Ilipoishia “Alipotoka Hospitalini Osman alikuwa mwenye mawazo na maumivuย makali sana, alipigiwa simu na Wazazi wake na kumtaka aachaneย na mpango wa kutaka kutoa figo kwani haitokuwa na faidaย yoyote kwake, Wazazi wa Osman waliamini kuwa Osman alikuwaย akitaka kutoa figo kwa ajili ya Mapenzi, walinuonya sana kwaย kile kilichomtokea kwa Zahra ila Osman aliwaambia Wazazi wakeย kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na Mimi bali ni ubinadamu tuย wa kutaka kuhakikisha afya yangu inaimarika.ย
Osman aliwasiliana na Hospitali nyingine ambayo ingefanyaย operesheni ya kupandikiza figo kwenye mwili wangu, kutokanaย na utajiri alionao aliweza kupata Hospitali Nchini India,ย tulisafiri kwenda huko. Osman alishauriwa na kuambiwa kilaย kitu kiafya kuhusu uamuzi wake. Endelea
SEHEMU YA NNE
alikubali kutoa figo.ย
Baada ya siku tatu, tulifanyiwa Operesheni, Osman aliondolewaย Figo yake ambayo ilikuwa safi kabisa, Mimi niliondolewa Figo zangu ambazo zilikuwa na matatizo kisha ilipandikizwa Figo yaย Osman katika mwili wangu. Mama yangu alikuwa ni Mtu wa kuliaย na kuomba Mungu kila jambo liende sawa, siku zilienda, unafuuย ulianza kuniingia, hata Osman unafuu ulimuingia, sikujuwaย kilichokua kimetokea.ย
Ilipita miezi miwili tukiwa Hospitalini India, hali yanguย ilizidi kuimarika siku hadi siku hatimaye nilipona kabisa,ย Mimi na Osman tulipona, tuliruhusiwa tukarudi Nchini.ย Tulifikia kwenye jumba la kifahari sana ambalo Osmanย alitununulia, Maisha yalibadilika sana kwetu, Osmanย alitufungulia Biashara kubwa. Nilisimuliwa kila kilichotokea,ย niliuona upendo wa Osman, pia niliuona upendo feki wa Mossesย
Siku moja Osman alinipeleka kwa Wazazi wake huko Dubai,ย Walifurahika kuniona. Walitupokea kwa shamra shamra sana,ย familia yao ilikuwa ni familia ya kitajiri sana.ย
“Karibu Jacklin katika Familia yetu” Alisema Baba yake Osmanย tukiwa tunapata chakulaย
“Asante Baba, nafurahika kuwaona” nilijibuย
“Usijali Jacklin, wewe ni damu yetu sababu una kiungo chaย Mtoto wetu, naona hata sura ya Osman imeng’aa kwa furaha,ย natumaini hautofanya kama alichokifanya Zahra” Alisema Mamaย yake Osman, nilishtuka kidogo sababu nilikuwa simjui huyoย Zahra, nilimtazama Osman akanipa ishara ya kutabasamu tu kuwaย atanieleza kila kitu, kilichonishangaza ni yale maongezi yao,ย ilionesha kuwa wao walikuwa wakijuwa kuwa Mimi na Osman niย wapenzi wakati hatukuwahi kuongelea kuhusu Mapenzi.ย
Baada ya Chakula tulioneshwa chumba cha kulala, kilikuwa niย chumba kimoja tu tulale mimi na Osman, tulipofika Chumbaniย nilimuuliza Osmanย
“Zahra ni nani?” Nilimuuliza nikiwa nimekaa kitandani, yeyeย alikuwa ameketi juu ya kiti.ย
“Mwanamke niliyempenda sana, aliyenifanya nikalia na kupotezaย kila kitu katika Maisha yangu” alisema Osmanย
“Kwahiyo ulinisaidia ili unitumie Osman, umewaambia niniย Wazazi wako na kwanini waseme maneno yale? Lengo lako nijeย kuonekana mbaya mbele za macho yao wakati unajuwa hali halisiย kuwa nina mpenzi?” Nilisema japo Mosses alikataa kutoa figoย na kumjibu Mama vibaya, niliamini pengine kuna jamboย hawakuelewana tuu ila bado alikuwa akinipenda nami nilikuwaย nikimpenda.
