Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pigo Takatifu Sehemu Ya Nne (04)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Nne (04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 15, 2024Updated:September 18, 20246 Comments12 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Asante Yesu” Mikono yake ikiwa juu, Mchungaji akaja naย  kumwinuaย 

    “Matilda, kanisa linakuhitaji useme neno” Mchungaji Georgeย  alimsogeza Matilda hadi Madhabauni, akampa kipaza sauti.ย  Aseme nini? ndicho ambacho Matilda alikua akiwaza, umatiย  ulikua mwingi hapo kanisani, macho yote yakawa kwa Matildaย  Msichana wa miaka 28ย 

    Alikua akitetemeka kwa kila alichofikiria kukisema, alikuaย  kama amepigwa shoti vile, alimtazama Mama Naomi ambaye alimpaย  ishara ya kumtia moyo kua aseme chochote hapo kanisani. Endelea

    SEHEMU YA NNE

    “Asanteni kwa wote, asanteni sana. Nilikata tamaa kabisaย  lakini roho mtakatifu ameniinua kupitia nyie” Alisemaย  Matilda, Chozi lilimbubujika kilio kikamzidi maarifa akawekaย  kipaza sauti huku akimpa ishara Mchungaji kua haweziย  kuzungumza kabisa.

    Kanisa kikazizima, hadithi ya Maisha ya Matilda ikawalizaย  wengi, bahati nzuri muda huo wataalam wa kuhesabu pesaย  walikuwa tayari wamemaliza, Mchungaji akawatangazia kuaย  wamepata Milioni tano, Matilda hakuamini masikio yakeย 

    “Sikutegemea kabisa kama kwa taarifa hii iliyo ghaflaย  tungeweza kukusanya kiasi kikubwa namna hii, pesa hii itaendaย  moja kwa moja Hospitali muda huu ili Mtoto aanze matibabu”ย  Alisema Mchungaji, Akawaambia waumini waendelee na ratibaย  zingine, yeye, Mama Naomi na Matilda wakaingia kwenye gari yaย  kanisa, safari ya kuelekea Hospitali ikaanza.ย 

    “Mama Matilda, napata hisia mbaya juu ya Mtoto wetu” Alisemaย  Baba Matilda akiwa ameketi kwenye Mkeka, Mama Matilda alikuaย  akimalizia kuweka kuni jikoni, kauli ya Mume wake ikamfanyaย  aache alichokua anakifanya, akapiga hatua za taratibu hukuย  sura yake ikijawa na Mshangao akamsogelea Mume wake,ย  akajishika kiunoย 

    “Kwanini unasema hivyo Baba Matilda?”ย 

    “Jana usiku nimeota ndoto mbaya sana kuhusu Matilda, sinaย  hakika kama Atakua hai na kama yupo hai basi anaishi kwaย  Mateso ya Golgota” Akasema Baba Matilda huku akikunja vizuriย  goti lake wakati huo Mama Matilda akivuta kigoda na kuketiย  huku macho yake yakiwa bize kwenye sura ya Mume wakeย 

    “Mungu amuepushe Binti yetu na majaribu yoyote yale, hujuiย  jinsi roho yangu inavyouma Baba Matilda” Akasema Mama Matildaย  huku akifuta chozi lakeย 

    “Tokea nikiwa shambani leo sijisikii vizuri kabisa,ย  nimeliweka jambo moyoni kama Mwanaume lakini Mwisho wa sikuย  nimeshindwa nimeona ni bora nilitoe, Huu wasiwasi sijuiย  utaondoka lini”ย 

    “Baba Matilda Mtoto yupo hai, na anatukumbuka sana. Eweย  Yehova tenda kwa ajili ya Binti yetu popote alipo, mpe rohoย  ya kurejea nyumbani ili sisi tuwe na Amani” Akasema Mamaย  Matilda mikono ikiwa juu, Hakika familia hii ilikua yenyeย  misingi thabiti ya dini.ย 

    “Kama siyo huu umasikini basi ningeenda Mjini kumtafutaย  Matilda, hatuna Mtoto mwingine sisi” Jinsi Baba Matildaย  alivyokua akilalamika alizidi kumfanya Mama Matilda adondosheย  chozi lake.ย 

