Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Moja(11)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Moja(11)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 24, 2024Updated:October 28, 202414 Comments6 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Umenisaliti eeh?” Aliuliza Mosses kama kawaida yake alikuwaΒ  na tabia ya wivu sanaΒ 

    “Siwezi kukusaliti Mosses, unanijuwa vizuri. Sina ujanjaΒ  kwako” nilisema lakini bila kumaanisha chochote na ilikuwaΒ  ndiyo mara ya kwanza nasema kitu mbele ya Mosses bilaΒ  kumaanisha, katika nyakati fulani nilijikuta nikianzaΒ  kujichukia Mwenyewe.Β 

    Mosses alitabasamu tuu kisha alinivuta na kunipiga busu, namiΒ  nilitoa tabasamuΒ 

    “Tulale” alisema Mosses, Basi tulilala Usiku huo hadiΒ  kulipopambazuka. EndeleaΒ 

     

    SEHEMU YA KUMI NA MOJA

    Siku iliyofuata ilikuwa ni Jumatatu iliyoanza kwa jua kali laΒ  mvua, nilimuaga Mosses, nilirudi nyumbani kujiandaa kwa ajiliΒ  ya kwenda kazini japo Mosses aliniambia niache kazi, hataΒ  Mama aliniulizaΒ 

    “Ulilala wapi na unaenda wapi?” Aliniuliza nikiwa tayari kwaΒ  ajili ya kutoka nyumbani kuelekea kaziniΒ 

    “Shikamoo Mama!!” Nilimsalimia kwanzaΒ 

    “Marahaba! Siku hizi unaamuwa tu kulala unapopajuwa wewe,Β  kufanya unachowaza wewe si ndiyo?” Aliniuliza, niliutupaΒ  mkoba kwenye sofa kisha niliketi Mama akiwa amesimamaΒ 

    “Mama nililala Hotelini” Nilimjibu Mama huku Moyo ukinisuta “Na unaenda wapi?” Aliniuliza

    “Naenda kazini” Nilimjibu Mama nikiwa ninafinya vidoleΒ  vyangu, Basi Mama alisogea kisha aliketi kando yanguΒ 

    “Jacklin ningekushauri usiende huko sababu ile ni kampuni yaΒ  Osman na Baba yake, kilichotokea baina yetu na ile FamiliaΒ  hakiwezi kuleta picha nzuri endapo tutaendelea kujihusisha naΒ  ile Familia” Alisema MamaΒ 

    “Mama chochote kilichotokea hakina mahusiano ya moja kwa mojaΒ  na kazi ninayoifanya kwao, hii ni kazi ambayoΒ Β 

    tumeandikishiana mikataba labda waamuwe kuvunja mikataba”Β  NilisemaΒ 

    “Inatosha Jacklin, usiende huko Mwanangu” Alisema Mama lakiniΒ  sikutaka kumsikiliza, moyo wangu uliniambia kuwa napaswa kuwaΒ  karibu zaidi na Osman japo yupo Hospitalini lakini kuwaΒ  ofisini kwake kungefanya moyo wangu utulieΒ 

    “Mama najuwa ninachokifanya, usijali kila kitu kitaenda sawa”Β  Nilisema kisha nilinyanyuka na kuondoka zangu.Β 

    Nilizongwa na mawazo kichwani, nilizongwa na hisia kali ndaniΒ  ya moyo wangu, hisia ambazo zilinikosesha raha kabisa.Β  Niliingia ofisini kwangu na kuanza kazi, nilitekelezaΒ  majukumu yangu ndani ya kampuni ya JM Motors. Siku hiyo MzeeΒ  Dhabi alikuja kwenye kampuni kukagua utendaji wa kaziΒ  unavyoendelea, hakujuwa kama Mimi ni mmoja wa wafanyakazi,Β  aliponiona aliniulizaΒ 

    “Wewe ni miongoni Mwao?” Akimaanisha hao Wafanyakazi “Ndiyo Baba” Nilimjibu tukiwa wawili tu ofisiniΒ 

    “Usiniite Baba, Niite Mzee Dhabi inatosha” Alisema MzeeΒ  Dhabi, hapo ndipo nilipokumbuka maneno ya Mama kuwa siyoΒ  busara sana kurudi kufanya kazi ndani ya kampuni ya BilioneaΒ  Dhabi kutokana na kilichotokea kati yangu na Kijana wakeΒ 

    “Mbona katika orodha ya Wafanyakazi wewe haupo, OsmanΒ  alikuajili vipi?” Aliuliza Mzee Dhabi kisha aliketi,Β  niliiyona chuki ndani yake, nilijawa na kigugumiziΒ 

    “Mbona nilishajaza mkataba na kupewa hii Ofisi” nilijibuΒ 

    “Hapana, Mimi ndiye Mwenye hii kampuni, Osman anasimamiaΒ  sababu ni Kijana wangu! Sikutambui, hakuna mkataba ulio mbeleΒ  yangu” Alisema Bilionea Dhabi tena kwa sura kavu sana

