Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Daktari Simba: Msiwaze! Aishi Manula atakua fiti
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Daktari Simba: Msiwaze! Aishi Manula atakua fiti

    David MohamedBy David MohamedJune 2, 2023No Comments1 Min Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Daktari Mkuu wa Simba, Edwin Kagabo ameshusha presha kwa mashabiki wa timu hiyo kuhusiana na hali ya kipa, Aishi Manula aliyeko nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ya nyama za paja.

    Kipa huyo na daktari huyo wapo Afrika Kusini, baada ya Uongozi wa Simba kufanya maamuzi hayo ya haraka kwa kuhakikisha anakuwa fiti ili aweze kurejea uwanjani kabla ya msimu ujao kuanza tena.

    “Niwatoe hofu kuhusu Aishi Manula kwamba atarejea uwanjani kucheza haraka iwezekanavyo ingawa siwezi kusema wazi ni kwa muda gani, kikubwa mashabiki waendelee kumuombea ili apone vizuri,” alisema.

    Aishi Manula, Golikipa Simba SC

    Aidha Kagabo aliongeza anaamini matibabu hayo yataleta manufaa makubwa kwa Manula kwani malengo yao ni kumuona mchezaji huyo akirejea kucheza haraka kutokana na umuhimu wake kikosini na hata timu ya taifa.

    Majeraha hayo yamemfanya kukosa michezo saba mfululizo tangu alipoumia katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Ihefu FC uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Aprili 7.

    Kuumia kwa Manula imetoa fursa kwa kipa namba tatu, Ally Salim kupata nafasi ya kuanza golini mbele ya Beno Kakolanya katika michezo mbalimbali ikiwemo ya Ligi Kuu Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Endelea kutufatilia zaidi hapa.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.