Ilipoishia sehemu ya tano ya In the name of LOVE
Upepo ulikua ukisukuma nywele zake, nilipata shahuku ya kutaka kuongea naye. Nilielekea mlangoni nikafungua mlango taratibu, sauti ya mlango ilimfanya ashtuke na kugeuka. Aliniona nikiwa nimesimama mlangoni nikimtazama, alikua akidondosha chozi bila kuficha.
Tulitazamana bila kusemeshana kwa sekunde kadhaa huku nikitafakari nini maana ya chozi lake, mbona Kila niwapo karibu naye hua nahisi Hali isiyo ya kawaida. Nilisogea taratibu nikimtazama, macho yetu yalikua thabiti yasiyo kwepana
Hadi namfikia hakuna aliyeongea na mwenzake, nilijikuta nikimweka vizuri nywele zake. Endelea
SEHEMU YA SITA
“Clara, Kwanini unalia, muda huu nilitegemea ungekua chumbani kwako” nilimuuliza, swali langu liliamsha chozi lake zaidi. Alidondosha chozi
“Nafikiria kuhusu Melisa, alichokisema wakati wa chakula” alisema Clara, nilikumbuka alichokisema Melisa. Ni kuhusu kunitia Mimi ‘Baba’
“Hilo halina shida, Mimi ni sawa na Baba yake. Au naweza kua Baba yake pale anapohisi anahitaji faraja ya Baba” nilisema, sikujua Masikini Kila neno lilikua kama mwiba kwake, alinitazama kwa jicho la maumivu zaidi
“Natamani Baba yake Angekua Hapa Jacob, Angekua anajua kua Melisa ni Binti yake” alisema.
“Kwani Baba yake yupo wapi?”
“Baba yake hamkumbuki tena Melisa, ameenda mbali na kumbukumbu zake nzuri. Mara ya mwisho ilikua ni siku ya Kumbukumbu ya Kuzaliwa kwa Melisa, tangu hapo hamkumbuki tena” alisema akiwa anamwaga chozi.
“Amemkimbia Mtoto au kimetokea nini?”
Akatikisa kichwa chake, akaniambia
“Asingeliweza kumkimbia, anampenda sana. Naamini ipo siku atamkumbuka Binti yake Melisa” alisema Kisha aliondoka mbele ya macho yangu mithiri ya nyoya la Kuku, upepo ulinipitia akinipita ubavuni na kurejea ndani, aliniacha na maswali mengi yasiyo na Majibu.
Upepo wa baridi ulinisindikiza nikiwa kama nimemwagiwa na Maji ya baridi.
“Jacob” Sauti ya Zaylisa ilisikika nyuma yangu, nilipogeuka nilimwona yeye akiwa anatabasamu.
“Umeniacha chumbani peke yangu Mpenzi, umekuja kupigwa na Baridi huku kweli?” nilitabasamu bila kua muwazi.
“Nilikua…” kabla sijamaliza alinikatisha, akaniambia
“Ulikua unapunga upepo, Mpenzi naumia ukiwa hivi. Kama Kuna chochote unanificha siwezi kujisikia vizuri Jacob, nimeachana na Mwanaume yule kwasababu niliolewa naye kwa shinikizo la Wazazi tu lakini siyo Upendo” alisema, sikutaka ajisikie vibaya. Nilimvuta na kumkumbatia kwa Huba liwakalo moto.
***
Siku iliyofuata, asubuhi ilianza kwa baridi Kali. Nilishtuka na kutoka kitandani, nilitikisa kichwa changu, kidogo nilihisi maumivu ya kichwa hasa upande wa Kushoto.
Nilijikuta nikiwa mwenyewe pale kitandani, Zaylisa hakuwepo.
“Aaah, Aaah” niligugumia kidogo sababu ya maumivu ya Kichwani, nilishusha pumzi nzito huku swali pekee nililojiuliza lilikua
“Zaylisa yupo wapi?” basi nilishusha miguu yangu pole pole, nikaikanyaga sakafu Iliyo baridi. Sakafu Iliyo Kimya isiyonikumbuka, nilitembea taratibu nikafungua mlango pole pole, nikaangaza eneo la Korido. Eneo lote lilikua kimya kama Chumba kilicho tupu.
Kabla sijafanya maamuzi ya kwenda popote nilianza kusikia sauti mbili zikiongea, zilikua ni sauti zenye kumbukumbu ndani yangu. Moja niliitambua kua ni ya Mpenzi wangu Zaylisa, nyingine ilikua ya Clara. Sauti zao hazikuashiria amani, walikua wakiongea kwa mafumbo sana
“Mh‼” niliguna, nikapikicha macho yangu katika Hali ya kuondoa uzito machoni, nikahisi wepesi machoni lakini uzito masikioni niliposikia Clara akisema
“Huu haukua mpango wetu Zaylisa, wewe ni Mke wa Mtu. Kilichokuleta hapa ni nini?” lilikua ni swali dogo lakini lilibeba hatma ya Maisha yangu, hapo hapo nilihisi Ubaridi puani.
