Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Huwezi Kumchukia Kayoko Kama Unaupenda Mpira
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Huwezi Kumchukia Kayoko Kama Unaupenda Mpira

    MhaririBy MhaririFebruary 15, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Ramadhan Kayoko
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mchezo wa mpira wa miguu Tanzania ni moja kati ya kitu ambacho kinapendwa sana na kuunganisha watu wengi kwa wakati mmoja kutoka sehemu mbalimbali na haswa mechi ambazo zinazikutanisha timu kubwa za soka hapa Tanzania.

    Ni sehemu pekee ambayo huwa kuna hisia na utani na ushabiki mkubwa zaidi huku ukichangiwa na matukio ambayo hujitokeza viwanjani huku mara nyingi yakiwa ni yale ambayo yanawahusisha waamuzi wa soka nchini kutokana na maamuzi ambayo yamekua yakijitokeza kutoka kwa waamuzi hao.

    Wakati nguvu kubwa inatumika ya kumshambulia mwamuzi wa kati Ramadhan Kayoko tukumbuke hata hao wenye mpira wao kuna wakati wanashindwa kutafsiri Sheria 17 za soka. Miaka nenda rudi timu zetu kongwe za Simba na Yanga zimekuwa zikinufaika na hawa hawa waamuzi lakini hakuna hata siku moja siku timu hizo zikipendelea viongozi au mashabiki wake wakatoka mbele na kukemea madudu yao

    Nitamkumbuka refalii Heri Sasii ambaye naye alikuwa akihukumiwa kwa kufanya makosa mara kadhaa tena aliwahi kuwapa goli Simba SC mchezo dhidi ya Azam FC na Ngoma ile kwenda sare, sikuwahi kuona mashabiki wakiandamana na kumkataa Sasii.

    Nashangazwa na hizi kampeni za kutaka kumkataa Kayoko wakati huyu ndiye mwamuzi ambaye kama Taifa tunamuangalia kwa umakini zaidi kwani tunafahamu kupata watu bora kama wao inakuwa ni ngumu na kuna muda tuache kulazimisha matokeo kama inakuwa siku mbaya kazini tusitengeneze presha kwa watu wengine.

    Leo hii kwenye vijiwe vya soka kila mtu ana lake kuhusu Kayoko vipi na hizo timu zingine ambazo zilikuwa zikiangukia pua maamuzi kama hayo nazo zisemejee, tuuwache mpira tusije kutengeneza vurugu kwa kuja na matokeo yetu mfukoni. Kufanya hivyo tutaaribu mpira na kupelekea kunyimwa hata ile nafasi ya kuaandaa michuano ya AFCON 2027.

    SOMA ZAIDI: Mzimu wa Mayele Uliomtesa Konkoni Na Sasa Uko Na Guede?

    kayoko refa kayoko

    1 Comment

    1. Pingback: JKT Tanzania vs Simba Mchezo Wa Historia Jeshini - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.