Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Nne (04)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Nne (04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 14, 2024Updated:October 28, 202433 Comments8 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Alipotoka Hospitalini Osman alikuwa mwenye mawazo na maumivuย  makali sana, alipigiwa simu na Wazazi wake na kumtaka aachaneย  na mpango wa kutaka kutoa figo kwani haitokuwa na faidaย  yoyote kwake, Wazazi wa Osman waliamini kuwa Osman alikuwaย  akitaka kutoa figo kwa ajili ya Mapenzi, walinuonya sana kwaย  kile kilichomtokea kwa Zahra ila Osman aliwaambia Wazazi wakeย  kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na Mimi bali ni ubinadamu tuย  wa kutaka kuhakikisha afya yangu inaimarika.ย 

    Osman aliwasiliana na Hospitali nyingine ambayo ingefanyaย  operesheni ya kupandikiza figo kwenye mwili wangu, kutokanaย  na utajiri alionao aliweza kupata Hospitali Nchini India,ย  tulisafiri kwenda huko. Osman alishauriwa na kuambiwa kilaย  kitu kiafya kuhusu uamuzi wake. Endelea

    SEHEMU YA NNE

    alikubali kutoa figo.ย 

    Baada ya siku tatu, tulifanyiwa Operesheni, Osman aliondolewaย  Figo yake ambayo ilikuwa safi kabisa, Mimi niliondolewa Figo zangu ambazo zilikuwa na matatizo kisha ilipandikizwa Figo yaย  Osman katika mwili wangu. Mama yangu alikuwa ni Mtu wa kuliaย  na kuomba Mungu kila jambo liende sawa, siku zilienda, unafuuย  ulianza kuniingia, hata Osman unafuu ulimuingia, sikujuwaย  kilichokua kimetokea.ย 

    Ilipita miezi miwili tukiwa Hospitalini India, hali yanguย  ilizidi kuimarika siku hadi siku hatimaye nilipona kabisa,ย  Mimi na Osman tulipona, tuliruhusiwa tukarudi Nchini.ย  Tulifikia kwenye jumba la kifahari sana ambalo Osmanย  alitununulia, Maisha yalibadilika sana kwetu, Osmanย  alitufungulia Biashara kubwa. Nilisimuliwa kila kilichotokea,ย  niliuona upendo wa Osman, pia niliuona upendo feki wa Mossesย 

    Siku moja Osman alinipeleka kwa Wazazi wake huko Dubai,ย  Walifurahika kuniona. Walitupokea kwa shamra shamra sana,ย  familia yao ilikuwa ni familia ya kitajiri sana.ย 

    “Karibu Jacklin katika Familia yetu” Alisema Baba yake Osmanย  tukiwa tunapata chakulaย 

    “Asante Baba, nafurahika kuwaona” nilijibuย 

    “Usijali Jacklin, wewe ni damu yetu sababu una kiungo chaย  Mtoto wetu, naona hata sura ya Osman imeng’aa kwa furaha,ย  natumaini hautofanya kama alichokifanya Zahra” Alisema Mamaย  yake Osman, nilishtuka kidogo sababu nilikuwa simjui huyoย  Zahra, nilimtazama Osman akanipa ishara ya kutabasamu tu kuwaย  atanieleza kila kitu, kilichonishangaza ni yale maongezi yao,ย  ilionesha kuwa wao walikuwa wakijuwa kuwa Mimi na Osman niย  wapenzi wakati hatukuwahi kuongelea kuhusu Mapenzi.ย 

    Baada ya Chakula tulioneshwa chumba cha kulala, kilikuwa niย  chumba kimoja tu tulale mimi na Osman, tulipofika Chumbaniย  nilimuuliza Osmanย 

    “Zahra ni nani?” Nilimuuliza nikiwa nimekaa kitandani, yeyeย  alikuwa ameketi juu ya kiti.ย 

    “Mwanamke niliyempenda sana, aliyenifanya nikalia na kupotezaย  kila kitu katika Maisha yangu” alisema Osmanย 

