Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nneย
“Assssh” aligumia Faudhia kutokana na maumivu ya kujigongaย kwenye meza, Mohd hakutaka kusubiri alimrushia ngumiย mfululizo, ngumi ambazo zilimpekeka Fuadhia ukutani, bahatiย mbaya ngumi nyingi zilimpata na kumfanya aumie usoniย
Mohd alimpiga Faudhia mateke mfululizo eneo la mbavu hukuย akimwambiaย
“Unakufa leo” Alisema huku akiwa anamuangalia Faudhia akiwaย anaanguka chini. Endelea
SEHEMU YA SITA
Mohd alimsindikiza Faudhia kwa teke kali lililomzimishaย Faudhia, Mohd alitoa kifaa kidogo ambacho kilikuwa na sindanoย ya sumu ndani yake, aliitoa kisha alimkita Faudhia eneo laย shingo.ย
Baada ya kuhakikisha amemdunga alielekea Kuvuta kochi kishaย aliitafuta simu yake ambayo ndiyo ilikuwa muhimu sana kishaย Bastola yake ambayo ingekuja kuwa ushahidi pale, aliichukuaย Bastola na simu kisha aliondoka eneo hilo.ย
Sekunde kumi na tano baadaye sindano ya sumu ilianza kufanyaย kazi yake, Faudhia alishtuka huku akiwa anateswa na sumuย ambayo ilikuwa ikisambaa kwa kasi mwilini, alijikuta akianzaย kuishiwa nguvu, alijivuta kisha alifungua kibegi chake kidogoย alitoa sindano, alivuta dawa haraka kutoka kwenye chupaย kidogo kisha alijidunga sindano akiwa anavuja damu, kishaย alianguka chini na kuzima.ย
Usiku huo, Mzee Shomari alikuwa akisubiria simu ya Mohd iliย kumpa taarifa ya kifo cha Faudhia. Alikuwa kwnye kiti chaย walemavu akitembea sebleni ndani ya Jengo la China plazaย jengo ambalo walilifanya kuwa makao yao ya siri walipoanzaย kupanga mipango ya Kigaidi, jengo hilo lilikuwa la rafikiย yake aliyeko Uholanzi ambaye ndiye aliyekuwa anafadhiliย ugaidi.ย
Alianza kukumbuka miaka mingi iliyopita katika Jiji la Mbeya.ย
Siku ambayo alikamatwa Baada ya kumuuwa Mama yake Diana,ย alimtazama kwa hasira sana Faudhia, alijenga chuki na kisasiย kwa Faudhia. Mzee Shomari alipelekwa Kituo cha polisi,ย alipewa mateso makali sana ikiwemo kuwekwa kwenye beseniย lenye maji na kukosa pumzi, alikumbuka jinsi alivyopigwa hadiย kuvunjwa mguu na ndiyo sababu ya yeye kuwa mlamavu ndiyoย maana anatembea kwenye kiti cha walemavu.ย
Alipelekwa mahakamani baada ya kupata matibabu ya mguu kishaย alihukumiwa kifungo cha Maisha jela, alipofika huko alikutanaย na mzungu aliyeitwa Damian, alijenga urafiki na Mzungu huyoย ambaye alikuwa na kesi ya kusafirisha madini kinyume chaย sheria kutoka Tanzania kwenda Thailand, walishibana wakiwaย gerezani.ย
Akiwa anaendelea kuwaza kilichotokea baada ya kufungwa, simuย ya Mzee Shomari iliita alipopokea alisikia sauti ya Mohdย ikimwambiaย
“Faudhia ni damu baridi” Alisema akiwa na maana kuwaย ameshamuuwa, Mzee Shomari alishangaa sana kwa jinsi ambavyoย alimuuwa Faudhia kisha alimuuliza
“Upo wapi?”ย
“Nipo njiani narudi Dar” Alisema Mohdย
“Tukio lilikuwaje?” Alihoji Mzee Shomari kwa unakini mkubwaย huku akionekana alikuwa mwenye akili sanaย
Mohd alimsimulia Mzee Shomari tukio lilivyotokea kisha Mzeeย Shomari alisemaย
“Ukifika Chalinze utaona kuna prado nyeusi, itumie” Alisemaย Mzee Shomari kisha alikata simu. Alisogea na kutazama chini,ย aliliona namna jiji la Dar lilivyokuwa likiwaka taa hukuย barabara ya kutoka Karume kwenda Kariakoo ikiwa nyeupe hakunaย Mtu wala gariย
Alinyanyua simu yake akapiga simu mahali kisha akasemaย
“Case Clossed ( Kesi imeisha ) ” alikata simu akajisukuma naย kuingia kwenye chumba kingine.ย
