Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pigo Takatifu Sehemu Ya Sita (06)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Sita (06)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 17, 2024Updated:September 18, 202411 Comments14 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Fanya haraka” Akaelekezwa mahali ambapo angemwona Matilda,ย  japo dakika mbili zisingetoshea kuzungumza naye ila alihitajiย  kumwona na kupata uhakika kua ana Mtoto na Bosi wake,ย  akapelekwa chumba kimoja ambacho kilikua rasmi kwa ajili yaย  kuonana na Mahabusu, akasubiria hapo Matilda aletwe, sekundeย  chache Matilda akafika hapo akiwa ameongozana na yule Polisiย 

    Hakumkumbuka Jack sababu alimwona kwa Mara ya kwanza paleย  ofisini kwa James hivyo ilikua rahisi kwake kukubali kuonanaย  na Jack, akaketi huku akiwa anamtazama sana Jackย 

    “Samahani na pole Matilda, Naitwa Jack” Alijitambulisha Jackย 

    “Unanifahamu Mimi?” akauliza Matilda akionekana alikuaย  ameteswa sana, uso ulikua na majeraha kadhaaย 

    “Ndiyo nakufahamu japo si sana”ย  Endelea

    SEHEMU YA SITAย 

    “Mbona Mimi sikufahamu?” akauliza Matildaย 

    “Mimi ni mfanyakazi wa James, nimekuja nahitaji kujua baadhiย  ya vitu kutoka kwako” Akasema Jackย 

    “Kwahiyo James amekutuma uje kwangu unilaghai kwa kutegemeaย  kua nitakubali si ndiyo, sikia nikwambie kitu kimoja,ย  Nimeamua kuishi Maisha ambayo sitaki kuitwa Msaliti na Mtotoย  wangu, nitasimama naye hadi mwisho na kama unafikiria utawezaย  basi nakwambia katu hautoweza kunishawishi kwa chochote kile,ย  nenda kamwambie James, kama Mtoto wangu atakufa basi atabebaย  msalaba na kamwe sitakubali” Alisema kwa hasira sana Matildaย  hadi yule polisi akaona ni bora amrejeshe Mahabusu maanaย  kusingezungumzika kabisaย 

    “Sina nia hiyo Matilda nakuomba unisikilize” akazungumzaย  lakini Matilda aliondolewa hapo, kisha baadaye yule polisiย  akamfuata Jackย 

    “Usirudi tena, hii ilikua nafasi pekee”ย 

    “Lakini sikua na nia ya kumkasirisha kabisa, nilihitajiย  kumsaidia” Akasema Jackย 

    “Hayo hayanihusu Mimi, nimetenda wema niliopaswa kukutendea,ย  utamsaidiaje ni juu yako” Akasema Polisi huku akimtaka Jackย  aondoke Kiunyonge sana tofauti na alivyoingia kituoni, Jackย  alionekana akishusha ngazi kwa kutumia kiatu chake kirefu,ย  Macho yake yakatua waliposimama Mchungaji na Mama Naomi, Maraย  moja wakasogea karibu kumpokeaย 

    “Vipi umefanikiwa kumwona?” akauliza Mchungajiย 

    “Anaendeleaje?” akauliza Mama Naomi huku nyuso zao zikioneshaย  shahuku kubwa ya kutaka kujua kilichotokea huko ndaniย 

    “Hataki kuzungumza na Mimi, inaonesha ana maumivu makaliย  sana” Akasema Jack akiwa anasogea karibu na gari yake,ย  Mchungaji na Mama Naomi wakiwa wanamfuataย 

    “Yupo salama?” akauliza Mchungaji, Jack akatikisa kichwa kamaย  ishara ya kua Matilda hayupo salama.ย 

    “Niambie Matilda amekuaje?” alihoji Mchungaji, yeye ndiyeย  aliyempokea Matilda kanisani kwa mara ya kwanza. hivyoย  Matilda kwake ni sawa na Mtoto wa kumzaa.ย 

