Ilipoishia “Alipotoka Hospitalini Osman alikuwa mwenye mawazo na maumivuΒ makali sana, alipigiwa simu na Wazazi wake na kumtaka aachaneΒ na mpango wa kutaka kutoa figo kwani haitokuwa na faidaΒ yoyote kwake, Wazazi wa Osman waliamini kuwa Osman alikuwaΒ akitaka kutoa figo kwa ajili ya Mapenzi, walinuonya sana kwaΒ kile kilichomtokea kwa Zahra ila Osman aliwaambia Wazazi wakeΒ kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na Mimi bali ni ubinadamu tuΒ wa kutaka kuhakikisha afya yangu inaimarika.Β
Osman aliwasiliana na Hospitali nyingine ambayo ingefanyaΒ operesheni ya kupandikiza figo kwenye mwili wangu, kutokanaΒ na utajiri alionao aliweza kupata Hospitali Nchini India,Β tulisafiri kwenda huko. Osman alishauriwa na kuambiwa kilaΒ kitu kiafya kuhusu uamuzi wake. Endelea
SEHEMU YA NNE
alikubali kutoa figo.Β
Baada ya siku tatu, tulifanyiwa Operesheni, Osman aliondolewaΒ Figo yake ambayo ilikuwa safi kabisa, Mimi niliondolewa Figo zangu ambazo zilikuwa na matatizo kisha ilipandikizwa Figo yaΒ Osman katika mwili wangu. Mama yangu alikuwa ni Mtu wa kuliaΒ na kuomba Mungu kila jambo liende sawa, siku zilienda, unafuuΒ ulianza kuniingia, hata Osman unafuu ulimuingia, sikujuwaΒ kilichokua kimetokea.Β
Ilipita miezi miwili tukiwa Hospitalini India, hali yanguΒ ilizidi kuimarika siku hadi siku hatimaye nilipona kabisa,Β Mimi na Osman tulipona, tuliruhusiwa tukarudi Nchini.Β Tulifikia kwenye jumba la kifahari sana ambalo OsmanΒ alitununulia, Maisha yalibadilika sana kwetu, OsmanΒ alitufungulia Biashara kubwa. Nilisimuliwa kila kilichotokea,Β niliuona upendo wa Osman, pia niliuona upendo feki wa MossesΒ
Siku moja Osman alinipeleka kwa Wazazi wake huko Dubai,Β Walifurahika kuniona. Walitupokea kwa shamra shamra sana,Β familia yao ilikuwa ni familia ya kitajiri sana.Β
“Karibu Jacklin katika Familia yetu” Alisema Baba yake OsmanΒ tukiwa tunapata chakulaΒ
“Asante Baba, nafurahika kuwaona” nilijibuΒ
“Usijali Jacklin, wewe ni damu yetu sababu una kiungo chaΒ Mtoto wetu, naona hata sura ya Osman imeng’aa kwa furaha,Β natumaini hautofanya kama alichokifanya Zahra” Alisema MamaΒ yake Osman, nilishtuka kidogo sababu nilikuwa simjui huyoΒ Zahra, nilimtazama Osman akanipa ishara ya kutabasamu tu kuwaΒ atanieleza kila kitu, kilichonishangaza ni yale maongezi yao,Β ilionesha kuwa wao walikuwa wakijuwa kuwa Mimi na Osman niΒ wapenzi wakati hatukuwahi kuongelea kuhusu Mapenzi.Β
Baada ya Chakula tulioneshwa chumba cha kulala, kilikuwa niΒ chumba kimoja tu tulale mimi na Osman, tulipofika ChumbaniΒ nilimuuliza OsmanΒ
“Zahra ni nani?” Nilimuuliza nikiwa nimekaa kitandani, yeyeΒ alikuwa ameketi juu ya kiti.Β
“Mwanamke niliyempenda sana, aliyenifanya nikalia na kupotezaΒ kila kitu katika Maisha yangu” alisema OsmanΒ
“Kwahiyo ulinisaidia ili unitumie Osman, umewaambia niniΒ Wazazi wako na kwanini waseme maneno yale? Lengo lako nijeΒ kuonekana mbaya mbele za macho yao wakati unajuwa hali halisiΒ kuwa nina mpenzi?” Nilisema japo Mosses alikataa kutoa figoΒ na kumjibu Mama vibaya, niliamini pengine kuna jamboΒ hawakuelewana tuu ila bado alikuwa akinipenda nami nilikuwaΒ nikimpenda.
