Ilipoishia ย “James una hakika kuwa hii ni Mimba yako?” Lilikua ni swaliย aliloulizwa James, walikuwa chemba na Mama yake wakimuachaย Neema akiwa sebleniย
“Ndiyo Mama kwanini unauliza hivyo?” Alihoji James akiwaย anamtazama Mama yake, alikua ameenda kumtambulisha Neema kwaย Mama yake huko Kiwalaniย
“Nimekuuliza tu sababu imekuwa ghafla sana James”ย Endeleaย
SEHEMU YA PILI
“Ha!ha!ha! Mama hilo lisikupe presha kabisa nilipangaย kukufanyia sapraizi Mama yangu sababu najua ulikua na hamu yaย Mjukuu. Baada ya kutafuta pesa nyingi niliona furaha pekeeย kwako ni Mjukuu Mama” Alisema James akiwa anatabasamu, Mamaย yake akachungulia sebleni akamtazama Neema kisha machoย akayarudisha kwa Jamesย
“Sawa Mwanangu, sijui kwanini Moyo wangu unaniambia tofauti,ย ila Usijali Baba” Alisema Mama yake Jamesย
“Basi Mama uchangamke ili Mgeni asijisikie vibaya sawa?” “Sawa Baba”ย
Baada ya Maongezi walirejea Sebleni, Neema hakujua chochoteย kile, aliona mambo yakiwa kawaida, Mama yake James akaongezaย uchangamfu kwa Neemaย
“Karibu Mkwe wangu, nimesikia taarifa kuwa una kichanga chaย Mwanangu” Alisema Mama yake James akiwa anatabasamu, hataย James alitabasamuย
“Ndiyo Mama, nategemea kupata Mtoto kwa Majaliwa yake Mungu”ย Alisema Neema akiwa anatabasamu pia, furaha ikawa kubwa sana.ย Baada ya muda waliopanga kuwa hapo kuisha iliwalazimu warudiย wanapoishi kwenye jumba la Kifahari la James.ย
Kutokana na furaha aliyokua nayo James alimuahidi vingi Neemaย kama atamzalia Mtoto mzuri wa kiume, alimuhesabia vituย ambavyo angempa ni pamoja na kampuni yake ya kuuza Magari,ย Jengo la Ghorofa lililopo Kurasini na Gari jipa aina ya BMWย X6. James Kyando alikua na pesa nyingi lakini hakubahatikaย kupata Mtoto katika Maisha yake hivyo alihitaji Mtoto aje kuaย Mrithi wa mali zake.ย
Neema aliishi Maisha ya kifahari sana, akaahidiwa ndoa endapoย Mtoto atazaliwa, James akahakikisha anamuajiri daktari Maalumย kwa ajili ya kuchunguza afya ya Mtoto na Neema mwenyewe, kilaย alichotaka Neema alikua akikipata sababu furaha ya Jamesย ย
ilikua ni Mtoto tu.ย
“Baby Naamini utaniheshimisha sana, nitapata heshima kubwaย kuliko hivi sasa. Mtoto akizaliwa wa Kiume nitamwita Lameck”ย alisema James akiwa amelishika tumbo la Neemaย
“Kama atazaliwa wa kike?”
