Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Benchikha Na Maaamuzi Magumu Yasiyo Na Uvumilivu
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Benchikha Na Maaamuzi Magumu Yasiyo Na Uvumilivu

    MhaririBy MhaririApril 15, 2024Updated:April 15, 202410 Comments2 Mins Read916 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Kocha Benchikha wa Simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kocha mkuu wa wekundu wa msimbazi yaani klabu ya Simba Abdelhak Benchikha ni miongoni mwa makocha wenye CV kubwa barani Afrika lakini pia na uzoefu ukichangiwa na uwezo mzuri wa kufundisha soka pia ni miongoni mwa makocha wasio wavumilivu wa nyakati ngumu katika kazi yake.

    Ukitazama kipindi hiki ambacho klabu ya Simba inapitia, kinafanya nikumbuke baadhi ya maamuzi magumu ambayo amekua akiyafanya na kuwa kama mmoja ya makocha mbao sio wavumilivu wanapokua katika majukumu yao.

    Tunapoelekea katika mechi ya watani nakumbuka tukio la mchezo wa mwisho ambapo Simba walipata sare dhidi ya Ihefu na dakika ambazo kocha huyu alikaa akitafakari baada ya mchezo kuisha wakiwa hawajapata ushindi katika mechi zao 4 mfululizo za michuano yote.

    Moja wapo ya maamuzi magumu kuwahi kuyachukua ni mwaka 2011 akiwa kama Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Algeria, alichukua alijiuzulu baada ya kufungwa mabao manne na timu ya Taifa ya Morocco katika mwendelezo mbovu wa matokeo katika timu yake hiyo.

    Mwaka 2023 akiwafundisha USM Alger, licha ya mafanikio makubwa aliyoyapata klabuni hapo ikiwemo kutwaa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Yanga, alijiuzulu kuifundisha Klabu hiyo kutokana na tukio la kuzomewa na mashabiki wakati na baada ya mechi kuisha Katika mwendelezo wa mechi za ligi kuu Algeria.

    Kituo kinachofuata kwa Simba ni dhidi ya Yanga, nini kitatokea, ni suala la muda na kusubiri Jumamosi ijayo ya Aprili 20.

    Je, Benchikha atabadili upepo wa mambo na kurejesha wimbi la ushindi Msimbazi au ataendelea pale alipoishia Roberto Oliveira ‘Robertinho’, aliyekumbana na kipigo cha aibu cha mabao 5-1 katika derby ya kwanza iliyopigwa Novemba 5 mwaka jana na kumfutisha kazi Msimbazi? Tusibiri tuone itakuwaje?

    SOMA ZAIDI: Barua Kwako Mo Dewji Rais Wa Heshima Simba Sc 

    Kocha simba simba sc leo simba vs yanga

    10 Comments

    1. Michael on April 15, 2024 12:45 pm

      Atulie tu kikosi cha simba ni kipana sana tatizo wanakosa muunganiko
      Kila mmoja anapambania jina lake binafsi na sio simba

      Reply
    2. Emmanuel Albogast on April 15, 2024 12:47 pm

      Huyu ni kocha mzoefu hatuwezi kupoteza tena, subiri kidogo Sana uone. Pia niwapongeze sana kwa taarifa za uhakika 👏

      Reply
    3. Beca Daud on April 15, 2024 12:48 pm

      Kuondoka kwa benchika sio suluhisho la matatizo yanayoikabili Simba…ni wakati wa viongozi kukaa chini na kutafakari jinsi ya kuinusuru time yetu.

      Reply
    4. Abdul Omary ngulluko on April 15, 2024 12:55 pm

      Yeye aturie tu maana ss mashabiki ndo tunaumia zaidi huku mtaani Hali nimbaya sana

      Reply
    5. Bofesia on April 15, 2024 1:00 pm

      Kuna wakati gari lenye dereva mzuri hupata ajali haina maana mara zote kuwa kosa ni la gari, barabara au dereva. Kuna wakati mifumo inakataana hivyo maboresho yanayotakiwa huwa makubwa itoke spea iwekwe nyingine, atoke mtu dhaifu awekwe Bora anaendana na mfumo. Kocha anao mfumo anahitaji watu wanao umudu, uondoke mfumo au spea!, kunyoa ama kusuka. Ni dhairi tairi ya gari mpya ni bora kuliko ya zamani ila tu isiwe feki.

      Reply
      • Joseph on April 15, 2024 1:29 pm

        Kuacha timu ni sehemu ya ukocha. Kwani ndo manzoni wa kupata change motor sehemu nyingine

        Reply
    6. Joseph on April 15, 2024 1:30 pm

      Kuacha timu ni sehemu ya ukocha. Kwani ndo manzoni wa kupata change motor sehemu nyingine

      Reply
    7. Sule Mohd on April 15, 2024 1:53 pm

      Naende tu Simba itakuja kumuua

      Reply
    8. Baraka mahongo on April 15, 2024 1:58 pm

      Simba viongizi tutawakata vichwa taree20 tukipigwa tena hamsa

      Reply
    9. Ohms on April 15, 2024 2:10 pm

      Tarehe 20 Mnyama anakuka 2-0

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.