Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » DR Congo Kumtoa Egypt Haijanishangaza Nilitegemea
    Africa | CAF

    DR Congo Kumtoa Egypt Haijanishangaza Nilitegemea

    MhaririBy MhaririJanuary 29, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wachezaji wa DR Congo wakishangilia baada ya kumtoa Egpt
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Unaweza kusema ni moja kati ya mchezo ambao bila shaka mashabiki wa soka walikua makini sana kuutazama na kila mmoja alikua anatamani kuona nani atapata ushindi wa kwanza katika michuano hii ikumbukwe kuwa katika hatua ya makundi wote wawili yaani DR Congo Pamoja na Egypt hakuna ambae alishinda mchezo hata mmoja zaidi ya kupata sare ambazo zimewapeleka mpaka hatua hii ya 16 bora.

    Katika mchezo ambao umewakutanisha mabingwa hawa wa zamani wa michuano hii ya mataifa barani Afrika tumeona namna ambavyo kumekua na matokeo ambayo yamekua hayatarajiwi na wengi kutokana na namna ambavyo timu zilivyokuja katika michuano hii zikiwa zimefanya uwekezaji mkubwa na maandalizi mazuri zaidi kwa ajili ya michuano hii.

    DR Congo aliingia kama timu dhaifu mbele ya Egypt na hii ni kwa sababu ameshapokea vipigo kadhaa kutoka kwa Egypt kuanzia zile mechi za kufuzu kombe la dunia mpaka baadhi ya mechi za mataifa ya soka barani Afrika.

    Mchezo huu mpaka kwenda hatua ya maamuzi ya penati ilikua ni bahati tu kwa timu ya taifa ya Egypt kwani sio timu ile ambayo ilikua sumbufu sana kama ambavyo ilikua miaka iliyopita lakini pia tuwapongeze DR Congo namna ambavyo walikuja na mikakati mizuri ya kuwaheshimu mabingwa hawa wa kihistoria wa michuano hii.

    Nilitegemea sana jambo hili kwasababu ukikitazama kikosi cha Misri ni kama hawakua tayari na michuano hii kuanzia kwa namna ambavyo wamekua wakiruhusu magoli ya kizembe kabisa ambazo ni wazi kabisa lawama zinaanzia kwa mabeki wao lakini pia jambo kubwa zaidi majeruhi kwa wachezaji wao muhimu kabisa ni jambo ambalo limewaangusha kabisa katika michuano hii.

    SOMA ZAIDI: Namibia Imetuonesha Umuhimu Wa Kumuamini Kocha Mzawa

     

    dr congo afcon egypt vs dr congo

    1 Comment

    1. Pingback: Waliotegemewa Wameduwazwa Na Wasiotegemewa AFCON - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.