Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Ratiba Kamili Ya FIFA CLUB WORLD CUP 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nne-04)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tatu-03)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tatu-03)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tatu-03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 29, 2025Updated:May 30, 202516 Comments10 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Sehemu Ya Pili

    “Kazi imeisha!” Alisema Diana kwa njia ya simuย 

    “Waoo Good Girl ( Vizuri Msichana mzuri ) ” ilisikika sautiย  nzito ya kizeeย 

    “Rudi Tanzania” Alimalizia kusema Mwanaume huyo kwa njia yaย  simu, simu hiyo ilikatika, tayali polisi walishafika nje yaย  Hoteli hiyo, Diana alichofanya ni kuingia kwenye chemba yaย  maji machafu akaenda kutokea mbali na eneo hilo.ย  Endeleaย ย 

    SEHEMU YA TATUย 

    Tayali ilifahamika ni wapi ambapo Faudhia angepatikana niย  mpaka wa Namanga, ilihitaji auawe kabla hajafika Tanzania.ย 

    Mishale ya saa 11 Alfajiri vijana wa Khalid Bangalaย  walijaribu kumtafuta Bosi wao bila mafanikio, hawakujuwaย  wafanye nini sababu maelekezo yote walikuwa wakipewa na Bosiย  wao ambaye alikuwa ameshauawa Hotelini, majadiliano yaoย  yalimuamsha Faudhia akiwa ndani ya Sanduku.ย 

    “Unafikiri tutafanya nini, Simu ya Khalid haipatikani,ย  tufanyaje na tunakaribia eneo lenye askari” Alisema mmoja waย  Vijana hao, Faudhia aliposikia hivi alihisi kuna hatari,ย  kutokana na mafunzo aliyoyapitia aligundua pengine kuna jamboย  halipo sawa, aligonga afunguliwe huku akisema amebanwa sanaย  na Haja. Vijana hao walisimamisha gari hilo, walikuwa juu yaย  mlima, kulikuwa kunapambazuka na iliwahitaji kutembea chiniย  ya Kilometa 15 kufika Mpakani. Faudhia hakutaka kujioneshaย  kuwa amehisi jambo lisilo la kawaida, hakutaka kuwaamini mojaย  kwa moja, walikuwa na bunduki ambazo walizificha, mmojaย  alimsindikiza Faudhia kujisaidia huku akiwa amemshikiliaย  Bunduki kwasababu alikuwa bado hajawalipaย 

    “Pale ni wapi?” Alihoji Faudhia akiwa anazidi kusogea sehemuย  ya kujisaidiaย 

    “Longido” alijibu Mwanaume huyoย 

    “Unamaanisha Tanzania?”ย 

    “Ndio, unapaswa kutulipa kwanza sababu umeshafika eneo husikaย  ambalo sisi hatuwezi kusogea huko, kuna ulinzi wa Askari waย  mpakani.” Alisema Mwanume huyo

    “Simama hapo basi au unataka kunichungulia!” Aliuliza Faudhiaย  na kumfanya Mwanaume huyo asimame lakini akiwa anamuoneshaย  Bunduki Faudhia ambaye alikuwa tayali ameashaanza kujisaidia.ย 

    Akiwa anajisaidia alisikia milio ya Risasi za haraka kishaย  ukimya ulitanda, yule aliyemsindikiza alirudi kule harakaย  akakuta wenzake tayari wameuawa, lilikuwepo kundi la watuย  tano ambalo lilitokea msituni na kumtaka Mwanaume huyoย  anyanyue mikono yake juu. Wanaume hao walikuwa wakiongeaย  rafudhi ya Kenya, haraka Faudhia alifungua kibegi chakeย  kidogo akatoa bastola yake, ukimya ulitawala, Faudhiaย  alijaribu kuchungulia eneo la tukio ndipo alipowaona Wanaumeย  hao, haraka alizama kwenye kichakaย 

    “Msichana yupo wapi?” Alihoji mmoja wa Watu hao huku akiwaย  amenyooshea bastola yule kijana wa Khalid aliyebakia, yuleย  Mwanaume hakuwa na chaguo ilibidi aoneshe mahali ambapoย  Faudhia alikuwa ameingia kwa ajili ya kujisaidia, alipigwaย  risasi yule Mwanaume kisha lile kundi liliongoza mahaliย  ambapo Faudhia alikuwa ameingia, ilikuwa inakaribia saa 12ย  asubuhi, kulishaanza kupambazuka.ย 

