Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Sita-26
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Sita-26

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 7, 2024Updated:September 7, 202412 Comments13 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Muhonzi akafanikiwa kukata kamba alivyofungwa, giza lilikua nene ndani ya Chumbaย  alichohifadhiwa, akajaribu kuchungulia dirishani kwa mtindo wa kuruka sababu dirishaย  lilikua juu sana lakini hakuambulia kuona chochote kile, akajaribu kuitaย 

    โ€œKuna nani hapo nahitaji Majiโ€ aliita kwa makusudi huku akifahamu fika kua eneo hilo linaย  ulinzi mkali kuhakikisha yeye hachomoki, akaita tena, ndipo aliposikia hatua za kiatu zikijaย  upande wake, akarudi haraka kuketi sakafuni alipokua ameketi.ย 

    Mara taa ikiwashwa, kisha akatupiwa maji aliyoyataka. Endeleaย 

    SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

    โ€œNitakunywaje sasa na umenifunga kamba?โ€ akauliza Muhonzi kwa ujanja huku akiwa tayariย  ameshakata ile kamba, yule Mlinzi akamtazama sana Muhonziย 

    โ€œNi kweli sasa nitakunywaje nina kiu sana Aaaaaahhhโ€ akazidi kusema Muhonzi hukuย  akijibaraguza kama Mtu aliyefungwa mikono yake, yule Mlinzi ikamlazimu kufungua sasaย  mlango wote kisha akaingia ndani ya chumba hicho, ndicho alichokua anakitaka Muhonzi.ย 

    Akaoneshwa Bunduki, kisha akaambiwaย 

    โ€œHuwezi kufanya ujanja wowote, nitakupa majiโ€ alisema yule Mlinzi, akaiokota chupa yaย  maji kisha akaifungua na kumsogezea Muhonzi ili amyweshe, hakujua kua alikuaย  ameshafanya kosa kubwa sana, pale pale Muhonzi akamtandika ngumi nzito ya pua,ย 

    akamfwata kwa haraka na kumvunja shingo. Akaiyokota ile Bunduki kisha akaanza kutafutaย  njia ya kutoka ndani ya Godauni.ย 

    Akatembea kwa taratibu kwa mahesabu mazito sana ili asije rudi mikononi mwa Zagamba,ย  akasikia sauti ya TV, akajua fika kua Walinzi wengine walikua huko. Akasogea hadi eneoย  hilo na kuwakuta walinzi wakiwa wanakunywa pombe na kuvuta sigara.ย 

    Hakutaka kusema nao, akatafuta kona nzuri akapita ili alifikie lango kuu la kutoka ndani yaย  Godauni hiyo iliyojaa giza zito. Taratibu sana Muhonzi akalisukuma lango kisha akatoka njeย  ya Godauni, muda ulivyozidi kwenda ndivyo ambavyo wale Walinzi walivyoshtuka baada yaย  kuona mwenzao harudi, akatumwa mmoja wao kwenda kuangalia, akamkuta akiwaย  ameshakufa. Msako wa kutafutwa kwa Muhonzi ukaaanza ndani ya lile Godauni, walipokujaย  kugundua kua alishatoka ndani ya Godauni tayari Muhonzi alikua ameshafika mbali kabisa.ย 

    **ย 

    Baada ya kuchomoka mikononi mwa Watu wa Zagamba, akakimbilia kwenye jumba la siriย  ambalo alikua akilitumia kufanyia kazi zake, kichwa chake kikiwa kinawaka moto kwanzaย  alihitaji kujisafisha mwili mzima baada ya kukaa godauni kwa siku kadhaa.ย 

    Maji ya Baridi yakakubali kuuufanyia Utakaso wa kutosha mwili wa Muhonzi, akili ilipokaaย  sawa akawa tayari kujua ni wapi alipo Elizabeth, bado aliamini kuwa alikua hai. Jambo laย  kwanza alilolifanya baada ya kuketi na kuwasha mitambo yake ni kuanza kusaka mara yaย  mwisho simu ya Elizabeth ilizimwa wapi.ย 

