Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Saba-07)
    Hadithi

    Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Saba-07)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 1, 202518 Comments13 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nyumba Juu Ya Kaburi 06

    Nilikua nikihema, Wazazi wangu walikua wamesimama vile vile kama Watu wasiojitambua.Β  Yule Bibi aliendelea kunisogelea huku mguu wake mmoja akiwa anauburuza. Ulikua kama unaΒ  dosari ya ukilema hivi, nilikua kwenye butwaa ambayo ilihitaji Mtu anitingishe ndiyo nitokeΒ  katika ile hali tata.Β 

    Fumba na kufumbua Macho yule Bibi Kizee alikua amejaa machoni pangu akinimulika naΒ  macho yake makali, nilishtuka na kutoka katika ile hali ya Butwaa. Nilipohitaji kukimbiaΒ  alinishika mkono na kunivuta kwake lakini alipigwa na shoti kali, niliona moto mkaliΒ  uliomsukuma na kumtupa chini.Β  Endelea

    SEHEMU YA SABA

    Alinitazama kwa Mshangao kisha aliniuliza kwa sauti yake kali.Β 

    β€œWewe ni Nani?” aliongea huku akitokwa na moshi mdomoni, bado mvua ilikua ikichapa.Β  Niliuangalia mkono wangu, niliiuona ule ushanga, ndio ulionisaidia. Sasa kilichobakia kwanguΒ  kilikua ni kuokoa Uhai wangu, nilirudi nyuma nyuma tayari kukimbia, yule Jini aliwaamrishaΒ  Wazazi wangu wanifukuze.Β 

    Niliipa miguu yangu mamlaka ya kukimbia, lakini sikufikiria kwenda mbali isipokua kurudiΒ  nyumbani mara moja, nilijigonga getini eneo la mguu lakini halikuninyima mwendo, nilijivutaΒ  haraka na kukimbilia ndani kisha nilifunga mlango.Β Β 

    Nilifika ndani nikiwa nimechoka, nimelowa na pia nimetawaliwa na hofu. Haikua hali yaΒ  kawaida niwakimbie Wazazi wangu niliowapenda, radi zilikua zikipasua anga halafu sauti yaΒ  kucheka ya yule jini ilikua ikisambaa kila kona.Β 

    Nilisimama nikiwa nina bubujikwa na machozi, Wazazi wangu walikua kama mazombiΒ  yasiyoelewa Mimi ni Nani kwao, sijui aliwafanyia nini hadi wakaanza kuniwinda kiasi hiki. BasiΒ  nilikua nikiwaona Wazazi wangu kupitia kioo cha mlangoni jinsi walivyokua wamebadilika.

    Macho yao yalikuwa hayana kiini cheusi, meupe kama karatasi, walikua wakitokwa na udenda. Niliumia ndani ya moyo wangu kuwaona Wazazi wangu katika hali ile ya ajabu, walikua naΒ  nguvu za ajabu kiasi kwamba walikua wakivunja kioo waingie ndani.Β 

    Nilitamani sana kuwasihi Wazazi wangu wanitambue lakini niliona isingelikua rahisi,Β  nikapandisha ngazi huku nikisikia namna walivyokua wakivunja kioo, nilikimbia kwa spidi sanaΒ  hadi chumbani kwangu, nikawa naitafuta simu yangu ili niombe Msaada nje.Β 

    Sijui simu nilikua nimeiweka wapi, niliitafuta kila kona. Nilianza kusikia sauti ya kusukumwaΒ  kwa mlango wangu kwa nguvu, walikua wameshafika mlangoni kwangu.Β 

    Nilikua natetemeka sana maana nafsi yangu ilikosa utetezi tena. Kwa bahati nzuri niliisikia simuΒ  yangu ikiita. Sijui ni saa ngapi iliingia uvunguni mwa kitanda, niliinama, ilikua mbali kidogoΒ  hivyo ni lazima nikivute kitanda kwanza, nilijivuta nikakisukuma kitanda nikaipata simu yangu.Β Β 

