Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barua Kwako Mwamuzi Arajiga Kuelekea Yanga vs Simba
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Barua Kwako Mwamuzi Arajiga Kuelekea Yanga vs Simba

    MhaririBy MhaririApril 19, 2024Updated:April 20, 202424 Comments2 Mins Read9K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Barua kwa Arajiga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kwa heshima na taadhima nakuandikia barua mwamuzi Ahmed Arajiga,

    Natumai barua hii inakukuta wewe na afya njema na ukiwa na ari kubwa zaidi kuelekea mchezo mkubwa wenye hisia kubwa zaidi miongoni mwa mashabiki unaozikutnisha klabu kubwa na kongwe Tanzania. Ningependa kueleza shukrani zangu kwa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kukuamini na kupewa filimbi ya kuuhezesha mchezo huu.

    Kama shabiki wa soka na mwanamichezo kutoka Kijiweni, tunatambua jukumu kubwa ulilonalo katika kuhakikisha mchezo unachezwa kwa haki na uadilifu lakini pia natambua pia kwamba kazi yako ni ngumu na mara nyingine inaweza kuwa changamoto kubwa.

    Napenda kukusihi utumie uzoefu wako na hekima katika kusimamia mchezo huu. Tunakutia moyo kufanya maamuzi kwa kufuata sheria za mchezo bila upendeleo au kuweka taswira mbaya yoyote ile kwa wapenzi wa soka Tanzania na Afrika kwa ujumla ambao watakua wanaufuatilia mchezo huu. Tunaamini utaweza kusimamia mchezo kwa haki na kuepuka migogoro au utata wowote.

    Sisi kama Kijiweni tunatambua kwamba jukumu lako ni muhimu sana katika kuhakikisha mchezo unamalizika kwa amani na furaha kwa pande zote mbili za mashabiki yaaani mashabiki wa Yanga lakini pia mashabiki wa Simba. Kwa hivyo, tunakuomba ufanye kazi yako kwa umakini na ustadi ili kutuletea matokeo yanayostahili.

    Tunakutakia mafanikio katika mchezo wako na tunaamini kuwa utakua mchezo mzuri na wenye kuvutia zaidi kwa upande wako wa maamuzi lakini pia kwa mbinu za makocha pamoja na utekelezaji wa mbinu hizo na wachezaji kwa ujumla wao n ani wazi kuwa tnasubiri kuona mchezo mzuri na wa kuvutia.

    Asante kwa kujitoa kwako na kwa huduma yako katika mchezo wa soka.

    Kwa heshima kubwa,

    Mhariri

    SOMA ZAIDI: Barua Nzito Ya Shabiki Kwa Viongozi Wa Simba Kuhusu Inonga

     

    live simba vs yanga mwamuzi arajiga simba leo YANGA LEO
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.