Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Moja(11)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Moja(11)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 24, 2024Updated:October 28, 202414 Comments6 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Umenisaliti eeh?” Aliuliza Mosses kama kawaida yake alikuwaย  na tabia ya wivu sanaย 

    “Siwezi kukusaliti Mosses, unanijuwa vizuri. Sina ujanjaย  kwako” nilisema lakini bila kumaanisha chochote na ilikuwaย  ndiyo mara ya kwanza nasema kitu mbele ya Mosses bilaย  kumaanisha, katika nyakati fulani nilijikuta nikianzaย  kujichukia Mwenyewe.ย 

    Mosses alitabasamu tuu kisha alinivuta na kunipiga busu, namiย  nilitoa tabasamuย 

    “Tulale” alisema Mosses, Basi tulilala Usiku huo hadiย  kulipopambazuka. Endeleaย 

     

    SEHEMU YA KUMI NA MOJA

    Siku iliyofuata ilikuwa ni Jumatatu iliyoanza kwa jua kali laย  mvua, nilimuaga Mosses, nilirudi nyumbani kujiandaa kwa ajiliย  ya kwenda kazini japo Mosses aliniambia niache kazi, hataย  Mama aliniulizaย 

    “Ulilala wapi na unaenda wapi?” Aliniuliza nikiwa tayari kwaย  ajili ya kutoka nyumbani kuelekea kaziniย 

    “Shikamoo Mama!!” Nilimsalimia kwanzaย 

    “Marahaba! Siku hizi unaamuwa tu kulala unapopajuwa wewe,ย  kufanya unachowaza wewe si ndiyo?” Aliniuliza, niliutupaย  mkoba kwenye sofa kisha niliketi Mama akiwa amesimamaย 

    “Mama nililala Hotelini” Nilimjibu Mama huku Moyo ukinisuta “Na unaenda wapi?” Aliniuliza

    “Naenda kazini” Nilimjibu Mama nikiwa ninafinya vidoleย  vyangu, Basi Mama alisogea kisha aliketi kando yanguย 

    “Jacklin ningekushauri usiende huko sababu ile ni kampuni yaย  Osman na Baba yake, kilichotokea baina yetu na ile Familiaย  hakiwezi kuleta picha nzuri endapo tutaendelea kujihusisha naย  ile Familia” Alisema Mamaย 

    “Mama chochote kilichotokea hakina mahusiano ya moja kwa mojaย  na kazi ninayoifanya kwao, hii ni kazi ambayoย ย 

    tumeandikishiana mikataba labda waamuwe kuvunja mikataba”ย  Nilisemaย 

    “Inatosha Jacklin, usiende huko Mwanangu” Alisema Mama lakiniย  sikutaka kumsikiliza, moyo wangu uliniambia kuwa napaswa kuwaย  karibu zaidi na Osman japo yupo Hospitalini lakini kuwaย  ofisini kwake kungefanya moyo wangu utulieย 

    “Mama najuwa ninachokifanya, usijali kila kitu kitaenda sawa”ย  Nilisema kisha nilinyanyuka na kuondoka zangu.ย 

    Nilizongwa na mawazo kichwani, nilizongwa na hisia kali ndaniย  ya moyo wangu, hisia ambazo zilinikosesha raha kabisa.ย  Niliingia ofisini kwangu na kuanza kazi, nilitekelezaย  majukumu yangu ndani ya kampuni ya JM Motors. Siku hiyo Mzeeย  Dhabi alikuja kwenye kampuni kukagua utendaji wa kaziย  unavyoendelea, hakujuwa kama Mimi ni mmoja wa wafanyakazi,ย  aliponiona aliniulizaย 

    “Wewe ni miongoni Mwao?” Akimaanisha hao Wafanyakazi “Ndiyo Baba” Nilimjibu tukiwa wawili tu ofisiniย 

    “Usiniite Baba, Niite Mzee Dhabi inatosha” Alisema Mzeeย  Dhabi, hapo ndipo nilipokumbuka maneno ya Mama kuwa siyoย  busara sana kurudi kufanya kazi ndani ya kampuni ya Bilioneaย  Dhabi kutokana na kilichotokea kati yangu na Kijana wakeย 

    “Mbona katika orodha ya Wafanyakazi wewe haupo, Osmanย  alikuajili vipi?” Aliuliza Mzee Dhabi kisha aliketi,ย  niliiyona chuki ndani yake, nilijawa na kigugumiziย 

    “Mbona nilishajaza mkataba na kupewa hii Ofisi” nilijibuย 

    “Hapana, Mimi ndiye Mwenye hii kampuni, Osman anasimamiaย  sababu ni Kijana wangu! Sikutambui, hakuna mkataba ulio mbeleย  yangu” Alisema Bilionea Dhabi tena kwa sura kavu sana

