Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya NneΒ
“Lengo la kuja huku ni kumpa taarifa Mama lakini hatuweziΒ kuondoka bila yeye kiridhia, Veronica mpenzi tuvumilie tuΒ hadi pale hasira zake zitakapoisha”Β
“Kwanini Mama ananifanyia hivi mimi, kama hakunizaa yeye?”Β nilijiuliza baada ya kukumbuka tukio la kubakwa na Anko SangaΒ ambapo Kwa maelezo ya Mama ilionesha kuwa alikuwa akijua kilaΒ kitu . EndeleaΒ
SEHEMU YA TANO
“Usiseme hivyo Veronica, Mama amechukia tu kwasababu taarifaΒ hii siyo njema kwa Mzazi yeyote yule….fikiria ingelikuwa niΒ wewe ndio Mzazi unamsomesha Mtoto kwa gharama kubwa alafuΒ anaishia kupata mimba? Inaumiza ndio maana nakwambiaΒ tusiondoke hadi tupate radhi zake” Yalikuwa ni maneno yaΒ Jonas yaliyojaa busara na hekimaΒ
“Nifanye kuwa Mkeo Jonas”Β
“Wewe tayari ni Mke wangu, tusubirie tu baraka za Mama yako”Β Kutokana na maneno mazuri ya Jonas nilijikuta nikitakaΒ kumwambia ukweli kuhusu kukeketwa lakini nikaona sio mudaΒ sahihi.Β
Ulipita mwezi mmoja Mama hakuonekana nyumbani na simu yakeΒ ikawa haipatikani, hofu ilianza kuniingia nikahisi labdaΒ amepatwa na tatizo. Nilimfuata yule jirani aliyenipa taarifaΒ kuwa Mama alichukuliwa na gari ndogo ile siku, nilichotakaΒ kujua ni nani alimchukuaΒ
“Jirani samahani, ni mwezi sasa Mama haonekani mpaka naanzaΒ kuingiwa na wasiwasi”Β
Nilimwambia baada ya kinipa nafasi ya kuzungumza nae “Ina maana tokea siku ile hadi leo hajarudi?”Β
“Ndio Jirani napata mashaka ni wapi alipo, hivi umemtambuaΒ aliyekuja kumchukua hapa?” Jirani alionekana kutafakari kablaΒ ya kunijibu ni wazi alikuwa akimtambuaΒ
“Sura yake sio ngeni sana”Β
“Anaonekanaje”Β
“Mweusi, sijui kuhusu urefu sababu alikuwa ndani ya gari” “Itakuwa Anko Sanga huyo”Β
Nilimuonesha picha ya Anko Sanga kupitia simu yangu iliΒ amtambue kama ni yeye au ni Mtu mwingineΒ
“Eeeh! ni huyu hapa, hata hivyo hupaswi kuwa na wasiwasi sanaΒ kwasababu huyu alikuwa akija hapa mara kwa mara, amesimamiaΒ ukarabati wa nyumba yenu mpaka ulipoisha”Β
“Oooopsss” Nilivuta pumzi na kuzitoaΒ
“Ahsante sana jirani”
Uvumilivu wa kuendelea kumsubiria Mama ulinishindaΒ nikamueleza Jonas kuwa nimechoka ikiwezekana tuondoke, mimbaΒ ilifikia miezi minne, hata upande wa Jonas vivyo hivyoΒ alianza kuchoka licha ya ujasiri wake wa kila siku kusemaΒ tuendelee kumsubiria.Β
Tulikusanya mabegi yetu ili tuondoke, tulipofika mlangoniΒ tulisikia Mlio wa gari, nilipochungulia nilimuona Mama akiwaΒ anashuka kwenye gari ya Anko Sanga.Β
Tukayarudisha yale mabegi kusudi asijue kama tulikusudiaΒ kuondoka. wote waliingia ndani na kutukuta tumekaa paleΒ sebleni. Anko Sanga alitusalimia na kuketi pamoja na sisiΒ lakini Mama alipita zake na kuingia chumbani kwakeΒ
“Hivi Mama yangu amepatwa na nini?” nilimuuliza Anko SangaΒ maana ndiye aliyekuwa karibu zaidi na MamaΒ