“Una mpenzi? Aliyekuacha ufe wakati alikuwa na uwezo waΒ kukusaidia?” Alisema Osman akiwa anakaa vizuriΒ
“Yeye alikataa ila wewe umenisaidia ili unitumie Osman, hunaΒ tofauti na mtu anayetoa msaada na kusubiria kulipwa. MossesΒ ni Mwanaume anayenipenda sana pamoja na yote yaliyotokea”Β Nilisema nikiwa ninajilazaΒ
“Samahani Jacklin, usiwachukie Wazazi wangu wala usiumie,Β sikukusaidia ili niwe na wewe ila samahani sana kwa kukufanyaΒ uhisi hivyo” Alisema Osman, sikumjibu chochote kile, nilionaΒ alikuwa akinipenda sana ila sikuwa na hisia za kimapenzi naΒ Osman, moyo wangu ulikuwa kwa Mosses. Tuliishi Dubai kwa wikiΒ mbili, tulikuwa tukiongea mbele ya Wazazi wa Osman lakiniΒ tukiwa wawili kila mmoja alikuwa kimya, tulirudi Nchini,Β nilifurahika sana kuonana na Mama yangu kwa mara nyingineΒ tena.Β
“Maisha ya huko yalikuwaje Mama” Aliuliza Mama yangu, wakatiΒ huo Osman alikuwa ameshaondokaΒ
“Mazuri sana Mama, nimefurahi sababu ilikuwa ndiyo mara yaΒ kwanza naenda nje ya Nchi” Mama alinikumbatia akaniambiaΒ
“Muweke Osman katika Maombi yako kila siku Mwanangu, jitihadaΒ zake zimeokoa Maisha yako, usilisahau hilo” Alisema MamaΒ
“Sawa Mama ngoja nikapumzike” Sikutaka kumwambia chochoteΒ Mama sababu niliamini yupo upande wa Osman, nilielekeaΒ chumbani kwangu, ilikuwa ni nyumba nzuri ambayo sikuwahiΒ kuiota katika Maisha yangu, umasikini tuliupa mkono waΒ kwaheri.Β
Nilitazama nje niliiyona gari yangu aliyoninunulia Osman,Β nilikumbuka kipindi ambacho nilikuwa natembea kwa mguu,Β nilikumbuka siku ambayo homa ilinianzia jinsi nilivyokuwaΒ nikitetemeka kwenye baridi, jinsi Osman alivyojitolea kiungoΒ chake ili kuokoa Maisha yangu, nilimshukuru kwa kumtumiaΒ ujumbe lakini hakujibu kabisa.Β
Siku iliyofuata nilipigiwa simu na Mmoja wa Wafanyakazi waΒ kampuni ya JM Motors kuwa natakiwa kuanza kazi, japo nilikuwaΒ na uchovu ila kazi hiyo ilikuwa ni ndoto yangu, pia nilionaΒ ni bora nifanye kazi kwa Osman ili kumshukuru kwa ukarimu naΒ msaada wake, basi nilijiandaa kisha nilielekea kazini kwaΒ kutumia usafiri wa kukodi maana nilikuwa sijui kuendeshaΒ gari. Nilipokelewa vizuri sana, nilioneshwa ofisi yangu,Β ilikuwa ni ofisi iliyotengenezwa kwa ajili yangu, nilikutaΒ picha yangu ukutani
Nikitabasamu sababu nilijuwa kuwa ni Osman ndiye aliyefanyaΒ hivyo, nilianza kazi rasmi katika kampuni ya JM Motors,Β mahusiano yangu na Osman yalipungua kwa kiasi kikubwa,Β alikuwa akinisalimia tu kisha kila Mtu alikuwa akiendelea naΒ Maisha yake. Siku moja nilihitaji Mafaili kutoka kwenye ofisiΒ yake, bahati mbaya hakuwepo ofisini, nilizungumza na MsaidiziΒ wake akaenda kunichukulia Mafaili hayo.Β
Aliponiletea nilianza kazi yangu, lilikuwa ni faili la WatuΒ waliokuwa wanasubiria mzigo wa Magari ambao ulitakiwa kuingiaΒ kesho yake, nilitakiwa kuhakiki taarifa zao, wakati naendeleaΒ kufungua mafaili hayo nilikutana na picha ya Mwanamke mzuriΒ sana, tena Mzuri kuliko Mimi, yaani mzuri hadi ukimtazamaΒ unagundua kuwa alikuwa mzuri kuliko mfano. Sikujuwa MwanamkeΒ huyo alikuwa akiitwa nani, nilipogeuza nyuma ya pichaΒ nilikutana na jina limeandikwa “ZAHRA”Β
