Ilipoishia “Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.ย
โKunywa Majiโ alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikuaย ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuulizaย
โMnanimalizia lini nikapumzike?โ Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chacheย nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambiaย
โKifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwajeโ alisema kisha akanipa maji, sikuwaย na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe hai. Endeleaย
SEHEMU YA NANE
Niliyafakamia yale maji kwanza hadi yalinipalia, halafu nikahema. Akanitolea vidonge vyaย kunituliza maumivu. Sikusita kumeza kiukweli maana nilikua na maumivu makali sana kishaย nilimshika mkono nikamuulizaย
โNingekuwa mdogo wako ungenifanyia hivi, unajua najisikiaje Kaka?โโ Chozi lilikuaย linanibubujika bila kuacha, akaniondoa mkono wangu kwa kutumia mkono wake mwingineย kisha akasimama, akaniambiaย
โKula upate nguvuโ hakuzungumza tena, alisimama kisha alipiga hatua lakini alipofika mlangoniย alisimama. Kama kuna kitu alitaka kuniambia lakini alighaili, hakujibu swali langu aliondoka naย kuufunga mlango kwa funguo, unajua hata kama angeuacha wazi sikuwa na nguvu ya kukimbiaย kwa namna nilivyokua sina nguvu.ย ย
Nilisikia akiondoka, nililia sana Mimi. Hakuna siku inapita bila kudondosha chozi langu,ย nilimpoteza Kaka Hamidu na nilijiona ni mkosaji, nilijilaumu sababu bila kuolewa na Saleheย basi Kaka Hamidu angekuwa hai hadi sasa. Kidogo zile dawa zilipunguza maumivu ya mwiliย lakini siyo maumivu ya Moyo wanguย ย
Haikuchukua hata dakika nyingi nilisikia yowe la Mwanaume mmoja, yowe lile lilisikika mojaย kwa moja kutoka kwenye ile nyumba niliyohifadhiwa Mimi. Moyo ulinilipuka, niliamini ilikuaย ni nyumba ya Mateso makali zaidi hata nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Nilisimama hataย nguvu sikujuwa ilitokea wapiย
Nilisogea mlangoni ili kuisikia zaidi ile sauti, ndiyo! Ilitoka ndani ya moja ya vyumba vya ileย nyumba, nilitamani kupaza sauti ila sikujua alikua akifanywa nini. Nilijiuliza
โNani yupo ndani ya hii nyumba, anamfanya nini huyu anayepiga yoweโ Ilikua ni sawa naย kujitekenya kisha kucheka mwenyewe, jibu lingetokea wapi ikiwa hata mimi mwenyewe sijuiย nipo wapiย
Yule Mwanaume baada ya kupiga yowe alianza kusemaย
โMsaada,Nani yupo ananisikia?โ aliendelea kusema hivi, nikapata picha huwenda hata yeyeย mwenyewe hajui amefikaje na Nani amemleta ndani ya hii nyumba. Kupitia dirishani nilianzaย kuona jua namna lilivyokuwa likifanya safari ya kwenda kupumzika baada ya kuipiga ardhi kwaย siku nzima.ย
Namna nyumba hii ilivyo ilionekana kujengwa kwa ajili ya kazi ya kuhifadhi Binadamu, hataย dirisha lake lilikua kama la Mahabusu, lilikua dogo lanye nondo,hapakuwa na taa ndani yaย chumba kiasi kwamba giza litakapoingia basi patakuwa giza tupu. Nilijikuta nikikaa mwenyeweย bila hata kuambiwa, kwa namna ilivyo hata ukipiga kelele vipi huwezi kupata Msaada wowote.ย
Kwanza sikujuwa Mtu yule alikua ni Nani, sauti yake haikufanana na ya Kaka Hamidu. Wala siย ya Mtu niliyehisi kuwa niliwahi zungumza naye.ย ย