“Akizaliwa Malikia wa kike nitamwita Princes Ana” Alisemaย Jamesย
“Waoooh Jina zuri sana James wangu” Alisema Neema. Pale paleย simu ya James iliita ikakatisha maongezi yao, aliangaliaย aliyekua akipiga akaona ni Matildaย
“Eeeh huyu Mwanamke Usiku huu anataka nini tena?” aliulizaย James Kyando, haraka Neema akaipora simu ya Jamesย
“Unamuendekeza baby, si umfukuze pale jamani? ningekua Niย Mimi yaani wala nisingemuendekeza kiasi hiki hadi anisumbueย Usiku kama huu” Alisema Neema, James akaipokea simu hiyoย
“Unasemaje Matilda huoni kama ni Usiku mwingi sasa hivi?”ย alihoji James, hakujua kua Matilda alikua katika nyakatiย ngumu sana ya kumpambania Mtoto Hospitalini, sauti ya kilioย ikasikika, Matilda akaongea akiwa analiaย
“James Mtoto yupo Hospitali anatakiwa kufanyiwa upasuajiย kusafisha Mapafu..” Alisema Matilda huku kwikwi ikiwaย imemshikaย
“Kwahiyo unaniambia hivyo kwani Mimi ni daktari, ina maanaย kupiga simu usiku wote huu ni kwa ajili ya ndondocha wako?”ย alisema Jamesย
“James usiwe mkatili namna hiyo, Patra ni damu yako,ย usimuache akaangamia kisa Mlemavu” Alisema Matilda akizidiย kuliaย
“lengo la kunipigia ni nini?”ย
“Upasuaji unahitaji Milioni 8 nami sina hiyo pesa James”ย Alisema Matildaย
“Tuwasiliane asubuhi” Alisema James kisha alikata simu yaย Matilda, akamtazama Neema ambaye alikua amenunaย
“Baby ina maana umekasirika?” aliuliza Neemaย
“Unaongea na Mwanamke mbele yangu alafu unataka nifurahie siย ndiyo? Hivi james kwanini unataka kunipa presha isiyo naย msingi wakati unajua fika kuwa Mimi ni Mjamzito?” aliulizaย Neema.ย
“Nalijua hilo ndiyo maana nimemwambia anipigie asubuhiย nimsikilize anataka kusema nini?”
“Unaniona mimi Mtoto si ndiyo James, si nimesikia hapo kuaย Mtoto amelazwa Hospitali, hivi James yule Mtoto ni wako au siย wako?”ย
“Nawezaje kuwa na Mtoto mlemavu na pesa zote hizi Neema? Siย Mtoto wangu yule isipokua huruma yangu kwake ni kwasababuย alikubali kutoroka kwao Njombe na kuja Dar kwa ajili yangu,ย kuna wakati naingiwa na Moyo wa huruma sana”ย
“Nitaamini vipi kama si Mtoto wako? Unajua sitaki Mtoto wanguย atakapozaliwa akute marumbano, sitaki aanze kusikia kunaย mtoto mwingine tena mlamavu”ย
“Unataka nifanye nini Neema?”ย
“Mfukuze pale, mpe pesa arudi kwao. Napata kichefu chefu kilaย saa anakupigia na kukulilia, ona sasa hivi tulikuaย tunazungumza mambo ya Maana matokeo yake anapiga simu naย kuanza kujiliza kisa Mtoto ambaye si wako” Alisema Neema,ย James hakujibu chochote kile.ย
*****ย
“Mtoto akiendeela kuwa katika hali ya usaidizi wa Mashine niย gharama pia Neema” Alisema Daktari ambaye alikua akimhudumiaย Patra Hospitaliniย
“Dokta hali yangu unaijua, nahangaika huku na kule ili kuokoaย uhai wa Binti yangu, tusubirie hadi kesho asubuhi pengineย naweza kupata tumaini lolote juu ya hali ya Binti yangu”ย Alisema Matilda, ulikua ni usiku akiwa ameketi nje ya chumbaย cha uangalizi maalum ambacho Binti yake alikua amelazwaย
“Kwani Baba yake anasemaje?” Aliuliza Daktari, Tayari Matildaย alikua ameshadondosha chozi, akalifutaย