Masaa matano baadaye Mohd alifika Chalinze usiku sana akiwaย na gari yake aina ya Toyota V8, mji ulikuwa kimya kabisa,ย alilliona Prado likiwa linawasha hazard kuashiria kuwaย lilikuwa ndiyo gari ambalo Mohd alitakiwa kulitumia, harakaย alishuka na kulielekea gari hilo, alipoingia aliangaza ndaniย ya gari hilo ili kuona kama kulikuwa na Mtu lakini gari hiloย halikuwa na Mtu, alivuta funguo na kuiwasha, kitendo chaย kuwasha tu gari hilo lililipuka, Mohd alifia ndani ya gariย hilo, pembezoni kulikuwa na roli, ndani ya Roli kulikuwa naย Mtu ambaye alisikika akiongea na simu akisemaย
“Target eliminated ( Mlengwa amemalizwa )” kisha roli hiloย liliwashwa na kueleka Upande wa morogoro.ย
Siku iliyofuata, Chogo alipewa kazi na Mzee Shomari yaย kuhakikisha anaifahamu ilipo chemba ya siri ambayo pesa hizoย za Kimarekani zilikuwa zimehifadhiwa, Mtu pekee ambayeย alidhaniwa kuwa anajuwa ilipo alikuwa ni Gavana wa Benkiย hiyo. Pesa ambazo akina Chogo walikuwa wanazitaka zilikuwa niย pesa za siri ambazo Tanzania iliyauzia madini Nchi ya Saudiย Arabia. Chogo alirudi ndani ya chumba ambacho Gavanaย alikuwemo na Mke wake, alikuwa ameweka rehani maisha ya mmojaย wa wafanyakazi wa Benki hiyo ili Gavana aseme mahali ambapoย pesa hizo zilikuwa zimehifadhiwa.ย
Gavana alimuuliza Chogo amajuwaje kama ndani ya Benki kunaย pesa za siri ambazo zilitokana na mauzo ya madini
“Acha kuuliza maswali ambayo kamwe hutoweza kupata majibuย yake, sema ilipo chemba ya siri vinginevyo namuuwa huyu!!”ย Alisema Chogo huku Bastola ikiwa kichwani kwa Mfanyakazi huyoย
Gavana alikaa kimya hakuonekana kumtetea Mfanyakazi asiuawe,ย alimtazama Mke wake kisha alirudisha macho kwa chogo.ย
“Umejuwaje?” Aliuliza tena kwa mshangao mkubwa sana, Chogoย alionekana kuwa ni Mtu katili mwenye hasira sana, alimpigaย risasi mfanyakazi kisha akamwambia Gavanaย
“Nakupa masaa matatu uoneshe ilipo chemba ya siri” Chogoย alisema kisha aliondoka ndani ya chumba hicho.ย
Upande wa pili, Mzee Shayo alianza kuingiwa na wasiwasiย kuhusu vijana wake wawili aliowatumainia, simu ya Mohdย haikupatikana baada ya kuuawa ndani ya gari, simu ya Faudhiaย iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa, ilimpa mashaka juu yaย usalama wao, alijitahidi sana kupiga simu lakini simu yakeย haikuweza kumpa majibu ya nini kilichokuwa kimetokea hukoย Arusha kwenye operesheni ya kujuwa kuhusu Chogo, alitumaย Askari wengine wa Kitengo kuelekea Arusha kwa ajili yaย kuwatafuta Mohd na Faudhia.ย
Punde alipokea simu ya Rais iliyomtaka aende Ikulu harakaย sana, kutoka Kigamboni yalipo makao makuu ya Kitengo cha siriย cha Usalama wa Taifa ilimchukua dakika kadhaa, tayali hali yaย tahadhari ilitangazwa hivyo hakukutakiwa Mtu yeyote kutokaย ndani, Jiji lilikuwa kimya sana kama makazi yaliyotelekezwa,ย Mzee Shayo alifika hadi Ikulu kisha alienda kwenye chumba chaย siri ambacho Rais na Waziri Mkuu walikuwa wamehifadhiwa.ย
Rais alihitaji kujuwa Mzee Shayo alifikia wapi katikaย harakati za kupambana na Kikosi hicho cha Kigaidi, waliketiย watu watatu na kuanza kuzungumza, Mzee Shayo alimwambia Raisย kuwa ametuma vijana kuelekea Arusha mbako inaaminika kuwaย Gaidi namba moja aliyeiteka Benki kuu anatokea hukoย
“Huo ni ujinga Shayo! Unafuatilia historia ya Mtu badala yaย kupambana naye sasa hivi, hadi umalize kuijuwa historia yakeย pengine gaidi atakuwa amemaliza kazi yake na kuondoka Nchini.ย Benki ipo chini yao Shayo, historia histori historiaย itasaidia nini?” Aliuliza Rais akionekana kuwa mwenye hasiraย
“Mkuu kila jambo linahitaji taaluma katika utendaji, kabla yaย kutatua tatizo ni lazima tuangalie lilipoanzia itatusaidiaย kujuwa ukubwa wake!” Alijitetea Mzee Shayo