**ย
Usiku ulipoingia ndiyo nililiona joto la jiwe, niliandamwa na ndoto za ajabu hadi niliamka, siyoย Mimi tu hata yule Mwanaume alikua akigugumia nahisi naye alikua kwenye hali kama yangu.ย Niliamka na kukaa kitako nikaegemea ukutaย
Nikiwa hapo nilianza kuona nuru ya mwanga, ikianza taratibu hadi ikaenea chumba chote, hapaย nilikua na uhakika kuwa haikuwa ndoto tena bali ni tukio halisi. Nilimuona tena yule Mtotoย mdogo anayetisha, safari hii alinionesha sura yake, nilikua kwenye Mshangao wa hali ya juuย sanaย
โUmeshindwa kutoka hapa, umeshindwa kujaribu kufanya chochote. Wewe ni Mtu wa aina gani,ย unataka kila Mtu afe kama Kaka yako Hamiduโ Ooh! Jamani nilishtuka, kama ningekua ninaย presha kwa haya yote ningekuwa tayari nimepotea kwenye uso wa Dunia, namna alivyokuaย anaongea alionesha alikua na tumaini na Mimi kwenye jambo fulani hasa la kuokoa uhai waย wengine lakini Mimi mwenyewe nilikua nimeshajikatia tamaa. Japo nilijawa na woga lakiniย nilimuulizaย
โWewe ni Nani, umetokea wapi?โ nilipomuuliza alidondosha chozi la damu, alikua Mtoto waย ajabu sanaย
โMimi ni Ashura Mtoto wa Mama Muuza chapati. Nenda kamwambie Mama yangu kuwa badoย naishi kwenye nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, Mimi sijafaโ alisema kwa kupaza sauti kaliย ambayo ilinifanya nishindwe kuhimili zile kelele, pale pale nilijikuta nikiishiwa nguvu naย kupoteza fahamu. Kitu pekee kilichobakia kwenye akili yangu ni ,kumbukumbu juu ya yuleย Mama anayeishi nyumba jirani na Mzee Mwinyimkuu, Mama aliyekuwa akiniuzia Chapati
Ndiyoโผ yeye ni Mama Ashura, nakumbuka alinitajia jina hili lakini sikuwahi kumuuliza huyoย Ashura yupo wapi, huyu Mtoto wa ajabu alijitambulisha kwangu kama Ashura na alinitakaย nimwambie Mama yake kuwa anaishi ndani ya nyumba ya Mzee Mwinyimkuu.ย
***ย
Baba yangu aliendelea kuumwa, Mama alikua anamuuguza huku akinitafuta Mimi kwa simuย lakini aliendelea kutonipata, zilipita wiki mbili bila kupata mawasiliano yoyote yale. Saleheย hakupatikana, hata Mzee Mwinyimkuu hakupatikana, Kaka Hamidu naye ilikua kama ndiyoย ย
kichocheo kipya cha hofu kwa Familia yangu. Mara ya mwisho aliwaeleza anakuja kuonana naย Mimi lakini baada ya hapo hawakujua kilichomfika na kupelekea kutopatikana kwenye simuย kwa wiki mbili.ย
Vikafanyika vikao vya kututafuta Mimi na Kaka Hamidu maana hawakujua naishi Rukwaย sehemu gani na pia Kaka Hamidu alikutwa na nini. Ni Mimi pekee ndiye niliyekuwa najua Kuaย Kaka Hamidu alikua ameuawa.ย
Familia ikamtuma Mjomba wetu aliyeitwa Kambona, alikua Mtu mzima na mwenye busaraย zake.ย ย
Akasafiri kutoka Dar-es-salaam hadi Rukwa akiwa na picha yangu, akaanza kunitafuta bilaย mafanikio kwa zaidi ya siku kumi. Mwishowe akaenda kituo cha Polisi maana sasa hakunaย aliyekua na amani bila kujua tupo wapi, wote waliamini wakinipata Mimi watajua mahali alipoย Kaka Hamidu maana mara ya mwisho aliwaambia anakuja kwangu. Polisi wakaanza kunitafutaย kila kona ya Rukwa lakini hakuna aliyeweza kujua niko wapi, lakini kupitia jina la Mwinyimkuu Ambalo Salehe alilitaja alipokua ananichumbia, ikawawezesha kufika hadi nyumbani kwa huyuย Mzee.ย
Hapa ndipo mahali ambapo nilikuwepo kabla ya kuhamishwa, nyumba hii ndimo alimouawaย Kaka Hamidu tena kikatili sana na Mzee Mwinyimkuu. Walipofika walimkuta tena walaย hakuwa na wasiwasi kabisa, najua alitumia akili sana kunihamisha vinginevyo polisiย wangenikuta mleย
