Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barua Nzito Kwa Simba Ili Iwe Imara Wawajibike Viongozi
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Barua Nzito Kwa Simba Ili Iwe Imara Wawajibike Viongozi

    MhaririBy MhaririApril 12, 2024Updated:April 13, 202410 Comments2 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Viongozi wa klabu ya Simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Habari Mhariri, 

    Nikiwa na afya njema kabisa na amani ya moyo, Napenda barua hii iwafikie viongozi wa klabu ya Simba maana kinachoendelea ndani ya uongozi matokeo yake ndio haya yanaonekana kwa kipindi cha misimu hii mitatu,

    Ikumbukwe Simba kipindi cha Barbara Gonzalez, tuliiona simba yenye ushindani na yenye mafanikio makubwa kana kwamba kumfunga mtu kama Al Ahly pale kwa Mkapa ikawa ni jambo la kawaida, mpaka hatua ya kuongoza kundi mbele ya bingwa wa kihistoria wa michuano ya mabingwa Afrika na kipekee ndio simba iliopofikia hatua za kutaka kufika mpaka nusu fainali kwa kumpiga Kaizer Chief ilihali mechi iliisha kwa idadi ya magoli isiokua rafiki kwa simba.

    Unadhani kumfukuza Kocha Robertinho ilikuwa suluhisho? mbona amekuja bingwa  wa shirikisho bado mambo ni yale yale?  Hii dhahiri huonyesha udhaifu katika uongozi wa Simba. Katika ukweli pasemwe ukweli kama Yanga wataendelea hivi misimu miwili au mitatu basi ni dhahiri nusu fainali na mpaka fainali wanaingia katika ligi ya mabingwa Afrika maana wamethubutu.

    Yanga ni timu yanye uongozi thabiti kupitia kwa Hersi Saidi na nikiri wazi kuwa anatakiwa kuigwa kwani timu ya soka ni uongozi na sio wachezaji

    Mfano  mzuri klabu ya Simba ilikua na mtu kama Augustine okrah, Jonas Mkude, Baleke Jean pamoja na Phiri Moses, hawa wote walikua wachezaji ambao kabla ya uongozi kupinda pinda wanafanya vizuri, ila sasa baada yake wakaonekana wabovu na kutemwa na ajabu walipo wanakiwasha vibaya mnooo.

    Wekundu wa msimbazi wana watu ambao kama wakienda timu kama Azam au hata Yanga lazima tutashangaa, lakini viongozi wamebaki kaa na kumpangia kocha wale vijana ambao damu bado changa wapo jukwaani,

    Mwisho niseme ikiendelea hivi hivi hata aje Messi au Ronaldo simba haiwezi kua imara kwani timu ni uongozi ndio wachezaji wafuate, 

    Katika Utekelezaji wa majukumu 

    Mohamedi Abdala Mohamedi 

    Mwanafunzi UDSM

    SOMA ZAIDI BARUA NYINGINE HAPA 

     

    simba sc simba sc leo
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.