Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    AFCON

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Tatu-03)
    Hadithi

    Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Tatu-03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaApril 25, 2025Updated:April 27, 202539 Comments11 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nyumba Juu Kaburi

    Tulipishana Mwaka mmoja wa kuingia chuoni, alinitendea wema kila nyakati. Hata wakatiย  ambao alipaswa kufurahi alinipa furaha yake na kisha yeye alibakiwa na huzuni yangu.ย  Nilimwona akiwa anafunguliwa kutoka juu ya feni akiwa amevalia gauni lake jekundu.ย 

    Hakika maneno ya yule Bibi yalianza kutimia, nilimpoteza mmoja nimpendaye. Nilijiegemezaย  ukutani nikilia kwa kwikwi nikiushuhudia mwili wa Zena ukiondolewa na Askari Polisiย  waliokua hapo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Mtaa.ย  Endelea

    SEHEMU YA TATU

    Mimi na Caren tulibakia chumbani kwa Zena tukilia, haikua rahisi kuamini kua Zena alikuaย  amekufa kikatili sana kwa kujinyonga. Mara simu yangu ilianza kuita kutoka kwenye mkobaย  wangu niliokua nimeutupia pembeni, nilishtuka sana. Niliacha kulia nikauvuta mkoba kishaย  nikaitoa simu yangu ambayo bado ilikua ikiendelea kuitaย 

    Moyo ulinipiga โ€˜Paaaโ€ผโ€™ nilipoona ni Mama yangu ndiye aliyekua akinipigia. Sikutaka kusikiaย  taarifa nyingine mbaya. Niliiacha simu iite hadi ilipo acha kuita, niliirudisha kwenye mkobaย  mara moja halafu fikra zangu zikawa nyumbani kwetu.ย 

    Maneno ya yule Bibi yalikua na nguvu ya kunizunguka kichwani, nilihisi nyumbani kwetuย  hapako salama. Niliumia ndani ya moyo wangu huku nikiitupa miguu yangu sakafuni.ย ย 

    Sikujua ni Nani alikua anafuata baada ya Zena, yule Bibi ni Nani na kwanini haya mauzauzaย  yameanza baada ya kuhamia kwenye ile nyumba. Maswali haya yote nilijua ni Nani anapaswaย  kuyajibu. Ni yule Mzee wa nyumba jirani, huwenda anafahamu jambo fulani la kutisha kuhusuย  nyumba yetu.ย 

    Nilinyanyuka kutoka sakafuni, nikamtazama Caren aliyekua amelegea kutokana na kukosaย  nguvu kwa kile kilichotokea, tulimpoteza rafiki mzuri sana katika mazingira ya kutatanisha.ย  Nilimwambia Carenย 

    โ€œNataka kupata majibu ya haya yote Caren, siwezi kuruhusu hii hali iendeleeโ€ sauti yangu ilitokaย  kwa hisia kali ya maumivu, nilifuta chozi langu. Caren naye alisimama. Tulikua wawili tu ndaniย  ya kile chumba cha Zena.ย ย 

    โ€œUkweli upi, ni kuhusu yule Bibi au kifo cha Zena?โ€ aliniuliza, nilimtazama kwa sekundeย  kadhaa kisha nilimwambiaย 

    โ€œVyote kwa pamoja, jina la Zena lilikua kwenye ile Barua uliyopewa na yule Bibi wa ajabu.ย  Sijui, lakini nahisi kuna shida sehemuโ€ Umakini wa Caren uliongezeka, akanitazama kwaย  shahuku akaniulizaย 

    โ€œShida Sehemu?โ€ย ย 

    โ€œNdiyo, baada ya kuhamia kwenye ile nyumba nilianza kupata hisia ya ajabu. Sitaki kuwaambiaย  Wazazi wangu kuhusu hilo lakini nahisi kuna Mtu anajua jambo kuhusu ile nyumba, Carenย  nisikilize Mimiโ€ nilisema kisha nilimshika mabega Caren ili nimueleze zaidi. Nilimfanya Carenย  kua Mshirika wangu

    โ€œKuna Mzee nyumba jirani nina wasiwasi anajua jambo, ile nyumba sio ya kawaida kabisa.ย  Sitaki Wazazi wangu wajuwe sababu watachanganikiwa. Tunaweza kuutafuta ukweli?โ€ย  nilimuuliza, alinitazama kwa tafakari fupi kisha aliniambiaย ย 