“Una mpenzi? Aliyekuacha ufe wakati alikuwa na uwezo waย kukusaidia?” Alisema Osman akiwa anakaa vizuriย
“Yeye alikataa ila wewe umenisaidia ili unitumie Osman, hunaย tofauti na mtu anayetoa msaada na kusubiria kulipwa. Mossesย ni Mwanaume anayenipenda sana pamoja na yote yaliyotokea”ย Nilisema nikiwa ninajilazaย
“Samahani Jacklin, usiwachukie Wazazi wangu wala usiumie,ย sikukusaidia ili niwe na wewe ila samahani sana kwa kukufanyaย uhisi hivyo” Alisema Osman, sikumjibu chochote kile, nilionaย alikuwa akinipenda sana ila sikuwa na hisia za kimapenzi naย Osman, moyo wangu ulikuwa kwa Mosses. Tuliishi Dubai kwa wikiย mbili, tulikuwa tukiongea mbele ya Wazazi wa Osman lakiniย tukiwa wawili kila mmoja alikuwa kimya, tulirudi Nchini,ย nilifurahika sana kuonana na Mama yangu kwa mara nyingineย tena.ย
“Maisha ya huko yalikuwaje Mama” Aliuliza Mama yangu, wakatiย huo Osman alikuwa ameshaondokaย
“Mazuri sana Mama, nimefurahi sababu ilikuwa ndiyo mara yaย kwanza naenda nje ya Nchi” Mama alinikumbatia akaniambiaย
“Muweke Osman katika Maombi yako kila siku Mwanangu, jitihadaย zake zimeokoa Maisha yako, usilisahau hilo” Alisema Mamaย
“Sawa Mama ngoja nikapumzike” Sikutaka kumwambia chochoteย Mama sababu niliamini yupo upande wa Osman, nilielekeaย chumbani kwangu, ilikuwa ni nyumba nzuri ambayo sikuwahiย kuiota katika Maisha yangu, umasikini tuliupa mkono waย kwaheri.ย
Nilitazama nje niliiyona gari yangu aliyoninunulia Osman,ย nilikumbuka kipindi ambacho nilikuwa natembea kwa mguu,ย nilikumbuka siku ambayo homa ilinianzia jinsi nilivyokuwaย nikitetemeka kwenye baridi, jinsi Osman alivyojitolea kiungoย chake ili kuokoa Maisha yangu, nilimshukuru kwa kumtumiaย ujumbe lakini hakujibu kabisa.ย
Siku iliyofuata nilipigiwa simu na Mmoja wa Wafanyakazi waย kampuni ya JM Motors kuwa natakiwa kuanza kazi, japo nilikuwaย na uchovu ila kazi hiyo ilikuwa ni ndoto yangu, pia nilionaย ni bora nifanye kazi kwa Osman ili kumshukuru kwa ukarimu naย msaada wake, basi nilijiandaa kisha nilielekea kazini kwaย kutumia usafiri wa kukodi maana nilikuwa sijui kuendeshaย gari. Nilipokelewa vizuri sana, nilioneshwa ofisi yangu,ย ilikuwa ni ofisi iliyotengenezwa kwa ajili yangu, nilikutaย picha yangu ukutani
Nikitabasamu sababu nilijuwa kuwa ni Osman ndiye aliyefanyaย hivyo, nilianza kazi rasmi katika kampuni ya JM Motors,ย mahusiano yangu na Osman yalipungua kwa kiasi kikubwa,ย alikuwa akinisalimia tu kisha kila Mtu alikuwa akiendelea naย Maisha yake. Siku moja nilihitaji Mafaili kutoka kwenye ofisiย yake, bahati mbaya hakuwepo ofisini, nilizungumza na Msaidiziย wake akaenda kunichukulia Mafaili hayo.ย
Aliponiletea nilianza kazi yangu, lilikuwa ni faili la Watuย waliokuwa wanasubiria mzigo wa Magari ambao ulitakiwa kuingiaย kesho yake, nilitakiwa kuhakiki taarifa zao, wakati naendeleaย kufungua mafaili hayo nilikutana na picha ya Mwanamke mzuriย sana, tena Mzuri kuliko Mimi, yaani mzuri hadi ukimtazamaย unagundua kuwa alikuwa mzuri kuliko mfano. Sikujuwa Mwanamkeย huyo alikuwa akiitwa nani, nilipogeuza nyuma ya pichaย nilikutana na jina limeandikwa “ZAHRA”ย
