Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJune 3, 2025Updated:June 4, 202527 Comments21 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nneΒ 

    “Assssh” aligumia Faudhia kutokana na maumivu ya kujigongaΒ  kwenye meza, Mohd hakutaka kusubiri alimrushia ngumiΒ  mfululizo, ngumi ambazo zilimpekeka Fuadhia ukutani, bahatiΒ  mbaya ngumi nyingi zilimpata na kumfanya aumie usoniΒ 

    Mohd alimpiga Faudhia mateke mfululizo eneo la mbavu hukuΒ  akimwambiaΒ 

    “Unakufa leo” Alisema huku akiwa anamuangalia Faudhia akiwaΒ  anaanguka chini. Endelea

    SEHEMU YA SITA

    Mohd alimsindikiza Faudhia kwa teke kali lililomzimishaΒ  Faudhia, Mohd alitoa kifaa kidogo ambacho kilikuwa na sindanoΒ  ya sumu ndani yake, aliitoa kisha alimkita Faudhia eneo laΒ  shingo.Β 

    Baada ya kuhakikisha amemdunga alielekea Kuvuta kochi kishaΒ  aliitafuta simu yake ambayo ndiyo ilikuwa muhimu sana kishaΒ  Bastola yake ambayo ingekuja kuwa ushahidi pale, aliichukuaΒ  Bastola na simu kisha aliondoka eneo hilo.Β 

    Sekunde kumi na tano baadaye sindano ya sumu ilianza kufanyaΒ  kazi yake, Faudhia alishtuka huku akiwa anateswa na sumuΒ  ambayo ilikuwa ikisambaa kwa kasi mwilini, alijikuta akianzaΒ  kuishiwa nguvu, alijivuta kisha alifungua kibegi chake kidogoΒ  alitoa sindano, alivuta dawa haraka kutoka kwenye chupaΒ  kidogo kisha alijidunga sindano akiwa anavuja damu, kishaΒ  alianguka chini na kuzima.Β 

    Usiku huo, Mzee Shomari alikuwa akisubiria simu ya Mohd iliΒ  kumpa taarifa ya kifo cha Faudhia. Alikuwa kwnye kiti chaΒ  walemavu akitembea sebleni ndani ya Jengo la China plazaΒ  jengo ambalo walilifanya kuwa makao yao ya siri walipoanzaΒ  kupanga mipango ya Kigaidi, jengo hilo lilikuwa la rafikiΒ  yake aliyeko Uholanzi ambaye ndiye aliyekuwa anafadhiliΒ  ugaidi.Β 

    Alianza kukumbuka miaka mingi iliyopita katika Jiji la Mbeya.Β 

    Siku ambayo alikamatwa Baada ya kumuuwa Mama yake Diana,Β  alimtazama kwa hasira sana Faudhia, alijenga chuki na kisasiΒ  kwa Faudhia. Mzee Shomari alipelekwa Kituo cha polisi,Β  alipewa mateso makali sana ikiwemo kuwekwa kwenye beseniΒ  lenye maji na kukosa pumzi, alikumbuka jinsi alivyopigwa hadiΒ  kuvunjwa mguu na ndiyo sababu ya yeye kuwa mlamavu ndiyoΒ  maana anatembea kwenye kiti cha walemavu.Β 

    Alipelekwa mahakamani baada ya kupata matibabu ya mguu kishaΒ  alihukumiwa kifungo cha Maisha jela, alipofika huko alikutanaΒ  na mzungu aliyeitwa Damian, alijenga urafiki na Mzungu huyoΒ  ambaye alikuwa na kesi ya kusafirisha madini kinyume chaΒ  sheria kutoka Tanzania kwenda Thailand, walishibana wakiwaΒ  gerezani.Β 

    Akiwa anaendelea kuwaza kilichotokea baada ya kufungwa, simuΒ  ya Mzee Shomari iliita alipopokea alisikia sauti ya MohdΒ  ikimwambiaΒ 

    “Faudhia ni damu baridi” Alisema akiwa na maana kuwaΒ  ameshamuuwa, Mzee Shomari alishangaa sana kwa jinsi ambavyoΒ  alimuuwa Faudhia kisha alimuuliza

    “Upo wapi?”Β 

    “Nipo njiani narudi Dar” Alisema MohdΒ 

    “Tukio lilikuwaje?” Alihoji Mzee Shomari kwa unakini mkubwaΒ  huku akionekana alikuwa mwenye akili sanaΒ 

    Mohd alimsimulia Mzee Shomari tukio lilivyotokea kisha MzeeΒ  Shomari alisemaΒ 

    “Ukifika Chalinze utaona kuna prado nyeusi, itumie” AlisemaΒ  Mzee Shomari kisha alikata simu. Alisogea na kutazama chini,Β  aliliona namna jiji la Dar lilivyokuwa likiwaka taa hukuΒ  barabara ya kutoka Karume kwenda Kariakoo ikiwa nyeupe hakunaΒ  Mtu wala gariΒ 

    Alinyanyua simu yake akapiga simu mahali kisha akasemaΒ 

    “Case Clossed ( Kesi imeisha ) ” alikata simu akajisukuma naΒ  kuingia kwenye chumba kingine.Β 

    Masaa matano baadaye Mohd alifika Chalinze usiku sana akiwaΒ  na gari yake aina ya Toyota V8, mji ulikuwa kimya kabisa,Β  alilliona Prado likiwa linawasha hazard kuashiria kuwaΒ  lilikuwa ndiyo gari ambalo Mohd alitakiwa kulitumia, harakaΒ  alishuka na kulielekea gari hilo, alipoingia aliangaza ndaniΒ  ya gari hilo ili kuona kama kulikuwa na Mtu lakini gari hiloΒ  halikuwa na Mtu, alivuta funguo na kuiwasha, kitendo chaΒ  kuwasha tu gari hilo lililipuka, Mohd alifia ndani ya gariΒ  hilo, pembezoni kulikuwa na roli, ndani ya Roli kulikuwa naΒ  Mtu ambaye alisikika akiongea na simu akisemaΒ 

