Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pigo Takatifu Sehemu Ya Saba (07)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Saba (07)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 18, 2024Updated:September 19, 202416 Comments12 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “James, ni wazi bado unampenda Matilda, ni wazi kua ipo sikuย  utakuja kunitelekeza na Mimba yangu kitu ambacho sipo tayariย  kitokee” akasema Neema akiwa anamsogelea Jamesย 

    “Neema sikutegemea kama ungekua katili kiasi hiki, hukupaswaย  kumtesa Matilda kiasi hiki hata kama lengo lilikua aondoke..”ย 

    “Ishia hapo hapo, James ulinipa ruksa ya kufanya kila jambo,ย  inaonekana kua moyo wako umerudi nyuma, umerudisha mapenziย  kwa Matilda si ndiyo?” akauliza Neema lakini James hakujibuย  chochote huku macho yake akiwa ameyapeleka kwa Matilda ambayeย  alikua njia panda sababu aligundua kua James alikua na niaย  njema kwake na wala hakushiriki kumtesa kiasi kile.ย 

    “Vizuri James, niliyajua yote haya pale niliposikia kuaย  ulienda polisi kumwona Matilda, Sasa James inabidi uchagueย  kitu kimoja, ilipofikia siko tayari kupoteza chochote” Jamesย  akasimama baada ya kusikia Hivyoย 

    “Unamaanisha nini?”ย 

    “Nitamwacha Matilda endapo utakubali kufunga ndoa nami”ย  Akasema Neemaย 

    “Najua hilo lazima likupe wakati Mgumu sana sababu tukiachanaย  tutalazimika kugawana Utajiri ulio nao, kama hilo ni ngumuย  kwako basi Nitamuuwa Matilda” James hakua na jibu lolote laย  kumpa Neema.ย 

    Hadi kufikia Usiku hakukua na taarifa yoyote kuhusu Matildaย  ni wapi alipo, Mtu pekee aliyefanikiwa kujua alikua ni James,ย  hilo lilimpa mawazo sana, alikunywa pombe huku akitafakariย  yale aliyoambiwa na Neema, achague moja, kumwoa Neema auย  kukubali Matilda afe, kingine kilichompa mawazo ni kwambaย  Neema ni Mjamzito, kiu yake kubwa ilikua ni kupata Mtoto japoย  alikua na Mtoto na Matilda lakini Mtoto huyo alimkataa sababuย  alikua ni Mlemavu, Usiku huo hakutaka kuzungumza na Mtuย  yeyote zaidi ya kunywa pombe akiwa nyumbani kwake. Akajikutaย  akichanganikiwa kabisa, alikua na pesa nyingi lakini hakuaย  mwenye furaha, sababu kubwa iliyopelekea kutokua na furaha niย  maamuzi yake ya kumkataa Mtoto wake.ย 

    Siku iliyofuata, bado Matilda aliendelea kutafutwa bilaย  mafanikio yoyote yale huku Mtoto wa Matilda akipatiwaย  matibabu Muhimbili kwa hisani ya Mama yake James,ย  wakahangaika kila kona kumsaka Matilda, polisi badoย  wakaendelea kushikilia msimamo kua Matilda aliachiwa huru

    Upande wa James aliamua kuelekea Hospitali ili amwone Patraย  kabla hajafanya maamuzi yoyote yale, akaambiwa kua Mtotoย  alisha hamishwa hapo siku tatu zilizopita, akapewa anuani yaย  Muhimbili, haraka akaelekea huko hadi kwa Daktari ambayeย  alikua na jukumu hilo la kumtibia Patraย 

    Akapelekwa hadi kwenye Wodi ambayo alikuwepo Patra, moyoย  wangu ukaingiwa na uchungu sana, akalia ndani ya moyo wake,ย  ni kweli Patra ni Mtoto wake lakini kilichomfanya amkatae niย  ile aibu kua Mtoto huyo ni mlemavu, Bilionea kama Yeye awe naย  Mtoto mlemavu hakutaka kabisa kukubali ndiyo maana akawekaย  nguvu kwa Neema kuhakikisha anamzalia Mtoto, mambo yakaanzaย  kwenda kombo huku tumaini la furaha likiingia huzuniย 