Nilishusha pumzi zangu kisha niliigeuza tena ile picha, ooh!ย Huyo Zahra kumbe ndiye huyu? Anastahili kuugalagaza moyo waย Osman,,hakika ni mzuri sana. Nilisema na Moyo wangu,ย niliirudisha picha nilipoitoa.ย
Katika hali ambayo sikuielewa nilijikuta nikikosa raha hataย kufanya kazi nilishindwa nilihisi moyo unaniuma, ilikuwa niย mishale ya saa saba Mchana, nilimuaga Mtu wa Usaidizi paleย kazini kisha niliondoka, nilifanya safari kwenda anapoishiย Mosses maana simu yake ilikuwa haipatikani, nilitumia usafiriย wa gari ya kukodi, nilipofika niligonga mlango kwenye chumbaย cha Mosses, alikuwa ni Kijana mwenye Maisha ya kati tu.ย Nilisubiria mlango ufunguliwe, aliyefungua alikuwa ni Mossesย mwenyewe, alinishangaa kisha alitabasamu, dimpozi zakeย zikajiachia. Mosses alikuwa anajuwa kuugalagaza moyo wanguย vile atakavyo, pamoja na yote kukataa kunitolea figo badoย nilikuwa nikimpenda na sikufikiria hata siku moja kamaย ningelimpenda Mwanaume mwingine, alinikumbatia akiwa amevaliaย taulo tu. Mwili ukaanza kunisisimka kama napandwa na sisimiziย hivi, mikono ya Mosses ilikuwa kama sumaku vile yaani hataย anishike wapi alikuwa akinipandisha ashki zangu.ย
Nilivuta hewa kisha nilimwambia Mossesย
“Nimekumiss sana Mosses” nilisema nikiwa nimemkumbatia kwaย nguvu, nilikuwa na hisia kali sana kwa Mossesย
“Nimekumiss pia Jacklin, pole kwa matatizo yaliyokupata,ย siamini kama bado unaishi, nilijuwa umeshakufa ndio maanaย niliamuwa kubadilisha namba” Alisema Mosses akiwa ananipigaย busu shingoni, nilifumba macho kwa utamu wa Busu, nilikuwaย nusu Chizi kwa Mwanaume huyu
“Naishi kwa ajili yako Mosses, kama siyo wewe ningelikuwaย nimekufa zamani sana ila nguvu ya Mapenzi niliyonayo juu yakoย ndiyo iliyonipa uhai nikaamka tena” Nilisema pia, aliniachiaย akanitazama jinsi nilivyokuwa nimependeza ilitosha kumfanyaย Mosses atambuwe kuwa maisha yangu yalikuwa yamebadilika kwaย kiasi kikubwa sana.ย
“Nakupenda sana Mosses” Nilimwambia, naye alirudisha jibuย zuri sanaย
“Umenipa sababu ya kuendelea kuishi Jacklin, niliposikia kuwaย huwezi kupona nilihisi unakufa, nilitamani kufanya kila kituย ili niokoe uhai wako” Alisema Mosses, nilijuwa ni uwongoย lakini nguvu ya mapenzi iliniambia kuwa anachokisena Mossesย kina ukweliย
“Tuachane na hayo Mosses naomba tuongee ndani” Nilisema kishaย tuliingia chumbani kwa Mosses. Nilitazama jinsi chumba chaย Mosses kilivyo, sikupenda aendelee kuishi hapo, nilikuwa naย uwezo wa kubadilisha Maisha ya Mosses sababu nilikuwaย nikimpenda sana.ย
“Mosses kwasasa nafanya kazi, Maisha yangu yamebadilika sana.ย Sitopenda uendelee kuishi hapa nitakupangia sehemu nzuri yaย kuishi” Nilimwambia Mossesย
“Jamani kweli Jacklin?” Aliuliza kama Mtu ambaye alikuwaย amechanganikiwaย
