Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pigo Takatifu Sehemu Ya Pili (02)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Pili (02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 13, 2024Updated:September 18, 202411 Comments9 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Β “James una hakika kuwa hii ni Mimba yako?” Lilikua ni swaliΒ  aliloulizwa James, walikuwa chemba na Mama yake wakimuachaΒ  Neema akiwa sebleniΒ 

    “Ndiyo Mama kwanini unauliza hivyo?” Alihoji James akiwaΒ  anamtazama Mama yake, alikua ameenda kumtambulisha Neema kwaΒ  Mama yake huko KiwalaniΒ 

    “Nimekuuliza tu sababu imekuwa ghafla sana James”Β  EndeleaΒ 

    SEHEMU YA PILI

    “Ha!ha!ha! Mama hilo lisikupe presha kabisa nilipangaΒ  kukufanyia sapraizi Mama yangu sababu najua ulikua na hamu yaΒ  Mjukuu. Baada ya kutafuta pesa nyingi niliona furaha pekeeΒ  kwako ni Mjukuu Mama” Alisema James akiwa anatabasamu, MamaΒ  yake akachungulia sebleni akamtazama Neema kisha machoΒ  akayarudisha kwa JamesΒ 

    “Sawa Mwanangu, sijui kwanini Moyo wangu unaniambia tofauti,Β  ila Usijali Baba” Alisema Mama yake JamesΒ 

    “Basi Mama uchangamke ili Mgeni asijisikie vibaya sawa?” “Sawa Baba”Β 

    Baada ya Maongezi walirejea Sebleni, Neema hakujua chochoteΒ  kile, aliona mambo yakiwa kawaida, Mama yake James akaongezaΒ  uchangamfu kwa NeemaΒ 

    “Karibu Mkwe wangu, nimesikia taarifa kuwa una kichanga chaΒ  Mwanangu” Alisema Mama yake James akiwa anatabasamu, hataΒ  James alitabasamuΒ 

    “Ndiyo Mama, nategemea kupata Mtoto kwa Majaliwa yake Mungu”Β  Alisema Neema akiwa anatabasamu pia, furaha ikawa kubwa sana.Β  Baada ya muda waliopanga kuwa hapo kuisha iliwalazimu warudiΒ  wanapoishi kwenye jumba la Kifahari la James.Β 

    Kutokana na furaha aliyokua nayo James alimuahidi vingi NeemaΒ  kama atamzalia Mtoto mzuri wa kiume, alimuhesabia vituΒ  ambavyo angempa ni pamoja na kampuni yake ya kuuza Magari,Β  Jengo la Ghorofa lililopo Kurasini na Gari jipa aina ya BMWΒ  X6. James Kyando alikua na pesa nyingi lakini hakubahatikaΒ  kupata Mtoto katika Maisha yake hivyo alihitaji Mtoto aje kuaΒ  Mrithi wa mali zake.Β 

    Neema aliishi Maisha ya kifahari sana, akaahidiwa ndoa endapoΒ  Mtoto atazaliwa, James akahakikisha anamuajiri daktari MaalumΒ  kwa ajili ya kuchunguza afya ya Mtoto na Neema mwenyewe, kilaΒ  alichotaka Neema alikua akikipata sababu furaha ya JamesΒ Β 

    ilikua ni Mtoto tu.Β 

    “Baby Naamini utaniheshimisha sana, nitapata heshima kubwaΒ  kuliko hivi sasa. Mtoto akizaliwa wa Kiume nitamwita Lameck”Β  alisema James akiwa amelishika tumbo la NeemaΒ 

    “Kama atazaliwa wa kike?”

    “Akizaliwa Malikia wa kike nitamwita Princes Ana” AlisemaΒ  JamesΒ 

    “Waoooh Jina zuri sana James wangu” Alisema Neema. Pale paleΒ  simu ya James iliita ikakatisha maongezi yao, aliangaliaΒ  aliyekua akipiga akaona ni MatildaΒ 

    “Eeeh huyu Mwanamke Usiku huu anataka nini tena?” aliulizaΒ  James Kyando, haraka Neema akaipora simu ya JamesΒ 

    “Unamuendekeza baby, si umfukuze pale jamani? ningekua NiΒ  Mimi yaani wala nisingemuendekeza kiasi hiki hadi anisumbueΒ  Usiku kama huu” Alisema Neema, James akaipokea simu hiyoΒ 

    “Unasemaje Matilda huoni kama ni Usiku mwingi sasa hivi?”Β  alihoji James, hakujua kua Matilda alikua katika nyakatiΒ  ngumu sana ya kumpambania Mtoto Hospitalini, sauti ya kilioΒ  ikasikika, Matilda akaongea akiwa analiaΒ 

