Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (05)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 9, 2025Updated:January 11, 202525 Comments10 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Sikuwa na maswali mengi kuwa chapati zinaenda kuliwa na Nani sababu hata ule MchichaΒ  nilikua na uhakika kuwa unaliwa na Misukule niliyoiona Usiku. Nilihisi kukonda kwa siku mojaΒ  tu ya hekaheka, nilitoka nikafungua geti kisha nikatoka ndani, taratibu nikawa naeleka kwa yuleΒ  Mama anayeuza Chapati nyumba kama ya Nne hivi kutoka nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu.Β 

    Macho yangu yaliitazama sana ile nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, nje Watu walikuaΒ  wakiendelea na shughuli zao, niliamini hakuna anayejuwa kinachoendelea. NilitamaniΒ  nimsimulie Mtu pengine nimwombe msaada lakini nikakumbuka onyo nililopewa na MzeeΒ  Mwinyimkuu, Ah! Hamu iliniisha. Endelea

    SEHEMU YA TANO

    β€œKaribu Binti” alisema yule Mama, sikuachia tabasamu kama lile la siku ya kwanza nililompaΒ  huyu Mama, moyo wangu ulikataa kuigiza furaha wakati napitia nyakati ngumu sana na zaΒ  mateso makali sana.Β 

    β€œAhsante, nataka chapati za hii hela” nilisema kwa sauti isiyo changamka, yule Mama akapokeaΒ  pesa kisha akawa ananichukulia chapati alizozitengeneza tayari, lakini akaacha akaniulizaΒ 

    β€œUpo sawa?” swali hili liliniumiza sana, nikawaza nimjibu nini ila nilishaonywa kuwa nikisemaΒ  chochote Wazazi wangu watauawa. Kwa simulizi nilizosikia kuhusu Uchawi inawezekana kabisaΒ  wakauawa wakiwa Mbali hivyo niliogopa sana. Wakati nawaza yule Mama akanishtua kwaΒ  kunitikisa maana nilishazama kimawazoΒ 

    β€œUpo hapa kweli Binti?” nikashtuka na kujibaraguza kama Mtu aliye sawa huku nikijuwa fikaΒ  kuwa nausaliti moyo wangu.Β 

    β€œNdiyo, nipo Mama. Samahani naomba chapati niwahi nimeacha chai jiko la gesi” nilisema,Β  nilishakuwa na uhakika kuwa pengine Mzee Mwinyimkuu aliweka mtego wake kwangu ndiyoΒ  maana akaniacha huru nje

    β€œMh!” akaguna tu kisha hakusema kingine, halafu akanifungia chapati za Elfu tano akaniwekeaΒ  kwenye mfuko.Β 

    β€œKaribu tena, Naitwa Mama Ashura. Ukikwama usisite nitakupa msaada” alisema yule MamaΒ  akanipa mfuko, Uwiiβ€Ό alinigusa ndani ya Moyo wangu kwa jinsi nilivyokua natamani kupataΒ  msaada Mimi kwa yanayonisibu lakini sikujua napataje msaada Mimi, naanzaje? NikajichekeshaΒ  tu kama mwehu kisha nikageuka na kuondoka pale.Β Β 

    Kitendo cha Kumpa mgongo Mama muuza chapati aliyejitambulisha kama Mama Ashura, choziΒ  lilinilenga. Safari ya kurudi ndani ilijaa maumivu makali sababu narudi tena kuivaa hofu naΒ  mateso ndani ya Nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Nilitamani kukimbia lakini niliwaza WazaziΒ  wangu, sikuwa na tumaini kiukweli.Β 

    Nilifungua geti na kuingia ndani kisha nikafunga geti, nilivyofunga geti chozi lilinibubujika sanaΒ  nikalifuta kwa kutumia mtandio wangu. Ilikua kama Mishale ya saa Tatu na dakika zake hivi,Β  nilichemsha chai na kumpa Mzee Mwinyimkuu sebleniΒ 

    β€œKula chapati moja, zilizobakia peleka kwenye kile chumba. Weka na maji ya kunywa kishaΒ  ondoka, ukimaliza njoo” alisema akiwa anakula chapati zake, nilifuata maagizo sababu hapakuaΒ  na jambo jipya. Nilishajua zinaliwa na Misukule ambao Mzee MwinyiMkuu ameniambia nifanyeΒ  nao mapenzi.Β Β 

    Nilipomaliza sikula, nikarudi sebleni kumsikiliza.Β 

    β€œKaa hapo” akaniamuru niketi kwenye kochi la kizamani, akagida funda kadhaa za chai kishaΒ  akasema tenaΒ 

    β€œHii simu imekumbana na Nini?”  