    โ€œKama hisia zako zinakwambia hivyo Celin, sina chaguoโ€ nilimkumbatia Caren, angalau nilipataย  Mtu anayeweza kunielewa.ย 

    Nilirudi nyumbani jioni, hofu na mashaka viliendelea kunitafuna hadi nafika nyumbani.ย  Niliogopa kukuta Watu wengi pale nyumbani, niliogopa kusikia sauti ya Kilio, niliogopaย  kupoteza Mtu mwingine. Nilipofika getini kwetu, nilisimama kidogo huku macho yanguย  yakielekea nyumbani kwa yule Mzee.ย 

    Palikua kimya, hapakua na dalili ya Mtu. Nilijiweka sawa kiakili ili Wazazi wangu wasigundueย  lolote, sikutaka wajuwe kuhusu kifo cha Zena wala jambo lolote lile lenye utata. Nilipoingiaย  Bustanini niliitazama sana nyumba yetu, nafsi yangu iliniambia kuna jambo lisilo kawaidaย  kuihusu hii nyumba lakini sikua na ushahidi wa kuthibitisha hilo.ย 

    Nilipata amani nilipowakuta Wazazi wangu wakiwa wameketi sebleni wanaangalia taarifa yaย  Habari, angalau moyo wangu ulipata kupumzika.ย 

    Niliwasalimia kisha nilipandisha ngazi nikaelekea chumbani kwangu. Nilisimama kando yaย  dirisha nikiitazama nyumba ya yule Mzee, bado ilikua kimya. Palikua na majani mengi sakafuniย  kuashiria kua eneo hilo halikufanyiwa usafi kwa muda mrefu.ย 

    Baada ya kusimama kwa muda kidogo nilirudi na kuketi kitandani nikiwa nakumbuka matukioย  ya siku nzima, chozi lilinitoka tena. Kusema ukweli kifo cha Zena kiliniumiza sana, kuna namnaย  nilijiona Mimi ni Mkosaji. Basi nilijiegesha kidogo, nikajikuta nikipitiwa na Usingizi.ย 

    Nilishtuka, bado palikua na giza. Mwili ulikua umechoka sana, hisia ya kua nililala muda mrefuย  ilinijia. Nilijinyoosha kidogo kabla ya kuchukua simu na kuangalia saaย 

    Niliona ilikua ni saa 7:11 Usiku, nilinyanyuka taratibu kutoka kitandani kisha nikasogea paleย  dirishani na kuangalia nyumbani kwa yule Mzee. Bado palikua kimya, hapakua na dalili yoyoteย  ile, Mbwa walikua wakibweka sana.ย 

    Nilifungua mlango taratibu kisha kwa mwendo wa kuchoka nilishusha ngazi, taa zilikua tayariย  zimezimwa kuashiria kua Wazazi wangu walikua wameshalala, swali pekee nililojiulizaย 

    โ€œInawezekanaje Wazazi wangu walale bila kuniamsha?โ€ Sikupata jibu la haraka, nilitembeaย  taratibu baada ya kufika sebleni kisha niliwasha taa, kisha nililielekea friji nikachukua maji yaย  Baridi na kuyanywa. Angalau niliusikia mwili wangu ukiwa umepoaย 

    Nilifikiria kuwagongea mlango wazazi wangu lakini niliona nitawasumbua, badala yake niliketiย  kwenye sofa. Bado taswira ya kifo cha Zena ilikua ikiendelea kunisakama.

