Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Nne-24
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Nne-24

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 5, 2024Updated:September 7, 202410 Comments9 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Mfukuzano ulikua mkali kwa hatua kadhaa, kisha ghafla yule Mwanaume alisimama,ย  aligeuka kisha aliliweka lile Brifkesi chini, akatabasamu na kumwambia Elizabethย 

    โ€œNajua umekuja kwa ajili ya Nyaraka M21, hiyo hapo lakini unapaswa kunimaliza kwanzaโ€ย  alisema kwa kujiamini sana, aliongea kwa sauti iliyojaa Bashasha kama walikua kwenyeย  utani, Elizabeth akajua hapo haitokua kazi rahisi kupambana na huyo Mtu, akaangalia saaย  yake.. Endeleaย 

    SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

    Alibakiza dakika chache za kutoka ndani ya jengo hilo vinginevyo vikosi vitafika hapo naย  kunaswa. Akageuka nyuma kuona kama Muhonzi alikua karibu ili kazi ya kupambana naย  Mwanaume huyo isiwe ngumu lakini palikua patupu, ilimpasa yeye mwenyewe alichukueย  Brifkesi hilo.

    Akajiweka sawa ili kuupima uwezo wake kwa Mwanaume huyo asiye mfahamu, wakatiย  anamtafakari akaona kwenye shati palikua na namba za utambulisho, akagundua kwa wepesiย  kua Mtu huyo alitokea Ikulu kwa Rais Mbelwa. Pengine hiyo ilikua ni silaha ya siri ya Raisย  Mbelwa ndani ya Jengo hiloย 

    Elizabeth akajiandaa kumshambulia kwa kasi ya kicheche ili amalize kazi mapema kulikoย  kawaida, lakini kila pigo alilolipeleka kwa Mwanaume huyo lilikumbata na upepo, yoteย  aliyoyarusha hayakumfikia aliyakwepa. Kisha alimpa tena tabasamu, Elizabeth akaona hizoย  ni dharau za kutosha, akajikunjua na ngumi mbili alizozipangiliaย 

    Zote zilikwepwa na mwanume huyo ambaye baada ya kukaa sawa alirusha mapigo matatu yaย  mguu wa kushoto, mapigo mawili yakatua kwenye bega la Elizabeth, wakati anapepesukaย  yule Mwanaume akadandia ukuta na kuachia pigo lingineย 

    Pigo hilo lilikua maalum kwa ajili ya kukita sehemu ya kifua cha Elizabeth lakini kwa haraka alijivingirisha na kujiokotanisha. Elizabeth akapanga tena pigo, safari hii hakutaka kwendaย  kwa pupa sababu alishagundua Mwanaume huyo ana ujuzi mkubwa wa Mapigano.ย 

    Akawa anatupa mapigo kwa akili kubwa sana, angalau sasa akaweza kumgusa Mwanaumeย  huyo kwa ngumi ya kuparaza iliyopita mbavuni hadi akakata kifungo cha Shati la mwanaumeย  huyo.ย 

    Yule Mwanaume akabonyea kidogo kama Mtu mwenye kibiongo halafu akawa anachezeshaย  kichwa chake kama nyoka Cobla, mtindo huo ukawa unamchangaya sana Elizabeth akajikutaย  akiambulia vichapo vya kufwatana hadi akaanguka chini, hakuweza kumsoma kabisaย  Mwanaume huyo ambaye alikua akibadilika sana kwenye mapigano.ย 

    Damu ikaanza kumtoka mdomoni, akazidi kupandwa na hasira akajikuta akikurupuka kwenye kurusha mapigo, akawa anapigwa kwa kila pigo alilokua anarusha hadi akabamizwaย  ukutani kwa nguvu sana, akashindiliwa na pigo zito la shingo, likampeleka chini, kisha yuleย  Mwanaume taratibu akamsogelea Elizabeth na kuanza kumkaguaย 

    โ€œNilikwambia hutoweza kupata M21โ€ alisema Mwanaume huyo, kisha alisimama naย  kunyanyua Mguu wake ili aikanyage sura ya Elizabeth, lakini ghafla alikutana na teke zitoย  lililomtupa mita kadhaa, mbele yake alimwona Kijana mwemye umbo kama lake, Kijanaย  huyo alikua ni Muhonziย 

    Kwanza yule Mwanaume hakuamini kama teke hilo zito lilitoka kwa Kijana huyoย  Mwembamba ambaye ukimtazama kwa haraka utaona ni namna gani alikua mlegevu, jamboย  la kwanza alihitaji kujua kuhusu hali ya Elizabeth Mlacha.ย 

    โ€œUko sawa?โ€ย ย 

    โ€œFaili iko kwnye hilo Brifkesiโ€ akasema Elizabeth akiwa anajivuta aketi vizuri, Brifkesiย  lilikua chini, kazi ilikua ni Nani anayeweza kuliokota Brifkesi kwa haraka. Wote wakaiwahiย  Brifkesi lakini kuiokota haikua jambo la urahisi, alipozubaa kidogo tu Muhonzi akalambwaย  mtama wa nguvu kisha yule Mwanaume akaliokota Brifkesi, alishajua kupambana naย  Muhonzi siyo jambo rahisi, alichofikiria hapo ilikia ni kutimka.