“Hivi kweli ulistahili kuwa Mkuu wa Kitengo cha Usalama waย Taifa? Magaidi wamechukua silaha Lugalo na makambi mengine,ย tayari Nchi hii imekuwa kisiwa cha vita unayajuwa madharaย yake? Kiasi kikubwa vita hii utapigana wewe na vijana wako,ย jeshi lipo katika hali ngumu ya kujinasua” Alisema Rais hukuย akionekana kuanza kususa mazungumzo hayo, Waziri Mkuuย akamwambia Mzee Shayoย
“Kuna hazina kubwa sana pale Benki pengine ndiyo sababu yaย Ugaidi huu, hakikisha unafaulu Shayo, vinginevyoย hatutokuelewa” Alisema Waziri Mkuu kisha Mzee Shayoย alinyanyuka na kuaga, alipoondoka Rais alimuuliza Waziri Mkuuย
“Nani anajuwa ilipo chemba iliyohifadhiwa pesa?” Aliulizaย akiwa makini sanaย
“Kuna Mdada wa pale Benki anaitwa Selina, yeye bahati mbayaย yupo ndani ya Benki na ameshikiliwa kama watafanikiwaย kumtambuwa basi mpango wote utavurugika” Alisema Waziri Mkuuย na kumpa muda wa kutafakari Raisย
“Una hakika Gavana hajui chochote?” Aliuliza Raisย
“Gavana anajuwa kuhusu pesa iliyohifadhiwa Benki ila hajuiย iliwekwa wapi sababu mpango ulifanywa kuwa siri kamaย ulivyoagizwa”. Alijibu Waziri Mkuuย
“Nina uhakika hawawezi kuchukua pesa za Kitanzania watahitajiย zile Dola, hili jambo sitaki lifahamike popote na kamaย itatokea Mtu amejuwa basi katisha Maisha yake” Aliagiza Raisย
Naaam!! Mzee Shayo alipotoka Ikulu alihitaji kwendaย kutembelea makazi yake yaliyopo Mikocheni B, alikuwaย akitembea kwa siri sana hadi alipofika, Kisha aliingia kwenyeย chumba ambacho alikuwa akikitumia kufanya kazi zake, aliketiย ili kujipa utulivu huku akifikiria afanye nini.ย
โขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขย
Nje kidogo ya Jiji la Arusha, kulionekana gari moja nyeusiย aina ya prado ikiwa imeacha barabara na kukita kwenye Mtiย
Tukio hilo lilionekana kutokea muda mrefu uliopita kutokanaย na ukimya ambao ulikuwepo, ndani ya gari hiyo alikuwemoย Faudhia akiwa ameegemea usukani, alikurupuka kama Mzimuย kutoka kifo.ย
“Uhhhh” alisikia maumivu makali ya kichwa, alionekana kuchokaย sana, alifungua mlango na kutoka ndani ya gari, alijivutaย hadi chini ya Mti, aliitoa simu yake kisha aliiangaliaย alikuwa ametafutwa na Nani, aliona ni Mkuu wa Kitengo alikuwaย amempigia zaidi ya mara 40, alimpigia Mkuu huyoย
“Aah Baba!!” Alisema Faudhia akionekana kuwa na maumivuย makali kisha alikohoa na kuanza kumtia hofu Mzee Shayoย
“Faudhia upo sawa?” Alihoji Mzee Shayoย
“Nilichungulia mlango wa kuzimu lakini bahati nzuri mafunzoย yamenisaidia kujinasua” Alisema Faudhiaย
“Mohd yuko wapi?” Alihoji Mzee Shayoย
“Baba!! Mohd ndiye aliyetaka kunipeleka kuzimu, nimeshtukaย anafanya kazi upande wa Magaidi, anatumika upande huo naย sijui ametumika kwa muda gani, alipewa agizo la kunimaliza”ย Alisema Faudhiaย
“What? ( Nini? )” aliuliza kwa mshituko sana Mzee Shayo.ย
“Ndio…alafu, Mhusika Mkuu wa ugaidi ni Mzee Shomari”ย Alisema Faudhia na kumuacha kinywa wazi Mzee Shayoย
“Una uhakika na maneno yako Faudhia? Mzee Shomari si yupoย gerezani?” Aliuliza Mzee Shayo,ย
“Hapana, nina uhakika na ninachozungumza na yeye ndiyeย aliyetoa maagizo ya kuuawa kwangu, nahisi ni yeye ndiyeย aliyehitaji kunimaliza kabla sijavuka mpaka wa Namanga”ย Alisema Faudhiaย
“Shit!! Sasa kwanini wametumia nguvu kubwa ya kuzuia habariย za Chogo ikiwa gaidi namba moja ni Mzee Shomari?” Aliulizaย Mzee Shayoย
“Kuna mtego mahali, inavyoonekana kuna mchezo unachezwa hapaย Baba” Alisema Faudhiaย
“Upo wapi kwa sasa?” Alihoji Mzee Shayoย
“Nipo nje kidogo ya Jiji la Arusha, jiji hili si salama tenaย Kwasasa”ย
“Sikia Faudhia, ni lazima umalize hiyo kazi, fuatilia ujuweย ni kwanini Chogo anafichwa, kuna ufunguo wa hili jambo katikaย Maisha ya Chogo, hujapata fununu yoyote?”