    β€œIlianguka Baba” nilijibu kwa heshima na wogaΒ 

    β€œUtaongea na Wazazi wako kwa kutumia simu yangu, Baba yako anaumwa na kama utafanyaΒ  zihaka nitamwondoa. Wasalimie waambie simu imeharibika ili wasisumbue, ole wako uonesheΒ  wasiwasi wowote ule” Nilishtuka, likanitoka neno bila kutarajia sababu nilikua nampenda sanaΒ  Baba yangu Jamani, sijui alipata wapi namba ya Mama yanguΒ 

    β€œBaba anaumwa?” Weee, nilikiona cha moto, alinimwagia chai ya moto usoni. Nilitapa tapa kwaΒ  maumivuΒ 

    β€œKimyaβ€Ό mshenzi wewe, unauliza ulichokisikia?” alisema Mzee MwinyiMkuu, sijui nikwambieΒ  nini Msomaji. Huyu Mzee alikua katili haswaa kuanzia sura yake hadi matendo yake, Watu kamaΒ  hawa nilikua nawaona kwenye filamu tu na wala sikutegemea kama wangekuwepo kweli hapaΒ  Duniani.

    Niliacha Kulia lakini maumivu ya moto yalikua makali sana japo taratibu yalianza kupoa, kishaΒ  nikasikia simu ikiwa imeshapigwa inaita, aliweka Loud Spika ili naye ayasikie mazungumzo,Β  hapo ndipo nilipoisikia sauti ya Mama yangu, chozi lilikua linanibubujika tu. Mama aliitaΒ Β 

    β€œHello” 

    β€œAbee Mama” nilimwitika Mama yangu kwa sauti niliyoshindwa kujizuia kabisa, nililia kwaΒ  mengi sana. Kwanza niliwakumbuka sana wazazi wangu japo ni muda mchache tu umepita naΒ  pili ninayoyapitia sikuwa na Mtu wa kumwambia wakati wazazi wangu wapoΒ 

    β€œHee! Saida Mwanangu, Unalia nini Mama na hii namba ya Nani?” Mama aliitambua sautiΒ  yangu na pia aligundua ninalia, yule Mzee akanikazia macho yakeΒ 

    Jamani sauti ya Mama yangu ilizidi kunichoma Moyoni, nilishindwa hata kuongea, laiti kamaΒ  Mama yangu angelijua nipo chini ya Ulinzi sijui ingekuwaje.Β 

    β€œSaida unalia nini Mwanangu, Mumeo amekufanya nini?” Si unajua ndoa ina siku tatu tu hivyoΒ  ni lazima Mama ahisi pengine nina tatizo na Salehe, nikafuta chozi nikasema neno moja tu kwaΒ  Mama kisha niliangua KilioΒ 

    β€œNimewakumbuka sana Mama na Baba…” Nililia kama Mtoto mdogo, Mama naye akalia, MimiΒ  ndiye Mtoto wao pekee na pendwa hivyo hawakuwahi kukaa mbali na Mimi nami sikuwahiΒ  kukaa mbali nao hata mara moja, walinilea kama mboni ya Jicho.Β 

    β€œSaida hata sisi wazazi wako tunakuwaza sana, nyumba imepooza mno lakini hakuna jinsi niΒ  lazima Maisha yendelee. Usilie najuwa utazoea hayo unayoyapitia, najua una upweke sana”  Mama alisema, laiti angejua kuwa naishi nusu mfu na nusu Mtu angelia sana.Β 

    β€œSawa Mama lakini siwezi kuacha kuwawaza kila siku ziendazo kwa Mungu, naomba sanaΒ  muwe na afya njema siku zote” angalau kidogo sauti ya kilio ilianza kuniacha, kimafua kwaΒ  mbali tu ndiyo kilikuwepo.Β 

    β€œAmen Mwanangu, hata hivyo Baba yako anaumwa” alichokisema Mama ndicho alichokuaΒ  ameniambia Mzee Mwinyimkuu, halafu safari hii akajifanya hana habari na mimi baliΒ  anaendelea kunywa chai, nilimtazama kwa jicho baya la hasira lakini sikuwa na cha kumfanyaΒ 

    β€œEeh imekuwaje tena Mama?” 

    β€œAsubuhi ameanguka chooni, yupo amelala na anahisi mkono mmoja hauna nguvu” alisemaΒ  Mama, Roho iliniuma sana. Chozi tu ndilo lililokuwa linanibubujika kwa wingiΒ 

    β€œMungu ni Mwema Mama, atapona Insha Allah” nilisema kwa hisia huku nikijuwa ni fitina zaΒ  kichawi za Mzee Mwinyimkuu.Β Β 

    β€œAmen, hii namba ya Nani? Nimejaribu kukupigia hupatikani.” 