    “Siwezi kuzungumza nahitaji kutuliza akili kuona ninamsaidiaย  vipi, Tutawasiliana” akasema Jack kisha akaingia kwenye gariย  yake na kuondoka hapo haraka sana, akawaacha Mchungaji naย  Mama Naomi wakiwa hawajui kilichoendelea kati ya Jack naย  Matilda.ย 

    “Ni bora angeeleza kiilichotokea kuliko kukaa kimya, hapanaย  shaka amemwona Matilda, roho inaniuma sana” Alisema Mamaย  Naomi akionekana kujawa na uchungu, chozi lilimlenga, alikuaย  hajatulia tokea asubuhi kwa ajili ya Matildaย 

    “Naomba urudi nyumbani giza linaanza kuingia, pesa hiiย  itakusaidia. Mimi narudi kanisani kwa ajili yaย  maombi….Najua shetani yupo mahali anafanya kazi yake”ย  Akasema Mchungaji kisha akampatia noti ya Elfu Kumi Mamaย  Naomiย 

    “Lakini Mchungaji natamani nilale hapa ili nijue Matildaย  anapitia wakati gani, naona kama tunamzika Matilda bilaย  kusikia kilio chake” Akasema Mama Naomi akiwa ameshika notiย  mkononi huku chozi likianza kuvujaย 

    “Usilie..Hakuna marefu yasiyo na Ncha, kua na imani kua Munguย  atatenda na Matilda atatoka”

    “Sawa Mchungaji” Alisema Mama Naomi, akaita Bajaji kwa ajiliย  ya kurejea anapoishi maana kwa muda huo ingekua shughuli pevuย  kupata daladala, kwa wanaoishi Dar wanajua liingiapo gizaย  vurugu za kugombania usafiri zinavyochukua sura tofauti.ย 

    Mchungaji alisubiria hadi Mama Naomi alipoondoka ndipo nayeย  akaondoka kituoni.ย 

    ********ย 

    Mawazo chungu mzima yalikua yakipita kwenye kichwa chaย  Bilionea James, alikunywa pombe ili kuondoa mawazo yaliyokuaย  kichwani pake, moyo wake haukua na pingamizi kua Mtoto Patraย  alikua ni damu yake lakini Neema alikua na ujauzito ambaoย  aliamini wazi ni wake.ย 

    Alikua na tumaini kubwa la kupata Mtoto ambaye angekuja kuaย  Mrithi wa utajiri wake uliokithiri, hakupokea simu ya Neemaย  wala Mama yake Neema, alizidi kuchanganikiwa, licha yaย  utajiri alio nao lakini alijikuta katika wakati mgumu sanaย  kisa Mtoto, akifikiria namna Matilda na Mtoto wanavyotesekaย  anajikuta akikuna kichwa chake, alitamani sana kumsaidiaย  Matilda lakini pia wazo la kua Mtoto afe lilikua likimtawala,ย  kauli ya Matilda kua atahakikisha anamfilisi ilianza kumyimaย  raha, akamtafuta Chilo ili apate ushauriย 

    “Yupo sahihi sababu ana Mtoto ambaye akipimwa DNAย  itagundulika wazi ni wako, akikufungulia kesi unafikiriaย  utatokea wapi Kaka? Hii serikali haiangalii una pesa kiasiย  gani, kwa kifupi alichosema ana uhakika nacho James” Alisemaย  Chilo wakiwa wameketi mahali wakipeana Ushauriย 

    “Sasa nifanye nini, Nimhudumie Mtoto kisha nimtoe Matilda?”ย 

    “Kama amekataa kurejea kwao hata kama utafanya yote badoย  atakugandamiza James, Kama nilivyokwambia serikali ipo machoย  sana kwa kesi za namna hii”ย 

    “Sasa unanishauri lipi Kaka”ย 

    “Kubali kua Patra ni Binti yako, mlee kama Binti yako, mfanyeย  Matilda aone mpo pamoja kisha mfanye wa siri ili Neema asijueย  chochote hadi pale atakapojifungua”ย 