    “Baba Matilda moyo unaniuma sana tena zaidi ya sana, nikiwaย  kama Mama naumia kuliko unavyofikiria” Alisema Mama Matildaย  kisha akaingia ndani akiwa analia, alimuacha Baba Matildaย  akiwa amejishika tama.ย 

    Mchungaji, Matilda na Mama Naomi walikua kwenye kordo laย  Hospitali tayari kuelekea kwa daktari kwa lengo la kukabidhiย  pesa ili upasuaji uanze. Ghafla polisi waliwasimamisha,ย  sintofahamu ikatawalaย 

    “Sisi ni Maafisa wa polisi, Matilda upo chini ya ulinziย  kuanzia sasa..” Alisema askari mmoja, Matilda alishtuka

    “Mimi?”ย 

    “Ndiyo” Akasema polisiย 

    “Afande…huyu Binti amefanya nini?” alihoji Mchungaji Georgeย  kwa Mshangao Mkubwa sana.ย 

    “Utajua ukifika kituoni, ruhusa ya kukamatwa kwake hii hapa”ย  Alioneshaย 

    “Polisi nimefanya nini Mimi jamani, tafadhali msinifanyieย  hivyo. Binti yangu ni mgonjwa sana anahitaji matibabu”ย  Alisema Kwa kilio Matilda lakini tayari pingu zilikuaย  zimeshafungwa kwenye mikono yake, pesa zilikua mkononi mwake,ย  haraka Mchungaji akataka kuzichukua lakini polisi wakazuiaย 

    “Chochote mtakachokifanya hapa kitatumika kama Ushahidiย  Mahakamani”ย 

    “Vijana, tafadhari sana hizo ni pesa kwa ajili ya matibabu yaย  Mtoto, kama mnamkamata Matilda basi hizo pesa hazihusiani naย  sababu yoyote ile ya Kumkamata, hizi ni pesa kutoka kanisani”ย  Alisema Mchungaji George akitaka pesa ziachwe lakini polisiย  hao walikua tayari wameanza kumchukua kwa nguvu Matildaย  ambaye alikua akipiga mayowe ya kutaka aachwe ili akamtibieย  Binti yake Patra.ย 

    Aliyeucheza mchezo huu alikua amejibanza mahali akiangaliaย  namna mpango wake unavyofanikiwa, Neema akashangilia baada yaย  Matilda kutupwa kwenye difenda ya polisi, gari hiyo ikaondokaย  haraka sana. Mchungaji na Mama Naomi wakatazamana kwaย  mshangao mkubwa hawakujua waende wapi, waingie kwa daktariย  bila pesa au waelekee Kituo cha polisi ambacho walikuaย  wametajiwa.ย 

    “Mchungaji nenda Polisi Mimi naenda kwa Mzazi mwenzake”ย  Alisema Mama Naomi huku taharuki ikizidi kuwa kubwa ndani yaoย 

    “Kwa Mzazi mwenzake wakati amemkataa Mtoto? Twende pamojaย  polisi kujua nini chanzo cha kukamatwa kwake”ย 

    “Na vipi kuhusu hali ya Mtoto Mchungaji?” Aliuliza Mama Naomiย 

    “Oooh hapa sasa nachanganikiwa Mimi, basi baki hapaย  ukiangalia hali ya Mtoto, wacha Mimi nikimbilie Polisi”ย  Alisema Mchungaji, akakimbilia kwenye gari na kuondoa gariย  kwa kasi sana, Mama Naomi alipoona Mchungaji ameondoka nayeย  akaondoka kuelekea kwa James kumpa taarifa.