โWewe ndiye Mwinyimkuu?โ aliuliza polisi baada ya salamu fupiย
โMnasemaje?โ aliwauliza, alikua haogopi chochote wala Mtu yeyote yule, jeuri na katili mno โSaida anaishi hapa?โ akauliza Polisi mmoja.ย
โYeye ni Nani?โ akawaulizaย
โUnajibu kwa dharau kiasi hicho Mzee, Saida ni Mpwa wangu Mimi. Ameolewa na Kijanaย anaitwa Salehe, upelelezi umeonesha kuwa ni Kijana wako huyo Salehe halafu unauliza niย Nani?โ akaingilia kati mjomba Kambona na kumshika shati Mzee Mwinyimkuu, Polisiย wakaokoa
โUnanivunjia heshiam si ndiyo?โ akauliza Mzee Mwinyimkuu kwa hasiraย
โSiyo heshima tu, ntaivunja hata hii nyumba kama hutonipatia Saida wanguโ Mjomba Kambonaย hakupoa kabisa, alijawa na hasira sana.ย
โHuyo Salehe unamfahamu?โ Polisi wakamuuliza Mjomba Kambonaย
โNdiyo, nimeozesha mwenyewe. Picha si hii hapa ya ndoaโ akatoa picha, ile picha akapewaย Mzee Mwinyimkuu.ย
โUmemtambua mtajwa pichani?โ akauliza Polisi mmoja, Mzee Mwinyimkuu akaangua kichekoย kisha akaita kwa sautiย
โSalehe, hebu njoo uone maajabu ya Duniaโ akaitikia Mtu kutokea ndani na kuwafanya Polisi naย Mjomba Kambona wakae mkao wa kula kumuona Salehe. Ikachukua kama sekunde kadhaa tuย Kijana mmoja akatoka ndani, Kijana aliyekuja hakufanana na Salehe wa kwenye picha.ย ย
โUnamfahamu Saida?โ akauliza Mzee Mwinyimkuu akimuuliza huyo Kijana aliyemtambulishaย kama Salehe, kiukweli hakuwa yule Salehe aliyeniowa kabisa yaani sura tofauti.ย
โHapana, kuna nini?โ akauliza huyo Salehe, kiukweli Mjomba Kambona alinywea. Lakini Polisiย mmoja akasemaย
โOngozana na Mimi Kijanaโ akamshika mkono Salehe na kwenda naye nje. Lengo la Polisi niย kutaka utambuzi kwa Majirani maana Upelelezi wao uliwaambia Salehe wa kwemye pichaย anapatikana kwa Mzee Mwinyimkuu. Wakafika hadi nyumbani kwa Mama Ashura maana ndipoย palikua na Watu njeย
Walipomuona Yule Kijana akiwa na Polisi vijana walikimbia hadi yule Polisi akashangaa, hataย Mama Ashura naye alikua anataka kukimbia ila Polisi akamzuia Mama Ashura na Kumwambiaย asikimbie ana maswali kadhaa anataka kumuuliza, ndipo Mama Ashura akabakia lakini kwa hofuย sanaย
โUnamtambua nani pichani?โ Yule Polisi akampa picha yule Mama, Mama Ashura akaipokeaย picha japo kwa wasiwasi lakini alipoiangalia ile picha alishtuka sana, akameza funda la mate.ย ย
โHapanaโโakajibu lakini kwa hofu sana kiasi kwamba yule polisi akahisi pengine kuna jamboย analificha. Kilichomshtua Mama Ashura ni kuniona Mimi kwenye ile picha ya ndoa ambayoย Mjomba Kambona aliwapatia polisiย
โNa huyu Kijana hapa?โ akauliza Polisi, Mama Ashura akamtazama yule Kijana. Akaachiaย tabasamu la hofu kisha akajibuย
โNi Salehe, anaishi paleโ akaonesha na kidole kabisa. Majibu haya yakamuacha yule polisiย kinywa wazi, basi akarudi hadi nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Hakuna ushahidi waย anachosema Mjomba Kambona. Lakini Mjomba akawaaambia
โNina namba ya huyu Mzee alikua anawasiliana na Mama yake Saida, hii namba nimepewa naย Mama Saida. Jina ni hilo la Mwinyimkuuโ akasema Mjomba japo kwa sauti ya kupoa, ikabidiย Polisi waipige ile namba.ย
