Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    In the name of LOVE – 01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป In the name of LOVE – 01
    Hadithi

    In the name of LOVE – 01

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoSeptember 8, 2025Updated:September 10, 20258 Comments8 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    โ€œJacob, nataka kuujua Msimamo wako kwangu. Utaniowa lini?โ€ Aliulizaย  Zaylisa, Nilishusha pumzi zangu. Nikageuka huku na kule kama Kuna Mtu alikua anatusikiliza pale Mgahawani. Nilikua nimevalia sare zangu za kaziย  ya Uhudumu wa Mgahawa.ย ย 

    โ€œZaylisa, naomba univumilie Hadi Mama yangu apone. Unajua fikaย  anaumwa, Mimi Ndiyo tegemezi. Halafu isitoshe Mpenzi wangu kwasasaย  kipato changu kipo chini unafikiria Wazazi wako watanielewa?โ€ย  Nilimuuliza, kiukweli nilikua napitia kipindi kigumu Cha kifedhaย 

    โ€œHadi lini Jacob?โ€ aliniuliza huku akianza kutokwa na Machozi, machoย  yake yalijaa Upendo sana lakini nilihisi Kuna jambo lililokua likimsumbuaย 

    โ€œMpenzi nivumilie tu, najua unavyojisikia lakini haiwezi kuchukua mudaย  mrefu nitakua nimejipataโ€ Ghafla Zaylisa aliondoka akiwa anakimbia hukuย  akionekana kama analia, sikuweza kumsimamisha sababu ulikua ni mudaย  wa kazi na sikutaka Mtu yeyote ajuwe kinachoendelea.ย 

    Nilijaribu kumpigia simu lakini hakupokea, niliumia sana. Sikutaka kuaย  chanzo Cha Zaylisa kulia, mara zote alikua akinihimiza kwenda kwaoย  kujitambulisha lakini nilijawa na hofu.ย 

    Familia Yao ilikua na uwezo kifedha, Mimi nilikua masikini ninayeishiย  kumlea Mama yangu mgonjwa. Basi nilishusha pumzi Kisha nikaendelea naย  kazi huku nikiwa mnyonge sana.ย ย 

    ***ย 

    Usiku baada ya Muda wa kazi kwisha nilijiandaa kwa ajili ya kuondoka.ย  Lakini ghafla alikuja Mdogo Wangu Melisa, alikuja mbio kama Mtuย  anayefukuzwa, alishindwa hata kuongea huku akisema.ย 

    โ€œKaka, Mamaaa!โ€ย 

    โ€œMama amefanya nini Melisa?โ€ nilimuuliza huku mapigo ya Moyo Wanguย  yakianza kwenda Mbio, hisia mbaya iliniingia. Nilihisi Kuna jambo lisilo laย  kawaida lilikua limetokea, hisia mbaya iliendelea kunipanda. Harakaย  nikamwambia rafiki yangu Sudi kua naelekea nyumbani.

    Tuliondoka mbio pale kuelekea Nyumbani, kutoka kazini kwangu Hadiย  nyumbani siyo mbali sana. Tulipofika, nilihisi mwili Wangu ulikuaย  unaishiwa nguvu baada ya kumwona Mama akiwa ananingโ€™inia kwenyeย  Kamba. Macho yalinitokaย 

    โ€œMamaaโ€ผโ€ nilimwita, alikua ameshajinyonga chumbani kwake. Nilifanyaย  haraka kufungua nikiamini pengine nitaweza kuokoa uhai wake.ย ย 

    Basi nikaita Bajaji haraka, tukampeleka Mama Hospitali. Nilimtazamaย  Mdogo wangu akiwa analia, iliniuma sana, tumaini la Mama kua hai lilikuaย  dogo sana.ย ย 

    Tuliketi Sehemu ya kumsubiria daktari aliyeingia chumbani, nilimkumbatiaย  mdogo wangu Melisa, roho iliniuma sana. Zilipita dakika kumi na tano,ย  daktari alitoka Kisha alisimama mbele yetuย 

    โ€œMnifuateโ€ alisema yule Daktari, haraka tulimfuata kuelekea kwenyeย  chumba kimoja. Alitukaribisha vizuri sana huku akiachia tabasamu kanaย  kwamba alikua na habari njema ya kutuambia kuhusu Hali ya Mama yetu.ย 

    โ€œNyie ni Nani yake?โ€ aliuliza. Tulitazamana Mimi na Melisa, tulihisi amaniย  ndani yetu.ย ย 