    “Lakini mbona nilifanya usahili hapa na kujaza mkataba waย  kazi iweje leo nisitambulike” Niliulizaย 

    “Ni huruma ya Osman ambayo imemteketeza ndiyo iliyokufanyaย  wewe kuwa hapa lakini hukupaswa kuwa hapa, nikiwa kamaย  Mmiliki wa hii kampuni, sihitaji kukuona hapa kuanzia mudaย  huu, kusanya kila kilicho chako” Alisema Bilionea Dhabi kamaย  vile hakuwahi kuniona kabla, ujuwe nilichoka sana kuanziaย  roho hadi mwili, ningesema nini na aliyesimama mbele yanguย  alikuwa ndiye mmiliki wa kampuni hiyoย 

    Nilifanya kama alivyosema tena akiwa amenisimamia, niliondokaย  kwenye kampuni ya JM Motors, nilijuwa chuki aliyoionesha Mzeeย  Dhabi ilitokana na jinsi nilivyokataa kuokoa uhai wa Kijanaย  wake japo dakika za mwisho niliufungua moyo wangu ilaย  nilikuwa nimeshachelewa, Chozi lilinibubujika. Tayari mvuaย  ilikuwa imeanza kunyesha.ย 

    Nilitembea kwenye mvua huku nikikumbuka siku ya kwanza kabisaย  ambayo Osman alinisaidia kwenye mvua, nilipofika nyumbaniย  nilimsimulia Mama kile kilichotokea.ย 

    “Nilikwambia Mwanangu lakini hata Usijali sana sababu umesomaย  utapata kazi sehemu nyingine na Maisha yataendelea” alisemaย  Mamaย 

    “Lakini Mama, natamani sana kulipa fadhila za Osman,ย  amebadilisha Maisha yetu kutoka kwenye Umasikini, ameokoaย  Maisha yangu kutoka kifo, nilichelewa kuiyona thamani yaย  Upendo na huruma yake” Nilisema nikiwa nimeegemea ukutaย 

    “Usijutie kwa chochote sababu anayepanga kila kitu ni Munguย  pekee, Maisha lazima yaendelee” Alisema Mama, mara tulisikiaย  honi ya gari. Mama alichungulia, aliona gari ya Mzee Dhabiย  ikiingia,ย 

    “Baba yake Osman anakuja” Alisema, nilikuwa nimelowa kutokanaย  na ile mvua hivyo nilihitaji kubadilisha nguo haraka,ย  nilielekea chumbani kwangu kubadilisha nguo, nilipotokaย  niliwakuta Mama na Bilionea Dhabi wakiwa wameketi hapanaย  shaka walikuwa wakinisubiria Mimi.ย 

    Niliketi kwa utulivu sana, nilimtazama Bilionea Dhabi ambayeย  alikuwa ameongozana na Mke wake.ย 

    “Shikamoo Mama” Nilimsalimia Mama yake Osman ambaye hataย  hakuitikia, nilipata ishara kuwa hawakuja kwa lengo zuri,ย  alianza Bilionea Dhabi kusema

    “Tumekuja kwa ajili ya mambo mawili makubwa, moja ni kuchukuaย  magari ambayo Osman alikununulia, mbili ni kuchukua nyumbaย  hii ambayo mnaishi” Alisema Mzee Dhabi kwa sura kavu sana.ย  Mama alishtuka sanaย 

    “Unasemaje?” Alihojiย 

    “Pesa iliyotumika hapa ni pesa yangu Mimi, maamuziย  ninayoyatoa yanatoka kwangu Mimi pia. Iwe mlipewa hati auย  hamkupewa Hati ya Hapa, mnaondoka na jeuri yenu” Alisemaย  Bilionea Dhabiย 

    “Baba tafadhali sana hebu fikiria tutakwenda wapi sisi?ย  Fikiria kwa kipindi hiki tutafanya nini?” Alisema Mama akiwaย  analia, nilizidi kuumia ndani ya nafsi yanguย 

    “Kwani zamani mlikuwa mnaishi wapi? Mlikuwa mnaishi vipiย  kabla ya kuanza kutumia pesa za Osman?” Aliuliza Bilioneaย  Dhabi, nilikaa kimya bila kusema chochote sababu sikuwa naย  cha kusemaย 

    “Nionee huruma Mimi, Mimi ni mtu mzima nitaishi vipi Baba,ย  fikiria hilo ina maana makosa ya Binti yangu yanatufanya tuweย  maadui?” Aliuliza Mama akiwa katika hali ile. Ile ya kilioย 