    Faudhia alishajuwa hali ya hatari ilikuwa imenukia eneo hilo,ย  alichofanya ni kuanza kukimbia kuelekea mpaka wa Namangaย  upande wa kaskazini ambako ndipo ilipo Wilaya ya Longido,ย  alikuwa na maelekezo maalum ya eneo gani anapaswa kupitaย  ambalo litakuwa salama lakini kutokana na milio ya Risasiย  kusikika iliwashtua askari wa mpakani wakatoka kwa ajili yaย  kuangalia kulikuwa na tatizo gani.ย 

    “Yule pale” Alisema kiongozi wa kundi hilo la Watu watano,ย  walipewa amri ya kumuuwa Faudhia kutoka kwa Mtu ambayeย  hakujulikana hadi kufikia wakati huo, ila Faudhia alijuwa niย  kwanini Watu hao walikuwa wakimfuatilia ila hakujua wametumwaย  na nani.ย 

    Milio ya Risasi iliendelea kurindima msituni hapo, Faudhiaย  alijitahidi kukimbia ili kuokoa Maisha yake. Ulikuwa niย  mtafutano wa zaidi ya dakika 10 bila mafanikio kwa Wanaume waย  kundi hilo kumpata Faudhia ambaye alishahitimu mafunzo yaย  ujasusi huko Mexico, Faudhia alifuata maelekezo maalum iliย  aonane na Mtu mwenye gari msituni hapo, bahati mbaya akiwaย  anakaribia alikutana na Askari wa mpakani ambao walikuwaย  wakifuatilia milio ya Risasi, Faudhia alisimama kwa sekundeย  kadhaa huku akiwa anatazama na Askari hao ambao walikuwaย  mbele yake Mita kadhaa tuu kutokea aliposimama, pumzi zaย  Faudhia zilimwambia kuwa hatuna jinsi bali kufa auย  kujikamatisha mikononi mwa Askari hao.

    “Weka silaha yako chini” Alisema mmoja wa Askari hao, Kilaย  hesabu aliyokuwa anaipiga Faudhia haikumpa jibu linalotakiwa,ย  alijikuta akijisalimisha mwenyewe, Askari walianza kusogeaย  taratibu kwa makini sana eneo ambalo Faudhia alikuwaย  amesimama, wale wanaume wa kundi la Kigaidi hawakujua kuwaย  Faudhia alikuwa amesimama mbele ya kundi la Askari polisi,ย  walitokea eneo hilo na kushtukizwa na askari polisi kishaย  mashambulizi ya Risasi yalianza kusikika huku haraka Faudhiaย  akichumpa na kujitupa kwenye poromoko dogo, Milio ya Risasiย  iliendelea kusikika lakini haikufamfanya Faudhia asimame walaย  arudi nyuma, alizidi kusonga mbele hadi alipofika mpaka waย  Namanga, alivuka na kuingia Tanzania.ย 

    Mashambulizi baina ya Askari polisi wa mpakani na Lile kundiย  yaliendelea na kumpa uhuru Faudhia kukutana na Mtuย  aliyepangiwa kukutana naye mpakani hapoย 

    “Ingia kwenye gari haraka tuondoke eneo hili” alisemaย  Mwanaume mmoja ambaye ndiye aliyetakiwa kumchukua Faudhiaย  mpakani na kumfikisha Arusha Mjini, Faudhia aliingia ndani yaย  gari na safari ilianza kuelekea Arusha Mjini.ย 

    โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขย 

    Jeshi la polisi liliizunguka Benki kuu ( B.O.T ) iliย  kuhakikisha hakuna anayetoka humo benki, ndani ya Benki hiyoย  alikuwepo Mtu hatari aliyeitwa Chogo, tayari alikuwa amemtekaย  Mke wa Gavana na Gavana mwenyewe ambao wote walikutwa ndaniย  ya Benki hiyo, nje ya Benki zilionekana maiti za Askariย  kadhaa ambao walikuwa wakitaka kufanya jaribio laย  kushambuliana na Magaidi hao ambao walionekana kuzungumzaย  kiswahili kizuri, ilikuwa ni mishale ya saa 1 asubuhi juaย  lilikuwa likichomoza, ukimya uliendelea kutawala na hakukuwaย  na Raia aliyekuwa akifanya safari. Muda huo huo Mzee Shayoย  aliwasili akiwa na gari yake, alikutana na Mkuu wa operesheniย  hiyo aliyeitwa Sir Jeff, waliitana chemba kwa ajili yaย  mazungumzo, wote walionekana kuanza kukata tamaa kwa jinsiย  Magaidi hao walivyokuwa na mbinu kali za kukabiliana naย  Askari.ย 

