Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (08)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 13, 2025Updated:January 14, 202524 Comments18 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.Β 

    β€œKunywa Maji” alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikuaΒ  ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuulizaΒ 

    β€œMnanimalizia lini nikapumzike?” Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chacheΒ  nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambiaΒ 

    β€œKifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwaje” alisema kisha akanipa maji, sikuwaΒ  na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe hai. EndeleaΒ 

    SEHEMU YA NANE

    Niliyafakamia yale maji kwanza hadi yalinipalia, halafu nikahema. Akanitolea vidonge vyaΒ  kunituliza maumivu. Sikusita kumeza kiukweli maana nilikua na maumivu makali sana kishaΒ  nilimshika mkono nikamuulizaΒ 

    β€œNingekuwa mdogo wako ungenifanyia hivi, unajua najisikiaje Kaka?’’ Chozi lilikuaΒ  linanibubujika bila kuacha, akaniondoa mkono wangu kwa kutumia mkono wake mwingineΒ  kisha akasimama, akaniambiaΒ 

    β€œKula upate nguvu” hakuzungumza tena, alisimama kisha alipiga hatua lakini alipofika mlangoniΒ  alisimama. Kama kuna kitu alitaka kuniambia lakini alighaili, hakujibu swali langu aliondoka naΒ  kuufunga mlango kwa funguo, unajua hata kama angeuacha wazi sikuwa na nguvu ya kukimbiaΒ  kwa namna nilivyokua sina nguvu.Β Β 

    Nilisikia akiondoka, nililia sana Mimi. Hakuna siku inapita bila kudondosha chozi langu,Β  nilimpoteza Kaka Hamidu na nilijiona ni mkosaji, nilijilaumu sababu bila kuolewa na SaleheΒ  basi Kaka Hamidu angekuwa hai hadi sasa. Kidogo zile dawa zilipunguza maumivu ya mwiliΒ  lakini siyo maumivu ya Moyo wanguΒ Β 

    Haikuchukua hata dakika nyingi nilisikia yowe la Mwanaume mmoja, yowe lile lilisikika mojaΒ  kwa moja kutoka kwenye ile nyumba niliyohifadhiwa Mimi. Moyo ulinilipuka, niliamini ilikuaΒ  ni nyumba ya Mateso makali zaidi hata nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Nilisimama hataΒ  nguvu sikujuwa ilitokea wapiΒ 

    Nilisogea mlangoni ili kuisikia zaidi ile sauti, ndiyo! Ilitoka ndani ya moja ya vyumba vya ileΒ  nyumba, nilitamani kupaza sauti ila sikujua alikua akifanywa nini. Nilijiuliza

    β€œNani yupo ndani ya hii nyumba, anamfanya nini huyu anayepiga yowe” Ilikua ni sawa naΒ  kujitekenya kisha kucheka mwenyewe, jibu lingetokea wapi ikiwa hata mimi mwenyewe sijuiΒ  nipo wapiΒ 

    Yule Mwanaume baada ya kupiga yowe alianza kusemaΒ 

    β€œMsaada,Nani yupo ananisikia?” aliendelea kusema hivi, nikapata picha huwenda hata yeyeΒ  mwenyewe hajui amefikaje na Nani amemleta ndani ya hii nyumba. Kupitia dirishani nilianzaΒ  kuona jua namna lilivyokuwa likifanya safari ya kwenda kupumzika baada ya kuipiga ardhi kwaΒ  siku nzima.Β 

    Namna nyumba hii ilivyo ilionekana kujengwa kwa ajili ya kazi ya kuhifadhi Binadamu, hataΒ  dirisha lake lilikua kama la Mahabusu, lilikua dogo lanye nondo,hapakuwa na taa ndani yaΒ  chumba kiasi kwamba giza litakapoingia basi patakuwa giza tupu. Nilijikuta nikikaa mwenyeweΒ  bila hata kuambiwa, kwa namna ilivyo hata ukipiga kelele vipi huwezi kupata Msaada wowote.Β 

    Kwanza sikujuwa Mtu yule alikua ni Nani, sauti yake haikufanana na ya Kaka Hamidu. Wala siΒ  ya Mtu niliyehisi kuwa niliwahi zungumza naye.Β Β 

    **Β 

    Usiku ulipoingia ndiyo nililiona joto la jiwe, niliandamwa na ndoto za ajabu hadi niliamka, siyoΒ  Mimi tu hata yule Mwanaume alikua akigugumia nahisi naye alikua kwenye hali kama yangu.Β  Niliamka na kukaa kitako nikaegemea ukutaΒ 

    Nikiwa hapo nilianza kuona nuru ya mwanga, ikianza taratibu hadi ikaenea chumba chote, hapaΒ  nilikua na uhakika kuwa haikuwa ndoto tena bali ni tukio halisi. Nilimuona tena yule MtotoΒ  mdogo anayetisha, safari hii alinionesha sura yake, nilikua kwenye Mshangao wa hali ya juuΒ  sanaΒ 

