Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tatu (03)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tatu (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 13, 2024Updated:October 28, 202414 Comments10 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Yaani Mama kisa tu ana hela basi umechanganikiwa kiasiย  hicho, kweli umasikini mbaya sana Mama, ila usijali siku siyoย  nyingi nitaanza kazi nitakufanyia kila kitu, sawa Mama?”ย 

    “Mmh! Sawa” Mama alisema kisha aliondoka zake ila aliniachaย  na jambo la kufikiria ndani ya akili yangu, nilikumbukaย  kitendo chake cha kuondoka pale wodini baada ya Mossesย  kuingia, ila ni yeye ndiye aliyempigia simu Mosses baada yaย  kuchukua namba kwenye simu yangu.ย  Endelea

    SEHEMU YA TATU

    Sikutaka sana kuanza kufikiria hilo jambo, niliona ni boraย  niwasiliane na Mosses maana baada ya kuachana naye kuleย  Hospitali sikuongea naye kabisa, simu ya Mosses ilikuwaย  imezimwa, ilinipa maumivu makali sana ndani ya moyo wangu,ย  nilijigeuza geuza kisha Usingizi ulinichukua.ย 

    Kulipopambazuka nilianza kuhisi hali ya tofauti, mwiliย  ulianza kuchoka hadi nilijishangaa, Mama aliendeleaย  kunihudumia huku akiendelea kutafuta uwezekano wa kupataย  Figo, alienda kwa daktari ambaye aliunganishwa na Osman,ย  upatikanaji wa Figo ulikuwa mgumu sana huku hali yanguย  ikizidi kudhohofu, nilikuwa napewa dawa tu nimeze, maumivuย  niliyokuwa nikiyasikia kwenye tumbo langu yalikuwa makaliย  sana nilitamani hata kufa kabisa, kwa siku zote hizoย  sikumuona wala kumpata Mosses kwenye simu, ilizidi kunifanyaย  niwe mgonjwa zaidi.ย 

    “Mama Mosses hapatikani leo siku ya kumi na mbili”ย  Nilimueleza Mamaย 

    “Usijali pengine amepatwa na tatizo kama hapa anapajuwa basiย  atakuja siku moja” Alisema Mama, angalau alinipa moyo naย  tumaini, lakini nilimuuliza

    “Haya maumivu makali yanatokana na nini Mama? Mwili wanguย  hauna nguvu kabisa nazidi kudhohofu” Nilipomuuliza nilionaย  macho ya Mama yaliyojaa maumivu, alitamani kulia lakiniย  hakusema shida iliyokuwa ikinisumbuaย 

    “Utapona Mwanangu! Mungu ni mwingi wa huruma, atakujalia afyaย  njema Binti yangu” Alisema Mama kisha alininywesha ujiย 

    “Hivi umewasiliana na Osman Mama?” Nilimuuliza Mamaย 

    “Ndiyo usiwe na wasiwasi ukipona tu utaanza kazi, pumzika kwaย  sasa” Mama alikuwa ameshamaliza kuninywesha uji, alinifuta naย  kuondoka zake, alipofika chumbani kwake alilia sana sababuย  tumaini la Mimi kupona lilikuwa hafifu sana, siku zilisogea.ย 

    Mama pamoja na daktari walijitahidi kutafuta Mtu wa kunitoleaย  Figo, walitangaza dau kubwa kadili siku zilivyokuwa zikiendaย  ila waliojitokeza walikuwa ni Watu wenye Afya zisizoridhisha,ย  figo zao pia zilionekana kuwa na Hitilafu, hazikufaa.ย  Ilipofika siku ya 20 nilipekwa Hospitalini nikiwa katika haliย  mbaya sana, nilikuwa sijitambui kabisa. Mama yangu alikuwaย  Mtu wa kulia kila wakati, pesa ilipatikana kwa ajili ya Figoย  lakini mtoaji wa figo hakupatikana, daktari alimwambia Mamaย 

    “Hakuna namna tunaweza kufanya, nahisi kukata tamaa Mamaย  Jacklin” Alisema Daktari wakiwa ofisini kwa Daktari huyoย  aliyeitwa Dokta Simonย 