    “Target eliminated ( Mlengwa amemalizwa )” kisha roli hiloΒ  liliwashwa na kueleka Upande wa morogoro.Β 

    Siku iliyofuata, Chogo alipewa kazi na Mzee Shomari yaΒ  kuhakikisha anaifahamu ilipo chemba ya siri ambayo pesa hizoΒ  za Kimarekani zilikuwa zimehifadhiwa, Mtu pekee ambayeΒ  alidhaniwa kuwa anajuwa ilipo alikuwa ni Gavana wa BenkiΒ  hiyo. Pesa ambazo akina Chogo walikuwa wanazitaka zilikuwa niΒ  pesa za siri ambazo Tanzania iliyauzia madini Nchi ya SaudiΒ  Arabia. Chogo alirudi ndani ya chumba ambacho GavanaΒ  alikuwemo na Mke wake, alikuwa ameweka rehani maisha ya mmojaΒ  wa wafanyakazi wa Benki hiyo ili Gavana aseme mahali ambapoΒ  pesa hizo zilikuwa zimehifadhiwa.Β 

    Gavana alimuuliza Chogo amajuwaje kama ndani ya Benki kunaΒ  pesa za siri ambazo zilitokana na mauzo ya madini

    “Acha kuuliza maswali ambayo kamwe hutoweza kupata majibuΒ  yake, sema ilipo chemba ya siri vinginevyo namuuwa huyu!!”Β  Alisema Chogo huku Bastola ikiwa kichwani kwa Mfanyakazi huyoΒ 

    Gavana alikaa kimya hakuonekana kumtetea Mfanyakazi asiuawe,Β  alimtazama Mke wake kisha alirudisha macho kwa chogo.Β 

    “Umejuwaje?” Aliuliza tena kwa mshangao mkubwa sana, ChogoΒ  alionekana kuwa ni Mtu katili mwenye hasira sana, alimpigaΒ  risasi mfanyakazi kisha akamwambia GavanaΒ 

    “Nakupa masaa matatu uoneshe ilipo chemba ya siri” ChogoΒ  alisema kisha aliondoka ndani ya chumba hicho.Β 

    Upande wa pili, Mzee Shayo alianza kuingiwa na wasiwasiΒ  kuhusu vijana wake wawili aliowatumainia, simu ya MohdΒ  haikupatikana baada ya kuuawa ndani ya gari, simu ya FaudhiaΒ  iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa, ilimpa mashaka juu yaΒ  usalama wao, alijitahidi sana kupiga simu lakini simu yakeΒ  haikuweza kumpa majibu ya nini kilichokuwa kimetokea hukoΒ  Arusha kwenye operesheni ya kujuwa kuhusu Chogo, alitumaΒ  Askari wengine wa Kitengo kuelekea Arusha kwa ajili yaΒ  kuwatafuta Mohd na Faudhia.Β 

    Punde alipokea simu ya Rais iliyomtaka aende Ikulu harakaΒ  sana, kutoka Kigamboni yalipo makao makuu ya Kitengo cha siriΒ  cha Usalama wa Taifa ilimchukua dakika kadhaa, tayali hali yaΒ  tahadhari ilitangazwa hivyo hakukutakiwa Mtu yeyote kutokaΒ  ndani, Jiji lilikuwa kimya sana kama makazi yaliyotelekezwa,Β  Mzee Shayo alifika hadi Ikulu kisha alienda kwenye chumba chaΒ  siri ambacho Rais na Waziri Mkuu walikuwa wamehifadhiwa.Β 

    Rais alihitaji kujuwa Mzee Shayo alifikia wapi katikaΒ  harakati za kupambana na Kikosi hicho cha Kigaidi, waliketiΒ  watu watatu na kuanza kuzungumza, Mzee Shayo alimwambia RaisΒ  kuwa ametuma vijana kuelekea Arusha mbako inaaminika kuwaΒ  Gaidi namba moja aliyeiteka Benki kuu anatokea hukoΒ 

    “Huo ni ujinga Shayo! Unafuatilia historia ya Mtu badala yaΒ  kupambana naye sasa hivi, hadi umalize kuijuwa historia yakeΒ  pengine gaidi atakuwa amemaliza kazi yake na kuondoka Nchini.Β  Benki ipo chini yao Shayo, historia histori historiaΒ  itasaidia nini?” Aliuliza Rais akionekana kuwa mwenye hasiraΒ 

    “Mkuu kila jambo linahitaji taaluma katika utendaji, kabla yaΒ  kutatua tatizo ni lazima tuangalie lilipoanzia itatusaidiaΒ  kujuwa ukubwa wake!” Alijitetea Mzee Shayo

    “Hivi kweli ulistahili kuwa Mkuu wa Kitengo cha Usalama waΒ  Taifa? Magaidi wamechukua silaha Lugalo na makambi mengine,Β  tayari Nchi hii imekuwa kisiwa cha vita unayajuwa madharaΒ  yake? Kiasi kikubwa vita hii utapigana wewe na vijana wako,Β  jeshi lipo katika hali ngumu ya kujinasua” Alisema Rais hukuΒ  akionekana kuanza kususa mazungumzo hayo, Waziri MkuuΒ  akamwambia Mzee ShayoΒ 

    “Kuna hazina kubwa sana pale Benki pengine ndiyo sababu yaΒ  Ugaidi huu, hakikisha unafaulu Shayo, vinginevyoΒ  hatutokuelewa” Alisema Waziri Mkuu kisha Mzee ShayoΒ  alinyanyuka na kuaga, alipoondoka Rais alimuuliza Waziri MkuuΒ 