    β€œUmeshindwa kutoka hapa, umeshindwa kujaribu kufanya chochote. Wewe ni Mtu wa aina gani,Β  unataka kila Mtu afe kama Kaka yako Hamidu” Ooh! Jamani nilishtuka, kama ningekua ninaΒ  presha kwa haya yote ningekuwa tayari nimepotea kwenye uso wa Dunia, namna alivyokuaΒ  anaongea alionesha alikua na tumaini na Mimi kwenye jambo fulani hasa la kuokoa uhai waΒ  wengine lakini Mimi mwenyewe nilikua nimeshajikatia tamaa. Japo nilijawa na woga lakiniΒ  nilimuulizaΒ 

    β€œWewe ni Nani, umetokea wapi?” nilipomuuliza alidondosha chozi la damu, alikua Mtoto waΒ  ajabu sanaΒ 

    β€œMimi ni Ashura Mtoto wa Mama Muuza chapati. Nenda kamwambie Mama yangu kuwa badoΒ  naishi kwenye nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, Mimi sijafa” alisema kwa kupaza sauti kaliΒ  ambayo ilinifanya nishindwe kuhimili zile kelele, pale pale nilijikuta nikiishiwa nguvu naΒ  kupoteza fahamu. Kitu pekee kilichobakia kwenye akili yangu ni ,kumbukumbu juu ya yuleΒ  Mama anayeishi nyumba jirani na Mzee Mwinyimkuu, Mama aliyekuwa akiniuzia Chapati

    Ndiyoβ€Ό yeye ni Mama Ashura, nakumbuka alinitajia jina hili lakini sikuwahi kumuuliza huyoΒ  Ashura yupo wapi, huyu Mtoto wa ajabu alijitambulisha kwangu kama Ashura na alinitakaΒ  nimwambie Mama yake kuwa anaishi ndani ya nyumba ya Mzee Mwinyimkuu.Β 

    ***Β 

    Baba yangu aliendelea kuumwa, Mama alikua anamuuguza huku akinitafuta Mimi kwa simuΒ  lakini aliendelea kutonipata, zilipita wiki mbili bila kupata mawasiliano yoyote yale. SaleheΒ  hakupatikana, hata Mzee Mwinyimkuu hakupatikana, Kaka Hamidu naye ilikua kama ndiyoΒ Β 

    kichocheo kipya cha hofu kwa Familia yangu. Mara ya mwisho aliwaeleza anakuja kuonana naΒ  Mimi lakini baada ya hapo hawakujua kilichomfika na kupelekea kutopatikana kwenye simuΒ  kwa wiki mbili.Β 

    Vikafanyika vikao vya kututafuta Mimi na Kaka Hamidu maana hawakujua naishi RukwaΒ  sehemu gani na pia Kaka Hamidu alikutwa na nini. Ni Mimi pekee ndiye niliyekuwa najua KuaΒ  Kaka Hamidu alikua ameuawa.Β 

    Familia ikamtuma Mjomba wetu aliyeitwa Kambona, alikua Mtu mzima na mwenye busaraΒ  zake.Β Β 

    Akasafiri kutoka Dar-es-salaam hadi Rukwa akiwa na picha yangu, akaanza kunitafuta bilaΒ  mafanikio kwa zaidi ya siku kumi. Mwishowe akaenda kituo cha Polisi maana sasa hakunaΒ  aliyekua na amani bila kujua tupo wapi, wote waliamini wakinipata Mimi watajua mahali alipoΒ  Kaka Hamidu maana mara ya mwisho aliwaambia anakuja kwangu. Polisi wakaanza kunitafutaΒ  kila kona ya Rukwa lakini hakuna aliyeweza kujua niko wapi, lakini kupitia jina la Mwinyimkuu Ambalo Salehe alilitaja alipokua ananichumbia, ikawawezesha kufika hadi nyumbani kwa huyuΒ  Mzee.Β 

    Hapa ndipo mahali ambapo nilikuwepo kabla ya kuhamishwa, nyumba hii ndimo alimouawaΒ  Kaka Hamidu tena kikatili sana na Mzee Mwinyimkuu. Walipofika walimkuta tena walaΒ  hakuwa na wasiwasi kabisa, najua alitumia akili sana kunihamisha vinginevyo polisiΒ  wangenikuta mleΒ 

    β€œWewe ndiye Mwinyimkuu?” aliuliza polisi baada ya salamu fupiΒ 

    β€œMnasemaje?” aliwauliza, alikua haogopi chochote wala Mtu yeyote yule, jeuri na katili mno β€œSaida anaishi hapa?” akauliza Polisi mmoja.Β 

    β€œYeye ni Nani?” akawaulizaΒ 

    β€œUnajibu kwa dharau kiasi hicho Mzee, Saida ni Mpwa wangu Mimi. Ameolewa na KijanaΒ  anaitwa Salehe, upelelezi umeonesha kuwa ni Kijana wako huyo Salehe halafu unauliza niΒ  Nani?” akaingilia kati mjomba Kambona na kumshika shati Mzee Mwinyimkuu, PolisiΒ  wakaokoa