“Sijui nikuulize wewe Veronica umemfanya nini Mama yako?”Β
“Mimi Anko Sanga? Mama simuelewi naona ameninunia tu,Β ameondoka bila kusema anaenda wapi!”Β
“Mama yako amechukizwa na ulichokifanya unapaswa kumuombaΒ sana msamaha Veronica, amekupigania sana lakini umemlipaΒ asichostahili”Β
“Anko! makosa hayarekebishwi kwa hasira bali busara zilizoΒ njema lakini kwa staili hii hapa anajenga au anabomoa?”Β alidakia JonasΒ
“Kijana hata Kama ungelikuwa wewe ndio Mzazi wa Veronica kwaΒ kilichotokea ungelitumia busara gani? Tunu ya Mama ni kuonaΒ Mtoto anafikia malengo aliyoyaweka Mzazi sasa kama MtotoΒ anafikia hatua ya kuharibu Maisha yake, Unafikiria MzaziΒ atakuwa kwenye wakati gani?”Β
“Imeshatokea na tumekiri Makosa, kinachotakiwa Kama MzaziΒ akubali kuwa Maji yameshamwagika, tuangalie kinachofuataΒ baada ya hapa….Ujauzito wake unakaribia miezi mitano,Β tukiendelea hivi atakonda kwa mawazo” Alisema tena Jonas,Β Dhahiri nilimuona Anko Sanga akimtazama kwa jicho la ubayaΒ Jonas.Β
Alikuwa akimtazama kama Mwanaume wangu au adui aliyekatizaΒ ndoto zangu? Mbona yeye aliutumia mwili wangu kwa stareheΒ zake tena akishirikiana na Mama yangu Mzazi? NilijiulizaΒ nikiendelea kumtazama
“Chakufanya hapa ni nyie kuongea na Mama Veronica, hakunaΒ njia nyingine” Alisema kikaksi akafunga mazungumzoΒ
“Anko Sanga…kama hatufikii makubaliano hapa nitaondoka,Β nitakuwa tayari kuishi bila baraka zenu”Β
Yalikuwa ndio maamuzi yangu na sikutaka Mtu anipinge, hataΒ nilipoongea na Mama nilimwambia hivyo hivyo ndipo nilipomuonaΒ akianza kulegeza hasira zakeΒ
“Kwahiyo unataka nifanye nini?” Aliniuliza baada ya kunisikiaΒ nilikuwa tayari kufanya maamuzi yangu binafsiΒ
“Kubali niolewe na Jonas”Β
“Unataka awe Mumeo?”Β
“Ndio Mama, hata ukisema hapana sitarudi nyuma. Mtoto aliyeΒ tumboni anatakiwa kulelewa na Baba yake Mzazi” Mama hakuwa naΒ Jinsi alikubali nifunge ndoa na Jonas, ruhusa ilienda sawa naΒ mipango ya haraka. Hatimaye tulifunga ndoa Arusha kwenye lileΒ Kanisa nililokiwa nikisali siku zote.Β
Tukarudi Dar tukiwa Mke na Mume Maisha ya ndoa yalianza naΒ furaha iliyatawala maisha yetu, tukaenda kuishi Mbezi na hukuΒ ndiko nilikokutana na Mama Sofia, alikuwa jirani yetu sikuΒ moja alinisaidia nilipokuwa najisikia vibaya ndio ukawaΒ mwanzo wa kufahamiana kwetu.Β
Tulijenga urafiki na huyu Mama mfanya biashara, alitokeaΒ kunipenda mno kwa jinsi nilivyokuwa na moyo wa ujasiri naΒ kujali,Β
“Jonas Mkeo ni Mtu wa pekee sana, ana moyo wa dhahabu”Β Alisema Mama Sofia, nikaona nimueleze kuwa nilikuwaΒ nimekeketwa na jambo hili lilikuwa siri kwanguΒ
“Mume wako anajua?”Β
“Hapana nimemficha kwa kitambo sasa”Β
“Hupaswi kumficha, atajua tu ni vema ukamueleza” “Nahofia ataniacha Mama Sofia”Β
“Usikubali roho ya uwoga ikutawale Veronica, mueleze ajue”Β Alinishauri hivyo, jinsi ya kumueleza Jonas ilikuwa ngumuΒ sana.