    “Nani anajuwa ilipo chemba iliyohifadhiwa pesa?” AliulizaΒ  akiwa makini sanaΒ 

    “Kuna Mdada wa pale Benki anaitwa Selina, yeye bahati mbayaΒ  yupo ndani ya Benki na ameshikiliwa kama watafanikiwaΒ  kumtambuwa basi mpango wote utavurugika” Alisema Waziri MkuuΒ  na kumpa muda wa kutafakari RaisΒ 

    “Una hakika Gavana hajui chochote?” Aliuliza RaisΒ 

    “Gavana anajuwa kuhusu pesa iliyohifadhiwa Benki ila hajuiΒ  iliwekwa wapi sababu mpango ulifanywa kuwa siri kamaΒ  ulivyoagizwa”. Alijibu Waziri MkuuΒ 

    “Nina uhakika hawawezi kuchukua pesa za Kitanzania watahitajiΒ  zile Dola, hili jambo sitaki lifahamike popote na kamaΒ  itatokea Mtu amejuwa basi katisha Maisha yake” Aliagiza RaisΒ 

    Naaam!! Mzee Shayo alipotoka Ikulu alihitaji kwendaΒ  kutembelea makazi yake yaliyopo Mikocheni B, alikuwaΒ  akitembea kwa siri sana hadi alipofika, Kisha aliingia kwenyeΒ  chumba ambacho alikuwa akikitumia kufanya kazi zake, aliketiΒ  ili kujipa utulivu huku akifikiria afanye nini.Β 

    β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’Β 

    Nje kidogo ya Jiji la Arusha, kulionekana gari moja nyeusiΒ  aina ya prado ikiwa imeacha barabara na kukita kwenye MtiΒ 

    Tukio hilo lilionekana kutokea muda mrefu uliopita kutokanaΒ  na ukimya ambao ulikuwepo, ndani ya gari hiyo alikuwemoΒ  Faudhia akiwa ameegemea usukani, alikurupuka kama MzimuΒ  kutoka kifo.Β 

    “Uhhhh” alisikia maumivu makali ya kichwa, alionekana kuchokaΒ  sana, alifungua mlango na kutoka ndani ya gari, alijivutaΒ hadi chini ya Mti, aliitoa simu yake kisha aliiangaliaΒ  alikuwa ametafutwa na Nani, aliona ni Mkuu wa Kitengo alikuwaΒ  amempigia zaidi ya mara 40, alimpigia Mkuu huyoΒ 

    “Aah Baba!!” Alisema Faudhia akionekana kuwa na maumivuΒ  makali kisha alikohoa na kuanza kumtia hofu Mzee ShayoΒ 

    “Faudhia upo sawa?” Alihoji Mzee ShayoΒ 

    “Nilichungulia mlango wa kuzimu lakini bahati nzuri mafunzoΒ  yamenisaidia kujinasua” Alisema FaudhiaΒ 

    “Mohd yuko wapi?” Alihoji Mzee ShayoΒ 

    “Baba!! Mohd ndiye aliyetaka kunipeleka kuzimu, nimeshtukaΒ  anafanya kazi upande wa Magaidi, anatumika upande huo naΒ  sijui ametumika kwa muda gani, alipewa agizo la kunimaliza”Β  Alisema FaudhiaΒ 

    “What? ( Nini? )” aliuliza kwa mshituko sana Mzee Shayo.Β 

    “Ndio…alafu, Mhusika Mkuu wa ugaidi ni Mzee Shomari”Β  Alisema Faudhia na kumuacha kinywa wazi Mzee ShayoΒ 

    “Una uhakika na maneno yako Faudhia? Mzee Shomari si yupoΒ  gerezani?” Aliuliza Mzee Shayo,Β 

    “Hapana, nina uhakika na ninachozungumza na yeye ndiyeΒ  aliyetoa maagizo ya kuuawa kwangu, nahisi ni yeye ndiyeΒ  aliyehitaji kunimaliza kabla sijavuka mpaka wa Namanga”Β  Alisema FaudhiaΒ 

    “Shit!! Sasa kwanini wametumia nguvu kubwa ya kuzuia habariΒ  za Chogo ikiwa gaidi namba moja ni Mzee Shomari?” AliulizaΒ  Mzee ShayoΒ 

    “Kuna mtego mahali, inavyoonekana kuna mchezo unachezwa hapaΒ  Baba” Alisema FaudhiaΒ 

    “Upo wapi kwa sasa?” Alihoji Mzee ShayoΒ 

    “Nipo nje kidogo ya Jiji la Arusha, jiji hili si salama tenaΒ  Kwasasa”Β 

    “Sikia Faudhia, ni lazima umalize hiyo kazi, fuatilia ujuweΒ  ni kwanini Chogo anafichwa, kuna ufunguo wa hili jambo katikaΒ  Maisha ya Chogo, hujapata fununu yoyote?”

    “Tulionana na Mama yake Chogo, alisema Mwanaye alifarikiΒ  Miaka mingi kwa ajali ya gari na alituonesha na kaburi lake,Β  lakini pia alituonesha picha ya Mtu aliyeleta Maiti ya ChogoΒ  alikuwa ni Mzee Shomari” Alisema FaudhiaΒ 

    “Hapo kuna taarifa juu ya taarifa, tukio juu ya Tukio, hiyoΒ  picha iliyopigwa Mzee Shomari alikuwa katika pozi lipi?”Β  Aliuliza Mzee Shayo akiwa nyumbani kwake MikocheniΒ 

    “Ilionekana ni picha iliyopigwa bila Mzee Shomari kujiandaa,Β  alikuwa akiongea na Mtu mwingine”Β 

    “Yes! Yes! Rudi Arusha haraka sana Faudhia, hakikishaΒ  unafahamu stori nzima, naelekea gerezani kujuwa kuhusuΒ  taarifa ya Mzee Shomari”Β 

    “Sawa Baba” Alisema Faudhia kisha alikata simu, alishushaΒ  pumzi zake, alikuwa na kazi nzito iliyojaa hatari mbele yake.Β 