    “Niambie mpango unaendaje?” Aliuliza Mzee Shayo hukuย  akitazama saa yakeย 

    “Gavana na Mke wake wameshikiliwa ndani ya Benki” alijibu Sirย  Jeff akiwa anamtazama Mzee Shayoย 

    “Hawajasema wanataka nini?” Aliuliza tena Mzee Shayo

    “Hakuna hata mmoja aliyezungumza hadi hivi sasa zaidi yaย  ishara tu kupitia kioo kikubwa”ย 

    “Shenzi sana!!” alisema Mzee Shayo, punde simu yake iliita,ย  alipoangalia aliona ni Faudhia alikuwa akimpigia kwa njia yaย  Whatssap, alisogea pembeni kuipokea sababu hakutakaย  kunshirikisha yeyote juu ya Ujio wa Faudhiaย 

    “Baba!! Nipo Arusha” Alisema Faudhia, hivi ndivyo ambavyoย  Faudhia alikuwa akimchukulia Mzee Shayo, alimchukulia kamaย  Baba yake mzazi baada ya kumsaidia kumtoa kwenye mikonoย  hatari ya Mzee Shomari miaka mingi iliyopitaย 

    “Sawa Faudhia! Nakutumia picha, nataka uchunguze huyo Mtuย  anafahamika vipi hapo Arusha, ndiye mshukiwa namba Moja waย  tukio hili la Ugaidi” Alisema Mzee Shayo kisha alimtumiaย  picha Faudhia, ilikuwa ni picha ya Martin Gimbo ambayeย  alijitambulisha kwa askari kama Chogo. Mara moja Faudhiaย  alianza kazi ndani ya Jiji la Arusha. Mfumo wa serikaliย  ulishawekwa kwenye kiganja cha Faudhia, alitumia kompyutaย  mpakato ambayo alitumiwa na Mzee Shayo kupitia jamaaย  aliyemchukua pale Mpakani, kompyuta hiyo ilikuwa naย  mawasiliano na Kitengo cha Usalama wa Taifa, muda huo Faudhiaย  alikuwa Hotelini akiifanya kazi hiyoย 

    Aliingiza picha kwenye mtandao wa Idara ya Usalama wa Taifa,ย  alimuona jamaa huyo aliyeitwa Martin Gimbo. Taarifa za Jamaaย  huyo zilionesha kuwa alizaliwa Arusha Mjini, aliona ni wapiย  alisoma hivyo ilikuwa ni kazi rahisi kwa Faudhia, juaย  lilikuwa limeshaweka makazi katika anga kwa ajili yaย  kuimulika Dunia, Faudhia aliutumia usafiri wa gari waliyotokaย  nayo mpakani akiwa na jamaa aliyeitwa Mohd, walienda kwenyeย  shule ambayo waliona kuwa Martin Gimbo alisoma, bahati nzuriย  ilikuwa ni siku ya Shule, waliingia hadi ofisi ya Mwalimuย  Mkuu, walienda shule ya Sekondari ambapo waliamini taarifa zaย  Martin zingepatikana.ย 

    Walikaribishwa na Mwalimu mkuu wa shule hiyo ambaye mudaย  mchache baadaye aliketi kuwasikiliza huku akionekanaย  kuzishangaa sura za akina Faudhiaย 

    “Naitwa Undercover Mohd kutoka kitengo cha Usalama wa Taifa”ย  alijitambulisha yule jamaa huku Faudhia akiwa kimya, Mohdย  alitoa kitambulisho ili kumuaminisha Mwalimu huyo ambayeย  alikuwa akitetemeka kutokana na woga sababu taarifa za ugaidiย  zilizizima katika Miji mikuu ya Dodoma na Dar-es-salaam.ย  Baada ya kujiridhisha Mwalimu huyo alishusha pumzi zake kishaย  aliondoa mawani

