Ilipoishia sehemu ya tatu
“Ndio, ni Mwanangu! Miaka mingi sasa tangia Martin alipofariki kwa ajali ya gari akiwa anaelekea Mjini, tangu siku hiyo sikuwahi kuamka na kukaa tena hata ongea yangu ilikuwa ya shida, Martin alikuwa ndiyo Mwanangu wa pekee niliyempenda, tumaini la Maisha yangu lilikuwa kwa Kijana wangu Martin baada ya Baba yake kufukiwa na kifusi huko Merelani akiwa anafanya kazi za mgodi” Alisema Mama huyo, kisha alimuomba Mjukuu wake amsindikize mahali.
“Nifuateni” Alisema Mama huyo ambaye alijitambulisha kama Mama yake Martin Gimbo ambaye alikuwa akitajwa kama gaidi kiongozi wa kundi la ESS. Endelea
SEHEMU YA NNE
Walizunguka nyuma ya nyumba, aliwaonesha kaburi la Martin Gimbo, kaburi hilo lilikuwa dogo tu kuashiri kuwa Martin alifariki akiwa bado Kijana Mdogo, hii iliwashangaza Faudhia na Mohd ambao ndimi zao zilikuwa kimya sana, Faudhia aliketi juu ya tofali moja akionesha kuchanganywa na maelezo ya Huyo Mama
“Hakuna aliyewahi kuja kumuulizia Martin Gimbo, nimeshtuka baada ya miaka mingi nyie kuja kumuulizia Martin, kwanini mmekuja kumuulizia?” Alihoji Mama huyo.
“Mama una hakika Martin amefariki?” Alihoji Mohd
“Ndiyo! Martin alizikwa hapa! Ilikuwa ni siku ngumu sana kwangu. Siku ambayo siwezi kuisahau katika Maisha yangu” Aliendelea kuelezea Mama Martin Gimbo, Faudhia alitoa picha ya Martin Gimbo kisha alimpatia Mama huyo ili kuona kama naweza akamtambua
Mama huyo aliiangalia picha kwa umakini sana, kisha aliwatazama Faudhia na Mohd
“Mnamaanisha nini?” Aliwauliza
“Mama, sisi ni Undercover kutoka kitengo cha Usalama wa Taifa, kama unavyojuwa sasa hivi tunakabiliwa na ugaidi hapa Nchini, huyo pichani ni mshukiwa namba moja, umemfahamu?” Alisema Mohd huku akiamuachia swali Mama huyo
Mama huyo aliirudia kuiangalia tena ile picha kisha alitikisa kichwa chake na kusema
“Anafanana na Martin! Lakini mbona Martin wangu alifariki miaka mingi iliyopita na alizikwa hapa” Alisema Mama huyo ambaye hali yake ilianza kubadilika baada ya kuanza kushtushwa na taarifa alizokuwa akizisikia
“Kifo cha Martin wako kilitokeaje?” Alihoji Faudhia haraka baada ya kutambua kuwa Mama huyo alikuwa kwenye hali mbaya ambayo ingepelekea kushindwa kuzungumza baada ya dakika kadhaa. Mama huyo alianza kusimulia ilivyokuwa siku ya kifo cha Mwanaye japo alikuwa akisimulia kwa shida
“Martin alipomaliza elimu ya sekondari, aliniaga kuwa anaenda kwa Baba yake Mkubwa huko Tabora, lakini majira ya mchana nilipokea taarifa kuwa gari alilopanda Martin lilipata ajali mbaya na kusababisha Mwanangu apoteze uhai, mwili wa Martin uliharibika mno ila kwasababu alipata ajali hapa hapa Arusha ilibidi aletwe kwa ajili ya maziko” Alisema Mama huyo huku akikohoa, chozi lilikuwa linambubujika
“Nani alitoa taarifa ya Kifo cha Martin?” Alihoji tena Faudhia kwa umakini sana, Mama huyo alikuwa na picha ambayo alipiga yeye na Mtu aliyetoa taarifa ya kifo cha Martin
“Huyu ndiye aliyenipigia simu, aliongozana na Watu wa Gari la kubebea maiti kuja hapa” Aliitoa picha iliyomuonesha Mtu aliyeenda na maiti ya Mwanaye Martin ikiwa imeharibika, Mohd aliiangalia picha hiyo kisha alimpatia Faudhia
Kilichomshtua Faudhia ni huyo Mtu aliyeleta maiti ya Martin Gimbo, hakuamini macho yake hadi presha ilimpanda, Mohd akamuuliza
“Unamfahamu huyo Mtu?” Aliuliza Mohd, Faudhia alimtazama Mohd kisha alisema
“Ndio namfahamu huyu Mtu, ni miaka mingi sana imepita sasa. Siamini kama baada ya makosa yale aliachiwa mapema hivyo” Alisema Faudhia, huku akirejea kuiangalia tena picha hiyo, alionekana Mzee Shomari ambaye alikuwa ni Baba wa kambo wa Faudhia akiwa amepiga picha na Mama yake Martin
“Huyu Mtu alikuja tena hapa?” Aliuliza
“Sikupata kumuona tena, hakuna aliyekuja hata kunipa pole, nilibakia Mimi na Dada yake Martin ambaye naye alifariki na kuniachia huyu Mjukuu” Alisema Mama yake Martin Gimbo.