    Waligawana majukumu, Faudhia alirudi Arusha, Mzee ShayoΒ  alielekea gereza la Segerea haraka sana, alitumia usafiri waΒ  pikipiki ambao aliamini asingeliweza kuchelewa walaΒ  kudhurika, Watu wachache sana ndio waliokuwa wakifanya safariΒ  za hapa na pale ila shughuli zilikuwa zimesimama kabisa,Β  ilimchukua takribani dakika 50 kutoka Mikocheni hadi LilipoΒ  gereza la Segerea, alikuwa akifahamika hivyo aliingia mojaΒ  kwa moja hadi kwa Mkuu wa gereza na kumuuliza kuhusu MzeeΒ  Shomari, alichojibiwa kilimchosha sana. Naaam!! Alipewa sasaΒ  simulizi ya Mzee Shomari akiwa gerezani hadi alivyotowekaΒ 

    “Baada ya kufungwa alikaa miezi kadhaa tuu, baadaye kulitokeaΒ  uvamizi hapa na hatimaye alitoroshwa ila ilifahamika kuwaΒ  baada ya kutoroka aliondoka Nchini na rafiki yake MzunguΒ  ambaye alikuwa mfungwa mwenzake wakaelekea Uholanzi” AlielezaΒ  Mkuu wa MagerezaΒ 

    “Shit!” Alisema Mzee Shayo na kukumbuka wakati tukio hiloΒ  linatokea yeye alikuwa mapumziko Nchini MorocoΒ 

    “Asante!” Alisema kisha aliondoka gerezani hapo akiwa naΒ  uhakika kuwa maneno ya Faudhia yalikuwa kweli ila alijiulizaΒ  sababu hasa ya ugaidi huo ilikuwa nini.Β 

    Aliondoka hapo kichwa kikiwa kimejaa moto, mzigo mzito waΒ  kupambana ulikuwa kichwani pake, Rais alikuwa akimkalia kooniΒ  kila wakati asijuwe afanyaje.Β 

    Upande wa Faudhia alikuwa tayari amerejea ndani ya Jiji laΒ  Arusha kuendelea kuutafuta ukweli kuhusu Chogo, alishaambiwaΒ ni Hospitali gani ilitoa gari kwa ajili ya kusafirisha mwiliΒ  wa Chogo, gari gani alipata nalo ajali, alifikiria aanzieΒ  wapi, aliona ni bora awasiliane na kampuni ya usafirishajiΒ  ambayo ilidaiwa gari lao ndio lilipata ajali na kupelekeaΒ  kifo cha Chogo, alipfika aliambiwa kampuni hiyo imefungwa kwaΒ  muda mrefu. Alikutana na mdada mmoja ambaye alionekana kuwaΒ  mfanyakazi wa kampuni hiyo, alijaribu kumbembeleza ili asemeΒ  chochote lakini mdada huyo aligoma kabisa, aliona ni boraΒ  aondoke.Β 

    Alipofika kwenye gari, aliketi na kutafakari aingilie wapi,Β  alipata wazo la kwenda Hospitalini. Lakini akiwa anawashaΒ  gari alitazama Side Mirror aliona kuna Mtu akitoka hapo akiwaΒ  na kikaratasi mfano wa tiketi hivi, alishangaa wakatiΒ  aliambiwa hakuna huduma katika kampuni hiyo, aliona ni boraΒ  azuge anaondoka, Naam! Alisogeza gari na kuificha mahaliΒ  kisha alirudi taratibu na kukuta mlango wa kampuniΒ  umefunguliwa wote wakati mwanzo ulikuwa umefungwa, kulikuwaΒ  na watu kadhaa ambao walikuwa wakitoka hapo, alifikiriaΒ  huenda wakawa wateja, alipoona Watu wameisha, aliingia humoΒ  kisha haraka alitoa bastola yake na kumuonesha Mdada huyo.Β  Faudhia Aligeuza maneno ya kibao kilichoandikwa HUDUMAΒ  INAPATIKANA akaweka TUMEFUNGA KWA MUDA.Β 

    Mdada huyo alionekana kujawa na hofu sana asijuwe anapaswaΒ  kufanya nini,Β 

    “Ulisema huduma zimesitishwa muda sasa lakini kumbe ulikuwaΒ  unajuwa unachokifanya si ndiyo?” Mdada aliendelea kutetemekaΒ  sanaΒ 

    “Niambie unafahamu nini kuhusu ajali mbaya ya gari iliyotokeaΒ  Miaka iliyopita, unamfahamu vipi Chogo? Ukifanya ujanjaΒ  wowote nazibua kichwa chako” Alisema FaudhiaΒ 

    “Naomba tafadhali usiniuwe nina ndugu ambao wananitegemeaΒ  Mimi” Alisema Mdada huyo akiwa analiaΒ 

    “Kama unataka nisikuuwe basi sema ukweli unafahamu niniΒ  kuhusu Chogo na kwanini ulikuwa unaficha jambo?” Aliuliza kwaΒ  masistizo Faudhia huku akijuwa fika kuwa eneo hilo halikuwaΒ  salama sana kwake, kwa hofu ya kuuawa Mdada alianza kufungukaΒ 

    “Nitasema kila kitu ila naomba usiniuwe”Β 

    “Mimi ni Undercover wa kitengo, unapaswa kusema ukweli sababuΒ  bila hivyo shingo yako itakuwa halali ya risasi nitakayoΒ  ifyatu hapa” Alisema Faudhia kwa msistizo sana.