    “Ushauri wako ni mzuri sana, nimetafakari usiku kuchaย  nawezaje kumaliza hili jambo katika namna ambayo itaniachaย  salama”ย 

    “Ikishindikana njia hiyo Kaka juwa kua hilo jambo ni gumuย  kuliko ufikiliavyo, hapana shaka Matilda ana hasira naweย  kwasababu anahisi wewe umeshilikiana na Neema ili kumwekaย  yeye ndani” Alisema Chiloย 

    “Naamini Patra akipatiwa matibabu hilo haliwezi kua shida kwaย  Matilda, ikibidi nitamtibia nje ya Nchi ili Matilda aende naย  Mtoto huko, hadi wao watakaporejea Nchini nitakuwaย  nimejipanga vizuri kuhakikisha hakuna kinachoharibika”ย 

    “Tena hapo utakua umeuwa ndege wawili kwa jiwe moja Kaka,ย  Acha Neema aamini kua Matilda amerudi kwao lakini upande waย  pili unapambana kuhakikisha anatibiwa, naamini utashinda”ย 

    Haikua rahisi kwa Jack kupata Usingizi usiku huo, taswira yaย  Patra namna anavyoteseka Hospitalini iliendelea kujirudiaย  katika Ufahamu wake wa akili, alijikuta akiwa katika nyakatiย  ambayo kila alichokiwaza kilizidi kuibomoa akili yake, ikawaย  ngumu kuukubali ukweli kua Bosi wake James alikua ametendaย  unyama ule.ย 

    *****ย 

    Asubuhi mapema, Jack akaondoka katika makazi yake, alifungaย  safari kuelekea kwa Mama yake James. Naam! alihitaji zaidiย  kujua baadhi ya mambo ambayo yangemfanya apate njia yaย  kulianza jambo hilo ambalo aliona wazi lilimhitaji kwa kiasiย  kikubwa, alipahafahamu kwa Mama yake James, hata Mama yakeย  James alikua akimfahamu sana Jack, alipomwona alimkaribishaย  ndani.ย 

    Jua lilikua tayari limeshaanza kuchoma na kuunguza ngozi,ย  chai ikawa tayari, wakaketi mezani kwa ajili ya kuzungumza,ย  Mama James alishagundua kua kuna jambo lililomleta Jack paleย 

    “Karibu sana Jacklin” Alisema Mama yake Jamesย 

    “Ahsante Mama”ย 

    “Umenisusa sana Mwanangu”ย 

    “Aaah Mama unajua majukumu ni mengi nakosa hata muda wa kujaย  huku siku hizi”ย 

    “Wala usijali naelewa”ย 

    “Mama kuna jambo linanitatiza sana katika akili yangu,ย  limekua ni jambo lililobadili kabisa mtazamo wangu juu yaย  James” Alisema Jack kisha alimtazama Mama yake James ambayeย  alikaa vizuri kumsikiliza huku chai ikiwa inatoa mvuke

    “Jambo lipi hilo mbona unanitisha Jack”ย 

    “Mama….sijui hata nianzie wapi, naomba kujua, James anaย  watoto wangapi?” aliuliza Jack, Mama James akashusha pumziย  baada ya kusikia swali hiloย 

    “James hana Mtoto..”ย 

    “Una hakika Mama?”ย 

    “Jack, Mimi ndiye Mama Mzazi wa James, akiwa na jambo niย  lazima anishirikishe……Hajawahi niambia chochote kileย  kuhusu kua na Mtoto, isipokua yupo Msichana anayetarajiaย  kumzalia Mtoto, huyu namfahamu sababu alishawahi kumletaย  Hapa, zaidi ya hapo hakuna Jack…sijui ni kwanini umeulizaย ย hilo swali”ย 

    “Mama naomba nikwambie hili jambo, pengine nitatua mzigoย  fulani kichwani pangu, James ana Mtoto ana miaka mitatu sasaย  anaitwa Patra” Alisema Jack, Mama James akashtuka kidogoย 