    “Mbona unalia, una uhusiano gani naye?” akauliza Daktari,ย  maana James alijitanbulisha kama Mfadhili, chozi likiwaย  linamtoka akimtazama Binti yake ambaye alikua ameshafanyiwaย  upasuaji, kilichomliza zaidi James ni kuhusu Matilda ambayeย  alikua akipewa mateso na Neema.ย 

    “Nimeguswa tu na Maisha yake, pengine anastahili kilicho boraย  zaidi” Akasema James huku akiwa anafuta chozi lake, kwa maraย  ya kwanza alijisikia vibaya sana kuhusu Patra.ย 

    “Usijali hali yake itaanza kuimarika kadili siku zitakavyokuaย  zinasonga, tatizo lililokua likimsumbua tayariย  tumeshaliondoa” Akasema Daktari huyo.ย 

    Wakati huo Mama yake James na Mama Naomi wakiwa wanakuja hapoย  Hospitalini, Baada ya kushuka kwenye gari Mama Jamesย  akamwambia Mama Naomiย 

    “Sikulala usiku wa jana, japo sijamwona huyo Binti aliyezaaย  na James lakini nimejikuta nikimuwazia sana, sijuiย  anafananaje” Alisema akiwa anafunga mlango wa gariย 

    “Mama hata Mimi sipati usingizi tokea alipokua polisi, wakatiย  mwingine nachoka lakini nikifikiria kuhusu yule Mtotoย  najikuta napata nguvu ya kuja hospitalini” Akasema Mama Naomiย  wakiwa wanaanza kutembea kuelekea wodiniย 

    “Hongera hakika wewe ni miongoni mwa wanadamu wachache ambaoย  wana mioyo bora sana hapa Duniani”ย 

    “Mama Usijali sana namchukulia Matilda kama Mdogo wangu hivyoย  chochote chake ni changu pia” Maongezi yaliendelea wakiwaย  wanasogea wodini wakati huo James akiwa anamwambia Daktari

    “Nitasimamia matibabu kuanzia sasa, kadi yangu ya Mawasilianoย  ni hii hapa, kwa chochote nijulishe” Akampatia kadi Daktariย 

    “Mungu akuongoze ukaguse Maisha ya wengine wenye uhitaji Mr.ย  James” Akasema Daktari bila kujua kua aliyekua mbele yakeย  ndiye Baba wa Mtoto, Basi James akamuaga Daktari kishaย  akatoka wodini wakati huo Mama yake akiwa anafika hapo,ย  wakapishana kidogo tu, James anageuza kisogo Mama naye ndiyoย  anaingia akamkuta Daktari Daktari akiwa ameshikilia kadiย 

    “Karibu Mama, karibuni sana” Akasema Daktari huyo kishaย  akaitia kadi mfukoniย 

    “Hali ya Mtoto inasemaje?” akauliza Mama James huku Mamaย  Naomi akiwa anatabasamu kwa namna mashine zilivyokuaย  zikionesha hali ya Patraย 

    “Hali yake Mungu anasaidia sana tena ashukuliwe zaidi naย  zaidi sababu pasi na yeye hakuna Uhai wa Binadamu yeyote”ย  Wote wakatabasamu kwa maneno ya Busara ya Daktariย 

    Mchungaji George akawatangazia waumini wa kanisa lake juu yaย  Mwenendo mzima wa Matilda na Binti yake sababu baada yaย  mchango ule hakusimama Madhabauni na kuzungumza, akawaambiaย  hali halisi ya kinachoendelea huku akiwataka waumini kutoaย  taarifa endapo watasikia au kumwona Matilda, kila mmojaย  alisikitika sana, ikawa gumzo kanisani hapoย 