“Mama una hakika kuwa huyu Mtu alikuja na Maiti hapa?”
“Ndio” alijibu Huyo Mama huku akianza kutetemeka kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimsibu.
“Faudhia, unahisia gani?” Alihoji Mohd
“Kwa jinsi nilivyoishi na Mzee Shomari, simulizi nilizosikia kuhusu yeye na matukio aliyoyafanya, napata mashaka kuwa huwenda yeye ndiye aliyemtengeza Chogo kuwa gaidi, sina uhakika na ninachokihisi lakini hisia zangu zinaweza kunipa majibu kutokana na picha hii, mwaka ambao Martin amefariki ni miezi michache baaada ya Mzee Shomari kufungwa kwa kosa la
Mauwaji huko Mbeya, najiuliza aliweza vipi kutoka? Kwa vyovyote yupo mfadhili katika haya yote, hayupo peke yake” Alisema Faudhia.
•••••••••••••••••••••••••••••••••
Jioni ilikuwa imeshangia, Chogo alikuwa ndani ya Benki hiyo, aliagiza Diana aende ndani ya Benki kuu. Muda huu alikuwa ndani ya chumba cha kuhifadhia pesa, chumba hicho kilikuwa na mateka wawili, Gavana na Mke wake ambao walikuwa wamefungwa kamba kwenye mikono yao.
Chogo alikuwa akiweka risasi kwenye Bastola yake, Mwanaume huyo alikuwa mweusi mwenye kipara, Gavana alimuuliza Chogo
“Mnataka nini?” Chogo hakujibu swali la Gavana
“Nakuuliza wewe, kwanini mmetuteka mnataka pesa?” Aliuliza tena Gavana wa Benki kuu
Chogo alikasirika kisha alimfuata Gavana kwa hasira akamshika shingoni
“Hata ukijuwa sababu huwezi kulipa kwa chochote, thamani ya nilichokipoteza haiwezi kufananishwa na pesa yenu chafu iliyojaa damu” Alisema Chogo kisha alimuachia Gavana ambaye alianza kukohoa
“Ukirudia tena kuuliza maswali ya kipuuzi nitakata shingo yako” Chogo alisema kisha alinyanyuka na kurudi alipokuwa amekaa, kisha alipomaliza kuweka risasi kwenye Bastola aliondoka chumbani hapo, Gavana alimsogelea Mke wake ambaye alikuwa akilia tu huku akisema
“Naogopa sana sijui hatma itakuwaje, sijui kesho itakuwa vipi!” Alisema maneno yaliyomfanya Gavana aseme
“Sesilia huna sababu ya kulia maana hata kama ukifanya hivyo huwezi kubadilisha chochote kile, cha msingi ni kuangalia tunafanya kitu gani” alisema Gavana
“Tutafanya nini mbele ya hawa Watu walioizidi akili Serikali? Sisi wawili hatujapitia hata mafunzo ya ujeshi hata mgambo tutafanya nini mbele yao?” Alisema Mke wa Gavana aliyejulikana kama Sesilia, Gavana alijisogeza kwa Mke wake akamwambia
“Unaiona ile meza ndogo?” Alisema Gavana huku akimuonesha Mke wake
“Ndio naiona” alijibu Mke wa Gavana
“Nyuma yake kuna Chemba ndogo ambayo kama ukiifikia na kubonyeza basi chumba hiki kitazungukwa na ngao ya Umeme, hawataweza kuingia humu tena kisha hapo hapo kuna swichi ambayo ukiibonyeza inazibua ukuta sababu pale kuna mlango wa siri sana” Alisema Gavana kisha Mke wake alimtazama Mume wake sehemu ya Mguu na kuona jinsi damu ilivyokuwa ikimmwagika Gavana.