“Tulionana na Mama yake Chogo, alisema Mwanaye alifarikiย Miaka mingi kwa ajali ya gari na alituonesha na kaburi lake,ย lakini pia alituonesha picha ya Mtu aliyeleta Maiti ya Chogoย alikuwa ni Mzee Shomari” Alisema Faudhiaย
“Hapo kuna taarifa juu ya taarifa, tukio juu ya Tukio, hiyoย picha iliyopigwa Mzee Shomari alikuwa katika pozi lipi?”ย Aliuliza Mzee Shayo akiwa nyumbani kwake Mikocheniย
“Ilionekana ni picha iliyopigwa bila Mzee Shomari kujiandaa,ย alikuwa akiongea na Mtu mwingine”ย
“Yes! Yes! Rudi Arusha haraka sana Faudhia, hakikishaย unafahamu stori nzima, naelekea gerezani kujuwa kuhusuย taarifa ya Mzee Shomari”ย
“Sawa Baba” Alisema Faudhia kisha alikata simu, alishushaย pumzi zake, alikuwa na kazi nzito iliyojaa hatari mbele yake.ย
Waligawana majukumu, Faudhia alirudi Arusha, Mzee Shayoย alielekea gereza la Segerea haraka sana, alitumia usafiri waย pikipiki ambao aliamini asingeliweza kuchelewa walaย kudhurika, Watu wachache sana ndio waliokuwa wakifanya safariย za hapa na pale ila shughuli zilikuwa zimesimama kabisa,ย ilimchukua takribani dakika 50 kutoka Mikocheni hadi Lilipoย gereza la Segerea, alikuwa akifahamika hivyo aliingia mojaย kwa moja hadi kwa Mkuu wa gereza na kumuuliza kuhusu Mzeeย Shomari, alichojibiwa kilimchosha sana. Naaam!! Alipewa sasaย simulizi ya Mzee Shomari akiwa gerezani hadi alivyotowekaย
“Baada ya kufungwa alikaa miezi kadhaa tuu, baadaye kulitokeaย uvamizi hapa na hatimaye alitoroshwa ila ilifahamika kuwaย baada ya kutoroka aliondoka Nchini na rafiki yake Mzunguย ambaye alikuwa mfungwa mwenzake wakaelekea Uholanzi” Alielezaย Mkuu wa Magerezaย
“Shit!” Alisema Mzee Shayo na kukumbuka wakati tukio hiloย linatokea yeye alikuwa mapumziko Nchini Morocoย
“Asante!” Alisema kisha aliondoka gerezani hapo akiwa naย uhakika kuwa maneno ya Faudhia yalikuwa kweli ila alijiulizaย sababu hasa ya ugaidi huo ilikuwa nini.ย
Aliondoka hapo kichwa kikiwa kimejaa moto, mzigo mzito waย kupambana ulikuwa kichwani pake, Rais alikuwa akimkalia kooniย kila wakati asijuwe afanyaje.ย
Upande wa Faudhia alikuwa tayari amerejea ndani ya Jiji laย Arusha kuendelea kuutafuta ukweli kuhusu Chogo, alishaambiwaย ni Hospitali gani ilitoa gari kwa ajili ya kusafirisha mwiliย wa Chogo, gari gani alipata nalo ajali, alifikiria aanzieย wapi, aliona ni bora awasiliane na kampuni ya usafirishajiย ambayo ilidaiwa gari lao ndio lilipata ajali na kupelekeaย kifo cha Chogo, alipfika aliambiwa kampuni hiyo imefungwa kwaย muda mrefu. Alikutana na mdada mmoja ambaye alionekana kuwaย mfanyakazi wa kampuni hiyo, alijaribu kumbembeleza ili asemeย chochote lakini mdada huyo aligoma kabisa, aliona ni boraย aondoke.ย
Alipofika kwenye gari, aliketi na kutafakari aingilie wapi,ย alipata wazo la kwenda Hospitalini. Lakini akiwa anawashaย gari alitazama Side Mirror aliona kuna Mtu akitoka hapo akiwaย na kikaratasi mfano wa tiketi hivi, alishangaa wakatiย aliambiwa hakuna huduma katika kampuni hiyo, aliona ni boraย azuge anaondoka, Naam! Alisogeza gari na kuificha mahaliย kisha alirudi taratibu na kukuta mlango wa kampuniย umefunguliwa wote wakati mwanzo ulikuwa umefungwa, kulikuwaย na watu kadhaa ambao walikuwa wakitoka hapo, alifikiriaย huenda wakawa wateja, alipoona Watu wameisha, aliingia humoย kisha haraka alitoa bastola yake na kumuonesha Mdada huyo.ย Faudhia Aligeuza maneno ya kibao kilichoandikwa HUDUMAย INAPATIKANA akaweka TUMEFUNGA KWA MUDA.ย
Mdada huyo alionekana kujawa na hofu sana asijuwe anapaswaย kufanya nini,ย
“Ulisema huduma zimesitishwa muda sasa lakini kumbe ulikuwaย unajuwa unachokifanya si ndiyo?” Mdada aliendelea kutetemekaย sanaย
“Niambie unafahamu nini kuhusu ajali mbaya ya gari iliyotokeaย Miaka iliyopita, unamfahamu vipi Chogo? Ukifanya ujanjaย wowote nazibua kichwa chako” Alisema Faudhiaย
“Naomba tafadhali usiniuwe nina ndugu ambao wananitegemeaย Mimi” Alisema Mdada huyo akiwa analiaย
“Kama unataka nisikuuwe basi sema ukweli unafahamu niniย kuhusu Chogo na kwanini ulikuwa unaficha jambo?” Aliuliza kwaย masistizo Faudhia huku akijuwa fika kuwa eneo hilo halikuwaย salama sana kwake, kwa hofu ya kuuawa Mdada alianza kufungukaย
“Nitasema kila kitu ila naomba usiniuwe”ย
“Mimi ni Undercover wa kitengo, unapaswa kusema ukweli sababuย bila hivyo shingo yako itakuwa halali ya risasi nitakayoย ifyatu hapa” Alisema Faudhia kwa msistizo sana.