    “James ana Mtoto? hilo haliwezekani Jack, hawezi kua na Mtotoย  alafu anifiche Mimi, angeniambia tu” akasema Mama Jamesย 

    “Hata Mimi nilishtuka na sikuamini kama wewe ambavyo huamini,ย  Mama,,James kua na Mtoto siyo tatizo ila tatizo ni kwanbaย  amemkataa huyo Mtoto kwasababu ni Mlemavu, na Hapaย  ninapozungumza Mtoto huyo yupo Hospitali Magomeni hali yakeย  siyo nzuri, Mama wa Mtoto yupo polisi kwa kesi ambayoย  inaonekana wazi kua James ameitengeneza…”ย 

    “Jack hivi unajua unazungumza maneno mazito sana ambayoย  hayaingii akilini mwangu, James hajawahi niambia kua anaย  Mtoto. Hili jipya kulisikia.”ย 

    “Mama hiyo ndiyo hali halisi, Mtoto amefanana sana na James.ย  Nimekuja hapa sababu sitaki Mjukuu wako azidi kuteseka,ย  sikujua kama James hakukwambia kuhusu hili, Mama nakuombaย  fanya jambo katika hili vinginevyo Mtoto anaweza kufarikiย  kule Hospitalini” Akasema Jack akiwa na uso ulio poteza nuru,ย  alihitaji huruma ya Mama James kuingilia kati huku akiaminiย  fika kua si rahisi kumfikia James ambaye ndiye Bosi wakeย 

    “Jack nahitaji kwanza kumwona huyo Mtoto ”ย 

    “Kama tunaweza ongozana Hospitali muda huu itakua vizuriย  Mama”

    “Sawa!!” Mama James na Jack wakakubaliana kua waelekeeย  Hospitali kwa ajili ya kumwona Patra.ย 

    Asubuhi hiyo, Neema akaelekea kituo cha polisi, akazungumzaย  na yule polisi ambaye alishapewa pesa ili kumshikiliaย  Matilda, wakazungumza kwa dakika kadhaa kisha Neema akaondokaย  hapo, kitendo cha kupokea simu ya polisi kua James aliendaย  Polisi kilimfanya atengeneze mpango mwingine kwa ajili yaย  kutekeleza takwa lake kwa Matilda ambaye kadili mudaย  ulivyokua ukienda alikua akiendelea kuteseka pale kituo chaย  polisi, yule polisi akarudi ndani ya kituo maana maongeziย  yalifanyika ndani ya gari ya Neema.ย 

    Masaa matatu yakapita baada ya polisi kuzungumza na Neema,ย  Mchungaji George alikua nje ya kituo hicho huku akimpa Mamaย  Naomi jukumu la kushinda kule Hospitali, gari ya polisiย  ikatoka. Mchungaji akaitazama sana gari hiyo pasipo kujuaย  kulikua na mpango ambao Neema alikua amepanga kuufanya.ย  Matilda alikua akihamishwa hapo kituoni muda huo huku ndaniย  ya kituo cha polisi kukiwa na jarada la kuachwa huru kwaย  Matilda, nje kidogo ya kituo Neema aliingia kwenye gari baadaย  ya kuliona gari la Polisi likitoka hapo, akalifuata kwaย  nyuma.ย 

    *********ย 

    “Dada, huyu ni Mama yake James” Ilikua ni sauti ya Jack, Mamaย  Naomi alimuona Mama James kwa mara ya kwanza, akamsalimia kwaย  heshima sanaย 