    Neema akajitokeza kisha akajinasbu kua ni lazima Matildaย  aondoke Dar.ย 

    ********ย 

    Mchungaji George alipofika kituo cha polisi alipaki gariย  kwenye maegesho, kisha akashuka haraka haraka na kukimbiliaย  ndani ya kituo hicho cha polisi. Akapandisha ngazi kabla yaย  kukutana na polisiย 

    “Afande nimekuja haraka sababu bado sijajua sababu yaย  kukamatwa kwa huyu Binti” Alisema Mchungaji akiwaย  anamwangalia Matilda ambaye alikua amekalishwa chiniย 

    “Nifuate” Alisema polisi huyo kisha akamnyanyua Matildaย  wakaelekea kwenye chumba kimoja ambacho kilionekana waziย  kilikua chumba cha mahojiano, Mlango ukafungwa, ndani kulikuaย  na askari wawili wengine ambao waliwakuta humoย 

    “Huyu Binti ni mwizi, mahali anapoishi siyo pake kuna Mtuย  amemweka akae hapo lakini mwenye nyumba amelalamika juu yaย  upotevu wa vitu vyenye thamani ya Zaidi ya Milioni 10”ย  Alisema polisi huyo akiwa na sura kavu sana.ย 

    “Ameiba?”ย 

    “Ndiyo”ย 

    “Afande Mimi siyo mwizi na sijawahi kuiba chochote kile,ย  nimeishi pale kwa zaidi ya mwaka mmoja iweje leo ionekaneย  Mimi ni Mwizi? James anakosea sana” Alisema kwa uchungu sanaย  Matildaย 

    “Kaa kimya hupaswi kuongea chochote kile hadi paleย  aliyekushtaki atakapofika hapa” Alisema polisi huyoย 

    “Jamani kuweni na huruma, huyu Binti ana Mtoto mdogo ambayeย  ni mgonjwa sana na yupo Hospitalini, hizo pesa mlizomkamataย  nazo ni michango ya kanisa kwa ajili ya Matibabu” Alisemaย  Mchungajiย 

    “Kwakua umeshafahamu nini kilichopelekea akakamatwa basi niย  vema ukakaa kimya huku ukisubiria uendeshwaji wa kesi hii,ย  kama unahitaji kuwa shahidi wa hili basi tukutane mahakamani”ย  Alisema Polisi huyo ambaye alishapewa Hongo na Neema ili kesiย  hiyo iwe haiย 

    “Nenda nje” Akasema polisi huyo akimtaka Mchungaji aondoke

    “Afande kua na moyo wa utu japo hata kidogo, Mtoto wakeย  anaangamia kule Hospitali kwa kukosa matibabu, ninaomba sanaย  na nipo chini ya Miguu yenu ikibidi hata kua Mdhamini waย  hili, hizo pesa nazihitaji zikamtibie Binti yake” Alisemaย  Mchungaji George akishinikiza apewe pesa hizo lakini polisiย  wakamtoa Nje Mchungaji Georgeย 

    Matilda alikua Mtu wa kulia muda wote huku akiomba kwa Munguย  kuhusu hali ya Binti yake, dakika chache baadaye aliingiaย  Neema akiwa ameambatana na yule Mwanaume anayeitwa Masudi,ย  akavuta kiti na kuketi, Matilda alishtuka baada ya kumwonaย  Neemaย 

    “Matilda, kama ulifikiria unaweza ukachomoka kwenye hili basiย  sahau kabisa” Alisema Neema, polisi wakatoka ili kuwaachiaย  wazungumzeย 

    “Kumbe ni wewe ndiye uliyenifungulia hii kesi isiyo na kichwaย  wala Miguu, wewe ni Mzazi mtarajiwa si ndiyo? utajisikiajeย  ukitendewa namna nitendewavyo Mimi…Kumbuka Binti yangu yupoย  Hospitalini na anahitaji Matibabu…” alisema kwa uchunguย  Matilda huku chozi likimvuja, alishindwa kufuta chozi sababuย  alifungwa pingu mikononiย 

    “Kumbe inaumiza eeeh? basi hivi ndivyo ambavyo Mimi piaย  naumia ninapokuona mbele ya macho yangu, una chaguo moja laย  kufanya, nalo ni kukubali kurudi kwenu kabla hujafikishwaย  mahakamani, ukikubali hii kesi naifuta haraka sana, sitakiย  kukuona ukiendelea kuwa karibu na James kwa lolote lile”ย  Alisema Neemaย 