    β€œUnanivunjia heshiam si ndiyo?” akauliza Mzee Mwinyimkuu kwa hasiraΒ 

    β€œSiyo heshima tu, ntaivunja hata hii nyumba kama hutonipatia Saida wangu” Mjomba KambonaΒ  hakupoa kabisa, alijawa na hasira sana.Β 

    β€œHuyo Salehe unamfahamu?” Polisi wakamuuliza Mjomba KambonaΒ 

    β€œNdiyo, nimeozesha mwenyewe. Picha si hii hapa ya ndoa” akatoa picha, ile picha akapewaΒ  Mzee Mwinyimkuu.Β 

    β€œUmemtambua mtajwa pichani?” akauliza Polisi mmoja, Mzee Mwinyimkuu akaangua kichekoΒ  kisha akaita kwa sautiΒ 

    β€œSalehe, hebu njoo uone maajabu ya Dunia” akaitikia Mtu kutokea ndani na kuwafanya Polisi naΒ  Mjomba Kambona wakae mkao wa kula kumuona Salehe. Ikachukua kama sekunde kadhaa tuΒ  Kijana mmoja akatoka ndani, Kijana aliyekuja hakufanana na Salehe wa kwenye picha.Β Β 

    β€œUnamfahamu Saida?” akauliza Mzee Mwinyimkuu akimuuliza huyo Kijana aliyemtambulishaΒ  kama Salehe, kiukweli hakuwa yule Salehe aliyeniowa kabisa yaani sura tofauti.Β 

    β€œHapana, kuna nini?” akauliza huyo Salehe, kiukweli Mjomba Kambona alinywea. Lakini PolisiΒ  mmoja akasemaΒ 

    β€œOngozana na Mimi Kijana” akamshika mkono Salehe na kwenda naye nje. Lengo la Polisi niΒ  kutaka utambuzi kwa Majirani maana Upelelezi wao uliwaambia Salehe wa kwemye pichaΒ  anapatikana kwa Mzee Mwinyimkuu. Wakafika hadi nyumbani kwa Mama Ashura maana ndipoΒ  palikua na Watu njeΒ 

    Walipomuona Yule Kijana akiwa na Polisi vijana walikimbia hadi yule Polisi akashangaa, hataΒ  Mama Ashura naye alikua anataka kukimbia ila Polisi akamzuia Mama Ashura na KumwambiaΒ  asikimbie ana maswali kadhaa anataka kumuuliza, ndipo Mama Ashura akabakia lakini kwa hofuΒ  sanaΒ 

    β€œUnamtambua nani pichani?” Yule Polisi akampa picha yule Mama, Mama Ashura akaipokeaΒ  picha japo kwa wasiwasi lakini alipoiangalia ile picha alishtuka sana, akameza funda la mate.Β Β 

    β€œHapana’’akajibu lakini kwa hofu sana kiasi kwamba yule polisi akahisi pengine kuna jamboΒ  analificha. Kilichomshtua Mama Ashura ni kuniona Mimi kwenye ile picha ya ndoa ambayoΒ  Mjomba Kambona aliwapatia polisiΒ 

    β€œNa huyu Kijana hapa?” akauliza Polisi, Mama Ashura akamtazama yule Kijana. AkaachiaΒ  tabasamu la hofu kisha akajibuΒ 

    β€œNi Salehe, anaishi pale” akaonesha na kidole kabisa. Majibu haya yakamuacha yule polisiΒ  kinywa wazi, basi akarudi hadi nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Hakuna ushahidi waΒ  anachosema Mjomba Kambona. Lakini Mjomba akawaaambia

    β€œNina namba ya huyu Mzee alikua anawasiliana na Mama yake Saida, hii namba nimepewa naΒ  Mama Saida. Jina ni hilo la Mwinyimkuu” akasema Mjomba japo kwa sauti ya kupoa, ikabidiΒ  Polisi waipige ile namba.Β 

    Ikapokelewa na Mtu mwingine kabisa tena Mwanamke akimuuliza yule Polisi Nani wewe?Β  Yalikua kama maigizo ya Filamu lakini lilikua tukio la kweli, nyakati zote hizo MzeeΒ  Mwinyimkuu alikua akitabasamu akiwa anamtazama Mjomba Kambona.Β Β 

    β€œMnaona anavyo nitazama, huyu anajua kila kitu” akasema Mjomba lakini hakuwa na ushahidi,Β  maneno yake yalikua ni sawa na kuupaka upepo rangi. Muda wote Mzee katili alikuaΒ  akitabasamu kwa mpango fulani ulio kichwani pakeΒ 