    β€œHii namba ni ya Mkwe Wangu. Nilidondosha simu ikapasuka, hata hivyo Mume wanguΒ  amesafiri kwa dharura jana hivyo akirudi nitapata simu nyingine. Ukinihitaji piga humu Mama”  

    β€œSawa Mwanangu…ndoa unaionaje Saida?” Lilipofika hili swali moyo wangu ulisinyaa ghafla,Β  niliumia sana kuulizwa kuhusu ndoa wakati nayoyapitia ni magumu kuliko magumu ya ndoa.Β  Mzee Mwinyimkuu akanikata jicho huku akinionya kwa kidoleΒ 

    β€œNina furaha sana Mama, familia inanionesha upendo wa hali ya juu sana. Samhani MamaΒ  naelekea jikoni mara moja” nilisema na kumuaga Mama, nilijijua kuwa ningeangua kilio chaΒ  Mtu mzima sababu nilisema uwongo kitu ambacho sikipendi hasa kumuongopea Mama yangu.Β Β 

    Nilikata simu kisha niliiweka mezani.Β 

    β€œKama utaendelea hivyo basi hatutagombana Mimi na wewe lakini kama utakuwa mkaidi basiΒ  utakiona cha Mtema Kuni” alisema Mzee Mwinyimkuu, nilinyanyuka taratibu nikatembea hadiΒ  jikoniΒ 

    Chai ilikuwa hapo inaniangalia lakini njaa haikuwepo kabisa, Taswira ya Maisha yanguΒ  ilibadilika mno. Nikajuta kwanini niliolewa Mimi Huuuhβ€ΌΒ 

    Nilikaa kwenye kigoda na kuanza kulia kwa sauti ya chini, huhβ€Ό nilishindwa kujizuia kusemaΒ  ukweli, maumivu yalikua makubwa kiasi kwamba chozi lilinibubujika bila hata kubisha hodi.Β 

    **Β 

    Baada ya kupita siku mbili, zikatimia siku tatu ambazo Mzee Mwinyimkuu aliniambia kuwaΒ  napaswa kufanya mapenzi na Misukule wake, hiyo siku nilisoma kila aya kwenye QuraanΒ  tukufu, nilipiga kila goti ili Mungu aniondoe ndani ya ile nyumba lakini haikua hivyo.Β  Aliniambia Usiku ndiyo nitafanya kitu hicho, akanipa dawa fulani alizozijua yeye akasemaΒ  napaswa kunywa kabla ya kuingiliwa na Msukule ili nisije pata UjauzitoΒ Β 

    Akanipa pia Kaniki nyeusi nijifunge bila kuvaa chochote ndani, kisha akaniambiaΒ 

    β€œJiandae saa moja Usiku utaingia kwenye kile chumba. Una uwezo wa kuhudumia WanaumeΒ  wangapi kwa mara moja?” Aliniuliza, haki ya Mungu nilijawa na hasira isiyo kifani. KwanzaΒ  sikuwahi kufanya mapenzi kabla ya kuingiliwa na yule Msukule Usiku ule nikifikiria ni SaleheΒ  hivyo sijui chochote kile kuhusu MapenziΒ Β 

    β€œNakuuliza wewe!” Akanishtua, nikashtuka haswa maana nilijua kama nitaendelea kuwa kimyaΒ  pengine ningekutana na kofi lake, nikajikuta naropoka tuΒ 

    β€œWatatu” Nikaliona tabasamu kwenye uso wa Mzee Mwinyimkuu.Β 

    β€œHaya pumzika hakikisha umekula vizuri, tuna masaa mawili tu kufika Usiku” alisema kishaΒ  aliniacha chumbani kwangu nikiendelea kukonda kwa mawazo. Kaniki ilikua mkononi mwanguΒ  nikiwaza eti nakuwa mtumwa wa mapenzi kwa Misukule, kipindi hicho nilishaacha kumuwazaΒ  Salehe sababu Baba yake aliniambia kuwa walikua timu moja kuniingiza matatizoni.

