Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Pili-02)
    Hadithi

    Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Pili-02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaApril 24, 2025Updated:April 27, 202542 Comments9 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nyumba Juu Ya Kaburi

    Caren alisimama baada ya kuniona simjibu alichokua akinisemesha, nilianza kuhema kwa kasi,ย  hofu ilikua imenitawala vya kutosha.ย 

    โ€œKuna nini Celin?โ€ aliniuliza, nilimjibu Caren kwa sauti ya chini iliyojaa hofu na mtetemo waย  Uwoga uliopitiliza.ย 

    โ€œKuna Mtu nyuma yetuโ€ Nilitamani kulia kwa jinsi woga ulivyokua umenishika, Caren aligeukaย  nyuma kisha akarejesha macho kwangu. Akaangua kicheko na kuanza kuongea kama mlevi . Endelea

    SEHEMU YA PILI

    โ€œKumbe umekunywa pombe Celin, Ha!ha! Hakuna Mtu. Ulisema hautumii pombe mbonaย  umelewa ha!ha!ha!โ€ Haraka niligeuka nyuma, hapakua na yeyote yule, lakini hisia yangu yaย  ndani iliniambia yule Mzee analifahamu jambo fulani kuhusu nyumba yetu. Nilitabasamu ili tuย  kumfanya Caren aamini kua nilikua nimelewa kidogo.ย 

    Tuliporudi ndani tulikuta Watu wakiendelea na tafrija hiyo fupi, baadaye mishale kama ya saaย  tano hivi walitawanyika na kutuacha Wana Familia pekee, Mimi, Baba na Mama. Kwakua Usikuย  ulikua mwingi, Baba akatuambia tukalale, asubuhi tutafanya kazi ya kuweka mazingira sawa.ย  Mimi niliingia chumbani kwangu, chumba changu kilikua juu.ย 

    Baada ya kuingia chumbani nilijikuta nikiendelea kufikiria hatua za yule Mzee, bahati nzuriย  dirisha langu lilikua likiitazama vizuri nyumba ya yule Mzee, nilisogea taratibu hadi dirishaniย  kisha nilichungulia, palikua kimya sana. Hapakua na dalili ya Mtu yeyote yule, nilisimama hapoย  kwa zaidi ya dakika kumi lakini sikuambulia chochote kile.ย 

    Nilikata shauri nikaingia bafuni kuoga kisha nilipomaliza nilirudi kitandani na kupumzika. ***ย 

    Nilichokiona, nilichokihisi kilibakia ndani yangu. Sikupenda kuwaingiza wazazi wangu kwenyeย  presha ya aina yoyote ile, kama ukweli nitautafuta mwenyewe.ย 

    Siku iliyofuata ilianza kwa baridi kali sana, nilipaswa kuelekea chuoni. Nilijiandaa, baada yaย  dakika kama kumi nilikua tayari kwa ajili ya kuondoka na kuelekea chuoni.ย 

    Niliwaaga wazazi wangu kisha niliondoka. Nilipofika nje nilipata wazo la kubadilisha njia,ย  niligeuka na kuelekea upande wa nyumba ya yule Mzee, mara zote nyumba yake ipo kimya.ย  Hapasikiki sauti ya aina yoyote ile, nilipiga hatua zangu za taratibu nikiwa nimevalia viatu virefuย  kama buti hivi, suruali nyeusi na shati jekundu kisha koti la kunikinga na baridi.ย 

    Nafsi yangu ilizidi kuniambia kua kuna jambo napaswa kulijua kuhusu nyumba yetu mpya, Mtuย  pekee ambaye alionesha hisia ya kujua jambo alikua ni huyu Mzee wa ajabu. Basi, nilipofikaย  aneo la geti lake niliona pameandikwa โ€˜Mwanzo wa Mwishoโ€™ย ย 

    โ€œMwanzo wa Mwisho?โ€ niliyarudia maandishi yaliyopo getini, nilihema. Yalikua ni manenoย  magumu kiasi kwamba sikuelewa chochote kile, hisia mbaya dhidi ya huyu Mzee ilichipua zaidiย  ndani yangu. Wakati huo jua lilikua likianza kuchomoza kwa mbali, palikua na mwanga waย  kutosha, upepo wa hapa na pale.ย 

    Niligeuka kuangalia nyumbani kwetu, kisha nilitazama tena pale getini, sikupata tafsiri ya harakaย  haraka juu ya yale maneno. Nilimeza funda zito la mate, nilitazama saa yangu, ilisoma ni saaย  2:13 Asubuhi.ย 