“Ilikuwa ni siku ya Jumatano, nilikuwa ndiyo kwanza nimeanzaย ajira hapa, alikuja Baba Mmoja mlemavu wa mguu, umri wakeย ulikuwa umeenda na kusema kuwa anahitaji kuongea na Bosiย wetu, bahati nzuri Bosi alikuwa ofisini kwake, Baba huyoย alionekana kuwa ni Mtu mwenye fedha nyingi. Alienda kwa Bosiย na sikujuwa kuwa alikuwa anaongea nini na Bosi, baadayeย alitoka kisha aliniaga kuwa anaondoka, Baada ya dakika 15ย Bosi alikuja na kuniambia kuwa kuna kijana atakuja kwa ajiliย ya kusafiri, nafikiri ndiyo huyo ambaye unamuulizia ila jnaย lake siwezi kulikumbuka, aliniambia akija nimuoneshe mahaliย pa kwenda kulala, ilikuwa ni ndani ya Ofisi hii kablaย haijajengwa upya. Nilichukulia ni jambo la kawaida tuu,ย alipokuja kijana majira ya saa moja usiku nilimkatia tiketiย kisha nilimuonesha mahali pa kwenda kulala, inaonesha Yuleย Baba alkuwa akimfuatilia kijana huyo maana baada ya kijanaย huyo kwenda kulala yule Baba alikuja”ย
“Aliniuliza Kijana yupo wapi, nilimuelekeza alipo sababuย nilimjuwa Baba huyo baada ya kuja mchana na kuzungumza naย Bosi, muda mchache baadaye Bosi naye alikuja kisha aliniulizaย alipo kijana nilimueleza alipo, alielekea huko na ukimyaย ulitawala, nilianza kusinzia lakini baadaye nilishtuka baadaย ya Bosi kuniita na kuniambia kuwa napaswa kuondoka usiku huo,ย nilikuwa na zamu ya kukesha hivyo kuambiwa vile nilifurahiย ili nikalale, lakini nilipoangalia vizuri niligundua yuleย Baba alikuwa akimsubiria Bosi nje ila alitoka na begi kubwaย hivi ambalo hata sikuliona wakati linaingia, nilifunga naย kuondoka zangu!!” Alisema Mdada huyo huku akihema juu juu,ย Faudhia alishusha Bastola yake baada ya kugudua sasa alikuwaย akiongea ukweli, alijuwa Baba huyo alikuwa ni Mzee Shomari.ย
“Enhee ilikuwaje baada ya hapo?”aliuliza tena Faudhiaย
“Baada ya hapo, siku iliyofuata niliambiwa nisiende kaziniย ila nitalipwa pesa ya siku kitu ambacho kilizidi kunipaย furaha, Mchana kupitia taarifa ya habari nilisikia taarifaย kuwa basi la Kampuni yetu lilipata ajali wakati likiwaย linafanya safari, Hakuna aliyepona katika ajali hiyo…lakiniย Bosi alinisistiza sana nisije nikasema chochote kuhusu yuleย Baba kuja usiku na yule kijana” Alisimulia Mdada huyo ambayeย alikuwa mnene kiasiย
“Sasa usiri wako umepelekea Nchi kuzama kwenye Lindi laย Ugaidi wa kutisha, muda siyo mrefu jiji hili litakuwa chiniย ya ESS, kama unaweza kuongozana na mimi twende” Alisemaย Faudhia akimwambia Mdada huyo ambaye alishapukiaย
Alionekana kuchanganikiwa, waliingia kwenye gari kisha gariย liliondoka eneo hilo kuelekea yalipokuwa makazi ya Mama yakeย Martin Gimbo, miili ya Mama Martin na Mjukuu wake ilishaanzaย kutoa harufu humo ndani, Faudhia aliingia kutafuta chochoteย kitakachomuwezesha kufukua kaburi hilo ambalo lilisemekanaย kuwa ni kaburi la Martin Gimbo.ย
“Naomba unisaidie hapa, tukishamaliza tunaondoka” Alisemaย Faudhia kisha alimpatia chepe mdada huyo, walianza kufukuaย kaburi hilo. Iliwachukua zaidi ya saa nzima hadi kumaliza,ย chini walikutana na sanduku kubwa ambalo kwa kawaida lilikuwaย ni sanduku la kuhifadhia mwili wakati wa kuzika. Walifanikiwaย kulivuta juu, wakati huo walianza kusikia milio ya Risasi kwaย mbali huku gari za polisi zikiliza ving’ora vyake.ย
Faudhia alianza kuligonga ili lifunguke, bahati nzuri alipataย nyundo ndani ya nyumba hiyo kisha alifanikiwa zoezi laย kulifungua Sanduku hilo, yule Mdada alitazama pembeni kwaย hofu ya kuona mabaki ya mwili wa marehemu Martin Gimbo,ย bahati mbaya ndani ya Sanduku hilo kulikuwa na brifkesi ndogoย na siyo mifupa wala mabaki ya mwili wa Martin Gimboย