    Polisi walikosa ushahidi, ikaonekana kuwa Mjomba Kambona aliyakosea maelezo yake. KibayaΒ  zaidi hata picha aliyowaonesha Polisi kuwa ndiye aliyeniowa ilikanwa kwa kuoneshwa SaleheΒ  mwingine na kilichotia nguvu kukosekana ushahidi ni maneno ya Mama Ashura. AngefanyajeΒ  Mjomba wangu zaidi ya kutoa kitambaa na kujifuta jasho ila moyoni aliamini MzeeΒ  Mwinyimkuu alikua anajua wapi nilipo, pia hapakua na ushahidi mwingine sababu MzeeΒ  Mwinyimkuu hakuhudhuria ndoa yanguΒ Β 

    Polisi wakamwambia Mjomba KambonaΒ 

    β€œTutaendelea na Uchunguzi, kwasasa wewe liachie jeshi la Polisi. Tutakupa taarifa ya UchunguziΒ  juu ya Saida pia huyo Kaka yake” haikua kauli yenye matumaini, ilimvunja moyo sana MjombaΒ  Kambona. Akamwambia Mzee MwinyimkuuΒ 

    β€œSaida hawezi kutoweka kirahisi, lipo unalolijua. Siondoki Rukwa hadi nihakikishe nampataΒ  Mpwa wangu” alisema hivyo kisha aliongozana na Polisi kuondoka, Salehe feki na MzeeΒ  Mwinyimkuu wakatazamana kisha wakawa wanawatazama namna Polisi na Mjomba KambonaΒ  walivyokuwa wanaondoka.Β Β 

    Wala hawakufika mbali, kabla hata hawajapanda kwenye gari ya Polisi. Mjomba KambonaΒ  alianguka na kufariki papo hapo akitokwa na Mapovu mdomoni. Licha ya jitihada za jeshi laΒ  polisi kumkimbiza Hospitali lakini alikua tayari amefarikiΒ 

    Taarifa ikarudi Dar-es-salaam kuwa Mtu waliyemtuma kuja kututafuta Mimi na Kaka HamiduΒ  alikua tayari ameshafariki. Yalikua ni majonzi juu ya Majonzi, taarifa hii ilipomfikia Baba yanguΒ  alifariki pia kwa presha. Bundi aliizingira familia yangu, misiba miwili ndani ya siku moja,Β  Mzee Mwinyimkuu akashinda tena kwa kishindo kikubwa sana.Β 

    **Β 

    Nilihesabu siku ambazo nilikua ndani ya ile nyumba ya mateso, zilitimia siku saba ngumu.Β  Nilikonda nikawa kama Mtoto mdogo, niliishiwa nguvu. Kilichokuwa kimebakia kwangu ilikuaΒ  ni kufa tu. Kila nilipoamka nilijikuta nimeshaondolewa kidole kimoja, pumua yangu ikawa yaΒ 

    shida sana. Nikakosa uwezo wa kuwatambua Watu kirahisi, yule Bodaboda aliendelea kunileteaΒ  chakula kila siku lakini pia sauti ya Mwanaume mmoja kugumia ilikua ni sauti ya Kila sikuΒ 

    Lilikua ni jambo la kawaida sana yeye kupaza sauti, sikuwahi kufahamu alikua akipitia matesoΒ  gani, ila dakika za mwisho niligundua kuwa naye alikua akipelekewa chakula na huyu huyuΒ  Bodaboda anayeniletea Mimi chakula.Β 

    Sikuweza kusimama tena, vidonda vilianza kutoa funza sababu sikuwa na dawa yoyote isitosheΒ  joto la mle ndani liliniathiri kwa kiasi kikubwa, Mwenzenu niliwahi kufika Jehannam nikiwaΒ  Hai.Β 

    Basi siku moja yule Bodaboda alikuja, siku yenyewe palikua na mvua kubwa. Aliingia akiwaΒ  ameloa sana anatetemeka kwa Baridi, japo nilikua katika nyakati za mwisho kabisa za uhaiΒ  wangu lakini niliweza kugundua kuwa Baridi lilikua tatizo kubwa kwake. Alikua akiniandaliaΒ  chakula huku akitetemeka nikagundua anasumbuliwa na tatizo linalo sababishwa na Baridi.Β 

    Akajikaza, akaniwekea chakula. Alipaswa kunilisha sababu Mimi nilikua siwezi tena hataΒ  kushika kijiko, nilikonda mno hadi mishipa ya Damu ilikua ikionekana. Akajitahidi kuniinua iliΒ  kunikalisha kitako niweze kuegemea ukuta anilishe vizuri, siku hii nilipanga kuacha kula ili nifeΒ  mapema maana mateso yalinizidi kabisa, Jamani naposema nilikonda basi ujue nilikonda nikawaΒ  na kilo chache sana halafu kichwa kikawa kikubwa.Β 

    Nilitamani kumuuliza ana shida gani, huyu Mtu hakuwahi kunitesa wala hakuwahi kunisemeaΒ  jambo baya isipokua alikua hajibu maswali yangu yote niliyokuwa namuuliza.Β 