Kila alipotaka kusex na mimi nilimwambia nasikia maumivu yaΒ tumbo, kwakuwa nilikuwa mjamzito ilimfanya anihurumie japoΒ niliona kama alikuwa anakosa raha.Β
Tulikaa miezi mitano bila kufanya mapenzi, mara ya mwishoΒ ilikuwa wakati tuko Chuo ambapo nilikuwa nahakikisha tumelewaΒ ndipo tunafanya hata hivyo alinikataza kutumia kilevi baadaΒ ya kuwa Mjamzito.Β
Nilijua tu ipo siku atajua lakini nilijipa muda ili akijuaΒ niwe nimejitayarisha kwa kila kitu, Nilipoanza KlinikiΒ daktari aligundua hili jambo na kibaya zaidi alikuwa niΒ rafiki wa JonasΒ
“Shem kumbe umekeketwa?” aliniuliza akiwa ananifanyia vipimoΒ kadhaa ikiwemo Ultra Sound ili kugundua Mtoto amekaaje naΒ jinsia yake.Β
“Ndio Shem” nilimjibu kwa wasiwasiΒ
“Mh!”Β
“Mbona unaguna?”Β
“Hapana” Nilijua tu atamwambia Jonas lile jambo,Β
“Najua umeshtuka sana lakini ndio ukweli huo, Jonas hajuiΒ hili jambo nakuomba usimueleze nitakaa naye chini nitaongeaΒ nae” Hakunijibu, aliendelea na vipimoΒ
Suala lile lilizidi kunipa mawazo sana na kunifanya nikumbukeΒ zamani nilipokeketwa, Mama ndiye aliyenilazimisha kufanyiwaΒ vile akisema ni mila zao na kama nitakataa nitatengwa.Β
Mimba ilipofika miezi 6, yule Daktari alinipigia simu naΒ kunitaka niende tena Hospitali, baada ya kumaliza vipimoΒ aliniulizaΒ
“Umeshaongea na Mumeo?”Β
“Hapana sijaongea naye, nitaongea naye siku za hivi karibuni”Β
“Ina maana hamkutani kimwili? ilikuwaje asilijuwe hiliΒ jambo?”Β
“Ni stori ndefu sana Dokta”Β
“Kuwa makini sana hili jambo halipaswi kuwa siri kabisa,Β mueleze ukweli” Alinipa tena mtihani wa kuongea na Jonas,
Nilipanga nizungumze naye niliporudi, kabla hata sijaongeaΒ naye Mama alinipigia simu na kunitaka niende Arusha, nilianzaΒ kumkatalia sababu alisema niende mwenyeweΒ
“Nenda Veronica” Jonas alisemaΒ
“Naendaje bila wewe Mume wangu?”Β
“Kitakachojiri huko utaniambia”Β
Moyo wangu ulisita sana kelekea Arusha tena bila Jonas, MamaΒ yangu nilianza kutomuelewa kwa kauli zake tata kilaΒ alipozungumza na mimi.Β
Sikuwa na budi bali kuondoka na kwenda Arusha kuitikia witoΒ wa Mama. Mimba ilifika miezi 7 kasoro, Mama alitaka nikaeΒ Arusha hadi nitakapo JifunguaΒ
“Mama hilo halitawezekana, nitajifungua vipi bila JonasΒ kuwepo?”Β
“Veronica usiwe mbishi, unatakiwa kujifungua kwa mila naΒ tamaduni za kabila letu” Alisema Mama kwa msistizo,Β nikakumbuka maneno ya daktari kuwa nilikuwa nina ujauzito waΒ Mtoto wa Kike, hofu ya mtoto wangu kufanyiwa kamaΒ nilivyofanyiwa ilinijia nikamwambia MamaΒ
“Mtoto wangu hawezi kufanyiwa kama mlivyonifanyia mimi” “Unamaanisha nini?”Β
“Hawezi kukeketwa kama mnavyotaka”Β
“Nani amekwambia tunataka kumkeketa Mtoto wako? na kama niΒ wakike ni lazima afanyiwe hivyo Veronica”Β
“Sitakubali Mama, nitapingana na wewe hadi naingia kuburini”Β
“Anhaa! Huyo Jonas anakupa kiburi sana, tutaona” Alisema MamaΒ kisha alicheka na kujifanya ameongea utani ila kwa akiliΒ zangu na jinsi nilivyomtafsiri niligundua kuwa alimaanishaΒ alichokisema.Β
Nilijawa na hofu kila nilipomfikiria Mwanangu, Yule jiraniΒ alinifuata na kunipongeza kutokana na ujauzito wanguΒ
“Ahsante Jirani, ndio ukubwa huu”Β
“Lakini Veronica unatakiwa kuwa makini sana na Mama yako!”
“Kwanini?”Β
“Mama yako ana sifa mbaya hapa mtaani, inasemekana yeye naΒ Kaka yake wanashiriki ushirikina”Β
“Unamaanisha Mama yangu ni Mchawi?”Β
Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TANO
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β
8 Comments
Huyu veronica nae kama hana akili….anapekekeshwa sna an mamake
Hii kaliiπ₯π₯ kesho zitoke mbili Admin.π
Aah hiki kipande ni. Shidaa,, admin tunaomba utuwahishie mwendelezo kwa wakati π
Kesho Fanya Utoa Double Mr Admin
Aah hiki kipande ni. Shidaa,, admin tunaomba utuwahishie mwendelezo kwa wakati π
Unachelewa Kutuma mwendelezo
Mzuri
mu34jk