Ikapokelewa na Mtu mwingine kabisa tena Mwanamke akimuuliza yule Polisi Nani wewe?ย Yalikua kama maigizo ya Filamu lakini lilikua tukio la kweli, nyakati zote hizo Mzeeย Mwinyimkuu alikua akitabasamu akiwa anamtazama Mjomba Kambona.ย ย
โMnaona anavyo nitazama, huyu anajua kila kituโ akasema Mjomba lakini hakuwa na ushahidi,ย maneno yake yalikua ni sawa na kuupaka upepo rangi. Muda wote Mzee katili alikuaย akitabasamu kwa mpango fulani ulio kichwani pakeย
Polisi walikosa ushahidi, ikaonekana kuwa Mjomba Kambona aliyakosea maelezo yake. Kibayaย zaidi hata picha aliyowaonesha Polisi kuwa ndiye aliyeniowa ilikanwa kwa kuoneshwa Saleheย mwingine na kilichotia nguvu kukosekana ushahidi ni maneno ya Mama Ashura. Angefanyajeย Mjomba wangu zaidi ya kutoa kitambaa na kujifuta jasho ila moyoni aliamini Mzeeย Mwinyimkuu alikua anajua wapi nilipo, pia hapakua na ushahidi mwingine sababu Mzeeย Mwinyimkuu hakuhudhuria ndoa yanguย ย
Polisi wakamwambia Mjomba Kambonaย
โTutaendelea na Uchunguzi, kwasasa wewe liachie jeshi la Polisi. Tutakupa taarifa ya Uchunguziย juu ya Saida pia huyo Kaka yakeโ haikua kauli yenye matumaini, ilimvunja moyo sana Mjombaย Kambona. Akamwambia Mzee Mwinyimkuuย
โSaida hawezi kutoweka kirahisi, lipo unalolijua. Siondoki Rukwa hadi nihakikishe nampataย Mpwa wanguโ alisema hivyo kisha aliongozana na Polisi kuondoka, Salehe feki na Mzeeย Mwinyimkuu wakatazamana kisha wakawa wanawatazama namna Polisi na Mjomba Kambonaย walivyokuwa wanaondoka.ย ย
Wala hawakufika mbali, kabla hata hawajapanda kwenye gari ya Polisi. Mjomba Kambonaย alianguka na kufariki papo hapo akitokwa na Mapovu mdomoni. Licha ya jitihada za jeshi laย polisi kumkimbiza Hospitali lakini alikua tayari amefarikiย
Taarifa ikarudi Dar-es-salaam kuwa Mtu waliyemtuma kuja kututafuta Mimi na Kaka Hamiduย alikua tayari ameshafariki. Yalikua ni majonzi juu ya Majonzi, taarifa hii ilipomfikia Baba yanguย alifariki pia kwa presha. Bundi aliizingira familia yangu, misiba miwili ndani ya siku moja,ย Mzee Mwinyimkuu akashinda tena kwa kishindo kikubwa sana.ย
**ย
Nilihesabu siku ambazo nilikua ndani ya ile nyumba ya mateso, zilitimia siku saba ngumu.ย Nilikonda nikawa kama Mtoto mdogo, niliishiwa nguvu. Kilichokuwa kimebakia kwangu ilikuaย ni kufa tu. Kila nilipoamka nilijikuta nimeshaondolewa kidole kimoja, pumua yangu ikawa yaย
shida sana. Nikakosa uwezo wa kuwatambua Watu kirahisi, yule Bodaboda aliendelea kunileteaย chakula kila siku lakini pia sauti ya Mwanaume mmoja kugumia ilikua ni sauti ya Kila sikuย
Lilikua ni jambo la kawaida sana yeye kupaza sauti, sikuwahi kufahamu alikua akipitia matesoย gani, ila dakika za mwisho niligundua kuwa naye alikua akipelekewa chakula na huyu huyuย Bodaboda anayeniletea Mimi chakula.ย
Sikuweza kusimama tena, vidonda vilianza kutoa funza sababu sikuwa na dawa yoyote isitosheย joto la mle ndani liliniathiri kwa kiasi kikubwa, Mwenzenu niliwahi kufika Jehannam nikiwaย Hai.ย
Basi siku moja yule Bodaboda alikuja, siku yenyewe palikua na mvua kubwa. Aliingia akiwaย ameloa sana anatetemeka kwa Baridi, japo nilikua katika nyakati za mwisho kabisa za uhaiย wangu lakini niliweza kugundua kuwa Baridi lilikua tatizo kubwa kwake. Alikua akiniandaliaย chakula huku akitetemeka nikagundua anasumbuliwa na tatizo linalo sababishwa na Baridi.ย