    Hali yake ilianza kuwa mbaya, akashindwa hata kunishikilia akaanguka chini na kuanza kugalaΒ  gala kwa maumivu Makali sana, mlango ulikuwa wazi hakuufunga sababu alipoingia alikuaΒ  tayari ana hiyo hali ya Maumivu, niliona ni nafasi ya kutoroka lakini sikuwa na akiba yoyote yaΒ  nguvu iliyobakiaΒ 

    Nikatamani kuendelea kuishi ghafla tu, namna pekee ya kuendelea kuwa hai ni kutoroka. HukoΒ  nje mvua ilikua ikinyesha na kusababisha kelele kubwa sana kwenye Bati. Sikuwa na nguvu yaΒ  kusimama, nikaona ni bora nijiburuze nione kama naweza kufika njeΒ 

    Yule Bodaboda alipoona naanza kujiburuza akajua nataka kumtoroka, akili yake ikatamaniΒ  anizuie lakini mwili ulimsaliti, nguvu zilimwisha akiwa sakafuni anapumua kwa shida sana.Β  Nikaendelea kujivuta taratibu huku nikiwa ninasali Mungu niliyemkatia tamaa azidi kunipaΒ  nguvu, unajua kwanini niliamini naweza kuondoka pale?Β 

    Kwasababu hapakua na mtu mwingine aliyekuwa anakuja isipokua yeye, hivyo hakuna tena waΒ  kunizuia, halafu niliwaza kufika chumba ambacho yule Mwanaume anagumia ili kama yeye anaΒ  nguvu tusaidiane kutoroka.Β 

    Nilijiburuza kama nyoka hadi nilipotoka nje ya chumba kile, palikua na funguo kwenye kitasa.Β  Nikapata akili ya dharura kuwa huwenda funguo ile inaweza nisaidia kufungua milango mingineΒ 

    maana ilikua na funguo tatu zilizowekwa sehemu moja, naipataje Funguo ni lazima nisimameΒ  niichomoeΒ 

    Kivumbi kilianzia hapo, nilikonda Mimi kiasi kwamba upepo unaweza nipeperusha, MalaikaΒ  Mtoa roho alikua amenisimamia akiniuliza nasimama au achukue roho yangu, sijui nguvuΒ  zilitoka wapi nikasimama kwa kuyumba huku nikitetemeka. Nikachomoa funguo, ile natakaΒ  kupiga hatua nikaangukaΒ 

    Basi nikagugumia kwa maumivu, nilihitaji kufanya haraka maana kama yule Bodaboda atapataΒ  nguvu basi sitaweza tena kuondoka, nikamkumbuka Mama na Baba yangu, nikamkumbuka KakaΒ  Hamidu. Ghafla nguvu zikaamkaΒ 

    Nikajikaza na kuanza kujiburuza sakafuni kama nyoka vile, kwa mwendo huo huo nilijikutaΒ  nikikiacha chumba kwa mbali kidogo, sikuufunga ule mlango wa chumba nilichomuachaΒ  Bodaboda.Β Β 

    Basi nilipofika kama chumba cha tano hivi nikasikia Mtu akiugonga mlango kwa nguvu hukuΒ  akisemaΒ 

    β€œNjoo unitoe humu Mshenzi wewe, mtauwa wangapi. Siku ikifika mtakufa kama Kuku” alisemaΒ  kwa hisia sana lakini hakujuwa kuwa Mimi nilikua tayari nipo mlangoni. Mlango ulikuaΒ  umefungwa, korido lilikuwa refu halafu vyumba vilikua mbali mbali. Nilijitahidi sana kusimamaΒ  nifungue mlango lakini nilikua nakosa nguvu, nilijaribu kama mara tatu lakini niliishia kuangukaΒ 

    Wakati nikiwa nimeanguka nikageuka nyuma, ndipo nilipomuona yule Bodaboda akijikongojaΒ  kwa maumivu kuja nilipo, alikua amelishikilia tumbo lake. Hapo sasa yule Malaika mtoa rohoΒ  nikamuona kama anachukua koleo kwa ajili ya kuichukua roho yangu.Β 

    Sauti ya yule Mwanaume ilizidi kusema, kibaya zaidi Mimi ndiye mwenye funguo halafu sautiΒ  yangu ilikua haitoki. Nikasema kama sisimami basi siondoki. Yule Bodaboda akawa anazidi kujaΒ  upande wangu kwa kasi akionekana kuanza kupiga hatua za nguvu. Nikamtaja Mungu nikasemaΒ 

    β€œMungu nipe nguvu niishinde hii vita” nikajivuta haraka nikasimama nikiwa ninayumba,Β  nikaanza kusaka tundu la kuweka funguo maana nguvu yenye ilikua sifuri, nikawa najitahidiΒ  huku nikiwa natetemeka. Mara naingiza mara nakosea, huku yule Bodaboda akizidi kunisogelea,Β  hata nilipopaatia nilikua nimeingiza funguo isiyo yake.Β 