    “Dada yangu kama unafikiria Mimi ni dhahifu kwenye hiloย  naomba usahau kabisa, ikibidi mniuwe lakini siwezi kuidhurumuย  haki ya Mwanangu Kumjua Baba yake” Alisema Matilda, akapigwaย  kofi na Neemaย 

    “Mshenzi mkubwa wewe, sasa endelea kujifanya Mjuaji kwenyeย  hili, mwisho wako unakuja” Alisema Neema kisha aliondoka hapoย  akiwa na Masudi, walipofika kwenye gari Neema alionekana kuaย  na hasira sana sababu lengo halikua kesi bali ni kumtisha tuย  Matildaย 

    “Usiwe na hasira, huu ni mwanzo tu Naamini matesoย  atakayoyapata atakubali kuondoka mwenyewe” Alisema Masudi,ย  Mwanaume ambaye alionekana kua karibu sana na Neema

    “Kama kuteswa inabidi ateswe haswa, kwasababu amekataaย  kuondoka kwa uhuru basi ataondoka kwa shari kama atakavyo”ย  Alisema Neema kisha aliondoa gari haraka sana.ย 

    “Nikusaidie nini?” lilikua ni swali aliloulizwa Mama Matildaย  baada ya kufika ofisini kwa James, hakukaribishwa ofisiniย  bali aliachwa getini azungumzeย 

    “Ni kuhusu Matilda” Alisema Mama Naomi akiwa anahema “Amefanyaje?”ย 

    “Amekamatwa na Polisi muda mchache uliopita, hadi sasaย  hatujui sababu ya kukamatwa kwake. Nakuomba James, hunijuiย  lakini Mimi ni jirani wa Matilda kule anakoishi, fanyaย  uwezalo ili aachiwe”ย 

    “Usinichekeshe ndugu yangu,, yaani umetoka kote huko hadiย  hapa ili kuniambia hicho tu? unaonekana kama Mwanamke mwenyeย  busara zako lakini sikutegemea kama mwisho wa siku ungesimamaย  na Mwizi” Alisema James akionekana hana wasiwasi kabisaย 

    “Mwizi? nimeishi naye kwa siku zote hakuwahi kuonekana naย  tabia hiyo ya wizi, hata kama akawa mwizi lakini ana haki yaย  kuokoa Maisha ya Binti yake, fanya kwa ajili ya Patra niย  Binti yako yule James” Alisema Mama Naomi, kofi likatuaย  kwenye shavu lake la kuliaย 

    “usirudie tena hiyo kauli, hakuna unachojua kuhusuย  Mimi…..Ondoka” Alisema kwa hasira sana Jamesย 

    “Laiti kama ungelijua Maisha anayopitia Matilda sasa hiviย  wala usingethubutu kunipiga, basi siyo Mtoto wako lakiniย  kumbuka wewe ndiye uliyemtoa kwao basi thamini utu kamaย  Binadamu wa kawaida” Alisema Mama Naomi kwa uchungu sana hukuย  Mtoto akiwa analia mgongoniย 

    “Nini ambacho hujanielewa?” Alisema James kwa hasira akiwaย  anamsogelea Mama Naomi, kelele hizo zikamtoa Sekretari hadiย  njeย 

    “Bosi kuna nini?” aliulizaย 

    “Simjui ananilazimisha nimsaidie, amekua king’ang’anizi sanaย  Jack!”

    “Halafu kama alikuja jana huyu na Mdada mwingine, suraย  nishaikumbuka kumbe walikua wanahitaji msaada? kwaniniย  usiwasaidie Bosi?” aliuliza Jackย 

    “Hujui kitu hakuna msaada unaotolewa kwa kung’ang’ania namnaย  hii, Kutoa ni moyo, sikia nenda ofisi zingine hapa hatusaidiiย  omba omba” Alisema James kisha akarudi ofisiniย 

    Jack akamtazama Mama Naomi. Akiwa kama Mwanamke alimuoneaย  huruma Mama Naomi na Mtoto aliye mgongoni, akatoa noti yaย  elfu tano akampaย 

    “Chukua hii itakusaidia” Alisema Jackย 

    “Asante lakini huu siyo msaada ambao Mimi niliutaka kutokaย  kwa Bosi wako” Alisema Mama Naomiย 