    “Ilikuwa ni siku ya Jumatano, nilikuwa ndiyo kwanza nimeanzaΒ  ajira hapa, alikuja Baba Mmoja mlemavu wa mguu, umri wakeΒ  ulikuwa umeenda na kusema kuwa anahitaji kuongea na BosiΒ  wetu, bahati nzuri Bosi alikuwa ofisini kwake, Baba huyoΒ  alionekana kuwa ni Mtu mwenye fedha nyingi. Alienda kwa BosiΒ  na sikujuwa kuwa alikuwa anaongea nini na Bosi, baadayeΒ  alitoka kisha aliniaga kuwa anaondoka, Baada ya dakika 15Β  Bosi alikuja na kuniambia kuwa kuna kijana atakuja kwa ajiliΒ  ya kusafiri, nafikiri ndiyo huyo ambaye unamuulizia ila jnaΒ  lake siwezi kulikumbuka, aliniambia akija nimuoneshe mahaliΒ  pa kwenda kulala, ilikuwa ni ndani ya Ofisi hii kablaΒ  haijajengwa upya. Nilichukulia ni jambo la kawaida tuu,Β  alipokuja kijana majira ya saa moja usiku nilimkatia tiketiΒ  kisha nilimuonesha mahali pa kwenda kulala, inaonesha YuleΒ  Baba alkuwa akimfuatilia kijana huyo maana baada ya kijanaΒ  huyo kwenda kulala yule Baba alikuja”Β 

    “Aliniuliza Kijana yupo wapi, nilimuelekeza alipo sababuΒ  nilimjuwa Baba huyo baada ya kuja mchana na kuzungumza naΒ  Bosi, muda mchache baadaye Bosi naye alikuja kisha aliniulizaΒ  alipo kijana nilimueleza alipo, alielekea huko na ukimyaΒ  ulitawala, nilianza kusinzia lakini baadaye nilishtuka baadaΒ  ya Bosi kuniita na kuniambia kuwa napaswa kuondoka usiku huo,Β  nilikuwa na zamu ya kukesha hivyo kuambiwa vile nilifurahiΒ  ili nikalale, lakini nilipoangalia vizuri niligundua yuleΒ  Baba alikuwa akimsubiria Bosi nje ila alitoka na begi kubwaΒ  hivi ambalo hata sikuliona wakati linaingia, nilifunga naΒ  kuondoka zangu!!” Alisema Mdada huyo huku akihema juu juu,Β  Faudhia alishusha Bastola yake baada ya kugudua sasa alikuwaΒ  akiongea ukweli, alijuwa Baba huyo alikuwa ni Mzee Shomari.Β 

    “Enhee ilikuwaje baada ya hapo?”aliuliza tena FaudhiaΒ 

    “Baada ya hapo, siku iliyofuata niliambiwa nisiende kaziniΒ  ila nitalipwa pesa ya siku kitu ambacho kilizidi kunipaΒ  furaha, Mchana kupitia taarifa ya habari nilisikia taarifaΒ  kuwa basi la Kampuni yetu lilipata ajali wakati likiwaΒ  linafanya safari, Hakuna aliyepona katika ajali hiyo…lakiniΒ  Bosi alinisistiza sana nisije nikasema chochote kuhusu yuleΒ  Baba kuja usiku na yule kijana” Alisimulia Mdada huyo ambayeΒ  alikuwa mnene kiasiΒ 

    “Sasa usiri wako umepelekea Nchi kuzama kwenye Lindi laΒ  Ugaidi wa kutisha, muda siyo mrefu jiji hili litakuwa chiniΒ  ya ESS, kama unaweza kuongozana na mimi twende” AlisemaΒ  Faudhia akimwambia Mdada huyo ambaye alishapukiaΒ 

    Alionekana kuchanganikiwa, waliingia kwenye gari kisha gariΒ  liliondoka eneo hilo kuelekea yalipokuwa makazi ya Mama yakeΒ Martin Gimbo, miili ya Mama Martin na Mjukuu wake ilishaanzaΒ  kutoa harufu humo ndani, Faudhia aliingia kutafuta chochoteΒ  kitakachomuwezesha kufukua kaburi hilo ambalo lilisemekanaΒ  kuwa ni kaburi la Martin Gimbo.Β 

    “Naomba unisaidie hapa, tukishamaliza tunaondoka” AlisemaΒ  Faudhia kisha alimpatia chepe mdada huyo, walianza kufukuaΒ  kaburi hilo. Iliwachukua zaidi ya saa nzima hadi kumaliza,Β  chini walikutana na sanduku kubwa ambalo kwa kawaida lilikuwaΒ  ni sanduku la kuhifadhia mwili wakati wa kuzika. WalifanikiwaΒ  kulivuta juu, wakati huo walianza kusikia milio ya Risasi kwaΒ  mbali huku gari za polisi zikiliza ving’ora vyake.Β 

    Faudhia alianza kuligonga ili lifunguke, bahati nzuri alipataΒ  nyundo ndani ya nyumba hiyo kisha alifanikiwa zoezi laΒ  kulifungua Sanduku hilo, yule Mdada alitazama pembeni kwaΒ  hofu ya kuona mabaki ya mwili wa marehemu Martin Gimbo,Β  bahati mbaya ndani ya Sanduku hilo kulikuwa na brifkesi ndogoΒ  na siyo mifupa wala mabaki ya mwili wa Martin GimboΒ 

    “Yes! Martin Gimbo ndiye Chogo” Alisema Faudhia hukuΒ  akimtazama Mdada huyo ambaye hakulijuwa hata jina lake.Β  Alilichukua Brifkesi hilo lakini hata kabla hawajapiga hatuaΒ  hata moja, Faudhia alisindikizwa chini na teke kaliΒ  lililopigwa kwa ustadi wa hali ya juu, ghafla alihisi ganziΒ  mkono wa kulia, aliliachia brifkesi hilo huku akiwa anaangukaΒ  chini, Sanduku lilidakwaΒ 

    Faudhia alishangaa namna upigaji wa teke hilo ulivyotumiaΒ  akili na ustadi wa hali ya juu sana, aligeuka kumtazamaΒ  aliyekuwa amempiga teke hilo, alikutana na sura aliyoifahamu.Β  Naaam! Alikuwa ni rafiki yake wa zamani Diana, Diana alikuwaΒ  ndani ya Koti jeusi, sketi nyeusi, pia alikuwa amevalia wigiΒ  jeusi.Β 