Akajikaza, akaniwekea chakula. Alipaswa kunilisha sababu Mimi nilikua siwezi tena hataย kushika kijiko, nilikonda mno hadi mishipa ya Damu ilikua ikionekana. Akajitahidi kuniinua iliย kunikalisha kitako niweze kuegemea ukuta anilishe vizuri, siku hii nilipanga kuacha kula ili nifeย mapema maana mateso yalinizidi kabisa, Jamani naposema nilikonda basi ujue nilikonda nikawaย na kilo chache sana halafu kichwa kikawa kikubwa.ย
Nilitamani kumuuliza ana shida gani, huyu Mtu hakuwahi kunitesa wala hakuwahi kunisemeaย jambo baya isipokua alikua hajibu maswali yangu yote niliyokuwa namuuliza.ย
Hali yake ilianza kuwa mbaya, akashindwa hata kunishikilia akaanguka chini na kuanza kugalaย gala kwa maumivu Makali sana, mlango ulikuwa wazi hakuufunga sababu alipoingia alikuaย tayari ana hiyo hali ya Maumivu, niliona ni nafasi ya kutoroka lakini sikuwa na akiba yoyote yaย nguvu iliyobakiaย
Nikatamani kuendelea kuishi ghafla tu, namna pekee ya kuendelea kuwa hai ni kutoroka. Hukoย nje mvua ilikua ikinyesha na kusababisha kelele kubwa sana kwenye Bati. Sikuwa na nguvu yaย kusimama, nikaona ni bora nijiburuze nione kama naweza kufika njeย
Yule Bodaboda alipoona naanza kujiburuza akajua nataka kumtoroka, akili yake ikatamaniย anizuie lakini mwili ulimsaliti, nguvu zilimwisha akiwa sakafuni anapumua kwa shida sana.ย Nikaendelea kujivuta taratibu huku nikiwa ninasali Mungu niliyemkatia tamaa azidi kunipaย nguvu, unajua kwanini niliamini naweza kuondoka pale?ย
Kwasababu hapakua na mtu mwingine aliyekuwa anakuja isipokua yeye, hivyo hakuna tena waย kunizuia, halafu niliwaza kufika chumba ambacho yule Mwanaume anagumia ili kama yeye anaย nguvu tusaidiane kutoroka.ย
Nilijiburuza kama nyoka hadi nilipotoka nje ya chumba kile, palikua na funguo kwenye kitasa.ย Nikapata akili ya dharura kuwa huwenda funguo ile inaweza nisaidia kufungua milango mingineย
maana ilikua na funguo tatu zilizowekwa sehemu moja, naipataje Funguo ni lazima nisimameย niichomoeย
Kivumbi kilianzia hapo, nilikonda Mimi kiasi kwamba upepo unaweza nipeperusha, Malaikaย Mtoa roho alikua amenisimamia akiniuliza nasimama au achukue roho yangu, sijui nguvuย zilitoka wapi nikasimama kwa kuyumba huku nikitetemeka. Nikachomoa funguo, ile natakaย kupiga hatua nikaangukaย
Basi nikagugumia kwa maumivu, nilihitaji kufanya haraka maana kama yule Bodaboda atapataย nguvu basi sitaweza tena kuondoka, nikamkumbuka Mama na Baba yangu, nikamkumbuka Kakaย Hamidu. Ghafla nguvu zikaamkaย
Nikajikaza na kuanza kujiburuza sakafuni kama nyoka vile, kwa mwendo huo huo nilijikutaย nikikiacha chumba kwa mbali kidogo, sikuufunga ule mlango wa chumba nilichomuachaย Bodaboda.ย ย
Basi nilipofika kama chumba cha tano hivi nikasikia Mtu akiugonga mlango kwa nguvu hukuย akisemaย
โNjoo unitoe humu Mshenzi wewe, mtauwa wangapi. Siku ikifika mtakufa kama Kukuโ alisemaย kwa hisia sana lakini hakujuwa kuwa Mimi nilikua tayari nipo mlangoni. Mlango ulikuaย umefungwa, korido lilikuwa refu halafu vyumba vilikua mbali mbali. Nilijitahidi sana kusimamaย nifungue mlango lakini nilikua nakosa nguvu, nilijaribu kama mara tatu lakini niliishia kuangukaย