    Nilikua natetemeka sana, mwili ulikua ukichuruzika maji. Mapigo yangu ya moyo yalikuaΒ  yakienda sambamba na pumzi zangu. Mate yalinikauka, kutoa nywira ya simu yangu ilinichukuaΒ  dakika nyingi kutokana na wasiwasi uliokua umenivaa. Nilishindwa hata kuifungua simu yangu,Β  mlango ulikua katika nyakati za mwisho kufunguka.Β 

    Nilidondosha simu yangu huku nikiwa nimeutolea macho mlango ukiwa unatikiswa haswa,Β  nilihisi harufu ya kifo. Taratibu nilianza kurudi nyuma nikitamani nipate msaada usiotarajiwa.Β  Hamadβ€Ό! Mlango ulifunguka, Baba na Mama yangu walikua mbele yanguΒ Β 

    Walikua katika fahamu zisizo zao, walisimama wakinitazama. Niliona huo ni muda waΒ  kuzungumza nao pengine ningeweza kuwashawishi wakarudi katika hali zao, chozi lilinitoka.Β  Sikuwahi kuwaza wala kuota kua siku moja Baba na Mama yangu wangekuwa katika hali kamaΒ  hiyo, hali ambayo wasingeliweza kunitambua Mimi binti yao wa pekee Celin.Β 

    β€œMamaβ€Ό Babaa‼” nilianza kwa sauti ya kilio cha maumivu sana, niliishiwa nguvu hata manenoΒ  niliyohitaji kuyatoa yalikua mazito kutoka mdomoni mwangu. Nilikua na maumivu makali sanaΒ  ndani yangu, udenda ulikua ukiwatoka Wazazi wangu.Β 

    β€œNi Mimi Celin, najua hamnitambui kama ambavyo ninyi hamjitambui Wazazi wangu. Mimi niΒ  Binti yenu, hampaswi kunidhuru” walikua wametulia kimya wakati naongea, nilihisi walikuaΒ  wanaanza kunisikiliza.Β 

    β€œOna, furaha yenu ni Mimi hapa, furaha yangu ni ninyi hapo. Hayo siyo Maisha yenu, sijawahiΒ  kuwaona mkiwa hivyo naomba wazazi wangu rudini katika halo zenu. Mna mengi ya kuyajuwaΒ  kuhusu hii nyumba” Nilisema, hapa sasa ndipo nilipoiona dhamira ya yule jini kwangu,Β  alichotaka ni kuhakikisha Wazazi wangu wananimaliza.Β 

    Walinifuata kwa spidi ya ajabu ili wanishambulie lakini kwa bahati nzuri niliweza kuwakwepaΒ  nikajigonga ukutani, Mama alikua kama Mbogo kwa jinsi alivyokua akitoa sauti ya hasira kamaΒ  Mnyama vile.

    β€œMama ni Mimi Celin” nilisema, angalau Baba yangu alikua hana hasira kama ambayo MamaΒ  yangu alikua nayo, alinivamia tena kunishambulia. Alinijeruhi kwa kucha ndefu, kishaΒ  nilimsukuma nikapata nafasi ya kuondoka pale chumbani, nikashusha ngazi haraka huku MamaΒ  akiendelea kunikimbiza.Β 

    Nilifika hadi chini, nilipogeuka Mama yangu alinirukia mithiri ya Ndege tai, alinidondosha chiniΒ  kama mzigo halafu akawa ananishambulia vibaya sana usoni kwa kucha, nilijitahidi sanaΒ  kupambana naye ili niinuke, nilifanikiwa kumsukuma lakini alikua amenikwaruza usoni vyaΒ  kutosha.Β Β 

    Nilisimama huku Mama akijiandaa tena kunishambulia, nilishaona kua kama sitakua ngangaliΒ  basi Mama angeweza kunimaliza, maana alinishambulia usoni bila huruma halafu alinikwanguaΒ  shingoni na kuniacha na maumivu makali sana. Nilipaswa kupambana naye bila kujali kuaΒ  hayupo katika fahamu zake.Β 