“Yes! Martin Gimbo ndiye Chogo” Alisema Faudhia hukuย akimtazama Mdada huyo ambaye hakulijuwa hata jina lake.ย Alilichukua Brifkesi hilo lakini hata kabla hawajapiga hatuaย hata moja, Faudhia alisindikizwa chini na teke kaliย lililopigwa kwa ustadi wa hali ya juu, ghafla alihisi ganziย mkono wa kulia, aliliachia brifkesi hilo huku akiwa anaangukaย chini, Sanduku lilidakwaย
Faudhia alishangaa namna upigaji wa teke hilo ulivyotumiaย akili na ustadi wa hali ya juu sana, aligeuka kumtazamaย aliyekuwa amempiga teke hilo, alikutana na sura aliyoifahamu.ย Naaam! Alikuwa ni rafiki yake wa zamani Diana, Diana alikuwaย ndani ya Koti jeusi, sketi nyeusi, pia alikuwa amevalia wigiย jeusi.ย
“Diana ni wewe?” Alihoji Faudhia, hakutegemea kukutana naย Diana katika nyakati hizo, aliona kama yupo ndotoni japoย alishatumiwa picha ya Miongoni mwa Watu waliokuwa wakiendeshaย ugaidi Tanzania.ย
Faudhia alijivuta na kusimama japo kwa maumivu makali, tekeย alilopigwa lilimfanya ahisi kizunguzungu.ย
“Umewezeje?” Aliuliza Faudhiaย
“Kwasababu nimekusubiria kwa zaidi ya miaka 7 Faudhia,ย nimekusubiri kwa lengo moja tu la kukupeleka kuzimu” Alisemaย Diana kisha aliweka Brifkesi pembeni, yule Mdada alivyoonaย hivyo alikimbia eneo hilo sababu alijuwa kuna hatari kubwaย inaenda kutokea hapo muda mchache ujao.
“Ulinisubiria unipeleke kuzimu?” Alihoji Faudhia “Ndiyo! Kwasababu ulimuuwa Mama yangu” alisema Dianaย
“Diana itakuwa umekosea njia, mimi nimemuuwa Mama yako? Inaย maana nawe umeingia kwenye mtego wa Mzee Shomari? Dianaย mnatumika na huyo Mzee ili atimize lengo lake, nisikilizeย rafiki yangu!! Mimi sikuuwa Mama yako bali yeye Mzee Shomariย ndiye aliyefanya hivyo na hiyo ndiyo sababu ya yeye kukaaย jela, amka kutoka usingizini Diana” Alisema Faudhiaย
“Leo tutaona Faudhia kati yangu Mimi na wewe nani yupoย Usingizini, Ukifa naondoka na Brifkesi, nikifa unaondoka naย Brifkesi” Alisema Diana huku akijiandaa kupambana na Faudhiaย
“Diana hebu nisikilize, hujapoteza kila kitu katika Maishaย yako, una muda wa kubadilisha kila kitu, ungana na Mimiย tumdhibiti Mzee Shomari” Alisema Faudhia, maneno ya Faudhiaย hayakubadilisha Chochote, Diana alikaa mkao wa kuanzaย kumshambulia Faudhia. Alianza kumfuata Faudhia kama Simbaย mwenye njaa huku Faudhia akiwa anarudi nyuma ili afikirieย namna ya kumzuia Diana.ย
Faudhia aligundua haraka kuwa Diana alikuwa anatumia piganoย maarufu nchini China linaloitwa Wing Chun, alijuwa sasa kumbeย Diana alikuwa na taaluma ya mapigano ya Martial artsย
Alipomfikia alitua kwenye mapaja ya Faudhia kisha alijirushaย na kumzunguka kwa nyuma kisha aligusa mfupa hadimu sana nyumaย ya mgongo wa Faudhia, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana,ย Faudhia alihisi kukatika kwenye uti wa mgongo ila alijikazaย asianguke, alifanya haraka na kumgeukia Diana kishaย alijipanga kupambana naye, alimwambiaย
“Acha Diana, Acha unachofanya kumbuka sisi ni marafiki”ย Alisema Faudhiaย
“Ningekuwa rafiki yako usingelithubutu kuniulia Mama yangu,ย alikukosea nini yule?” Alisema Diana huku akionekana kuzidiย kujawa na hasira, alijiandaa tena kumpa pigo lingine la Wingย Chun…Faudhia alijitahidi kuisoma mikimbio ya Diana ambayoย ilikuwa ya haraka mno.ย
Alifanya kama vile anamkimbia, alimpa mgongo kisha alipohisiย Diana yupo nyuma karibu na kumnasa alimchumpa na kugusa mguuย mmoja kwenye mti kisha alijipindua na kukutana na Dianaย ambaye hakutegemea kama Faudhia angejifyetua kisha Faudhiaย alimpa teke la Maana Diana, alisogezwa pembeni huku akitemaย damu, ilizidi kumpa hasira, alimfuata tena na kufanyaย mpambano huo uzidi kuwa mtamu. Ilikuwa ni vita kati yaย marafiki wawili waliogeuka kuwa maadui, ndipoย walipothibitisha kuwa kuna Msitari mwembamba sana kati yaย Upendo na chuki.ย