Wakati nikiwa nimeanguka nikageuka nyuma, ndipo nilipomuona yule Bodaboda akijikongojaย kwa maumivu kuja nilipo, alikua amelishikilia tumbo lake. Hapo sasa yule Malaika mtoa rohoย nikamuona kama anachukua koleo kwa ajili ya kuichukua roho yangu.ย
Sauti ya yule Mwanaume ilizidi kusema, kibaya zaidi Mimi ndiye mwenye funguo halafu sautiย yangu ilikua haitoki. Nikasema kama sisimami basi siondoki. Yule Bodaboda akawa anazidi kujaย upande wangu kwa kasi akionekana kuanza kupiga hatua za nguvu. Nikamtaja Mungu nikasemaย
โMungu nipe nguvu niishinde hii vitaโ nikajivuta haraka nikasimama nikiwa ninayumba,ย nikaanza kusaka tundu la kuweka funguo maana nguvu yenye ilikua sifuri, nikawa najitahidiย huku nikiwa natetemeka. Mara naingiza mara nakosea, huku yule Bodaboda akizidi kunisogelea,ย hata nilipopaatia nilikua nimeingiza funguo isiyo yake.ย
Akawa karibu zaidi kiasi kwamba akipiga hatua tatu anakuwa amenifikia na kunizuia kuufunguaย mlango, nikapapasia kwa bahati nzuri nikapatia funguo nikavuta nguvu za mwisho nikatekenyaย kitasa lakini tayari Bodaboda alikua ameshanivaa na kuniangusha chini, Bahati nzuri ule mlangoย ulikua tayari umeshafungukaย
Akatoka mwanaume mmoja na kuanza kumkita mateke yule Bodaboda hadi akamtupilia mbaliย huko akiwa hoi sana anatokwa na damu mdomoni, eneo la Korido lilikua linawaka taa isipokuaย
vyumbani tu. Sikuamini macho yangu Mtu ambaye nilikuja kumuona na kumtambua japoย nilimuona mara moja tuย ย
Alikua ni yule Mwanaume niliyemuazimaga simu kule Buchani, Ndio! Ni Abuu, masikini nayeย alikua mateka wa Mzee Mwinyimkuu baada ya kujulikana ananifuatilia Mimi, kwa muda mfupiย naye alikua amepungua sana japo alikua na nguvu.ย
Hakuniuliza chochote zaidi ya kuninyanyua na kuweka mkono wangu kwapani kwake tukawaย tunaelekea nje, mvua bado ilikua inanyesha. Tulipokua tunakaribia kutoka kabisa tukamuonaย Mtu anakuja Mbio, tena akikimbia kwenye mvua, ikatubidi tujifiche nyuma ya Mlango waย kutokeaย
Yule Mtu alipofika, breki ya kwanza ilikua vyumbani kisha akamrudia yule Bodaboda aliyekuwaย anagala gala. Akamuuliza kwa hasiraย
โUmefanya nini Mpuuzi wewe?โ aliuliza kwa sauti ambayo niliitambua, ilikua ni sauti ya Mzeeย Mwinyimkuu. Nilishtuka na kupata nguvu, nilipokumbuka kuwa yeye ndiye mtesi wangu basiย mkojo ulinibana. Ghafla tu nikajiona ni Binadamu ninayehitaji kujiteteaย
โNenda, hatuwezi kuondoka wote. Kaiambie Dunia kuhusu huyu Mzee, kama nitarudi tutakutanaย na kama nitafia hapa basi Roho yangu itakua salamaโ alisema Abuu, roho iliniuma. Sikua naย uwezo wa kuzungumza. Mdomo wangu wa juu na chini nilihisi kama vimeungana sababu nilikuaย na vidonda mdomoni hivyo kukaa kimya ndiyo yalikua maisha yangu.ย
Nikaitikia kwa kutumia kichwa kisha nikasimama kama Mzimu, Mungu akaamua kunikumbuka.ย Akanipa nguvu na ujasiri, alichotaka Abuu ni kumzuia Mzee Mwinyimkuu. Wakati naanza safariย Mzee Mwinyimkuu akaja mbio nahisi alikua anaanza kutusaka, sijui alijuaje kuwa tunatoroka.ย Huyu Mzee alikua Mchawi haswa, aliponikaribia tayari Abuu alimdaka Mzee Mwinyimkuuย wakaanza kupalangana, muda huo nami nikaanza kujivuta kuondoka pale taratibu hadi nikaingiaย kwenye mvua.ย
Ulikua mchana lakini anga lilikua na wingu la kutosha kiasi kwamba palikua na giza fulaniย isitoshe palikua Porini. Nilipopigwa na mvua nikapata nguvu ya kuanza kuchanganya Miguuย yangu vizuri. Nikaanza kukimbia huku nikiyumba kama mleviย