    “Kwahiyo ulinisaidia ili unitumie Osman, umewaambia niniย  Wazazi wako na kwanini waseme maneno yale? Lengo lako nijeย  kuonekana mbaya mbele za macho yao wakati unajuwa hali halisiย  kuwa nina mpenzi?” Nilisema japo Mosses alikataa kutoa figoย  na kumjibu Mama vibaya, niliamini pengine kuna jamboย  hawakuelewana tuu ila bado alikuwa akinipenda nami nilikuwaย  nikimpenda.

    “Una mpenzi? Aliyekuacha ufe wakati alikuwa na uwezo waย  kukusaidia?” Alisema Osman akiwa anakaa vizuriย 

    “Yeye alikataa ila wewe umenisaidia ili unitumie Osman, hunaย  tofauti na mtu anayetoa msaada na kusubiria kulipwa. Mossesย  ni Mwanaume anayenipenda sana pamoja na yote yaliyotokea”ย  Nilisema nikiwa ninajilazaย 

    “Samahani Jacklin, usiwachukie Wazazi wangu wala usiumie,ย  sikukusaidia ili niwe na wewe ila samahani sana kwa kukufanyaย  uhisi hivyo” Alisema Osman, sikumjibu chochote kile, nilionaย  alikuwa akinipenda sana ila sikuwa na hisia za kimapenzi naย  Osman, moyo wangu ulikuwa kwa Mosses. Tuliishi Dubai kwa wikiย  mbili, tulikuwa tukiongea mbele ya Wazazi wa Osman lakiniย  tukiwa wawili kila mmoja alikuwa kimya, tulirudi Nchini,ย  nilifurahika sana kuonana na Mama yangu kwa mara nyingineย  tena.ย 

    “Maisha ya huko yalikuwaje Mama” Aliuliza Mama yangu, wakatiย  huo Osman alikuwa ameshaondokaย 

    “Mazuri sana Mama, nimefurahi sababu ilikuwa ndiyo mara yaย  kwanza naenda nje ya Nchi” Mama alinikumbatia akaniambiaย 

    “Muweke Osman katika Maombi yako kila siku Mwanangu, jitihadaย  zake zimeokoa Maisha yako, usilisahau hilo” Alisema Mamaย 

    “Sawa Mama ngoja nikapumzike” Sikutaka kumwambia chochoteย  Mama sababu niliamini yupo upande wa Osman, nilielekeaย  chumbani kwangu, ilikuwa ni nyumba nzuri ambayo sikuwahiย  kuiota katika Maisha yangu, umasikini tuliupa mkono waย  kwaheri.ย 

    Nilitazama nje niliiyona gari yangu aliyoninunulia Osman,ย  nilikumbuka kipindi ambacho nilikuwa natembea kwa mguu,ย  nilikumbuka siku ambayo homa ilinianzia jinsi nilivyokuwaย  nikitetemeka kwenye baridi, jinsi Osman alivyojitolea kiungoย  chake ili kuokoa Maisha yangu, nilimshukuru kwa kumtumiaย  ujumbe lakini hakujibu kabisa.ย 

    Siku iliyofuata nilipigiwa simu na Mmoja wa Wafanyakazi waย  kampuni ya JM Motors kuwa natakiwa kuanza kazi, japo nilikuwaย  na uchovu ila kazi hiyo ilikuwa ni ndoto yangu, pia nilionaย  ni bora nifanye kazi kwa Osman ili kumshukuru kwa ukarimu naย  msaada wake, basi nilijiandaa kisha nilielekea kazini kwaย  kutumia usafiri wa kukodi maana nilikuwa sijui kuendeshaย  gari. Nilipokelewa vizuri sana, nilioneshwa ofisi yangu,ย  ilikuwa ni ofisi iliyotengenezwa kwa ajili yangu, nilikutaย  picha yangu ukutani