    โ€œWatoto wakeโ€ nilijibu Kisha nilimwulizaย 

    โ€œHali yake ipoje Dokta, ni mzima?โ€ Daktari akabadilisha uso wake,ย  akaondoa tumaini mioyoni mwetu, sura yake ikaonesha kua Kuna asilimia sifuri ya Uhai wa Mama yetu.ย ย 

    โ€œPoleni, amefarikiโ€ alisema.ย ย 

    โ€œMamaa!โ€ aligumia Melisa, pale pale alipoteza fahamu. Tulianzaย  kuhangaika na Hali ya Melisa, akakimbizwa wodini haraka. Chozi lilikuaย  likinibubujika bila kukoma, hapakua na Mtu kando yangu wa kuhisiย  maumivu yangu, Niliketi peke yangu nikiweweseka, sikujua nilishike lipi niliache lipiย 

    Moyo Wangu uligawanyika, upande mmoja alikuwepo kwa Meliza naย  Upande mwingine alikuwepo kwa Marehemu Mama yangu. Dunia ilikuaย  nzito, ilishuka kichwani kwanguย 

    Chozi lilikua likinibubujika, siku yangu iliharibika dakika za jioni kabisa.ย ย 

    Nilijiinamia, nilikosa tumaini. Ghafla nilihisi kuguswa begani, nilishtuka.ย  Niliinua kichwa changu ili nimtazame aliyenishika

    Macho yangu yalikutana na sura ya Mwanamke mmoja, sikukumbuka kamaย  niliwahi kumwona popote katika Maisha yangu, sikumfahamu lakini suraย  yake ilionesha kunitambua na kuguswa na ninayoyapitia. Nilifuta choziย  langu Kisha nilijiweka tayari kumsikilizaย 

    โ€œPole..โ€ sauti yake ya kwanza ilinifanya nizidi kudondosha chozi, alikua niย  Mtu wa kwanza kunitia moyo. Niliitikia kwa kichwa, mdomo Wangu ulikuaย  mzito, ulikua ukitetemeka tu.ย 

    โ€œNaitwa Clara, sijui kama unanikumbukaโ€ nilitikisa kichwa changuย  kuashiria kua nilikua simkumbukiย ย 

    โ€œUsijali, kimetokea nini? Ulitoka mgahawani mbio, niliguswa sana. Hataย  hivyo Mimi ni mteja uliyenihudumia kwenye meza namba 6โ€ Niliitikia kwaย  kichwa huku chozi likinibubujika, sikuweza kusema chochote zaidi ya kulia.ย  Akaniweka kifuani pake, alionesha kunijali sana. Nililia Hadi nililalaย  kifuani kwake, akaja kunishtua saa Sita Usikuย 

    Melisa alikua amesharejesha fahamu, daktari alitupatia utaratibu wa jinsiย  ya kuuchukua mwili wa Mama. Gharama zote za Hospitali akazilipa Claraย 

    โ€œAsante sana Claraโ€ nilimshukuru, sijui ningetoa wapi pesa za matibabu yaย  Melisa pamoja na gharama za kutoa Mwili wa Mama.ย 

    โ€œUsijali, tutakua pamoja Hadi mwisho Jacob. Mungu alipanga iwe hiviโ€ย  alisema. Tukaurudisha mwili wa Mama nyumbani, tulipofika tulikutaย  ndugu wengine wakiwa wamefika hapo, Mjomba Masawe alikuaย  amesimama Mlangoni Kisha akaniuliza swaliย 

    โ€œHukuona umuhimu wa kutupigia simu Hadi tumetaarifiwa na Majirani?โ€ย  alikua amekasirika, mara zote yeye ni mkorofi sana.ย 

    โ€œAnko, ningewezaje? Nilikua nimechanganikiwa sana. Samahaniโ€ nilisema,ย  Clara aliniangalia kwa jicho lenye maswali mengi sana. Basi akatupishaย  tukaingiza maiti ndani, taratibu na mipango ya mazishi ikaanzaย 

    Hakuna aliyenishirikisha kwa lolote, walikaa vikao vyao vya Siri naย  kupanga taratibu zote. Sikujali sana sababu hata Mama alipokua haiย  walikua ni Watu wenye Hila zao, hawakutaka sisi tuishi kwenye nyumbaย  Yao ya Urithi, walipigania kuiuza ila Mama ndiye aliyekua kizuizi chao.ย 

    Siku iliyofuata, mazishi ya Mama yalifanyika. Baadaye kikao Cha familiaย  kiliketiย 

    Walikubaliana kwa Kauli Moja kua Mimi na Melisa tuondoke, wanauzaย  nyumba Yao. Hatukua na mahali pa kwenda. Nilimtia moyo Melisa,ย 

    tulikusanya Kila kilicho chetu, hatukujua tungeenda wapi, hatukujuaย  tungeishi vipi lakini tulijipa moyo kua Kila kitu kitakua sawaย 