    “James Mtoto yupo Hospitali anatakiwa kufanyiwa upasuajiΒ  kusafisha Mapafu..” Alisema Matilda huku kwikwi ikiwaΒ  imemshikaΒ 

    “Kwahiyo unaniambia hivyo kwani Mimi ni daktari, ina maanaΒ  kupiga simu usiku wote huu ni kwa ajili ya ndondocha wako?”Β  alisema JamesΒ 

    “James usiwe mkatili namna hiyo, Patra ni damu yako,Β  usimuache akaangamia kisa Mlemavu” Alisema Matilda akizidiΒ  kuliaΒ 

    “lengo la kunipigia ni nini?”Β 

    “Upasuaji unahitaji Milioni 8 nami sina hiyo pesa James”Β  Alisema MatildaΒ 

    “Tuwasiliane asubuhi” Alisema James kisha alikata simu yaΒ  Matilda, akamtazama Neema ambaye alikua amenunaΒ 

    “Baby ina maana umekasirika?” aliuliza NeemaΒ 

    “Unaongea na Mwanamke mbele yangu alafu unataka nifurahie siΒ  ndiyo? Hivi james kwanini unataka kunipa presha isiyo naΒ  msingi wakati unajua fika kuwa Mimi ni Mjamzito?” aliulizaΒ  Neema.Β 

    “Nalijua hilo ndiyo maana nimemwambia anipigie asubuhiΒ  nimsikilize anataka kusema nini?”

    “Unaniona mimi Mtoto si ndiyo James, si nimesikia hapo kuaΒ  Mtoto amelazwa Hospitali, hivi James yule Mtoto ni wako au siΒ  wako?”Β 

    “Nawezaje kuwa na Mtoto mlemavu na pesa zote hizi Neema? SiΒ  Mtoto wangu yule isipokua huruma yangu kwake ni kwasababuΒ  alikubali kutoroka kwao Njombe na kuja Dar kwa ajili yangu,Β  kuna wakati naingiwa na Moyo wa huruma sana”Β 

    “Nitaamini vipi kama si Mtoto wako? Unajua sitaki Mtoto wanguΒ  atakapozaliwa akute marumbano, sitaki aanze kusikia kunaΒ  mtoto mwingine tena mlamavu”Β 

    “Unataka nifanye nini Neema?”Β 

    “Mfukuze pale, mpe pesa arudi kwao. Napata kichefu chefu kilaΒ  saa anakupigia na kukulilia, ona sasa hivi tulikuaΒ  tunazungumza mambo ya Maana matokeo yake anapiga simu naΒ  kuanza kujiliza kisa Mtoto ambaye si wako” Alisema Neema,Β  James hakujibu chochote kile.Β 

    *****Β 

    “Mtoto akiendeela kuwa katika hali ya usaidizi wa Mashine niΒ  gharama pia Neema” Alisema Daktari ambaye alikua akimhudumiaΒ  Patra HospitaliniΒ 

    “Dokta hali yangu unaijua, nahangaika huku na kule ili kuokoaΒ  uhai wa Binti yangu, tusubirie hadi kesho asubuhi pengineΒ  naweza kupata tumaini lolote juu ya hali ya Binti yangu”Β  Alisema Matilda, ulikua ni usiku akiwa ameketi nje ya chumbaΒ  cha uangalizi maalum ambacho Binti yake alikua amelazwaΒ 

    “Kwani Baba yake anasemaje?” Aliuliza Daktari, Tayari MatildaΒ  alikua ameshadondosha chozi, akalifutaΒ 

    “Baba yake amemkataa sababu ni mlemavu Dokta, roho inaniumaΒ  sana, katika vitu ambavyo namuomba Mungu katika hii DuniaΒ  basi ni kuhusu Binti yangu kupona sababu najua huu mzigo niΒ  wangu peke yangu” Alisema Matilda akiwa analia, Dokta akaketiΒ  ili amsikilize vizuriΒ 

    “Usilie Matilda, hebu nieleze ilikuwaje?” Aliuliza Dokta,Β  Matilda alianza kumsimulia Dokta namna ilivyokua japo alikuaΒ  analia lakini alimudu kueleza

    Wakati Matilda akiwa shule huko Kijijini Njombe alikutana naΒ  James kwenye Mashamba ya Maparachichi, James alikua akilimaΒ  Maparachichi huko, walipokutana kwa mara ya kwanza MatildaΒ  alipokua akiomba kazi ya kuvuna Maparachichi, James alivutiwaΒ  sana na MatildaΒ 

