Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tano-05)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tano-05)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tano-05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJune 1, 2025Updated:June 3, 202513 Comments7 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nne

    “Na siku zote Muuwaji hawezi kuishi, ndiyo maana nilikutoaย  gerezani ili uje kuitafuta haki iliyoporwa na Faudhia”ย  Alikazia Mzee Shomari kisha alimruhusu Diana kuelekea ndaniย  ya Benki, mpango wa Mzee Shomari ulikuwa ni Kumuuwa Faudhia,ย  kisha kuiba pesa za kimarekani ambazo zilihifadhiwa ndani yaย  Benki hiyo katika chemba ya siri, ilikuwa ni zaidi ya Dolaย  Bilioni 900 , alimtumia Chogo kama ngao ya kufanya mambo yakeย  huku akiweka ubia na rafiki yake wa zamani ambaye alikuwaย  akiishi Uholanzi, ndiye aliyemtoa jela na kumfadhili pesa zaย  kufanya ugaidi Tanzania, hivyo Mzee Shomari alikuwa ndiyeย  Gaidi aliyekuwa akiratibu mipango yote, alikusanya vijana naย  kuwapatia silaha nzito, akiwemo Diana na Martin Gimbo maarufuย  kama Chogoย 

    Jinsi alivyowapata Diana na Chogo utakuja kufahamu mbele,ย  hebu tosonge..ย 

    Usiku ulikuwa umeingia, ndani ya Jiji la Arusha, Faudhiaย  alikuwa akimlaumu Mohd kwa kosa la Kumuuwa Mama yake naย  Martin Gimbo.

    SEHEMU YA TANO

    “Hakukuwa na sababu ya kuuwa Watu wasio na hatia Mohd, umeuwaย  Mwalimu, umeuwa Bibi na Mjukuu wake” Alisema Faudhia kwaย  hasira sanaย 

    “Unanilaumu kwa kutekeleza mipango yangu ya kazi? Unanilaumuย  kwa kusafiaha ushahidi wa mwote tulimopita? Faudhia wewe siyoย  Mfanyakazi wa kanisa au msikiti, wewe ni askari wa siri waย  kitengo cha Usalama wa Taifa! Sisi tunauwa kwa ajili yaย  Taifa” Alijitetea Mohdย 

    “Unauwa kwa ajili ya usalama wa Taifa? Taifa lipi? Kuuwa Watuย  wasio na hatia ndio majukumu ya Usalama wa Taifa? Pengineย  umeelewa vibaya mafunzo uliyoyapata, siwezi kuendelea kufanyaย  kazi na wewe Mohd” Alisema Faudhia kisha alipiga simu kwaย  Mzee Shayo akamwambia ambadilishie Mtu wa kufanya naye kaziย 

    “Kwanini unataka abadilishwe?” Alihoji Mzee Shayo kwa njia yaย  simuย 

    “Sijisikii uhuru wa kuifanya kazi yangu” Alisema Faudhia hukuย  akiwa anamtazama Mohd ambaye alikuwa na hasira sana akiwaย  ameketi kwenye kiti

    “Faudhia Mwanangu..” kabla hata hajamaliza alikatiswa naย  Faudhiaย 

    “Baba nimesema nibadilishie huyu Mtu” Alisema kwa hasira naย  sauti ya juu kuonesha msisitizo kuwa alikuwa akimaanishaย  alichokisema na hakikuwa utani.ย 

    “Mpe simu Mohd,” mara moja Mohd alipewa simu na Faudhia,ย  kabla hajaongea na Mzee Shayo alimtazma sana kwa hasiraย  Faudhia.ย 

    “Natoa amri ya wewe kurudi Makao Makuu haraka sana” Alisemaย  Mzee Shayoย 

    “Lakini Mkuu..” kabla Mohd hajamaliza kujitetea alikatishwaย  na Mzee Shayoย 

    “Hakuna cha Lakini Mohd, rudi Makao makuu” Alisistiza Mzeeย  Shayo, mara moja Mohd alimtupia simu Faudhia kisha alichukuaย  koti lake akatoka chumbani hapo lakini kwa bahati mbayaย  alikuwa amesahau simu yake ambayo ilikuwa kwenye kochi,ย  kitendo cha Mohd kutoka ndani ya chumba hicho, simu yakeย  ilianza kuita, Faudhia alinyanyuka na kuangalia aliyekuwaย  akipigaย 

    Aliona namba imeandikwa Boss, alifikiria afanye kitu ganiย  aipokee au aiache iendelee kuita hadi ikate, aliichukua naย  kuchungulia dirishani, alimuona Mohd akilielekea gari lakeย  kwa ajili ya kuondoka, aliona ni bora aipokee simu hiyoย  sababu alimtilia sana Mashaka kuwa huenda akawa sio Mtu mzuriย  kutokana na mauwaji ya Watu wasio na hatia ambayo alikuwaย  akiyafanya.ย 