    Tulienda kwa Sudi maana ndiye Mtu pekee ambaye ningeweza kwendaย  kwake na kutarajia msaada, ni rafiki pekee niliye naye. Sudi alitupokeaย  vizuri tu lakini palikua na kikwazo kimoja, tutawezaje kukaa wote watatuย  chumba kimoja, Melisa ni Mwanamke angalau Angekua Mwanaumeย 

    โ€œKaka, tusaidie kwa siku kadhaa wakati Mimi nahangaika nijue nampelekaย  wapi Melisaโ€ nilimwambia Sudi, akamtazama Melisa Kisha akakubali.ย ย 

    Tulianza Maisha mapya nyumbani kwa Sudi, siku iliyofuata nilimtafutaย  Zaylisa maana tokea ile siku hatukuwasiliana tena. Simu ya Zaylisa ilikuaย  haipatikani, ilianza kunipa Mashaka. Hapakuwahi kutokea siku Zaylisaย  asipatikane kwa simu, nilijiuliza huwenda alikua amepata tatizo maanaย  sikumwona hata kwenye Mazishi ya Mama.ย 

    Tuliondoka na Sudi kuelekea kazini, nilifanya kazi Hadi mida ya Mchana.ย  Baadaye niliitwa na Bosi, nilitegemea kusikia akinipa pole lakini Hali ilikuaย  ya tofauti kabisa, alinieleza kua hawezi kuendelea na Mimi kwambaย  amepata Mtu mwingine.ย ย 

    โ€œBosi, kwanini ni ghafla?โ€ย ย 

    โ€œJacob, siku zote Shilingi Ina pande mbili. Huu ni upande mwingine ambaoย  ulikua hauutazamiโ€ alisema, nilihema. Sikutegemea kabisa kamaย  ningeikosa kazi bila sababu ya Msingi tena ndani ya Siku chache tu zaย  Matatizo ya kufiwa na Mama yangu.ย 

    Miguu yangu ilikufa ganzi, mwili mzima ulikua ukiweweseka lakini manenoย  ya Bosi yalikua kama msumali wa mwisho uliogongwa moyoni mwangu,ย  kilichoniumza zaidi ni Maisha tunayoishiย 

    โ€œAsante Bosi..โ€ Nilisema, Kisha niligeuka na kuondoka zangu, sikuaminiย  kama nilikua nikiziacha Kuta nilizozizoea, Watu niliowazoea hata kelele naย  usumbufu wa wateja ambao nilishauzoea.ย ย 

    Sudi alipoiona sura yangu alijua nilikua nimezongwa na mawazo, nilipotezaย  Nuru. Niliona nimepoteza thamani juu ya uso wa Dunia, nilihisi uzito waย  Mzigo mwingine mzito nilioubebaย 

    โ€œJacobโ€ฆMbona una huzuni?โ€ aliniuliza Sudi, nilishusha pumzi hukuย  nikizuia chozi lisinitoke mbele yake. Nikajikaza Kiume lakini moyo Wanguย  ulijenga ufa.

    โ€œMoshi mweusi Sudi, nimepoteza tena Mimiโ€ nilisema, ule Ujasiri ulianzaย  kuondoka niliangusha kilio mbele ya Sudi, chozi likinitiririka.ย ย 

    โ€œUna maanisha nini?โ€ย 

    โ€œSina kazi tena, nimefukuzwa. Sijui nimeambukizwa mkosi gani Sudi, sijuiย  wengine wamemfanyia nini Mungu ambacho Mimi sifanyiโ€ย 

    โ€œShii! Bro, nenda nyumbani, tutaongea zaidi hukoโ€ alisema Sudi,ย  niliondoka kazini taratibu. Macho yangu yalikua yakiyatazama mazingiraย  ya Mgahawa kwa mara ya mwisho, nilitembea kama Mtu aliyepoteza Kilaย  kitu.ย ย 

    Nilipofika nyumbani kwa Sudi, nilimkuta Melisa akiwa ameketi kwenyeย  kochi dogo, aliponiona aligundua haraka sana kua siko sawa, alinifuata naย  kunikumbatia. Sikusita kulia tena mbele yake, nilikosa ule Ujasiri waย  Kiume mbele yakeย 

    Tuliketi nikamsimulia kilichotokea, niliona jinsi hata moyo wakeย  ulivyosononekaย 

    โ€œUlifanikiwa kumpata Wifi kwenye simu?โ€ aliniuliza baada ya kumalizaย  kumsimulia kuhusu kazi. Kiukweli Hadi muda huo simu ya Zaylisa ilikuaย  haipatikani, sikujua kama alipatwa na tatizo au aliamua kuzima simu yake,ย  kwa jinsi nilivyokua namfahamu isingelikua rahisi akae siku zote hizo bilaย  kuwasiliana na Mimi.ย 

