Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane 

“Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba kingine  ikisema 

“Safi” wakimaanisha kuwa vyumba vyao vipo salama hapo ndipo  Faudhia aliposhtuka kuwa anapaswa kuwa nje ya chumba haraka  sana ili awawahi Wanaume hao, alifanya hivyo upesi sana huku  akiwa ameelekeza Bastola yake mbele mahali ambako sauti hizo  zilitoka, wale wanaume hawakuisikia sauti ya tatu ya mwenzao  ndipo walipotoka nje haraka ila walikuwa wamechelewa,  walikutana na mishale ya risasi kutoka kwa Faudhia, Msichana  kutoka Mbeya, aliwamaliza kimya kimya bila kusikika popote  sababu bastola ilikuwa na kiwambo cha kuzuia sauti . ENDELEA 

SEHEMU YA NANE

Aliikumbuka vyema ile ramani, ramani ilisema kuwa kwenye  kordo hiyo mbele kwenye ukuta ndipo ulipo mlango wa kuelekea  ilipo chemba, alipoangalia ukuta huo aliona kulikuwa na  picha, aliifuata na kuifunua aliona kuna mlango mdogo wa siri  ambao ulifunikwa na picha hiyo kubwa yenye Msaafu, hapo  aligundua kuwa mpango huo wa kuiba pesa haukuwa rahisi kiasi  hicho. 

Ndani ya China Plaza, Mzee Shayo alizidi kuzama ndani kwa  kutumia ngazi, jengo lilikuwa refu kiasi chake na haikuwa  salama sana kwake kutumia Lifti. Alisogea taratibu tena kwa  umakini wa hali ya juu huku akitambuwa fika kuwa uzembe wa  aina yoyote utaondoa Maisha yake sababu watu hao ni hatari  sana.

Kabla hajafika Floo ya tatu alimuona Mlinzi wa kwanza ndani  ya jengo, alikuwa ametulizana akivuta sigara, alisogea kwa  umakini sana hadi alipomfikia, alimgusa bega la kulia  alipogeuka alimpa ngumi nzito eneo la pua, alimtuliza kwa  kumzimisha kisha alisonga mbele. 

Alikagua kila mahali, sehemu zingine alikuta familia  zilizokuwa zimejificha kwa woga aliwaambia muda wa ukombozi  umefika, alihakikisha anamfikia Mzee Shomari kwa mara ya pili  baada ya miaka mingi kupita, akiwa ameshafika floo za juu  kabisa alisikia sauti ya Mtoto akiwa analia, sauti hiyo  ilimkumbusha mbali sana alipokuwa mdogo wakati Nyumba yao  ilipokuwa inawaka moto na kuwateketeza Wazazi wake wote  wawili, wazo hilo lilimtoa kwenye lengo lililo mbele yake ile  anatahamaki alimuona adui mbele yake, alimchapa risasi,  kelele za Risasi ziliposikika ziliamsha hali za maadui zake  na kujuwa kuwa eneo hilo halikuwa salama. 

Yees!! Chogo alimfuata Selina na kumwambia 

“Pole sana kwa kila kilichotokea hapa, haikuwa nia yangu  kukufanyia vile bali upendo ulioniingia ghafla, natamani  kukuona ukitabasamu tena katika Maisha yako japo najuwa  itakuwa ngumu sana” Maneno ya Chogo yaliamsha mchozi na kilio  kwa Selina, alimwambia Chogo 

“Wewe siyo Binadamu, huna utu, hufai hata kusamehewa” Alisema  kwa hasira sana 

“Selina! Nakupenda sana, nahisi upendo wako kwenye damu  yangu, nazisikia punzi zako kwenye masikio yangu, kilio chako  ni huzuni kwangu! Unapaswa kupumzika” Alisema Chogo kisha  aliachia tabasamu lililomshangaza Selina, Chogo alipiga hatua  kadhaa ili kuondoka kisha alimgeukia Selina na Kumwambia  tutaonana siku moja, Chogo alifyatua risasi na kumuuwa Selina  akiwa juu ya Meza, haraka alikimbilia kwenye chemba ya siri  ambayo aliwaambia vijana wake atawakuta huko kisha safari yao  kuelekea Upanga ilianza. 