    “Unaposema hivyo daktari unanipa wakati mgumu wa kuangaliaย  mbele, sitaki kuamini kama siku za kuishi za Jacklin zimefikaย  mwisho, Huyu ndiye Binti yangu wa pekee, sisi ni masikiniย  sana, basi toa figo yangu kwa ajili ya Binti yangu” Alisemaย  Mama, ilifika wakati ambao Mama alishindwa kuhimili maumivuย  aliyokuwa akiyasikia katika kifua chakeย 

    “Mama Jacklin, umri wako na hilo jambo haviwezi kwendaย  sambamba. Najuwa tumaini ni dogo sana katika jambo hili,ย  lakini…”ย 

    “Dokta, kama kufa Mimi kutamsaidia Binti yangu hilo siyoย  tatizo, hajawahi kuishi Maisha ya furaha katika Maisha yake,ย  ndiyo kwanza alikuwa amepata kazi….leo afe aaaah hapana”ย  Alisema Mama akiwa analia, alionesha uchungu wake kwanguย 

    “Sawa Mama! Ngoja tuiangalie kama itafaa” Alisema Doktaย  Simon, kisha waliongozana hadi chumba cha Uchunguzi. Mamaย  alitakiwa kufanyiwa uchunguzi wa figo yake ili niwekewe Mimiย  nipate kunusuru Maisha yangu ambayo yalikuwa hatua za mwishoย  sana.

    Huu ndiyo upendo ambao Mama huwa nao kwa Mtoto wake,ย  watakukimbia wote katika Maisha lakini Mama yako atasimamaย  kwa ajili yako kila siku za Maisha yako, Mama alianzaย  kufanyiwa uchunguzi. Bahati mbaya figo ya Mama ilikuwa naย  Mawe hivyo isingeliweza kunifaa, Mama alilia sanaย 

    “Dokta weka hiyo hiyo ili Jacklin aamke, tumaini langu niย  yeye pekee” Mama alilia hadi Dokta Simon alidondosha Choziย  lakeย 

    “Mama usilie, tuna siku 10 zilizobakia, Mungu atafanya wepesiย  wa hili jambo, kwasasa Jacklin anahitaji Maombi” Alisemaย  Dokta Simon, Mama alifikiria afanye nini, alichukua namba yaย  Mosses kisha aliipiga akiwa Hospitaliniย 

    Bahati nzuri siku hiyo simu ya Mosses iliita aliipokea, Mamaย  alimueleza Mosses hali ya afya yangu kwa wakati huo, Mossesย  alimwambia Mama kuwa alipata tatizo ndiyo maana alishindwaย  kuja akaahdi kuwa atakuja Hospitalini. Kweli, Mchana Mossesย  alifika Hospitalini, aliishuhudia hali ya Afya yangu ambayoย  alisimuliwa kama hadithi za Amza Stories, alikubali kuwa Mimiย  nilikuwa mgonjwa sana kwa jinsi nilivyodhohofu, pumua yanguย  ilikuwa ya shida mnoย 

    “Hali ndiyo hiyo, leo siku ya tatu haongei wala hafumbuiย  Macho. Kama unampenda Jacklin jitolee Mosses Mungu atakulipaย  kwa wema wako” Mama alisema, walikuwa wodini wakiwa na yuleย  Daktari Simonย 

    “Mama Mimi nitajitoa kwenye nini tena ikiwa mmetangaza dauย  kubwa na bado figo haijapatikana, tumuombee Jacklin pengineย  Mungu atampa nafuu” Alisema Mossesย 

    “Kuomba tunaomba lakini hatuwezi kukaa kimya bila kufanyaย  jitihada zozote Baba, mimi leo siku ya tatu sijala chochote,ย  nione sina raha kwasababu ya Jacklin” Alisema Mama hukuย  akibubujika Mchozi, Dokta Simon aliingilia kati akamwambiaย  Mossesย 

