Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Simba SC Yazidiwa kete Kumnasa Kipa Marumo Gallants
    Africa | CAF

    Simba SC Yazidiwa kete Kumnasa Kipa Marumo Gallants

    David MohamedBy David MohamedJune 2, 2023No Comments1 Min Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni rahisi kusema Simba wamezidiwa tena ujanja baada ya kipa wanaodaiwa kumtaka Washington Arubi kutoka Marumo Gallants kusaini timu nyingine.

    Arubi alionyesha kiwango cha juu wakati Marumo walipovaana na Yanga kwenye hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika na kuelezwa kuwa Simba walionyesha nia ya kumsajili.
    Chanzo cha uhakika kutoka ndani ya Simba kimeeleza kuwa, jina la kipa huyo lilikuwa mezani kwa kocha Olvier Robert Robertinho likijadiliwa lakini jana wakapata taarifa kuwa ameshasaini sehemu nyingine.

    Taarifa iliyoripotiwa na magazeti ya Afrika Kusini inasema kuwa kipa huyo ambaye pia alikuwa akiwindwa na Simba ameshasaini mkataba wa mwaka mmoja kwenye kikosi cha Sekhukhune United.

    Arubi ameondoka Marumo bure kwa kuwa mkataba wake umeshamalizika na sasa ataitumikia timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini kwenye michuano ya Shirikisho Afrika msimu ujao.

    Washington Arubi

    Washington Arubi alikuwa na kipindi kizuri na Marumo na mwishoni mwa msimu alikuwa mmoja kati ya wachezaji waliopewa tuzo kutokana na mchango wao mkubwa kwenye timu hiyo ambayo imeshuka daraja.

    Habari zinasema Simba walikuwa wanamhitaji kipa huyo raia wa Zimbabwe ili awe msaidizi wa Aishi Manula ambaye kwa sasa yupo Afrika Kusini akisubiri kufanyiwa upasuaji wa nyama za paja.

    Kwa taarifa zaidi za usajili, tufatilie hapa.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.