangu.  

    Matilda akaangaza huku na kule Kisha akaniambia 

    “Hayupo”  

    Hatukujua alienda wapi, alipotea kama Mzimu? Yeye ni Nani na alikuja  kufanya nini pale, hatukua na Majibu ya maswali yetu. Zilikua dakika  chache za kustaajabisha, dakika zilizozaa maswali zaidi ya majibu. 

    Tulisaidiana kumpeleka Zaylisa ndani, Matilda alibeba mkoba pamoja na  viatu vya Zaylisa. Tulimpeleka Hadi chumbani, alikua hajitambui kabisa  yaani alilewa kwa kiwango kisicho Cha Kawaida.  

    Matilda aliondoka pale chumbani, nilimfuata Kisha nilimsimamisha  kwenye korido, alisimama akiangalia mbele bila kugeuka. Taratibu  nilimfuata nikasimama nyuma yake, ukimya wenye maswali mengi  ulinizonga 

    “Ahsante Matilda” nilisema, aliondoka zake bila kunijibu chochote kile.  Nilihema kidogo, Kisha nilirudi chumbani, nilimpunguza nguo Zaylisa  Kisha nilimlaza vizuri, alikua hajitambui kabisa 

    Kisha nilitembea taratibu na Kuketi kitini, nilimtazama tena Zaylisa Kisha  nilijiuliza ni kwanini amelewa, lini alianza kutumia kilevi? Maana katika  mahusiano yetu sikupata kabisa kumwona akitumia pombe  

    Nilipogeuza shingo yangu kuelekea Upande mwingine ilinijia ile taswira ya  yule Mtu nisiyemfahamu, yule Mwanaume aliyekuja muda mfupi kabla ya  Zaylisa kuingia. Nilijiuliza alihitaji kusema nini, kwanini aliuliza kama hapa ni nyumbani kwa Clara? 

    Kichwa changu kilikua kizito kikiwa na maswali mengi, yaliyotokea siku  iliyopita yaliendelea kuniwinda huku nikiamini kua palikua na Maisha  yangu yaliyorukwa, sikua na kumbukumbu za Maisha Fulani. Nilijikuta tu  chozi likinitiririka bila kujizuia. 

    Sikuweza kupata hata lepe la Usingizi, nilielekea sebleni. Palikua kimya  sana, nilielekea ilipo simu ya Mezani, nilinyanyua na kuipiga namba ya  Clara, Bado ilikua haipatikani. Nilizidi kuchoka sana, nikaketi kochini  nikiendelea kufikiria. Nilijikuta nikipitiwa na Usingizi wa ajabu, Usingizi  ulionichukua bila magutu Hadi kulipo pambazuka

    Niliposhtuka asubuhi, nilipiga mihayo ya Uchovu huku nikijinyoosha  kidogo. Akiili yangu ilivyotulia ilimkumbuka Zaylisa, haraka nilielekea  Chumbani. 

    Zaylisa hakuwepo kitandani, moyo ulinidunda sana nikawa nimekodoa  macho kitandani nilipomwacha ule Usiku, nilijiuliza alikua ameenda wapi?  Mara nilisikia Maji yakimwagika mafuni, nikashusha pumzi zangu baada ya  kugundua Zaylisa alikua bafuni. 

    Niliketi kitandani nikiwa nimejiinamia, nilihitaji zaidi kuongea na Zaylisa  ili aniambie kwanini alirudi akiwa amelewa.  

    Alipotoka bafuni alinikuta nikiwa nimekaa kitandani, alikua akijifuta Maji  mwilini mwake akiwa amevalia taulo tu. Alisogea Hadi karibu yangu 

    “Umeamkaje my love” alinisalimia kwa sauti nzuri huku akitoa tabasamu.  

    “Salama japo sio salama sana” nilijibu kama Mtu aliyesusa, basi akaacha  kujifuta Maji akasogea karibu yangu zaidi 

    “Kuna nini?” aliuliza akiwa ananitazama kwa umakini usoni kwangu. 

    “Jana ulirudi ukiwa umelewa, sikuwahi kukuona ukiwa umelewa hata siku  Moja tangu nimekufahamu” nilisema, alipepesa macho yake kama aliingiwa  na mdudu Kisha alinionesha uso wake wa huzuni kidogo akasema 

    “Jana nilipoenda kwa Baba, nilikutana na Mjomba wangu. Alinisemea  maneno mabaya sana kua simjali Baba yangu” alisema Kisha alikatishwa na  chozi, halafu akaendelea 

    “Kiukweli niliumia sana. Sikuweza kuzuia hisia zangu niligombana naye,  nilipotoka nilikua na hasira nikajikuta nikipata wazo la kunywa” alisema,  alikua akidondosha chozi lake. Baada ya Mama yangu na Melisa huyu ndiye  Mwanamke ninaye mwamini sana, sikupata hata huo muda wa kuchuja  maneno yake 

    Nilimvuta na kumkumbatia huku nikikisikia kilio chake kwa karibu zaidi.  Nililengwa na Mchozi lakini sikutaka utoke, niliuzuia huku nikimbembeleza 

    “Pole Mpenzi wangu, ukiwa katika Hali ya huzuni unanifanya naumia.”  Nilisema kwa sauti ya utaratibu iliyojaa mapenzi, Zaylisa akajitoa mwilini  Kisha akafuta chozi lake kwa kutumia mikono yake, akanitazama usoni  akaniambia 

    “Samahani sana Jacob”  

    “Hata usijali Mpenzi, nimekuelewa” 

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya KUMI NA MOJA

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love 

    riwaya leo riwaya mpya riwaya za mapenzi

    3 Comments

    1. Salma Ibrahim on September 28, 2025 8:25 pm

      Usituche kila siku kurudia hadithi hiyohiyo kama bando ni bureee.

      Reply
    2. Frank1146 on September 28, 2025 8:38 pm

      https://shorturl.fm/PXhLS

      Reply
    3. Sopu on September 28, 2025 9:39 pm

      Unazingua hadithi kali ila unazingua unachelewa kuleta muendelezo kaka

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 28, 2025

    In the name of LOVE – 10

    Ilipoishia sehemu ya tisa ya In the name of LOVE “Kumbe haikua inshu kubwa sana…

    In the name of LOVE – 09

    In the name of LOVE – 08

    In the name of LOVE – 07

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.