Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Huyu Ndio Beki Katili Wa Nyavu AFCON
    Africa | CAF

    Huyu Ndio Beki Katili Wa Nyavu AFCON

    MhaririBy MhaririJanuary 24, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Beki Katili Wa Nyavu AFCON
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mpaka sasa yale majina makubwa ambayo yalikua yanategemewa kuwa yataibuka kuwa wafungaji bora wa michuano ya mataifa barani Afrika(AFCON) wamezidiwa kwa idadi kubwa kabisa ya magoli na mchezaji ambaye hakutegemewa kabisa kama atakua na mabao mengi kiasi hiki mpaka sasa.

    Anaitwa Emilio Nsue ambaye akiwa katika klabu yake ya CF Intercity ambayo inashiriki ligi daraja la tatu anacheza kama kama beki wa kulia lakini katika timu yake ya taifa ya Guinea ya Ikweta anacheza kama mshambuliaji huku nafasi hiyo ikimlipa zaidi katika michuano hii kwani mpaka sasa anaongoza orodha ya wafungaji bora akiwa na mabao 5 huku anayemfuatia akiwa na mabao 2.

    Katika maajabu ambayo yametokea katika michuano hii, Nsue ndie mchezaji pekee ambaye amefunga mabao matatu katika mchezo mmoja huku akiwafunga mabao 2 wenyeji wa michuano ya msimu huu timu ya Ivory Coast.

    Katika hatua ya makundi ambayo mpaka sasa inaelekea kutamatika huku baadhi ya timu za taifa zikiwa tayari zimefuzu katika hatua inayofata ya 16 bora mchezaji pekee ambaye alifunga zaidi ya mabao 5 katika hatua ya makundi ni Laurent Pokou kutoka nchini Ivory Coast ambaye alishinda mabao 7.

    Kuna wakati unajiuliza kwanini yale majina makubwa kutoka ligi kubwa mbalimbali ulaya hawajafanikiwa kufikia idadi kubwa kama hii aliyonayo Nsue lakini unaamua kukaa kimya na kuendelea kuamini maneno ya Rais wa Shirikisho la soka Afrika (CAF) Patrice Motsepe aliposema michuano hii itakua michuano bora zaidi kutazama barani Afrika.

    Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mara nyingi huleta pamoja wachezaji wanaotoka katika ligi tofauti duniani, na ni wazi kuwa wachezaji wanaotamba katika ligi kubwa ulaya hawatilii sana maanani katika AFCON. Hali hii inaweza kueleweka kwa kuchambua mambo kadhaa yanayoweza kuchangia utendaji duni wa wachezaji hawa wakati wa michuano hiyo.

    Wachezaji wanaotoka katika ligi kubwa ulaya mara nyingi hupata changamoto kubwa kutokana na tofauti za utamaduni na mifumo ya timu wanazojiunga nazo katika AFCON. Wanaweza kuwa hawajazoea mifumo mipya au njia tofauti za kucheza, na hivyo kuchukua muda Kwenda saw ana mazingira ya timu husika.

    Wachezaji wa ligi kubwa ulaya mara nyingi hushiriki katika msimu mrefu na unaoshughulika na mashindano mengi kama vile Ligi Kuu ya England, La Liga, Serie A, na Bundesliga. Kabla ya kushiriki katika AFCON, wengi wao wanaweza kuwa wamechoka kimwili na kiakili kutokana na majukumu mengi ya michezo wanayoshiriki.

    SOMA ZAIDI: Tanzania Dhidi Ya DR Congo Ni Vita Ya Kujuana

    AFCON 2023 Emilio Nsue

    1 Comment

    1. Pingback: Taifa Stars Ilikosa Kujiamini Hakukua Na Mipango Sahihi - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.