    “Mama huyu ni kama ndugu kwa Matilda ndiye anayeshinda hapaย  Hospitali kuangalia hali ya Mjukuu wako” Alisema Jack, Mamaย  James hakutaka kuyaamini maneno ya Jack hadi paleย  atakapomwona Patra, wakapewa ruhusa na Daktari kishaย  wakaingia ndani ya wodi, Mama James akamwona Patra kwa maraย  ya kwanza, alikua katika Mshangao Mkubwa sana, sura ya Patraย  ilikua imefanana sana na sura ya James, Chozi la Mama Jamesย  likaanza kutiririka kila alivyozidi kumwangalia Patra, siyoย  tu kwasababu ni Mjukuu wake bali kilichomliza ni jinsiย  ambavyo Patra alikua juu ya kitanda akipigania uhai wake,ย  Mashine pekee ndizo zilizokua zikimpa uhai Mtoto huyoย 

    “Kwanini hukuniambia James?” aliuliza Mama yake James akiwaย  ameshikilia kitanda kwa uchungu mkubwa sana, Jack akasogea naย  kumshika Mkono Mama James akimtaka atulize hasira zakeย 

    “Mama hiyo ndiyo hali halisi, jinsi unavyoumia wewe ndivyoย  ambavyo Mama wa Mtoto huyu anaumia akiwa kituo cha polisi”ย  Alisema Jack huku Mama Naomi akiwa ametulia kimya

    “Jack, miaka yangu 65 katika huu uso wa Dunia, sikuwahiย  kuumia kama ambavyo leo naumia, hili ni Pigo Takatifu kwangu,ย  najiuliza kwanini James hakutaka kusema juu ya ujauzito hadiย  Mtoto anazaliwa, Sina Mtoto mwingine zaidi ya James, pengineย  sina Mjukuu zaidi ya huyu aliyelala hapa, lazima nipiganieย  uhai wake” Alisema Mama yake James.ย 

    “Lakini Mama pamoja na yote, sitaki James agundue kua Mimiย  ndiye niliyekupa hizi taarifa”ย 

    “Hilo usijali Jack, kikubwa ni huyu Mtoto awe salama,ย  atahamishwa hapa na kutibiwa kwa siri, kwakua James alimkataaย  huyu Mimi nitalifanya hili kwa siri sana, pia nipo tayariย  kuandaa wakili kwa ajili ya huyo Msichana aliye polisi,ย  nitalimaliza hili bila kuharibu upande wowote ule” Akasemaย  Mama yake Jamesย 

    Muda wote huo Mama yake Naomi alikua akilia kwa furaha baadaย  ya mzigo huo kutuliwa, mzigo ulikua mzito upande wao maanaย  ilikua ni ngumu sana kupata pesa za matibabu ya Mtoto.ย 

    Mama James akazungumza na uongozi wa Hospitali kwa ajili yaย  kumhamisha Patra kumpeleka Muhimbili kwa ajili ya Upasuaji,ย  jambo hilo likafanyika haraka sana, Gari maalum ya wagonjwaย  ikaondoka na Patra na Mama Naomi huku Jack na Mama Jamesย ย 

    wakielekea Polisi kwa ajili ya kuzungumza na Matilda, hadiย  kufikia muda huo hakuna aliyajua kua Matilda alikuaย  ameondolewa kituo cha polisi huku mpango huo ukisukwa naย  Neema.ย 

    Safari ya gari ya polisi ilikua ni nje kabisa ya Jiji laย  Dar-es-salaam, palikua na jumba moja lililo kando ya Msitu,ย  Matilda akaingizwa ndani ya jumba hilo lililoonekana kutuliaย  sana, Neema akaingia pia.ย 

    “Kua Makini nimefanya kwa upande wangu, nahitaji hicho kiasiย  kabla ya kupambazuka ili kama kuna kitakachotokea nisife kamaย  Mzoga” Akasema Polisi ambaye alicheza mchezo huo waย  kumhamisha Matilda na kuaandaa Jarada kua aliachiwa huruย 

    “Ndani ya Masaa 12 kuanzia sasa kiasi kitakua ndani yaย  akaunti yako, ondoa shaka. Ahsante kwa hili, nikwambie tu kuaย  kazi yako imeishia hapa lakini si mwisho wa Mimi na wewe, huuย  ni mwanzo mzuri” Alisema Neema kisha akatoa bahasha ambayoย  ilikua imetuna akampatia Polisi huyo, Polisi akachunguliaย  akaona alichokiona ambacho kilimfanya atabasamu, kishaย  akaondoka hapo mara moja.