    “Ulikua unahitaji msaada gani?” Jack akapata shahuku yaย  kutaka kujua zaidi maana hakuna ombaomba ambaye anawezaย  kukataa shilingi elfu tano, akasogeaย 

    “Bosi wako James amezaa na Msichana yule ambaye nilikuja nayeย  jana, James amemkataa Mtoto sababu ni mlemavu, Mtoto yupoย  mahututi Hospitalini, Yule Msichana amekamatwa na polisi mudaย  siyo mrefu ndiyo maana nilikuja hapa ili kumpa taarifaย  akamsaidie hata Mtoto sababu anahitaji matibabu, hakuna pesaย  ya kumtibia” Alisema kwa uchungu Mama Naomi huku akikaribiaย  kudondosha chozi, Jack aliumia sanaย 

    “Sikia chukua hii kadi yangu, kwa lolote naomba unipigie,ย  nenda sababu James ana hasira sana” Alisema Jack, kilaย  alivyomtazama Mama Naomi akiwa anaondoka alisikitika kishaย  akarudi Ofisini, akamkuta Bosi wake akiwa anataka kutokaย 

    “Yaani Watu wengine Bwana kutaka kuharibiana siku tu, kwaniย  ni lazima kumsaidia Ombaomba….Mimi natoka sijisikii kufanyaย  chochote kwa sasa, siku nyingine usiruhusu Omba omba katikaย  ofisi yangu”ย 

    “Sawa Bosi” Aliitikia Jackย 

    Jua lilikua kali lakini Mchungaji George alihitaji kujuaย  hatma ya Maisha ya Matilda, Mateso yalianza upande waย  Matilda, alipigwa bila kosa lolote lile. Lengo lilikua niย  kumtaka aondoke Dar ili asiwe kero kwa James, ndichoย  alichokipanga Neema.

    Baada ya Saa nzima aliingia Mama Naomi akamkuta Mchungajiย  George akiwa anachomwa na jua la Mchanaย 

    “Eeeh kulikoni Huko Hospitali kuna usalama?” aliulizaย  Mchungaji George kwa Mshtuko sababu alimuacha Mama Naomiย  Hospitaliย 

    “Sijui Mchungaji lakini natumaini hakuna kitakachoharibika,ย  Mungu aliye hai anapigana vita nzito muda huu, vipi kuhusuย  Matilda?”ย 

    “Bado yupo kituoni, hizo sauti unazozisikia ni zake,ย  anaonekana kua kwenye mateso makali” Alisema Mchungajiย 

    “Jamani sasa amewakosea nini?”ย 

    “Wanasema ameiba vitu vyenye thamani kwenye nyumba anayoishi”ย 

    “Ameiba? si kweli, Maisha anayoishi Matilda ni ishara toshaย  kua hawezi kuiba, hawa Watu kwanini waneamua kumkatili Bintiย  wa watu jamani”ย 

    “Hatuna namna Zaidi ya kusubiri muda utupe majibu sahihi,ย  Kama hakufanya hivyo basi ataachiwa tu ila kinachonipa hofuย  ni kuhusu Binti yake, sijui itakuaje”ย 

    “Mchungaji hapo ni pazito zaidi sababu uliponiacha Hospitaliย  nilitoka na kwenda kwa Mwanaume aliyezaa naye lakini huweziย  amini kamkana mbele ya Macho yangu, kanipiga kofi pia”ย  Alisema Mama Naomi akiwa anamweka vizuri Mtotoย 

    “Sijui hata tufanye nini, kwani wazazi wa Matilda wapo wapi?”ย 

    “Wazazi wake wapo Njombe, pamoja na shida anazopitia lakiniย  alisema hawezi kurudi kwao wala kusema chochote kwa Wazaziย  wake”ย 

    “Oooh Mungu wangu, basi wewe ungerudi tu nyumbani Mimiย  nitabakia hapa kwa masaa kadhaa kwa ajili ya kujua Hatma yaย  Matilda” Alisema Mchungaji Georgeย 