    “Mohd! Muuwe Faudhia sasa hivi kisha urudi hapa” Ilisikikaย  sauti ambayo Faudhia aliitambua, ilikuwa ni sauti ya kizee yaย  Mzee Shomari, mara moja aligundua kuwa Mohd alikuwa ni askariย  aliyekuwa akifanya kazi na magaidi, akatambuwa kuwaย  kilichobakia kwake ni kifo pekee. Alipochungulia tenaย  alimuona Mohd akiwa anapiga hatua kurudi ndani baada yaย  kugundua kuwa amesahau simu yake, Faudhia alimtazama vizuriย  Mohd akiwa bado amesimama pale pale, Mohd alikifikia kitasaย  cha mlango bila kujuwa kuwa Faudhia alikuwa amemshtukia kuwaย  ni Mamluki anayekisaliti kitengo cha Usalama wa Taifa.ย 

    Alipofungua mlango alimkuta Faudhia akiwa amesimama, Unajuwaย  Mohd alikuwa ni askari wa kitengo cha Usalama wa Taifa hivyoย  alipoingia tu aligundua kuwa kuna jambo ambalo halikuwa sawa,ย  alimtazama sana Faudhia akiwa ameganda pale mlangoni,ย  walikutanisha macho yao ya Kijasusi huku kila mmoja akiwaย  anamsoma mwenzake.

    Mara simu ya Mohd iliita tena na mpigaji alikuwa ni yule yuleย  Mzee Shomari, aliisikilizia kidogo kisha aliifuata simuย  lakini kabla hajapokea Faudhia alimnyooshea Mohd Bastolaย 

    “Tulia hivyo hivyo Msaliti wewe, kumbe wewe ni mamlukiย  unayefanya kazi na Mzee Shomari? Nilikuwa nakutilia mashakaย  sana Mohd” Alisema Faudhia, Mohd alikuwa amesimama huku simuย  ikiendelea kuita mkononi mwakeย 

    “Isogeze hiyo simu kwangu” Alisema tena Faudhia hukuย  akihakikisha kuwa Mohd hachomoki wala hafanyi ujanja wa ainaย  yoyote ile. Mohd alimtazama Faudhia kisha alimsoma jinsiย  alivyokuwa amesimama ila Faudhia alishtuka mapema kuwa Mohdย  anamsoma kisha akamwambia.ย 

    “Ujanja wowote utakaoufanya Mohd napasua kichwa chako”ย  Alisema Faudhia, Mohd aliinama kidogo kisha aliiburuza simuย  ikafika kwenye miguu ya Faudhiaย 

    “Umeanza kutumika upande huo kwa muda gani?” Aliuliza Faudhiaย  huku akizuga ili ainame aichukue simuย 

    “Faudhia! Usifikiri kamwe naweza nikasema chochote au hiiย  siri ikafika makao makuu, katu kitengo hakita ifahamu hiiย  siri” Alisema Mohd kwa kujiamini kisha alishusha mikono yakeย  akamwambia Faudhiaย 

    “Si ulikuwa unataka kunitwanga risasi? Fanya hivyo kablaย  sijakuwahi” Alisema maneno yaliyojaa ulaghai Mkubwa, ilikuwaย  ngumu kwa Faudhia kumuuwa Mohd, alichotaka ni kufikishaย  taarifa kwenye kitengo cha Usalama wa Taifa.ย 

    Mohd alianza kumsogelea Faudhia taratbu huku akizidi kuongeaย  maneno ambayo yalimchanganya Faudhiaย 

    “Wewe ndiyo sababu ya Mama yako kufa, hukustahili kubaki haiย  kwa uchafu ambao ulikuwa ukimfanyia Mama yako, laiti kamaย  taarifa hizi zitavuja ndani ya kitengo basi hautokuwa na sifaย  ya kuwa Undercover!! Mtu ambaye amemsaliti Mama yake kwa Babaย  yake anaweza vipi kutunza siri za Nchi hii” Alisema Mohd hukuย  akizidi kusogea, Maneno ya Mohd yalimtia uchungu sanaย  Faudhia, ni kama alitoneshwa kidonda kilichoanza kukaukaย 

    “Acha Mohd! Achaaaaa” Alisema Faudhia kisha aliweka kidoleย  sehemu ya kufyatulia risasi ili ammalize Mohd, haraka Mohdย  alimuwahi Fadhia na kuushika mkono ambao ulikuwa na Bastola,ย  Faudhia alipofyatua risasi zote zilipiga juu ya dali. Mohdย  alimkunja Faudhia na kumpa mateke matatu ya Mbavu kabla yaย  Faudhia kujikunjua

    Bastola ilikuwa chini, aliponyanyuka Faudhia alijikuta akiwaย  mikono mitupuย 

    “Nilikwambia hii siri haiwezi kufika kitengo cha Uslama waย  Taifa, kwakuwa nimepigiwa simu nirudi Makao makuu basi weweย  utaonekana umeuawa kwa kuvamiwa hapa Hotelini.” Alisema Mohdย  huku akiwa anakunja Shati lake, alikuwa ni mwanaume mwenyeย  mazoezi na roho ya kikatili sana.ย 

