Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04
    Hadithi

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJuly 15, 202514 Comments7 Mins Read532 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu

    Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume wake kisha kwa  mshangao akamwambia 

    “Mume wangu unatokwa na Damu puani” alisema akiwa anarudi nyuma taratibu,  Mume wake akapeleka kidole puani. Alikua akitetemeka akikiangalia kidole chake  kilichotapakaa damu. Kisha alimtazama Mke wake, aliiyona damu pia puani kwa Mke 

    wake. Akamnyooshea kidole kumwambia kua anatokwa na damu, naye Mke alipopeleka  kidole puani aliiyona damu mbichi.  

    SEHEMU YA NNE

    Hali ya hatari na taharuki vilianza kutawala, hisia mbaya iliwangia. Papo hapo, mke  Wake alianza kutapika Damu.  

    Aliishiwa nguvu akajikuta akianguka chini kama mzigo huku akiwa amebanwa na  kwikwi mbaya. Mume wake alikua amesimama pale pale huku damu zikizidi kumtoka  puani na Mdomoni, alikua akianza kukosa pumzi. Alihisi kifo mbele yake huku akiwa  amelishikilia koo lake kuashiria alikua anapoteza uwezo wake wa kupumua. 

    “Mungu nisa…mehe” ilikua ni kauli ya mwisho ya Mume wa yule Mwanamke,  akadondoka na kufariki papo hapo huku Mke wake naye akimalizikia kufariki hapo.  

    *** 

    Jua la Utosi lilikua tayari limeshatua. Nyumbani kwa Mzee Kova waliendelea  kumsubiria Mlinzi arudi lakini masaa yaliendelea kutembea, Mzee Kova akawaambia  Wazee wengine kua waongozane kuelekea nyumbani kwa Mtimbe. Walinzi wawili  waliachwa ili kuhakikisha Zahoro na Baba yake Mzee Miroshi hawatoroki. 

    Mguu kwa mguu, walipofika njia panda walikutana na Miili mitatu akiwemo Mlinzi wa  Kijiji. Kila mmoja alishtuka sana kumwona Mlinzi wa Kijiji akiwa amekufa huku damu  ikiwa imetapakaa usoni, miili mingine ilikua na hali hiyo hiyo kuashiria kua wote  walikufa kifo kinacho fanana. 

    Maiti moja ilikutwa na kipande cha karatasi, Mzee Kova akaagiza asomewe kilichomo  ndani yake. Mlinzi mmoja akakichukua na kumsomea  

    “MWISHO UMEFIKA” alisema yule Mlinzi kwa sauti ya usikivu, lakini hapo hapo  alianza kutokwa na damu puani, masikioni huku hali ya kuchanganikiwa ikianza  kumzonga. Ilibidi wote wasogee nyuma huku wakimtazama yule Mlinzi akiwa anatapa  tapa chini, hadi alipofariki mbele ya macho yao. 

    Halikua pigo la kawaida, liliwatingisha Wazee wote akiwemo Mzee Kova na Mzee  Kisugu. Maiti Nne zilikua mbele ya macho yao, wakiwa hawajui nini wanatakiwa  kufanya, ghafla wingu jekundu lilianza kutanda angani likisindikizwa na Upepo mkali  sana. 

    Upepo mkali sana ulizidi kusukuma na kulipanga wingu jekundu angani, giza lilianza  kuingia. Taharuki ilianza, Watu walianza kukimbizana wasijue wanaelekea wapi. Sauti  ya Bibi Lugumi ilisikika Kijijini pote ikiitangaza laana ambayo tayari ilikua imeshakivaa  Kijiji cha Nzena. 

    Sasa ilikua rasmi masikioni mwa kila mwenye akili na ufahamu kua, vifo na mabadiliko  ya hali ya hewa vyote vilitokana na Laana ya Bibi Lugumi kutokana na kifo cha  Masumbuko. Vilio vilitanda kote, giza lilishamili kwa kasi na kukifunika Kijiji chote cha  Nzena. 

    Ndani ya dakika mbili, kijiji chote kilikua giza tupu. Upepo mkali uliacha kuvuma kisha  mvua ilianza kunyesha. 

    ** 

    “Baba” Zahoro alimwita Mzee Miroshi aliyekua amejiinamia. Mzee huyo aliinua kichwa  chake na kumtazama Zahoro, sura yake ilipoteza raha.  

    “Nini mwisho wa kila kitu?” aliuliza Zahoro, sauti yake ilikua juu kidogo sababu bado  mvua kubwa ilikua ikiendelea kunyesha. 

    “Kifo” alijibu kwa sauti kavu Mzee Miroshi. Hakutaka kumtazama tena Zahoro aliyeanza  kudondosha chozi la kukosa tumaini. 

    “Tutakufa sote?” aliuliza tena Zahoro, Mzee Miroshi alitikisa kichwa chake. Koroboi  ilikua ikiwaka ili kuwapatia mwanga kidogo.  

