Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Goryanah Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Goryanah Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJune 5, 2024Updated:June 11, 202430 Comments6 Mins Read8K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya ya Goryanah
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Utangulizi: 

    Katika dunia hii kila mtu amekuwa akiuchukia umaskini, na familia zisizokuwa na uwezo nazo zimekuwa zikifedheheshwa na watu matajiri wakiamini katika jamii hawana mchango wowote! Leo tunakutana na binti aitwae GORYANAH kwa kifupi muite (GORII )ni binti shupavu mwenye umri wa miaka kumi na saba anaishi na mamake mzazi pekee kwani Babake alipoteza maisha ikiwa bado ni binti mdogo.

    Mamake huwa anauza mbongambonga analangua kwa wakulima kisha anampatia binti yake kutembeza mtaani huku yeye akiendelea kuchoma vitumbua nyumbani kwake ilimradi wazidi kuzichanga shilingi. Ndoto kubwa ya binti Goryanah aliamini ipo siku atauepuka umaskini katika familia yake kama ataongeza nguvu katika kupambana, fedhea kwa mamake kuitwa “msimbe” zitaisha endapo watapata pesa nzuri!

     

    SONGA NAYO… SEHEMU YA KWANZA

    Huku mtaani Goryanah alikuwa akizidi kutembeza mboga mboga! Jua nalo halikuangalia kuwa binti huyu anapitia wakati mgumu liliweza kuangaza zaidi misiri ya Moto uwakao.

    Goryanah alifika kwenye mti mkubwa uliokuwa na kimvuli aliamua kutua hapo, huku akichukua chupa yake ya maji angalau anywe! Wakati akiwa anamalizia kunywa alisikia sauti ikimuita kwa nyuma ilibidi ageuke.

    “” Mudy! Ulijuaje kuwa nipo hapa!

    “”Dada Gorii!!” Siku ya leo naona biashara ni ngumu! Nimejaribu kutembeza matunda hutaamini watu hawanunui! Hapa nawaza labda twende stand angalau tutauza!?” Goryanah Alibaki akimtizama, Kisha alimpatia chupa ya maji anywe.

    “” Utakuwa na kiu Sana mudy! Ila na wewe unisaidie, Mimi na njaa huwezi kunipatia hata ndizi mbili tu nikapunguza njaa?

    “” Aaah! Dada Gorii” unajua huwa wanisaidia sana! Mimi nikikutana na wewe naomba uchukue tu! Kuhusu mama nitamwambia ziliharibika!”

     

    Goryanah aliishia kucheka huku akichukua zile ndizi na kuanza kula, baada ya kumaliza kula ilibidi amgeukie.

    “” Lakini mudy! Mi kwenda stand haitowezekana! Mimi nauza mboga mboga! Stand wamejaa wasafiri hawawezi kununua! Fanya hivi wewe nenda ukatembeze stand, Mimi naingia mtaani! Jioni tukutane hapa ili tuaangalie mahesabu Kama tutakuwa tumefanikiwa!

    “” Sawaa! Kuwa makini Dada” halafu usipite zile chocho unazopitaga Kuna wahuni huwa wanakuwinda!”

    “” Usijali, Goryanah ni binti jasiri! Anapambana na watu waovu siku zote! Kuwa makini hata wewe wasikunyanganye matunda pamoja na pesa.

    Huku mtaani Goryanah alikuwa akizidi kutembeza mboga mboga! Kuna wamama walikuwa wakisukana walimuita akawa ameenda.

    “” Wewe Binti wa Ma’ Goryanah! Naona unamsaidia mamako mlipe Kodi! Kazana make hii mabibo mtazidi kuhama hama muda wote!

    Ni mama mmoja aliongea huku akizidi kuchagua mboga mboga, upande wa pili kulikuwa kunae kina mama wawili wakizidi sukana, walimtizama Goryanah Kisha walinong’onezana.

    “” Huyu ndie binti yake! Mamake anatoka na mzee rajab Yule! Naskia ameungua! Daaah! Maskini binti wa watu atabaki yatima sahii tu! Sijui maisha ndio yalimfanya mamake amchukue Yule mzee apate kula!?”

    Wakati wakizidi kuzungumza Goryanah hakuwasikia, muda wote alikuwa akihesabu pesa alizoziuza Kisha aliweka kwenye kimkoba alichokuwa akitunzia pesa!

    Baada ya kumaliza mboga zote ilibidi arudi kwenye ule mti waliokubaliana watakutana! Alikaa huku akimsubili Mudy Kisha alitoa pesa huku akizihesabu, siku hiyo alikuwa amekusanya Kama elfu kumi na moja na Mia mbili, wakati akizidi kuhesabu Kuna kikaratasi kilianguka ilibidi akiokote Kisha alikikunjua akisome.