    Alikua akiunguruma kama Simba mwenye njaa, nilikimbilia jikoni lakini kabla hata sijafungaΒ  mlango aliusukuma kwa nguvu, alikua akinifuata taratibu baada ya kuingia jikoni, nilirudiΒ  nyuma nyuma nikifikiria nifanye jambo gani. Mama alinisogelea bila haraka, alijuaΒ  nisingeliweza kukimbilia popote tena. Nilifika mwisho wa jiko, nikakutakana na meza na ukutaΒ  nyuma yangu.Β 

    Upande wa kushoto palikua na kisu, nilisogea taratibu huku nikiiambia nafsi yangu kuwaΒ  nisipojiokoa sitaweza kupona, nilimpenda Mama yangu lakini aligeuka kua adui yangu. Nilipaswa kumshambulia kama alivyokua akinishambuliaΒ 

    Nilipapasa na kukishika kisu.Β 

    β€œMama, ni Mimi Celin, Mwanao hupaswi kunitendea hivi” nilisema kwa mara ya mwisho, kamaΒ  atanisikia na kuacha kunishambulia kwa maelekezo ya yule jini mbaya. Haikusaidia, MamaΒ  alikuja tena mithiri ya ndege tai ili anishambulieΒ 

    Sikujiuliza mara mbili nilipaswa kufanya nini, nilimkita kisu Cha shingo Mama yangu. KilizamaΒ  upande mmoja na kutokea upande mwingine. Mama aligugumia kwa mumivu mkali, ile hali yaΒ  ushetani ilimtoka ghafla tu akawa Yule Mama niliyempenda kisha alidondoka chini akihema kwaΒ  shida.Β 

    β€œMamaa‼” nilimwita kwa sauti iliyojaa mashaka, kisha nilikaa chini na kukipakata kichwaΒ  chake. Mama alikua akitapatapa kwa maumivu, alikua hawezi kusema chochote kutokana na kileΒ  kisu nilicho mchoma nacho.Β 

    Alianza kukosa hewa, nilikua ninalia na kumwomba msamaha Mama yangu. Baba alikuja jikoniΒ  akiwa katika hali ya kujitambua kabisa, alikua ameloa nguo zake. Alipotuona alishangaa sanaΒ  kisha alikuja haraka pale chini na kuniuliza kilichompata Mama.

    Niliishia kulia nikimtazama Mama, Baba akaniambia tumpeleke Hospitali Mama akapateΒ  huduma ya kwanza, sikuwa na chaguo isipokua kumsikiliza, sote tulikua tumechanganikiwa ilaΒ  Baba alichanganikiwa zaidi maana alionekana kutojua chochote kilichotokea. Muda huo mvuaΒ  ilikua imeacha kunyesha, palikua tulivu na wala hapakua na hali yoyote yenye kutia wasiwasi.Β 

    Baba alimbeba Mama hadi nje, bahati nzuri palikua na Taxi moja iliyokua ikipita.Β  Tuliisimamisha kisha tulimpakiza Mama, tulianza safari ya kuelekea Hospitali. Tulipofika,Β  Mama alipokelewa kama mgonjwa mahututi anayehitaji huduma haraka sana bila maelezoΒ  yoyote yale, aliingizwa chumba cha Upasuaji mara moja.Β 

    Mimi na Baba tulikaa kwenye Benchi, uso wa Baba yangu uliniambia vingi, kimojaΒ  kilichotawala zaidi ni swali la nini kilichotokea hadi Mama akawa katika hali ile, Mimi ndiyeΒ  niliyepaswa kumpa majibu Baba lakini atanielewa?Β Β 