Ndani ya Chemba hiyo, Faudhia alikuwa akisogea kuelekea Benki  kuu wakati huo Chogo na vijana wake walikuwa wakielekea alipo  faudhia ambako ndiko iliko njia ya kuchomoka kwenye chemba  hiyo yenye giza. 

Chogo na vijana wake walikuwa na shahuku ya kuwa Mamilionea,  Faudhia alikuwa na shahuku ya kuhitimisha ugaidi huo. Muda  huo Mkuu mpya wa Kitengo cha Usalama wa Taifa alikuwa  akiwasiliana na Rais, kilichosubiriwa ni amri ya Rais  kuhakikisha wanaishambulia benki hiyo mara moja. Punde waliwaona Mateka waliokuwa ndani ya Benki hiyo wakikimbia  hovyo kuelekea nje, ilibidi wapeane taarifa kuwa wanapaswa  kwanza kuwa watulivu huku wakiwa makini na Mateka hao kuwa  huwenda wakawa wamechanganika na Magaidi. 

Iliwabidi wawahoji Mateka hao, walisema kile walichokiona  lakini kilichowaduwaza Askari ni namna mateka hao walivyosema  kuwa Watekaji walikuwa wameshaondoka, iliwalazimu kuingia  dani ya benki hiyo kwa utulivu na umakini wa hali ya juu  sana, walichunguza kila kona walikuta mwili wa Selina,  walimkuta Gavana akiwa hoi sana baada ya kuvuja kwa damu  nyingi, Mke wa Gavana alikuwa akilia sana kwa kuhisi Mume  wake angelikufa. 

Mkuu mpya wa kitengo cha Usalama wa Taifa alimwambia Rais  kuwa Huyo Selina ameshauawa, pesa zote zilikuwa zimeshaondoka  ndani ya Benki hiyo na haikujulikana magaidi walikuwa  wameondoka vipi eneo hilo kwani hata dalili tu kuwa  walichimba mahali haikuonekana, iliwapa maswali ya kujibu  Askari wa Kitengo na wale wa kawaida, walihangaika kujuwa  Magaidi hao waliondoka vipi ndani ya Benki hiyo, kumbe  walichofanya Magaidi hao ni kupita juu ya Siling Board na  kutokea chumba kingine ambacho kilikuwa cha siri sana ndani  ya benki hiyo kisha walichimba huko na kutengeneza njia hivyo  ukiingia kwa kawaida tu huwezi kuona japo alama kuwa  walichimba wapi, Naam!! Huyo ndiye Mzee Shomari aliyekuwa  akiratibu yote hayo na kusuka mipango ya hatari sana. 

“Mkuu hakuna mahali ambapo panaonesha hawa jamaa wametoka,  pengine wapo humu ndani wamecheza mchezo ili kuvuruga akili  zetu” alisema Mkuu mpya wa kitengo akiwa anazungumza na Rais 

“Inawezekana vipi Dinonga? Hicho ni kiasi kikubwa sana cha  pesa, hakikisha hawaondoki” Alisema Rais kwa sauti  iliyoashiria kuwa alikuwa amepagawa. 

Msako uliendelea ndani ya Benki kuu huku taarifa za habari  zikiendelea kuripoti tukio la kuwa huru kwa mateka waliokuwa  ndani ya Benki hiyo. 

Mzee Shayo akiwa amejibanza kwenye kona huku tayari akiwa  ameshaamsha akili za maadui zake ndani ya jengo la China  plaza, alijikuta akiwa anahema juu juu huku akili na moyo  wake ukizidi kumwambia kuwa kazi hiyo ni hatari sana. Mlango  ambao wale maadui walikuwa wakitokea ndiyo sehemu ambayo Mzee  Shomari alikuwemo. 

Mzee Shayo alifumba macho yake na kuibusu Bastola aliyoishika  mkononi, zaidi ya Wanaume sita walikuwa wakisogea mahali ambapo Mzee Shayo alikuwa amejificha tena wlaikuwa makini  sana baada ya kutambuwa kuwa Mtu huyo alikuwa hatari sana  kwao. 