    Alimpatia kazi katika Shamba hilo kubwa la kisasa ili aweΒ  kibarua ili tu apate kua karibu naye, akamueleza jinsiΒ  alivyovutiwa naye siku moja wakiwa shambaniΒ 

    “Mmh!! Mimi masikini hivi nije kuwa na wewe, haitowezekanaΒ  tafuta Msichana mnayelingana kifedha” Alisema MatildaΒ 

    “Mapenzi ni upofu Matilda, moyo hauna macho wala hauoni,Β  popote hutua kama ndege kwenye Bustani nzuri ya Maua” AlisemaΒ  James, maneno ya James yalimuingia Matilda akawa anatabsamuΒ  tuΒ 

    “Ukikubali kua na Mimi na ukanizalia Mtoto nitakupa nusu yaΒ  Mali zangu Matilda, utajiri huu utakua wako na nitakuowa,Β  pamoja na hela zote nilizo nazo Mimi sina Mtoto hata waΒ  kusingiziwa” Alisema jamesΒ 

    Matilda aliomba muda wa kutafakari jambo hilo, hakutakaΒ  kukurupuka sababu bado alikua mwanafunzi wa chuo cha ufundiΒ  veta, Baada ya siku tatu alimpa jibu JamesΒ 

    “Najua kwanini inakua ngumu kwako, sababu unaogopa wazaziΒ  wako lakini nataka kukwambia kitu Matilda, endapo utakubaliΒ  basi utaokoa Maisha ya familia yako itaondokana na UmasikiniΒ  kabisa” Alisema James wakiwa ndani ya gari ya JamesΒ 

    “Nataka uje kuishi na Mimi Dar, nitakutunza kama MalkiaΒ  Matilda” Maneno ya James yalimshawishi sana Matilda, JamesΒ  aliporudi Dar baada ya kumaliza mavuno, aliwasiliana naΒ  Matilda kupitia simu ambayo alimnunulia,,Matilda akatorokaΒ  kwao Njombe akaenda kuishi Dar na James.Β 

    Wakati Matilda anamsimulia Dokta, mara ikaja taarifa kuwaΒ  hali ya Patra imebadilika, Dokta akakimbilia chumba chaΒ  Uangalizi kwa ajili ya kuangalia hali ya Patra.Β 

    Matilda alikesha akimuomba Mungu asimchukue Binti yake kwaniΒ  bado anampenda sana, asubuhi ilimkuta akiwa macho. Mama NaomiΒ  alikuja Hospitalini asubuhi hiyo kwa ajili ya Kumjulia haliΒ  PatraΒ 

    “Hali ya Patra ilibadilika Usiku, hata hivyo hadi sasa hakunaΒ  taarifa yoyote ile Mama Naomi” Alisema Matilda

    “Mungu atampigania Binti yako, Usijali sana Matilda, wewe niΒ  Jasiri sana” Alisema Mama Naomi, akampatia Matilda chupa yaΒ  chai na Chapati ili apate kifungua kinywa maana tokea janaΒ  hakula chochote zaidi ya kulia. Mara simu ya Matilda iliita,Β  aliyekua akipiga alikua ni James, akafuta chozi kishaΒ  akapokea haraka sana.Β 

    “JM hospital, Magomeni Mapipa” Alisema Matilda kisha simuΒ  ilikatwaΒ 

    “Nani huyo?”Β 

    “James”Β 

    “Anakuja?”Β 

    “Ndiyo Mama Naomi”Β 

    “Asante Mungu pengine huu mzigo atakutua Matilda, nilikwambiaΒ  Mungu yupo macho anaona” Matilda aliitikia kwa kutumia kichwaΒ  huku akivuta pumzi kubwa, chozi lilikua likimbubujika mudaΒ  wote hata alipokua akilifuta halikuacha kudondoka, Mama NaomiΒ  aliona ni jinsi gani Matilda alikua katika wakati mgumu sanaΒ 

    Mama Naomi aliketi kando kisha akamnyonyesha Naomi maanaΒ  alikua bado Mdogo, kilichokua kinamsukuma zaidi Mama NaomiΒ  kumsaidia Matilda ni kwasababu hata yeye amepitia Maisha hayoΒ  bada ya kujifungua, Baba Naomi alimtelekeza na kwenda kuishiΒ  na Mwanamke mwingine, alimuacha akiwa hajui atakula nini walaΒ  ataishi vipi, alishawahi mwambia Matilda kua atasimama nayeΒ  bega kwa bega hadi pale Mambo yatakapokua sawa.Β 