    β€œCelin” Baba aliniita, alikua amevalia shati la Mistari myeupe na suruali nyeusi na kiatu cheusiΒ  chini. Niligeuka kumtazama maana nilikua nimejiinamia nikilia, chochote kitakachotokea basiΒ  Mimi ndiye niliyesababisha. Chozi lilikua linanivujaΒ 

    Baba alipepesa macho yake akanitazama mara moja kisha akaangalia chini na kuniuliza kwaΒ  sauti ya taratibu sana.Β 

    β€œMama yako amefikwa na nini, kile kisu Nani amemchoma?” aliuliza Baba, nilibana midomoΒ  yangu. Kila jibu nililo lifikiria kua lingekua jibu kwa Baba lingezua maswali zaidi, nilimtazamaΒ  Baba ili kusoma sura yake alikua akifikiria nini.Β 

    Kisha nilimwambia Baba β€œSijui Baba, sijui nini kimetokea. Nimemkuta Mama katika hali ile”  Nililazimika kusema uwongo, Baba alishusha pumzi ndefu. Mtu mzima yeye, alihitaji ushawishiΒ  zaidi kuamini nilikua sijui chochote kuhusu Mama.Β 

    β€œPolisi watakuja, tutawajibu hatujui?” aliniuliza. Nilizidi kudondosha chozi.Β 

    β€œBaba, niamini sijui chochote. Nilimkuta akiwa katika hali ile Mimi” nikizidi kujitetea mbele yaΒ  Baba. Chozi lilikua likinibubujika huku nafsi yangu ikinisuta. Chochote kitakachomkuta Mama,Β  wa kulaumiwa ni Mimi hapa Celin.Β 

    Basi Baba aliniegemeza kwenye bega lake ili kunipa faraja, niliendelea kulia huku tukisubiriaΒ  taarifa kutoka chumba cha Upasuaji. Tulikaa kwa zaidi ya masaa mawili, jua lilikua likikimbiaΒ  kwa kasi kuelekea kuzama, jioni ilikua imeshaingia, taa ziliwashwa kuonesha kua giza lilikuaΒ  linajiandaa kuingia.Β 

    Nilikua na uchovu wa kukimbizana huku na kule, mwili ulikua na maumivu pia nilikua naΒ  majeraha kadhaa ya kucha za Mama. Baada ya dakika kumi kupita, Daktari mmoja alitokaΒ  chumba cha Upasuaji, tulikua tunasubiria kwa muda mrefu, tuliposikia mlango ukifunguliwaΒ  tulisimama mara moja na kutazama.

    Tulipomwona Daktari tulisogea aliposimama akituangalia, alikua akitokwa na jasho, alivuaΒ  Barakoa kisha akajishika kiuno. Sura yake ilikosa tumaini, nilijikuta nikilegea mwili mzima.Β  Baba akamuulizaΒ 

    β€œHali ya mgonjwa inaendeleaje?” aliulza Baba kwa shahuku sana, yule Daktari akamtazamaΒ  Baba, akashusha pumzi kidogo akasemaΒ 

    β€œTumejitahidi sana” kisha akatikisa kichwa halafu akaendeleaΒ 

    β€œJitihada zimezidi kudra, amefariki” sauti ya yule Dakati siwezi kuisahau, yaani ndani ya wikiΒ  moja nilipoteza Watu watatu muhimu sana Maishani mwangu. Nilianza kumpoteza Zena, kishaΒ  Caren, leo nampoteza Mama yangu Mzazi tena kwa mikono yangu Mimi mwenyewe, nilianguaΒ  kilio cha Mtu mzima, nilihitaji nilie kwa uchungu tena kwa sauti kubwa kabisa.Β 

    Baba alinishikilia maana nilikua ninalia kwa kusaga meno, kilichoniliza zaidi ni kwambaΒ  Mikono yangu ndiyo iliyoondoa Uhai wa Mama yangu, nilimuuwa mwenyewe katika hali yaΒ  kujiokoa. Baba alitokwa na machozi huku akiwa ameufunga mdomo wake, aliitumia mikono yake kunibembeleza lakini haikusaidia.Β 