    Matilda hakujua amepelekwa wapi, Nani aliye nyuma ya mchezoย  huo, mara akasikia mlango ukifunguliwa katika chumba ambachoย  alikuwepo, akamwona Neema akiingia, aliongozana na Wanaumeย  wawili ambao walijazia vizuri, Matilda hakusema chochoteย  baada ya kumwona Neemaย 

    “Ulihisi natania Matilda, pengine hujui wewe ni kikwazo kiasiย  gani katika mipango yangu, uwepo wako ni tatizo kubwa kwangu”ย  Alisema Neemaย 

    “Mimi sijakuzuia kumzalia James, lakini siwezi kuishiย  mafichoni kisa wewe” Akasema Matilda, akapigwa kofiย 

    “Hivi unajua unazungumza nini wewe Mshenzi? James ana Mtotoย  mmoja tu, huyu aliye tumboni na si vinginevyo, kwanini unakuaย  king’ang’anizi, sasa utakua hapa na Dunia itakutafuta sanaย  Matilda, hakuna atakayekuja kukusaidia hapa, na kamaย  utaendelea kuleta ubishi basi nitamuuwa Binti yako” Alisemaย  Neema, alionesha wazi kua hakua Mtu wa masiala kabisaย 

    “Unasemaje….Umuuwe Mtoto wangu? laiti kama kitamkutaย  chochote Patra basi nitakulipiza”ย 

    “Hata haumaanishi, utatokaje hapa hilo ni suala unalopaswaย  kujiuliza kisha ndiyo uwaze utanizuia vipi…” Neema akatoaย  simu yake kisha akamwonesha video ambayo ilivuruga akili yaย  Matilda, video hiyo ilimwonesha Neema akiwa katika wodiย  ambayo Patra alikua amelazwa, ilimdhihirishia wazi Matildaย  kua Neema anaweza akafanya chochote kwa ajili ya kumdhuruย  Patra.ย 

    Tayari Mama James na Jack walikua wamefika kituoni, wakatoaย  maelezo kua wanahitaji kumwona Matilda, wakaambiwa kuaย  Matilda alikua ameachiwa huru muda mchache uliopita,ย  iliwashangaza sana sababu kama angelikua ameachiwa huru basiย  wangemwonaย 

    “Afande Mimi nimekaa hapo nje kwa takribani masaa matano,ย  kama angekua ameachiwa basi ningemwona lakini sikumwona hebuย  angalia vizuri” Akadakia Mchungaji Georgeย 

    “Jarada lake hili hapa, sisi tunafanya kazi kwa maandishi,ย  tayari ameachiwa huru. Hatukuona sababu ya kumshikilia kwaniย  Mlalamikaji alikuja na kusema kua haitaji kuendelea na kesi”ย  Alisema tena yule polisiย 

    “Polisi Mimi ni Mama wa mlalamikaji, nimekuja kwa ajili yaย  kumwona huyo Binti tafadhali” Alisema Mama James

    “Jamani nimeshawaambia kua Msichana ameachiwa, jukumu laย  kujua yupo wapi ni la kwenu sababu kwetu ameshatoka”ย  Akasistiza polisi huku akionekana haitaji kuendelea kubishanaย  naoย 

    Taratibu watatu wakashusha ngazi hadi chini, Jack akapigaย  simu Hospitali ambako walikua wameenda kwa ajili ya Matibabu,ย  wakapata taarifa kua Matilda hakwenda huko. Taharuki ikawaย  kubwa, hakuna aliyejua mahali ambapo Matilda alikua ameendaย 

    “Sasa atakua ameenda wapi au ameelekea kule Hospitali ambakoย  Mtoto amehamishwa?” akauliza Jack, akili zao zikawaza kwaย  pamoja kua huwenda Matilda akawa ameenda huko, mara moja Mamaย  James na Jack wakaelekea Magomeni ilipo Hospitali ya JM.ย 