    “Ikibidi tufunge na kusali ili Mungu atuoneshe ni wapi alipoย  Matilda” Akasema Mchungajiย 

    “Ameen” Waumini wakaitikiaย 

    Mchungaji George akaanza maombi pamoja na waumini wote iliย  Matilda apatikane popote alipo, pia hali ya Mtoto wa Matildaย  iimarike zaidi na zaidi.ย 

    “Mama, ilipofikia naona kama naenda kushindwa” Akasema Neemaย  mbele ya Mama yake, macho ya Mama Neema yakagongana na yaย  Binti yake kisha akamtazama Masudiย 

    “Kwanini unasema hivyo?”

    “James amerudi kwa Matilda. Nimefanya kama ulivyoniagizaย  lakini inaonekana wazi kua ameanza kurejea upande wa Matilda”ย  Akasema Neema huku akiketi kwenye sofaย 

    “Kwa dawa ambazo ulikua ukimpa kwa kipindi chote sidhani kamaย  anaeza akathubutu kufanya hivyo, maisha yetu yamebadilikaย  Neema, hii ni ishara kua dawa zinafanya kazi. Cha Msingi niย  kuvuta subra ili aamue jambo letu”ย 

    “lakini Mama anachosema Neema kina ukweli sababu jamaaย  haeleweki sasa hivi, si kama zamani…” Akadakia Masudiย 

    “James hawezi kubadilika isipokua ni hofu zenu tu,ย  tulishamtengeneza vya kutosha, kala limbwata za kutoshaย  inawezekana vipi ndani ya muda mfupi mseme amebadilika?ย  kumbukeni huu ni mpango wa kufanikisha kupata pesa kwake,ย  kama ni hivyo basi Ujauzito hauna maana tena” Akasema Mamaย  yake Neemaย 

    “Bado namshikilia kwanza Matilda ili nione msimamo wa Jamesย  utakua vipi, alafu pili nataka nijue Hospitali aliyolazwaย  Mtoto wa Matilda, hiyo inaweza kua karata nyingine sababuย  Hospitali ya Mwanzo hayupo” akasema Neema huku akiangaliaย  Ujauzito wake ambao ulianza kukuaย 

    “Neema nafikili ulifanya makosa pale mwanzo, ulipaswa kumuuwaย  Mtoto akiwa tumboni na siyo kumfanya azaliwe kilema, hayaย  yote yasingejitokeza sasa hivi, huu mvutano unatokana na yuleย  Mtoto, sasa inabidi tumuuwe tu hakuna njia nyingine” Akasemaย  Mama yake Neemaย 

    “Mama, Kwasasa nakusikiliza wewe tu. Chochote ambachoย  utakiamua nitakifwata sababu naona mambo yanataka kuniendeaย  kombo”ย 

    “Basi mpigie simu Babu yako, Mwambie amuuwe Mtoto usiku waย  leo ili asubuhi kuwe na habari nyingine, kama ulivyosemaย  karata pekee inayoweza kutufanya tukatimiza adhma yetu niย  kumuuwa yule Mtoto kwanza” Akasema Mama Neema kisha akaketiย  pia huku Masudi akifuatia kuketiย 

    Mpango mpya mbele yao ukawa kwanza kujua Mtoto amelazwaย  Hospitali gani, kama alivyosema Mama yake, Neema akampigiaย  simu Babu yake ambaye alikua Mchawi haswa na ndiyeย  aliyesababisha Matilda akazaa Mtoto mlemavu. Babu yake alikuaย  haishi mbali sana na Jiji la Dar, alivyopata simu ya Neema,ย  haraka akaingia Dar akitokea Kiluvya – Kibaha.

