Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Pili-02)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Kwanza-01)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi Na Moja-11)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Kwanza-01)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Kwanza-01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 27, 2025Updated:May 28, 202517 Comments7 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mzee Shayo alikuwa ameketi katika kiti chake huku akitingisha  mguu wake ambao ulikuwa ndani ya kiatu cheusi chenye kung’aa  sana. Mbele yake kulikuwa na picha halisi ya matukio  yaliyokuwa yakiendelea kurindima, taarifa za Habari kutoka  Aljazeera, DW, Sky News zilikuwa zikirusha kuhusu matukio  yaliyokuwa yakiendelea Nchini humo. Pembezoni kulikuwa na  bendera ndogo ya Tanzania iliyokuwa ikipeperushwa na upepo wa  feni ya juu. 

    Chozi lilimbubujika Mzee Shayo, simu zake zilikuwa bize kuita  lakini hakuzipokea sababu alikuwa katika msongo mzito wa  mawazo. 

    Hadithi inaanzia katika Eneo la Majengo pacha, Posta Jijini  Dar-es-salaam ilipo Benki kuu ya Tanzania, kutokana na hali  ya machafuko ulinzi mkali unaimarishwa kuhakikisha hakutokei  wizi wa aina yoyote ile, Gavana wa Benki hiyo aliyejulikana  kama Profesa Maliki anafikiria kukiondoa kiasi kikubwa cha  pesa kwa kutumia ndege ya Shirika la Emirates kuelekea Nchini  Marekani. 

    Akiwa ofisini ndani ya Benki hiyo alijaribu kumpigia simu  Mkuu wa kitengo cha Usalama wa Taifa aliyeitwa Ezekiel Shayo  maarufu kama Mzee Shayo, simu yake haikupokelewa, taarifa  aliyokuwa nayo Mzee Shayo wakati huo akiwa katika ofisi yake  ya Usalama ilikuwa ni kutekwa kwa Jiji la Dodoma na kundi  dogo la kigaidi lililofahamika kama ESS 

    “Bado hajapokea simu?” Aliuliza Waziri Mkuu wa Tanzania  alipokuwa akizungumza na Profesa Maliki ili kuangalia  uwezekano wa kuhamisha fedha hizo 

    “Hapokei simu yake, napata mashaka kama yupo hai au amekufa”  Alijibu Gavana huyo huku kukiwa na taarifa kuwa majira ya  Mchana Benki hiyo itavamiwa na kundi hilo la ESS ambalo  lilikuwa likiongozwa na Mtu mmoja aliyefamika kwa jina moja  tu la Chogo.

    “Umezungumza na Waziri wa Ulinzi?” Aliuliza Waziri huyo  aliyeitwa Jackson Ikuda 

    “Ndio, ameniongezea ulinzi hapa” alijibu Profesa Maliki kwa  sauti iliyoonesha kuwa alikuwa ni mwenye kukata tamaa 

    “Andaa Magari hakikisha kiasi kikubwa cha fedha kinahamishwa  hapo, naelekea Ikulu. Mengine nitakupa taarifa baada ya  kuzungumza na Mkuu wa Nchi, ndege zipo tayali, kilichobaki ni  wewe kuhamisha fedha tu” Alisema Waziri Jackson Ikuda. 

    Upande wa pili yaani kule ofisini kwa Mkuu wa Kitengo cha  usalama wa Taifa kwa Mzee Shayo, alikuwa ameshasimama huku  akiziangalia ‘Screen’ zilizo mbele yake, zilikuwa zikionesha  baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar-es-salaam, Benki kuu ilikuwa  ikionekana kwa kutumia kamera iliyopewa jina la Nyati. 

    “Upsss!” Aliwaza na kuwazua nini afanye ili kuhakikisha  anazuia jaribio la kuvamiwa kwa Benki kuu ya Tanzania. Muda  huo huo simu yake iliita akiwa ametumbua macho yake aliona ni  namba ngeni ikiwa inaita, alitoka chumba cha kuongoza kamera  alirudi ofisini kwake. Alijitupa kitini huku akiitafakari  simu hiyo iliyopigwa kwa kodi za nje ya Nchi 

    “Hello!” Aliitika Mzee Shayo baada ya kuwa ameiweka simu  sikioni huku kijasho chembamba kikiwa kinamtiririka, ilikuwa  ni sauti iliyoonesha ukomavu wa maigizo sababu kiukweli Mzee  Shayo pamoja na ukuu wake wa kitengo lakini hakuwahi  kukumbana na nyakati ngumu kama hizi. 

    “Shayo!” Ilisikika sauti nzito kiasi iliyoambatana na uvutaji  wa hewa kama vile alikuwa akivuta sigara, Mzee Shayo alikaa  kimya kumsikiliza mpigaji ambaye alikuwa akiongea kwa  kupangilia sana maneno yake. 