    Daktari akamwomesha Baba chumba kitupu ili tukakae huko kwa muda, Baba alinipeleka hukoΒ  na kufunga mlango ili nilie hadi maumivu yaishe, palikua na viti viwili. Baba aliketi na kuniachaΒ  sakafuni nilie hadi nimalize, nililia sana Mimi. Hakuna siku nililia sana kwenye Maisha yanguΒ  kama siku hii, maneno ya yule Jini Bibi kizee yalitimia, nilitambaa hadi miguuni kwa BabaΒ  nikamwambiaΒ 

    β€œNisamehe Baba” nilisema nikiwa ninalia, japo nilikua ninalia lakini niliona maumivu hayaweziΒ  kwisha kama sitasema ukweli mbele ya Baba yangu aliyekua hajui nini kilitokea, alikuaΒ  akinitazama tu.Β Β 

    β€œNisamehe Mimi Baba , ni makosa yangu” niliendelea kusema, Baba alishangaa inawezekanajeΒ  yakawa ni makosa yangu. Aliniyanyua na kuniulizaΒ 

    β€œInawezekanaje ukasema ni makosa yako Celin?” nilifuta chozi, nilihitaji ujasiri sasa kumwelezaΒ  ukweli Baba. Nilianza kusema β€œKifo cha Mama ni Makosa yangu, mikono yangu niliyoipendaΒ  imeondoa uhai wa Mtu ninayempenda” Baba alihamaki akaniuliza kwa sauti kavuΒ 

    β€œUnasemaje?” 

    β€œBaba, sikukusudia. Nimemuuwa Mama kwa bahati mbaya Mimi, nisamehe Baba Aaaah‼”  niliendelea kulia, nilimweleza Baba ukweli lakini hakuonekana kuukubali kabisa. Alinilea naΒ  kunifundisha tabia njema, akasemaΒ 

    β€œSikukuzaa Muuwaji Celin, sitaki kuyaamini maneno yako” alisema Baba kwa uchungu sanaΒ  kisha alipiga hatua za haraka na kwenda kujiinamia ukutani. Nilisikia kilio cha chinichini chaΒ  Baba na manung’uniko, nilielewa ni vita ya ndani kwa ndani ndiyo iliyokua ikiendelea kwake.

    Nilijiuliza nimwambie nini Baba yangu aniamini, nilimfuata alipo, hali ilibadilika na mimi ndiyeΒ  niliyekua namtuliza Baba baada ya Baba kunituliza MimiΒ 

    β€œBaba‼” nilimwita, alikua amejiinamia. Hakutaka nilione chozi lake kabisa. Nilimwita tenaΒ  akaniambiaΒ 

    β€œCelin, wewe siyo Muuwaji Mwanangu tena huwezi kumuuwa Mama yako Mzazi. Sitaki kusikiaΒ  hizo hadithi, niambie nini kimemkuta Mama yako?” alisema Baba akiwa ameuficha uso wakeΒ  ukutani, macho yangu yalikua hayakauki chozi hata kidogo, niliendelea kububujisha choziΒ Β 

    β€œBaba, Mwanao nimepitia Mazingira magumu sana tena kwa siri msijue nyinyi” nilisema, kilioΒ  kilianza upya. Baba aligeuka kunitazama. Macho yake yalikua yamejawa na chozi, alihitajiΒ  kusikia nilichotaka kukisema. Nilimtazama.Β 

    β€œChanzo cha yote ni ile nyumba Baba, ina majini na kaburi ambalo ndugu wawili wamezikwaΒ  mle. Hakuna aliyeweza kuishi ndani ya ile nyumba salama, hata kifo cha Mama ni matokeo yaΒ  usiri wangu” Nilisema jambo ambalo lilimfanya Baba ashangae sanaΒ 