    Niliona bado nina muda wa kutosha kabla ya kuelekea chuoni pengine naweza kuzungumza naย  yule Mzee angalau nipate ufumbuzi wa maswali magumu yaliyojaa kichwani pangu. Nilisita-sitaย  lakini niliweza kugonga geti

    Palikua kimya sana kama sehemu isiyotembelewa na Mtu kabisa. Niligonga tena, nikagongaย  zaidi kwa kutumia mkono wangu wa kushoto huku nikisemaย 

    โ€œKuna yeyote?โ€ nilikua makini sikutaka wazazi wangu wajue chochote kile, palikua kimya sana.ย  Nilikata tamaa, sikuona dalili ya kufunguliwa Geti hilo dogo. Nililipa mgongo lile geti kishaย  niliondoka hapo, nikasogea Barabara kuu nikapanda treni iliyokua ikielekea katikati ya Jiji, hukoย  ndiko nilikokua ninasoma.ย 

    Niliketi siti namba 25, kando yangu alikuwepo Bibi mmoja. Nilimsalimu kwa heshima sana,ย  baada ya treni kuondoka aliniulizaย 

    โ€œKuna jambo linakutatiza?โ€ sijui aliweza vipi kujua kua nilikua natatizwa na jambo fulani,ย  niliachia tabasamu kiasi ili kumjibu yule Bibi.ย ย 

    โ€œKiasi, hata hivyo ni jambo la kawaidaโ€ nilimjibu, hakusema chochote. Alikaa kimya namiย  nilikaa kimya nikisubiria kusikia angesema nini lakini aliendelea kukaa kimya. Dakika kamaย  kumi hivi, yule Bibi akaniambiaย 

    โ€œNashuka kituo kinachofuata, kua makini sana Mjukuu wangu. Unakaribia kupoteza Watuย  uwapendao kwa mpigo, kua jasiri. Wakati mwingine Maisha yanatupeleka shimoni makusudiโ€ย  Moyo wangu ulilipuka mithiri ya Volkano, simjui yule Bibi. Aliwezaje kuongea maneno mazitoย  kiasi kile, Watu niliowapenda sana walikua ni Wazazi wanguย 

    โ€œSamahani unasemaje?โ€ nilimkujia sura yangu, aliachia tabasamu tu akaniambiaย 

    โ€œHuwezi kuwaokoa, Hatma imewafikiaโ€ maneno yake yalikua mazito sana, kiasi kwambaย  yalinifanya nilegee mwili mzima. Nilihisi ganzi moyoni mwangu, huzuni na hisia ya hasira.ย  Nikiwa ninaendelea kuyarudia maneno yake, mara treni ilikua imefika kituoni, yule Bibiย  alishuka kisha alisimama akinipungia mkono wa kuniaga.ย 

    Moyo uliniuma sana, hata safari yangu ya kuelekea chuoni niliiona kua ilikua nzito sana. Hapoย  hapo nikaitoa simu yangu kwenye begi nikampigia Mama yangu kumuuliza kama walikuaย  salama. Mama alinitoa hofu, hata sauti yake ilionesha palikua shwari kabisa.ย 

    Pumzi niliyoishusha ilikua kubwa, ilishuka kama gia ya gari. Kifua kilikua kizito, presha siyoย  presha, yale maneno yalikua yanazidi kunipigia kelele masikioni mwangu. Ndani ya siku mbiliย  nilikutana na mauzauza ya kutisha, nilipiga moyo konde nikiamini hakuna anayeweza kuijuaย  hatma ya Mtu mwingine isipokua Mungu pekee.ย 

    Nilipofika chuoni, nilikua na maswali mengi kichwani. Nilijiinamia kwenye meza, nilihisi kamaย  nilikua nimebeba mzigo mzito sana kichwani mwangu. Nikiwa hapo alikuja Caren, akanifanyiaย  utani ambao haukua kipaumbele kwanguย 

    โ€œUna shida gani Celin?โ€ aliniuliza, niliweka mikono yangu usoni, nilitamani kumueleza Carenย  lakini sikupata ujasiri wa kufanya hivyo.ย 

    โ€œCelin, niambie una tatizo gani?โ€ aliniuliza tena, bado nilikua kimya nikimwangalia.ย 