    Nikiwa hapo nilianza kuhisi mwili wangu ukisisimka sana kama vile nilikua napandwa naย  sisimizi, kichwa kilianza kua kizito huku nikianza kuisikia sauti fulani ya ajabu. Nilisikia sautiย  ya kugonga, ilisikika ikigongwa kwa utaratibu sanaย 

    โ€œMhโ€ผ hii sauti inatokea wapi?โ€ nilijiuliza, nilisimama taratibu huku sauti ya kochi ikisikikaย  wakati nanyanyuka. Niliisikilizia vizuri ile sauti niligundua ilikua ikitokea kwenye chumbaย  kimoja pale eneo la chini.ย ย 

    Chumba hicho tulihifadhia baadhi ya vitu ambavyo hatuvitumii mara kwa mara, mfano wa stooย  hivi. Woga ulianza kunijia kisha nilianza kusikia sauti ya Mwanamke akiimba, sikujua alikuaย  akiimba nyimbo gani lakini sauti ilikua ikitoka mule mule chumbani.ย ย 

    Ilikua ni sauti laini inayoimba kwa umaridadi sana, mapigo ya moyo wangu yaliongezeka sana,ย  yalikua yakidunda kama ngoma. Hata pumzi ziliongezeka, woga ulinishika sana, mwiliย  uliendelea kusisimka kwa kasi huku nikihisi kama nina hali ya kuchanganikiwa. Nilipiga hatuaย  za taratibu sana kuelekea nilipoisikia sauti ile, korido ilikua tupu isipokua Mimi pekee.ย 

    Nilimeza funda zito la mate ili kujipa utulivu ambao kwa hali ilivyo ulihitajika sana, hatua zanguย  zilikua za kusuasua sana huku nikitembea kama Mtu nsiye na uhakika wa kufika ninapohitaji.ย  Nilizidi kutembea taratibu sana kuuelekea mlango, mara nilisikia sauti nyuma yanguย 

    โ€œCelin?โ€ ilikua ni sauti ya Mama yangu aliyeonekana kusimama kwa sekunde kadhaaย  akinitazama kwa kunishangaa, uso wake haukuwa na hofu kama wangu, jasho lilikua likinitoka. Kwa mara nyingine tena nilijiapiza kua siwezi kumweleza chochote kile Mama yangu.ย 

    โ€œMamaaโ€ผโ€ nilimwita kwa sauti ya mshituko kidogo, sikutegemea angekua akinitazama.ย  Mkononi alikua ameshikilia glasi yenye maji ya Baridi. Taratibu alisogea akionesha kuwa alikuaย  na maswali ya kuniuliza, aliponifikia aliniulizaย 

    โ€œKuna nini mbona unaonekana kama ni Mtu unayevizia Usiku huu?โ€ swali la Mama lilinifanyaย  nigundue kuwa alikua hajasikia chochote kile. Ile sauti haikusikika tenaย 

    โ€œHakuna Mama, sio kituโ€ nilisema kisha nilitaka kuondoka lakini Mama akanisimamishaย 

    โ€œKuna jambo unanificha Celin, nakujua nje na ndani, wewe ni Binti yangu ukisema ukweli najuaย  na ukisema uwongo vile vile najua. Nieleze, ulikua unavizia nini?โ€ nilimshika Mama begaย  nikamwambiaย 

    โ€œMama usijali, hakuna jambo lolote lile. Nipo sawaโ€ nilisema kisha nilipandisha ngazi nikarejeaย  chumbani, nilijuwa nyuma yangu Mama alikua na maswali mengi ambayo sikutaka kuendeleaย  kuyasikia. Nilipofika Chumbani, haraka nilichukua simu yangu na kumpigia Caren lakiniย  hakuipokeaย 

    Niliitupa simu kitandani, kisha nilisogea dirishani. Niliitazama tena nyumba ya yule Mzee,ย  niliamini alikua na majibu mengi ya maswali yangu, nilisimama kwa dakika kama tatu hivi kishaย 

    nilikata tamaa, nikataka kufunga dirisha lakini ghafla nilihisi kama kuna Mtu amesimamaย  dirishani kwenye nyumba ya yule Mzee akinitazama.ย 

    Nikishtuka sana, nyumba yake ilikua ya kawaida sio ya ghorofa. Dirisha moja lilikua likiwakaย  taa, hapo ndipo nilipomwona Mtu akinitazama. Ilionesha wazi kua alikua anajua kua nina tabiaย  ya kuichunguza nyumba hiyo, nikajificha kidogo na kuanza kuchunguza kwa siri.ย 

    Nilishtuka sana, niliyemwona akinitazama alikua ni yule Bibi niliyepanda naye kwenye Treni,ย  ndiye aliyenitamkia maneno ya ajabu na ndiye aliyempa Caren bahasha yenye karatasi yenyeย  jina la Zena. Kwa namna yoyote ndiye anayehusika na kifo cha Zena, moyo ulilipuka mithiri yaย  Volkano nikiwa nimejibanza, niliipa mgongo nyumba ya yule Mzeeย 

