Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tanzania Tukubaliane Kuondoka Kwenye Mpira Wa Mdomoni
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Tanzania Tukubaliane Kuondoka Kwenye Mpira Wa Mdomoni

    MhaririBy MhaririMarch 22, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kwanza kama Tanzania, tunapaswa kujipongeza kwa ukuaji wa soka letu hakika mpira wetu umekuwa sana tujipige kifua katika hilo. Lakini wanasema kwenye kila ongezeko la maendeleo ndivyo na majaribu yanaongeza tusikatishwe tamaa tuyafanye kuwa mtaji.

    Vilabu vyetu vya Simba SC na Yanga SC vilikuwepo toka enzi na enzi, Yanga SC ikianza mwaka 1935 huku mwaka mmoja mbele Simba SC ikafuata mwaka 1936, itakuwa ngumu kusema hakuna Mtanzania ambaye hashabiki moja ya klabu hizo. Huyo atakuwa siyo mtu wa mpira pengine.

    Katika ukuaji wa soka lakini tusisahau na hii mitandao ya kijamii nayo inakua kwa kasi, ongezeko ni kubwa na watu wameendelea kutumia, shida siyo unaitumiaje ila unautumia vipi mtandao wa kijamii. Nimeanza kuona baadhi ya wadau wa soka kupitia huu utani wa Simba na Yanga wanataka kuingiza chuki kupitia mpira, zipo lugha zisizofaa na wengine wanapandikiza chuki za wazi wazi.

    Tuambiane kitu hapa kuwa duniani kote ukiona maendeleo ya mpira ujue nyuma yake wapo matajiri wamewekeza yaani wameingiza gharama zao kwamaana ya Pesa/Fedha Sasa itakuwa ngumu wewe mtu mmoja uje uvuruge hili.

    Kama tumekubaliana kuondoka kwenye mpira wa MDOMONI na kuuleta MGUUNI hakuna haja ya kuenezeana chuki ni ngumu kumvumilia binadamu wa namna hiyo. Tangu na tangu, enzi na enzi nchi yetu inasifika kuwa kisiwa cha amani kwahiyo hatutakubali kuona mtu mmoja anataka kuivuruga amani yetu, hapo hatuko tayari.

    Tumuogope mwanadamu ambaye yuko tayari kumkwamisha mwingine kwa maslahi yake binafsi au uchawa kazini ilimradi tu aonekane bora huku akiiteketeza familia ya mwingine.

    Narudia tena, Tanzania mpira unakua, Soka lanazidi kupaa juu kwaiyo tusikubali kuharibu tunu hii Kwa kuondekeza Uchawa ilimradi tu usifiwe na Boss halafu upige pesa MCHONGO. Hiyo siyo sawa.

    SOMA ZAIDI: Barua Kwa Waziri Ndumbaro Kuhusu Jezi Na Uzalendo

    FIFA SERIES 2024 Tanzania vs Bulgaria
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.