    “Diana ni wewe?” Alihoji Faudhia, hakutegemea kukutana naΒ  Diana katika nyakati hizo, aliona kama yupo ndotoni japoΒ  alishatumiwa picha ya Miongoni mwa Watu waliokuwa wakiendeshaΒ  ugaidi Tanzania.Β 

    Faudhia alijivuta na kusimama japo kwa maumivu makali, tekeΒ  alilopigwa lilimfanya ahisi kizunguzungu.Β 

    “Umewezeje?” Aliuliza FaudhiaΒ 

    “Kwasababu nimekusubiria kwa zaidi ya miaka 7 Faudhia,Β  nimekusubiri kwa lengo moja tu la kukupeleka kuzimu” AlisemaΒ  Diana kisha aliweka Brifkesi pembeni, yule Mdada alivyoonaΒ  hivyo alikimbia eneo hilo sababu alijuwa kuna hatari kubwaΒ  inaenda kutokea hapo muda mchache ujao.

    “Ulinisubiria unipeleke kuzimu?” Alihoji Faudhia “Ndiyo! Kwasababu ulimuuwa Mama yangu” alisema DianaΒ 

    “Diana itakuwa umekosea njia, mimi nimemuuwa Mama yako? InaΒ  maana nawe umeingia kwenye mtego wa Mzee Shomari? DianaΒ  mnatumika na huyo Mzee ili atimize lengo lake, nisikilizeΒ  rafiki yangu!! Mimi sikuuwa Mama yako bali yeye Mzee ShomariΒ  ndiye aliyefanya hivyo na hiyo ndiyo sababu ya yeye kukaaΒ  jela, amka kutoka usingizini Diana” Alisema FaudhiaΒ 

    “Leo tutaona Faudhia kati yangu Mimi na wewe nani yupoΒ  Usingizini, Ukifa naondoka na Brifkesi, nikifa unaondoka naΒ  Brifkesi” Alisema Diana huku akijiandaa kupambana na FaudhiaΒ 

    “Diana hebu nisikilize, hujapoteza kila kitu katika MaishaΒ  yako, una muda wa kubadilisha kila kitu, ungana na MimiΒ  tumdhibiti Mzee Shomari” Alisema Faudhia, maneno ya FaudhiaΒ  hayakubadilisha Chochote, Diana alikaa mkao wa kuanzaΒ  kumshambulia Faudhia. Alianza kumfuata Faudhia kama SimbaΒ  mwenye njaa huku Faudhia akiwa anarudi nyuma ili afikirieΒ  namna ya kumzuia Diana.Β 

    Faudhia aligundua haraka kuwa Diana alikuwa anatumia piganoΒ  maarufu nchini China linaloitwa Wing Chun, alijuwa sasa kumbeΒ  Diana alikuwa na taaluma ya mapigano ya Martial artsΒ 

    Alipomfikia alitua kwenye mapaja ya Faudhia kisha alijirushaΒ  na kumzunguka kwa nyuma kisha aligusa mfupa hadimu sana nyumaΒ  ya mgongo wa Faudhia, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana,Β  Faudhia alihisi kukatika kwenye uti wa mgongo ila alijikazaΒ  asianguke, alifanya haraka na kumgeukia Diana kishaΒ  alijipanga kupambana naye, alimwambiaΒ 

    “Acha Diana, Acha unachofanya kumbuka sisi ni marafiki”Β  Alisema FaudhiaΒ 

    “Ningekuwa rafiki yako usingelithubutu kuniulia Mama yangu,Β  alikukosea nini yule?” Alisema Diana huku akionekana kuzidiΒ  kujawa na hasira, alijiandaa tena kumpa pigo lingine la WingΒ  Chun…Faudhia alijitahidi kuisoma mikimbio ya Diana ambayoΒ  ilikuwa ya haraka mno.Β 

    Alifanya kama vile anamkimbia, alimpa mgongo kisha alipohisiΒ  Diana yupo nyuma karibu na kumnasa alimchumpa na kugusa mguuΒ  mmoja kwenye mti kisha alijipindua na kukutana na DianaΒ  ambaye hakutegemea kama Faudhia angejifyetua kisha FaudhiaΒ  alimpa teke la Maana Diana, alisogezwa pembeni huku akitemaΒ  damu, ilizidi kumpa hasira, alimfuata tena na kufanyaΒ mpambano huo uzidi kuwa mtamu. Ilikuwa ni vita kati yaΒ  marafiki wawili waliogeuka kuwa maadui, ndipoΒ  walipothibitisha kuwa kuna Msitari mwembamba sana kati yaΒ  Upendo na chuki.Β 

    Ulikuwa ni mpambano mkali sana, vita ya kurushiana ngumiΒ  ilitanda, Ilikuwa kama vile walikuwa wakipeana zamu, dakikaΒ  tatu kwa Faudhia na dakika tatu kwa Diana. Wakati wanapiganaΒ  lile Brifkesi lilikuwa pembeni, Faudhia hakujuwa kulikuwa naΒ  jambo gani ndani ya Bridkesi hilo jeusi.Β 

    Jua lilikuwa likiendelea kuwaka kwa ukali wake. Kutokana naΒ  ile sumu ambayo iliingizwa mwilini mwake na Mohd japoΒ  alijitahidi kuizuia kwa kujichoma sindano ila ilianzaΒ  kumletea shida alianza kutokwa jasho, ndio muda ambao DianaΒ  aliutumia kumfanyia kitu mbaya Faudhia.Β 

    Alipeleka ngumi zaidi ya 10 mfululizo, Faudhia alijitahidiΒ  kadiri ya uwezo wake kuzipangua lakini hakuwa na nguvu yaΒ  kuzipangua zote alijikuta akiruhusu mwili wake kukutana naΒ  ngumi nzito za Diana, alijikutana akishuka chini na kupigaΒ  magoti, Diana alilichukua lile brifkesi kisha alimwambiaΒ  FaudhiaΒ 