    ********Β 

    “Umemwambia Maimuna?” Aliuliza Baba yake MatildaΒ 

    “Ndiyo huwenda ameenda Njombe Mjini kama atafanikiwa kumwonaΒ  basi amueleze kua sisi tunamtafuta sana, arejee tu walaΒ  hatuwezi kua na hasira naye” Ilikua ni kauli ya Mama yakeΒ  MatildaΒ 

    Familia ilikua katika nyakati nzito zilizojaa maumivu ndaniΒ  yao, walikua masikini waliotegemea vibarua katika Mashamba yaΒ  Parachichi. Matilda alikua ni Mtoto pekee kwao.Β 

    Yalipita masaa matatu, James aliwasili JM Hospital akiwa naΒ  gari yake ya kifahari, jinsi alivyo ilitosha kukwambia kuaΒ 

    alikuwa na kila kitu katika Maisha yake, aliposhukaΒ  hakuhitaji kuhangaika akavuta simu akampigia Matilda, MaraΒ  moja Matilda alifika alipo James,Β 

    Chozi lilikua likimbubujika, James alifanana sana na PatraΒ  kila alipomuangalia alizidi kuumia ndani ya nafsi yake,Β  alisimama mbele ya James aliyekua akitabasamu, ilionekanaΒ  wazi kua alikua akimdhihaki Matilda, akavua Miwani kishaΒ  akamuuliza MatildaΒ 

    “Utaendelea kuishi kwenye kivuli cha Patra hadi lini?” “Unasemaje James?”Β 

    “Umenisikia, sikia nikwambie Matilda, ni bora urudi kwenuΒ  sababu muda utafika na hautokua na sehemu ya kuishi, nitakupaΒ  pesa umtibie Mtoto wako na pia uondoke hapa Mjini” AlisemaΒ  JamesΒ 

    “James!! tumepima DNA na majibu unayajua kua Patra ni MtotoΒ  wako, kwanini damu yako unaiacha iteseke kisa ulemavu?”Β  alisema Matilda, alipigwa kofi hadi waliokua karibuΒ  walishtukaΒ 

    “Wewe Mshenzi sitaki urudie hiyo kauli, nakwambia nitakufanyaΒ  kitu kibaya endapo utaendelea kusema kua yule kiwete ni MtotoΒ  wangu, Mtoto halali kwangu atazaliwa kwa Neema na siyoΒ  vinginevyo, kwanini unapenda kuniharibia siku Mjinga wewe?”Β  alifoka James, japo alikua kijana mtanashati lakini alikua naΒ  hasira sana.Β 

    Matilda alikasirika, sababu alipigwa mbele za Watu, MamaΒ  Naomi alikua akiona pia japo alikua kwa mbali kidogo lakiniΒ  ilikua ni aibu kubwa, alikimbilia Hospitalini. James nayeΒ  aliondoka huku akiacha minong’ono kwa kilichotokea hapo,Β  aliondoa gari haraka sana.Β 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TATU Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    11 Comments

    1. Amayner on September 13, 2024 12:52 pm

      Next please

      Reply
    2. G shirima on September 13, 2024 3:55 pm

      Well done

      Reply
      • Richmao on September 13, 2024 6:27 pm

        Ni story inayofundisha na kuelimisha jamii ya sasa πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

        Reply
        • GIDMAS on September 14, 2024 2:51 pm

          Hongera kwa utunzi mzuri wa stori kunakitu Cha kujifunza

          Reply
    3. Mike on September 13, 2024 5:56 pm

      Tupe nyingine mkuu
      U

      Reply
    4. Director SanJO 🎬 on September 13, 2024 6:05 pm

      James anakiti chake sehemπŸ™„πŸ™„

      Reply
    5. Leokadia Haule on September 13, 2024 9:20 pm

      fupi Sana alafu inachelewa Sana,, but tamu sana

      Reply
    6. Amosi sanga on September 14, 2024 9:01 am

      Ni elimu tosha katika kizazi hiki

      Reply
    7. Siwema malekwa on September 17, 2024 9:17 am

      Jamani inauma pole dada

      Reply
    8. [email protected] on September 18, 2024 3:48 pm

      Nzuri sana

      Reply
    9. πŸ“ Message; SENDING 1.502407 BTC. GET =>> https://yandex.com/poll/7HqNsFACc4dya6qN3zJ4f5?hs=b599ffa8fa41d85d67d3aae4f5317756& πŸ“ on June 3, 2025 11:03 am

      oremy4

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.