    “” Huyu nae Kila siku haishi kuniletea vibarua! Eti anioe ili niepukane na kuungua jua! Ani ananionea huruma Mimi! Sa akifanya vile ndio ataniepusha umaskini vipi kuhusu mamangu!?”

     

    Goryanah ilibidi acheke kwanza, huku akiichana ile karatasi! Kwa mbali ndio anamuona Mudy akija na beseni lake likiwa tupu huku akicheza cheza njiani.

    “” Ooh! Afadhari hata Mudy nae kamaliza! Muone anavyocheza kwa furaha! Barabara kaifanya yake!”

    Mudy baada ya kufika ilibidi akae kwanza chini Kisha alijilaza kwenye mchanga chali akibaki kutizama mti ule, alimuita Goryanah kwa kifupi.

    “” Gorii! Unajua leo umeninenea vizuri! Hutaamini nimefika pale stand! Kuna wasukuwa watatu wamenunua ndizi zote!”

    Goryanah baada ya kusikia vile ilibidi alale nae kifudifudi huku akikaa sitaili fulani ya kumsikiliza mtu kwa umakini.

    “” Ni wasukuma watatu ndio wamenunua!?” Kwanini wawe wasukuma tu!?” Mudy alicheka huku akigeuka kumtizama Goryanah! Kisha aliongea..

    “” Mamangu anaumwa ujue! Nimemuacha akikohoa muda wote! Sijui ni vumbi la shambani, majuzi kati tulienda kupalilia mihogo nahisi ni hili vumbi ndio limemuathili.”

    Goryanah ilibidi akae huku akikumbuka kipindi yupo anauza mboga alisikia kwa mbali wale wamama wakimuita Msimbe(mwanamke aliyeachika au asiye na mme) mamake” Ilibidi ajikaze japo hapendi kusikia mamake akiitwa vile.

    “” Tuondoke kwanza! Hata Mimi mamangu atakuwa akinisubili kwa hamu!”

    Mudy aliinuka taratibu, walianza kutembea huku sitori zikiendelea njiani, lakini kwa Mudy alikuwa akitembea Kama akichechemea Gorii alimuona ilibidi amsimamishe Kisha alichuchumaa chini.

    “” Ayaa! Nyanyua mguu wako nijue umekuwaje? Make watembea ukichechemea.”

    Mudy baada ya kuinua mguu, alikuwa kajeruhiwa na chupa, Gorii ilibidi amkalishe chini Kisha alitizama upande wa pili aliona Kuna mgomba, alitabasamu Kwanza huku akikimbia kuchukua jani la mgomba akija nalo taratibu akilipikicha.

     

    “” Hii inakata sumu! Baada ya siku tatu mguu wako utakuwa vizuri! Tutaendelea kufanya biashara tenaa!”

    Mudy alibaki akimtizama Goryanah! Alimchukulia Kama Dadake na yeye alimchukulia Kama Kaka japo umri wao ulikuwa sawa! Mudy nae alikuwa akiishi na mamake pamoja na wadogo zake wawili wao walikuwa Darasa la tatu! Mamake ni mtu mwenye khari ya chini, anae genge anauza mboga mboga Nyumbani kwake, na muda mwingi alimtegemea Mudy. kwa ujumla maisha yake na Goryanah ni Kama yalifanana kutokana na kipato chao.

    Baada ya Goryanah kumaliza kumhudumia alimwambia akanyagie mguu wake chini, ili dawa ifanye kazi vizuri. Goryanah Alibaki akimtizama Mudy jinsi dawa inavyozidi kumuingia, aliona uso ukianza kukunjamana ilibidi acheke kwanza.

    “” Hivo hivo! Piga hatua ndio unazidi kupona! Kama vile unaumia ee!?”

    “” Naumia “Gorii” siyo Kama natania hapa!”

    “” Basi kaa tena!”

    Ilibidi akae huku akizidi kuunyosha mguu wake misuri ikae vizuri, baadae alijisikia unafuu ilibidi amtizame kwanza Goryanah.

    “” Goriii…!”‘

    “” Vipi? Bado inauma!?”

    “” Hapana..!”

    “” Ilaa…!”

    “” Wewe ni mzuri!”

    Goryanah ilibidi asitishe kwanza zoezi lake make alikuwa akimchua taratibu kwenye mishipa ya miguu.

    “”Aaah! Twende bhana! Unanitizama Sana! Au wataka nikuonee huruma! Mimi kwenye maisha ya mtu huwa naangalia afya yake tu.

    Walianza kutembea taratibu huku Goryanah akipiga hatua ndefu, akifika mbele kidogo ilibidi asimame kumsubilia Mudy, make mwendo wake ulikuwa ni wa taratibu

    “” Aaah! Mudy nawee! Unakuwa Kama sio mwanaume tu! Wewe huwezi ukatembea kwa uharaka tukawahi!?” Harafu tupo maeneo siyo!”