    β€œUmetoa wapi hayo unayoyasema Celin?” aliniuliza Baba kwa Mshangao mkubwa sana, nilifutaΒ  chozi langu nikaivaa roho ya Ujasiri ili nimsimulie Baba kila kitu. Nilimsimulia kila hatua, kilaΒ  jambo. Hadi namaliza kumweleza Baba alikua ameketi kitini akinitazama kwa uzito sana. SuraΒ  ya majonzi ilimtawala Baba yanguΒ 

    β€œKwanini ulificha jambo kubwa namna hiyo Celin, siri yako imeharibu Maisha yetu, siri yakoΒ  imeondoa uhai wa Mama yako Celin” alinilaumu Baba, nilikua tayari kupokea lawama zoteΒ  maana tayari maji yalinifika shingoni, nilikua naangamia.Β 

    β€œUnafikiria Polisi wataelewa haya?” aliniuliza Baba, tayari kitengo cha Polisi kilipokea taarifaΒ  ya shambulio la Mama yangu. Walikua wameshafika, mlango ulikua ukigongwaΒ 

    Baba alinisogelea akaniambiaΒ 

    β€œKama unaweza kumaliza kila kitu basi maliza Celin” alisema, kabla hata sijamjibu chochote Baba alielekea mlangoni na kufungua mlango, polisi walikua wamesimama mlangoni.Β 

    Baba aligeuka na kunitazama kisha alinipa ishara ya tumaini kwa kuniachia tabasamu.Β 

    β€œSisi ni maafisa wa Polisi, tunahitaji kuondoka na ninyi kwa ajili ya mahojiano” alisema PolisiΒ  mmoja, Baba akasemaΒ 

    β€œHaina haja ya kuondoka na sisi, peke yangu nitathibitisha kila kitu. Binti yangu hakuwepo eneoΒ  la tukio” alisema Baba, kauli yake ya ghafla ilionesha kua alikua ameubeba msalaba wangu.Β  Polisi walinitazama kwa sekunde kadhaa huku nikiwa mwoga maana Mimi ndiye Muuwaji,Β  kisha waliondoka na Baba yangu. Nililia sana, sikuwa na Mtu karibu yangu wa kuniambiaΒ  maneno ya faraja.

    Mama yangu alikua amefariki, Baba alikua mikononi mwa Polisi kwa makosa yangu Mimi. Nilijiinamia baada ya kulia kwa muda mrefu, baadaye nilitoka kwenye kile chumba. NilipataΒ  Ujasiri wa kuuliza namna ya kuipata Maiti ya Mama kwa ajili ya Maziko. Utaratibu ulikua niΒ  lazima tulipie pesa kidogo ndipo watupatie maiti, sikua na pesa nilimwambia Daktari natakiwaΒ  kurudi nyumbani kuchukua pesa. Akaniangalia kisha akaniambiaΒ 

    β€œUsijali Msichana, tayari maiti imelipiwa” nilishangaa sana, ni Nani anayeweza kuilipia maiti yaΒ  Mama yangu ili itoke Hospitalini. Nilimtazama kwa Mshangao halafu nikamuulizaΒ 

    β€œHivi nimekusikia ipasavyo?”  

    β€œNdiyo, Mjomba wako amelipia” alipomaliza kusema nikamwona Mjomba Mgina akiwaΒ  anakuja tulipokua tumesimama na Daktari. Huzuni iliniingia Upya kabisa, nilimkimbiliaΒ  Mjomba na Kumkumbatia kwa Uchungu sana.Β 

    β€œPole Celin, pole sana Mjomba” alisema huku akinipiga piga taratibu mgongoni katika hali yaΒ  kunipoza machungu. Chozi lilinibubujika tena, kwakua tayari nilikua nimemueleza kila kituΒ  Baba yangu sikutaka kuleta tena Mkanganyiko.Β 

    β€œInaniuma Mjomba, Mama amekufa kikatili sana” nilisema, maumivu yaliyokua yamejaaΒ  moyoni mwangu yalikua yakinichoma mithiri ya sidano.Β 