    Mapigo ya moyo wangu yaliongezeka kasi, nilifumba macho ili kuvuta nguvu ya kirejeaย  kumtazama tena, nilipopeleka tena macho yangu yule Bibi hakuwepo, isipokua ile taa iliyokuaย  ikiwaka kwa mwanga mkali ilikua ikiangaza.ย 

    Japo nilikua mwoga sana Maishani mwangu lakini nilipata ujasiri wa kutaka kuelewa zaidi,ย  nilipata wazo la kwenda kwenye ile nyumba. Usiku ulizidi kuwa mwingi, sikutaka Mtu yeyoteย  yule ajuwe kuwa ninatoka. Nilichukua koti langu kisha nikalivaa, nilivuta pumzi nikiwaย  nimesimama tayari kwa ajili ya kuelekea nyumbani kwa yule Mzee.ย ย 

    Simu yangu ilinidokeza kua ilikua imeshapata saa Nane kasoro za Usiku. Nilijiambia kuwaย  liwalo na liwe lakini ni lazima niujuwe mzizi wa yote, nisingeliweza kukubali kupotezaย  wapendwa wangu, nilifungua mlango taratibu huku nikiisikia sauti ya Baba yangu akikoroma.ย 

    Sikua na shaka yoyote kua alikua amelala, hofu yangu ilikua kwa Mama yangu. Nilihakikishaย  nakua makini sana, nilizichunga hatua zangu za taratibu hadi nilipofika chini, kisha nilifunguaย  mlango ambao ulinitii bila kupiga kelele zozote zile, nilipiga hatua za haraka baada ya kutoka njeย  hadi nilipoondoka ndani ya Uzio wa nyumba yetu.ย 

    Nyumba ya jirani, mbwa alikuwa akiendelea kubweka tena alibweka kwa kasi sana, sauti yaย  Bundi ilikua ikiendelea kusikika pia, ulikua ni Usiku mwingi kiasi kwamba hapakua na yeyoteย  nje isipokua Mimi na shahuku yangu. Upepo wa hapa na pale ulikua ukiendelea kuvuma taratibu,ย  ulifanya hali ya Ubaridi iongezeke.ย 

    Nilipofika nje kabisa, niliitazama nyumba yetu. Akili na nafsi yangu viliniambia haikua nyumbaย  ya kawaida, basi nilishupaza shingo yangu kuelekea nyumbani kwa yule Mzee, nilikua naย  uhakika wa kupata Majibu ya maswali yangu usiku huu. Taratibu niliendelea kupiga hatuaย 

    Nilipofika mbele ya nyumba ya yule Mzee nilisimama kwanza huku nikijiuliza mara mbili mbiliย  kama nilikua tayari kufanya nilichokua nataka kukifanya. Nilijiambia ndani yangu kwa sautiย  isiyo na mawimbi ya njeย 

    โ€œNi lazima niwe jasiri, vinginevyo naweza kupoteza kila nikipendachoโ€ ilikua ni sauti iliyojaaย  ujasiri mwingi ndani yangu. Macho yangu yaliendelea kuitazama ile nyumba kisha nilisukumaย 

    geti, halikua geti kubwa, geti dogo lililozungushiwa na uzio wa Miti fulani yenye miiba ndogoย  ndogoย 

    Urefu wa geti iliishia kifuani pangu, nilipolisukuma nilipokelewa na sauti ya Bawaba za geti hiloย  ambazo zilipiga kelele fulani ya maumivu ya kufunguliwa mithiri ya nyumba isiyo kaliwa naย  yeyote yule. Sauti hii ilinipa maswali mengi, nilichukua simu na kuwasha tochi nione kama hisiaย  zangu zilikua sahihi.ย ย 

    Macho yangu yalishuhudia kile ambacho nafsi yangu iliniambia, geti lilizungukwa na kutu,ย  Bawaba zilifichwa na kutu. Hapana shaka geti hili halikufunguliwa kwa muda mrefu, sasaย  nilijiuliza nikiwa nimesimama pale pale getini.ย 