Mzee Shayo aliutumia ufundi wake kwa kusoma milio ya hatua ya  maadui hao kisha akatambuwa namna walivyokuwa wamejipanga,  alihesabu 1,2,3,4,5,6 kisha alijitoa mafichoni kama chui  mwenye hasira 

Alifanya kama vila anakatisha kwenye korido kutoka ukuta  mmoja hadi mwingine huku akiwa amefumba macho yake, hisia  pekee ndizo zilizokuwa zikimuongoza, alifyetua risasi sita  ambazo aliamini zilikuwa ndiyo misumali ya kuwamaliza Maadui  hao, sauti za kuanguka zilisikika, Ndiyo!! Mzee Shayo  alifanikiwa kuwamaliza maadui hao sita kwa kutumia hisia zake  kali za Kijeshi. Alipofika ukuta mwingine alijipa muda wa  kuendelea kusikiliza tena lakini hakukuwa na sauti ya hatua  hata moja iliyokuwa ikisikika. 

Aliweka vizuri bastola yake kisha alichomoka kwa makini sana,  alisogea taratibu akiwa anaegemea ukuta huku Bastola yake  ikielekeza kwenye ule mlango ambao wale maadui walikuwa  wametokea, alipiga hatua 10 za Kijasusi hadi alipofika,  mlango ulikuwa wazi na hakukuonekana kuwa na dalili za kuwa  na Mtu kwenye chumba hicho, aliona chupa za vinywaji na  Michoro baadhi ya tukio walilokuwa wakilifanya 

Aliona ni bora azidi kupandisha juu ambako kulikuwa na hiyo  Helkopta ili kama Mzee Shomari anatoroka aweze kumnasa. 

Tuachane na Mzee Shayo, sasa turudi ndani ya Chemba ya  kusafirishia pesa, Chogo na Watu wake walizidi kuchanja  mbunga bila kujuwa kuwa Faudhia alikuwa akienda upande wao,  walipofika katikati ya safari yao Chogo aliwaambia vijana  wake watulie, alihisi ujio mbele yao, ni kweli Faudhia  alikuwa mbele yao, naye alihisi ujio wa Watu. Mkononi alikuwa  na Bastola huku Bastola nyingine akiwa ameiweka kiunoni,  alijiweka sawa huku Chogo na Watu wake wakijiweka sawa ili  kukabiliana na hatari iliyo mbele yao, eneo ambalo  liliwatenganisha Faudhia na Timu ya Chogo ni sehemu yenye  kona, Faudhia alizima tochi yake ili kuwe giza, upande wa  pili Chogo naye aliwaambia vijana wake wazime tochi zao.  Walivalia miwani ambazo ziliwasaidia kuona kwenye giza,  walikuwa wamejipanga huku kila mmoja akiwa na Begi moja lenye  pesa 

Chogo alituma Watu wawili wasogee mbele zaidi kuangalia  kulikuwa na nini, Faudhia alishashtuka aliweka sawa Bastola  yake ili awashambulie, walipojitokeza japo kulikuwa na giza 

Faudhia aliweza kucheza na hisia kama alivyofanya Mzee  Shomari na ndiyo yalikuwa mafunzo ya kupambana na adui pale  ambapo unahisi kwa macho ya kawaida huwezi kufanya hivyo,  alisikiliza hatua za Wanaume hao wawili akajuwa namna walivyo  kaa, wanaume hao walikuwa na AK47 mikononi mwao hivyo Faudhia  alipaswa kuwa makini zaidi, alifumba macho na kuinyanyua  bastola yake hadi usawa ambao aliona unafaa. 

Aliendelea kusikiliza hatua zao kisha alifyatua risasi mbili  kwa kutumia Bastola yake ambayo ilifungwa kiwambo, risasi  hizo zilifika kwenye paji la uso la kila mmoja, japo sauti ya  risasi haikutoka lakini sauti ya kuanguka kwao iliwashtua  Akina Chogo ambao haraka walianza kurusha risasi mbele,  Faudhia alijificha mahali huku ule mwanga wa zile risasi  ukimfanya aone watu aliowauwa kuwa walikuwa wamevalia miwani  za kuona wakati wa giza, baadaye risasi hizo zilikoma. 

Hakuna risasi iliyomfikia Faudhia kwenye mwili wake kwasababu  alikaa kwenye kona, alipoona ukimya umetawala alipiga  mahesabu ya kuichukua miwani, alitoa bastola zake mbili kisha  aliziweka sawa, alijichomoa na kuanza kurusha risasi kwa  lengo la kuwazuga huku haraka akichomoka na kufika zilipo  zile maiti mbili, alisogea kwa mmoja na kumvua ile miwani ila  bahati mbaya alipigwa risasi ya Bega, alijibu mapigo huku  akiokota AK47 kisha alirudi kujificha, alikuwa na maumivu  makali ya bega. 