Nilishusha pumzi zangu kisha niliigeuza tena ile picha, ooh!Β Huyo Zahra kumbe ndiye huyu? Anastahili kuugalagaza moyo waΒ Osman,,hakika ni mzuri sana. Nilisema na Moyo wangu,Β niliirudisha picha nilipoitoa.Β
Katika hali ambayo sikuielewa nilijikuta nikikosa raha hataΒ kufanya kazi nilishindwa nilihisi moyo unaniuma, ilikuwa niΒ mishale ya saa saba Mchana, nilimuaga Mtu wa Usaidizi paleΒ kazini kisha niliondoka, nilifanya safari kwenda anapoishiΒ Mosses maana simu yake ilikuwa haipatikani, nilitumia usafiriΒ wa gari ya kukodi, nilipofika niligonga mlango kwenye chumbaΒ cha Mosses, alikuwa ni Kijana mwenye Maisha ya kati tu.Β Nilisubiria mlango ufunguliwe, aliyefungua alikuwa ni MossesΒ mwenyewe, alinishangaa kisha alitabasamu, dimpozi zakeΒ zikajiachia. Mosses alikuwa anajuwa kuugalagaza moyo wanguΒ vile atakavyo, pamoja na yote kukataa kunitolea figo badoΒ nilikuwa nikimpenda na sikufikiria hata siku moja kamaΒ ningelimpenda Mwanaume mwingine, alinikumbatia akiwa amevaliaΒ taulo tu. Mwili ukaanza kunisisimka kama napandwa na sisimiziΒ hivi, mikono ya Mosses ilikuwa kama sumaku vile yaani hataΒ anishike wapi alikuwa akinipandisha ashki zangu.Β
Nilivuta hewa kisha nilimwambia MossesΒ
“Nimekumiss sana Mosses” nilisema nikiwa nimemkumbatia kwaΒ nguvu, nilikuwa na hisia kali sana kwa MossesΒ
“Nimekumiss pia Jacklin, pole kwa matatizo yaliyokupata,Β siamini kama bado unaishi, nilijuwa umeshakufa ndio maanaΒ niliamuwa kubadilisha namba” Alisema Mosses akiwa ananipigaΒ busu shingoni, nilifumba macho kwa utamu wa Busu, nilikuwaΒ nusu Chizi kwa Mwanaume huyu
“Naishi kwa ajili yako Mosses, kama siyo wewe ningelikuwaΒ nimekufa zamani sana ila nguvu ya Mapenzi niliyonayo juu yakoΒ ndiyo iliyonipa uhai nikaamka tena” Nilisema pia, aliniachiaΒ akanitazama jinsi nilivyokuwa nimependeza ilitosha kumfanyaΒ Mosses atambuwe kuwa maisha yangu yalikuwa yamebadilika kwaΒ kiasi kikubwa sana.Β
“Nakupenda sana Mosses” Nilimwambia, naye alirudisha jibuΒ zuri sanaΒ
“Umenipa sababu ya kuendelea kuishi Jacklin, niliposikia kuwaΒ huwezi kupona nilihisi unakufa, nilitamani kufanya kila kituΒ ili niokoe uhai wako” Alisema Mosses, nilijuwa ni uwongoΒ lakini nguvu ya mapenzi iliniambia kuwa anachokisena MossesΒ kina ukweliΒ
“Tuachane na hayo Mosses naomba tuongee ndani” Nilisema kishaΒ tuliingia chumbani kwa Mosses. Nilitazama jinsi chumba chaΒ Mosses kilivyo, sikupenda aendelee kuishi hapo, nilikuwa naΒ uwezo wa kubadilisha Maisha ya Mosses sababu nilikuwaΒ nikimpenda sana.Β
“Mosses kwasasa nafanya kazi, Maisha yangu yamebadilika sana.Β Sitopenda uendelee kuishi hapa nitakupangia sehemu nzuri yaΒ kuishi” Nilimwambia MossesΒ