    Akaanza kukimbia kuuelekea Mlangoni lakini Muhonzi akafyatua risasi ikamchapaย  Mwanaume huyo Mguuni akaanguka chini, Muhonzi akasogea hapo na kuliokota Brifkesi,ย  kisha akamtandika risasi nyingine tatu za kumnyongโ€™onyeza. Haraka akarudi kumfwataย  Elizabeth, wakaongozana ili waondoke lakini walipofika mlangoni walisikia michakacho,ย  wakajua haraka kua kuna askari waliofika hapo.ย 

    โ€œTunafanya nini?โ€ akauliza Muhonzi, Elizabeth akautoa mkoba wake mdogo aliouvaaย  mgongoni, akatoa baruti, akaziwasha zikaanza kutoa moshi mzito kisha haraka akaufunguaย  mlango na kuziachia, zikasababisha moshi mzito. Walinzi wakajikuta hawaoni chochote,ย  muda huo Elizabeth na Muhonzi wakautumia kupambana na walinzi wachache kishaย  wakazivaa nguo zao na kutoka nje ya jengo la Piza Hunt, huko nje tayari Watu walishaanzaย  kujaa baada ya milio ya Risasi kusikika, Muhonzi na Elizabeth walitoka wakiwa wamezibaย  sura zao kwa Mask ambazo wale walinzi waliingia nazo.ย 

    Hakuna aliyewashitukia, wakavuka barabara na kuingia kwenye gari ambayo Elizabethย  alifika nayo, wakaishika barabara ya kuelekea njia panda ya Keko, wakatokomea.ย 

    **ย 

    Taarifa ya kutoweka kwa Elizabeth na Muhonzi ilizidi kupasua kichwa cha Rais Lucasย  Mbelwa, kibaya zaidi tayari mafaili yalikua yameshaibiwa ikiwemo nyaraka M21 ambayoย  ilikua na siri za kutosha za Rais Mbelwa. Akaagiza Wasakwe kila koja ya Nchi, tena Msakoย  ufanyike kimya kimya ili usije leta taharuki.ย 

    โ€œHatuna muda wa kuendelea kua hapa Muhonzi, cha Msingi kwasasa ni kukutana naย  Mnunuzi tumpatie taarifa kisha tusunde kibunda cha pesa tutafute Nchi tukafurahiโ€ alisemaย  Elizabeth baada ya kufika yalipo Makazi yao ya Siri, maeneo ya Ilala Bungoni.ย 

    Tabasamu pana likaipamba sura ya Muhonziย 

    โ€œNina imani tutaishi Maisha ya kifahari sana, kwanini tusiende Moroco my love?โ€ akaulizaย  Muhonziย 

    โ€œPopote utakapo, nitaambatana na weweโ€ mara simu ya siri ilianza kuita, hakua mwingine bali Zagamba, alishapewa taarifa na Mke wa Rais Mbelwa kua tayari faili limeibiwa,ย  Elizabeth akaipokea simu hiyo.ย 

    โ€œUko wapi?โ€ akahoji Zagamba kwa sauti iliyotoka bila salamu.ย 

    โ€œHapana shaka umesikia kua nyaraka zimepatikana, niambie tunafanyaje makabidhianoโ€ย  akauliza Elizabeth, ukimya ukatamaraki kidogo kisha akajibu.ย 

    โ€œJitahidi ufike Msata, nakutumia Anuani sasa hiviโ€ akasema Zagamba Halafu simu ikakatika,ย  ikamwacha Elizabeth na wasiwasiย 

    โ€œAnasemaje?โ€

    โ€œAnahitaji nifike Msata, sijui kwanini, Oooh anuani imeingiaโ€ akaifungua anuani, akakuta niย  Msata tena nyakati za Usiku, kwa kiasi kikubwa ilimpa wasiwasi.ย 