    “Lakini mbona nilifanya usahili hapa na kujaza mkataba waΒ  kazi iweje leo nisitambulike” NiliulizaΒ 

    “Ni huruma ya Osman ambayo imemteketeza ndiyo iliyokufanyaΒ  wewe kuwa hapa lakini hukupaswa kuwa hapa, nikiwa kamaΒ  Mmiliki wa hii kampuni, sihitaji kukuona hapa kuanzia mudaΒ  huu, kusanya kila kilicho chako” Alisema Bilionea Dhabi kamaΒ  vile hakuwahi kuniona kabla, ujuwe nilichoka sana kuanziaΒ  roho hadi mwili, ningesema nini na aliyesimama mbele yanguΒ  alikuwa ndiye mmiliki wa kampuni hiyoΒ 

    Nilifanya kama alivyosema tena akiwa amenisimamia, niliondokaΒ  kwenye kampuni ya JM Motors, nilijuwa chuki aliyoionesha MzeeΒ  Dhabi ilitokana na jinsi nilivyokataa kuokoa uhai wa KijanaΒ  wake japo dakika za mwisho niliufungua moyo wangu ilaΒ  nilikuwa nimeshachelewa, Chozi lilinibubujika. Tayari mvuaΒ  ilikuwa imeanza kunyesha.Β 

    Nilitembea kwenye mvua huku nikikumbuka siku ya kwanza kabisaΒ  ambayo Osman alinisaidia kwenye mvua, nilipofika nyumbaniΒ  nilimsimulia Mama kile kilichotokea.Β 

    “Nilikwambia Mwanangu lakini hata Usijali sana sababu umesomaΒ  utapata kazi sehemu nyingine na Maisha yataendelea” alisemaΒ  MamaΒ 

    “Lakini Mama, natamani sana kulipa fadhila za Osman,Β  amebadilisha Maisha yetu kutoka kwenye Umasikini, ameokoaΒ  Maisha yangu kutoka kifo, nilichelewa kuiyona thamani yaΒ  Upendo na huruma yake” Nilisema nikiwa nimeegemea ukutaΒ 

    “Usijutie kwa chochote sababu anayepanga kila kitu ni MunguΒ  pekee, Maisha lazima yaendelee” Alisema Mama, mara tulisikiaΒ  honi ya gari. Mama alichungulia, aliona gari ya Mzee DhabiΒ  ikiingia,Β 

    “Baba yake Osman anakuja” Alisema, nilikuwa nimelowa kutokanaΒ  na ile mvua hivyo nilihitaji kubadilisha nguo haraka,Β  nilielekea chumbani kwangu kubadilisha nguo, nilipotokaΒ  niliwakuta Mama na Bilionea Dhabi wakiwa wameketi hapanaΒ  shaka walikuwa wakinisubiria Mimi.Β 

    Niliketi kwa utulivu sana, nilimtazama Bilionea Dhabi ambayeΒ  alikuwa ameongozana na Mke wake.Β 

    “Shikamoo Mama” Nilimsalimia Mama yake Osman ambaye hataΒ  hakuitikia, nilipata ishara kuwa hawakuja kwa lengo zuri,Β  alianza Bilionea Dhabi kusema

    “Tumekuja kwa ajili ya mambo mawili makubwa, moja ni kuchukuaΒ  magari ambayo Osman alikununulia, mbili ni kuchukua nyumbaΒ  hii ambayo mnaishi” Alisema Mzee Dhabi kwa sura kavu sana.Β  Mama alishtuka sanaΒ 

    “Unasemaje?” AlihojiΒ 

    “Pesa iliyotumika hapa ni pesa yangu Mimi, maamuziΒ  ninayoyatoa yanatoka kwangu Mimi pia. Iwe mlipewa hati auΒ  hamkupewa Hati ya Hapa, mnaondoka na jeuri yenu” AlisemaΒ  Bilionea DhabiΒ 

    “Baba tafadhali sana hebu fikiria tutakwenda wapi sisi?Β  Fikiria kwa kipindi hiki tutafanya nini?” Alisema Mama akiwaΒ  analia, nilizidi kuumia ndani ya nafsi yanguΒ 

    “Kwani zamani mlikuwa mnaishi wapi? Mlikuwa mnaishi vipiΒ  kabla ya kuanza kutumia pesa za Osman?” Aliuliza BilioneaΒ  Dhabi, nilikaa kimya bila kusema chochote sababu sikuwa naΒ  cha kusemaΒ 

    “Nionee huruma Mimi, Mimi ni mtu mzima nitaishi vipi Baba,Β  fikiria hilo ina maana makosa ya Binti yangu yanatufanya tuweΒ  maadui?” Aliuliza Mama akiwa katika hali ile. Ile ya kilioΒ 