Alichana kilemba kisha alijifunga kwenye bega kwa usaidizi wa  meno yake, alivalia miwani akawa anaona kama kwenye mwanga  vile, kisha aliiweka sawa AK47 kwa ajili ya majibizano ambayo  yalianza kuwashtua polisi walio ndani ya Benki huku  wakijiuliza risasi hizo zilikuwa zikitokea wapi, Chogo na  timu yake walijipanga vizuri, walikuwa kama Watu 11  waliobakia 

Faudhia alianza kutoka pale huku akisogea kwa tahadhari  kubwa, alikuwa na ujuzi wa kulenga hivyo ilikuwa kazi rahisi  sana kwake kukabiliana na Wanaume hao, alipochungulia aliona  miguu yao ikisogea, alilenga miguu ya Watu wawili akafyatua  risasi, walipoanguka aliwamaliza moja kwa moja na kufanya  idadi yao kupungua, Alizidi kuwamaliza kwa kuwavizia hadi  alipofanikiwa kuwabakiza maadui wanne tu, chogo akawaambia 

“Turudi ndani ya Benki” Alisema kisha waliokota mabegi  machache huku mengine yakiwa chini, waliona hawataweza  kukabiliana na Hatari hiyo huku wakishindwa kujuwa kuwa Mtu  huyo alikuwa peke yake au kilikuwa kikundi cha Watu.

“Benki itakuwa imeshavamiwa na askari” Alisema mmoja wa  vijana wake 

“Sasa tufanye nini, tusogee tukafe?, turudi ndani ya Benki”  Alisistiza Chogo, wakiwa wanarudi, Faudhia aliwatungua wawili  kati yao na kuwabakisha wawili ambao ni Chogo na mwenzake  mmoja, chini huko hakukuwa na mtandao labda angewasiliana na  Mzee Shomari na kumuomba msaada hata hivyo Mzee Shomari  mwenyewe alikuwa akijivuta na mguu wake mbovu kuifuata ilipo  Helkopta ili aweze kukimbia baada ya kuona Mambo hayapo sawa. 

Mzee Shayo alikuwa nyuma yake akiwa anakuja kwa kasi  kuhakikisha Mzee Shomari hachomoki, ilikuwa ni wahi nikuwahi,  kama siyo Mguu mbovu wa Mzee Shomari basi angelikuwa  ameshaifikia Helkopta, alifanikiwa kuufungua mlango wa mwisho  kisha Mtu mmoja alishuka kutoka kwenye Helkopta ili ampe  msaada Mzee Shomari, ghafla jamaa huyo alipigwa risasi ya  kichwa na Mzee Shayo ambaye alikuwa ameshafika eneo la  Mlango, kuona hivyo Mzee Shomari aligeuka akamwambia Mzee  Shayo 

“Ni bora uniache niondoke vinginevyo nitabonyeza hii rimoti  kwa ajili ya kutegua mabomu yote yaliyopo kwenye makambi ya  Jeshi Nchi nzima” Alisema Mzee Shomari, maneno yake yalileta  uzito kwa Mzee Shayo alifikiria afanye nini huku Mzee Shomari  akiwa anataka kubonyeza Kitufe 

“Sawa!! Nakuacha uwende” Alisema Mzee Shayo huku akiweka  silaha yake chini, Mzee Shomari alicheka sana kwa kuamini  kila jambo linaenda kuwa sawa, alimwambia Mzee Shayo 

“Itupe hiyo Bastola” Alisema kwa mkwara, Mzee Shayo aliiokota  na kuitupa chini ya ghorofa hilo, hapo Mzee Shomari aliamini  kuwa yupo salama kumbe nyuma ya Mgongo wa Mzee Shayo kulikuwa  na Bastola aliyoificha, Mzee Shomari alipogeuka ili apande  Helkopta alipigwa risasi nyingi mgongoni, hakuamini macho  yake, alitamani kubonyeza kitufe ili afe na Askari wengi  lakini nguvu ya kufanya hivyo ilimuisha hatimaye alianguka  chini, haraka Mzee Shayo alifyetua risasi kwa dereva wa  Helkopta ambaye alitaka kutoweka eneo hilo, alimpiga risasi  ya shingo na kusababisha Helkopta kuruka bila uelekeo maalum  hatimaye ilienda kuripuka kwenye kituo cha Mabasi ya mwendo  kasi eneo la Gerezani. 