“Jamani kweli Jacklin?” Aliuliza kama Mtu ambaye alikuwaΒ amechanganikiwaΒ
“Ndiyo! Hadhi yako ndani ya moyo wangu ni kubwa sanaΒ hustahili kuishi hapa, tafuta nyumba eneo lililotuliaΒ nitalipia kila kitu na kununua vitu vipya” Nilisema, maraΒ moja Mosses alinivaa na kuanza kunipiga mabusu ambayoΒ yaliamsha hisia zangu, nilijikuta nikiwa na hamu ya kufanyaΒ Mapenzi na Mosses, daktari alisema sipaswi kufanya hivyo hadiΒ miezi sita itakapoisha lakini nilijikuta nikifanya mapenzi naΒ Mosses, baada ya kumaliza nilimshukuru Mosses kwa penzi tamuΒ alilonipa.Β
“Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisemaΒ Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwaΒ pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalalaΒ palepale.Β
Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwaΒ nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,Β alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwaΒ nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kamaΒ nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipoΒ nyumbani.
Β
Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TANO Ya PUMZI YA MWISHO
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMΒ Β
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ
32 Comments
Huyu dada n jauuuuuuuuu
Uyu dada wawapi vp mbona siyo muelewa kweli mapenzi ni giza
Mbona fupiiii leo
Ila jackline ni kiazi sanaππ
Dah bora uyu mdad angekufa2π’
MH!
Jacqueline hafai hata kwa kulumagia Dah!!πππππ
Ivi hii ndo maana ya β the when a woman loves….βπ° namhurumia Osman
Maskini osmani daah!! Jacklin bora angekufa mwandishi naomba hii story isituboe
Siyo kuboa tuu inaweza kukuliza huko mbeleeπππ
Yani ishaanza kuboa ila sisi wanawake basi tu jacklin wewe mmhπ π π
MH!
Sjawahi Comment Ila WANAWAKE JAU πππ
Fear women..
kesho muendeleze jaman kali kinoma
kesho muendeleze jaman kali
Jau kubabeq
Adimn kuchoshana ww andik zeEND…..mosses anamzurum jack……akn bado Osman anamsamehe
Ahahahaha siyo kumdhulumu atakuja kumcheat uyo demu….. hii story naifananisha na tamthiliya moja inaitwa mfadhili yaani ni mule mule..badae kati ya osman ama uyo jack mmoja atakufa
Kumbe na ww umeona eh…huyu ni dania kabisa yan…
Jacklin, sio
Fwalaaa sanaa mpaka hasira zimenipandaa wanawake bhanaa afukuzwe hata kazi tuu ubwa huyu
Madem jau sana duuh
π
Dah huyu dad ni zaidi ya shetan ani
Mwenye huruma hanaga bahati
EWAAAH!! DATS KAMA MLIFATILIA COMMENT ANGU YA SIKU ZA NYUMA…NILISEMA HAPO LAZIMA KUNA NAMNA ITAKUWA ANI UYO JACKLINE MPKA AJE KUFUNGUKA AKILI NI BAADAE SANA WAKATI MAMB YAMEHARIBIKAπ₯²π₯²π₯² KAMA UNAE MOYO MDGO UTALIA ππ ILA KI UHALISIA WATU NDO WALIVO JMNIII
Wakina moses mikono juuu…….yaaan zitoke tatu kwa siku
Sasa osmad anashida gani, anatongoza kwa kuhonga, binafsi sijaona kosa la jackline, kwani wameshakubaliana kuwa wapenzi?????
πππ
figo ya kiume imeingiliwa au figo haina jinsia
Kama ni Mimi naenda kuchukua Figo yangu
qqw0kc