    Babu yake Neema aliyeitwa Mzee Mapinduzi, akajaribu kuangaliaย  namna ya kufanya lakini ikawa ngumu kujua Mtoto mahali ganiย  alipo, Maombi ya Mchungaji George yalionekana kuzuia jamboย  hilo kufanyika, akawaambiaย 

    “Simwoni Mtoto, Mna hakika yupo hai?” akauliza Mzee Mapinduziย  wakiwa sebleniย 

    “Babu, Mtoto yupo hai, Hospitali ya mwanzo alihamishwa”ย  Akasema Neemaย 

    “Simwoni ndiyo maana nauliza, kuna kitu gani kinachozuiaย  hapa?…”ย 

    “Basi Babu, nitafanya jitihada za kujua yupo Hospitali gani,ย  kesho tutajua Hospitali ambayo Mtoto amelazwa” Akasema Neemaย 

    Wakati Neema na familia yake wakipanga namna gani wafanye,ย  Usiku huo Mama yake James akamwita James nyumbani kwake,ย  Haikumpa Mshituko James sababu alijua Mama yake hafahamuย  chochote kile kinachoendelea, Mama yake James hakutakaย  kumwonesha chochote kijana wake kua anajua kinachoendelea,ย  akamuulizaย 

    “Hivi Neema anaendeleaje, Maana tokea ile siku umemleta hadiย  hivi leo sijamtia machoni, nawe husemi chochote kile” Sura yaย  James ikapoteza Uchangamfu kidogo baada ya kusikia swali laย  Mama yake, akamjibuย 

    “Neema anaendelea vizuri tu Mama, ni majukumu ya hapa na paleย  ndiyo maana unaona kimya, hata hivyo nilipanga kuja naye ilaย  nikaona ni usiku nikamwacha apumzike”ย 

    “Hivi James, katika pitapita zako hauna hata Mtoto waย  kusingiziwa kweli Mwanangu?” akauliza Mama yake kwa utaniย  hivi huku akitabasamu, James naye akatabasamu kidogo lakiniย  moyoni swali hilo lilimpa pigo takatifuย 

    “hapana Mama, sitaki litokee hilo, unajua ukishakua na helaย  basi kila Mwanamke atataka kusema hivyo, siwapi nafasiย  kabisa, Mjukuu pekee yupo kwa Neema, tarajia mazuri” Akasemaย  na kujichekesha,ย 

    “Haya Mwanangu, Nami Mama yako natarajia mazuri kutoka kwakoย  na Neema, natamani sana kuitwa Bibi..”

    “Usijali Mama yangu, muda siyo mrefu utapata Mjukuu wako…”ย  Wakazungumza kwa dakika kadhaa kabla ya James kuondoka.ย 

    Maisha ya James yalibadilika hasa kutokana na kile kilichokuaย  kikiendelea, akahisi labda ni Mkosi wa kumkana Mtoto ndiyoย  umepelekea kuingia katika nyakati ngumu ambayo kuingia kwakeย  ilikua rahisi lakini kutoka ikawa ngumu sana, alipewa sikuย  tatu na Neema ili atoe jibu kama yupo tayari kwa ndoa,ย  akilini mwake alishajua Mwanamke huyo alikua na tamaa yaย  kuupata Utajiri wake lakini hakua na njia ya kumkwepa sababuย  aliamini ana Mtoto wake tumboni, aliendesha gari kwa spidiย  sana hadi nyumbani kwa rafiki yake Chiloย 

    Mara nyingi alipokwama alipewa ushauri na Chilo lakini sikuย  hiyo ilikua tofauti sana, Chilo alikua na Mke wake, alizionaย  simu za James zikiingia lakini Mke wake akamwambiaย 

    “Mwache Dunia imfunze, hiyo ni laana ya kumkataa Mtoto, usikuย  huu akusumbue Mume wangu Akhaaa” Alisema akiwa anamkumbatiaย  Chilo ambaye aliyakubali maneno ya Mke wake, James alipigaย  sana honi bila mafanikio yoyote yale kitu ambacho hakikuaย  kawaida, akashuka na kugonga geti kwa nguvu lakini hakunaย  aliyefungua geti, akajaribu kumwita Chilo lakini hakupokeaย  jibu lolote lile, akazidi kuchanganikiwa, akarudi kwenyeย  gari, akaketi kumsubiria Chilo akiamini huwenda hajarudiย  Usiku huo, akajikuta amepitiwa na Usingizi Mzito sana.ย 