    “Sawa Mchungaji kwa chochote kile tuwasiliane” Alisema Mamaย  Naomi kisha akaondoka kituoni hapo.ย 

    Upande wa pili, gari moja lilikua likiendeshwa kwa spidiย  kubwa sana, ndani yake alikuwepo James akionekanaย  kuchanganikiwa, maneno ya Mama Naomi yaliendelea kujirudiaย  ndani ya Kichwa chake, akawa anapiga usukani kwa hasira,ย  alikanyaga mafuta hadi nyumbani kwake, akateremka harakaย  kisha akaingia ndani

    Kama akili yake ilivyomtuma ndivyo alivyokuta, Neema alikuaย  ameketi huku akitikisa miguu yake, pembeni kukiwa na embeย  bichi ambalo lilikua linasukuma tabasamu lake, baada yaย  kumwona James akiwa ameingia na taharuki akamuulizaย 

    “Kulikoni Baby mbona una taharuki?” aliuliza Neema akiwaย  ameacha kula embe Bichiย 

    “Nenda kafute kesi inayomkabili Matilda” Alisema James kishaย  akajitupa kochini kama Mtu aliyechoka sanaย 

    “Unasemaje?”ย 

    “Ulivyosikia ndivyo nilivyosema, hakuna sababu ya kuendeleaย  na kesi, tuangalie namna nyingine ya kumfanya Matilda aondokeย  hapa Mjini” Neema akamtazama Kwa hasira Jamesย 

    “James Mimi natarajia kua Mama wa Mtoto wako, siwezi kuzaaย  Mtoto katika familia yenye migogoro namna hii, ikishindikanaย  nitoe ujauzito ili ulee Mtoto wako na Matilda” Alisema Neemaย 

    “Sina maana hiyo Neema, Sina lengo hilo nawe huna sababu yaย  kufanya hivyo, tambua kiu yangu ni Mtoto lakini naona Matildaย  anateseka sana, Mtoto wake yupo Hospitalini”ย 

    “Kwahiyo umeanza kua na huruma si ndiyo? Basi hakuna sababuย  ya kujificha, jitokeze hadharani ujitangaze kua Bilioneaย  mwenye Mtoto Mlemavu, si una shida sana ya Mtoto basi hakunaย  sababu ya Mimi kubeba huu mzigo wakati una Mtoto unaye muoneaย  huruma” Alisema Neema kwa hasira zaidi, akanyanyuka iliย  aondoke lakini James akamshika mkono kwa lengo la kumzuiaย  asiondokeย 

    “Mpenzi hupaswi kua na hasira sababu wewe ni Mama mtarajiwa,ย  natamani haya mambo yaishe kwa namna nzuri, basi nitaendaย  Polisi kwa ajili ya kuzungumza na Matilda ili aondoke hapaย  Mjini” Alisema James lakini Neema akatoa Mkono wa Jamesย  akaelekea chumbani.ย ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TANO Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    6 Comments

    1. Sir, Yowas on September 15, 2024 4:38 pm

      Sawa

      Reply
      • Given Gihsy on September 16, 2024 12:02 am

        kama ni kwel duuh matlida anapep yake

        Reply
    2. Lus twaxie on September 15, 2024 8:35 pm

      Aiseee huyu enema anazngua ..s wampe pesa Ile mchungaj jmn ๐Ÿ˜ฃ๐Ÿ˜ฃ

      Reply
    3. Sabiti on September 16, 2024 10:50 am

      Moyo wangu unauma hadi joz dah!! Tukija kwenye uhalisia sure ni maisha watu wanapitia jmn

      Reply
    4. Ibrahim on September 17, 2024 12:14 pm

      Hadithi nzri nakama ina uhalisia fulani hivi

      Reply
    5. ๐Ÿ“… โœ‰๏ธ Unread Alert - 1.95 Bitcoin from partner. Review funds => https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=9eeffce00173706dd9e1b1d98186c9ce& ๐Ÿ“… on October 9, 2025 6:24 pm

      a1na1b

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Odds za Moto November 8, 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    Kampuni ya michezo ya kubashiri LEONBET Tanzania imezidi kudhihirisha ubunifu wake katika kukuza michezo na…

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.