    Yale masaa mawili yalikwisha, roho iliniuma na hofu juu, nililia jamani. Halafu sasa huyu MzeeΒ  alianzisha tabia moja, aliacha kugonga mlango wa chumba changu badala yake aliigia tu kamaΒ  upo wazi. Alinikuta nimekaaΒ 

    β€œJitayarishe Binti” alikuja kuniambia hivyo tu, nilimeza funda zito la mate. Laiti kamaΒ  ningelikua huru basi ningeli mrushia tusi la nguoni lakini nilikua kifungoni japo nilikua na uhuruΒ  wa kuchagua kati ya kupoteza Wazazi wangu au kujipotza mimi mwenyewe ndani ya ile nyumbaΒ  ya KichawiΒ 

    Basi, nilifanya kama alivyosema. Niliivaa ile kaniki kama khanga vile nikiwa nimeyafungaΒ  matiti yangu. Sijui aliona nachelewa basi akaja mkuku-mkuku na kunipeleka kwenye kileΒ  chumba ambacho siku ile niliwaona Misukule.Β 

    β€œSaida, kama utakua Binti mzuri nakuahidi utaishi kwa raha sana na wazazi wako watakuwa hai.Β  Unatakiwa utambue jambo moja kuwa unapofanya mapenzi na hawa Misukule wanapata nguvuΒ  zaidi ya kunipa utajiri na nguvu za Kichawi. Huu ni ufalme niliourithi kutoka kwa Baba yangu,Β  nami nitamrithisha Salehe hivyo ni lazima hizi nguvu zitunzwe na kulindwa zaidi ya chochoteΒ  kile. Usiogope ila nitakuwa mkali kama utanifanya nisuburi zaidi” alisema Mzee MwinyimkuuΒ  akiwa anatoa sauti ya kawaida iliyojaa Ulaghai mtupuΒ 

    Akawasha zile udi zake akaweka kila pande ya chumba kisha akaniambia nikae katikati yaΒ  Chumba kama siku ile ya kwanza. Sijui nikwambiaje uelewe kuwa Mzee Mwinyimkuu alikuwaΒ  na sura mbaya ya kutisha kiasi kwamba akikutazama kwa macho yake mekundu ni lazimaΒ  uogope na ujasiri ukuishe, na kingine yeye kukupa pigo ni dakika moja tu wala hawazi.Β 

    Chozi lilinitoka siwezi kuongopa, haikua kawaida. Mara ghafla wakatokea misukule WatatuΒ  wakiwa uchi wa Myama, ilikua kama filamu ya maigizo hivi lakini ndiyo ukweli wenyeweΒ  unaouma zaidi moyoni, nahisi walikua wanajuwa walichoitiwa. Niliona Midudu yao ikiwaΒ  imesimama sana, halafu ni mikubwa Jamani Oooohβ€ΌΒ 

    Nilianza kuogopa huku nikimwambia yule MzeeΒ 

    β€œSamahani Baba naweza kufanya kila kitu lakini hii siwezi, nihurunie Mtoto wa mwenzakoΒ  Mimi. Niache nirudi kwetu” nilisema nikiwa ninalia, Msukule mmoja akanivaa kwa nguvu naΒ  kuniondoa ile Khaniki, nikabaki Uchi wa Mnyama kama alivyotaka Mzee Mwinyimkuu.Β  Niliingiliwa kwa nguvu na wale Misukule huku nikipiga kelele za kuomba Msaada, kwa jinsiΒ  nilivyogumia nina uhakika kuwa majirani walisikia maana nilikua na maumivu makali sanaΒ 

    Walinichana huku chini, damu zilinitoka nikiwa nimelala sakafuni. Nililia kwa kwikwi sitakujaΒ  kusahau namna nilivyojisikia Usiku ule. Yule Mzee akanifuata na kunitaka nikae kimyaΒ  vinginevyo angenichoma kile kisu, nilijinyamazisha haraka sana huku nikimuomba yule Mzee

    β€œKwanini unanitendea unyama kiasi hivi, nimekukosea nini Mimi? Naomba nirudi kwetu MimiΒ  siwezi jamani Aaaah‼” yaani kama angelikuwa ni Mtu mwenye roho nzuri basi angelinihurumiaΒ  mara moja na kuniacha niondoke lakini akanipa Mtihani mwingine mgumu sana ambao uliniachaΒ  na kilema cha Maisha hadi hivi leoΒ 

    Kitu cha kwanza alichofanya ni kuzungumza maneno yake wale Misukule wakaondoka kamaΒ  walivyokuja kupitia pembe za ukuta, lakini pili Mzee Mwinyimkuu aliniambiaΒ 

    β€œKama utaendelea kunisumbua basi hapa patakuwa Jahannam yako na hutokaa utoke MileleΒ  Daima. Kingine napaswa kukuvuna viungo kila unapofanya mapenzi na Misukule, sikuΒ  nikimaliza nitakuacha urudi kwenu” Nilijiuliza anivune viungo kivipi, kauli yake ilinianbia kwaΒ  haraka kuwa Kifo kilikua kimenigongea hodi, kipo karibu zaidi na Mimi.Β 

    β€œUnasema nini?” niliuliza nikiwa ninalia kwa sauti ya Chini.Β 

    Haraka yule Mzee akanipulizia unga fulani aliokuwa ameushikilia mkono wa kushoto, ulikuaΒ  mweupe ulionifikia hadi usoni kwangu. Nikajikuta nikiwa nimelegea vya kutosha kiasi kwambaΒ  sijitambui, hatimaye giza tu lilinitanda na sikujua kilichokuwa kimeendelea nyuma yangu.