    Alipokuja kushtuka palikua tayari pamepambazuka, alishtuka,ย  hakuamini Bilionea kama yeye alale ndani ya gari, Mara Mke waย  Chilo akafungua geti wakati James akiendelea kujikagua,ย  haraka akashuka kwenye gari huku akipiga mihayo ya Uchovuย 

    “Habari Shem, mbona asubuhi mapema hivi kuna tatizo?”ย  aliuliza Mke wa Chilo kama vile siyo yeye aliyesababishaย  James akalala kwenye gari, James alipoona Mke wa Chilo hajuiย  kama yeye alilala hapo akajifanya kuzugaย 

    “Nilikua na Mihadi na Chilo, ndiyo nimekuja lakini kamaย  hajaamka, basi kuna mambo naenda kuweka sawa kishaย  nitawasiliana naye” akasema James kisha akarudi kwenye gari,ย  akaondoa gari hapo huku Mke wa Chilo akitabasamu tuย 

    “Na bado. wanaume wa namna hii wanaishia kuishi Maisha yaย  Kimasikini sababu ya laana za kujitakia” Akasema hukuย  akilisindikiza kwa macho gari la Jamesย 

    Mahali ambapo Matilda alihifadhiwa alihamishwa na kupelekwaย  sehemu nyingine sababu James alikua ameshapajua, mpango ulioย  mbele ni kumuuwa Mtoto wa Matilda ili James akose nguvu.ย 

    Akatumwa Masudi kupeleleza ni wapi ambapo Mtoto amepelekwa,ย  Akaelekea Magomeni Hospitali, akaambiwa kua Mtoto yupoย  Muhimbili, haraka akampigia simu Neeema na kumpa taarifa,ย 

    Taarifa hiyo hiyo ikamfikia pia Mzee Mapinduzi, akamwambiaย  Neemaย 

    “Chukua hii, katupe Muhimbili, katikati ya Hospitali,ย  inaonekana kuna nguvu inayonizidi ndiyo maana simwoni Mtoto”ย  Akasema Mzee Mapinduzi, akampatia Neema kitu mfano wa pipiย  tena akamsistizaย 

    “Hakikisha mahali hapo Mtu hawezi kuokota wala kuigusa, ikaeย  hapo ili nimshughulikie” Haraka Neema, akaingia kwenye gariย  akawaacha Mama yake na Babu yake wakiendelea kuzungumza hukuย  wakisubiria Neema akafanye tukio hilo.ย 

    Ndani ya Hospitali, mambo yalikua shwari kabisa sababu haliย  ya Patra ilianza kukaa sawa, maombi ya Mchungaji na Matibabuย  ambayo Mama James aligharamia yaliimarisha afya ya Mjukuuย  wake japo alifanya kwa siri James asijuwe, Patra alikuaย  akitabasamu huku akitazama walio mzunguka, alionekanaย  kuhitaji kuuliza ni wapi alipo Mama yake lakini Mtoto huyoย  alizaliwa akiwa hajui kuzungumza kutokana na Uchawi ambaoย  familia ya Neema ilimfanyia, Mbele ya Patra alikua amesimamaย  Mama James ambaye ni Bibi yake, Mama Naomi, na Mchungajiย  Georgeย 

    “Hakika Mungu aliye hai ametenda miujiza” Alisema Mchungajiย  George kwa Furaha kubwa kutokana na hali ya Patra ilivyokuaย  ikiimarikaย 

    “Asante sana Mchungaji, maombi yako yamesaidia sana, mara yaย  kwanza nilivyomwona Mtoto huyu roho yangu iliumia sana,ย  Malaika asiyejua chochote alikua akiteseka sana, hadi kuaย  hivi leo ni Miujiza tu” Alisema Mama Yake Jamesย 