    “Siyo maadui tu bali ni maadui wa Maisha, adui wa Maisha yaΒ  Kijana wangu ni adui yangu pia, mna siku mbili za kuhakikishaΒ  mnahama hapa, gari zinaondoka sasa hivi” Alisema BilioneaΒ  Dhabi kisha yeye na Mke wake walinyanyuka, Mke wa BilioneaΒ  Dhabi hakusema chochote kama ambavyo Mimi sikusema chochote,Β  Mama na Bilionea Dhabi ndio ambao walikuwa wakirushianaΒ  manenoΒ 

    “Nakuomba tuonee huruma sisi, tutaenda wapi, siku mbiliΒ  jamani Aaah” Mama alisema lakini hakukuwa na maelewano, MzeeΒ  Dhabi aliondoka bila hata kuchukua Funguo za Magari. NililiaΒ  sana, nilikumbuka kuwa Kulikuwa na pesa kwenye akaunti yaΒ  Benki zaidi ya Milioni 60 ambazo Osman alinipatia, kadiΒ  ilikuwa kwa Mosses, haraka nilimpigia na kuhitaji kuonanaΒ  naye.Β 

    Alinielekeza alipo niliondoka na kumuacha Mama akiwa analia,Β  nilienda kuonana na Mosses. Nilimsimulia kilichotokea,Β  nilihitaji Milioni 40 ili kununua nyumba ya kuishi Na MamaΒ  ila majibu ya Mosses yalinigandisha damu, alisema Pesa zoteΒ  aliziweka kwenye Biashara yake ya Mazao hivyo nisubirie ndaniΒ  ya mwezi mmoja angenipatia pesa hizo.

    “Lakini Mosses mbona hukuniambia kama unafungua Biashara?Β  Unafikiria ndani ya huo mwezi Mimi na Mama tutakuwa tunaishiΒ  wapi?” Nilimuuliza MossesΒ 

    “Sasa Jacklin unafikiria pesa inahifadhiwa benki kama pamboΒ  la nyumba? Pesa ni lazima izunguke ili izae halafu Mimi niΒ  Mwanaume nimefanya maamuzi ya kiume” Alisema Mosses, suraΒ  yake ilianza kutanda hasira. Sikutaka kuendelea kubishanaΒ  naye nilimkubaliaΒ 

    “Sawa Mume wangu! Nakutegemea wewe kwasasa” nilisema “Usijali” alijibu Mosses, nilimuaga nikarudi nyumbani kwetu.Β 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya KUMI NA MBILI Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ 

    Pumzi ya mwisho

    14 Comments

    1. Esther on October 24, 2024 5:18 pm

      πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    2. Juju boy on October 24, 2024 5:45 pm

      Thank you, hapo good,

      Reply
      • G shirima on October 25, 2024 12:16 am

        Fupi sana Jamani dah

        Reply
    3. Hamis on October 24, 2024 5:55 pm

      Anakumbuka shuka kumesha kucha

      Reply
    4. Irene LiwayaπŸ’ž on October 24, 2024 5:56 pm

      Mambo ni Fire oooooohπŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯ amechezea bahati ona anavyopata tabu…! Hivi dunia ya sasa wapo watu kama kina jack maaaana oh mie weeee mapema na kwa haraka sana ningemkubalia osman I don’t care na mahusiano yanguπŸ€ͺπŸ€ͺπŸ‘ŒπŸΌπŸ‘ŒπŸΌπŸ‘ŒπŸΌπŸ‘ŒπŸΌ

      Reply
    5. Dr paul on October 24, 2024 6:38 pm

      Unyama liwaya zuri

      Reply
    6. Asaphnaah on October 24, 2024 7:19 pm

      Kwann hamna comment ya voice note jmn duuh ila admin endelea ubaya ubwelaπŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
      • Siwema on October 24, 2024 11:15 pm

        Kilanga koma

        Reply
    7. Roda on October 24, 2024 8:42 pm

      🀣ukiskia mtot kautak ndy huku saaa 🀣kibur hakisaidii kitu jack na kibur chak cha uzima xhek xxπŸ€£πŸ‘Œ

      Reply
    8. Hamisi on October 24, 2024 8:48 pm

      Ya leo umetuonea fupi sana..
      Au kwasababu ya utamu?

      Reply
    9. Rachel Richard on October 24, 2024 9:17 pm

      Ivi mnaniruhusu nmtukane Jack maana nnavompatia hasira jaman 🀨😠

      Reply
    10. Negro jr on October 25, 2024 5:24 pm

      Jaman jack amazingatia mno mapenz kuliko maokoto

      Reply
    11. Sharo love malkx πŸ’– on October 26, 2024 3:43 pm

      Shida yangu afee tuu uyo binti
      Jack chanπŸ€”πŸ€”

      Reply
    12. πŸ–‡ + 1.821248 BTC.NEXT - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=f606e273765951e4c4ede8ed9cb384fa& πŸ–‡ on July 4, 2025 8:16 am

      6ciw4u

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 14, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya pili Alipiga magoti na kujiinamia huku chozi likimtoka Zahoro,…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.