    โ€œPicha ya Ndegeโ€ ndiyo sehemu pekee ambayo simu ya Elizabeth ilizimwa kwa mara yaย  mwisho, aina ya simu aliyoitumia ilionekana lakini uzuri simu hiyo bado ilikua Hewani,ย  Usiku ulikua mwingi, akajipumzisha kwanza Kitandani ili akiamka aendelee na upekuziย  wake kwa njia ya Mtandao, masuala hayo ndiyo yaliyokoleza ukaribu wake na Elizabethย  Mlacha.ย 

    **ย 

    Saa 3 Asubuhi, Tanzaniaย 

    Muuwaji wa kuaminika alikua akipata chai ya asubuhi sehemu fulani ya Tanzania, safariย  yake ya Usiku mzima ilikomea kwenye moja ya Hoteli, alipumzika hapo ili afanye safari yaย  kuelekea eneo nyeti la Black Site.ย 

    Baada ya kumaliza, aliingia kwenye gari kisha akaendelea na safari yake ya Masaa matatuย  baada ya Chai, sasa aliushika Msitu mmoja, akaisweka gari eneo fulani, akachukua begi lakeย  na kupandisha kilima kimoja. Alionekana ni Mtu anayejua anachokifanya, kazi aliyopewa naย  Waziri Mkuu ni kuhakikisha anamchukua Elizabeth kutoka Mikononi mwa Walinzi wa Balckย  Site.ย 

    Begi alilolibeba lilikua na silaha moja ya masafa marefu pamoja na Darubini, aliketi juu yaย  kilele cha kilima hicho, huku macho yake akiyaelekeza eneo la umbali wa Kilomita Nane,ย  hapo ndipo ilipo Black Site.

    Akatoa Ramani ya jengo la Black Site, ramani hiyo ilichukuliwa Ikulu baada ya Waziri Mkuuย  kuikamata Ikulu, muuwaji akatabasamu. Kisha akalala usawa mzuri na kuiweka Bunduki yaย  Masafa marefu vizuri, akachukua Darubini na kuanza kulikagua jengo hilo kwa uzuri.ย 

    Akajifunika kofia nyeusi, kisha akairejesha Darubini ndani ya Begi, akaanza kuitumiaย  Darubini iliyo kwenye Bunduki yake, macho na hisia zake akayaelekeza ilipo Black Site,ย  eneo alilolala alikua akilitazama jengo hilo lenye vioo kwa uzuri sana.ย 

    Aliona na kuhesabu idadi ya Walinzi walio ndani ya Jengo ambao ni Makomandoo waย  kuaminika aliokua akiwatumia Rais Lucas Mbelwa, alihitaji kuwamaliza kwanza. Ndani yaย  jengo palikua na zaidi ya Makomandoo hamsini. Wote aliwapigia mahesabu, kisha akaikunjaย  Bunduki yake na kuizamisha ndani ya Begi, akarudi chini ya Kilima na kuanza kutembeaย  kwa kutumia barabara ya vumbi iliyokua ikielekea Black Site.ย 

    Muuwaji huyo, alipokaribia aligundua kwa haraka uwepo wa ulinzi maalum wa Nyayaย  nyembamba za Umeme ambazo ndizo zilizokua zikilinda eneo hilo, alishajiandaa sababu siriย  za ulinzi wa ndani na nje ya Jengo alikua amezipata.ย 

    Akachomoa kifaa kidogo chenye mfanano na Simu, kisha akauzima umeme huo ndani yaย  sekunde ishiri akawa amezivuka nyaya hizo. Taratibu akakimbia na kujificha nyuma ya ukutaย  wa jengo la Black Site, kuhusu idadi ya walinzi wa ndani ya Jengo hakua na wasiwasi naoย  sababu alishawapigia mahesabu makali sana.ย 

    Akasimama hapo kwa mahesabu mazito, kisha akachungulia, jengo hilo lililokua na viooย  vingi ambavyo vingefanya urahisi wa Muuwaji kujulikana kua amefika, akapiga hatua zaย  haraka na kuuwahi ukuta wa pili, akajificha kisha akatoa kamba kutoka ndani ya Begi lake,ย  akairusha kamba kuelekea juu, iliponasa akawa na zoezi moja tu la kuifuata paa ya jengoย  hilo.ย 