Nilivuta tena hewa Kisha niliitoa pole pole, nilikua nimesimama mlangoni Bado.
“Clara, ukitaka kua salama usiyaguse Maisha yangu. Nina ufunguo, nikiamua nafungua popote. Muda wowote ninaoutaka” alisema Zaylisa, sikuelewa walikua wakibishania kitu gani ambacho Kila mmoja alikua
akiongea kwa mafumbo. Basi, niliamua kuzifuata sauti zao nikipita Korido Iliyo Kimya
Baada ya hatua mbili nilijikuta nikisimama taratibu, miguu yangu iligoma kufanya safari. Nilihisi palikua na Mtu nyuma yangu, Mtu huyo alikua kimya lakini alikua na hisia iliyounganishwa na Mimi
Taratibu niligeuka kuangalia nyuma, chumba Cha Mwisho kabisa Mlangoni alikua amesimama Melisa. Huyu siyo Melisa Mtoto, Bali ni Mdogo wangu Melisa, alikua amevalia nguo nyeupe mithiri ya Malaika.
Tabasamu lake lilikua linanipa ujumbe wa Siri niliokua nashindwa kuufungua. Jicho langu Moja lilianza kudondosha chozi, pole pole midomo yangu ilianza kutetemeka
Tabasamu la Melisa lilikua thabiti machoni pangu, lilikua ni tabasamu lile lile lililofanana na Marehemu Mama. Jicho lingine likadondosha chozi la Hisia Kali ya maumivu, nilinyoosha Mkono ili Melisa aje kwangu
Alikua ameshafariki lakini kwanini nilikua namwona, sikuweza kupata Majibu.
“Melisa” niliita, aliendelea kutabasamu tu. Kisha alisema
“Kumbuka Kaka, usijipoteze kamwe, kumbuka wewe ni Nani. Wewe ni Jacob, Ndiyo jikumbuke Kaka….” Alisema huku akinitazama Usoni, nilikua na maswali mengi lakini mdomo Wangu uligoma kuuliza chochote.
Nilianza kutembea kuelekea alipokua amesimama, sikutaka kuchelewa nilitaka kumkumbatia Melisa, nilikua nimemkumbuka sana. Nilisogea na kumkumbatia kwa hisia Kali sana, nililipata joto lake, nilihisi kua Sehemu salama sana Maishani mwangu
“Melisa, nimekukumbuka sana. Usiondoke ukaniacha tena” nilisema huku chozi langu likimdondoka mabegani kwa Melisa
“Usiniache tena, Baki na Mimi. Nakuahidi sitaondoka tena, sitakuacha peke Yako…..nitakulinda Maisha yangu yote, nitatimiza ahadi zangu..” nililia sana, sikutegemea kama ningemwona tena Mdogo wangu Melisa
Nilikaa kimya kusubiria aseme chochote, nilipepesa macho yangu pole pole.
Japo nilizungumza sana lakini kwa Melisa ilikua kimya, palikua kimya zaidi ya kimya nilichowahi kukisikia. Kama vile Dunia ilikua ikisimama na Kila Mtu akiwa anasubiria jambo Fulani, ghafla nikaisikia sauti kutoka kwa Melisa
“Babaa” ilikua ni sauti ya Mtoto mdogo, nilihisi kurukwa na akili yangu. Nilijikuta nikiwa nimechuchumaa nikiwa nimemkumbatia Mtoto Melisa, sikuamini kua ilikua ni ndoto ya kutisha iliyokua ikitembea.
Niliinua uso wangu, Ndiyo‼ Melisa Alikua mbele yangu, aliniita tena
“Babaa‼” huku chozi likiwa linamtiririka, nilihisi kuvuta hewa nzito yenye joto, halafu kabla hata sijafikiria zaidi nilisikia sauti ya kugombana. Clara na Zaylisa walikua wakigombana Sebleni
Haraka nilikimbilia Sebleni, nilimkuta Msichana wa kazi akiwa anaamua ugomvi wao, sikujua walikua wakigombana nini lakini Zaylisa alikua akilia baada ya kuniona Kisha alinifuata na kunikumbatia akiniambia
“Jacob, Clara hataki niishi hapa” alisema huku chozi likiwa linamvuja, nilinyanyua uso na kumtazama Clara, niliona jinsi alivyopata Kigugumizi kusema. Lakini nilihisi alikua anataka kujitetea, nilimkagua na Msichana wa kazi. Naye alinitazama kidogo kwa aibu halafu akamtazama Clara
Pale pale Melisa aliingia na kwenda Moja kwa moja kwa Mama yake Kisha akamkumbatia huku naye chozi likimbubujika, hata sura yake ilionesha huzuni sana. Nilijihisi kutoelewa Kila kitu nilichokiona na kukisikia
Chembe chembe ya maumivu iliniingia ghafla, macho yangu yakachemka chem chem ya Machozi mithiri ya Mtu aliyewekwa pilipili machoni, nilimkubatia zaidi Zaylisa.