    Akawa karibu zaidi kiasi kwamba akipiga hatua tatu anakuwa amenifikia na kunizuia kuufunguaΒ  mlango, nikapapasia kwa bahati nzuri nikapatia funguo nikavuta nguvu za mwisho nikatekenyaΒ  kitasa lakini tayari Bodaboda alikua ameshanivaa na kuniangusha chini, Bahati nzuri ule mlangoΒ  ulikua tayari umeshafungukaΒ 

    Akatoka mwanaume mmoja na kuanza kumkita mateke yule Bodaboda hadi akamtupilia mbaliΒ  huko akiwa hoi sana anatokwa na damu mdomoni, eneo la Korido lilikua linawaka taa isipokuaΒ 

    vyumbani tu. Sikuamini macho yangu Mtu ambaye nilikuja kumuona na kumtambua japoΒ  nilimuona mara moja tuΒ Β 

    Alikua ni yule Mwanaume niliyemuazimaga simu kule Buchani, Ndio! Ni Abuu, masikini nayeΒ  alikua mateka wa Mzee Mwinyimkuu baada ya kujulikana ananifuatilia Mimi, kwa muda mfupiΒ  naye alikua amepungua sana japo alikua na nguvu.Β 

    Hakuniuliza chochote zaidi ya kuninyanyua na kuweka mkono wangu kwapani kwake tukawaΒ  tunaelekea nje, mvua bado ilikua inanyesha. Tulipokua tunakaribia kutoka kabisa tukamuonaΒ  Mtu anakuja Mbio, tena akikimbia kwenye mvua, ikatubidi tujifiche nyuma ya Mlango waΒ  kutokeaΒ 

    Yule Mtu alipofika, breki ya kwanza ilikua vyumbani kisha akamrudia yule Bodaboda aliyekuwaΒ  anagala gala. Akamuuliza kwa hasiraΒ 

    β€œUmefanya nini Mpuuzi wewe?” aliuliza kwa sauti ambayo niliitambua, ilikua ni sauti ya MzeeΒ  Mwinyimkuu. Nilishtuka na kupata nguvu, nilipokumbuka kuwa yeye ndiye mtesi wangu basiΒ  mkojo ulinibana. Ghafla tu nikajiona ni Binadamu ninayehitaji kujiteteaΒ 

    β€œNenda, hatuwezi kuondoka wote. Kaiambie Dunia kuhusu huyu Mzee, kama nitarudi tutakutanaΒ  na kama nitafia hapa basi Roho yangu itakua salama” alisema Abuu, roho iliniuma. Sikua naΒ  uwezo wa kuzungumza. Mdomo wangu wa juu na chini nilihisi kama vimeungana sababu nilikuaΒ  na vidonda mdomoni hivyo kukaa kimya ndiyo yalikua maisha yangu.Β 

    Nikaitikia kwa kutumia kichwa kisha nikasimama kama Mzimu, Mungu akaamua kunikumbuka.Β  Akanipa nguvu na ujasiri, alichotaka Abuu ni kumzuia Mzee Mwinyimkuu. Wakati naanza safariΒ  Mzee Mwinyimkuu akaja mbio nahisi alikua anaanza kutusaka, sijui alijuaje kuwa tunatoroka.Β  Huyu Mzee alikua Mchawi haswa, aliponikaribia tayari Abuu alimdaka Mzee MwinyimkuuΒ  wakaanza kupalangana, muda huo nami nikaanza kujivuta kuondoka pale taratibu hadi nikaingiaΒ  kwenye mvua.Β 

    Ulikua mchana lakini anga lilikua na wingu la kutosha kiasi kwamba palikua na giza fulaniΒ  isitoshe palikua Porini. Nilipopigwa na mvua nikapata nguvu ya kuanza kuchanganya MiguuΒ  yangu vizuri. Nikaanza kukimbia huku nikiyumba kama mleviΒ 

    Sijui nilikimbia umbali gani lakini nilikimbia bila kuangalia nyuma, nilikimbia sana hadiΒ  nilichoka kabisa nikaanguka na kupoteza fahamu zangu.Β 

    Nilirudisha fahamu na kuanza kujitambua nikiwa naburuzwa kwa kasi sana, watu walikua kamaΒ  vile wamenizunguka. Walikua na mavazi ya kufanana, nilikua kwenye kitanda kiendacho kwaΒ  kasi mno, nikawasikia wakisemaΒ 

    β€œApelekwe ICU Haraka sana, kazi ianze mara moja” niligundua nilikua Hospitalini, waleΒ  wauguzi walionekana kunikatia tamaa sababu nilikua na hali mbaya sana. Lakini mimiΒ 

    mwenyewe nilijiona ni mzima wa Afya zote, mahali nilipokuwepo palikua ni hatari zaidi yaΒ  Kuzimu.Β Β 

    Chozi lilinibubujika nikafumba macho yangu huku nikimshukuru Mungu. Madaktari walifanyaΒ  kazi yao kwa wiki tatu kuhakikisha najitambua zaidi, wakaniweka kwenye uangalizi maalumΒ  kwa kipindi chote hicho hadi nilipokumbuka yaliyonisibu.Β 