    โ€œInawezekanaje? Ina maana walio ndani wanapitia wapi kama geti hili halifunguliwi?โ€ Lilikuaย  swali la kwanza la Msingi, bado nilikua njia panda. Sikutaka kurudi nyuma, niliazimia ni lazimaย  niichunguze nyumba pamoja na wanaoishi ndani ya hii nyumba.ย ย 

    Nilipiga hatua za kunyata, nikafanikiwa kufika mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya nyumbaย  hii. Nilipofika hapa niliwaza kidogo, jibu nililolipata ni kulielekea dirisha lile ambalo nilimwonaย  yule Bibi wa ajabu, basi taratibu nilianza kutembea kwa mwendo wa kunyata hadi nilipolifikiaย  dirisha.ย 

    Bado palikua panawaka taa, taratibu nilianza kuchungulia ndani, sikumwona yeyote yule lakiniย  mazingira yote yaliniambia kua ndani ya nyumba palikua na Mtu au Watu kama ambavyoย  nilimwona yule Bibi nikiwa chumbani kwangu.ย 

    Nilisimama hapo kwa dakika kadhaa, palikua kimya sana. Bado upepo wa taratibu ulikuaย  ukiendelea, nilipata wazo la kuuelekea mlango hivyo nilirudi hadi mlangoni. Nilisimama kwaย  sekunde kadhaa, kisha nilijaribu kutekenya kitasa cha mlangoย 

    Cha ajabu, Mlango ulifunguka kirahisi sana. Baada ya kufungua mlango niliweza kuangaza kwaย  ndani ya nyumba hiyo, nilikutana na sebule inayowaka taa kali, palikua na Kochi moja jekunduย  lililo chakaa sana, niliona sahani juu ya meza, nilimuona paka akiwa ameketi kando ya meza.ย 

    Paka huyo alikua ametulizana sana, alikua akinitazama kwa macho yake makali ya kungโ€™aa.ย  Uwepo wa Paka ilikua ni ishara nyingine kua nyumba hii inakaliwa na Mtu, paka hawezi ishiย  mahali ambapo hakuna chakula. Nilishusha pumzi zangu huku moyo ukiendelea kunigonga sana.ย 

    Bado kichwa changu kiliendelea kugonga kwa maswali yasiyo na majibu ya Uhakika, wazo laย  kuingia ndani ya nyumba hiyo lilinijia, moyo haukuacha kudunda kwa nguvu, kijashoย  chembamba kilikua kinanitoka, nilipoanza kupiga hatua niliingiwa na Ubaridi, kwa nguvu sanaย  nilivutwa nje na kuzibwa mdomo wangu kisha nikasogezwa pembeni, nikafichwa nyuma ya Uaย  moja.ย 

    Hata nilipojaribu kufurukuta sikuweza kisha nikaisikia sauti ya Caren

    โ€œShiiโ€ผ ni Mimiโ€ aliongea kwa sauti ya kunongโ€™oneza. Aliniachia, hapo hapo kabla sijamuulizaย  alifikaje, sote tulimwona Yule Mzee akiwa ameshikilia tochi, alikua akichungulia pale mlangoniย  nilipotaka kuingilia, kwa namna nilivyomwona ni kama alihisi uwepo wa Mtu. Alimulika tochi huku na kule lakini hakufanikiwa kutuona kisha aliufunga mlango wa Nyumba yake.ย 

    Hapo tuliachia pumzi ndefu maana tulikua tumezibana kuhofia asije akatushtukia.ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TATUย 

    COMMENTS ZIWE NYINGI SASAย 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx

    riwaya mpya Riwaya Nyumba Ya Majini Kijiweni riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua

    39 Comments

    1. Fau the boss on April 25, 2025 4:52 pm

      Firee๐Ÿ”ฅ

      Reply
    2. GLIMENT TWEVE on April 25, 2025 6:46 pm

      Ni nzur saana

      Reply
    3. Hank4749 on April 25, 2025 7:20 pm

      Very good https://lc.cx/xjXBQT

      Reply
      • Sospiter Paulo Samwel on April 25, 2025 11:59 pm

        It is so very good and attractive

        Reply
        • Nailaty on April 26, 2025 10:38 am

          Nasoma naogopa mwenyewe

          Reply
      • Sagent on April 27, 2025 12:44 am

        Dah n ๐Ÿ”ฅ

        Reply
    4. Piana on April 25, 2025 7:47 pm

      ๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ

      Reply
      • Karimu on April 25, 2025 10:00 pm

        Hakika ipo vyema ๐Ÿค—

        Reply
    5. Karimu on April 25, 2025 10:00 pm

      Hakika ipo vyema ๐Ÿค—

      Reply
    6. Calvin paul on April 25, 2025 10:49 pm

      Hii ni motoo

      Reply
    7. KingzJeelay on April 25, 2025 11:06 pm

      Alooooooo mambo ni๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ kaka mkubwaaa

      Reply
    8. KingzJeelay on April 25, 2025 11:08 pm

      KAKA MKUBWA EEEEE…
      TUANDALIE NA STORY ZA UJASUSI๐Ÿ’‚๐Ÿฝโ€โ™‚๏ธ๐Ÿ’‚๐Ÿฝโ€โ™‚๏ธ๐Ÿฅท๐Ÿฝ๐Ÿฅท๐Ÿฝ๐Ÿฅท๐ŸฝNAZIKUBARI MNOOOO NA NAZITAMANI SANAAAAA๐Ÿ’ช๐Ÿฝ๐Ÿ’ช๐Ÿฝ๐Ÿ’ช๐Ÿฝ๐Ÿ’ช๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ

      Reply
      • Sumaiya on April 30, 2025 5:51 pm

        Nzurii jmn lkn inanitishaaaaa mpk watu tunamalizaaa bando

        Reply
    9. Jorge2482 on April 26, 2025 5:06 am

      Awesome https://lc.cx/xjXBQT

      Reply
    10. Rebecca1468 on April 26, 2025 3:37 pm

      Very good https://short-url.org/10VGf

      Reply
    11. Hamisi halidi on April 26, 2025 6:14 pm

      Duh๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ฅ

      Reply
    12. David ben on April 26, 2025 6:43 pm

      Nzuri sana

      Reply
    13. Susana nicholas abely on April 26, 2025 7:44 pm

      .

      Reply
      • Susana nicholas abely on April 26, 2025 7:44 pm

        ๐Ÿ’ฏ

        Reply
    14. Susana nicholas abely on April 26, 2025 7:44 pm

      ase ni balaa๐Ÿ’ฏ

      Reply
    15. Jackson Wasokye Ramazani on April 26, 2025 8:10 pm

      Usiku wa manane huo Caren katokea wapi, kajuaje kama Celin yupo kwenye nyumba jirani ?

      Hii ya moto kwelikweli.

      Reply
    16. Damian170 on April 26, 2025 9:30 pm

      Good https://t.ly/tndaA

      Reply
    17. cathy on April 26, 2025 10:15 pm

      Jmn woiiiiii ya mot san

      Reply
    18. Alhaji Kising'a on April 26, 2025 11:24 pm

      Twende kazii master

      Reply
    19. Trinity921 on April 27, 2025 4:30 am

      Good https://t.ly/tndaA

      Reply
      • Brown on April 27, 2025 8:10 pm

        Type muendelezo

        Reply
    20. Leonel4053 on April 27, 2025 1:55 pm

      Awesome https://t.ly/tndaA

      Reply
    21. hottest trans porn on April 28, 2025 7:22 am

      I’m very pleased to discover this website. I want to to thank you
      for your time just for this wonderful read!! I definitely appreciated every little bit
      of it and i also have you bookmarked to check out new stuff on your site.

      Reply
    22. Frederick174 on April 28, 2025 1:38 pm

      Good https://rb.gy/4gq2o4

      Reply
    23. Cathbert on May 2, 2025 2:52 pm

      Iko poa xnaa

      Reply
    24. Laksana Petir Hk Rabu on May 7, 2025 4:57 am

      Write more, thats all I have to say. Literally, it seems as though you relied on the video to make your point.
      You clearly know what youre talking about, why waste your intelligence on just posting videos to your site when you could be giving us something
      informative to read?