    โ€œJana usiku ulikua hivi, unanificha kitu. Hata hivyo nimepewa hii barua nikupatieโ€ Nilishtukaย  kidogoย 

    โ€œImetoka wapi?โ€ย ย 

    โ€œNimepewa na Bibi mmoja hapo nje amesema nikupatie weweโ€ Nilishtuka sana, niliogopa kishaย  nilikimbilia nje ya geti la chuo, nilitazama huku na kule kama ningemwoma huyo Bibi, nilikuaย  na uhakika huwenda ni yule Bibi niliyekutana naye kwenye Treni muda mchache uliopita. Maraย  Caren alifikaย 

    โ€œSikuelewi Celin, kuna nini?โ€ aliniuliza, nilimsogelea nikiwa nina hisia ya hofu na Mashakaย  makubwa.ย 

    โ€œYupoje?โ€ย 

    โ€œMwembamba, amevaa koti la suti lililochakaa. Gauni la bluu, halafu amevalia raba chiniโ€ sifaย  alizozitaja Caren zilifanana na sifa za yule Bibi niliyekutana naye kwenye treni.ย 

    โ€œCaren kuna kitu hakipo sawa, nilikutana na huyo Bibi kwenye treni. Ameongea maneno yaย  kutisha sana, nipe hiyo Baruaโ€ Haraka Caren alinipatia Barua kisha niliifungua haraka,ย  nilikutana na karatasi nyeupe iliyoandikwa jina moja โ€˜ZENAโ€™ย 

    โ€œZenaโ€ nilisema kwa hofu, nilirudi nyuma nyuma nikiwa nina hofu hadi pale nilipofika mwishoย  nikakutana na ukuta wa uzio wa chuo, Caren alisogea naye akiwa kwenye Mshangao mkubwaย  sana. Jina la Zena liliandikwa kwa herufi kubwa na wino mwekundu. Chozi lilikua linanitokaย  huku ile kauli kua nitapoteza niwapendao kwa Mpigo ilikua ikijirudia akilini mwangu.ย 

    Zena ni rafiki yetu, tokea nimefika chuo sikumwona. Nikamuuliza Carenย 

    โ€œUmemwona popote?โ€ย 

    โ€œNani?โ€ย 

    โ€œZenaโ€ย 

    โ€œHapana, nilijaribu kumpigia nilipofika chuo lakini simu yake ilikua ikiita tu. Hebu niweke waziย  kuna nini?โ€ Caren aliniuliza kwa hofu huku akiweka mikono yake kichwake pake, alikua njiaย  panda nami sikua na muda wa kumweleza zaidi.ย 

    โ€œTwende kwake Caren, tafadhali twendeโ€ nilisema huku chozi likizidi kunibubujika. Nilikua naย  uchungu moyoni mwangu, nilianza kuwa na wasiwasi kua kuna jambo lililomfika zena. Manenoย  ya yule Bibi yalizidi kujirudia akilini mwangu. Nilisimamisha Taxi haraka, tuliingia kwenye Taxiย  huku Caren akinilazimisha niseme kinachoendelea, nilikua ninalia tu.

    โ€œSasa Celin, usiposema nitajua nini. Yule Bibi ni Nani yako, kwanini amekutumia Barua yenyeย  jina la Zena?โ€ aliniuliza Caren alikua amejawa na hofu, wasiwasi kwa pamoja. Niligeukaย  kumtazama huku chozi likinibubujikaย ย 

    โ€œSali, lisimfike lolote. Dunia inanigeuka Carenโ€ nilisema kwa Uchungu, sikuweza kuongeaย  zaidi. Nilihisi uzito uliopitiliza, nilihisi kuchanganikiwa huku sura na maneno ya yule Bibi kizeeย  yakizidi kuendelea kutembea kichwani kwangu.ย ย 

    Zena alikua anaishi kilomita chache kutoka pale chuoni, wastani wa nusu saa tulikuaย  tumeshafika mahali alipokua amepanga. Niligonga geti kwa nguvu kisha tulisubiria kwa sekundeย  kadhaa kisha geti lilifunguliwa na Mama mwenye nyumba.ย 

    Alionesha tabasamu mbele yetu sababu alikua akitufahamu, tulikua tukienda hapo mara kwaย  mara lakini safari hii hakuna aliyerudisha tabasamu. Tulimpita kama wanariadha wa mbio ndefuย  za Marathon, breki tulifunga mlangoni kwa Zenaย 