Alishusha pumzi zake kisha alipiga magoti, kazi ilikuwa ngumu  sana kwake, alijikuta akicheka kwa maumivu makali ndani ya  nafsi yake, ngoma ilikuwa ngumu upande wa Faudhia ndani ya  Chemba ya pesa, Chogo alikuwa akirudi ndani ya Benki wakati  huo Faudhia akiwafuata kwa nyuma kuhakikisha hakuna atakayetoka salama eneo hilo, majibizano ya risasi  yaliendelea ndani ya chemba hiyo, polisi walio juu  walifanikiwa kufahamu kuwa risasi hizo zilikuwa zikifyatuliwa  chini kabisa ya Ardhi hivyo waligundua huenda Magaidi wapo  chini wanajibizana na askari wengine. 

Mkuu mpya wa Idara ya Usalama wa Taifa alimpa taarifa Mkuu wa  Nchi kwa kile kichokuwa kikiendelea huko Chini, Rais  alimwambia asikilizie ni jambo gani lilikuwa huko chini. 

Akina Chogo walijitahidi kukimbia kurudi ndani ya Benki  lakini Faudhia alikuwa makini kuwawinda, alimpiga risasi mtu  wa Chogo, iliamsha hasira sana kwa Chogo, alisimama kisha  aliokota AK47 kisha alianza kumimina risasi nyingi mfululizo  upande wa Faudhia, alifanikiwa kumfanya Faudhia alale chini  huku akijificha kwenye moja ya maiti, alipomimina risasi kwa  hasira hadi alipozimaliza, Faudhia alipojuwa kuwa alikuwa  amemaliza Risasi alisimama akiwa na bastola yake, alipiga  risasi moja mguuni kwa Chogo, alipiga nyingine kwenye bega la  chogo kisha alitaka kumaliza mchezo lakini Bastola yake  iliisha Risasi. 

Chogo alichomoka kama Mzimu, Faudhia hakuamini kuwa Mtu  aliyempiga risasi alikuwa akija kama Duma kwenye mbuga ya  wanyama, alimfika Faudhia eneo la tumbo na kuumtupa pembeni,  wote walikuwa na mawani maalum za kuona kwenye giza. 

Chogo alikuwa kama amepagawa hivi hakutegemea kama  angelikutana na upinzani wakati wa kupata kiasi hicho cha  pesa, alimvaa Faudhia na kuanza kumpa mvua ya ngumi ambazo  zilimrudisha tena Faudhia Chini, kabla hajakaa sawa  alishindiliwa na teke tumboni zaidi ya mara tatu haidi  alitema damu. 

“Nani amekutuma?” Aliuliza Chogo akiwa kama kichaa, alishusha  ngumi nyingine nzito kwa Faudhia na kumfanya azidi kutema  damu na kuishiwa nguvu, kisha alimuacha akiwa anahema juu juu  kama Mgonjwa wa presha, aliokota jiwe zito ili amshindilie  Faudhia lakini alisita kufanya hivyo kisha akamwambia 

“Nakuacha ufe taratibu” Chogo alilitupa jiwe hilo pembeni  kisha aliokota mabegi mawili yenye pesa na kuanza kuyaburuza  ili atoke nayo nje ya chemba. Japo Faudhia alikuwa katika  hali mbaya sana lakini alifikiria kama jamaa huyo  angeliondoka ndani ya Chemba hiyo ingekuwa kazi yote  aliyoifanya ni sawa na bure tuu. 

Alijivuta kwa kazi sana ili aokote AK47 ambayo ilikuwa kando  yake, Chogo alikuwa akizidi kusepa huku akiikaribia ile kona ambayo kama atazama hapo basi Faudhia atamkosa Chogo na jinsi  alivyo na hali mbaya asingeliweza kunyanyuka na kumfukuzia,  alifanikiwa kuikota kisha aliiweka sawa, alihema kwa nguvu  kisha alivuta hisia zake, akafyatua Risasi kuelekea kwa  Chogo, alikuwa na hisia kali sana na kufanikiwa kumpiga Chogo  kwenye kichwa, Chogo alienda Chini. 