    Kisha taratibu akatembea juu ya paa la jengo huku akiwa anapiga mahesabu yake vizuri,ย  alikua na ramani nzima ya jengo hilo la Black Site, ilikua rahisi kwake kujua ni wapi atawekaย  kambi hapo juu ya paa ya Jengo, akafika mahali ambapo palikua na pambo kubwa la saa,ย  eneo hilo lilikua karibu na mlango Mkuu wa Kuingia ndani ya Jengo hilo, kando ya jengoย  ndimo walimokua wakikaa makomandoo.ย 

    Kwake hao ndiyo kikwazo kikubwa kufanikisha kazi ya Kumchukua Elizabeth, akaiwekaย  vizuri kofia yake kisha akalala kwa ustadi mzuri huku akilitazama jengo ambaloย  Makomandoo walikua wakipatikana.ย 

    Akaishusha Bunduki yake ya Masafa marefu kutoka ndani ya Begi lake kisha, akaitega vizuriย  kuelekea kwenye jengo, kichwani alikua na ramani yote. Kitu pekee alichohitaji kukifanyaย  hapo ni kuufunga mlango wa Umeme ambao ndio uliokua ukitumika na Makomandoo hao,ย  mwendo wa dakika ishirini awe tayari ameshamchukua Mateka wake kwani kupambana naย  Makomandoo hao haikua kazi rahisi kwake.ย 

    Akafunga kiwambo cha kuzuia sauti, kisha akalenga kitasa cha Umeme ambachoย  kingemfanya atenganishe kati ya Makomandoo na Walinzi wa kawaida wa Black Site,ย  umbali wa jengo hilo ni zaidi ya Mita sabini.

    Dakika moja na nusu ilimtosha kujihakikishia kua risasi atakayoiachia hapo itaenda kukataย  mawasiliano ya jengo la Makomandoo na jengo la Black Site. Akavuta hewa nyingi kishaย  akaiachia taratibu na kukaza mikono yake kisha kidole kikafanya kazi ya kusukuma risasiย ย 

    Haraka Alam ikalia kuashilia kua palikua na hitilafu mlangoni, hii ni baada ya Muuwaji huyuย  kukita risasi mlangoni. Haraka walinzi wa Black site pamoja na Makomandoo walio ndani yaย  jengo lililopigwa risasi wakawa kwenye taharuki nzito, akasubiria kwa sekunde kadhaa iliย  Mlango wa Black Site ufunguliwe, alipousikua umefunguliwa akajirusha mithiri ya Nyaniย  mzeeย 

    Akatua chini kama Buibui, haraka akaachia pigo takatifu la Risasi za mahesabu naย  kusambaratisha walinzi watatu waliokua eneo la Mlango kisha akaingia ndani ya Jengo hilo.ย 

    Elizabeth aliposikia Alam ikilia kuashiria kuna tatizo alishaanza kuhisi ujio wa Mtu mbayaย  ndani ya Jengo la Black Site, japo alikua amechoka sana lakini akaweza kumwambia Mlinziย  kua amfungue kwani eneo hilo siyo salama kabisaย 

    โ€œUsipofanya hivyo Utakufaโ€ akakazia Elizabeth huku akijitingisha kwa nguvu chacheย  alizobakiwa nazo, yule Mlinzi hakutaka kumwelewa Elizabeth hadi pale aliposikia risasiย  ikisikika karibu na Mlango wa chumba cha Mateso ambacho Elizabeth alikua amehifadhiwa.ย 

    โ€œNifungue tafadhaliโ€ alisema Elizabeth, lakini akili ya yule Mlinzi ikajikuta imezubaaย  kidogo, ghafla akapigwa risasi ya Kichwa, kisha Mlango ukafunguliwa, akaingia Muuwaji,ย  akamtazama Elizabeth kisha akatoa tabasamu la kufanikisha kazi yake.ย 

    Hakutaka kupoteza muda akamzimisha kwa kumchoma sindano ya Usingizi, akamfungua naย  kumweka begani, maiti za Walinzi zilikua za kutosha sakafuni, akatoka hadi nje ya Jengo laย  Black Site wakati huo Makomandoo wakiwa wanahangaika namna ya kufungua ule Mlangoย  wa Umeme ambao kwa kawaida hufunguka baada ya dakika ishirini endapo utapata Hitilafu.ย 