    Wakati wao wanatoka kituo cha polisi, gari nyingine nyeusi yaย  kifahari ikaingia hapo, akashuka James, yaani kama angewahiย  kidogo tu angekutana na Mama yake na Mfanyakazi wake hapoย  Kituoni, James alihitaji kuzungumza na Matilda, hakujua kuaย  Matilda alikua ameondolewa hapo na Neema, akaingia naย  kujitambulisha, akapewa maelezo yale yale ambayo Akina Jackย  walipewa, haraka akatoka hapo akajaribu kuipiga simu ya Matilda lakini haikuita, akampigiaย  simu Neemaย 

    “Neema Nahitaji kuongea nawe sasa hivi, nieleze mahali ulipo”ย  Akasema James, akaelezwa mahali ambapo Neema alikuwepo,ย  akawasha gari kuelekea huko.ย 

    Ilikua ni nje kabisa ya Mji, kitu ambacho kilianza kumpaย  Mashaka James, akasogea hadi kwenye jengo ambalo Neemaย  alikuwa amemuelekeza James aende, Palikua ni msituni. Jengoย  hilo lilikua katika eneo la peke yake kabisa, Jamesย  aliposhuka macho yake yakawa kwenye jengo hilo lililo kimyaย  sana, James akasogea kama alivyoelekezwa na Neemaย 

    Alipoingia alisikia sauti ya Matilda ikiita, akashtuka sanaย  akaenda hadi kwenye hicho chumba akamkuta Matilda akiwaย  amefungwa kambaย 

    “Matilda?” akaita James kisha akamkimbilia Matilda alipokuaย  amekaa, Chozi lilikua likimbubujika Matilda, James akamwambiaย  Matildaย 

    “Nataka nikutoe hapa sawa?” Akawa anafungua kamba lakiniย  akasikia Watu wakija kwenye chumba hicho, James akashtuka,ย  alipogeuka akamwona Neema, Masudi na wanaume wengine wawiliย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya SITA Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    11 Comments

    1. Jack bujo on September 17, 2024 3:57 pm

      Leo wa kwanza Mimi jamani but story is very very ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    2. Moderich on September 17, 2024 4:29 pm

      Mambo ni motooo

      Reply
    3. Asilina chibwana on September 17, 2024 4:32 pm

      Jins nlivyonashauku natamn miendelez Sasa hv

      Reply
      • Pretty on September 17, 2024 5:20 pm

        Wow nautamani uo mwisho wa neema๐Ÿ”ฅ

        Reply
    4. GIDMAS on September 17, 2024 4:49 pm

      Inavitia kuendelea kusoma hadi rahaaa,tuone ni kitakiri kwa jemsi na maltida wake

      Reply
    5. Pauline on September 17, 2024 5:21 pm

      Daaaah jmn huyu Neema ana roho mbaya kiasi hiki ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

      Reply
    6. G shirima on September 17, 2024 5:41 pm

      Yaani hi dunia jamaa anapigania mimba ambayo syo yake ..wanaume tuna tabu sana..

      Reply
    7. Hamis on September 17, 2024 6:35 pm

      Adimini una baya ukifa uhozi ukiozo unuki twend Kaz sanaoma simulizi kama naangalia TV yan yan dah

      Reply
    8. Enock, Nm on September 17, 2024 9:23 pm

      Namuona James akitapeliwa, Neema kuishia pabaya

      Reply
    9. ๐Ÿ“Ÿ + 1.893194 BTC.GET - https://graph.org/Ticket--58146-05-02?hs=69a8d05cce13b86b16fe714c08d5d602& ๐Ÿ“Ÿ on May 4, 2025 8:49 am

      r97ubn

      Reply
    10. ๐Ÿ“• + 1.276412 BTC.NEXT - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=69a8d05cce13b86b16fe714c08d5d602& ๐Ÿ“• on June 29, 2025 11:56 pm

      9xirvd

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.