    Nikawaandikia jina Langu, mahali nilipotoka maana nilikua siwezi kuzungumza tena, HospitaliΒ  ikasambaza jina na taarifa zangu ndipo Mama yangu alipokuja Mbeya akiongozana na NduguΒ  wengine kunitambua. Mama alilia sana, sikuwahi kumuona Mama yangu akilia namna ile, yaleΒ  Maisha yaliniathiri sana kisaikolojia. Nikapoteza uwezo wa kuzungumza kabisa. Taarifa ya KifoΒ  cha Baba ilinihuzunisha mno, ikanitoa chozi.Β 

    Polisi walipokuja niliandika maelezo yangu, ilikua baada ya wiki sita. Mwezi mmoja na sikuΒ  kadhaa, afya yangu ilianza kukaa sawa lakini sikuwa na Uwezo wa kuzungumza chochoteΒ  isipokua kuandika. Polisi walinichukua ili nikawapeleke mahali nilipoteswa yaani nyumbani kwaΒ  Mzee MwinyimkuuΒ Β 

    Mimi na Mama tulienda, palikua ni pale pale kwa Mzee Mwinyimkuu. Namba ya nyumba ilikuaΒ  ni ile ile, mazingira yale yale, chozi lilinibubujika sana hadi Mama akashindwa kujizuia.Β Β 

    Nilikua natembezwa kwenye kiti cha Walemavu maana bado miguu ilikua haipo sawa pia sikuaΒ  na vidole nilikua najiuguza. Nikampa ishara Mama yangu kuwa anipeleke kwanza nyumbaΒ  jirani, pale kwa muuza chapati, nilimkuta Mwanamke mwingine kabisa akitengeneza chapati,Β  nikaandika kwenye karatasiΒ 

    β€œMama Ashura yupo wapi?” nilikua na ujumbe wa Mtoto wake Ashura nilitaka kwanza nimpeΒ  ujumbe, wakati huo polisi walikua wameizingira nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. MamaΒ  akamsomea yule Mwanamke, lakini cha ajabu eti akadai yeye ndiye Mama Ashura, nilishtukaΒ  alafu kingine kilichonipa mshituko ni kumuona Ashura mwenyewe, alikua ni Ashura yule yuleΒ  niliyemuona Nyumbani kwa Mzee MwinyimkuuΒ 

    Haya mambo yalinifanya nianze kuonekana akili yangu bado haiko sawa, nikajitahidiΒ  kuwaambia kwa maandishi lakini niliishia kupewa pole tu, kisha nikapelekwa kwa MzeeΒ  Mwinyimkuu. Nako nikakutana na stori mpya kabisaΒ 

    Kwanza ile nyumba si ya Mzee Mwinyimkuu, hawamfahamu. Wao wanaishi hapo Kwa MiakaΒ  mingi, nilitokwa na Mchozi, nyumba ile ile mazingira yale yale lakini stori tofauti. NikaombaΒ  niingizwe ndani, nikapelekwa kwenye chumba nilichokuwa nalalaΒ 

    Nikakuta magunia ya vyakula, tena kilikua chumba chenye makorokoro mengi sana naΒ  hakikuonekana kua chumba cha kulala Mtu. Mama akaniambiaΒ 

    β€œSaida, najua umeteseka sana huku lakini hukumbuki chochote tena. Siku ukikumbuka nakuahidiΒ  tutarudi, yule Kijana na Baba yake watalipa” Kauli ya Mama yangu ilinimaliza akili yangu,Β 

    nilifikia hatua nikakubali kuwa akili yangu haipo sawa, inawezekanaje kila kitu kibadilike kwaΒ  haraka vile. Hakuna aliyeniaminiΒ 

    Lakini sasa wakati natoka nikajikuta nikipeleka macho yangu jikoni, nikaiona ile sufuria kubwaΒ  ambayo kwa mara ya kwanza nilipika mchicha mwingi, nikashtuka alafu nikauona MchichaΒ  mwingi ukiwa kwenye Beseni. Kilichonishtua ni kwamba nilimuona Msichana wa umri wanguΒ  akiutengeneza.Β 

    Nilijikuta nikipiga yowe kali sana. Hali ya afya yangu ikawa sio nzuri nikarudishwa tenaΒ  Hospitali. Tokea siku ile nilikua Msichana ninayekaa kimya hadi leo hii nawasimulia hiki kisa,Β  sikumpata Mzee MwinyiMkuu wala Salehe, lakini sitakubali. Siku moja nitarudi Rukwa iliΒ  walipe kwa maumivu na mateso makali ninayoyapitia hadi sasa.Β 

    Kwasasa nimerudishwa kwetu Dar-es-salaam, niko Magomeni. Maisha yangu yamekuwa yaΒ  Ukimya sana, Sijazungumza tena tokea siku ile nilipozungumza kwa mara ya mwisho Rukwa,Β  sijaandika chochote na wala sitaki kusema chochote kile ila kupitia mkasa huu nataka ujifunze.Β 