    Akauvuka uzio wa Umeme kisha akaanza kuzikata Kilomita kuelekea lilipo gari lake aanzeย  safari ya kurejea Ikulu, mara zote alikua akiitazama saa yake kwa maana zikitimia dakikaย  ishirini wale Makomandoo watatoka ndani ya jengo na kuanza kumsaka kila kona. Akaianzaย  riadha baada ya kugundua kua alikua amebakisha dakika tatu kumalizika kwa ule mudaย  aliokua ameupangilia kulifanya tukio la kuvamia Black Site.ย 

    Ndani ya jengo tayari makomandoo walishajiandaa kutoka huku wakisubiria muda muafakaย  ambao Mlango huo wa umeme utakapokua umefunguka, Muuwaji alikua akikimbia naย  Elizabeth aliyepoteza fahamu, akapandisha kilima kidogo lakini kwa Bahati mbaya akaterezaย  na kujikuta akimtupa Elizabeth ambaye akavingirika na kutumbukia kwenye korongo, kwaย  Bahati nzuri akanasa kwenye Mti.ย 

    โ€œShit!!โ€ akasema Muuwaji, akaanza harakati za kutaka kumtoa Elizabeth, lakini kelele zaย  Makomandoo zikasikika, akatazama saa yake na kuona tayari muda ulikuwa umekwisha naย  tayari Makomandoo walikua wakija kwa kasi mahali ambapo Muuwaji alikua amesimama.ย 

    Kwanza akatafuta mahali na kujificha ili Makomandoo wasiweze kumwona, akaangalia risasiย  zilizopo kwenye Bastola yake, kisha haraka akaenda mbali na eneo lile, akauzunguka mlimaย  mmoja na kwenda kujificha huko kisha haraka akaitoa Bunduki yake kutoka ndani ya Begi.

    Akaielekeza eneo ambalo Elizabeth alikua ametumbukia, alikua akihema kutokana naย  kukimbia kwa muda mrefu, Makomandoo wakalipita lile eneo kisha walipofika mbeleย  walitawanyika ili kumsaka kwa uzuri adui yao baada ya kugundua adui yao hakuitumiaย  Barabara ya vumbi bali alizama Msituni.ย 

    Muuwaji akautumia Mwanya huo kuuzunguka Mlima mdogo na kisha kutokea nyuma yaย  Makomandoo kisha akapiganisha akili namna ambavyo anaweza kumchukua Elizabethย  kutoka juu ya Mti ulio korongoni, mara akasikia mlio wa gari ukija kutokea Upande wa kuliaย  ambapo ndiyo palikua na njia ya kutoka Black Site, haraka akajitupa Korongoni na kutuaย  kwenye ule Mti ambao Elizabeth alinasia kisha kwa haraka akamsomba na kushuka nayeย  chini ambako palikua Na Msitu wa kutosha.ย 

    Akajipigiza bega kwenye jiwe, kila mmoja akatua upande wake lakini hakuna Hataย  Komandoo mmoja aliyeshtuka kua Adui yao alikua Korongoni, wenge zito likamzongaย  Muuwaji akiwa anajitafuta, akayaruhusu macho yake kutulia, akamwona Elizabeth akiwaย  mita kadhaa kutoka alipo yeye.ย 

    โ€œAgggghhhโ€ akagugumia kwa maumivu makali huku akinyoosha bega lake, lililo jaa damu,ย  kisha akajisomba na kumsogelea Elizabeth. Akasimama na kuvuta hewa ya kujituliza vyemaย  halafu akaangaza juuย 

    Jua lilikua likiwaka, ndege wa Msituni walikua wakipiga kelele za hapa na pale, Purukushaniย  eneo la juu zilikua za kutosha kisha akajishika kiuno chake na kujinyoosha vyema, hakuishiaย  hapo akachana tisheti lake na kujifunga eneo la Bega, kisha akiwa amebakiwa na vest nyeusiย  akajitwika Elizabeth, akaanza kuisaka njia ndani ya Msitu wenye giza.ย 

    Haikua rahisi kwake kujua alikua akielekea upande upi kwasababu alikua ameshapotezaย  mwelekeo sahihi, akajikuta akisambaa Msituni kwa muda mrefu hadi pale Helkopta za Blackย  site zilipoanza Msako kila kona ya Msitu.ย 

    **ย 

    Kelele za popo na sokwe zilianza kusikika ndani ya Msitu wa Magoroto, hatua kubwa zaย  vishindo zilimfanya Benjamin Kingai aliye ndani ya pango atoke, kwanza alikutana naย  Zandawe akiwa amevaa nguo za ngozi za wanyama. Pili alikua ameongozana na kundiย  kubwa la Popo waliozingira eneo la juu ili kumpa kinvuli.ย 