    “Haikuwa rahisi kuwaamini sababu Wanafunzi na Waalimuย  wameanza kukimbia Mji huu kwasababu ya uvumi kuwa baada yaย  Dodoma na Dar utafuata Mji huu kuwa chini ya Magaidi” alisemaย  Mwalimu huyo kisha alishushia maji yaliyo ndani ya chupa,ย  alionekana kuwa na mengi ya kusema, alinyanyuka na kwendaย  kufunga mlango kisha ndani kukawa giza aliwasha taaย 

    “Niwasaidie nini vijana?” Aliuliza Mwalimu huyo ambayeย  alikuwa na mvi kiasi kuashiria kuwa umri wake ulikuwaย  umeenda. Faudhia alitoa picha ya Chogo akamuonesha Mwalimuย  huyo, Mwalimu aliichukua picha hiyo kisha aliisogeza kwenyeย  Mwanga, alishtuka baada ya kumuona chogo kisha alimpatiaย  picha Faudhiaย 

    “Unamfahamu huyo Mtu?” Alihoji Mohdย 

    “Hapana” Alijibu Mwalimu baada ya kukaa kimya kwa sekundeย  kadhaaย 

    “Mwalimu, ukweli wako utaliweka Taifa hili huru. Sura yakoย  inaonesha unamfahamu, tuambie anaishi wapi na unamfahamuย  vipi?” Alidakia Faudhiaย 

    “Nimesema simjui mnanilazimisha ili iweje? Simjui huyo Mtuย  hebu nendeni” alisema Mwalimu kwa hasira huku akifoka mithiriย  ya chatu aliyejeruhiwaย 

    “Unamjuwa huyu Mtu ndio maana unajaribu kuficha, Mwalimuย  tuambie huyu Mtu anaishi wapi na unamfahamu vipi?” Alisemaย  Mohd kwa sauti iliyokaukaย 

    “Nimesema simjui, hebu ondokeni ofisini kwangu haraka sana”ย  Alisema Mwalimu kwa sauti ile ile huku akinyanyuka kitiniย  mfano wa Mtu aliyetaka kuondoka ofisini hapo, Faudhiaย  alichomoa bastola na kumuonesha Mwalimu huyo.ย 

    Bastola ilimfanya Mwalimu anywee kidogoย 

    “Endapo utaendelea kukanusha nitapasua ubongo wako sasa hivi,ย  unamjuwa huyu Mtu anaitwa Martin Gimbo. Alisoma hapa kwaย  miaka minne” Alisema Faudhia akiwa amemshikilia Bastolaย  Mwalimu,ย 

    “Sisi siyo Watu wabaya ila unatulazimisha kufanya huo ubaya,ย  kama hutaki kusema hebu tupatie faili la Martin” Alisema Mohdย 

    Mwalimu hakuwa na neno jasho lilikuwa likimtiririka, alivutaย  droo la meza alitoa faili lenye maelezo yanayomuhusu Martinย  Gimbo, Faudhia alipolifunua Faili hilo, halikuwa na picha yaย 

    Martin, halikuwa na maelezo kuwa Martin alikuwa akiishiย  sehemu ganiย 

    “Taarifa zimeenda wapi?” Alihoji Faudhiaย 

    “Msijaribu kulifuatilia hilo jambo, hamtafanikiwa nawaambia,ย  mtakufa kabla ya kujuwa chochote kile” Alisema Mwalimu huyoย 

    “Ona hii” Alisema Mohd baada ya kuangalia kwa makini walionaย  namba ya simu nyuma ya faili hilo, ilibidi walichukue failiย  hilo, Mohd alichukua bastola na kumpiga mwalimu huyo.ย 

    “Kwanini unauwa?” Alihoji Faudhiaย 

    “Hana faida yoyote” Alisema Mohdย 

    “Tuondoke haraka sana” Aliongeza Mohd kisha waliingia ndaniย  ya gari na kutoweka eneo hilo, wakiwa ndani ya gari waliipigaย  namba hiyo, ilipokelewa na Mwanamke mwenye sauti dhaifu sana,ย  ilionekana alikuwa mgonjwa maana alikuwa akikohoa sanaย 

    Faudhia aliutumia ujanja wa mafunzo yake, walielekezwa alipoย  mpokeaji wa simu hiyo, walienda kuonana naye lakini njianiย  Faudhia alijiuliza Kwanini Mohd alimuuwa Mwalimu Mkuu baadaย  ya kuyatamka maneno yale? Hakutaka kuyapa kipaumbele,ย  walisogea hadi eneo husika, walikutana na Mama mmoja dhaifuย  sana wa mwili wake, alikuwa akiishi na Mjukuu wake wa miakaย  16ย 