    Tulisimama kwa sekunde kadhaa za kuhesabu, mlango ulionekana kua wazi sababu palikua naย  upenyo mdogo. Tulitazamana, sura ya Caren ilijaa maswali mengi yasiyo na Majibu, sikuwezaย  kumweleza chochote kile hadi muda huo.ย 

    Nilipopiga hatua kuusogelea mlango, Caren alinishika mkono akaniulizaย 

    โ€œNini kinaendelea Celin?โ€ Alianza kuniuliza kwa sauti ya chini iliyojaa kilio cha hisia kali yaย  hofu na woga kwa pamoja. Ni kama Caren alikua amenielewa, nilitikisa kichwa kumdhihirishiaย  kua Zena alikua shidani. Chozi lilikua likitububujika, nyuma yetu alifika Mama mwenye nyumbaย 

    โ€œMabinti, kuna nini?โ€ aliuliza yule Mama Mtu mzima, ndiye mmiliki wa nyumba ambayo Zenaย  alikua amepanga kwa ajili ya masomo ya Chuo. Niligeuka kumtazama huku chozi likinibubujika,ย  naye Mama akautazama Mlango wa Zena, akiwa kama Mtu mzima alikua ameelewa kua Zenaย  alikua matatizoni na pengine alikua ameshakufa.ย ย 

    Macho yake pia yalimlenga kwa Mchozi. Nilielekeza macho yangu mbele kisha niliufunguaย  mlango taratibu, nikautosa mguu wangu ndani ya chumba, nilichokiona kilinifanya nipige yoweย  kali la kuchanganikiwa.ย 

    Kila mmoja wetu aliingia kushuhudia kile ambacho macho yangu yalikuwa shuhuda wa kwanza.ย  Zena alikua akiningโ€™inia kwenye kitanzi cha Khanga kilichofungwa kwenye feni, alikuaย  akizungushwa huku na kule kama Mzigo usio na thamani tena, ama kweli utu wa Mtu ni uhaiย  wakeย 

    Zena alikua amekufa muda mrefu sana, binafsi nililia kwa uchungu sana. Mama mwenyeย  nyumba akakimbilia kumwita Mjumbe na mwenyekiti wa Mtaa. Bila hata kutumia vipimoย  walithibitisha kifo cha Zena, rafiki aliyenipokea chuoni na kunifundisha Maisha ya Chuo jinsiย  yalivyo.

    Tulipishana Mwaka mmoja wa kuingia chuoni, alinitendea wema kila nyakati. Hata wakatiย  ambao alipaswa kufurahi alinipa furaha yake na kisha yeye alibakiwa na huzuni yangu.ย  Nilimwona akiwa anafunguliwa kutoka juu ya feni akiwa amevalia gauni lake jekundu.ย 

    Hakika maneno ya yule Bibi yalianza kutimia, nilimpoteza mmoja nimpendaye. Nilijiegemezaย  ukutani nikilia kwa kwikwi nikiushuhudia mwili wa Zena ukiondolewa na Askari Polisiย  waliokua hapo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Mtaa.ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TATUย 

    COMMENTS ZIWE NYINGI SASAย 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx

    riwaya mpya Riwaya Nyumba Ya Majini Kijiweni Riwaya Ya Kisasi Changu riwaya ya koti jeusi riwaya za bure riwaya za kijasusi

    42 Comments

    1. Jeannette4357 on April 24, 2025 7:05 am

      Very good https://shorturl.at/2breu

      Reply
      • Atiya on April 24, 2025 7:35 pm

        Mh atali

        Reply
    2. Wasokye Ramazani on April 24, 2025 10:17 am

      Mmmm, hii noma, hachia kipande kingine tuone nani anafata kufa baada ya ZENA, Hooo Zena R.I.P !!!