    Tatu, alikua ameshikilia Mkuki aliouchomeka chini, vyote hivi vikamfanya Benjaminย  ashangae, lakini tabasamu la kuchanua lilikua likiongezeka kwenye sura ya Malkia Zandawe.ย  Taratibu Benjamin alisogea karibu na Zandawe na kumuuliza kwa utaratibuย 

    โ€œKuna nini?โ€ alihoji kwa sauti ya chini ili adokezwe lakini Malkia Zandawe akajibu kwaย  sauti.ย 

    โ€œLeo ni siku ya Ukombozi Benjamin, siku ambayo unaenda kurudisha kila ulichokipotezaโ€ย  alisema kisha alikaa kimya, akamfanya Benjamin atupe swali jingineย 

    โ€œUnamaanisha nini kusema kila nilichokipoteza?โ€ akauliza Benjamin Kingai, kisha akamezaย  funda zito la mate huku kivuli cha wale popo ambao ndiyo jeshi la kuaminika la Malkiaย 

    Zandawe likiwa linamsaidia pia Benjamin kuikimbia mionzi ya jua ambayo ilianza kuaย  Mikali.ย 

    โ€œUmepoteza familia, umepoteza haki ya kuishi ndani ya Nchi yako, pia Mtoto na Mpenziย  wako.โ€ Benjamin akatoa tabasamu lenye Maswali mengiย 

    โ€œUnamaanisha……โ€ kabla hajamaliza kusema alikuja ndege mpelelezi wa Zandawe kishaย  akatua chini na kusema kwa Lugha ya ndege kisha Zandawe akamjibu Benjaminย 

    โ€œEneo uliloteswa imevamiwaโ€ alisema Kama vile Mtu aliyejua haswa anachosema, taarifaย  zote alipewa na ndege wake mpelelezi, hii ilimshtua sana Benjamin akajawa na taharukiย 

    โ€œVipi kuhusu Mtoto na….โ€ย 

    โ€œMpenzi wakoโ€ akadakika Zandawe kisha akasemaย 

    โ€œInatupasa kwenda sasa hivi huko kujua kinagaubaga, huo uvamizi hatuna hakika unafanywaย  kwa lengo gani, lakini yupo Msichana aliyetoroshwa hukoโ€ alisema Malikia Zandawe kishaย  alisubiria jibu la Benjamin, kabla hajajibu chochote Benjamin akamtazama yule ndege kishaย  akainama na kumwambia ndege huyoย 

    โ€œAhsanteโ€ aliposimama akamuuliza Malikia Zandaweย 

    โ€œTunafikaje huko?โ€ย 

    Malikia Zandawe akatabasamu kisha akamjibu kwa kumwambia nifuate, aliposema alikuaย  tayari amegeuka na kuanza kutembea huku wale Popo wakimfuata kwa juu, akamsogeza hadiย  eneo la wazi ambalo lilikua halina Miti kabisa ila lilizungukwa na Msitu mkubwa waย  Magoroto.ย 

    Katikati ya eneo hilo palikua na kitu kilichofunikwa Majani mengi makavu, Malkia Zandaweย  akasogea hadi hapo kisha akaanza kuondoa yale Majani yaliyokuaa yamerundikana,ย  Benjamin alipata Mshangao mkubwa baada ya kuona Helkopta ikiwa ndiyo iliyokuaย  imefunikwa hapo.ย 

    Pale pale kabla hata hajamaliza kushangaa akaletwa Mtu mmoja aliyefungwa mdomo wake kwa kitambaa, aliletwa na Sokwe Mkubwa ambaye ni rafiki wa Malkia Zandawe, Mtu huyoย  alikua na mavazi ya Urubani, alionekana wazi kua ndiye aliyekua rubani wa Helkopta hiyo.ย 

    โ€œNitakuacha Huru ukinifikisha nitakapoโ€ alisema Malkia Zandawe kisha akamtoa kitambaaย  eneo la Mdomo.ย ย 

    โ€œSiyo Mtu mbaya, ila mmenifanya nimekua Mbaya kwasababu hamtaki kuuheshimu naย  kufuata Misingi na mila za Msitu huuโ€ alisema Malikia Zandaweย 