“Ndiyo! Hadhi yako ndani ya moyo wangu ni kubwa sanaย hustahili kuishi hapa, tafuta nyumba eneo lililotuliaย nitalipia kila kitu na kununua vitu vipya” Nilisema, maraย moja Mosses alinivaa na kuanza kunipiga mabusu ambayoย yaliamsha hisia zangu, nilijikuta nikiwa na hamu ya kufanyaย Mapenzi na Mosses, daktari alisema sipaswi kufanya hivyo hadiย miezi sita itakapoisha lakini nilijikuta nikifanya mapenzi naย Mosses, baada ya kumaliza nilimshukuru Mosses kwa penzi tamuย alilonipa.ย
“Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisemaย Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwaย pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalalaย palepale.ย
Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwaย nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,ย alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwaย nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kamaย nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipoย nyumbani.
ย
Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TANO Ya PUMZI YA MWISHO
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMย ย
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย
33 Comments
Huyu dada n jauuuuuuuuu
Uyu dada wawapi vp mbona siyo muelewa kweli mapenzi ni giza
Mbona fupiiii leo
Ila jackline ni kiazi sana๐๐
Dah bora uyu mdad angekufa2๐ข
MH!
Jacqueline hafai hata kwa kulumagia Dah!!๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ
Ivi hii ndo maana ya โ the when a woman loves….โ๐ฐ namhurumia Osman
Maskini osmani daah!! Jacklin bora angekufa mwandishi naomba hii story isituboe
Siyo kuboa tuu inaweza kukuliza huko mbelee๐๐๐
Yani ishaanza kuboa ila sisi wanawake basi tu jacklin wewe mmh๐ ๐ ๐
MH!
Sjawahi Comment Ila WANAWAKE JAU ๐๐๐
Fear women..
kesho muendeleze jaman kali kinoma
kesho muendeleze jaman kali
Jau kubabeq
Adimn kuchoshana ww andik zeEND…..mosses anamzurum jack……akn bado Osman anamsamehe
Ahahahaha siyo kumdhulumu atakuja kumcheat uyo demu….. hii story naifananisha na tamthiliya moja inaitwa mfadhili yaani ni mule mule..badae kati ya osman ama uyo jack mmoja atakufa
Kumbe na ww umeona eh…huyu ni dania kabisa yan…
Jacklin, sio
Fwalaaa sanaa mpaka hasira zimenipandaa wanawake bhanaa afukuzwe hata kazi tuu ubwa huyu
Madem jau sana duuh
๐
Dah huyu dad ni zaidi ya shetan ani
Mwenye huruma hanaga bahati
EWAAAH!! DATS KAMA MLIFATILIA COMMENT ANGU YA SIKU ZA NYUMA…NILISEMA HAPO LAZIMA KUNA NAMNA ITAKUWA ANI UYO JACKLINE MPKA AJE KUFUNGUKA AKILI NI BAADAE SANA WAKATI MAMB YAMEHARIBIKA๐ฅฒ๐ฅฒ๐ฅฒ KAMA UNAE MOYO MDGO UTALIA ๐๐ ILA KI UHALISIA WATU NDO WALIVO JMNIII
Wakina moses mikono juuu…….yaaan zitoke tatu kwa siku
Sasa osmad anashida gani, anatongoza kwa kuhonga, binafsi sijaona kosa la jackline, kwani wameshakubaliana kuwa wapenzi?????
๐๐๐
figo ya kiume imeingiliwa au figo haina jinsia
Kama ni Mimi naenda kuchukua Figo yangu
qqw0kc
pjnfar