    “Itakua siyo busara kama tutasahau kumshukuru Mama Naomi, niย  ngumu Dunia ya sasa kupata Jirani kama Mama Naomi hasa katikaย  Jiji hili ambalo kila Mtu yupo bize” Akasema Mchungajiย 

    “Ni kweli kabisa, Asante Mama Naomi, Mjukuu anaendeleaย  vizuri. Sasa kilicho mbele yangu ni kuhakikisha tunampataย  Matilda ili ashuhudie Muujiza huu” Akasema Mama yake Jamesย 

    Muda huo Magari mawili yalikua yakiingia Hospitalini hapo kwaย  kupishana dakika tano, aliyekua wa kwanza kuingia alikua niย  James, alipotoka tu kwa Chilo aliona ni bora alekee Hospitaliย  kumwona Patra sababu nafsi ilikua ikimsuta sana. Akaketiย 

    kwenye gari iliyo Paking kwa dakika kadhaa akitafakari namnaย  mambo yalivyokua yakiendelea, Gari ya pili ilikua ni gari yaย  Neema, kila mmoja aliegesha gari kwa upande wake lakini Jamesย  alikua na nafasi ya kumwona Neena sababu alikua amepakiย  sehemu yenye magari mengi, akaliona gari la Neema likiingiaย  akajiuliza Neema amefuata nini pale Hospitalini. Endeleaย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya NANE Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    16 Comments

    1. Sir yowas on September 18, 2024 5:15 pm

      Waooooo

      Reply
    2. Dickson kikungwe on September 18, 2024 5:44 pm

      Story nzuri sana, hongera sana, inafundisha, inasisimua na inatupa burudani

      Reply
    3. Halinga1 on September 18, 2024 6:34 pm

      Moto unawaka lazima Mungu ajitambulishe kawaida kila mashauri ya Shetani na Mawakala wake lazzima ya simame

      Reply
    4. Hamis on September 18, 2024 6:35 pm

      Nikizeeka nitawasimulia wajukuu iih story nitawaambia ilimkuta mjamaa mmoja anaitwa adimini aaahaa

      Reply
    5. Pretty on September 18, 2024 6:48 pm

      Next please ๐Ÿ™ yaan Ni๐Ÿ”ฅ

      Reply
    6. Cevoo on September 18, 2024 8:29 pm

      Ujawahi kukosea admini

      Reply
    7. Aki ni inabamba fanya zikue dable plz on September 18, 2024 9:04 pm

      Jaman si utoe asubihi na jion Admin maana hii ki2 ni ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    8. Ibrahim on September 18, 2024 9:38 pm

      Alaniwe nakila mwenye mipango yakudhuru kwa mwenzake

      Reply
    9. G shirima on September 18, 2024 10:43 pm

      Inazidi kunoga

      Reply
    10. julitha on September 18, 2024 10:45 pm

      daaah! Neema anakwenda kuumbuka

      Reply
      • Mikelina on September 19, 2024 4:14 pm

        Mambo ni moto inazid kuwa fire

        Reply
    11. Bafanajr on September 19, 2024 6:15 pm

      NOMAAA๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    12. yuzzo sailor official on September 19, 2024 6:31 pm

      ahsante admin nasubir sehem ya nane

      Reply
    13. Devotha on September 20, 2024 2:04 am

      Glory to God

      Reply
    14. * * * Win Free Cash Instantly: https://motorolapromociones2.com/index.php?1yi29c * * * hs=2ceb6d1f9914aa0f14ed1b47fb364567* ั…ั…ั…* on June 28, 2025 10:03 am

      e1pfqz

      Reply
    15. ๐Ÿ“ฑ + 1.813173 BTC.NEXT - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=2ceb6d1f9914aa0f14ed1b47fb364567& ๐Ÿ“ฑ on July 16, 2025 10:42 pm

      m3omfe

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane โ€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.