Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Wachezaji Waliofunga Magoli Ya Mapema Bongo
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Wachezaji Waliofunga Magoli Ya Mapema Bongo

    MhaririBy MhaririDecember 12, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    NBC PREMIER LEAGUE
    Logo rasmi ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ligi kuu Tanzania Bara (NBC Premier League) imeendelea kushika hatamu na rekodi mblimbali zikiendelea kuwekwa katika ligi hiyo. Mpaka sasa anayeongoza ligi ni Azam Fc akiwa amecheza michezo 12 na alama zake 28 huku Mtibwa Sugar akishika mkia na alama zake 5 katika mechi 12 alizocheza.

    Zipo rekodi mbalimbali ambazo mpaka sasa zinaendelea kuwekwa lakini hapa tutazame wachezaji waliofunga mabao ya mapema zaidi katika msimu huu mwaka 2023/2024 katika ligi kuu Tanzania Bara (NBC Premier League).

    SOSPETER BAJANA :Anashikilia rekodi ya kufunga bao la mapema zaidi mpaka sasa msimu huu mwaka 2023/2024 akifunga goli sekunde ya 54 kwenye mchezo uliowakutanisha Azam Fc dhidi ya JKT Tanzania uliomalizika kwa AZAM Kushinda mabao 2:1.

    YASSIN MGAZA :Alifunga bao dakika ya kwanza tu ya mchezo kwenye mechi iliyowakutanisha Tabora United dhidi ya Dodoma Jiji mchezo ambao Tabora aliondoka na ushindi wa mabao 2:1 katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora.

    AWESU AWESU:Huyu ni kapteni wa wakusanya mapato wa Kinondoni ( KMC) alifunga goli dakika ya 1 tu kwenye mchezo uliowakutanisha KMC dhidi ya Mashujaa katika uwanja wa Uhuru. Matokeo yakiwapa faida Kmc wakiibuka na ushindi wa mabao 3:2.

    ZIDANE SERERI :Mchezaji huyu wa Dodoma Jiji alifunga goli kwenye mchezo uliowakutanisha Dodoma Jiji dhidi ya KMC katika uwanja wa Uhuru ambapo alifunga goli dakika ya 2 ya mchezo.

    FEISAL SALUM :FEITOTO alifunga goli dakika ya 2 ya mchezo katika mechi iliyowakutanisha AZAM dhidi ya Tabora United katika uwanja wa Azam Complex. Mchezo ambao ulimalizika kwa Azam kuondoka na ushindi wa mabao 4:0.

    PACOME ZOUZOUA :Zidane wa Ivory Coast kutoka kwa Wananchi alifunga bao la mapema zaidi katika mchezo ambao Yanga walipoteza kwa bao 2:1 kutoka kwa Ihefu katika uwanja wa Highland Estate. Pacome alifunga goli dakika ya 3 ya mchezo.

    KENNEDY MUSONDA :Alifunga goli dakika ya 3 ya mchezo uliowakutanisha watani wa jadi Simba dhidi ya Yanga katika Uwanja wa Benjamin Mkapa ulioisha kwa matokeo ya Yanga kuondoka na ushindi wa mabao 5:1.

    Soma zaidi kuhusu ligi kuu Tanzania Bara kwa kugusa hapa.

     

    ligi kuu
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.