    Nikitabasamu sababu nilijuwa kuwa ni Osman ndiye aliyefanyaย  hivyo, nilianza kazi rasmi katika kampuni ya JM Motors,ย  mahusiano yangu na Osman yalipungua kwa kiasi kikubwa,ย  alikuwa akinisalimia tu kisha kila Mtu alikuwa akiendelea naย  Maisha yake. Siku moja nilihitaji Mafaili kutoka kwenye ofisiย  yake, bahati mbaya hakuwepo ofisini, nilizungumza na Msaidiziย  wake akaenda kunichukulia Mafaili hayo.ย 

    Aliponiletea nilianza kazi yangu, lilikuwa ni faili la Watuย  waliokuwa wanasubiria mzigo wa Magari ambao ulitakiwa kuingiaย  kesho yake, nilitakiwa kuhakiki taarifa zao, wakati naendeleaย  kufungua mafaili hayo nilikutana na picha ya Mwanamke mzuriย  sana, tena Mzuri kuliko Mimi, yaani mzuri hadi ukimtazamaย  unagundua kuwa alikuwa mzuri kuliko mfano. Sikujuwa Mwanamkeย  huyo alikuwa akiitwa nani, nilipogeuza nyuma ya pichaย  nilikutana na jina limeandikwa “ZAHRA”ย 

    Nilishusha pumzi zangu kisha niliigeuza tena ile picha, ooh!ย  Huyo Zahra kumbe ndiye huyu? Anastahili kuugalagaza moyo waย  Osman,,hakika ni mzuri sana. Nilisema na Moyo wangu,ย  niliirudisha picha nilipoitoa.ย 

    Katika hali ambayo sikuielewa nilijikuta nikikosa raha hataย  kufanya kazi nilishindwa nilihisi moyo unaniuma, ilikuwa niย  mishale ya saa saba Mchana, nilimuaga Mtu wa Usaidizi paleย  kazini kisha niliondoka, nilifanya safari kwenda anapoishiย  Mosses maana simu yake ilikuwa haipatikani, nilitumia usafiriย  wa gari ya kukodi, nilipofika niligonga mlango kwenye chumbaย  cha Mosses, alikuwa ni Kijana mwenye Maisha ya kati tu.ย  Nilisubiria mlango ufunguliwe, aliyefungua alikuwa ni Mossesย  mwenyewe, alinishangaa kisha alitabasamu, dimpozi zakeย  zikajiachia. Mosses alikuwa anajuwa kuugalagaza moyo wanguย  vile atakavyo, pamoja na yote kukataa kunitolea figo badoย  nilikuwa nikimpenda na sikufikiria hata siku moja kamaย  ningelimpenda Mwanaume mwingine, alinikumbatia akiwa amevaliaย  taulo tu. Mwili ukaanza kunisisimka kama napandwa na sisimiziย  hivi, mikono ya Mosses ilikuwa kama sumaku vile yaani hataย  anishike wapi alikuwa akinipandisha ashki zangu.ย 

    Nilivuta hewa kisha nilimwambia Mossesย 

    “Nimekumiss sana Mosses” nilisema nikiwa nimemkumbatia kwaย  nguvu, nilikuwa na hisia kali sana kwa Mossesย 

    “Nimekumiss pia Jacklin, pole kwa matatizo yaliyokupata,ย  siamini kama bado unaishi, nilijuwa umeshakufa ndio maanaย  niliamuwa kubadilisha namba” Alisema Mosses akiwa ananipigaย  busu shingoni, nilifumba macho kwa utamu wa Busu, nilikuwaย  nusu Chizi kwa Mwanaume huyu

    “Naishi kwa ajili yako Mosses, kama siyo wewe ningelikuwaย  nimekufa zamani sana ila nguvu ya Mapenzi niliyonayo juu yakoย  ndiyo iliyonipa uhai nikaamka tena” Nilisema pia, aliniachiaย  akanitazama jinsi nilivyokuwa nimependeza ilitosha kumfanyaย  Mosses atambuwe kuwa maisha yangu yalikuwa yamebadilika kwaย  kiasi kikubwa sana.ย 