    “Mradi wa kukutengeneza wewe uje kuwa Askari wa kitengoย  unafia hapa rasmi” Alisema Mohd kisha alimfuata Faudhiaย  ambaye alikuwa amejiandaa kukabiliana naye, alirusha ngumiย  mfululizo ambazo zote Faudhia alizikwepa lakini alifanyaย  ujanja wakati anamaliza kurusha ngumi ya mwisho alikunjuaย  Mguu wa kulia na kumpiga teke la tumbo Faudhia, alijikutaย  akianguka chini kisha alijinyanyua na kupanga pambano upya.ย 

    Wote walikuwa na mafunzo ya Kijeshi hivyo kila mmoja alijuwaย  namna ya kupambana, Faudhia alijibu mapigo kwa kumpa matekeย  mawili yaliyofika hadi kwenye kifua cha Mohd, alisogezwaย  pembeni karibu na mlango ambapo kochi lipo, aliangalia chiniย  kulikuwa na Bastola, pembeni kulikuwa na simu yake yenye siriย  nzito, aliona ni bora afanye ujanja.ย 

    Aliokota mto wa kochi kisha alimtupia Faudhia usomi kishaย  aliinama ili aichukue bastola lakini Faudhia alikuwa shapu,ย  kabla hajaokota Bastola alipigwa teke la Mgongo kisha Faudhiaย  akaipiga teke ile simu na Bastola vikaingia uvunguni mwaย  Kochi, alimlazimisha Mohd apambane kwanza.ย 

    Mohd aliinuka na kunvaa Faudhia, aliambulia kutupwa chiniย  kutokana na namna Faudhia alivyo Shapu. Kabla hajakaa sawaย  alipokea ngumi la shingo ambalo lilimsogeza kwenye kochi,ย  kabla hajatulia tena Faudhia alimpelekea Mohd teke ambaloย  Mohd alilidaka kisha alitumia nguvu kubwa alimsukuma Faudhiaย  ambaye aliangukia kwenye mezaย 

    “Assssh” aligumia Faudhia kutokana na maumivu ya kujigongaย  kwenye meza, Mohd hakutaka kusubiri alimrushia ngumiย  mfululizo, ngumi ambazo zilimpekeka Fuadhia ukutani, bahatiย  mbaya ngumi nyingi zilimpata na kumfanya aumie usoniย 

    Mohd alimpiga Faudhia mateke mfululizo eneo la mbavu hukuย  akimwambiaย 

    “Unakufa leo” Alisema huku akiwa anamuangalia Faudhia akiwaย  anaanguka chini.

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA SITA

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    Riwaya Nyumba Ya Majini Kijiweni riwaya za kusoma mtandaoni soma riwaya bure

    13 Comments

    1. David ben on June 1, 2025 5:52 pm

      Mbona fupi sana jamani

      Reply
    2. Joy on June 1, 2025 5:57 pm

      Imeishia patamuu

      Reply
    3. Daudi Antony kilyenyi on June 1, 2025 5:58 pm

      mbna fupi hvo mzee

      Reply
    4. Jackson Wasokye Ramazani on June 1, 2025 6:02 pm

      Bado mda huko adm, rusha sehemu ya sita. Hii tamu sana kabisa.

      Reply
    5. Cathbert on June 1, 2025 6:21 pm

      Good ๐Ÿ‘๐Ÿ‘

      Reply
    6. Adam on June 1, 2025 8:15 pm

      Admn Ahsante Kwa Story Nzuri Saanaa Hii

      Reply
    7. Salma Ibrahim on June 1, 2025 9:08 pm

      Fupi inakera

      Reply
    8. Lus twaxie on June 1, 2025 11:14 pm

      Fupi innboa sana jmn ….kama utaki acha tu kutuma

      Reply
    9. KingzJeelay on June 2, 2025 1:34 am

      Admin hapa umezingua….
      Stori ni fupi mnooooo ๐Ÿ˜ฏ๐Ÿ˜ฏ๐Ÿ˜ฏ

      Reply
    10. Diana on June 2, 2025 11:08 am

      Admini hauna vitabu tununue tu

      Reply
    11. ๐Ÿ“’ Reminder- + 1.425308 bitcoin. Receive >> https://yandex.com/poll/DCTzwgNQnzCykVhgbhD581?hs=c68e35f9f994198fbd7c29c235410dbc& ๐Ÿ“’ on June 3, 2025 11:04 am

      8qqlk0

      Reply
    12. ๐Ÿ— + 1.194462 BTC.GET - https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=c68e35f9f994198fbd7c29c235410dbc& ๐Ÿ— on June 4, 2025 2:27 pm

      3z4675

      Reply
    13. ๐Ÿ—‘ Notification- Operation 1,853725 BTC. Receive => https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=c68e35f9f994198fbd7c29c235410dbc& ๐Ÿ—‘ on June 5, 2025 6:26 pm

      urf8ny

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 4, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sita “Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tano-05)

    Ratiba Kamili Ya FIFA CLUB WORLD CUP 2025

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.