    Kamwe kwenye Maisha yako usiolewe au kuowa Mtu usiye mfahamu, Dunia ni Kichaka chaΒ  Mateso. Wasichana wengi wanayapitia mateso niliyoyapitia, wengi wanauawa, wengi wanapataΒ  ugonjwa wa akili. Hata wanaume wapo waliopoteza kila kitu, Siku nikifungua kinywa changuΒ  nitawasimulia mengi, kwasasa naishia hapa, naweka kalamu yangu chini.Β 

    AHSANTE……….MWISHO

    Comments zikiwa nyingi TUNAANZA MPYA Chaap

    USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kutuma Message WhatsApp Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xxΒ  Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    24 Comments

    1. Mwaija Seleman on January 13, 2025 5:00 pm

      Hadi mwili umenisisimka πŸ™Œ

      Reply
    2. Halinga1 on January 13, 2025 5:03 pm

      Kaka umetisha

      Reply
    3. Mama Edward on January 13, 2025 5:05 pm

      Wowoooh fupi na inafundisha sana nmepata somo apa nmejifunza mengi poleee saida wetu.

      Reply
      • Amasa tz on January 14, 2025 7:36 am

        Hatar sana,, mungu amekpgania pakubwa,, mm kama kijana ambae sjaoa hakka nmepata kitu kwa riwaya hii,, mungu akupe maisha mazur

        Reply
    4. Egibeth on January 13, 2025 5:05 pm

      Dag

      Reply
      • jas on January 15, 2025 10:57 pm

        pole sana

        Reply
    5. Eva Mpume on January 13, 2025 5:22 pm

      Jamani hatujajua mwisho wa kijana aliyemukoa Saida,,, mwandishi ungesogeza kidogo

      Reply
    6. G shirima on January 13, 2025 5:31 pm

      Lini utafungua kiywa Chako tuendelee maan bado nataka kujua zaid

      Reply
    7. Ahmed Ruta on January 13, 2025 5:46 pm

      HahahahahaπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… umepigaje apooooooooooooooβœοΈπŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘

      Reply
    8. Ahmed Ruta on January 13, 2025 5:48 pm

      Navuta picha mwandishi mwili wako ulikua kama wa Ile muv BABU SISU

      Reply
    9. Msangazi Rams on January 13, 2025 6:50 pm

      Hii ya leo machozi yamenibubujika sijui nisemeje lakin naamin Allah anajua zaid yaliyopo mioyon mwetu wanadamu

      Reply
    10. Fawziya Hassan on January 13, 2025 7:30 pm

      Maskini Saida jamani πŸ˜₯
      Simulizi ya Maajabu Nzuri yenye mazingatio makubwa jamani
      Uchawi upo
      Ila uchawi wa MwinyiMkuu ni zaidi ya Uchawi
      Mungu atunusuru maisha yetu na Wachawi
      Mungu AWAANGAMIZE WASHIRIKINA WOTE MOTONI.
      Ameen.

      Reply
    11. Fatbaloz on January 13, 2025 11:32 pm

      Safi sana mtunzi tumejifunza sana mim pamoja nawasomaji wenzangu Big up

      Reply
    12. Dorcus semu on January 14, 2025 12:07 am

      Inauzunisha sana pole saida 😒

      Reply
    13. Cathbert on January 14, 2025 7:16 am

      Kazi mzuri na pole sana

      Reply
    14. Abuu bura on January 14, 2025 7:20 am

      😭😭😭😭😭😭😭😭😭nimelia kama mtoto

      Reply
    15. Steven on January 14, 2025 10:35 am

      Daah atali

      Reply
    16. Juma on January 14, 2025 6:51 pm

      Ni hatar

      Reply
    17. Gyakiee on January 15, 2025 6:16 am

      Munguu hamtupii mja wake hakika Munguu ni mwemaa

      Reply
    18. Given Gihsy on January 16, 2025 2:56 pm

      πŸ₯Ήnianze kwa kuhiluzunika ,ila mtu kuna sehem nmecheka dadeq, KWAMBA NYIE WASHENZ NIFUNGUENI MTAKUF KAMA KUKU , YAN MUUNI YUPO KWENY MATATZO ILA BADO AJAL, KWEL MAN IS STRONG NATURAL

      Reply
    19. Perfect on January 18, 2025 11:23 pm

      Kwani story ni yakwel

      Reply
    20. Sharo love malkx πŸ’– on January 24, 2025 8:25 am

      Dah sijui niseme nini
      Mhhh ila pole

      Reply
    21. Hermione2202 on April 12, 2025 11:37 pm

      http://terios2.ru/forums/index.php?autocom=gallery&req=si&img=4457

      Reply
    22. πŸ—’ πŸ”” Alert - 0.3 BTC waiting for withdrawal. Confirm >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=245ecef015fd586244ce32903a04bac6& πŸ—’ on October 17, 2025 1:46 am

      gx3yc0

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.