Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Babacar Diop Niasse : Golikipa Mrefu Zaidi AFCON
    Africa | CAF

    Babacar Diop Niasse : Golikipa Mrefu Zaidi AFCON

    MhaririBy MhaririJanuary 8, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Golikipa Babacar Diop
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kuanza kwa michuano ya AFCON nchini Ivory Coast tayari vikosi vitakavyowakilisha nchi zilizofuzu vimekwishatangazwa na moja ya kikosi kilichotangazwa ni cha timu ya Taifa ya Mauritania kikiwa na golikipa mrefu zaidi katika michuano hii anayefahamika kama Babacar Diop Niasse.

    Babacar ni golikipa anayechezea kikosi cha FC Nouadhibou kinachopatikana nchini Mauritania na amezaliwa katika jiji la Ksar nchini Mauritania tarehe 17/09/1995 akiwa na urefu wa Mita 1.90 na futi 6 na inchi 3 anatajwa kama golikipa mrefu zaidi katika michuano hii ya AFCON 2023.

    Licha ya kuchezea klabu ya FC Nouadhibou lakini pia aliwahi kuchezea timu kama ACS Ksar ya kwao ambapo alicheza msimu wa 2016 hadi 2018 kabla ya kutimkia katika kikosi cha ASC Police kuanzia msimu wa 2018 mpaka 2021 kabla ya kujiunga na Nouadhibou anayochezea mpaka sasa.

    Wakiwa na kocha Amir Abdou, Mauritania au jina lao la utani kama Mourabitouns wamefuzu Afcon msimu huu kwa kupata ushindi dhidi ya Sudan wa mabao 3-0 huku wakisare mchezo wa kwanza dhidi ya Gabon kwa bila ya kufungana lakini pia wakipoteza mara 2 mbele ya DR Congo na kushinda mechi 2 za mwisho ambapo alimfunga Sudan bao 3:0 na Gabon bao 2:1.

    Hawajawahi kuchukua ubingwa wa AFCON lakini hii ni mara yao ya 3 kushiriki katika michuano hii ya AFCON ambapo katika ngazi ya dunia wanashika nafasi ya 105 na hii kwa mujibu wa takwimu za FIFA na wamefuzu AFCON wakitoka kundi I.

    Golikipa huyu ana kibarua Kizito cha kuhakikisha nyavu zake hazitikswi na wapinzani kwani wamepangwa kundi D akiwa na timu kama Algeria, Angola na Burkina Faso zenye wachezaji wenye uchu wa kuweka rekodi katika michuano hii kwa msimu huu. Michuano ya AFCON inatarajiwa kutimua vumbi kuanzia tarehe 13/01/2024 mpaka tarehe 13/02/2024 nchini Ivory Coast

    Endelea kufuatilia zaidi taarifa mbalimbali kuhusu AFCON kwa kugusa hapa.

     

     

     

     

     

     

     

    AFCON 2023 BABACAR DIOP babacar diop mauritania mauritania

    1 Comment

    1. Pingback: Makocha 5 Wanaolipwa Pesa Ndefu Zaidi AFCON - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.