Sikujua walikua wakigombana nini lakini nilichagua kua Upande wa Zaylisa, hisia ziliniambia alikua akionewa na Clara.
Nilimtazama tena Clara, niliona akinyanyua midomo yake ili aongee lakini nilitikisa kichwa changu kuashiria kua asiongee chochote sababu nilielewa.
Niliondoka na Zaylisa, tukaelekea chumbani taratibu huku Zaylisa akilia kwa sauti ya chini, Melisa alinitazama, nilihisi alihitaji sana kuniambia kitu Fulani muhimu lakini alikua amefungwa minyororo ndani ya akili yake .
Miguu yangu ilihesabu hatua pole pole Hadi tulipozama na kufunga Mlango. Nilimtazama Zaylisa, macho yake yalikua mekundu kwasababu ya kulia, nilimketisha kitandani Kisha nilitumia kitambaa kumfuta chozi lake taratibu kama Daktari wa Macho.
“Asante..” alisema. Nilimshika mikono yake huku uso wangu ukiwa na Upole usio mithirika.
“Mpenzi wangu” hatimaye nilisema. Alinitazama zaidi, sikuona hata chembe ya Uwongo machoni pake
“Pole kwa kilichotokea, sijui ilianzaje lakini….”
“Jacob, hauniamini?”
“Hapana Mpenzi sijasema sikuamini, lakini haikua njia nzuri kulumbana naye kiasi kile. Nafikiria ingekua busara zaidi ungenieleza bila kubishana naye” nilisema kwa sauti ya Upole, Mungu alinijaalia sauti nzuri na nzito iliyotoka kwa mpangilio
“Kilichomiuma, aliniita Masikini pia changudoa. Tokea umenijua umewahi kuniona Mimi nikiwa changudoa Jacob? Hilo la Umasikini halina shida kwangu kwasababu pesa zinatafutwa” nilishusha pumzi zangu Kisha nilipepesa macho yangu huku feni ya juu ikiendelea kuzunguka na kutupatia Upepo
“Wacha nikazungumze naye, nimkanye asirudie kukuita hivyo na kama atarudia basi tutaondoka hapa”
“Jacob….Haina haja, sitaki uende mbali Mpenzi wangu, kaa kando yangu” alisema Zaylisa Kisha alijilaza mapajani mwangu, aliizuia rasmi nia yangu ya kwenda kwa Clara. Nilitabasamu na kuanza kuchezea nywele zake
“Itakuaje akitufukuza?” aliniuliza Zaylisa.
“Tutatafuta Sehemu ya kuishi Zaylisa.”
“Jacob, hauna kazi upo hapa tu unafikiria itakua rahisi?”
“Sasa nifanye nini au nikueleze nini Mpenzi, nimefukuzwa kazi kule Mgahawani. Nimewapoteza Mama na Mdogo wangu Melisa, ndani ya kipindi kifupi Kila jambo limebadilika, nikuonapo nahisi tumaini kubwa likichipua ndani yangu, sitaacha nitapambana”
“Siku Moja ntakuambia nini Cha Kufanya Jacob, ukifanya hicho utakua na pesa nyingi na hakuna Mtu atakaye thubutu kucheza na Utu wako” alisema Zaylisa, aliniacha na mzigo mzito wa maswali yasiyo na Majibu, nilijiuliza ataniambia nifanye nini ili nipate pesa nyingi kiasi hicho
Niliendelea kumbembeleza taratibu huku tukiuruhusu ukimya utawale. Nywele za Zaylisa zilikua laini, zilinipa Raha kuzipapasa
Mara mlango uligongwa, Zaylisa aliinuka Kisha alinitazama. Sote tulijiuliza ni Nani aliyekua anaugonga mlango, Mimi nilinyanyuka na kuelekea Mlangoni, nilipofungua nilikutana na sura ya Msichana wa kazi, alianza kunitazama kwa jicho la Upole sana Kisha akaniambia
“Dada anakuita” niligeuka kumwangalia Zaylisa, hakusema chochote ila alinitazama kwa jicho la kuniambia kua nitakacho kiamua kitakua sawa kwake. Nilishusha pumzi kidogo halafu nikamjibu
“Sawa, nakuja” sauti ya taratibu iliyojaa uzito ilinitoka. Yule Msichana aliondoka zake, nilifunga mlango. Nikamwangalia tena Zaylisa, nilishusha pumzi Kisha nikafungua tena mlango nikatoka kwa ajili ya kwenda kuonana na Clara.
Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya SABA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love