    โ€œNaomba tafadhali, mateso niliyopata yametosha kua funzo kwangu, naomba niendeย  nitawaeleze ukweli kuhusu huu Msitu, naamani hakuna mwingine atakayetia mguu kwenyeย  huu Msitu.โ€ Alisema yule rubani huku chozi likimbubujika, Malkia Zandawe akainama naย  kumwambia

    โ€œNimeshakwambia kua sina ubaya na wewe, hamkutaka kusikiliza onyo langu, ukawe chanzoย  cha wengine kuupa heshima huu Msituโ€ Alisema kisha aliposimama akamwambiaย 

    โ€œNaamini hili litakua funzo kubwa kwenu, sikutaka kukuuwa kwa maana nilikua na Uwezoย  wa kukufanyia ubaya kama niliowafanyia wengine walioingia ndani ya Msitu bila kufuataย  utaratibu. Kuna viumbe vinaishi humu, vinahitaji utulivu n amani kama ambavyo nyinyi kilaย  siku mnapiganiaโ€ alisema Malikia Zandawe, kidogo akaanza kulengwa na Mchozi.ย 

    Benjamin akamsogelea Malkia Zandawe na kumtuliza kwa kumshika bega, hata yule rubaniย  wa Helkopta ya Kijeshi aliona wazi kua Binti huyo alikua akizungumza kwa hisia kali iliyomuumiza. Malkia Zandawe akafuta chozi lake kisha akamwambia ndege wake mweupeย  aongoze njia, akamtaka na Benjamin aingie ndani ya Helkopta hiyo pamoja na sokwe wakeย  ampendaye.ย 

    Kitendo cha ndege kuruka kiliwafanya na Popo kuzama Msituni zaidi kwa kukimbia kwaย  spidi kali kisha Benjamin, rubani, Malkia Zandawe na Sokwe wakaingia ndani ya Helkoptaย  hiyo tayari kuelekea ndani ya Black Site kuikomboa familia ya Benjamin Kingai. Dakikaย  tano baadaye Helkopta ikawa angani ikimfuata ndege mkubwa mpelelezi aitwaye Gola.ย 

    Nini kitaendelea?ย 

    Usikose SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost MSALA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    12 Comments

    1. Cesilia Nkunga on September 7, 2024 6:21 pm

      Hatareee, mambo ni ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    2. Given Gihsy on September 7, 2024 6:26 pm

      nice sasa kwel ubaya ubwela , ila prime minister๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ

      Reply
    3. Katie on September 7, 2024 6:28 pm

      Wooow mambo yanzd kuwa mambo๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    4. Rumbyambya Jr on September 7, 2024 6:36 pm

      Tuwekee na sehemu inayofata ya 27 leo saa 3 ๐Ÿ˜

      Reply
    5. Ganai on September 7, 2024 7:00 pm

      Konki

      Reply
    6. Bplm1664 on September 7, 2024 7:04 pm

      ๐Ÿ๐Ÿ

      Reply
    7. Deo on September 7, 2024 7:09 pm

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    8. Yuliakimario on September 7, 2024 7:43 pm

      Admin kazi nzuri ๐Ÿ‘๐Ÿ‘

      Reply
    9. Clever David on September 8, 2024 8:30 am

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    10. ๐Ÿ“Œ + 1.955327 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/E34y9iSdaRJD7QXHZ9jb9R?hs=68578d5d8d139fabbfc1ecb548b67a2e& ๐Ÿ“Œ on June 17, 2025 4:02 am

      v2wr11

      Reply
    11. ๐Ÿ“™ โณ Alert: 0.9 BTC expiring. Open wallet > https://graph.org/CLAIM-YOUR-CRYPTO-07-23?hs=68578d5d8d139fabbfc1ecb548b67a2e& ๐Ÿ“™ on August 9, 2025 10:31 pm

      2fgjhv

      Reply
    12. ๐Ÿ“‡ ๐Ÿ”ท Pending Deposit: 0.25 BTC from external sender. Review? => https://graph.org/REDEEM-BTC-07-23?hs=68578d5d8d139fabbfc1ecb548b67a2e& ๐Ÿ“‡ on August 29, 2025 7:30 pm

      hnz7m6

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE โ€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.