    “Ndugu najuwa inaweza kuwa ngumu kwako lakini kama huyu Mtuย  ana umuhimu kwako jitolee figo moja kwa ajili ya kumuamsha”ย  Alisema Dokta, Mosses alishtuka akaulizaย 

    “Nitoe nini?”ย 

    “Figo kwa ajili ya Mpenzi wako” Alijibu Dokta Simon huku Mamaย  akiwa analia pembeni,

    “Nitoe figo? Hiyo ni hatari sana Dokta nitafanya vyote lakiniย  siyo kutoa figo yangu, ingekuwa wote wanaopendana wanatoleanaย  viungo basi hii Dunia ingejaa walemavu kila kona” Alisemaย  Mosses, Maneno yake yalimchukiza sana Mama alinyanyuka naย  kumpiga kofi Mossesย 

    “Mama hupaswi kufanya hivyo hapa ni Hospitalini istoshe niย  wodini ambako panahitaji utulivu sana” Alisema Dokta Simonย 

    “Dokta huyu ni mshenzi anawezaje kusema maneno ya kikatiliย  namna hiyo hakuona neno lingine la kusema? Huyu si ndiyeย  ambaye alikuwa akikupa furaha, leo amelala hujali tena siย  ndiyo?” Alihoji Mama huku akiwa anahema juu juuย 

    “Unathubutu vipi kunipiga Mimi? Unanijuwa Mimi? Kama Maishaย  yake ni muhimu kwangu basi hata kwako ni Muhimu kwanini weweย  usitoe hiyo figo? Siwezi kutoa kiungo kisa Mapenzi tena kwaย  kiumbe anayeitwa Mwanamke, Jacklin akipona Mimi nipo akifaย  Maisha yataendelea” Alisema Mosses kisha aliondoka Wodini,ย  Mama alilia sana, kauli ya Mosses ilizidi kumfanya akateย  tamaa, Dokta Simon alimwambia Mamaย 

    “Siku bado zipo tuzidi kufanya jitihada na Maombi” Alisemaย  kisha aliondoka zake, Mama aliendelea kulia kwa kukata tamaaย  alinisogelea akasemaย 

    “Jacklin nimekuzaa kwa shida sana, nimekulea kwa tabu mno,ย  leo nakupoteza Mama kwa shida sana, Nisamehe Mama yakoย  nimefanya jitihada zote lakini nimeshindwa Mimi sababu hataย  Mungu hayupo upande wangu tena” Maneno ya Mama niliyasikia,ย  Chozi lilinivuja, sikuwa na nguvu ya kufanya chochote kileย 

    โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขย 

    Ndani ya Dubai, Kilichompeleka Osman Dubai kilikuwa niย  kumtafuta Zahra, achana na kiasi kikubwa cha pesa ambachoย  Mwanamke huyo aliondoka nacho na kwenda huko kuishi naย  Mwanaume mwingine, Osman alikuwa akimpenda sana Mwanamkeย  huyo, jitihada za kumpata Zahra ziligonga mwamba. Alirudiย  Nchini, aliitafuta Familia ya Zahra lakini wazazi wa Zahraย  walionekana kufurahia ambacho Bitni yao alikifianya.ย 

    Hawakuwa na huruma, Osman alijitoa sana kuhakikisha Maisha yaย  Wazazi wa Zahra yanakuwa bora, aliwajengea jumba la kifahari,ย  aliwanunulia magari ya kutembelea, alibadilisha Maisha yaoย  kwa kiasi kikubwa sana, Osman aliondoka na kwenda kwenyeย  gari, alikumbuka jinsi ambavyo aliishi kwa furaha na amani naย  Zahra, alilia sana, Maumivu yalijaa ndani ya kifua chakeย  alipoikumbuka meseji ya mwisho ambayo Zahra aliituma, mesejiย  hiyo ilisema