    “Siyo maadui tu bali ni maadui wa Maisha, adui wa Maisha yaย  Kijana wangu ni adui yangu pia, mna siku mbili za kuhakikishaย  mnahama hapa, gari zinaondoka sasa hivi” Alisema Bilioneaย  Dhabi kisha yeye na Mke wake walinyanyuka, Mke wa Bilioneaย  Dhabi hakusema chochote kama ambavyo Mimi sikusema chochote,ย  Mama na Bilionea Dhabi ndio ambao walikuwa wakirushianaย  manenoย 

    “Nakuomba tuonee huruma sisi, tutaenda wapi, siku mbiliย  jamani Aaah” Mama alisema lakini hakukuwa na maelewano, Mzeeย  Dhabi aliondoka bila hata kuchukua Funguo za Magari. Nililiaย  sana, nilikumbuka kuwa Kulikuwa na pesa kwenye akaunti yaย  Benki zaidi ya Milioni 60 ambazo Osman alinipatia, kadiย  ilikuwa kwa Mosses, haraka nilimpigia na kuhitaji kuonanaย  naye.ย 

    Alinielekeza alipo niliondoka na kumuacha Mama akiwa analia,ย  nilienda kuonana na Mosses. Nilimsimulia kilichotokea,ย  nilihitaji Milioni 40 ili kununua nyumba ya kuishi Na Mamaย  ila majibu ya Mosses yalinigandisha damu, alisema Pesa zoteย  aliziweka kwenye Biashara yake ya Mazao hivyo nisubirie ndaniย  ya mwezi mmoja angenipatia pesa hizo.

    “Lakini Mosses mbona hukuniambia kama unafungua Biashara?ย  Unafikiria ndani ya huo mwezi Mimi na Mama tutakuwa tunaishiย  wapi?” Nilimuuliza Mossesย 

    “Sasa Jacklin unafikiria pesa inahifadhiwa benki kama pamboย  la nyumba? Pesa ni lazima izunguke ili izae halafu Mimi niย  Mwanaume nimefanya maamuzi ya kiume” Alisema Mosses, suraย  yake ilianza kutanda hasira. Sikutaka kuendelea kubishanaย  naye nilimkubaliaย 

    “Sawa Mume wangu! Nakutegemea wewe kwasasa” nilisema “Usijali” alijibu Mosses, nilimuaga nikarudi nyumbani kwetu.ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya KUMI NA MBILI Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย 

    Pumzi ya mwisho

    14 Comments

    1. Esther on October 24, 2024 5:18 pm

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    2. Juju boy on October 24, 2024 5:45 pm

      Thank you, hapo good,

      Reply
      • G shirima on October 25, 2024 12:16 am

        Fupi sana Jamani dah

        Reply
    3. Hamis on October 24, 2024 5:55 pm

      Anakumbuka shuka kumesha kucha

      Reply
    4. Irene Liwaya๐Ÿ’ž on October 24, 2024 5:56 pm

      Mambo ni Fire ooooooh๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ amechezea bahati ona anavyopata tabu…! Hivi dunia ya sasa wapo watu kama kina jack maaaana oh mie weeee mapema na kwa haraka sana ningemkubalia osman I donโ€™t care na mahusiano yangu๐Ÿคช๐Ÿคช๐Ÿ‘Œ๐Ÿผ๐Ÿ‘Œ๐Ÿผ๐Ÿ‘Œ๐Ÿผ๐Ÿ‘Œ๐Ÿผ

      Reply
    5. Dr paul on October 24, 2024 6:38 pm

      Unyama liwaya zuri

      Reply
    6. Asaphnaah on October 24, 2024 7:19 pm

      Kwann hamna comment ya voice note jmn duuh ila admin endelea ubaya ubwela๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
      • Siwema on October 24, 2024 11:15 pm

        Kilanga koma

        Reply
    7. Roda on October 24, 2024 8:42 pm

      ๐Ÿคฃukiskia mtot kautak ndy huku saaa ๐Ÿคฃkibur hakisaidii kitu jack na kibur chak cha uzima xhek xx๐Ÿคฃ๐Ÿ‘Œ

      Reply
    8. Hamisi on October 24, 2024 8:48 pm

      Ya leo umetuonea fupi sana..
      Au kwasababu ya utamu?

      Reply
    9. Rachel Richard on October 24, 2024 9:17 pm

      Ivi mnaniruhusu nmtukane Jack maana nnavompatia hasira jaman ๐Ÿคจ๐Ÿ˜ 

      Reply
    10. Negro jr on October 25, 2024 5:24 pm

      Jaman jack amazingatia mno mapenz kuliko maokoto

      Reply
    11. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on October 26, 2024 3:43 pm

      Shida yangu afee tuu uyo binti
      Jack chan๐Ÿค”๐Ÿค”

      Reply
    12. ๐Ÿ–‡ + 1.821248 BTC.NEXT - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=f606e273765951e4c4ede8ed9cb384fa& ๐Ÿ–‡ on July 4, 2025 8:16 am

      6ciw4u

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane โ€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.