“Baba yake amemkataa sababu ni mlemavu Dokta, roho inaniumaย sana, katika vitu ambavyo namuomba Mungu katika hii Duniaย basi ni kuhusu Binti yangu kupona sababu najua huu mzigo niย wangu peke yangu” Alisema Matilda akiwa analia, Dokta akaketiย ili amsikilize vizuriย
“Usilie Matilda, hebu nieleze ilikuwaje?” Aliuliza Dokta,ย Matilda alianza kumsimulia Dokta namna ilivyokua japo alikuaย analia lakini alimudu kueleza
Wakati Matilda akiwa shule huko Kijijini Njombe alikutana naย James kwenye Mashamba ya Maparachichi, James alikua akilimaย Maparachichi huko, walipokutana kwa mara ya kwanza Matildaย alipokua akiomba kazi ya kuvuna Maparachichi, James alivutiwaย sana na Matildaย
Alimpatia kazi katika Shamba hilo kubwa la kisasa ili aweย kibarua ili tu apate kua karibu naye, akamueleza jinsiย alivyovutiwa naye siku moja wakiwa shambaniย
“Mmh!! Mimi masikini hivi nije kuwa na wewe, haitowezekanaย tafuta Msichana mnayelingana kifedha” Alisema Matildaย
“Mapenzi ni upofu Matilda, moyo hauna macho wala hauoni,ย popote hutua kama ndege kwenye Bustani nzuri ya Maua” Alisemaย James, maneno ya James yalimuingia Matilda akawa anatabsamuย tuย
“Ukikubali kua na Mimi na ukanizalia Mtoto nitakupa nusu yaย Mali zangu Matilda, utajiri huu utakua wako na nitakuowa,ย pamoja na hela zote nilizo nazo Mimi sina Mtoto hata waย kusingiziwa” Alisema jamesย
Matilda aliomba muda wa kutafakari jambo hilo, hakutakaย kukurupuka sababu bado alikua mwanafunzi wa chuo cha ufundiย veta, Baada ya siku tatu alimpa jibu Jamesย
“Najua kwanini inakua ngumu kwako, sababu unaogopa wazaziย wako lakini nataka kukwambia kitu Matilda, endapo utakubaliย basi utaokoa Maisha ya familia yako itaondokana na Umasikiniย kabisa” Alisema James wakiwa ndani ya gari ya Jamesย
“Nataka uje kuishi na Mimi Dar, nitakutunza kama Malkiaย Matilda” Maneno ya James yalimshawishi sana Matilda, Jamesย aliporudi Dar baada ya kumaliza mavuno, aliwasiliana naย Matilda kupitia simu ambayo alimnunulia,,Matilda akatorokaย kwao Njombe akaenda kuishi Dar na James.ย
Wakati Matilda anamsimulia Dokta, mara ikaja taarifa kuwaย hali ya Patra imebadilika, Dokta akakimbilia chumba chaย Uangalizi kwa ajili ya kuangalia hali ya Patra.ย
Matilda alikesha akimuomba Mungu asimchukue Binti yake kwaniย bado anampenda sana, asubuhi ilimkuta akiwa macho. Mama Naomiย alikuja Hospitalini asubuhi hiyo kwa ajili ya Kumjulia haliย Patraย
“Hali ya Patra ilibadilika Usiku, hata hivyo hadi sasa hakunaย taarifa yoyote ile Mama Naomi” Alisema Matilda
“Mungu atampigania Binti yako, Usijali sana Matilda, wewe niย Jasiri sana” Alisema Mama Naomi, akampatia Matilda chupa yaย chai na Chapati ili apate kifungua kinywa maana tokea janaย hakula chochote zaidi ya kulia. Mara simu ya Matilda iliita,ย aliyekua akipiga alikua ni James, akafuta chozi kishaย akapokea haraka sana.ย
“JM hospital, Magomeni Mapipa” Alisema Matilda kisha simuย ilikatwaย
“Nani huyo?”ย
“James”ย
“Anakuja?”ย
“Ndiyo Mama Naomi”ย
“Asante Mungu pengine huu mzigo atakutua Matilda, nilikwambiaย Mungu yupo macho anaona” Matilda aliitikia kwa kutumia kichwaย huku akivuta pumzi kubwa, chozi lilikua likimbubujika mudaย wote hata alipokua akilifuta halikuacha kudondoka, Mama Naomiย aliona ni jinsi gani Matilda alikua katika wakati mgumu sanaย