    “Nilikwambia kitengo hakiwezi kuzuia chochote nilichokipanga,  sio jaribio tena baada ya kuliteka Jiji la Dodoma sasa ni  zamu ya Dar-es-salaam” alisema Mwanaume huyo ambaye jina lake  halikutajwa 

    “Wewe ni Nani na unataka nini hasa?” Alihoji Mzee Shayo huku  akimuita msaidizi wake aweze kuangalia simu hiyo ilipigwa  kutokea wapi. 

    “Shayo! Ni Mimi rafiki yako katika Ujenzi wa Taifa hili,  Miezi kadhaa iliyopita nilikuwa nikikutumia Barua pepe kuwa  Kitengo chako ni dhaifu sana mjiandae kwa kazi maalum!!”  Alisema Jamaa huyo kisha alicheka sana

    “Unahitaji nini sasa?” Aliuliza Mzee Shayo huku mkono wake  ukiwa unatetemeka, msaidizi wa Mzee Shayo aliligundua hilo,  hakuamini kama Mzee huyo alifikia ukomo wa kuweza kufikiria  sababu alikuwa na sifa nyingi zilizotukuka ndani ya Taifa  hili. 

    “Siku moja nitakupa hadithi ya kusisimua sana kabla hujafa  Shayo! Naitwa Chogo” Alisema kisha alikata simu haraka, muda  huo huo simu ya Chogo ilikuwa imefanikiwa kutambulika kuwa  alikuwa akiongelea kutokea wapi lakini cha ajabu na  kilichomshangaza na kumuogopesha Mzee Shayo, simu ya Chogo  ilipigwa kutokea pale pale makao makuu ya Kitengo cha Usalama  wa Taifa. 

    “Mkuu simu imepigwa hapa hapa kutoka chumba cha kuongoza  Kamera za Jiji hili” Alisema msaidizi wa Mzee Shayo, haraka  Mzee Shayo alikurupuka kuelekea chumba cha uongozaji wa  Kamera hizo. 

    Pembezoni kwenye meza moja kulikuwa na simu juu yake, simu  hiyo ilikuwa ikiita. Mzee Shayo aliifuata na kuiokota kisha  aliipokea haraka, ilisikika sauti ya Chogo ikisema 

    “Nilikwambia kitengo chako ni dhaifu sana Mzee Shayo,  Najiuliza kitengo kinachosimamia usalama wa Nchi kinakuwa  legelege namna hiyo!” Alisema Chogo, haikujulikana huyo Chogo  alikuwa ni nani na hata picha yake haikuweza kupatikana zaidi  ya sauti ambayo ukiisikiliza vizuri utagundua ilikuwa  imechezewa. 

    Haraka Mzee Shayo alipata wazo la kutazama Screen zilizokuwa  zikionesha baadhi ya maeneo ya Jiji, simu ilikuwa hewani,  akili yake ilifanya kazi mara mia zaidi ya uwezo wake wa  kawaida 

    “Niwekee kamera Nyati haraka sana” Alisema Mzee Shayo huku  akiwa amekata kinasa sauti kwenye simu hiyo alafu  akakirudisha huku akiwa makini kuitazama kamera nyati, mara  moja simu ilikatwa 

    “Rudisha nyuma rekodi ya Kamera nyati kwa dakika mbili  zilizopita” Alisema Mzee Shayo baada ya kuanza kuhisi jambo,  muda ambao alikuwa akizungumza na Chogo alikuwa akisikia  sauti ya Pantoni, hivyo haraka alihisi Chogo alikuwa karibu  na eneo la Benki kuu. 

    “Simamisha, vuta hiyo picha” Alisema Mzee Shayo baada ya  kumuona Mtu aliyevalia koti la Njano akiwa anazungumza na  simu huku akiwa amesimama mbele ya Benki hiyo.

    “Ni nani huyo?” Aliuliza Mzee Shayo, haraka kitengo husika  kilianza kazi ya kuifahamu sura hiyo ilikuwa ni sura ya Nani. 

    “Anaitwa Martin Gimbo mkazi wa Mkoa wa Arusha, miaka 34”  Alisema Mtaalamu huyo huku akiwa anampatia picha Mzee Shayo 

    “Piga simu kwa Gavana wa Benki kuu profesa Maliki haraka sana  kisha niwekee niongee naye” alisema Mzee Shayo akiwa ndani ya  suti nyeusi, ya mikono mifupi maarufu kama Kaunda suti. 

    “Maliki, kuna Mtu ameingia hapo amevaa koti la njano, jinzi  nyeusi, hakikisha anakamatwa haraka sana” Alisema Mzee Shayo,  kabla hata Profesa Maliki hajajibu chochote zilisikika alamu  kuashiria kuwa tayali kulikuwa na hali ya Hatari 

    “Tumevamiwa” alijibu Profesa Malikini kisha mawasiliano  yalikatika. 

