Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tunamkosea Heshima GSM Tuuzungumze Ukweli Tu
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Tunamkosea Heshima GSM Tuuzungumze Ukweli Tu

    MhaririBy MhaririFebruary 28, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    GSM
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Tujikite zaidi kwenye ukweli na tupunguze zile propaganda za soka, kwanini hatutaki kuuzungumza ukweli juu ya kufanikiwa kwa mfanyabiashara Ghalib Said Mohamed ‘GSM’ baada ya kuelekeza nguvu zake ndani ya Yanga SC.

    Kabla ya Ghalib kuingia Yanga, mkumbuke vizuri klabu hiyo ilikuwa kwenye mazingira yapi, ilikuwa kwenye hali mbaya ya kifedha timu ilikuwa ikihahaa kupata japo hata ule usafiri tu kufika kwenye michezo yake. Klabu hii ilifikia wakati wa kuchangishana na kuliita BAKULI la MCHONGO.

    Ghalib Said anaingia Yanga na kwenda kuyaondoa yote hayo sema tu tunapenda kusifia tuvipendavyo. GSM kukaa kwao hapo Yanga imeenda kubadilisha kila kitu, leo hii Yanga ni mabingwa wa Ligi Kuu mara mbili mfurulizo, Yanga ililipa kisasi cha mabao 5 kwZ mtani lakini kubwa zaidi ni kucheza fainali ya Kombe la Shirikisho.

    Yanga SC imecheza fainali ya Kombe la Shirikisho na kuifunga timu ngumu ya USM Alger nchini Algeria pamoja na kulikosa kombe Lakini alama imewekwa. Kama inasifiwa timu iliyocheza robo tatu za Ligi ya mabingwa, vipi Ghalib Said ambaye kuwepo kwake tu Yanga SC imeshaingia Robo fainali na pia inatazamiwa kuingia Nusu Fainali ya michuano hiyo mikubwa kwa ngazi za vilabu.

    Ukizungumza mambo kama haya watatokea Machawa Kisha kutumia account fake kuupondo ukweli huu. Katika ukweli tuseme kama aliwahi kusifiwa mtu kufanya vyema basi Ghalib Said Mohamed na watu wao nao tuwapongeze. Ukweli ni kwamba, GSM wameubadilisha mpira wameipa Yanga thamani ya KIMATAIFA hakuna asiyelijua hili.

    Wacha ninyamaze sema wale wasemaji wapunguza kauli za Mtaani kuja kutumika kwenye taasisi kubwa zilizojaa watu wenye heshima zao. Itakushusha hata kama umesoma mpaka level ipi ya Elimu, tuchunge ndimi zetu.

    SOMA ZAIDI: Karabaka Ni Dhahabu Iliyopo Simba Isiyotumika Vyema

    gsm yanga

    1 Comment

    1. Pingback: Freddy Anahitaji Msaikolojia, Ana Tatizo Hili Kubwa - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.