Hali ya Faudhia haikuwa nzuri alikuwa akivuja damu nyingi  ndani ya Chemba hiyo yenye giza, aliona kama angeliendelea  kubakia hapo basi angelikufa kwa kukosa hewa na kuvuja damu  nyingi, Alijivuta kuelekea Benki ambayo ilikuwa na Askari na  hakukuwa na taarifa yoyote kuwa kulikuwa na Askari wa siri wa  kitengo aliyekuwa akifanya operesheni ndani ya Chemba hiyo,  Askari walikuwa tayari wamefanikiwa kuona mahali walipopita  akina Chogo yaani pale kwenye dali kabla ya kutokea kwenye  chumba cha siri ambacho walichimba hiyo chemba. 

Walianza kuhisi ujio wa Mtu kwenye Siling Board, Mkuu wa  kitengo alitoa maelekezo wafyatue risasi, Ooooh!! Risasi  zilifyetuliwa za kutosha hadi pale alipowaambia waache  kufanya hivyo, ukimya ulitawala kwa sekunde kadhaa kisha  waliona eneo hilo likibomoka, mwili wa Mtu ulianguka hadi  chini ya Sakafu, ulikuwa ni mwili wa Faudhia. 

Alikuwa akitema damu nyingi sana, muda huo huo aliingia Mzee  Shayo, alipoangalia vizuri alimuona Faudhia, alimuona  Msichana aliyemkuza kama Mtoto wake akiwa amelala chini ya  sakafu akiwa anatokwa na damu nyingi huku akiwa na matundu  mengi ya risasi 

“Faudhiaaaaa!!!” Aliita Mzee Shayo kwa uchungu wa hali ya juu  sana, alimkimbilia Faudhia 

“Faudhia! Faudhia Mwanangu!! Huyu ni Askari wa kitengo na  ndiye aliyekuwa akifanya operesheni hii kwa siri, mmeniulia  mwanangu” Alilia Mzee Shayo wakati Faudhia akiwa anahema kwa  shida sana, alifanikiwa kumuita Mzee Shayo 

“Ba….baaaa” Aliita na kukata kauli yake, Faudhia alifia  mikononi mwa Mzee Shayo, alilia sana Mzee Shayo, tena kwa  Uchungu mkubwa sana. 

“Nimekuponza Mwanangu!! Faudhiaaa, Faudhiaaaa”” alilia kwa  Uchungu, Mwili wa Faudhia ulichukuliwa kupelekwa Hospitali  kwa ajili ya Uchunguzi, Baadaye Mzee Shayo alitoa taarifa kwa  makambi ya Jeshi kuwa Mabomu yaliyotegwa humo yaliweza  kuzuiliwa, Jeshi lilitoka na kuhakikisha linakomboa Miji  iliyokuwa chini ya Kundi la ESS. 

BAADA YA WIKI MOJA.

Ndani ya Ndege ya Shirkika la Emirates, Mzee Shayo alikuwa  anasafiri kuelekea mapunzikoni baada ya kumfyeka Mzee Shomari  na kundi lake, mkononi alikuwa na picha ya Faudhia, aliibusu  kisha aliiweka Mfukoni. Aliitoa simu moja ambayo aliichukua  kutoka kwa Mzee Shomari, alitafakari jambo lililomshangaza  sana. 

Ndani ya simu ya gaidi Mzee Shomari kulikuwa na namba ya Rais  wa Nchi, na namba hiyo ilionekana kuwasiliana na Mzee Shomari  siku ya tukio tena kwa muda mrefu, aliwaza Rais alikuwa  akiongea nini na Mzee huyo? Alivuta punzi kisha alisema 

“Sitostaafu, nitahakikisha nagundua siri ambayo Rais  anaificha” Aliiweka simu hiyo ndani ya Mfuko kisha aliendelea  na safari yake ya kuelekea Brazil kupumzika. 

MWISHO.

IFUATE RIWAYA YA AINA GANI? MAPENZI , UJASUSI , UCHAWI au MAISHA?  COMMENTS ZIKIFIKA 100 Naachia Kesho MAPEMA SANA

JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

 

28 Comments

  1. UJASUSI IS ALWAYS THE BEST ASEEE….
    BRING BACK 🔙 AGAIN LAKINI IWE MICH BETTER THAN THAT 🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽

Leave A Reply

Exit mobile version