    “Osman! Najua ujumbe wangu utakupa maumivu makali sana lakiniย  inabidi uupokee sababu ndiyo maamuzi yangu, asante kwaย  kubadilisha Maisha ya Wazazi wangu kwa kiasi kikubwa lakiniย  hukuwa chaguo la Moyo wangu japo ulinipenda sana, kwasasaย  mimi nipo Dubai na Mwanaume ambaye ninampenda. Usiwazumbueย  wazazi wangu wala usinitafute, pesa zote zilizo kwenyeย  akaunti yako ya Benki nimezichukua, unaweza kujiona Mjingaย  lakini hiyo ndiyo nguvu ya Mapenzi ambayo ninayo, nilikufanyaย  ukawa dhahifu kwangu! Nakutakia Maisha Mema, ni Mimi Zahra”ย 

    Ulikuwa ndiyo ujumbe wa Zahra baada ya hapo simu yakeย  haikupatikana tena,, alipoupata ujunbe huo Osman alipotezaย  fahamu akaenda kuzinduka kwenye Hospitali ya Dokta Simon,ย  aliishi Maisha yaliyojaa maumivu na aliapa kuwa hatokujaย  kupenda tena.ย 

    Basi, alifuta chozi akiwa ndani ya gari yake ya kifahari,ย  alipotoka kwa Wazazi wa Zahra alikuja moja kwa mojaย  Hospitalini maana aliwasiliana na Mama na akaambiwa kuwa haliย  yangu siyo nzuri na haina tumaini.ย 

    Alimkuta Mama akiwa analia nje, Osman alimuuliza Mama “Hali yake kwasasa ipoje Mama?” Alimuuliza baada ya salamย 

    “Kama nilivyokueleza Baba, hali ya Jacklin ni mbaya sana,ย  ninahofu juu ya uhai wake” Alisema Mama akiwa anaendeleaย  kumwaga choziย 

    “Pole Mama, wakati mwingine Dunia inakuwa katili sana, naombaย  nikamuone” Alisema Osman, walirudi wodini, Osman aliponionaย  hakuamini kama ni Mimi ndiye niliyemchachafya siku kadhaaย  zilizopita, nilikuwa nimekonda sana, nilikuwa nikipumua kwaย  shida sana, alidondosha chozi akamuuliza Mamaย 

    “Upatikanaji wa figo?” Mama alitikisa kichwa kuashiria kuwaย  hakukuwa na uwezekano wa kupatikana figo kabisa japoย  zilisalia siku 10ย 

    “Nitarudi Mama” Osman alitoka haraka akaelekea ofisini kwaย  Dokta Simon.ย 

    “Bilonea Kijana karibu sana” Alisema Dokta Simon sababuย  alikuwa akimfahamu sana Kwa ukaribu Osmanย 

    “Dokta Simon, Mama Jacklin amesema uwezekano wa kupatikanaย  Figo ni mdogo sana, nataka kusikia kutoka kwako!”ย 

    “Huo ndiyo ukweli Osman, kilichobakia ni kudra za Mwenyeziย  Mungu pekee, tumepima Watu wengi lakini hakuna hata mmojaย mwenye figo yenye afadhali alafu kibaya zaidi Mpenzi wa huyoย  Jacklin amegoma kufanya hivyo” Alisema Dokta Simonย 

    “Nitatoa Figo yangu” Alisema Osman, kauli hii ilimshtua sanaย  Dokta Simonย 

    “Unatoa figo yako? Umefikiria mara mbili Osman? Hii familiaย  inakuhusu nini wewe ikiwa mpenzi wa Jacklin amekataa, ufanyeย  hivyo wewe kama Nani? Umesahau kilichokutokea Osman?”ย  Aliuliza Dokta Simonย 

    “Natoa kama Binadamu niliyeguswa na hili Dokta Simon, Maishaย  ya yule Msichana ni tunu Kwa Mama yake, ni furaha kwenyeย  macho ya Mama yake ambaye muda wote analia. Umewahi kufikiriaย  jinsi Mama yule anavyokosa raha kwasbabu ya Binti yake?ย  Unajuwa ni furaha kiasi gani ataisikia endapo Binti yakeย  atasimama tena?” Aliuliza Osman kwa hisia kali sanaย 

    “Fikiria mara mbili sikushauri kufanya hivyo Osman, wewe niย  Bilionea Mkubwa hupaswi kuishi Maisha yenye kasoro kiasiย  hicho!”ย 