Sijui nilikimbia umbali gani lakini nilikimbia bila kuangalia nyuma, nilikimbia sana hadiย nilichoka kabisa nikaanguka na kupoteza fahamu zangu.ย
Nilirudisha fahamu na kuanza kujitambua nikiwa naburuzwa kwa kasi sana, watu walikua kamaย vile wamenizunguka. Walikua na mavazi ya kufanana, nilikua kwenye kitanda kiendacho kwaย kasi mno, nikawasikia wakisemaย
โApelekwe ICU Haraka sana, kazi ianze mara mojaโ niligundua nilikua Hospitalini, waleย wauguzi walionekana kunikatia tamaa sababu nilikua na hali mbaya sana. Lakini mimiย
mwenyewe nilijiona ni mzima wa Afya zote, mahali nilipokuwepo palikua ni hatari zaidi yaย Kuzimu.ย ย
Chozi lilinibubujika nikafumba macho yangu huku nikimshukuru Mungu. Madaktari walifanyaย kazi yao kwa wiki tatu kuhakikisha najitambua zaidi, wakaniweka kwenye uangalizi maalumย kwa kipindi chote hicho hadi nilipokumbuka yaliyonisibu.ย
Nikawaandikia jina Langu, mahali nilipotoka maana nilikua siwezi kuzungumza tena, Hospitaliย ikasambaza jina na taarifa zangu ndipo Mama yangu alipokuja Mbeya akiongozana na Nduguย wengine kunitambua. Mama alilia sana, sikuwahi kumuona Mama yangu akilia namna ile, yaleย Maisha yaliniathiri sana kisaikolojia. Nikapoteza uwezo wa kuzungumza kabisa. Taarifa ya Kifoย cha Baba ilinihuzunisha mno, ikanitoa chozi.ย
Polisi walipokuja niliandika maelezo yangu, ilikua baada ya wiki sita. Mwezi mmoja na sikuย kadhaa, afya yangu ilianza kukaa sawa lakini sikuwa na Uwezo wa kuzungumza chochoteย isipokua kuandika. Polisi walinichukua ili nikawapeleke mahali nilipoteswa yaani nyumbani kwaย Mzee Mwinyimkuuย ย
Mimi na Mama tulienda, palikua ni pale pale kwa Mzee Mwinyimkuu. Namba ya nyumba ilikuaย ni ile ile, mazingira yale yale, chozi lilinibubujika sana hadi Mama akashindwa kujizuia.ย ย
Nilikua natembezwa kwenye kiti cha Walemavu maana bado miguu ilikua haipo sawa pia sikuaย na vidole nilikua najiuguza. Nikampa ishara Mama yangu kuwa anipeleke kwanza nyumbaย jirani, pale kwa muuza chapati, nilimkuta Mwanamke mwingine kabisa akitengeneza chapati,ย nikaandika kwenye karatasiย
โMama Ashura yupo wapi?โ nilikua na ujumbe wa Mtoto wake Ashura nilitaka kwanza nimpeย ujumbe, wakati huo polisi walikua wameizingira nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Mamaย akamsomea yule Mwanamke, lakini cha ajabu eti akadai yeye ndiye Mama Ashura, nilishtukaย alafu kingine kilichonipa mshituko ni kumuona Ashura mwenyewe, alikua ni Ashura yule yuleย niliyemuona Nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuuย
Haya mambo yalinifanya nianze kuonekana akili yangu bado haiko sawa, nikajitahidiย kuwaambia kwa maandishi lakini niliishia kupewa pole tu, kisha nikapelekwa kwa Mzeeย Mwinyimkuu. Nako nikakutana na stori mpya kabisaย
Kwanza ile nyumba si ya Mzee Mwinyimkuu, hawamfahamu. Wao wanaishi hapo Kwa Miakaย mingi, nilitokwa na Mchozi, nyumba ile ile mazingira yale yale lakini stori tofauti. Nikaombaย niingizwe ndani, nikapelekwa kwenye chumba nilichokuwa nalalaย
Nikakuta magunia ya vyakula, tena kilikua chumba chenye makorokoro mengi sana naย hakikuonekana kua chumba cha kulala Mtu. Mama akaniambiaย