      Reply
    3. Neema gervas on April 24, 2025 4:03 pm

      Hatari๐Ÿ’๐Ÿ’

      Reply
      • Aura on April 24, 2025 7:49 pm

        Daah ๐Ÿ˜ž๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ zena R.I.P who is next ๐Ÿฅบ
        Achia nyingine kijiweni tupo pamoja

        Reply
    4. Rio on April 24, 2025 7:09 pm

      Daah hii kalii

      Reply
    5. alle on April 24, 2025 7:11 pm

      imeanxa kaa story naona imeanza kugeuka kua zile hallowin movieza wazungu ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

      Reply
      • Aura on April 24, 2025 7:50 pm

        Daah ๐Ÿ˜ž๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ zena R.I.P who is next ๐Ÿฅบ
        Achia nyingine kijiweni tupo pamoja km

        Reply
        • Alvin audax on April 24, 2025 8:10 pm

          Daah!bonge la storry

          Reply
      • Salama on April 26, 2025 12:23 pm

        โค๏ธ

        Reply
    6. Manka on April 24, 2025 7:33 pm

      Ooh I can’t wait

      Reply
    7. Manka on April 24, 2025 7:34 pm

      OMG ๐Ÿ˜ณ

      Reply
    8. Aura on April 24, 2025 7:46 pm

      Daah ๐Ÿ˜ž๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ zena R.I.P who is next ๐Ÿฅบ
      Achia nyingine kijiweni tupo pamoja

      Reply
    9. Zoulovie_store on April 24, 2025 8:17 pm

      Duuuuh

      Reply
    10. Yuster on April 24, 2025 9:46 pm

      Dunia inamgeuka Celin

      Reply
    11. Karimu on April 24, 2025 10:14 pm

      Aah hakika ipo vyema๐Ÿค—

      Reply
    12. ร‡lรฃssรฏรงjr_10 on April 24, 2025 10:25 pm

      Kama muvi flani ivi ๐Ÿ˜‚
      Dondosha cha tatu

      Reply
      • Abdallah Tenge on April 25, 2025 8:02 pm

        Duuuu

        Reply
    13. Alhaji Kising'a on April 25, 2025 12:34 am

      Hakika utu wa mtu ni uhai wake.

      Reply
      • Abdallah Tenge on April 25, 2025 8:04 pm

        Ntakutafuta mkuu tuandae bajeti tufanye movie hii story

        Reply
    14. KingzJeelay on April 25, 2025 5:12 am

      Mwanzoni nilihofia nikajua ni wazaz wakeโค๏ธโ€๐Ÿ”ฅโค๏ธโ€๐Ÿ”ฅ
      Anewei RIP Kwa Zena na pole Kwa Celin..
      Mola ampe ujasiri kwakwel.๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿ™„๐Ÿ™„

      Reply
    15. Crystal859 on April 25, 2025 5:34 am

      Good https://lc.cx/xjXBQT

      Reply
    16. Astery Komba on April 25, 2025 8:11 am

      hii nimeikubali

      Reply
    17. sara g on April 25, 2025 11:31 am

      Nomaah san jmn R.I.P zenaa joomn

      Reply
    18. Posiano on April 25, 2025 4:20 pm

      Nimeipenda iko vizur sana mkuu

      Reply
      • Ole mbuzi on April 25, 2025 5:21 pm

        Amini hiki chuma

        Reply
        • Sumaiya on April 30, 2025 5:45 pm

          Jamn inatishaaaa km tamthiliya vile mmh kweli maisha ni uhai

          Reply
          • Justin Peter on April 30, 2025 11:27 pm

            Halafu mm naisoma usiku ๐Ÿฅท

            Reply
    19. Ole mbuzi on April 25, 2025 5:20 pm

      Aah hii riwaya ni nzuri sana ina mafunzo makubwa sana ndani yake.

      Reply
    20. Hamisi halidi on April 25, 2025 6:42 pm

      Mbona inaogopesha

      Reply
    21. G shirima on April 26, 2025 8:09 pm

      Kwani ufalime wa zombie imeishia wap

      Reply
    22. Anastasia1774 on April 29, 2025 12:50 pm

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    23. Warren1037 on April 29, 2025 2:26 pm

      Awesome https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    24. Greyson4045 on April 29, 2025 8:02 pm

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    25. Marc874 on April 30, 2025 3:15 am

      Good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    26. Omar4331 on April 30, 2025 7:08 pm

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    27. Justin Peter on April 30, 2025 11:25 pm

      ๐Ÿค”๐Ÿ™†

      Reply
    28. Emily1797 on May 1, 2025 12:33 am

      Awesome https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    29. Cathbert on May 1, 2025 10:20 am

      Nyumba ya kununua sio mzuri sana
      Bora ukajenge ya kwako tu..

      Reply
    30. Terrence1625 on May 1, 2025 10:30 am

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    31. Marley1596 on May 1, 2025 2:30 pm

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    32. Emanuely Daudy on May 5, 2025 11:18 pm

      Iko powa sana tatu please

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.