    โ€œMelisa, Usijali. Naenda kwao sasa hivi nikazijue mbivu na Mbichi. Usijaliย  Mdogo wangu, Kila kitu kitakua sawa. Nitampata pia nitapata kazi nzuriย  itakayobadilisha Maisha yetuโ€ nilisema, angalau nilifamfanya atabasamuย  kidogo, nikamfuta chozi lakeย 

    โ€œVipi ulikula?โ€ย 

    โ€œNdiyo Kaka, nimebakiza kwa ajili Yakoโ€ย ย 

    โ€œUsijali, nikirudi nitakula sawa?โ€ย 

    โ€œSawa, unaenda sasa hivi eeeh?โ€ย 

    โ€œNdiyo, angalau nikimwona nitajisikia ahueni. Ubaki salamaโ€ nilisemaย  Kisha niliondoka.ย ย 

    **ย 

    Nilipofika nyumbani kwao Zaylisa ilikua ni mishale ya jua la utosi lililokuaย  likikimbia haraka, jasho lilikua likinitoka maana nilitembea kwa umbaliย 

    mrefu. Nilishtuka kuona palikua na magari mengi, pia Watu walikua wengi.ย  Ilinifanya nijiulize maswali mengi yasiyo na Majibuย 

    โ€œKuna nini? Itakua amepatwa na Tatizo gani, au labda amefiwa na Wazaziย  wake, auโ€ฆ?โ€ kabla hata sijamaliza kutafakari nilimwona Mtu mmoja akijaย  upande Wangu akitokea nyumbani kwao Zaylisa. Niliona ni Boraย  nimuulize, nilimsimamisha Kisha nilimsalimia kwa sauti ya kiungwanaย  sana, baadaye nikamuulizaย 

    โ€œSamahani Kaka, pale Kuna nini mbona naona Kuna Watu wengi?โ€ย  akanitazama Kisha naye akageuka kuangalia tena kama vile hakutokeaย  huko, Kisha akaniulizaย 

    โ€œWewe ni ngeni hapa mtaani?โ€ nikajichekesha chekesha kidogo Kishaย  nikamjibuย 

    โ€œNdiyo, nilikua napita tu.โ€ย 

    โ€œKuna harusiโ€ย 

    โ€œHarusi?โ€ย 

    โ€œNdiyo, vipi umeshtuka Mzee?โ€ย 

    โ€œNani anaolewa?โ€ย 

    โ€œMtoto wa Mwenye nyumba anaolewa, anaitwa Zaylisaโ€ alisema Kishaย  aliondoka zake, hakujua alikua ameupasua moyo Wangu kiasi gani, hakujuaย  alikua ameuunguza moyo Wangu kwa kiasi gani. Chozi la pole pole lilianzaย  kunitoka, nilihisi kuishiwa nguvu.

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya PILI

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xxย 

    riwaya leo riwaya mpya riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za mapenzi

    8 Comments

    1. Sheila2693 on September 8, 2025 7:17 pm

      https://shorturl.fm/AdLg6

      Reply
    2. Vivian1029 on September 8, 2025 7:54 pm

      https://shorturl.fm/uQzHP

      Reply
    3. Zhen on September 8, 2025 10:37 pm

      Naqubali

      Reply
    4. Bingwa on September 8, 2025 11:10 pm

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ˜”

      Reply
    5. Celeste1151 on September 9, 2025 5:08 am

      https://shorturl.fm/ZSSyX

      Reply
    6. vzfwgrulvj on September 9, 2025 8:09 am

      wtmpejopseftlhugezzqkjgiyifqzi

      Reply
    7. ๐Ÿ”‘ ๐Ÿ’ฐ Limited Offer: 1.25 BTC bonus waiting. Activate today โ†’ https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=abf1b242921621c338c5ff3518b9c02a& ๐Ÿ”‘ on September 9, 2025 9:20 pm

      8iqutt

      Reply
    8. ๐Ÿ“ช ACCOUNT NOTICE - Unauthorized transfer of 0.9 BTC. Stop? > https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=abf1b242921621c338c5ff3518b9c02a& ๐Ÿ“ช on September 10, 2025 11:02 am

      z4zfch

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 11, 2025

    In the name of LOVE – 03

    Ilipoishia sehemu ya pili ya In the name of LOVE โ€œSikumbuki chochote Clara, natamani nikumbuke…

    In the name of LOVE – 02

    In the name of LOVE – 01

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 08

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.