Ulikuwa ni mpambano mkali sana, vita ya kurushiana ngumiย ilitanda, Ilikuwa kama vile walikuwa wakipeana zamu, dakikaย tatu kwa Faudhia na dakika tatu kwa Diana. Wakati wanapiganaย lile Brifkesi lilikuwa pembeni, Faudhia hakujuwa kulikuwa naย jambo gani ndani ya Bridkesi hilo jeusi.ย
Jua lilikuwa likiendelea kuwaka kwa ukali wake. Kutokana naย ile sumu ambayo iliingizwa mwilini mwake na Mohd japoย alijitahidi kuizuia kwa kujichoma sindano ila ilianzaย kumletea shida alianza kutokwa jasho, ndio muda ambao Dianaย aliutumia kumfanyia kitu mbaya Faudhia.ย
Alipeleka ngumi zaidi ya 10 mfululizo, Faudhia alijitahidiย kadiri ya uwezo wake kuzipangua lakini hakuwa na nguvu yaย kuzipangua zote alijikuta akiruhusu mwili wake kukutana naย ngumi nzito za Diana, alijikutana akishuka chini na kupigaย magoti, Diana alilichukua lile brifkesi kisha alimwambiaย Faudhiaย
“Onja uchungu wa kifo ambao ulimpatia Mama yangu” Alichomoaย sindano ili aweze kumchoma Faudhiaย
“Diana! Umesahau kila kitu? Kumbuka wewe ni nani, Mzeeย Shomari anakutumia” Alisema Faudhia japo kwa shida sana hukuย akihisi kizunguzungu, Diana alitoa kichupa kidogo kishaย alifyonza sumu kwa kutumia sindanoย
“Niliwahi kusimuliwa kuwa Mtu anayekaribia kufa huwa naย majuto sana ila nakushangaa wewe Faudhia bado unakaidi kuwaย hukumuuwa Mama yangu” Diana alimsongelea Faudhia, alimshikaย nywele na kupindisha shingo kisha alimchoma sindano, kablaย hajaruhusu sumu iweze kusambaa mwilini mwa Faudhia, alipigwaย na kitu kizito kichwani, Diana alishindwa kumalizia zoezi,ย alijitahidi kugeuka lakini alishindwa alijikuta akiangukaย chini na kupoteza fahamu. Nyuma yake alisimama yule Mdadaย ambaye alimpa taarifa ya ajali ya Basi, Naam! Ndiyeย aliyempiga na kitu kizito Diana.ย
Faudhia alimwambia Mdada huyo kuwaย
“Chukua Brifkesi tuondoke hapa, si unajuwa kuendesha gari?”ย Aliulizaย
“Ndio najuwa”
“Tuondoke hapa haraka sana” Alisema Faudhia, hakutakaย kummaliza Diana siku hiyo sababu licha ya uadui badoย alimtambuwa Diana kama rafiki yake, yule Mdada alimsaidiaย Faudhia kuingia kwenye gari walilokuja nalo, Milio ya risasiย ilitanda kila kona ya Jiji la Arusha, isingelikuwa salama kwaย Faudhia kuendelea kukaa hapoย
“Tunaenda wapi?” Alihoji mdada akiwa anaingia barabara kuuย
“Dar-es-salaam” Alisema Faudhia huku akilifungua Brifkesiย hilo ili ajuwe ndani yake kulikuwa na nini na kwaniniย lilizikwa.ย
โขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขย
Jina la Selina lilifika mikononi mwa Chogo, aliambiwa kuwaย ndiye anayefahamu ilipo chemba ya siri iliyohifadhi kiasiย kikubwa cha pesa, Chogo alitoka kwenye moja ya Chumba baadaย ya kumaliza kuzungumza na Mzee Shomari na kupewa taarifa hiyoย kuwa kuna Mwanamke anaitwa Selina na yupo ndani ya Benki,ย yeye pekee ndiye anayefahamu ilipo chemba ya siri. Chogoย alitoka akiwa ameshikilia Bunduki aina ya AK47ย
Mateka walikuwa wamekaa chini kando ya sehemu ya Mapokezi,ย alipofika aliulizaย
“Selina ni nani?” Ilikuwa ni sauti iliyojaa mamlaka sana,ย aliuliza kwa kumaanisha kuwa alikuwa akimuhitaji Mdada huyo.ย Selina mwenyewe aliposikia hivyo alijuwa ni kitu gani Magaidiย hao walikuwa wakihitaji, baadhi ya Magaidi sura zaoย walizificha Ila baadhi hawakuzificha akiweno Chogo ambayeย waliamini hawezi kutambulika kwa urahisi.ย
“Selina ni nani?” Aliuliza tena Chogo kisha aliiandaa bundukiย kwa lengo la kuleta kitishoย
“Mimi hapa” alijitokeza huyo aliyeitwa Selina akiwa amevaliaย sare za wafanyakazi wa Benki, alikuwa Mwanamke mmoja mzuriย mweusi mwenye rasta asilia.ย