    โ€œSikia Muhonzi, hatuwezi kwenda wote huko, utabaki hapa na nitakupa taarifa ya kila hatuaย  nitakayoipiga, kama kuna baya basi lisitupate wote, naamini hii itakua kazi ya mwishoโ€ย  alisema Elizabeth kisha akayatupa macho yake kwemye Brifkesi.ย 

    โ€œUnafikiria nini?โ€ akauliza Muhonzi akiwa naye analikodolea macho Brifkesi lililo juu yaย  meza ndogoย 

    โ€œNi lazima tulifungue kwanza, hatuwezi kuifanya Biashara tusiyoielewaโ€ akasema Eizabethย  kisha akafungua droo na kuchukua vifaa kwa ajili ya kufungua Brifkesi hilo lililofungwa kwaย  namba Maalum, ikawachukua dakika ishirini kulifungua bila kulivunja, ndani yakeย  mlihifadhiwa Flashi moja mpya, ndicho kitu pekee kilichotunzwa humo.ย 

    โ€œNafikiri hii ndiyo yenye kutunza, basi tuiangalie kwanzaโ€ akasema Elizabeth, akampatiaย  Flashi Muhonzi. Baada ya kuiweka kwenye kompyuta yao walianza kuziona taarifa zaย  kutisha ambazo zilitunzwa ndani ya flashi.ย ย 

    Giza lilipoingia Elizabeth alianza safari ya kuelekea Msata kwa ajili ya kufanyaย  Makabidhiano na Zagamba, ndipo Mkasa mzito ulipomkuta huko hadi akakutana naย  Benjamin Kingai.ย 

    **ย 

    Muhonzi alipomaliza kukumbuka namna walivyoiba Nyaraka M21, akakumbuka kua alikuaย  na kazi ya kuhakikisha anatoroka ndani ya Godauni hiyo vinginevyo anaweza akauawa hapoย  na Zagamba mwenye hasira. Akajisogeza hadi mlangoni, palikua na eneo la ukuta lenyeย  ncha, akaanza kufanya jitihada za kukata ile kamba kwa nyuma, aliendelea na zoezi hilo kwaย  zaidi ya dakika kumi na tano bila mafanikio hadi akakata tamaa ya kutoroka hapo.ย 

    Upande wa Pili, ndami ya Msitu wa Magoroto. Jua la utosi lilikua likiipiga ardhi hiyo pamojaย  na kila kilichomo ndani yake, Malikia Zandawe alikua amesimama juu ya mlima mdogo ulioย  pembezoni mwa Msitu huo, macho yake yalikua yakiangalia uzuri wa Bonde la Maji lililokuaย  likitiririsha Maji kutoka juu ya Kilima hicho.ย 

    Hali ya hewa ilikua nzuri na ya kuvutia sana iliyompa utulivu wa kutosha, mara ndege wake anayemtumia kwa ajili ya Ulinzi alifika hapo, ndege huyo aliyempa jina la Gola alituaย  akitokea safari ya Mbali kuitafuta Black Site ambako mateso makali yalikua yakifanyika.ย 

    Haraka Zandawe alipiga goti ili azungumze na ndege huyo kwa Lugha ya ndege ambayoย  alikua akiielewa vizuri, akapewa taarifa ya wapi ilipo Black Site, Basi uso wa Zandaweย  ukatawaliwa na tabasamu la maana, akampa busu ndege huyo kisha akamruhusu aondoke,ย  yeye akakimbilia yalipo Makazi yake.ย 

    Akamkuta Benjamin akiwa anacheza na Sokwe Mkubwa ambaye ni rafiki wa Zandawe,ย  alifika akiwa anahema huku tabasamu likizidi kuongozekaย 

    โ€œKuna nini, mbona uso umechanua kiasi hicho?โ€ aliuliza Benjamin huku akiacha kucheza naย  sokwe, akili yote akaihamishia kwa Zandawe.

    โ€œNimejua ni wapi ilipoโ€ย 

    โ€œIlipo nini?โ€ย 

    Basi Zandawe akamsogelea Benjamin na kumwambiaย 

    โ€œSehemu uliyoteswaโ€ย 

    โ€œSehemu niliyoteswa?โ€ akahoji Benjamin kwa Mshangao mkubwa sana, alichokisikia alihisiย  kama yupo Usingizini, ndipo akakumbuka kua Zandawe alimtuma ndege kuchunguza ilipoย  Black Site. Akanyanyuka alipokua ameketi akamsogelea Zandaweย 

    โ€œUna hakika?โ€ย 

    โ€œNilikwambia, Gola ni mpelelezi wangu nimtumainiye, yeye ndiye anayenipa taarifaย  nisizozijua, nzuri na Mbaya, hata siku ulipoanguka kutoka juu ya Helkopta ni yeye ndiyeย  aliyenipa taarifaโ€ alisema Zandawe, uso wa Mshangao ukamjaa Benjamin Kingai.ย 

