Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barua Kwako Pacome Zouzoua Profesa Wa Boli
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Barua Kwako Pacome Zouzoua Profesa Wa Boli

    MhaririBy MhaririMarch 19, 20242 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mpendwa Pacome Zouzoua,

    Natumai barua hii inakukuta ukiwa mzima japokua sijajua unaendeleaje na goti lililokufanya usimalize mchezo dhidi ya Azam Fc lakini natambua unapiga hatua kubwa katika kazi yako ya soka. Ningependa kwanza kabisa kukupongeza kwa juhudi zako zinazoendelea na mafanikio yako katika klabu ya Yanga. Umeonesha kiwango cha juu tangu ufike mpaka sasa kwani una uwezo wa kipekee na kujitolea kwako kwa timu.

    Kutambuliwa kwa kiwango chako bora na kuitwa kujiunga na timu ya taifa ya Ivory Coast ni hatua kubwa katika kazi yako ya mpira wa miguu japokua nafahamu kuwa ushawahi kuichezea kipindi flani. Hii ni heshima kubwa sana ambayo unastahili kupata. Kuwakilisha nchi yako katika viwango vya kimataifa ni ndoto ambayo wengi hunuia kuifikia, na wewe unapata fursa hiyo.

    Hata hivyo, ninatambua pia umuhimu wa kuendelea kuihudumia Yanga kwani tunajua kuna michezo migumu mbeleni ambayo bila shaka ni muhimu mno kwa historia ya klabu ya Yanga pamoja na Tanzania kwa ujumla.

    Hakuna anayepinga kwamba Yanga inakutegemea wewe Pacome na uwezo wako wa kipekee kuchangia katika mafanikio yao kimataifa kwani ushafanya maajabu makubwa mengi tu. Tunathamini mchango wako katika timu na jinsi unavyoleta uzoefu na ujuzi wako kwa wenzako.

    Kwa hivyo, ninakuandikia barua hii ili kukuomba utafakari kwa makini chaguo lako. Unaweza kuendelea kuitumikia Yanga na kusaidia timu hii kufikia malengo yao waliyonayo, au unaweza kuchukua fursa ya kujiunga na timu ya taifa ya Ivory Coast na kuiwakilisha nchi yako kwa Fahari ingawa tunafahamu mchezo wa mwisho ulipata majeraha na kushindwa kuumaliza mchezo.

    Ninakuamini utafanya uamuzi sahihi kwa mustakabali wako binafsi na kazi yako ya mpira wa miguu. Tunakutakia kila la heri katika safari yako ya soka,

    Kwa heshima na ukarimu,

    SOMA ZAIDI: Barua Kwenu Washirikina Wa Mpira Wa Miguu Tanzania

    chama na pacome pacome yanga

    2 Comments

    1. Pingback: Hili La AL HILAL Kucheza Ligi Kuu Ya Tanzania Limenitafakarisha - Kijiweni

    2. Pingback: Barua Kwa Waziri Ndumbaro Kuhusu Jezi Na Uzalendo - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.