    “Onja uchungu wa kifo ambao ulimpatia Mama yangu” AlichomoaΒ  sindano ili aweze kumchoma FaudhiaΒ 

    “Diana! Umesahau kila kitu? Kumbuka wewe ni nani, MzeeΒ  Shomari anakutumia” Alisema Faudhia japo kwa shida sana hukuΒ  akihisi kizunguzungu, Diana alitoa kichupa kidogo kishaΒ  alifyonza sumu kwa kutumia sindanoΒ 

    “Niliwahi kusimuliwa kuwa Mtu anayekaribia kufa huwa naΒ  majuto sana ila nakushangaa wewe Faudhia bado unakaidi kuwaΒ  hukumuuwa Mama yangu” Diana alimsongelea Faudhia, alimshikaΒ  nywele na kupindisha shingo kisha alimchoma sindano, kablaΒ  hajaruhusu sumu iweze kusambaa mwilini mwa Faudhia, alipigwaΒ  na kitu kizito kichwani, Diana alishindwa kumalizia zoezi,Β  alijitahidi kugeuka lakini alishindwa alijikuta akiangukaΒ  chini na kupoteza fahamu. Nyuma yake alisimama yule MdadaΒ  ambaye alimpa taarifa ya ajali ya Basi, Naam! NdiyeΒ  aliyempiga na kitu kizito Diana.Β 

    Faudhia alimwambia Mdada huyo kuwaΒ 

    “Chukua Brifkesi tuondoke hapa, si unajuwa kuendesha gari?”Β  AliulizaΒ 

    “Ndio najuwa”

    “Tuondoke hapa haraka sana” Alisema Faudhia, hakutakaΒ  kummaliza Diana siku hiyo sababu licha ya uadui badoΒ  alimtambuwa Diana kama rafiki yake, yule Mdada alimsaidiaΒ  Faudhia kuingia kwenye gari walilokuja nalo, Milio ya risasiΒ  ilitanda kila kona ya Jiji la Arusha, isingelikuwa salama kwaΒ  Faudhia kuendelea kukaa hapoΒ 

    “Tunaenda wapi?” Alihoji mdada akiwa anaingia barabara kuuΒ 

    “Dar-es-salaam” Alisema Faudhia huku akilifungua BrifkesiΒ  hilo ili ajuwe ndani yake kulikuwa na nini na kwaniniΒ  lilizikwa.Β 

    β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’Β 

    Jina la Selina lilifika mikononi mwa Chogo, aliambiwa kuwaΒ  ndiye anayefahamu ilipo chemba ya siri iliyohifadhi kiasiΒ  kikubwa cha pesa, Chogo alitoka kwenye moja ya Chumba baadaΒ  ya kumaliza kuzungumza na Mzee Shomari na kupewa taarifa hiyoΒ  kuwa kuna Mwanamke anaitwa Selina na yupo ndani ya Benki,Β  yeye pekee ndiye anayefahamu ilipo chemba ya siri. ChogoΒ  alitoka akiwa ameshikilia Bunduki aina ya AK47Β 

    Mateka walikuwa wamekaa chini kando ya sehemu ya Mapokezi,Β  alipofika aliulizaΒ 

    “Selina ni nani?” Ilikuwa ni sauti iliyojaa mamlaka sana,Β  aliuliza kwa kumaanisha kuwa alikuwa akimuhitaji Mdada huyo.Β  Selina mwenyewe aliposikia hivyo alijuwa ni kitu gani MagaidiΒ  hao walikuwa wakihitaji, baadhi ya Magaidi sura zaoΒ  walizificha Ila baadhi hawakuzificha akiweno Chogo ambayeΒ  waliamini hawezi kutambulika kwa urahisi.Β 

    “Selina ni nani?” Aliuliza tena Chogo kisha aliiandaa bundukiΒ  kwa lengo la kuleta kitishoΒ 

    “Mimi hapa” alijitokeza huyo aliyeitwa Selina akiwa amevaliaΒ  sare za wafanyakazi wa Benki, alikuwa Mwanamke mmoja mzuriΒ  mweusi mwenye rasta asilia.Β 

    “Mleteni” Alisema Chogo, mara moja Selina alisogezwa mahaliΒ  aliposimama Chogo, Selina alionekana kuwa muoga sana, ChogoΒ  alimwambia SelinaΒ 

    “Usiogope sababu una kazi moja tu ya kufanya, ukishamalizaΒ  nitakuacha huru sawa?” Alisema akiwa anatabasamu, SelinaΒ  aliitikia kwa woga kisha Chogo alisema

    “Tuongozane” Alimpa ishara Selina amfuate kwenye moja yaΒ  chumba.Β 

    Nje ya Benki polisi walizingira benki hiyo wakiwa na silahaΒ  za moto huku wakiwa na tahadhari kubwa, walikuwa wakitumiaΒ  kipaza sauti kuzungumza, Chogo alipofika Chumbani na SelinaΒ  alimwambiaΒ 

    “Nisubirie hapa, naenda kuongea na polisi” Alisema kishaΒ  alichukua AK47 na kuelekea nje ya Benki hiyo.Β 

    Kitendo cha Chogo kutoka nje ya Benki kilileta utayari kwaΒ  polisi na vitengo vyote vilivyokuwa makini na Benki, ChogoΒ  alitoka akiwa hajavaa shati, mwili wali wake ulijaa michoroΒ  mingi, alionekana kujiamini sana huku polisi wakiambiana kuwaΒ  wanapaswa kumsikiliza sababu alikuwa na mateka ndani ya BenkiΒ 

    Chogo alisimama katikati ya Barabara iliyotoka kivukoniΒ  kwenda mjini kisha aliwauliza polisiΒ 