    Walimsalimia Mama huyo kisha walimuulizaย 

    “Hapa ni nyumbani kwa Martin Gimbo?” Alipouliza hivi huyoย  Mama alipata nguvu hata ya kukaa, Mjukuu wake alishangaa sanaย  kwa Mama huyo kuketi mwenyewe wakati mara zote alikuwaย  akimsaidia kukaa, Mama huyo alikaa kimya sanaย 

    “Je? Wewe ni Mama yake Martin?” Alihoji Faudhia, Mama huyoย  aliwatazama kisha aliwaulizaย 

    “Mnamuulizia Martin Gimbo?” Aliuliza kama vile Mtu aliyetakaย  kupata uthibitisho wa alichokisikiaย 

    “Ndio, Martin Gimbo, unamfahamu?” Alihoji Mohdย 

    “Ndio, ni Mwanangu! Miaka mingi sasa tangia Martinย  alipofariki kwa ajali ya gari akiwa anaelekea Mjini, tanguย  siku hiyo sikuwahi kuamka na kukaa tena hata ongea yanguย  ilikuwa ya shida, Martin alikuwa ndiyo Mwanangu wa pekeeย  niliyempenda, tumaini la Maisha yangu lilikuwa kwa Kijanaย wangu Martin baada ya Baba yake kufukiwa na kifusi hukoย  Merelani akiwa anafanya kazi za mgodi” Alisema Mama huyo,ย  kisha alimuomba Mjukuu wake amsindikize mahali.ย 

    “Nifuateni” Alisema Mama huyo ambaye alijitambulisha kamaย  Mama yake Martin Gimbo ambaye alikuwa akitajwa kama gaidiย  kiongozi wa kundi la ESS .

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NNE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni soma riwaya bure

    16 Comments

    1. Ariel4453 on May 29, 2025 10:20 am

      https://shorturl.fm/m8ueY

      Reply
    2. Luccah on May 29, 2025 12:43 pm

      Hii Ik0 0n ๐Ÿ”ฅ

      Reply
      • Edifons on May 29, 2025 11:37 pm

        Noma sana

        Reply
    3. Adam on May 29, 2025 1:09 pm

      Inakuja Kwa Wakati Saana Jamani Hadi Raha Ahsante Admn

      Reply
    4. KingzJeelay on May 29, 2025 2:33 pm

      Wanaenda kufanywa nn… Kama ye ndo mkuu wa kitengo ๐Ÿ™†๐Ÿฝโ€โ™‚๏ธ๐Ÿ™†๐Ÿฝโ€โ™‚๏ธ๐Ÿ™†๐Ÿฝโ€โ™‚๏ธ๐Ÿฅฑ๐Ÿฅฑ

      Reply
    5. Octavian on May 29, 2025 4:09 pm

      Tupe nyingine admin

      Reply
    6. VERONICA on May 29, 2025 5:27 pm

      Nzuri sana Admin

      Reply
    7. Maestro05 on May 29, 2025 9:10 pm

      Hii ya Moto Sana Admin

      Reply
    8. Gervase on May 29, 2025 11:50 pm

      Mama anajambo lake,๐Ÿค“ admin tunahitaji mwendelezo kwa wakati tafadhal,,,simulizi nzuri sana๐Ÿ‘

      Reply
    9. Tyler2934 on May 30, 2025 6:42 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    10. Wilson4781 on May 30, 2025 11:11 am

      https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    11. Gilbert66 on May 30, 2025 11:44 am

      https://shorturl.fm/9fnIC

      Reply
    12. Alan2244 on May 30, 2025 1:26 pm

      https://shorturl.fm/6539m

      Reply
    13. Francisco4352 on May 31, 2025 6:04 pm

      https://shorturl.fm/xlGWd

      Reply
    14. Gilbert914 on June 1, 2025 1:22 am

      https://shorturl.fm/f4TEQ

      Reply
    15. Will4832 on June 1, 2025 3:11 am

      https://shorturl.fm/nqe5E

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Kombe la Dunia May 31, 2025

    Ratiba Kamili Ya FIFA CLUB WORLD CUP 2025

    Hii hapa ratiba ya mechi za Kombe la Dunia la Klabu la FIFA 2025 ambapo…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nne-04)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tatu-03)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Pili-02)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.