“Mleteni” Alisema Chogo, mara moja Selina alisogezwa mahaliย aliposimama Chogo, Selina alionekana kuwa muoga sana, Chogoย alimwambia Selinaย
“Usiogope sababu una kazi moja tu ya kufanya, ukishamalizaย nitakuacha huru sawa?” Alisema akiwa anatabasamu, Selinaย aliitikia kwa woga kisha Chogo alisema
“Tuongozane” Alimpa ishara Selina amfuate kwenye moja yaย chumba.ย
Nje ya Benki polisi walizingira benki hiyo wakiwa na silahaย za moto huku wakiwa na tahadhari kubwa, walikuwa wakitumiaย kipaza sauti kuzungumza, Chogo alipofika Chumbani na Selinaย alimwambiaย
“Nisubirie hapa, naenda kuongea na polisi” Alisema kishaย alichukua AK47 na kuelekea nje ya Benki hiyo.ย
Kitendo cha Chogo kutoka nje ya Benki kilileta utayari kwaย polisi na vitengo vyote vilivyokuwa makini na Benki, Chogoย alitoka akiwa hajavaa shati, mwili wali wake ulijaa michoroย mingi, alionekana kujiamini sana huku polisi wakiambiana kuwaย wanapaswa kumsikiliza sababu alikuwa na mateka ndani ya Benkiย
Chogo alisimama katikati ya Barabara iliyotoka kivukoniย kwenda mjini kisha aliwauliza polisiย
“Mlitaka nitoke ndani, nimeshatoka, mlikuwa mnasemaje?”ย Aliuliza kwa ujasiri, kipaza sauti kilisikikaย
“Kwanza tunahitaji usalama wa mateka wote walio ndani yaย Benki, pili tunataka kujuwa mnahitaji nini?”ย
“Oooh! Siwezi kuuwa Raia ambao hawana kosa lolote, ilaย mkileta ujanja nitauwa kila Mtu ndani ya Benki, masaa 24ย yajayo nitaiachia Benki hii” Alisema Chogo kisha alirudiย ndani ya Benki, hakuna askari hata mmoja aliyejaribuย kumshambulia Chogo, moja kwa moja alienda kwenye kile chumbaย alichomuacha Selina, aliweka Bunduki pembeni kisha alifungaย mlango, Chogo alimtazama Selina kwa jicho la kumtamani sanaย ukizingatia sketi ya Selina ilikuwa imepasuka kidogo hivyoย paja lilikuwa njeย
Selina alikuwa mwingi wa kutetemeka, Chogo alimfuata Selinaย kisha alimtandika busu, alimshika matiti na Makalio, alimvuaย nguo Selina na kumbaka, baada ya kumaliza alimwambia Selinaย
“Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie wapiย ilipo chemba ya siri iliyohifadhi pesa za Kimarekani” Alisemaย Chogo akiwa anavaa nguo zake, alipomaliza alikuwa badoย hajapata jibu kutoka kwa Selina ambaye alikuwa akitetemekaย kwa wogaย
“Ukimya wako unaashiria kuwa ni bora ufe kuliko kusema ilipoย Chemba si ndiyo?” Aliuliza tena Chogo, safari hiiย alibadilisha sura yake na kujaza hasira
“Tafadhali usiniuwe, ipo chumba namba 43” Alisema Selinaย
LEO NIMEWEKA NDEFU SANA COMMENTS ZIKIWA CHACHE NARUDI KWENYE KUWEKA FUPI
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA SABA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
24 Comments
Leo kwel ni ndefu had nimefulai
Hongera
Nimeipenda
Haha admini usitunyanyase ww weka unay0jiskia fupi au ndefu ss tunas0ma t ๐
Leo Kweli Nimefrahia Saana Kuusoma Hii Story
Hongera san ni nzur na ya kuvutia unasoma lkin kam vile ni video ipo mbele yko unaiagalia๐ฏ
Hongera ndefu alafu tamu
Asante sana leo ndefu
Nzuri sana
Ndo kusema chogo alikua na ugwadu๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ
Nzur sana boss leo mzigo wa uhakika
Leo imefika mahala pake..
Mashaallah asante
Imekaa pouuuwaa
Aah Admin we nouma ,, Leo ndefu Hadi Raha๐ช
Apo sawa admin ๐ฅ๐ฅ
nzuri san
Ya Leo imekuwa ndefu pia nzuri..Bigup Sana Admin
Aisee kuipata yote tunabonyeza ngapi mkuu๐ ๐ ๐ โ ๏ธ
Story nzuri inavutia sana inanifanya kila saaa niwe naingia kwenye kundi kuitafta jitahdi luifanya iwe ndefu pia itoke kwa wakati
Mbona ya Saba hutoi Admin sio poa bwana
Tumesubir sana huweki
nzuri sana
7x51ai