    “Nakupenda sana Mosses” Nilimwambia, naye alirudisha jibuย  zuri sanaย 

    “Umenipa sababu ya kuendelea kuishi Jacklin, niliposikia kuwaย  huwezi kupona nilihisi unakufa, nilitamani kufanya kila kituย  ili niokoe uhai wako” Alisema Mosses, nilijuwa ni uwongoย  lakini nguvu ya mapenzi iliniambia kuwa anachokisena Mossesย  kina ukweliย 

    “Tuachane na hayo Mosses naomba tuongee ndani” Nilisema kishaย  tuliingia chumbani kwa Mosses. Nilitazama jinsi chumba chaย  Mosses kilivyo, sikupenda aendelee kuishi hapo, nilikuwa naย  uwezo wa kubadilisha Maisha ya Mosses sababu nilikuwaย  nikimpenda sana.ย 

    “Mosses kwasasa nafanya kazi, Maisha yangu yamebadilika sana.ย  Sitopenda uendelee kuishi hapa nitakupangia sehemu nzuri yaย  kuishi” Nilimwambia Mossesย 

    “Jamani kweli Jacklin?” Aliuliza kama Mtu ambaye alikuwaย  amechanganikiwaย 

    “Ndiyo! Hadhi yako ndani ya moyo wangu ni kubwa sanaย  hustahili kuishi hapa, tafuta nyumba eneo lililotuliaย  nitalipia kila kitu na kununua vitu vipya” Nilisema, maraย  moja Mosses alinivaa na kuanza kunipiga mabusu ambayoย  yaliamsha hisia zangu, nilijikuta nikiwa na hamu ya kufanyaย  Mapenzi na Mosses, daktari alisema sipaswi kufanya hivyo hadiย  miezi sita itakapoisha lakini nilijikuta nikifanya mapenzi naย  Mosses, baada ya kumaliza nilimshukuru Mosses kwa penzi tamuย  alilonipa.ย 

    “Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisemaย  Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwaย  pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalalaย  palepale.ย 

    Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwaย  nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,ย  alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwaย  nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kamaย  nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipoย  nyumbani.

    ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TANO Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย 

    Pumzi ya mwisho

    33 Comments

    1. Lus twaxie on October 14, 2024 9:57 pm

      Huyu dada n jauuuuuuuuu

      Reply
      • G shirima on October 14, 2024 10:33 pm

        Uyu dada wawapi vp mbona siyo muelewa kweli mapenzi ni giza

        Reply
    2. Farnoush on October 14, 2024 10:11 pm

      Mbona fupiiii leo
      Ila jackline ni kiazi sana๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

      Reply
    3. France on October 14, 2024 10:34 pm

      Dah bora uyu mdad angekufa2๐Ÿ˜ข

      Reply
      • Wiga son Tz on October 14, 2024 11:29 pm

        MH!

        Reply
      • Ngeleja on October 15, 2024 1:56 am

        Jacqueline hafai hata kwa kulumagia Dah!!๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

        Reply
    4. Maxwell on October 14, 2024 10:42 pm

      Ivi hii ndo maana ya โ€œ the when a woman loves….โ€๐Ÿ˜ฐ namhurumia Osman

      Reply
    5. Sadick on October 14, 2024 11:01 pm

      Maskini osmani daah!! Jacklin bora angekufa mwandishi naomba hii story isituboe

      Reply
      • Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 15, 2024 12:05 pm

        Siyo kuboa tuu inaweza kukuliza huko mbelee๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ

        Reply
    6. Ebia Dastanie on October 14, 2024 11:19 pm

      Yani ishaanza kuboa ila sisi wanawake basi tu jacklin wewe mmh๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…

      Reply
    7. Wiga son Tz on October 14, 2024 11:30 pm

      MH!