    “Mkamilifu ni Mungu pekee, nitatoa Figo yangu kuokoa Maishaย  yake” Alisema Osman kisha aliondoka akarudi Wodini, Doktaย  Simon hakukubaliana na uamuzi wa Osman alinyanyua simu naย  kuwapigia Wazazi wa Osman, aliwapata taarifa hiyo ambayoย  iliwakasirisha sana Wazazi wa Osmanย 

    Basi, Osman aliporudi alimwambia Mama kuwa nitapona na kuanzaย  kazi mara moja, japo Mama alikuwa katika hali ya huzuni sanaย  ila maneno ya Osman yalimjaza tumaini.ย 

    Alipotoka Hospitalini Osman alikuwa mwenye mawazo na maumivuย  makali sana, alipigiwa simu na Wazazi wake na kumtaka aachaneย  na mpango wa kutaka kutoa figo kwani haitokuwa na faidaย  yoyote kwake, Wazazi wa Osman waliamini kuwa Osman alikuwaย  akitaka kutoa figo kwa ajili ya Mapenzi, walinuonya sana kwaย  kile kilichomtokea kwa Zahra ila Osman aliwaambia Wazazi wakeย  kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na Mimi bali ni ubinadamu tuย  wa kutaka kuhakikisha afya yangu inaimarika.ย 

    Osman aliwasiliana na Hospitali nyingine ambayo ingefanyaย  operesheni ya kupandikiza figo kwenye mwili wangu, kutokanaย  na utajiri alionao aliweza kupata Hospitali Nchini India,ย  tulisafiri kwenda huko. Osman alishauriwa na kuambiwa kilaย  kitu kiafya kuhusu uamuzi wake.ย 

    Nini Kitaendelea? Osman atatoa FIGO? Usikose Sehemu Ya NNE Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย 

    Pumzi ya mwisho

    14 Comments

    1. Farnoush on October 13, 2024 4:21 pm

      Duuuh Osman ni mwanaume wa maana๐Ÿ˜‚

      Reply
      • Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 13, 2024 4:31 pm

        Ila sas ili ujue binadamu jau๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„ au ngoja …. nisiharibu uhondo siku ikifikia ntakwambiaa…hii tamthiliya inaweza kuliza watu huko mbele ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ me siyo mtabiri akin

        Reply
    2. Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 13, 2024 4:30 pm

      ๐Ÿ˜Ž mule mule baba admin…..hujai kosea

      Reply
    3. Tumpe on October 13, 2024 5:09 pm

      Sas huyu binti akitaka kutukera apone af arud kumpenda mosses tena wakat osman katoa figo hap๐Ÿ˜

      Reply
    4. Calvin paul on October 13, 2024 5:30 pm

      Wanaume kama osman tumebaki wachache sanaa

      Reply
      • Joyce on October 14, 2024 12:44 pm

        Calvin kabisa ๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„

        Reply
    5. Lus twaxie on October 13, 2024 5:38 pm

      Huyu dada nna was was akipona …atanboaaaa

      Reply
      • Kevin Winton mwasambiri on October 14, 2024 12:55 am

        Niko njia Panda naomba mosses
        Afutwe uhusika๐Ÿ˜ฃ

        Reply
    6. Chingu on October 13, 2024 5:43 pm

      Huu uzi sio poa hatariii kama ungekuwa unaachia mbili mbili vile daah hatarii๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    7. Stella on October 13, 2024 6:24 pm

      Yani wanawake sisi Sijui kama atakumbuka wema Na fadhila
      ๐Ÿ˜’

      Reply
    8. Junior on October 13, 2024 8:39 pm

      Mmmh tusubili namba 04 ๐Ÿค”๐Ÿค”

      Reply
    9. Henderson on October 13, 2024 11:15 pm

      NAUZA FIGO +255788414957

      Reply
    10. Sabiti on October 14, 2024 12:15 am

      !!!!!!!! Kuna mtu ata ๐Ÿ’”

      Reply
    11. Dj Shoti on October 14, 2024 1:30 am

      ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜…

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.