    “Kwanini sasa hiyo laana isihukumu walio husika, kwanini itutese ambao hatukuwa  sehemu ya Maisha yaliyopita?” aliuliza Zahoro kwa sauti ya Kilio kilicho jaa lawama,  Mzee Miroshi hakutaka kumjibu chochote Zahoro.  

    Ukimya wa Mzee Miroshi ulimsumbua Zahoro, aliamua kumtikisa Baba yake atoe jibu,  ndipo Mzee Miroshi akapaza sauti yake kwa ukali akisema 

    “Alitulaani sisi na vizazi vyetu, hata wewe umelaanika Zahoro. Sote hapa Kijijini  tutakufa, usiniuliza chochote. Nimechoka, nimechoka kabisa” alisema kwa sauti kali ya  kufoka huku chozi likimtoka Mzee Miroshi, Zahoro alielewa namna Baba yake alivyokua  akijisikia. Akasogea pembeni na kujiinamia huku akiwa analia chini kwa chini. 

    Masaa mawili yalipita, mvua iliacha kunyesha. Palikua bado giza, kimya pekee ndicho  kilichokua kinaongea. Bundi walianza kulia kila kona ya Kijiji huku hofu na Mashaka  vikizidi kusikika. 

    Familia moja ya Mama, Baba na Mtoto mdogo ilikua imejikunyata ndani ya kijumba  chao kidogo cha Nyasi. Palikua kimya kabisa isipokua sauti za Bundi huko nje, sauti hizo  zilizidi kuongeza hofu baina yao. 

    Si Baba, wala Mama aliyepata Ujasiri wa japo kutoa sauti ya aina yoyote ile. Walianza  kusikia kishindo huko nje, kisha dakika kadhaa zilipita pakiwa kimya, kisha mlango wao  wa Bati ulianza kugongwa kwa utaratibu. Pumzi zao zilizidi kuongezeka huku hofu  ikizidi kuwachapa, mgongaji hakusema chochote isipokua kuendelea kugonga 

    Baba wa hiyo familia ambaye ni Mzee wa makamo, alijikuta akisimama kama  Mwanaume kisha taratibu alisogea mlangoni. Mgongaji aliendelea kugonga bila kusema  chochote 

    Yule Mzee hakuweza kuvumilia kukaa kimya, kwa sauti ya upole iliyojaa kitete aliuliza 

    “Nani?” Baada ya Mzee huyo kuongea, mgongaji aliacha lakini baadae aligonga tena.  Ndipo Mzee huyo akauliza tena 

    “Nani wewe unagonga na hausemi?” Zikapita sekunde kadhaa za Ukimya, Mzee huyo  akakata shauri ili arudi alipoiacha familia yake lakini mgongaji aligonga tena. Yule Mzee  akahamaki akauliza kwa sauti ya hasira kidogo 

    “Ni Nani wewe?” 

    “Mimi ni laana nimekuja kukumaliza” ilisikika sauti nzito ambayo ilimduwaza, akajikuta  akiishiwa nguvu. Mara mlango ulifunguka wenyewe kisha mwanga uliingia ndani na  kuwaangaza 

    Kitu cha ajabu kilimwingia yule Mzee kisha aliigeukia Familia yake na kuitazama pale  ilipojificha. Mke wake alijawa na hofu sana, aliona wazi kua kuna ufahamu usio wa  kawaida ulimwingia Mume wake 

    Yule Mzee akaingia chumba kingine kisha akatoka akiwa ameshikilia Upanga mkononi,  akasimama mbele ya Mke na Mtoto wake akawaambia 

    “Laana imewafikia” kisha aliunyanyua upanga na kuanza kuwachakata kama kuni bila  huruma yoyote ile, ile sauti ya ajabu ilizidi kumwambia kua aimalize familia hiyo. Yule  Mzee alihakikisha anawauwa wote wawili, kisha ile sauti ikamwambia 

    “Hata wewe umelaaniwa, laana imekufikia” alipoambiwa hivi alipiga magoti kisha  alianza kujichinja mwenyewe, damu ilikua ikiruka, alianguka na kufa pale pale. Sauti ile  ya ajabu ilizunguka nyumba nyingi hapo Kijijini.  

    **** 

    Siku iliyofuata. Kijiji kizima kilikua kimetulia sana, hakuna aliyefungua mlango na  kutoka ndani ya Nyumba yake. Jua lilipochomoza na kukimulika Kijiji chote ndipo  walipoanza kufungua Milango taratibu kwa tahadhali ya Hali ya juu sana. 

    Baada ya muda mchache kupita, watu wengi walikua nje. Ndipo walipokuta vifo vingi  sana vya familia moja moja, damu zilikua zimetapakaa kila kona.  

    Hali ya Kijiji ilijaa simanzi na huzuni sana, pia moshi ulikua ukifuka. Kila mmoja  aliogopa, Ndani ya muda mfupi tu zaidi ya Watu 72 walikua wamefariki 

    Mzee Kova akaitisha mkutano wa Kijiji kizima kujadili hatma ya Kijiji chao cha Nzena.  