      Reply
    8. Huncho on October 14, 2024 11:42 pm

      Sjawahi Comment Ila WANAWAKE JAU ๐Ÿ˜’๐Ÿ˜’๐Ÿ˜’

      Reply
      • Jacqueline Henry on October 15, 2024 7:58 am

        Fear women..

        Reply
    9. yahaya on October 14, 2024 11:45 pm

      kesho muendeleze jaman kali kinoma

      Reply
    10. yahaya on October 14, 2024 11:47 pm

      kesho muendeleze jaman kali

      Reply
    11. Oppa on October 15, 2024 1:09 am

      Jau kubabeq

      Reply
    12. [email protected] on October 15, 2024 1:43 am

      Adimn kuchoshana ww andik zeEND…..mosses anamzurum jack……akn bado Osman anamsamehe

      Reply
      • Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 15, 2024 12:03 pm

        Ahahahaha siyo kumdhulumu atakuja kumcheat uyo demu….. hii story naifananisha na tamthiliya moja inaitwa mfadhili yaani ni mule mule..badae kati ya osman ama uyo jack mmoja atakufa

        Reply
        • Angel on October 15, 2024 9:21 pm

          Kumbe na ww umeona eh…huyu ni dania kabisa yan…

          Reply
    13. Malongo on October 15, 2024 3:31 am

      Jacklin, sio

      Reply
    14. Calvin paul on October 15, 2024 6:37 am

      Fwalaaa sanaa mpaka hasira zimenipandaa wanawake bhanaa afukuzwe hata kazi tuu ubwa huyu

      Reply
    15. Yudah on October 15, 2024 7:27 am

      Madem jau sana duuh

      Reply
    16. Sabiti Mussa23 on October 15, 2024 7:46 am

      ๐Ÿ’”

      Reply
    17. Abdul (young daddy) on October 15, 2024 11:44 am

      Dah huyu dad ni zaidi ya shetan ani

      Reply
    18. Mkandarasi on October 15, 2024 11:59 am

      Mwenye huruma hanaga bahati

      Reply
    19. Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 15, 2024 12:07 pm

      EWAAAH!! DATS KAMA MLIFATILIA COMMENT ANGU YA SIKU ZA NYUMA…NILISEMA HAPO LAZIMA KUNA NAMNA ITAKUWA ANI UYO JACKLINE MPKA AJE KUFUNGUKA AKILI NI BAADAE SANA WAKATI MAMB YAMEHARIBIKA๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ KAMA UNAE MOYO MDGO UTALIA ๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„ ILA KI UHALISIA WATU NDO WALIVO JMNIII

      Reply
    20. Best mbwilo son on October 15, 2024 3:00 pm

      Wakina moses mikono juuu…….yaaan zitoke tatu kwa siku

      Reply
    21. Sir yowas on October 15, 2024 6:45 pm

      Sasa osmad anashida gani, anatongoza kwa kuhonga, binafsi sijaona kosa la jackline, kwani wameshakubaliana kuwa wapenzi?????

      Reply
    22. Dj Shoti on October 15, 2024 11:38 pm

      ๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜…

      Reply
    23. Robbiey on October 16, 2024 12:19 pm

      figo ya kiume imeingiliwa au figo haina jinsia

      Reply
    24. Jackson Felician on October 18, 2024 7:54 am

      Kama ni Mimi naenda kuchukua Figo yangu

      Reply
    25. ๐Ÿ“‹ + 1.591965 BTC.GET - https://yandex.com/poll/76RuKke5vYn6W1hp2wxzvb?hs=9fd2933a2e60b65ec47a79a56b0b0662& ๐Ÿ“‹ on June 4, 2025 2:25 pm

      qqw0kc

      Reply
    26. ๐Ÿ“Ÿ Message; Process 1.721767 bitcoin. Next >>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=9fd2933a2e60b65ec47a79a56b0b0662& ๐Ÿ“Ÿ on June 29, 2025 5:07 am

      pjnfar

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.