    Comments ziwe nyingi hapa

    Nini Kitaendelea?USIKOSE SEHEMU YA SITA YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    25 Comments

    1. Deogratias on January 9, 2025 6:11 pm

      Duuuh ni nomaaa

      Reply
    2. Janeth on January 9, 2025 6:27 pm

      Duuu ni balaaaπŸ”₯

      Reply
      • jas on January 9, 2025 7:03 pm

        duh jmn pole sana

        Reply
        • mwanah on January 9, 2025 7:26 pm

          Masikin saidaπŸ˜—πŸ˜—πŸ€—

          Reply
    3. Ziana Muhidin on January 9, 2025 6:56 pm

      Duh jamani!

      Reply
    4. Frae on January 9, 2025 7:31 pm

      πŸ’”πŸ˜­

      Reply
    5. Fawziya Hassan on January 9, 2025 8:45 pm

      Maskini Saida jamani hadi huruma πŸ˜”
      Simulizi ya vitisho yenye mazingatio makubwa

      Reply
    6. Hamisi halidi on January 9, 2025 9:07 pm

      DuhπŸ’₯πŸ’₯

      Reply
    7. [email protected] on January 9, 2025 10:50 pm

      Amekupofusha mbwa huyo . Dah! Huyo bwaanako salehe Yuko wp jmn kwnn lkn? MUNGU akutowe huko peke yake yy tu ndo anaweza Kwa kweli

      Reply
    8. [email protected] on January 9, 2025 10:52 pm

      Hongera sn Admin . Story inafundiaha sn hii

      Reply
    9. Emanueli on January 9, 2025 11:07 pm

      https://dm.wa.link/tlvtqh

      Reply
    10. G shirima on January 9, 2025 11:20 pm

      Mh wew mtunzi mbona inatisha ivi kama naona live

      Reply
    11. Frae on January 10, 2025 8:13 am

      Muendelezo plzzzz

      Reply
    12. Joshua on January 10, 2025 12:37 pm

      Mhh,mungu tunusuru sisi waja wako kwa kila hatua ya maisha yetu

      Reply
    13. Rehema Adam on January 10, 2025 4:31 pm

      Inatisha sana

      Reply
    14. Fatbaloz on January 10, 2025 8:13 pm

      Haa hii nishida sasa

      Reply
    15. Deogratius on January 10, 2025 8:44 pm

      Mmhh! DuniaπŸ₯Ί

      Reply
    16. [email protected] on January 10, 2025 9:43 pm

      Mwendelezo mkuu .

      Reply
    17. David Emmanuel on January 11, 2025 12:13 am

      Mnachelewa kutuma vipange jamani, tunasubiri sana aisee

      Reply
    18. THOMAS MWITA on January 11, 2025 12:19 am

      Hili ni funzo kubwa sana kwetu ndo maana wazee wetu kuoa walikua mpaka wachunguze familia au ukoo

      Reply
    19. Cathbert on January 13, 2025 8:15 pm

      Hizi pesa ni shidaaa xnaa aisee

      Reply
    20. Elias Benjamin Michael on January 21, 2025 9:30 am

      Uchawi ni balaa

      Reply
    21. πŸ“ˆ πŸ’° Bitcoin Credit - 0.42 BTC detected. Withdraw here >> https://graph.org/WITHDRAW-BITCOIN-07-23?hs=0940f590ca33220304bb7df04b91b9c2& πŸ“ˆ on August 3, 2025 9:15 pm

      x2mk3k

      Reply
    22. πŸ›  πŸ’Έ Bitcoin Reward - 3.14 BTC added. Access here β†’ https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=0940f590ca33220304bb7df04b91b9c2& πŸ›  on September 13, 2025 11:26 pm

      isrprk

      Reply
    23. binance on January 28, 2026 5:24 pm

      Your point of view caught my eye and was very interesting. Thanks. I have a question for you.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 23, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    IlipoishiaΒ  Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayariΒ  tulishazungumza. Nilimeza funda…

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.