“Mguu wangu una maumivu makali sana, unapaswa kufanya hivyo Sesilia vinginevyo tutafia humu” Alisema Gavana lakini alitambuwa kuwa Mke wake alikuwa mwenye woga sana, alikuwa akitetemeka na kulia, kabla hawajazungumza chochote aliingia Mlinzi kwa ajili ya kuwaangalia Gavana na Mke wake, maongezi yalikoma hapo baada ya kumuona Mlinzi.
Upande wa pili, ndani ya Ghorofa la China plaza maeneo ya Karume, floo ya mwisho kabisa, alionekana Mzee mmoja mwenye mvi nyeupe na kitambi, Mzee huyo alikuwa akizungumza na simu
“Hakikisha taarifa inatoka sasa hivi” Alisistiza Mzee huyo kisha alikata simu, alipogeuka nyuma yake alikuwepo Diana rafiki wa Faudhia, Mzee huyo alikuwa ni Mzee Shomari. Diana alionekana kutaka kusema jambo, Mzee Shomari alimkaribisha akae kwanza kisha alimpatia kinywaji
“Vipi mpango umeenda sawa?” Aliuliza Mzee Shomari
“Faudhia amekwepa mtego wa kifo, yupo Arusha anamfuatilia Martin Gimbo” alisema Diana
“Shit!!” Alisema Mzee Shomari
“Wameenda hadi shule aliyosoma Martin lakini Mkuu wa Shule alifanya kama tulivyomwambia lakini walimuuwa” Alielezea tena Diana
“Hakikisha Utambulisho wa Chogo haufahamiki, tuma Watu wamuuwe Mama yake Chogo, endapo Chogo atafahamu kuwa tumemdanganya basi ngoma itakuwa ngumu sana, ni lazima tufanikishe mpango ulio mbele yetu haraka sana” Alisema Mzee Shomari, haraka Diana alinyanyua simu na kumpigia Mtu
“Uwa panya bila kelele” Alisema Diana, Mzee Shomari akiwa amekaa kwenye kiti cha walemavu alitabasamu sana kisha alisema
“Nakuaminia sana Mtoto wangu, hakika wewe ni simba jike unayewinda kimya kimya” Alisema Mzee Shomari
“Siku zote nimeishi na kisasi ndani ya moyo wangu, kifo cha Mama yangu ni lazima Faudhia akilipie, nafanya yote kuhakikisha Mama yangu anafurahi huko alipo” Alisema Diana
“Na siku zote Muuwaji hawezi kuishi, ndiyo maana nilikutoa gerezani ili uje kuitafuta haki iliyoporwa na Faudhia” Alikazia Mzee Shomari kisha alimruhusu Diana kuelekea ndani ya Benki, mpango wa Mzee Shomari ulikuwa ni Kumuuwa Faudhia, kisha kuiba pesa za kimarekani ambazo zilihifadhiwa ndani ya Benki hiyo katika chemba ya siri, ilikuwa ni zaidi ya Dola Bilioni 900 , alimtumia Chogo kama ngao ya kufanya mambo yake huku akiweka ubia na rafiki yake wa zamani ambaye alikuwa akiishi Uholanzi, ndiye aliyemtoa jela na kumfadhili pesa za kufanya ugaidi Tanzania, hivyo Mzee Shomari alikuwa ndiye Gaidi aliyekuwa akiratibu mipango yote, alikusanya vijana na kuwapatia silaha nzito, akiwemo Diana na Martin Gimbo maarufu kama Chogo
Jinsi alivyowapata Diana na Chogo utakuja kufahamu mbele, hebu tosonge..
Usiku ulikuwa umeingia, ndani ya Jiji la Arusha, Faudhia alikuwa akimlaumu Mohd kwa kosa la Kumuuwa Mama yake na Martin Gimbo.
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NNE
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
9 Comments
Ya 5🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🔥🔥🔥💪🏽💪🏽💪🏽
Nouuuuumaaaa
Duuuh kwa hyo mohd nae ni mmoja wa magaidi au next plz
aaaaaah! muongeze kdg hii ni 🌤🔥🔥
Mbona fupi ila 🔥🔥🔥
𝑱𝒐𝒎𝒐𝒏𝒊 𝒚𝒂 5 𝒊𝒔𝒊𝒄𝒉𝒆𝒍𝒆𝒘𝒆,,,,𝒊𝒘𝒆 𝒏𝒅𝒆𝒇𝒖 𝒏𝒅𝒆𝒇𝒖
https://shorturl.fm/eAlmd
https://shorturl.fm/MVjF1
https://shorturl.fm/PFOiP