    โ€œKwahiyo imejulikana ilipo, sasa…โ€ Benjamin mwenye wenge zito akakatishwa na kauli yaย  Malkia Zandaweย 

    โ€œTulia kwanza Benjamin, naamini kama Mtoto wako na Mpenzi wako wapo hai basiย  utawapata tuโ€ kisha aligeuka pembeni, japo alisema hivyo lakini alijisikia kuumia ndani yaย  nafsi yake, kisha akageuka akiwa mwenye kutabasamuย 

    โ€œTutaenda huko kwa ajili ya kuikomboa familia yakoโ€ alisema Malkia Zandawe kishaย  aliondoka hapo ndani ya Pango, yule Sokwe akamfwata kwa nyuma Zandawe. Woteย  walimwacha Benjamin akiwa ana furaha ya ajabu sana.ย 

    **ย 

    Mateso makali yalikua ndiyo sehemu ya Maisha ya Elizabeth Mlacha, kila kona ya mwiliย  wake ilitawaliwa na maumivu makali, alikua amefungwa mnyororo mikononi akiwaย  ananingโ€™inia huku damu iliyoambatana na udenda ikiwa inaendelea kumvuja. Hata nguoย  aliyokua ameivaa ilikua imetapakaa damuย 

    โ€œIko wapi M21?โ€ aliuliza Bi. Sandra, masaa kadhaa yalipita Elizabeth akiwa anaendeleaย  kuteswa bila kusema chochote.ย 

    โ€œIf you want to Kill Me, just Go ahead, but youโ€™ll find nothing ( Kama unataka kuniuwaย  niuwe lakini hutoambulia chochote)โ€ alisema Elizabeth kwa sauti chovu iliyojaa maumivuย  makali sana, Bi. Sandra alimtazama Elizabeth, moyoni akajisemeaย 

    โ€œSijapata kumwona Mwanadamu Mbishi na Mgumu kama huyuโ€ aliutupa mkono wakeย  uliojaa damu kwa hasira sana kisha akarudi kuketi kitini akitafakari ni namna gani afanye iliย  apate taarifa nyeti. Haraka akanyanyuka kutoka kitini kwa hasira akamfwata tena Elizabeth,ย  akamwambia

    โ€œUkiendelea kuwa jeuri utamfuata Rais alipoโ€ alisema kisha akaondoka ndani ya chumbaย  hicho, haraka Elizabeth akatambua fika kua Rais alikua ameshauawa na kilichokua kinaendaย  kufanyika ni Uasi mkubwa wa kuitawala Nchi.ย 

    Elizabeth akiwa ananingโ€™inia akaukumbuka Usiku wa Heka Heka.

    Nini kitaendelea?ย 

    Usikose SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost MSALA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    10 Comments

    1. Ammar Hassanain on September 5, 2024 5:32 pm

      Leo nami mnisome wa kwanza jmn

      Reply
    2. Lus twaxie on September 5, 2024 5:41 pm

      WA kwanza kusomaaaa mieeee

      Reply
    3. Yudah on September 5, 2024 5:47 pm

      Duuuh msala unazidi kuwa msala๐Ÿ”ฅ, haswa kwa wenye msala,,๐Ÿ‘‰ can’t wait for the next episode ๐Ÿ‘‰๐Ÿ‘‰

      Reply
    4. Migo on September 5, 2024 6:00 pm

      Tukumbuke kidogo๐Ÿ˜‡

      Reply
    5. Transporter on September 5, 2024 8:07 pm

      Unajua naisoma mara mbili mbili lakini naona Bado napaswa kuirudia kongore sana Kwa ndugu Mwandishi hakika ni utunzi maridhawa

      Reply
    6. Calvin paul on September 5, 2024 9:03 pm

      Adimi utapata chodaaa

      Reply
    7. Mr. Lonely on September 6, 2024 10:36 am

      Admin unaatarii nitakupa dada๐Ÿ‘๐Ÿ˜‰

      Reply
    8. Xalim on September 6, 2024 2:16 pm

      ๐Ÿ”ฅ

      Reply
      • Nelca on September 6, 2024 5:29 pm

        Kaa.move vile najiona natazama๐Ÿ˜œ๐Ÿ˜œ

        Reply
    9. Maxmilan on September 9, 2024 6:58 pm

      Jaman simulizi nzuri ningepata kuanza simulizi mwanzo ningefurahi sana naipataje admin

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.