      http://w1.paitowarnasgp.cfd/

      Reply
    25. Prediksi Jitu Togel Cambodia on May 25, 2025 9:00 pm

      Hmm is anyone else having problems with the pictures on this blog loading?
      I’m trying to determine if its a problem on my end or if
      it’s the blog. Any responses would be greatly appreciated.

      http://w2.prediksijitutogel.xyz/

      Reply
    26. 1WIN on August 10, 2025 12:40 am

      https://t.me/s/TgGo1WIN/21

      Reply
    27. 1Win on August 12, 2025 6:22 am

      ะžั„ะธั†ะธะฐะปัŒะฝั‹ะน Telegram ะบะฐะฝะฐะป 1win Casinะพ. ะšะฐะทะธะฝo ะธ ัั‚ะฐะฒะบะธ ะพั‚ 1ะฒะธะฝ. ะคั€ะธัะฟะธะฝั‹, ะฐะบั‚ัƒะฐะปัŒะฝะพะต ะทะตั€ะบะฐะปะพ ะพั„ะธั†ะธะฐะปัŒะฝะพะณะพ ัะฐะนั‚ะฐ 1 win. ะ ะตะณะธัั‚ั€ะธั€ัƒะนัั ะฒ ะฒะฐะฝ ะฒะธะฝ, ัะพะฒะตั€ัˆะธ ะฒั…ะพะด ะฒ ะพะดะธะฝ ะฒะธะฝ, ะฟะพะปัƒั‡ะฐะน ะฑะพะฝัƒั ะธัะฟะพะปัŒะทัƒั ะฟั€ะพะผะพะบะพะด ะธ ะฝะฐั‡ะฝะธั‚ะต ะธะณั€ะฐั‚ัŒ ะฝะฐ ั€ะตะฐะปัŒะฝั‹ะต ะดะตะฝัŒะณะธ.
      https://t.me/s/Official_1win_kanal/3651

      Reply
    28. ๐Ÿ”— โšก Quick Transfer - 1.9 BTC sent. Finalize here >> https://graph.org/GET-FREE-BITCOIN-07-23?hs=8e821f0785c1f93dd7f9a9bfd3af9b4c& ๐Ÿ”— on August 27, 2025 3:00 am

      sd7iy8

      Reply
    29. ๐Ÿ”— โš ๏ธ Verification Required: 0.6 BTC transfer blocked. Proceed now >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=8e821f0785c1f93dd7f9a9bfd3af9b4c& ๐Ÿ”— on September 12, 2025 5:18 am

      xy9m1t

      Reply
    30. ๐Ÿ““ ๐Ÿ“ฌ Unread Message - 0.45 Bitcoin from partner. Accept transfer >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=8e821f0785c1f93dd7f9a9bfd3af9b4c& ๐Ÿ““ on October 21, 2025 11:52 am

      3xj9a0

      Reply
    31. Anya149en on December 23, 2025 1:05 am

      Hello pals!
      I came across a 149 very cool resource that I think you should take a look at.
      This tool is packed with a lot of useful information that you might find insightful.
      It has everything you could possibly need, so be sure to give it a visit!
      [url=https://www.pandaancha.mx/noticias/que-hacer-solicitar-retiro-casino-en-linea.html]https://www.pandaancha.mx/noticias/que-hacer-solicitar-retiro-casino-en-linea.html[/url]

      Furthermore remember not to overlook, everyone, โ€” one always are able to within this particular piece discover responses to your the very confusing questions. We tried to explain the complete data in the most very easy-to-grasp method.

      Reply
    32. Anya149en on December 23, 2025 12:32 pm

      Hello pals!
      I came across a 149 fantastic page that I think you should check out.
      This site is packed with a lot of useful information that you might find valuable.
      It has everything you could possibly need, so be sure to give it a visit!
      [url=https://www.hockey-live.sk/news/2344-na-co-sa-zamerat-pri-stavkach-na-hokej]https://www.hockey-live.sk/news/2344-na-co-sa-zamerat-pri-stavkach-na-hokej[/url]

      And remember not to forget, folks, which one always may within this piece find solutions for the the absolute complicated queries. Our team made an effort โ€” lay out the complete content using the extremely accessible method.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    AFCON
    Africa | CAF January 1, 2026

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya michuano ya TotalEnergies CAF AFCON Morocco 2025 imekamilika…

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.