    Basi, tuliitoa Maiti Hospitalini na kuipeleka nyumbani kwa Mjomba Mgina. Palitawala MajonziΒ  na vilio, maswali yasiyo na Majibu. Uvumi kua Baba yangu alikua amemuuwa Mama yanguΒ  ulianza kusambaa miongoni mwa waombolezaji, kila Mtu alimwita jina baya Baba yangu.Β 

    Nilizidi kuumia ndani ya Nafsi yangu, Baba yangu aliitwa Muuwaji kwa sababu ya kunisaidiaΒ  Mimi. Alijivesha ngozi yangu kunificha Muuwaji halisi, nililia kwa mambo mengi yasiyo naΒ  Majibu. Macho yalinivimba, kesho yake tulimzika Mama kwenye Makaburi ya Jiji.Β 

    Hatimaye Mama yangu aliungana na Zena na Caren kwenye makazi ya milele. KilichokuaΒ  kimebakia kwangu kilikua fumbo kubwa, hakuna aliyejua kuhusu ile nyumba yenye kaburi naΒ  jini anayeuwa.Β 

    Sikutaka kumwambia yeyote, moyo wangu ulijawa na kisasi. Sikuuona umuhimu wa kuendeleaΒ  kuishi ikiwa nimepoteza Wapendwa wangu kwa usiri wangu. Baba alifikishwa Mahakamani sikuΒ  Nne baada ya kumzika Mama, alikiri mbele ya Mahakama kua alitenda Mauwaji hayo kwaΒ  mikono yake kwa kile alichokiita wivu wa Mapenzi.Β 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya NANE

    COMMENTS ZIWE NYINGI SASAΒ 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx

    riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia

    18 Comments

    1. Alfred1573 on May 1, 2025 7:40 am

      Good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    2. Jocelyn832 on May 1, 2025 7:42 am

      Awesome https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    3. Fred3290 on May 1, 2025 10:30 am

      Good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    4. Deborah3133 on May 1, 2025 2:29 pm

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
      • Sumaiya on May 1, 2025 8:07 pm

        Aisee admin story timu kinomaaaaaa shusaa ya 8

        Reply
      • bayser on May 3, 2025 3:36 pm

        ishiii mbna marudioo mzee

        Reply
    5. Nassor on May 1, 2025 4:55 pm

      Admin mm ndy wa kwanza hii st0ry ip0 0n πŸ”₯ asee

      Reply
    6. Ayla4434 on May 1, 2025 5:35 pm

      Good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    7. Sumaiya on May 1, 2025 8:06 pm

      Aisee story timu admin yaan leta ya 8

      Reply
    8. David ben on May 2, 2025 11:01 pm

      Tunasubiri sehemu ya 8

      Reply
    9. Salma on May 3, 2025 2:25 pm

      Marudio hii admin

      Reply
      • Salma on May 3, 2025 2:27 pm

        Marudio hii umetufowadia ya tarehe 1 .

        Reply
      • bayser on May 3, 2025 3:36 pm

        ishiii mbna marudioo mzee

        Reply
    10. Neema Tesha on May 3, 2025 3:03 pm

      Story ni πŸ”₯πŸ”₯ sanaa,,tupe ya 8 bhas

      Reply
    11. Rqy on May 4, 2025 3:24 pm

      Admin umenikamata aiseee story tamuuu

      Reply
    12. Justin Peter on May 16, 2025 10:35 pm

      πŸ”₯

      Reply
    13. Paul kahabi on May 20, 2025 10:41 am

      Naomba group

      Reply
    14. πŸ“ˆ πŸ’Ή Portfolio Alert: +0.6 BTC detected. Check now β†’ https://graph.org/GRAB-FREE-BTC-07-23?hs=0d2a36e1f29972421efc3620030dbb7c& πŸ“ˆ on July 27, 2025 10:57 am

      yp2bmc

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane β€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.