Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Vita vya ‘Panzi’ Kupanda kwa Ligi Kuu Yanoga
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Vita vya ‘Panzi’ Kupanda kwa Ligi Kuu Yanoga

    David MohamedBy David MohamedMarch 31, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kutokana na mtifuano ulivyo baina ya Kitayosce na Pamba katika vita ya kupanda ligi kuu, huenda mikoa ya timu hizo ikakata kiu ya kuziona tena Simba na Yanga msimu ujao, huku Mashujaa FC nao wakichomoza.

    Pamba ya jijini Mwanza iliyowahi kutwaa ubingwa wa Kombe la Muungano mwaka 1999, kisha kushuka daraja mwaka 2000, haijarejea tena ligi kuu na sasa inajipapatua kufuta mzimu msimu ujao.

    Kitayosce ya mkoani Tabora wao ni msimu wa pili kushiriki Championship na imeonyesha nia ya kupanda ligi kuu baada ya mkoa huo kukosa burudani hiyo kwa zaidi ya misimu saba tangu Rhino Rangers waliposhuka msimu wa 2013/14. Kitayosce ipo nafasi ya pili kwa pointi 49 huku Pamba akifuata kwa 47 na Jumamosi hii wapinzani hao watakutana Uwanja wa Nyamagana.

    Kama haitoshi, nao Mashujaa wameonyesha uhitaji wa kucheza ligi kuu baada ya Kigoma kukosa uhondo huo na kufanya vita kuendelea kuwa nzito kupanda daraja baada ya kukusanya pointi 41, nafasi ya nne.

    Hadi sasa JKT Tanzania ndio wameingiza mguu mmoja ligi kuu baada ya kuwa na pointi 56, wakisaka alama sita tu kati ya michezo mitano iliyobaki.

    Pamba imebakiza michezo sita ikiwa ni dhidi ya Kitayosce, Mbuni, African Sports, JKT Tanzania na Fountain Gate, huku Kitayosce ikiwa na mechi tano dhidi ya wapinzani hao, JKT Tanzania, Fountain Gate, Mbuni na African Sports.

    Mashujaa wao wana michezo mitano wakianza dhidi ya Pamba, Fountain Gate, JKT Tanzania, African Sports na Mbuni FC ambazo zitaamua hatma ya timu hiyo kupanda au kubaki.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.