โSaida, najua umeteseka sana huku lakini hukumbuki chochote tena. Siku ukikumbuka nakuahidiย tutarudi, yule Kijana na Baba yake watalipaโ Kauli ya Mama yangu ilinimaliza akili yangu,ย
nilifikia hatua nikakubali kuwa akili yangu haipo sawa, inawezekanaje kila kitu kibadilike kwaย haraka vile. Hakuna aliyeniaminiย
Lakini sasa wakati natoka nikajikuta nikipeleka macho yangu jikoni, nikaiona ile sufuria kubwaย ambayo kwa mara ya kwanza nilipika mchicha mwingi, nikashtuka alafu nikauona Mchichaย mwingi ukiwa kwenye Beseni. Kilichonishtua ni kwamba nilimuona Msichana wa umri wanguย akiutengeneza.ย
Nilijikuta nikipiga yowe kali sana. Hali ya afya yangu ikawa sio nzuri nikarudishwa tenaย Hospitali. Tokea siku ile nilikua Msichana ninayekaa kimya hadi leo hii nawasimulia hiki kisa,ย sikumpata Mzee MwinyiMkuu wala Salehe, lakini sitakubali. Siku moja nitarudi Rukwa iliย walipe kwa maumivu na mateso makali ninayoyapitia hadi sasa.ย
Kwasasa nimerudishwa kwetu Dar-es-salaam, niko Magomeni. Maisha yangu yamekuwa yaย Ukimya sana, Sijazungumza tena tokea siku ile nilipozungumza kwa mara ya mwisho Rukwa,ย sijaandika chochote na wala sitaki kusema chochote kile ila kupitia mkasa huu nataka ujifunze.ย
Kamwe kwenye Maisha yako usiolewe au kuowa Mtu usiye mfahamu, Dunia ni Kichaka chaย Mateso. Wasichana wengi wanayapitia mateso niliyoyapitia, wengi wanauawa, wengi wanapataย ugonjwa wa akili. Hata wanaume wapo waliopoteza kila kitu, Siku nikifungua kinywa changuย nitawasimulia mengi, kwasasa naishia hapa, naweka kalamu yangu chini.ย
AHSANTE……….MWISHO
Comments zikiwa nyingi TUNAANZA MPYA Chaap
USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kutuma Message WhatsApp Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย
Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xxย Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx


23 Comments
Hadi mwili umenisisimka ๐
Kaka umetisha
Wowoooh fupi na inafundisha sana nmepata somo apa nmejifunza mengi poleee saida wetu.
Hatar sana,, mungu amekpgania pakubwa,, mm kama kijana ambae sjaoa hakka nmepata kitu kwa riwaya hii,, mungu akupe maisha mazur
Dag
pole sana
Jamani hatujajua mwisho wa kijana aliyemukoa Saida,,, mwandishi ungesogeza kidogo
Lini utafungua kiywa Chako tuendelee maan bado nataka kujua zaid
Hahahahaha๐ ๐ ๐ ๐ umepigaje apooooooooooooooโ๏ธ๐๐๐๐๐
Navuta picha mwandishi mwili wako ulikua kama wa Ile muv BABU SISU
Hii ya leo machozi yamenibubujika sijui nisemeje lakin naamin Allah anajua zaid yaliyopo mioyon mwetu wanadamu
Maskini Saida jamani ๐ฅ
Simulizi ya Maajabu Nzuri yenye mazingatio makubwa jamani
Uchawi upo
Ila uchawi wa MwinyiMkuu ni zaidi ya Uchawi
Mungu atunusuru maisha yetu na Wachawi
Mungu AWAANGAMIZE WASHIRIKINA WOTE MOTONI.
Ameen.
Safi sana mtunzi tumejifunza sana mim pamoja nawasomaji wenzangu Big up
Inauzunisha sana pole saida ๐ข
Kazi mzuri na pole sana
๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ๐ญ๐ญnimelia kama mtoto
Daah atali
Ni hatar
Munguu hamtupii mja wake hakika Munguu ni mwemaa
๐ฅนnianze kwa kuhiluzunika ,ila mtu kuna sehem nmecheka dadeq, KWAMBA NYIE WASHENZ NIFUNGUENI MTAKUF KAMA KUKU , YAN MUUNI YUPO KWENY MATATZO ILA BADO AJAL, KWEL MAN IS STRONG NATURAL
Kwani story ni yakwel
Dah sijui niseme nini
Mhhh ila pole
gx3yc0