    Wanakijiji wote walikusanyika sehemu ya Mkutano mahali pa wazi, Mzee Kova  alisimama kama Mzee wa Kijiji na kuzungumza na Wanakijiji wenzake. Vilio  havikukona licha ya Mkutano wa Kijiji kuendelea ili kupata suluhu.  

    “Nyote mlikua mashahidi miaka iliyopita baada ya kumtoa kafara Masumbuko, Kijiji  kilipata neema kwa miaka zaidi ya Kumi, yote haya yanayoendelea hapa Kijijini  yametokana na Usiku ule, Bi. Lugumi aliitamka laana kwa kinywa chake kisha alijiuwa  kwenye moto. Maneno yake ndiyo yanayo kitafuna Kijiji leo hii. Hali ni mbaya kila kona,  mauwaji ya kutisha yanaendelea kutokea.” Alipaza sauti Mzee Kova lakini sauti yake  ilizimwa na Mwanakijiji mmoja aliyepaza sauti na kusema 

    “Ulikua ni ubabe wako wa kutosikiliza wengine, uchawi uliokua ukikitesa Kijiji hiki  ulitokana na wewe na wazee wengine. Mlimtoa masumbuko kafara kwasababu ya  kuficha uchafu wako, Mimi nimepoteza kila kitu hivyo siogopi tena unaweza  ukaniadhibu tu” Sauti ya mwanakijiji huyu ilijaa hisia ya maumivu makali sana, kisha  ilifuatiwa na Minong’ono ya Wanakijiji wengine. 

    “Tulieni, hamuoni kama Tutakosa suluhu?” alipaza sauti Mzee Kisugu, lakini Mama  mmoja aliyekua akilia alimjibu

    “Hamuwezi kutuzuia kuongea kwasasa, mlijigawia Kijiji chote na kukitawala kwa ukatili  na mabavu. Haya ni matokeo ya Uchafu wenu nyie Wazee, mtawajibika” hali ya utulivu  ilianza kukosekana, Walinzi kadhaa wa Kijiji walisogea na kumpa msaada Mzee Kova  huku Wanakijiji wakipaza sauti zao kua Mzee Kova anapaswa kuwajibishwa 

    Wakiwa wanaendelea kujibizana, walianza kusikia sauti ya Bi. Lugumi ikisema 

    “Kufaaaaa‼ kufaaaa‼” kila aliyeisikia sauti hii alianza kutetemeka huku damu nzito  ikimtoka puani kisha walikufa papo hapo, hali ya taharuki iliingia na kufanya kila  mmoja atawanyike anakokujua yeye mwenyewe. Sauti ya Bibi Lugumi ilizidi kusambaa,  ilikua ni sauti ya kunong’ona iliyotoka kwa kuivuta sana. 

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TATU Hapa Hapa Kijiweni

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

     

    riwaya riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua riwaya za kuvutia

    14 Comments

    1. Jake3933 on July 15, 2025 5:17 pm

      Your audience, your profits—become an affiliate today! https://shorturl.fm/DrJwQ

      Reply
    2. King zahoro on July 15, 2025 7:28 pm

      Nice

      Reply
    3. G shirima on July 15, 2025 8:18 pm

      Good job

      Reply
      • Karim on July 15, 2025 9:40 pm

        Mkasa wa kutisha unaosisimua huku tukijifunza Kuwa mwisho wa ubaya mauti

        Reply
        • VERONICA on July 16, 2025 2:30 pm

          Malipo ni duniani

          Reply
    4. Eunice Timba on July 15, 2025 9:38 pm

      Hii nzuri sana yaaan sehemu ya 4 tu ndo iko moto hv sipati picha huko mbele

      Reply
    5. Ankush on July 15, 2025 11:07 pm

      Mambo yazidi kunogaa

      Reply
    6. Maestro05 on July 15, 2025 11:09 pm

      Kazi nzuri Sana Admin

      Reply
    7. Kourtney2233 on July 16, 2025 4:40 am

      Earn passive income on autopilot—become our affiliate! https://shorturl.fm/WVEQI

      Reply
    8. 🔨 Ticket; Operation 1,958539 BTC. GET > https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=879ce32d98ae1693cfd100fee748b1be& 🔨 on July 16, 2025 8:59 am

      773dw1

      Reply
    9. Lora251 on July 16, 2025 5:51 pm

      Earn big by sharing our offers—become an affiliate today! https://shorturl.fm/rsKiz

      Reply
    10. Vivian483 on July 16, 2025 5:59 pm

      Tap into a new revenue stream—become an affiliate partner! https://shorturl.fm/zYTbj

      Reply
    11. Isher on July 16, 2025 6:57 pm

      Next

      Reply
    12. Alexandria2220 on July 16, 2025 8:07 pm

      Start earning instantly—become our affiliate and earn on every sale! https://shorturl.fm/6Zw4r

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.