    “Ni yeye” Alisema Mzee Shayo huku akiwa anakuna macho yake. 

    “Weka kamera nyati kwenye kioo kikubwa” Alisema Mzee Shayo  akionekana kupagawa kwa namna Benki kuu ilivyovamiwa na Mtu  aliyeitwa Chogo. Muda huo huo simu iliita kwa Mzee Shayo,  aliipokea, sauti iliyosikika ilikuwa ni sauti ya Chogo  ikisema 

    “Nipo mahali ambapo utajiri wa Nchi unapatikana, ni muda wa  kufanya nilichokwambia kwa Barua pepe zangu ambazo ulikuwa  ukizipuuza” Alisema Chogo kisha alikata simu. 

    Maongezi yaliamuacha Mzee Shayo akiwa Hoi bin taabani,  alirudi nyuma kisha aliketi kwenye kiti, ilikuwa ni majira ya  saa 6 Mchana, Jiji la Dar-es-salaam lilizizima kwa muda  mchache tu baada ya taarifa kuwa Benki kuu ya Tanzania ( BOT)  imevamiwa na gaidi aliyeitwa Chogo, kupitia kamera nyati  walifanikiwa kuliona gari jeupe likiingia ndani ya benki hiyo  kupitia Geti la nyuma 

    “Mkuu gari hili si la Benki, ni gari spesho. Hapana shaka  Magaidi ndio wanaingia” Alisema msaidizi wa Mzee Shayo!! 

    “Shika hatamu kwasasa hapa ndani Gibson, natoka mara moja”  Alisema Mzee Shayo, aliondoka Kitengo cha Usalama wa Taifa  akiwa ndani ya gari ndogo aina ya Subaru! Alipofika getini  alisimama kisha alilitazama jengo la Usalama wa Taifa ambalo  

    lilikuwa chini huku juu yake kukiwa na kanisa la KKT, kitengo  kilikuwa eneo la Kigamboni.

    Kupitia daraja la Kigamboni, Mzee Shayo aliendesha Subaru  kama yupo kwenye mbio za Magari, wakati huo Barabara zilikuwa  nyeupe, Watu wengi waliogopa kupoteza uhai wao, walibakia  majumbani mwao huku wachache wakiendelea kufanya safari,  ilimuwezesha Mzee Shayo kufika Ikulu ya Magogoni haraka sana,  alikuta ulinzi umeimarishwa hapo lakini alipowatazama Walinzi  hao alijikuta akikata tamaa, aliona ni ngumu sana kupambana  na huyo Mwanaume anayeitwa Chogo .  Nini Kitaendelea

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Riwaya ya Goryanah riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia

    17 Comments

    1. Mama eddy on May 27, 2025 5:26 pm

      Haiyaaaaa , lakin admin story fupi sana et

      Reply
      • Luccah on May 27, 2025 6:21 pm

        Ila ch0g0 😆

        Reply
    2. Josephat on May 27, 2025 5:47 pm

      Chogo kaxhawasha moto uko 🔥🔥🔥🔥

      Reply
      • Adam on May 27, 2025 7:59 pm

        Daaaah

        Reply
    3. Markson on May 27, 2025 6:46 pm

      Chogo hachekesh🤣

      Reply
    4. Hamisi halidi on May 27, 2025 7:01 pm

      Chogo uku kakiwasha aah

      Reply
    5. Kyoma on May 27, 2025 7:22 pm

      Chogo kama chogo

      Reply
    6. Alex on May 27, 2025 7:31 pm

      Mbn hujamalizia riwaya iliyopita admin

      Reply
    7. Horace550 on May 27, 2025 8:58 pm

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    8. Helena830 on May 27, 2025 11:31 pm

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    9. Brylee4061 on May 28, 2025 7:14 am

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    10. Quentin1858 on May 28, 2025 7:15 am

      https://shorturl.fm/m8ueY

      Reply
    11. KingzJeelay on May 28, 2025 7:58 am

      Shida stori inaanza sterling anakurupuka badala ya kutumia plan za kijasusi😀😀
      Anyway ngoja tusubir mwendelezo huenda tukapata yaliyo mazur zaiz🔥🔥🔥

      Reply
    12. Cathbert on May 28, 2025 6:37 pm

      Let mambo

      Reply
    13. Corey3267 on May 29, 2025 1:36 am

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    14. Morgan3482 on May 29, 2025 2:19 am

      https://shorturl.fm/a0B2m

      Reply
    15. Ashton2806 on May 29, 2025 3:43 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi May 28, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Pili-02)

    Ilipoishia  Kupitia daraja la Kigamboni, Mzee Shayo aliendesha Subaru  kama yupo kwenye mbio za Magari,…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Kwanza-01)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi Na Moja-11)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi-10)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.