    “Mlitaka nitoke ndani, nimeshatoka, mlikuwa mnasemaje?”Β  Aliuliza kwa ujasiri, kipaza sauti kilisikikaΒ 

    “Kwanza tunahitaji usalama wa mateka wote walio ndani yaΒ  Benki, pili tunataka kujuwa mnahitaji nini?”Β 

    “Oooh! Siwezi kuuwa Raia ambao hawana kosa lolote, ilaΒ  mkileta ujanja nitauwa kila Mtu ndani ya Benki, masaa 24Β  yajayo nitaiachia Benki hii” Alisema Chogo kisha alirudiΒ  ndani ya Benki, hakuna askari hata mmoja aliyejaribuΒ  kumshambulia Chogo, moja kwa moja alienda kwenye kile chumbaΒ  alichomuacha Selina, aliweka Bunduki pembeni kisha alifungaΒ  mlango, Chogo alimtazama Selina kwa jicho la kumtamani sanaΒ  ukizingatia sketi ya Selina ilikuwa imepasuka kidogo hivyoΒ  paja lilikuwa njeΒ 

    Selina alikuwa mwingi wa kutetemeka, Chogo alimfuata SelinaΒ  kisha alimtandika busu, alimshika matiti na Makalio, alimvuaΒ  nguo Selina na kumbaka, baada ya kumaliza alimwambia SelinaΒ 

    “Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie wapiΒ  ilipo chemba ya siri iliyohifadhi pesa za Kimarekani” AlisemaΒ  Chogo akiwa anavaa nguo zake, alipomaliza alikuwa badoΒ  hajapata jibu kutoka kwa Selina ambaye alikuwa akitetemekaΒ  kwa wogaΒ 

    “Ukimya wako unaashiria kuwa ni bora ufe kuliko kusema ilipoΒ  Chemba si ndiyo?” Aliuliza tena Chogo, safari hiiΒ  alibadilisha sura yake na kujaza hasira

    “Tafadhali usiniuwe, ipo chumba namba 43” Alisema SelinaΒ 

    LEO NIMEWEKA NDEFU SANA COMMENTS ZIKIWA CHACHE NARUDI KWENYE KUWEKA FUPI

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA SABA

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    riwaya za bure riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia

    27 Comments

    1. Octavian simplisius kazikulima on June 3, 2025 11:58 am

      Leo kwel ni ndefu had nimefulai

      Reply
      • Bunju5 on June 4, 2025 3:29 pm

        Hongera

        Reply
    2. Fadhili magimba on June 3, 2025 2:33 pm

      Nimeipenda

      Reply
    3. Luccah on June 3, 2025 2:48 pm

      Haha admini usitunyanyase ww weka unay0jiskia fupi au ndefu ss tunas0ma t πŸ˜‚

      Reply
    4. Adam on June 3, 2025 2:55 pm

      Leo Kweli Nimefrahia Saana Kuusoma Hii Story

      Reply
    5. Rifai on June 3, 2025 4:04 pm

      Hongera san ni nzur na ya kuvutia unasoma lkin kam vile ni video ipo mbele yko unaiagaliaπŸ’―

      Reply
    6. Benedict juma yanga on June 3, 2025 4:17 pm

      Hongera ndefu alafu tamu

      Reply
    7. David ben on June 3, 2025 5:50 pm

      Asante sana leo ndefu

      Reply
    8. Ignas talsis mumba on June 3, 2025 5:51 pm

      Nzuri sana

      Reply
    9. Josephat on June 3, 2025 6:01 pm

      Ndo kusema chogo alikua na ugwadu🀣🀣🀣🀣

      Reply
    10. Sulee on June 3, 2025 7:23 pm

      Nzur sana boss leo mzigo wa uhakika

      Reply
      • Salma Ibrahim on June 3, 2025 9:40 pm

        Leo imefika mahala pake..

        Reply
      • Salma Ibrahim on June 3, 2025 9:41 pm

        Mashaallah asante

        Reply
    11. Samwel mkangi on June 3, 2025 11:03 pm

      Imekaa pouuuwaa

      Reply
    12. Gervase on June 4, 2025 7:03 am

      Aah Admin we nouma ,, Leo ndefu Hadi RahaπŸ’ͺ

      Reply
    13. Lucas George on June 4, 2025 8:24 am

      Apo sawa admin πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
      • Azimara rajabu on June 5, 2025 11:18 am

        nzuri san

        Reply
    14. Maestro05 on June 4, 2025 8:52 am

      Ya Leo imekuwa ndefu pia nzuri..Bigup Sana Admin

      Reply
    15. Masoud on June 4, 2025 11:05 am

      Aisee kuipata yote tunabonyeza ngapi mkuuπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…βœ…οΈ

      Reply
    16. KASIBETH NDIKUMWAMI on June 4, 2025 3:26 pm

      Story nzuri inavutia sana inanifanya kila saaa niwe naingia kwenye kundi kuitafta jitahdi luifanya iwe ndefu pia itoke kwa wakati

      Reply
    17. Safina on June 4, 2025 6:13 pm

      Mbona ya Saba hutoi Admin sio poa bwana

      Reply
      • Safina on June 4, 2025 6:14 pm

        Tumesubir sana huweki

        Reply
    18. Azimara rajabu on June 5, 2025 11:19 am

      nzuri sana

      Reply
    19. πŸ”“ + 1.333214 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/76RuKke5vYn6W1hp2wxzvb?hs=64f1178154d728143e05eb423d7c652a& πŸ”“ on June 5, 2025 6:25 pm

      7x51ai

      Reply
    20. Verena on June 6, 2025 7:49 am

      Tamu na ndefu hadi raha

      Reply
    21. πŸ“œ Notification: + 1,124258 bitcoin. GET > https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=64f1178154d728143e05eb423d7c652a& πŸ“œ on June 6, 2025 10:49 am

      cgnsok

      Reply
    22. Cathbert on June 7, 2025 8:04 am

      Good πŸ‘πŸ‘

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.