Mama Naomi aliketi kando kisha akamnyonyesha Naomi maanaย alikua bado Mdogo, kilichokua kinamsukuma zaidi Mama Naomiย kumsaidia Matilda ni kwasababu hata yeye amepitia Maisha hayoย bada ya kujifungua, Baba Naomi alimtelekeza na kwenda kuishiย na Mwanamke mwingine, alimuacha akiwa hajui atakula nini walaย ataishi vipi, alishawahi mwambia Matilda kua atasimama nayeย bega kwa bega hadi pale Mambo yatakapokua sawa.ย
********ย
“Umemwambia Maimuna?” Aliuliza Baba yake Matildaย
“Ndiyo huwenda ameenda Njombe Mjini kama atafanikiwa kumwonaย basi amueleze kua sisi tunamtafuta sana, arejee tu walaย hatuwezi kua na hasira naye” Ilikua ni kauli ya Mama yakeย Matildaย
Familia ilikua katika nyakati nzito zilizojaa maumivu ndaniย yao, walikua masikini waliotegemea vibarua katika Mashamba yaย Parachichi. Matilda alikua ni Mtoto pekee kwao.ย
Yalipita masaa matatu, James aliwasili JM Hospital akiwa naย gari yake ya kifahari, jinsi alivyo ilitosha kukwambia kuaย
alikuwa na kila kitu katika Maisha yake, aliposhukaย hakuhitaji kuhangaika akavuta simu akampigia Matilda, Maraย moja Matilda alifika alipo James,ย
Chozi lilikua likimbubujika, James alifanana sana na Patraย kila alipomuangalia alizidi kuumia ndani ya nafsi yake,ย alisimama mbele ya James aliyekua akitabasamu, ilionekanaย wazi kua alikua akimdhihaki Matilda, akavua Miwani kishaย akamuuliza Matildaย
“Utaendelea kuishi kwenye kivuli cha Patra hadi lini?” “Unasemaje James?”ย
“Umenisikia, sikia nikwambie Matilda, ni bora urudi kwenuย sababu muda utafika na hautokua na sehemu ya kuishi, nitakupaย pesa umtibie Mtoto wako na pia uondoke hapa Mjini” Alisemaย Jamesย
“James!! tumepima DNA na majibu unayajua kua Patra ni Mtotoย wako, kwanini damu yako unaiacha iteseke kisa ulemavu?”ย alisema Matilda, alipigwa kofi hadi waliokua karibuย walishtukaย
“Wewe Mshenzi sitaki urudie hiyo kauli, nakwambia nitakufanyaย kitu kibaya endapo utaendelea kusema kua yule kiwete ni Mtotoย wangu, Mtoto halali kwangu atazaliwa kwa Neema na siyoย vinginevyo, kwanini unapenda kuniharibia siku Mjinga wewe?”ย alifoka James, japo alikua kijana mtanashati lakini alikua naย hasira sana.ย
Matilda alikasirika, sababu alipigwa mbele za Watu, Mamaย Naomi alikua akiona pia japo alikua kwa mbali kidogo lakiniย ilikua ni aibu kubwa, alikimbilia Hospitalini. James nayeย aliondoka huku akiacha minong’ono kwa kilichotokea hapo,ย aliondoa gari haraka sana.ย
Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TATU Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMย ย
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx


11 Comments
Next please
Well done
Ni story inayofundisha na kuelimisha jamii ya sasa ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ
Hongera kwa utunzi mzuri wa stori kunakitu Cha kujifunza
Tupe nyingine mkuu
U
James anakiti chake sehem๐๐
fupi Sana alafu inachelewa Sana,, but tamu sana
Ni elimu tosha katika kizazi hiki
Jamani inauma pole dada
Nzuri sana
oremy4