    Mudy baada ya kumfikia ilibidi asimame nyuma yake make alikuwa amenuna. Goryanah ndio anageuka huku akipaza sauti, ndipo anakutana na Mudy uso kwa uso ilibidi hasira zishuke Kisha alicheka tu.

    “” Hapo sawa’ make nilikuwa naenda kukufokea vibaya! Harafu leta hizo pesa ulizokusanya make Kuna vijana hapa nimeona mtu mmoja akirusha jiwe upande wa pili naona Kama wanashituana hivi! Hawa wanahitaji pesa, fanya hivi wewe kaa utulie.”  Itaendelea…….

     

    Usikose kufatilia simulizi yetu mpya! Na huu ndio mwanzo wa simulizi yetu, ushirikiano wenu ndio utatufikisha tamati wa simulizi yetu pendwa. Unapomaliza Kusoma Acha Na Comment Yako 

    Ulipitwa na SIMULIZI NYINGINE? 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa Kumtumia Chochote

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM 

    Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

    Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii [email protected]  

     

    Goryanah Goryanah Kijiweni Riwaya ya Goryanah

    30 Comments

    1. Khan on June 5, 2024 5:23 pm

      Imeanz na motoo

      Reply
      • Khairat on June 10, 2024 7:55 am

        Nzuri Sana

        Reply
    2. Carina on June 5, 2024 7:22 pm

      Mbona kukata kwenye utam

      Reply
    3. Greezy on June 5, 2024 7:24 pm

      Woow it’s amazing 2naisubr ya pili

      Reply
      • Itc collin on June 5, 2024 9:59 pm

        Unyam🙌🙌

        Reply
      • Veronica William on June 6, 2024 6:33 pm

        Nzri sana

        Reply
      • Switcher on June 7, 2024 10:22 am

        Ni motoooo🔥🔥

        Reply
    4. Eric on June 5, 2024 7:29 pm

      Shida ni fupi Sana mzee

      Reply
      • Sabra on June 6, 2024 4:31 pm

        😮😮😮😮

        Reply
    5. Shabani Jumbe on June 5, 2024 7:30 pm

      Hiii n yetu sote kina gorii na mudy tuko wengi umu😔😔😔

      Reply
    6. Abdul on June 5, 2024 7:34 pm

      Imeanza na moto san
      leta ya pili

      Reply
    7. Lalu boy on June 5, 2024 7:35 pm

      Nice story hujawah kosea yan

      Reply
    8. Mo Wa Tanga on June 5, 2024 7:39 pm

      Iko vyema sanaa

      Reply
    9. Seb Jr. on June 5, 2024 7:50 pm

      Stori km hizi ndo zenyewe, ziko na maudhui na mandhari za asilimia kubwa ya Watanzania. Big up admin 💪

      Reply
      • Bplm1664 on June 5, 2024 8:15 pm

        Iko na vibeeeee sanaaaaaa na mwanzo tu

        Reply
        • Lusitaah on June 6, 2024 12:37 pm

          Inavutia🥰

          Reply
    10. John Pombe Magufuli on June 5, 2024 8:04 pm

      ADMIN 🙌

      Reply
    11. John Pombe Magufuli on June 5, 2024 8:06 pm

      JAMANI LIPA NAMBA YA ADMIN MNAIONA…?? JAMBO MNGELIFANYA KUMFANYA ATUUMIZE ZAIDI 🙌

      Reply
    12. Rumbyambya Jr on June 5, 2024 8:22 pm

      Ukiachana na Utamu wa Story Tuizingatie na Lipa # ya Admin aisee

      Reply
    13. Madam P on June 5, 2024 10:50 pm

      Imekaa powa

      Reply
    14. Patrick on June 5, 2024 11:48 pm

      Hat zikiw 3 mbna fresh xna

      Reply
    15. Hawa on June 6, 2024 7:17 am

      Jamani imenigusaa ndo maisha yetu kitaan daah😥

      Reply
    16. Cesilia Nkunga on June 6, 2024 7:55 am

      Dah, ni 🔥🔥🔥

      Reply
    17. Tuma on June 6, 2024 10:26 am

      Kwenye maisha Kuna changamoto sana, tupambane

      Reply
    18. Imma MK on June 6, 2024 10:43 am

      If you appreciate the Admin tafadhali Tuma kitu😎

      Reply
    19. Lusitaah on June 6, 2024 12:36 pm

      Inavutia

      Reply
    20. Bintii kimmy on June 6, 2024 4:29 pm

      🔥🔥

      Reply
    21. Jozee on June 8, 2024 6:57 pm

      Nzuri haichoshi

      Reply
    22. Dickson on June 10, 2024 7:51 am

      Iko njema mno…..

      Reply
    23. Godfrey on June 12, 2024 3:50 pm

      Mzigo umekaa vzr sana mzee kilichobaki ni kukujaza thu maokoto

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.